Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: ni J2 njema tujenge ndoa zetu tena........

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 34
    1. #1
      gfsonwin's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 12th April 2012
      Posts : 10,729
      Rep Power : 27101
      Likes Received
      10088
      Likes Given
      14003

      Default ni J2 njema tujenge ndoa zetu tena........

      wapendwa wana mmu. habari za jumapili? natumai ni njema sana kwani wengine mko kwenye sherehe za vipaimara na wengine mko na mechi ya spain na italy. yote ni heri tu katika kujipa raha.

      Leo nimekuja tena na mada hapa nataka tuidadavue kuhusu mahusiano yetu na wenzi wetu.
      Hivi ni kwanini wapenzi tunazoeana sana kiasi kwamba tunashindwa kabisa kudumisha mapenzi yetu? kwa nini inakuwepo dhana ya kuzoeana sana kuliko pitiliza kunakopelekea kuona mwenzi wangu ni mtu wa kawaida tu?

      mathalani mama/binti akishakaa na mwenzi wake baada ya muda hakuna tena hata kuflirt nae, akimtumia sms kama ni mchana basi ni ile ya kawaida tu ambayo haionyeshi kujali au haimuhamasishi mpenzi wako. Pia na wanume nao hivyo hivyo. kwanini?

      miye kungwi wenu kwa usukununu wangu nimegundua kuwa wanaotuibia wapenzi wetu wako makini sana mara zote anatuma sms kwa mpenzi kumbembeleza, kumsifia na wengine wanakumbushia hata mchezo walivyofaidi ili hali sisi tulioko ndani tumekaa kimya tunajua ni wangu tu, kwanini nimvizie na manati....lol jamani turudi nyuma tena tuanze kuweka vizuri mapenzi yetu.


      mwenye masikio na asikie neno hili.
      Young Master and Neiwa like this.

    2. RukaaJuu Final

    3. #2
      cartura's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 13th August 2009
      Location : Bongo
      Posts : 3,053
      Rep Power : 2726
      Likes Received
      747
      Likes Given
      6

      Default Re: ni J2 njema tujenge ndoa zetu tena........

      mmh, mwalimu @work once again...; nakubaliana na wewe kabisa kwamba kuna kujenga mazoea na ku-take things for granted sana... mtu unaweza hata kumpa zawadi wala asionyeshe shukrani yeyote... it's like 'si ulipaswa kunipa tu'... vicheche na nyumba ndogo bila kusahau vidumu vina-capitalize sana kwenye hii weakness...
      Neiwa and gfsonwin like this.

    4. BAK
      #3
      BAK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2007
      Location : Mfaranyaki
      Posts : 26,610
      Rep Power : 44967
      Likes Received
      8365
      Likes Given
      8343

      Default Re: ni J2 njema tujenge ndoa zetu tena........

      Let your graceful words fly out into the World, carried on winds of courage, imagination and joy. Let them inspire others to step into action

    5. #4
      gfsonwin's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 12th April 2012
      Posts : 10,729
      Rep Power : 27101
      Likes Received
      10088
      Likes Given
      14003

      Default Re: ni J2 njema tujenge ndoa zetu tena........

      Quote By cartura
      mmh, mwalimu @work... ; nakubaliana na wewe kabisa kwamba kuna kujenga mazoea na ku-take things for granted sana... mtu unaweza hata kumpa zawadi wala asionyeshe shukrani yeyote... it's like 'si ulipaswa kunipa tu'... vicheche na nyumba ndogo bila kusahau vidumu vina-capitalize sana kwenye hii weakness...
      halafu sijui kwanini huwa hatuelimiki kabisa. Ukiuliza binti yeyote anayetembea na mume wa mtu atakwambia jinsi anavyo wajibika kwa yule bwana sms hata 50 kwa siku anatuma. siye tulioko ndani we tend to assume things to be easy and simple. hivi kweli mwenzi akitoka kwaajili ya busu alilokumbushiwa mchan na kabinti/kidumu chake utalalamika wakati wee kuandika tu sms ya i love you mkono ni mzito?
      Reply With Quote

    6. #5
      Neiwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th February 2012
      Location : My Profile
      Posts : 607
      Rep Power : 6930
      Likes Received
      456
      Likes Given
      545

      Default Re: ni J2 njema tujenge ndoa zetu tena........

