Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Kwa walioko kwenye ndoa, mawazo yenu please

    Report Post
    Page 2 of 2 FirstFirst 12
    Results 21 to 38 of 38
    1. #1
      bornagain's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th January 2012
      Location : Nyakanazi - Biharamulo
      Posts : 1,767
      Rep Power : 726
      Likes Received
      480
      Likes Given
      353

      Default Kwa walioko kwenye ndoa, mawazo yenu please

      Jamani mimi ni kijana wa kiume nimeoa miezi mitatu iliyopita, naomben wadau mnisaidie kina jambo linanitatiza. Mimi kwetu ni Dar es Salaam na wazazi wangu wanakaa Dar es Salaam. Lakini mke wangu yeye kwao ni mkoani na wazazi wake wanaishi huko mkoani. Swali langu ni hili, hivi naweza kwenda nyumbani kuwasalimia wazazi wangu bila kuwa na mke wangu mfano nimetoka kazini halafu nikapitia nyumbani then nikamwambia mke wangu kuwa nimepitia kwetu, hiyo itakua mbaya au inatakiwa kila nikienda nyumbani niwe na mke wangu au nimfahamishe mapema kabla ya safari? Naombeni ushauri wenu na namna ya kuhandle hili suala maana mimi bado mchanga kwenye ndoa.
      There is a saying in aviation "You haven't crashed until you've crashed. Until then, keep flying the plane".


    2. #21
      Geofrey_1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th February 2012
      Posts : 271
      Rep Power : 484
      Likes Received
      30
      Likes Given
      2

      Default Re: Kwa walioko kwenye ndoa, mawazo yenu please

      Quote By bornagain View Post
      Jamani mimi ni kijana wa kiume nimeoa miezi mitatu iliyopita, naomben wadau mnisaidie kina jambo linanitatiza. Mimi kwetu ni Dar es Salaam na wazazi wangu wanakaa Dar es Salaam. Lakini mke wangu yeye kwao ni mkoani na wazazi wake wanaishi huko mkoani. Swali langu ni hili, hivi naweza kwenda nyumbani kuwasalimia wazazi wangu bila kuwa na mke wangu mfano nimetoka kazini halafu nikapitia nyumbani then nikamwambia mke wangu kuwa nimepitia kwetu, hiyo itakua mbaya au inatakiwa kila nikienda nyumbani niwe na mke wangu au nimfahamishe mapema kabla ya safari? Naombeni ushauri wenu na namna ya kuhandle hili suala maana mimi bado mchanga kwenye ndoa.
      ongea na mkeo uone yeye analichukuliaje hilo, vunja ukimya zungumza na mwenzio
      bornagain likes this.
      !!gams "G" baby!!

    3. #22
      KipimaPembe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th August 2007
      Posts : 785
      Rep Power : 768
      Likes Received
      347
      Likes Given
      131

      Default Re: Kwa walioko kwenye ndoa, mawazo yenu please

      Ameshasema kwa waliooa tu; halafu mtu anaingia anasema "ingawa mimi sijaoa ........". Huku ni kutomtendea haki mwenye maada. Yeye anataka waliooa tu waseme! Wale ambao hamjaoa, kaeni kimya, msikilize waliooa wanasema nini; nafasi yenu ipo!

      Ukishaoa au kuolewa, surprises huwa si kitu kizuri. Kifupi ni kuwa ukienda sehemu ambayo mwenzio hajui kuwa umekwenda huko ni vizuri umtaarifu, jamani technolojia inaruhusu. Zamani enzi za barua na simu za waya tu ilikuwa vigumu, ila sasa ni rahisi, kwa nini usimtip mwenzio kuwa unapitia kwa dingi wako?

      Kupita pita huko mara kwa mara peke yako kuna mpa wasi wasi mwenzio kuwa pengine una mambo unajadili na wazazi wako ambayo hutaki yeye ajue. Hizi perceptions kwenye ndoa ni kitu kibaya sana na kinaleta wasi wasi usio na msingi. Mwambie mwenzio nitapitia kwa wazee.

      Kupita pita huko vile vile peke yako kunamfanya mwenzio aonekane yeye hawajali wazee wako. Mbona wewe wapita yeye haji? Wale wazazi wako wanaweza kufikiri kuwa unaenda peke yako sababu hutaki kufuatana na mkeo.

