Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Tusisikitike sana kwa kukosa tuvipendavyo maishani.

    Report Post
    Results 1 to 9 of 9
    1. #1
      Mkwaruzo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st February 2011
      Location : Zanzibar
      Posts : 536
      Rep Power : 524
      Likes Received
      80
      Likes Given
      7

      Default Tusisikitike sana kwa kukosa tuvipendavyo maishani.

      Kupenda ni jambo muhimu
      katika maisha ya
      mwanadamu, kwa sababu
      asilimia kubwa ya matendo
      ya mtu huongozwa na
      mapenzi. Miongoni mwetu kuna watu wanapenda
      waume/wake zao, mali,
      watoto, magari vyakula,
      vinywaji, michezo na pengine aina fulani ya maisha. Baadhi yetu tuko tayari kupoteza maisha kama tutaachwa na wapenzi au kukosa mambo tuliyoyapenda.

      Pamoja na kwamba moyo
      hupata maumivu pale mazuri yanapokosekana, bado kuna ukweli juu ya madhara ya kujitakia yanayoweza kuepukwa na mtu anayeumia kwa kiwango cha kukosa usinginzi, kulia mara kwa mara kiasi cha kushindwa
      kufanya kazi zake kama kawaida. Kupenda kwa kiwango cha kushindwa kujizuia na kuvumilia ni hatari kwa afya ya mwanadamu, kwani uchunguzi unaonesha kuwa
      watu wengi wanaosumbuliwa na ugonjwa wa vidonda vya tumbo, moyo na wale wenye magonjwa yasiyoonekana kitalaamu pamoja na wanaokufa ghafla ni athari za msongo wa mawazo utokanao na kukosa mazuri wanayohitaji katika maisha yao.(Jiulize ni kipi kinachokutia simanzi moyoni mwako).
      Kisaikolojia kuutesa moyo kwa sababu mpenzi wako kakukataa ni matokeo ya kufikiri vibaya kwani ushahidi uliopo miongoni mwetu unaonesha kuwa mapenzi si kitu cha kudumu kwa miaka mingi na anayesema anaweza
      kupenda jambo moja milele
      kwa kiwango kilekile ni mtu
      anayejiwekea mtengo
      utakaomnasa mwenyewe na kumtesa. Watu wengi tunaowaona
      wakipagawa baada ya
      kupewa talaka na waume
      zao au kuondolewa mambo
      fulani waliyokuwa
      wanayapenda ni wale walioyachukulia mapenzi
      kama kitu cha kudumu
      kisichoweza kubadilika, huku
      wakisahau ukweli kuwa
      wanayopenda kwa wakati
      huo hawakuzaliwa nayo na wala hawakuyapenda kabla.
      Licha ya kuwepo kwa
      umuhimu wa kujiaminisha katika kupenda kwa msingi wa muda mrefu, mtu hatakiwi kukataa mabadiliko yanapotokea kwani ni wazi kwamba tuliyopenda tulipokuwa watoto si yale tunayopenda sasa.
      Hivyo ni jukumu la kila mtu
      anayetaka kuwa salama na
      maumivu ya moyo ya kumkosa ampendaye ni kuwa tayari kubadilika kutoka kupenda kitu cha awali mpaka kijacho, kuliko
      kung’ang’ania wazo moja na kujitesa nalo.

      Historia ya mafanikio ya watu inaonesha kuwa waliokuwa tayari kuacha walivyovipenda na kuanza mambo mapya ndiyo waliofanikiwa. Mafanikio na
      usalama wa maisha unataka
      mtu awe jasiri wa kupokea
      changamoto zinazohusu
      mapenzi. Ikiwa umekaa na mwanaume kwa muda mrefu na ukabaini kuwa hana mtazamo wa kimaendeleo, uwe tayari
      kukubali mabadiko ya kumwacha na kuanza maisha mapya. Rafiki yangu, unaumia kwa sababu mpenzi wako ameamua kuachana na wewe na sasa unafikiria kujiua, hebu kaa chini ufikirie kabla ya kuwa na huyo maisha yalikuwa hayaendi? Kama sivyo kinachokuumiza hasa ni nini mpaka unashinda unalia na kuutesa moyo wako? Tambua kuwa dunia ina vitu vingi sana vya kupenda, ambavyo vimeumbwa kwa ajili ya mwanadamu, usipopenda hiki haina maana hakuna cha kukufaa kipo na asipokupenda ndugu yako wapo marafiki watakaochukua nafasi ya mapenzi moyoni mwako na maisha yatasonga mbele kwa mafanikio makubwa, unachotakiwa ni kujiamini.
      Nafuatisha samahani kutokana na urefu wa topic.

