Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Usilipize kisasi!!!!!!!!!!!

    Report Post
    Results 1 to 14 of 14
    1. #1
      Jpinduzi's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 26th February 2011
      Posts : 135
      Rep Power : 448
      Likes Received
      60
      Likes Given
      8

      Post Usilipize kisasi!!!!!!!!!!!


      Kuna hasara zinazoweza kukupata ukiamua kulipa kisasi kwa mambo uliyofanyiwa ambayo hayakupendezi. Ikiwa ni masuala ya kikabila, usilipe kisasi. Ikiwa ni masuala ya kidini, usilipe kisasi. Ikiwa ni masuala ya kifamilia, usilipe kisasi. Ikiwa ni masuala ya kikazi, usilipe kisasi. Ikiwa ni masuala ya uhusiano wako na majirani zako, usilipe kisasi.Ndiyo! Usilipe kisasi! Kwa nini? Kwa sababu"imeandikwa kisasi ni juu yangu Mimi; Mimi nitalipa, anena Bwana".
      Lakini ikiwa utaona ya kuwa Mungu hawezi kukusaidia na ukaamua kujichukulia madaraka ya kujilipiza kisasi hasara zifuatazo hakika zitakupata!

      Hasara ya Kwanza:
      UTASHINDWA!
      Katika jambo lolote lile lililokukasirisha - liwe la kidini, au kikabila, au kifamilia, au kikazi, na kadhalika ukiamua kulipa kisasi utashindwa wewe kwa sababu vita hivyo si vya mwili na wala silaha ambazo Mungu amekupa si za mwili! Tunasema hivi kwa sababu katika 2 Wakorintho 10:3- 5 imeandikwa hivi:"Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi yamwili; maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome, tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikra ipate kumtii Kristo".

      Tena katika kitabu cha Waefeso 6:12 imeandikwa hivi: "Kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho".
      Uwanja wa mapambano uliyonayo ni "katika ulimwengu wa roho" na mapambano uliyo nayo "si juu ya damu na nyama" - ingawa unaona ya kuwa ni watu na ni binadamu kama wewe wanaokusonga - lakini fahamu hili ya kuwa wanatumiwa tu na ibilisi!
      Mbinu mojawapo ya shetani anayotumia akitaka kukuangamiza ni kukufanyia kitu kitakachokukasirisha ili uamue kujibu au kushindana kimwili kwa sababu anajua ukishindana "kimwili" au katika mwili utashindwa hakika, maana vita hivyo si vya mwili wala silaha ambazo Mungu amekupa si za mwili!

      Hasara ya Pili:
      MATATIZO HAYATAKWISHA!
      Kumbuka imeandikwa hivi katika kitabu cha Wagalatia 6:7; "Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi; kwa kuwa chochote ampandacho mtu. Ndicho atakachovuna".
      Ikiwa umeamua kulipa kisasi kwa kumfanyia ubaya yule aliyekufanyia - ubaya hautakwisha, kwa sababu utavuna ulichopanda.Ndiyo maana imeandikwa hivi:"Yeye arudishaye mabaya badala ya mema, mabaya
      hayataondoka nyumbani mwake" (Mithali 17:13)
      Ukiamua kulipiza kisasi kwa kumfanyia ubaya yule wa nyumbani mwako - Biblia inasema "mabaya hayataondoka nyumbani mwako" Hii ndiyo maana matatizo mengi katika ndoa na katika jamii hayaishi - kwa sababu mtu akifanyiwa ubaya naye analipa kisasi.
      Ukiamua kulipa kisasi kwa kumfanyia ubaya yule wa nchini mwako ujue hakika mabaya hayataondoka nchini mwako. Hili ndilo lililowapata wenzetu wa nchi za Burundi na Rwanda - kulipizana kisasi - matokeo ni uhasama usiotaka kupotea - pamoja na juhudi zote za kimataifa kutafuta suluhisho.
      Ukiamua kulipa kisasi kwa kumfanyia ubaya yule wa kazini kwako - fahamu mabaya hayataondoka kazini kwako. Ikiwa ni shuleni - mabaya hayataondoka hapo shuleni.
      Tena hali ya mwisho inakuwa mbaya zaidi,kila wakati kisasi kinapoendelea kupandwa. Kwa sababu ukiwapa watu ubaya - nawe utapewa ubaya kwa; "kipimo cha kujaa na kushidiliwa, na kusukwa - sukwa - hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile upimacho ndicho mtakachopimiwa (Luka 6:38)
      Kumbuka ubaya haushindwi na ubaya mwingine, bali unashindwa na wema - kama vile dawa ya chuki si chuki bali upendo! Ndiyo maana Warumi 12:21 inasema; "Usishindwe na ubaya, bali uushinde ubaya kwa wema".

