Naona Watanzania wanaonyesha ushabiki wao kuhusu nani wanamtaka awe Rais Kenya kati ya Raila na Uhuru. Si vibaya kufanya hivyo kwani Kenya ni ndugu zetu. Tumetenganishwa tu na mipaka iliyowekwa na wakoloni kwa ajili ya kutupora utajri wetu. Huu mimi ni mtazamo wangu kuhusu kinyang'anyiro hicho cha Urais:
Mimi ni kati ya watu wale ambao walipenda sana Odinga achukuwe madaraka kipindi kilichopita ili kuondoa hali ya kabila moja kutawala Kenya lenyewe tu na kuyaacha makabila mengine kwani ni jambo linalotudhalilisha Waafrika wote!!!!!
Bahati mbaya sana Odinga hakuweza kuchukua madaraka juu ya kwamba yeye alikuwa na kila support ya Wakenya wenyewe na dunia nzima kwa ujumla kwamba ni mshindi halali wa uchaguzi ule. Lakini the so called “mbabe wa dunia” wakati ule chini ya urais wa Bush Junior akatumia ubabe wa Taifa lake kulazimisha Wakenya na Dunia nzima wakubali Raila ni Rais wa Kenya against the will of Kenyans kwa kutumia maneno ya kibabe kama LAZIMA maamuzi feki ya kupikwa yaheshimiwe ili Kibaki apite!
Kibaki akapita kwa mgongo wa Marekani (Bush Junior) na tena kwa gharama kubwa ya damu ya raia wa Kenya wasio na hatia! Kiasi gani Kibaki alimlipa Bush kupitia mali za Kenya ili amkingie kifua kuendelea kun’gan’gania madaraka Mungu ndio anayejua.
Bush ukaisha mda wake wa utawala. Akaingia Rais mwingine, Barrack Obama. Kwa mtazamo wangu akaona kwamba Odinga ameonewa na Wakenya wameuliwa kwa makosa kwa ajili ya Bush Junior kuangalia maslahi yake binafsi zaidi ya maslahi ya Wakenya. Nadhani ikamuuma sana kwa sababu hakuna mtu angeweza kuishawishi Mahakama ya Kimataifa iwafuatilie wauaji wa kimbari wa Kenya kwenye uchaguzi ule wa Kenya ambapo Raila alikuwa mshindi rasmi zaidi ya Marekani kwa sababu aliyeufunika ule ukatili alikuwa ni Rais wa Marekani wa wakati ule (Bush Junior) kwa kunyamanzisha mataifa yote ya ulimwenguni ambayo hayakuwa tayari kuona Wakenya wananyimwa haki yao halali ya kumchagua Rais wao (Waingereza ambao walikuwa wakoloni nchini Kenya walijitokeza wazi wazi kwenye sakata lile na wakaamua kua upande wa Mungu kwa kutetea haki za Wakenya wampate Rais wao waliyomchagua lakini walifyata mkia baada ya Bush Junior kutumia ubabe kutishia dunia nzima kuhusu mpango wake wa kuhakikisha kwamba Kibaki anakua Rais wa Kenya kwa gharama yeyote ile! )
Sasa baada ya kuingia Obama, vumbi la kuwavurumisha madagaa wa uuwaji wa kimbari Kenya (Kina Uhuru etal) na kuwaacha waasisi wakuu wa mauaji hayo ya kimbari (Kibaki na Bush) likapamba moto!!
Ni wazi kwamba Mwafrika yeyote mwenye akili timamu hata support move hii ya kumhukumu Uhuru kwani aliyeruhusu mauaji ya kimbari ya Wakenya in the first place ni Rais wa Markenai (Bush Junior chini ya utawala wake) na anayetaka kugeuza kibao kwa kuwaacha wahalifu halisi na kuwavamia vidagaa ni Rais huyo huyo wa Marekani (Obama).
Am sorry to say that itakuwa ni ujinga mkubwa sana kwa Wakenya kutompigia kura Uhuru kwa sababu wanahofia ataburutwa the Hague kutokana na hayo niliyoyaeleza hapo juu. Lakini nafahamu vile vile kwamba Wakenya si wajinga. Ni kati ya Waafrika ambao ni waerevu.
Kama kweli tunataka kutoa hukumu kwa mauaji ya kimbari yaliyofanyika Kenya basi ni lazima Bush Junior na Kibaki wawe washtakiwa wakuu huko the Hague. Vinginevyo tuache kuwadharau Waafrika. Hata kama sisi ni masikini wa kutupwa kwani umasikini wetu ni mfumo tu wa dunia wa uloloni mambo leo unaokumbatiwa na watawala wetu wasioona mbali ambao wanapewa support na mataifa yaliyoendelea ambayo hayana nia yeyote ya kutunyanyua sisi Waafrika zaidi ya kutuibia na kutudharau!!!!!
Kizazi kipya cha Afrika chenye kujiamini na ambacho kiko tayari kupambana kwa nguvu zote na udhalilishaji wa Waafrika duniani kimeanza kujiweka sawa. Tumegundua kwamba hatuwezi kutegemea viongozi wetu wa kisiasa wanaowekwa kwa maslahi ya mataifa machache kutukomboa sisi Waafrika.
A Bottom up movement is around the corner and it will spread throughout Africa for the betterment of not only Africans but the rest of the world since a productive African will add value to the rest of the world and increase economic space for all global citizens and hence a better world for all.
MUNGU IBARIKI AFRICA. MUNGU IBARIKI DUNIA.




Follow Us Here