      Kifupi ni mengi sana ya hisia tu, ila yana matokeo mabaya. Mwambie kuwa utapita huko, kama ana nafasi naye aungane nawe!
      bornagain likes this.

    4. #23
      jc--'s Avatar
      Member Array
      Join Date : 3rd February 2012
      Posts : 87
      Rep Power : 389
      Likes Received
      12
      Likes Given
      14

      Default Re: Kwa walioko kwenye ndoa, mawazo yenu please

      Quote By Eiyer View Post
      Kwanza siko kwenye ndoa so sidhani kama naweza ruhusiwa changia hapa!
      Ilibidi usijibu chochote kabisa, ingebidi hata usingefungua hii thread..

    5. #24
      Prime Dynamics's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th December 2010
      Location : Kamachumu
      Posts : 292
      Rep Power : 487
      Likes Received
      119
      Likes Given
      21

      Default Re: Kwa walioko kwenye ndoa, mawazo yenu please

      Mimi nadhani unamtafutia balaa mke wako. Majukumu ya familia yako yakiaanza kubana ukisha pata mtoto automatically hizo safari kwa wazazi zitapungua kwa asilimia kubwa sana. Then results zake zinaweza kuwa mbaya itasemekana kwamba mke wako ameanza kuzuia then kitakacho fuata mke wako hatokuwa in good terms na wakwe zake. Pangilia safari zako you have to get used to it ndio maana ukawaacha wazi wako ukambatana na mkeo. Also kumbuka wazi wako pia waliwaacha wazazi wao.
      Our regrets in life are not those decisions we took and they turned out wrong, but rather those we did not take.

    6. #25
      Freema Agyeman's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd March 2011
      Posts : 1,706
      Rep Power : 4182
      Likes Received
      1076
      Likes Given
      892

      Default Re: Kwa walioko kwenye ndoa, mawazo yenu please

      Live your lives guys
      "The louder the protester, the more there is in their closet"


    7. #26
      mapanga3's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 1st May 2012
      Posts : 208
      Rep Power : 401
      Likes Received
      26
      Likes Given
      2

      Default Re: Kwa walioko kwenye ndoa, mawazo yenu please

      wazazi wako.wanajua kuwa unakwako hivyo ni vyema.safari za nyumbani kwenu zipungue. Mkeo ni mtu muhimu sana na karibu kuliko yoyote mpe nafasi aone umuhimu wake kwako, pangani pamoja kutembelea wazazi wa pande zote, tangu ulipooa mkeo ndiyo mtu wa kwanza kwako, ni vizuri mnapotembelea wazazi muwe pamoja tena muwe na kiasi isiwe mara kwa mara.

    8. #27
      bornagain's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th January 2012
      Location : Nyakanazi - Biharamulo
      Posts : 1,767
      Rep Power : 726
      Likes Received
      480
      Likes Given
      353

      Default Re: Kwa walioko kwenye ndoa, mawazo yenu please

      Guys I am really overwhelmed for your comments and contributions, kweli Jamii Forums ni kila kitu ,ntazingatia michango yote na naamini hakuna kitakachoharibika, asanteni sana na Mungu awabarikini kwa michango yenu mizuri

      There is a saying in aviation "You haven't crashed until you've crashed. Until then, keep flying the plane".

    9. #28
      jamiif's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th April 2012
      Posts : 957
      Rep Power : 551
      Likes Received
      242
      Likes Given
      513