      Hasara ya Tatu:
      UNAMZUIA MUNGU KUKUPIGANIA
      Unaweza ukashangaa, lakini ndivyo ilivyo! Ukiamua kulipa kisasi juu ya tatizo ulilonalo - unamzuia Mungu asikusaidie kulitatua.Mungu hawezi kukusaidia kwa sababu imeandikwa "msijilipize kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya Mungu; maana, imeandikwa, kisasi ni juu yangu mimi; mimi nitalipa, anena Bwana".
      Neno "ipisheni" limeandikwa kwa sababu kulipa kisasi "kunazuia" ghadhabu ya Mungu isipigane upande wako! Tena si hivyo tu lakini ukilipa kisasi unaingilia kazi ambayo si yako! Ni kazi ya Mungu maana anasema "Kisasi ni juu yangu mimi; mimi nitalipa, anena Bwana" Ikiwa kisasi ni juu ya Mungu kulipa, basi huhitaji wewe kulipa. Je, tunakwenda pamoja katika hili?
      Hatua yako ya kulipa kisasi inazuia mkono wa Mungu kukupigania - kwa hiyo ipishe ghadhabu ya Mungu kwa kutokujilipizia kisasi!

      Hasara na Nne:
      UNAJICHUMIA DHAMBI!
      Unapoamua kulipa kisasi, unajichumia dhambi! Hii ni kwa sababu kulipa kisasi huja kwa njia ya chuki iliyojengeka ndani yako kwa ajili ya mambo mabaya uliyofanyiwa. Huwezi kulipa kisasi bila ya kumchukia huyo unayejilipizia kisasi kwake. Na Biblia inasema hivi:
      "Kila amchukiaye ndugu yake ni mwuaji: nanyi mnajuaya kuwa kila mwuaji hana uzima wa milele ukikaa ndani yake" (1 Yohana 3:15).
      Umeona hilo! Chuki huzaa kisasi, na huzaa dhambi ya kuua! Na
      Isaya 59:2b inasema; "dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia".
      Kwa hiyo kama umekwisha lipa kisasi au umekusudia moyoni mwako kulipa kisasi ni muhimuutubu ili Mungu akusamehe na mawasiliano yako na Yeye yawe mazuri.source -mwakasege.
      Masikini_Jeuri and NTINGINYA like this.


    2. #2
      NTINGINYA's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 5th October 2010
      Location : tabora
      Posts : 231
      Rep Power : 488
      Likes Received
      31
      Likes Given
      82

      Default Re: Usilipize kisasi!!!!!!!!!!!

      Jameni punguzeni kidogo mnatupa uvivu wakusoma
      mama D likes this.
      together we can heal the scars Of loves

    3. #3
      NATA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th May 2007
      Posts : 4,258
      Rep Power : 8420
      Likes Received
      1135
      Likes Given
      390

      Default Re: Usilipize kisasi!!!!!!!!!!!

      Kama mtu amekutendea kitu kibaya.
      Mimi huwa nafikilia kuwa huyo mtu hajui atendalo so
      Unamrudi kwa kumtendea lile lile ili iwe fundisho kwake kwani atagundua kuwa
      Oh kumbe halifai
      Mungu atakubariki sana kwa kuweza kumsaidia huyo jamaa asidhidi kukwaza watu na kuchuma dhambi.