      Kuna mahala humu humu mmu nilisoma akiwa ni mpenzi wako kweli hainogi, inatakiwa ambae sie... lolz naona ugumu huja hapo.
      "The past and the future are Irrelevant... When the moment is everything"

    7. Miaka 50

    8. #6
      gfsonwin's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 12th April 2012
      Posts : 10,729
      Rep Power : 27101
      Likes Received
      10088
      Likes Given
      14003

      Default Re: ni J2 njema tujenge ndoa zetu tena........

      Quote By BAK
      BAK hizi dedication kila siku n huku jf unatuma je mkeo umeshamtumia? leo ni siku ya kulea ndoa jamani. hebu dedicate kwa mkeo huko.
      super thinker likes this.

    9. #7
      gfsonwin's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 12th April 2012
      Posts : 10,729
      Rep Power : 27101
      Likes Received
      10088
      Likes Given
      14003

      Default Re: ni J2 njema tujenge ndoa zetu tena........

      Quote By Neiwa
      Kuna mahala humu humu mmu nilisoma akiwa ni mpenzi wako kweli hainogi, inatakiwa ambae sie... lolz naona ugumu huja hapo.
      kwanni isinoge Neiwa .........?watu siku hz sms za xtrem kibao mtumie basi jibaraguze basi na wewe? lol kuibiwa kunauma sasa kama ndio mbinu na sisi tuapply hiyo.

    10. BAK
      #8
      BAK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2007
      Location : Mfaranyaki
      Posts : 26,610
      Rep Power : 44967
      Likes Received
      8365
      Likes Given
      8343

      Default Re: ni J2 njema tujenge ndoa zetu tena........

      Quote By gfsonwin
      BAK hizi dedication kila siku n huku jf unatuma je mkeo umeshamtumia? leo ni siku ya kulea ndoa jamani. hebu dedicate kwa mkeo huko.
      hahahahah LOL! ni wimbo tu huo bana si dedication kwa mtu yeyote hapa jamvini....Ndoa ni ndoano zinataka kazi sana ili kuzifanikisha hasa katika miaka hii ukilinganisha na miaka ile ya Wazee wetu. Wengine wanafanikiwa pamoja na mikiki chungu nzima ndani ya ndoa na wengine hawafanikiwi.
      gfsonwin likes this.
      Let your graceful words fly out into the World, carried on winds of courage, imagination and joy. Let them inspire others to step into action

    11. #9
      Neiwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th February 2012
      Location : My Profile
      Posts : 607
      Rep Power : 6930
      Likes Received
      456
      Likes Given
      545

      Default Re: ni J2 njema tujenge ndoa zetu tena........

      Quote By gfsonwin
      kwanni isinoge Neiwa .........?watu siku hz sms za xtrem kibao mtumie basi jibaraguze basi na wewe? lol kuibiwa kunauma sasa kama ndio mbinu na sisi tuapply hiyo.

      mie sio mtaalam gfsonwin, nafanya tu kusoma comments za wadau. kama ni kweli ama uongo, sijui..
      gfsonwin likes this.
      "The past and the future are Irrelevant... When the moment is everything"

    12. #10
      BADILI TABIA's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 13th June 2011
      Location : DUNIANI
      Posts : 14,573
      Rep Power : 5617
      Likes Received
      6211
      Likes Given
      2283

      Default Re: ni J2 njema tujenge ndoa zetu tena........

      kesho nitamtumia msg, kila baada ya saa moja msg moja
      gfsonwin likes this.

    13. #11
      gfsonwin's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 12th April 2012
      Posts : 10,729
      Rep Power : 27101
      Likes Received
      10088
      Likes Given
      14003

      Default Re: ni J2 njema tujenge ndoa zetu tena........

      Quote By BADILI TABIA
      kesho nitamtumia msg, kila baada ya saa moja msg moja
      BADILI TABIA lakin umeaha kujiuliza ama kutafakari juu ya hili? yaani kuna watu wengine hata zawadi tu akipewa hakuna asante wala nini wakati kuna mtu akipewa leso tu anaikumbuka milele na kuheshimu. ifike mahali tuache kuzoena tuish kama marafiki katika mahusiano yetu

    14. #12
      cartura's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 13th August 2009
      Location : Bongo
      Posts : 3,053
      Rep Power : 2726
      Likes Received
      747
      Likes Given
      6

      Default

      Quote By gfsonwin
      BAK hizi dedication kila siku n huku jf unatuma je mkeo umeshamtumia? leo ni siku ya kulea ndoa jamani. hebu dedicate kwa mkeo huko.
      na mimi nikuulize kitu gfsonwin (ingawa wewe si mmoja wao teh teh teh), hivi yale maneno matamu in form of 'intimate' flirts yanayomwagwa humu ndani yangeelekezwa angalau siku moja moja kwa spouses, mahusiano yasingeboreshwa kweli? maana nyumbani mtu kanuna siku nzima, akiingia JF anajimwaga mwanzo mwisho...
      gfsonwin likes this.