      Default Re: Kwa walioko kwenye ndoa, mawazo yenu please

      habari kaka. Mimi ushauri wangu katika suala hili ni kuwa, hata kama huendi na mke wako kwa wazazi wako, ni muhimu KUMPA TAARIFA yaani awe anajua kuwa umepitia kwa wazazi wako. Unajua kaka, katika hiyo hiyo ndoa, kila mmoja wenu anatakiwa awe anafanya kitu kwa mwenzake ambacho hata yeye anapenda, yaani hapa namaanisha hata ingekuwa ni yeye wazazi wake wanaishio hapa dar, WEWE USINGEPENDA akapitia kwao huko BILA kukupa wewe taarifa... kwa sisi waislam, hata ukienda msikitini unatakiwa umpe taarifa mwenzako awe na taarifa zako. Sasa kama unaenda bila kumjulisha halafu unapata matatizo njiani kwa namna yeyote ile, ndio utaanza kumtafuta au?hatuombei hayo ila tunatakiwa kufikiria kwa upande wa pili pia. UWE UNAMUAGA/KUMPA TAARIFA na ARIDHIE, ndio uendelee na safari zako. Ni hayo tu.
      Quote By bornagain View Post
      Jamani mimi ni kijana wa kiume nimeoa miezi mitatu iliyopita, naomben wadau mnisaidie kina jambo linanitatiza. Mimi kwetu ni Dar es Salaam na wazazi wangu wanakaa Dar es Salaam. Lakini mke wangu yeye kwao ni mkoani na wazazi wake wanaishi huko mkoani. Swali langu ni hili, hivi naweza kwenda nyumbani kuwasalimia wazazi wangu bila kuwa na mke wangu mfano nimetoka kazini halafu nikapitia nyumbani then nikamwambia mke wangu kuwa nimepitia kwetu, hiyo itakua mbaya au inatakiwa kila nikienda nyumbani niwe na mke wangu au nimfahamishe mapema kabla ya safari? Naombeni ushauri wenu na namna ya kuhandle hili suala maana mimi bado mchanga kwenye ndoa.

    10. #29
      Arvin sloane's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th July 2011
      Posts : 889
      Rep Power : 578
      Likes Received
      131
      Likes Given
      40

      Default Re: Kwa walioko kwenye ndoa, mawazo yenu please

      Quote By Jestina View Post
      mie nahisi umeoa ukiwa mdogo sana,maswala mepesi kama hayo yanakushinda kufanya maamuzi,je yakija mazito si utakufa kwa pressure?
      Mi nadhani kila jambo kama kuna uwezekano wa kuomba ushauri ni bora uombe alf mwisho wa siku unaatoa maamuzi kuzingatia ushauri uliopewa hata kwa masuala mazito.
      bornagain likes this.

    11. #30
      jeromyeddy's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 27th February 2012
      Posts : 3
      Rep Power : 0
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Kwa walioko kwenye ndoa, mawazo yenu please

      hilo swali hukustahili kulilta humu kwani linahitaji akili kidogo sana. wewe umeoa, that means wewe na mke ni kitu kimoja. but suala la kwenda nymbani kwenu lisiwe kisingizio cha kila siku ukitoka kazini.

      kama kuna ulazima wa kupita nyumbani then unaweza kwenda bila wasiwasi ila ni vyema ukamjulisha mkeo kua ukitoka kazini utapita kwenu as kuna ishu inayokupeleka huko.

      Mara nyingine funga safari wewe na mkeo muende wote kwa wazazi wako na pia hata wazazi wake. ila mjenge mazoea pia ya kwenda kuwasilimia wazazi wako mara kwa mara kwani nae ni mmoja wa familia yenu kwa sasa.

    12. #31
      mtotowamjini's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd April 2012
      Location : None of Your Business
      Posts : 4,542
      Rep Power : 1269
      Likes Received
      1109
      Likes Given
      29

      Default Re: Kwa walioko kwenye ndoa, mawazo yenu please

      kusalimia mara moja moja sio mbaya but usifanye tabia..maana baada ya mda mke ataanza kumaindi...
      Every saint has a past, every sinner has a future' ...Oscar Wilde

      One man's good fortune is another man's misfortune


    13. #32
      bombu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th June 2011
      Posts : 1,038
      Rep Power : 882
      Likes Received
      497
      Likes Given
      592

      Default Re: Kwa walioko kwenye ndoa, mawazo yenu please

      Quote By Eiyer View Post
      Kwanza siko kwenye ndoa so sidhani kama naweza ruhusiwa changia hapa!
      Ndo ushachangia ivoo
      Knowledge is knowing that a tomato is a fruit, but Wisdom is knowing not to put it in a fruit salad

    14. #33
      Angel Msoffe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st June 2011
      Posts : 6,358
      Rep Power : 1848
      Likes Received
      1412
      Likes Given
      0

      Default Re: Kwa walioko kwenye ndoa, mawazo yenu please

      Usiende mwenyewe Hebu jaribu kwenda na mkeo kwa wazazi japo weekend mojamoja kuepusha lawama na manung'uniko yasiyo na lazima. Umeoa maana yake ni umekua mambo ya kufatanafatana na wazazi kila dakika si mazuri.