    2. Study Abroad

    3. #2
      Ferds's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th October 2010
      Posts : 878
      Rep Power : 609
      Likes Received
      26
      Likes Given
      153

      Default Re: Tusisikitike sana kwa kukosa tuvipendavyo maishani.

      mzee nakuunga mkono kwa signature yangu
      Usipopata ulipopenda, penda ulipopata

    4. #3
      Maria Roza's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st April 2009
      Posts : 6,433
      Rep Power : 1843
      Likes Received
      787
      Likes Given
      333

      Default Re: Tusisikitike sana kwa kukosa tuvipendavyo maishani.

      Ngoja nijifunze kupenda
      If u can't stand for something , u will fall for anything !

    5. #4
      Mkwaruzo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st February 2011
      Location : Zanzibar
      Posts : 536
      Rep Power : 524
      Likes Received
      80
      Likes Given
      7

      Default Re: Tusisikitike sana kwa kukosa tuvipendavyo maishani.

      Quote By Maria Roza
      Ngoja nijifunze kupenda
      then ndo iweje?

    6. #5
      Tasia I's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st April 2010
      Posts : 1,138
      Rep Power : 692
      Likes Received
      150
      Likes Given
      129

      Default Re: Tusisikitike sana kwa kukosa tuvipendavyo maishani.

      Quote By Maria Roza
      Ngoja nijifunze kupenda
      hivi na wewe unatatizo la kupenda kama mimi??
      we unajifunzia wapi kupenda niwe nakuja!

    7. FemaTV & Radio

    8. #6
      The Boss's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 18th August 2009
      Location : DARESALAAM
      Posts : 18,144
      Rep Power : 21610
      Likes Received
      13469
      Likes Given
      17780

      Default Re: Tusisikitike sana kwa kukosa tuvipendavyo maishani.

      too long
      Watch your thoughts,They become words, Watch your words, They become deeds, Watch your deeds, They become habits, Watch your habits, They become character, Watch your character, It becomes your destiny!

    9. #7
      itnojec's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st March 2011
      Location : the under world
      Posts : 1,718
      Rep Power : 759
      Likes Received
      250
      Likes Given
      64

      Default Re: Tusisikitike sana kwa kukosa tuvipendavyo maishani.

      hamna kupenda siku hizi, tusidanganyane!

    10. #8
      Mkwaruzo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st February 2011
      Location : Zanzibar
      Posts : 536
      Rep Power : 524
      Likes Received
      80
      Likes Given
      7

      Default Re: Tusisikitike sana kwa kukosa tuvipendavyo maishani.

      Quote By The Boss
      too long
      nitajitahidi ili niiaifanyie remix

    11. #9
      Maria Roza's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st April 2009
      Posts : 6,433
      Rep Power : 1843
      Likes Received
      787
      Likes Given
      333

      Default Re: Tusisikitike sana kwa kukosa tuvipendavyo maishani.

      Quote By Tasia I
      hivi na wewe unatatizo la kupenda kama mimi??
      we unajifunzia wapi kupenda niwe nakuja!
      hahah nimeanza jifunza kupenda hela

    12. Miaka 50

    Similar Topics

    1. Mtu Muhimu Sana Maishani Mwako
      By Lizzy in forum Mahusiano, mapenzi, urafiki
      Replies: 44
      Last Post: 24th March 2013, 18:49
    2. Ni uwoga kukosa uvumilivu kukosa imani ama!?
      By Ame in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 1
      Last Post: 22nd August 2011, 10:41
    3. Replies: 35
      Last Post: 16th May 2011, 23:48
    4. Bidhaa adimu maishani
      By Nazjaz in forum Mahusiano, mapenzi, urafiki
      Replies: 30
      Last Post: 6th April 2011, 11:58
    5. maishani...
      By Mbu in forum Mahusiano, mapenzi, urafiki
      Replies: 10
      Last Post: 21st November 2008, 16:42

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...