    15. #13
      Eiyer's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th April 2011
      Posts : 8,909
      Rep Power : 6889
      Likes Received
      2734
      Likes Given
      34

      Default Re: ni J2 njema tujenge ndoa zetu tena........

      Bado nitakuwa palepale.Unapovutwa na mwili wa mtu na kuanzisha uhusiano au ndoa haya ndo matokeo yake.Narudia kusema tena haya ni matokeo ya kutafuta mwenza/mpenzi kwa vigezo vya mwilini visivyokua na mashiko kama rangi,pesa,kimo n.k.Unapoanzisha mahusiano kwa kigezo cha ubinadamu hauwezi kumchoka wala kumzoea.Wewe unampima na kumwangalia kwa ubinadamu wake sio,rangi au hips,rangi au hips zinapofade ndipo matatizo ya kuchokana yanapokuja!
      Dotworld and gfsonwin like this.

    16. #14
      Young Master's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 22nd December 2008
      Location : Arusha, Tanzania.
      Posts : 6,127
      Rep Power : 7422
      Likes Received
      2095
      Likes Given
      1489

      Default Re: ni J2 njema tujenge ndoa zetu tena........

      Quote By gfsonwin
      wapendwa wana mmu. habari za jumapili? natumai ni njema sana kwani wengine mko kwenye sherehe za vipaimara na wengine mko na mechi ya spain na italy. yote ni heri tu katika kujipa raha.

      Leo nimekuja tena na mada hapa nataka tuidadavue kuhusu mahusiano yetu na wenzi wetu.
      Hivi ni kwanini wapenzi tunazoeana sana kiasi kwamba tunashindwa kabisa kudumisha mapenzi yetu? kwa nini inakuwepo dhana ya kuzoeana sana kuliko pitiliza kunakopelekea kuona mwenzi wangu ni mtu wa kawaida tu?

      mathalani mama/binti akishakaa na mwenzi wake baada ya muda hakuna tena hata kuflirt nae, akimtumia sms kama ni mchana basi ni ile ya kawaida tu ambayo haionyeshi kujali au haimuhamasishi mpenzi wako. Pia na wanume nao hivyo hivyo. kwanini?

      miye kungwi wenu kwa usukununu wangu nimegundua kuwa wanaotuibia wapenzi wetu wako makini sana mara zote anatuma sms kwa mpenzi kumbembeleza, kumsifia na wengine wanakumbushia hata mchezo walivyofaidi ili hali sisi tulioko ndani tumekaa kimya tunajua ni wangu tu, kwanini nimvizie na manati....lol jamani turudi nyuma tena tuanze kuweka vizuri mapenzi yetu.


      mwenye masikio na asikie neno hili.
      Dah!!! Isee mada tamu hii hadi nimejilamba vidole. Ni kweli kabisa usemayo gfsonwin. Watu wengi baada ya kuingia katika ndoa husahau kuwapa wapenzi wao mambo motomoto na mapenzi ambayo alikuwa akimpa kipindi cha nyuma kabla hawajaoana. Hali hii inaweza kusababisha kupungua kwa mapenzi kati yao na kutoa mwanya wa watu wengine kuweza kuingilia na kuharibu ndoa yao. Kwa utafiti niloufanya mimi nimebaini kuwa hali hii inasababishwa na mambo mawili makuu;
      • Kujisahau - Hili ni jambo kuu la kwanza ambalo linasababisha hali hii kutokea. Wengi mara baada ya kuingia katikaa ndoa hujisahau kana kwamba wamefika na hakuna yoyote anayeweza kutenganisha ndoa yao. Pia majukumu ya uzazi na kazi huchangia pia kujisahau hali ambayo hutoa mwanya mkubwa wa mmoja wapo kuweza kutoka nje ya ndoa na kwenda kutafuta kile ambacho ulikuwa unampa zamani na mabacho anakimiss kwa sasa. Nadhani na hii pia hutokana na hii dhana ya kuogopana kwa sababu wengi wetu baada ya kuingia katika ndoa ule uwazi na ukweli mbao tulikuwa nao kabla ya kuingia katika ndoa unaondoka na kuendekeza uoga wa kumuogopa kumueleza mwenzi wako pale anapokosea au kujisahau na badala yake kuamua kutoka nje na kuhangaika kutafuta kile ambacho unakihitaji wakati kama ungekuwa muwazi kitu hicho hicho ungeweza kukipata kwa mume wako.
      • Kuchokana - Hali hii pia huweza kutokea pale wanandoa wanapoanza kuchokana hasa kwa wanawake ambao ambao mara nyingi hukosa mapenzi ya dhati kutoka kwa waume zao hasa pale baada ya kujifungua ambayo husababisha kupoteza umbile lake la ki usichana la zamani alilokuwa nalo ambalo likuwa likimvutia mume wake na kuwa umbo jipya la kimama ambalo kiukweli wanaume wengi huwa hatulipendi. Kuchokana huku kunsababishwa na interest au mambo ambayo yalikuvutia kwa mpenzi wako kabla hamjaona. Mfano: Kama kilichokuvutia kutoka kwa mpenzi wako hadi ukampenda ni umbo lake bila shaka akija kulipoteza mapenzi kwake yatapungua kwa sababu kile kilichokuwa kinaudatisha moyo wako hakipo tena.
      gfsonwin likes this.
      Advertise your products, business & services with us 100% free |www.globaladverts.biz