    15. #34
      MWananyati's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 3rd February 2011
      Posts : 123
      Rep Power : 448
      Likes Received
      31
      Likes Given
      48

      Default Re: Kwa walioko kwenye ndoa, mawazo yenu please

      Mimi nijuavyo akishakua na familia yako wewe mtoto wa kiume yabidi uwe ni mtu wa msimamo. Na kitu kimoja kinachoangaliwa ni uwezo wa kujitegemea - kiuamuzi.

      Kwenda kusalimia wazazi sio mbaya, ila ni mara ngapi unaenda kusalimia? yaan unaenda kwa mdingi wako afu mwapiga stori mwishowe wawaambia nilipita tu kimtindo kuwacheki? itakushushia hadhi yako wewe kijana. either wanaweza kufikiri una tatizo kwe familia yako ila kusema unashindwa au you are not grown up.

      na usipomwambia mkeo kuwa umepita kwenu, baadae mkweo akampigia simu kumwambia kuwa ulikuwepo kule, jua hapo unatengeneza ugomvi mwingi ne kwa mama watoto-kuwa kule kwa wazazi ulifuata nini bila kumshirikisha?

      na isitoshe sio kila mara lazima ukutane na wazazi wako wote. waweza kumita m-sure sehemu mkapiga stori, then kila mtu akachukua hamsini zake. na hii itakua na maana sana kuliko kuwa hukauki nyumbani kwao.

      KIufupi, Ndoa huwa inathibitisha maturity yako. sasa jiulize a matured person anatakiwa a-behave vp?

    16. #35
      GodfreyTajiri's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th September 2010
      Posts : 563
      Rep Power : 555
      Likes Received
      80
      Likes Given
      63

      Default Re: Kwa walioko kwenye ndoa, mawazo yenu please

      ukipita kila siku/mara kwa wazazi wako unaweza mpa hisia mwenzi wako kwamba maamuzi yako mengi
      yanatoka kwa wazazi wako, hivyo mkitofautiana kidogo tu na mkeo lawama zinaweza angukia kwa wazazi
      wako. hivyo epukana na trip za mara kwa mara kwa wazazi wako.

      jee wazazi wa mkeo wangekuwa na wao wapo hapo mlipo utafurahia mkeo akiwa kila siku anashinda kwa
      wazazi wake?
      “Unless power is legitimate there can be no social order“
      P. F. Drucker

    17. #36
      Crucial Man's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th January 2011
      Posts : 1,350
      Rep Power : 698
      Likes Received
      272
      Likes Given
      16

      Default Re: Kwa walioko kwenye ndoa, mawazo yenu please

      asubui unapotoka home mwambie,honey leo ntapitia home kuwapa hi.aki obligate then pospone mpange siku muende wote.au kama vp mjulishe kwa njia ya simu kwamba unapitia home kuwapa hi.

    18. #37
      BlackBerry's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd March 2011
      Location : Down Town
      Posts : 1,840
      Rep Power : 786
      Likes Received
      919
      Likes Given
      701

      Default Re: Kwa walioko kwenye ndoa, mawazo yenu please

      punguza safari za nyumbani za mara kwa mara, na kuna siku unaweza pita pia ukampa taarif, ni namna tu ya nyie mlivyozoea, sie tuna mfanyakazi mwenzetu mwanaume, hata tukisema tukapate lunch mje ya ofisi anainu simu utasikia naenda kula nje ya ofisi niko na blackberry,nokia, kimchina nk, nashangaa kweli, mi hapo wala sisemi wakati mie mwanamke,mahusiano ni nyie wenyewe mlivyojipangia
      Simple Look But Tough in Wallet

    19. #38
      mdida's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th July 2011
      Location : Middle East
      Posts : 487
      Rep Power : 498
      Likes Received
      217
      Likes Given
      100

      Default Re: Kwa walioko kwenye ndoa, mawazo yenu please

      ni vizuri ukimtaarifu mkeo ili kuepuka maswali yasiyokuwa na majibu

    Page 2 of 2 FirstFirst 12

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...