      Usimtendee jirani yako kile wewe usingependa kutendewa.
      Amen!

    4. #4
      Sizinga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th October 2007
      Location : Mars
      Posts : 4,041
      Rep Power : 1457
      Likes Received
      1545
      Likes Given
      1654

      Default Re: Usilipize kisasi!!!!!!!!!!!

      Ukiwa mtu wa visasi kama Kikwete huwezi kufanikiwa. Si unaona nchi inavyoyumba hii.
      Ni ujinga kusign muswada wa katiba wakati wananchi hawana baraka nayo.
      Masikini_Jeuri and mama D like this.
      GESI KWANZA KOROSHO BAADAE!!

    5. #5
      Masikini_Jeuri's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th January 2010
      Location : Igangidung'u
      Posts : 5,953
      Rep Power : 2083
      Likes Received
      703
      Likes Given
      5039

      Default Re: Usilipize kisasi!!!!!!!!!!!

      umenena kweli.............niliwahi kutumbukia kwenye huo mtego wa kulipa kisasi; nikfanikiwa kuleta madhara zaidi ya nililotendewa lakini haikumaliza kabisa hasira niliyokuwa nayo!

      Ni upuuzi kufikiria kulipa kisasi! Ni kujiumiza na kujichumia dhambi kweli!
      24 hours in a day! 24 beers in a case, Coincidence? I think not!


    6. #6
      IGWE's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2011
      Location : Blue Plaza Building-Arusha
      Posts : 5,321
      Rep Power : 3309
      Likes Received
      1336
      Likes Given
      1241

      Default Re: Usilipize kisasi!!!!!!!!!!!

      Quote By NATA View Post
      Kama mtu amekutendea kitu kibaya.
      Mimi huwa nafikilia kuwa huyo mtu hajui atendalo so
      Unamrudi kwa kumtendea lile lile ili iwe fundisho kwake kwani atagundua kuwa
      Oh kumbe halifai
      Mungu atakubariki sana kwa kuweza kumsaidia huyo jamaa asidhidi kukwaza watu na kuchuma dhambi.

      Usimtendee jirani yako kile wewe usingependa kutendewa.
      Amen!
      Yap_na hiyo ni sheria ya manabii(Musa)...jino kwa jino,.....ahahahaahaaaaaaaa and it works in the real world.
      "We should learn to help others,not only in our prayer but also in daily life,if we cannot help them_then,the least thing we can do is to desist from harming them"

    7. #7
      Lizzy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th May 2009
      Location : UngaLTD!
      Posts : 21,403
      Rep Power : 14601
      Likes Received
      7869
      Likes Given
      1969

      Default Re: Usilipize kisasi!!!!!!!!!!!

      NTINGINYA...Kwasababu tu baadhi yenu hampendi kusoma haina maana ndo watu waandike makala zisizojitosheleza na kupoteza maana ya kile wanachoandika. Because then ujumbe wake hautafika vile anakavyotaka na hata nyie (msiopenda kusoma)mkisoma hamtapata alichokusudia hivyo ni kazi bure.....So stop complaining...Kama wewe unaesoma tu unalalamika je yeye alietumia muda wake kutafakari na kuandika hicho unachoona ni kazi sana kusoma???
      NTINGINYA and Jpinduzi like this.
      Back to reality......

      If it’s a broken part, replace it. If it’s a broken arm then brace it. If it’s a broken heart, then face it.

      Aika Rua!

    8. #8
      Mkono Mwekundu's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 24th November 2011
      Posts : 1
      Rep Power : 0
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Usilipize kisasi!!!!!!!!!!!

      Ooooo Yeah ....

    9. #9
      feis buku's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th August 2011
      Posts : 2,367
      Rep Power : 868
      Likes Received
      644
      Likes Given
      574

      Default Re: Usilipize kisasi!!!!!!!!!!!

      Quote By NTINGINYA View Post
      Jameni punguzeni kidogo mnatupa uvivu wakusoma
      mmh!! usiusemee moyo,sema unanipa uvivu na sio unatupa uvivu!!
      NTINGINYA likes this.