    17. #15
      gfsonwin's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 12th April 2012
      Posts : 10,729
      Rep Power : 27101
      Likes Received
      10088
      Likes Given
      14003

      Default Re: ni J2 njema tujenge ndoa zetu tena........

      Quote By Young_Master
      Dah!!! Isee mada tamu hii hadi nimejilamba vidole. Ni kweli kabisa usemayo gfsonwin. Watu wengi baada ya kuingia katika ndoa husahau kuwapa wapenzi wao mambo motomoto na mapenzi ambayo alikuwa akimpa kipindi cha nyuma kabla hawajaoana. Hali hii inaweza kusababisha kupungua kwa mapenzi kati yao na kutoa mwanya wa watu wengine kuweza kuingilia na kuharibu ndoa yao. Kwa utafiti niloufanya mimi nimebaini kuwa hali hii inasababishwa na mambo mawili makuu;
      • Kujisahau - Hili ni jambo kuu la kwanza ambalo linasababisha hali hii kutokea. Wengi mara baada ya kuingia katikaa ndoa hujisahau kana kwamba wamefika na hakuna yoyote anayeweza kutenganisha ndoa yao. Pia majukumu ya uzazi na kazi huchangia pia kujisahau hali ambayo hutoa mwanya mkubwa wa mmoja wapo kuweza kutoka nje ya ndoa na kwenda kutafuta kile ambacho ulikuwa unampa zamani na mabacho anakimiss kwa sasa. Nadhani na hii pia hutokana na hii dhana ya kuogopana kwa sababu wengi wetu baada ya kuingia katika ndoa ule uwazi na ukweli mbao tulikuwa nao kabla ya kuingia katika ndoa unaondoka na kuendekeza uoga wa kumuogopa kumueleza mwenzi wako pale anapokosea au kujisahau na badala yake kuamua kutoka nje na kuhangaika kutafuta kile ambacho unakihitaji wakati kama ungekuwa muwazi kitu hicho hicho ungeweza kukipata kwa mume wako.
      • Kuchokana - Hali hii pia huweza kutokea pale wanandoa wanapoanza kuchokana hasa kwa wanawake ambao ambao mara nyingi hukosa mapenzi ya dhati kutoka kwa waume zao hasa pale baada ya kujifungua ambayo husababisha kupoteza umbile lake la ki usichana la zamani alilokuwa nalo ambalo likuwa likimvutia mume wake na kuwa umbo jipya la kimama ambalo kiukweli wanaume wengi huwa hatulipendi. Kuchokana huku kunsababishwa na interest au mambo ambayo yalikuvutia kwa mpenzi wako kabla hamjaona. Mfano: Kama kilichokuvutia kutoka kwa mpenzi wako hadi ukampenda ni umbo lake bila shaka akija kulipoteza mapenzi kwake yatapungua kwa sababu kile kilichokuwa kinaudatisha moyo wako hakipo tena.
      sasa Young_Master hapa pana jambo la maana sana umelizungumzia kuhusu kuchokana..........ni sawa labda umbo la kimama limeniharibu na kuwa baya, au hata wewe limekuharibu ukawa mbaya. sasa kama katikati yetu tukawa na desturi ya kuambiana maneno matamu kila mara pasipo kujali hayo tena yenye kuchochea hisisa za mapenzi unafikir ni rahisi sana kwa wewe kuondoa mawazo yako juu ya mpenzi wako?

      kuna kitu ambacho mimi nimekianyia utafiti, % kubwa ya watu niliwah kusuluhisha ndoa zao kuna mtu kaingilia katikati. na mara nyingi sana kati ya ndoa 10 mathalan 8 kati yake ni wanaume ndioa wenye mtu wa pemben na wanawake ni 2 tu, hapa palinifanya nianze darasa la tofauti kabisa na wababa.

      huwez ukaamini mara zote nikiongea na mbaba privately kwann anatoka nje anakwambia sitamania lakin huyu binti ananizid maarifa. kila mara sms nzuri za mahaba mpaka najikuta nadindisha. ukweli niliingiwa na hofu sana juu ya maisha yetu sisi akuna mama nikaona jinsi ambavyo tumejiachia na kubweteka na kazi za kulea tu pasi kutafuta pia amani ya nyumbani kwako. hakuna uchawi katika hili mchawi ni sisi wenyewe wanandoa.
      Young Master likes this.

    18. #16
      gfsonwin's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 12th April 2012
      Posts : 10,729
      Rep Power : 27101
      Likes Received
      10088
      Likes Given
      14003

      Default Re: ni J2 njema tujenge ndoa zetu tena........

      Quote By Eiyer
      Bado nitakuwa palepale.Unapovutwa na mwili wa mtu na kuanzisha uhusiano au ndoa haya ndo matokeo yake.Narudia kusema tena haya ni matokeo ya kutafuta mwenza/mpenzi kwa vigezo vya mwilini visivyokua na mashiko kama rangi,pesa,kimo n.k.Unapoanzisha mahusiano kwa kigezo cha ubinadamu hauwezi kumchoka wala kumzoea.Wewe unampima na kumwangalia kwa ubinadamu wake sio,rangi au hips,rangi au hips zinapofade ndipo matatizo ya kuchokana yanapokuja!
      Eiyer nisawa kabisa kuwa maisha ndivyo yanavyo paswa kuwa kwamba tupende kwa dhati. na hli halina mjadala kwamba utapenda kwa dhati kabisa.

      nikuulize mfano juzi dada mamuu aliandika comment juu ya kuchungulia mshedede ukitoka na kuingia kunako wakati wa tendo na aka justfy kabisakwamba kwake yy ile ndio starehe kubwa. unakumbuka wewe ulicomment nini? kuwa umeskia baridi. mwili mzima, pia kuna siku uliwa kuniuliza nimevaa nite dress nikakujibu kuwa ndiyo, na kukuelezea jins ilivyokaa, unakumbuka ulicomment nini? bora nimeiona hii post asbh ningeiona usiku ingenoharibia usiku wangu.

      based on these things eiyer maisha yana tricky sana. kama tu maandsh yanakufanya unadata basi kuna mwingine ukikutana naye tu waweza kujikuta umeanguka dhambini. kuna watu wanamvuto acha kabisa na hapa siyo uzuri huu bali ni mvuto tu ukimuona tu lazima utamani kwenda naye kunako 6*6.

      mtu wa aina hii iwapo usipo kuwa makin waweza kujikuta umeanguka dhambini na yeye huwa ana maneno matamu hadi balaa.

    19. #17
      gfsonwin's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 12th April 2012
      Posts : 10,729
      Rep Power : 27101
      Likes Received
      10088
      Likes Given
      14003

      Default Re: ni J2 njema tujenge ndoa zetu tena........

      Quote By cartura
      na mimi nikuulize kitu gfsonwin (ingawa wewe si mmoja wao teh teh teh), hivi yale maneno matamu in form of 'intimate' flirts yanayomwagwa humu ndani yangeelekezwa angalau siku moja moja kwa spouses, mahusiano yasingeboreshwa kweli? maana nyumbani mtu kanuna siku nzima, akiingia JF anajimwaga mwanzo mwisho...
      umeoina hiyo eeh! lkn hii kwa sisi wana physikia tunaita minimum factor of safety kama mwandisi utakuwa umenisoma. ile some flirting huwa ni kali sana best lakin ndipo mtu anapotolea uvivu wake au wengine wapo wasubirie hayo maneno matam wakacopy na kupaste kwa spouses wao.