    10. #10
      Lizzy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th May 2009
      Location : UngaLTD!
      Posts : 21,403
      Rep Power : 14601
      Likes Received
      7869
      Likes Given
      1969

      Default Re: Usilipize kisasi!!!!!!!!!!!

      Na kuhusu kulipa kisasi mtoa mada... I prefer looking at it as teaching someone a lesson.Kuna watu ambao wanahitaji kuonyeshwa ubaya wa kile walichofanya ili wajifunze...wasiendelee kutendea wengine hivyo.Ila hii ni kama unajali atakayofanya huko mbeleni...otherwise unampotezea na kuendelea na maisha yako.Wakati mwingi hii ya pili inauma zaidi maana kama mtu alijaribu kukuangusha mahali ukampotezea na kuongeza kasi ya mafanikio yako ataishia kuumwa roho kichinichini.
      NTINGINYA likes this.
      Back to reality......

      If it’s a broken part, replace it. If it’s a broken arm then brace it. If it’s a broken heart, then face it.

      Aika Rua!

    11. #11
      NTINGINYA's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 5th October 2010
      Location : tabora
      Posts : 231
      Rep Power : 488
      Likes Received
      31
      Likes Given
      82

      Default Re: Usilipize kisasi!!!!!!!!!!!

      NTINGINYA.Nikweli maneno yako samani kwate niliowakwaza. hatahivyo nimeirejea kusoma nimefaidika








      Kwasababu tu baadhi yenu hampendi kusoma haina maana ndo watu waandike makala zisizojitosheleza na kupoteza maana ya kile wanachoandika. Because then ujumbe wake hautafika vile anakavyotaka na hata nyie (msiopenda kusoma)mkisoma hamtapata alichokusudia hivyo ni kazi bure.....So stop complaining...Kama wewe unaesoma tu unalalamika je yeye alietumia muda wake kutafakari na kuandika hicho unachoona ni kazi sana kusoma???[/QUOTE]
      Lizzy likes this.
      together we can heal the scars Of loves

    12. #12
      Nsuri's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd October 2011
      Posts : 606
      Rep Power : 511
      Likes Received
      199
      Likes Given
      141

      Default Re: Usilipize kisasi!!!!!!!!!!!

      Nimesoma heading tuu!!!
      " To be happy, we must not be too concerned with others"

    13. #13
      Lizzy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th May 2009
      Location : UngaLTD!
      Posts : 21,403
      Rep Power : 14601
      Likes Received
      7869
      Likes Given
      1969

      Default Re: Usilipize kisasi!!!!!!!!!!!

      Quote By Nsuri View Post
      Nimesoma heading tuu!!!
      Kwahiyo..........???
      Back to reality......

      If it’s a broken part, replace it. If it’s a broken arm then brace it. If it’s a broken heart, then face it.

      Aika Rua!

    14. #14
      mikatabafeki's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th December 2010
      Posts : 4,873
      Rep Power : 1408
      Likes Received
      778
      Likes Given
      1463

      Default Re: Usilipize kisasi!!!!!!!!!!!

      huuuuuuh na hvi metoka kwa office mechoka hbu nlale ntadeal nayo nkiamka
      when love goes wrong,nothing goes right.

    Similar Topics

    1. Kama huridhiki mwambie, usilipize
      By Mtambuzi in forum Mahusiano, mapenzi, urafiki
      Replies: 8
      Last Post: 25th August 2011, 00:37
    2. Usilipize baya kwa baya bali kwa jema
      By Mitchell in forum Jokes/Utani + Udaku/Gossips
      Replies: 1
      Last Post: 18th August 2011, 10:17
    3. Usilipize baya kwa baya bali kwa jema
      By Mitchell in forum Jokes/Utani + Udaku/Gossips
      Replies: 0
      Last Post: 18th August 2011, 10:06
    4. Kisasi
      By KAKA A TAIFA in forum Jokes/Utani + Udaku/Gossips
      Replies: 0
      Last Post: 25th May 2011, 16:16

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...