    20. #18
      gfsonwin's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 12th April 2012
      Posts : 10,729
      Rep Power : 27101
      Likes Received
      10088
      Likes Given
      14003

      Default Re: ni J2 njema tujenge ndoa zetu tena........

      Lakini pia wana mmu tusisahau kuwa mapenzi ya nje yananoga sana kwakua huyu muusika na mpenzi wake they dont meet oftenly, wao watakutana once in a week, ila kila siku wanabembeleza na sms kali na tamu. so wakikutana kila siku ni wapya ni stresses, hakuna kununiana ni full shangwe tu na hata game inakuwa surperb , kwani kila mmoja ana hamu na mwenziye na wamedumu wk nzima wakinyegeshana.

      ila sisi tulioko ndani tunaonana kila siku, makosa tunatendeana wakati huo huo wavivu wa kunyegeshana lolest tunategemea nn? tujali hata kuwa innovative zaid basi tuyafanye mahusino kuwa bora zaid tutoke siku moja moja twende tukalale hotelin just tufanye ya kwetu tu, tupeane raha ili hao wanaomndea wenzi wetu washindwe.

      siku muanze menzio mkumbushie basi hata kalekamchezo kama kalikuwa katam au pale alipokufikisha mwambie uone jinsi atakavyo badilika....wanao toka mchana maofisi kwenda gesti ukiwauliza sababu wata kwambia. wengine wamenyegeshana hadi basi sasa inabidi waibe dk chache waende kwa faragha wamalize hamu yao. akirudh ome mwenzio mwepesii wala hujui kumbe kesha jisevia muda mrefu tu.

    21. #19
      Eiyer's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th April 2011
      Posts : 8,909
      Rep Power : 6889
      Likes Received
      2734
      Likes Given
      34

      Default Re: ni J2 njema tujenge ndoa zetu tena........

      Quote By gfsonwin
      Eiyer nisawa kabisa kuwa maisha ndivyo yanavyo paswa kuwa kwamba tupende kwa dhati. na hli halina mjadala kwamba utapenda kwa dhati kabisa.

      nikuulize mfano juzi dada mamuu aliandika comment juu ya kuchungulia mshedede ukitoka na kuingia kunako wakati wa tendo na aka justfy kabisakwamba kwake yy ile ndio starehe kubwa. unakumbuka wewe ulicomment nini? kuwa umeskia baridi. mwili mzima, pia kuna siku uliwa kuniuliza nimevaa nite dress nikakujibu kuwa ndiyo, na kukuelezea jins ilivyokaa, unakumbuka ulicomment nini? bora nimeiona hii post asbh ningeiona usiku ingenoharibia usiku wangu.

      based on these things eiyer maisha yana tricky sana. kama tu maandsh yanakufanya unadata basi kuna mwingine ukikutana naye tu waweza kujikuta umeanguka dhambini. kuna watu wanamvuto acha kabisa na hapa siyo uzuri huu bali ni mvuto tu ukimuona tu lazima utamani kwenda naye kunako 6*6.

      mtu wa aina hii iwapo usipo kuwa makin waweza kujikuta umeanguka dhambini na yeye huwa ana maneno matamu hadi balaa.
      Wakati najibu yale majibu yote mawili sikuwa siriouz,ila labda nikuambie jambo moja mpaka mwili wako univute kufanya ngono jua nimeamua.hivyo hayo mambo ya mwili kwangu hayana nafasi kabisa.Huu ni ukweli na kwenye hili niko SIRIAZ!
      gfsonwin likes this.

    22. #20
      gfsonwin's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 12th April 2012
      Posts : 10,729
      Rep Power : 27101
      Likes Received
      10088
      Likes Given
      14003

      Default Re: ni J2 njema tujenge ndoa zetu tena........

      Quote By Eiyer
      Wakati najibu yale majibu yote mawili sikuwa siriouz,ila labda nikuambie jambo moja mpaka mwili wako univute kufanya ngono jua nimeamua.hivyo hayo mambo ya mwili kwangu hayana nafasi kabisa.Huu ni ukweli na kwenye hili niko SIRIAZ!
      umesema vizuri sana Eiyer, hapo kwenye red believe it or not unaweza kuamua kufanya hivyo kwa watu wengi utakavyo tena hakuna kitu cha kijinga kama moyo kwa maamuzi ya kipuuzi kabisa na akili ikatii, maamuzi ya moyo au nafsi yako.

      Ila pia ukiamua kwa dhati, na kuona kuwa napata kila nitakacho na siboreki na haya maishsa yangu ya ndoa. you can.

    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...