Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: New Movement needed: Mabadiliko ya Katiba - Uzalendo

    Report Post
    Page 21 of 32 FirstFirst ... 11192021222331 ... LastLast
    Results 401 to 420 of 630
    1. #1
      Zakumi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2008
      Location : Mtoni
      Posts : 3,975
      Rep Power : 1347
      Likes Received
      893
      Likes Given
      374

      Default New Movement needed: Mabadiliko ya Katiba - Uzalendo

      Amani kwenu wazalendo wenzangu:

      Baada ya salaam ningependa kusema kuwa uchaguzi uliopita una mapungufu makubwa sana. Mapungufu mengi ni ya masuala ya kikatiba ambayo yamekuwepo kwa muda mrefu kuanzia uchaguzi wa 1995. Mapungufu hayo hayakujionyesha sana katika vipindi vya uchaguzi vilivyopita kwa sababu wagombea wa chama tawala walikuwa hawana upinzani mkubwa. Hivyo kasoro zote za kikatiba zilifunikwa na umaarufu wa kihistoria wa CCM. Kwa kipindi cha uchaguzi cha 2015, Tanzania itakaribisha wapiga kura wapya wapatao 1.5 miloni au waliozaliwa mwaka 1995 na baadaye.

      Hatutajitendea haki wenyewe na kizazi kipya iwapo tutaendelea kutumia katiba iliyo sasa kama mwongozo wa kuendeleza nchi. Hivyo kwa maombi yangu binafsi, wazalendo wa Tanzania tuanze kusukuma mabadiliko ya kikatiba. Ninapoita wazalendo, nina maana wananchi bila kujali itikadi zao vyama vya kisiasa, dini au ukabila.

      Bila ya kutaja matatizo ya katiba yetu, ningependa kueleza toka tumepata uhuru katiba ya Tanzania imekuwa ni kitu kisichoeleweka wazi kwa wananchi. Tuliosoma shule wakati somo la siasa linafundishwa mashuleni, tulikuwa tunafundishwa katiba ya CCM na miongozi ya chama hicho. Hivyo basi kuna uwezekano mkubwa hata wanasiasa wetu wengi hawajui umuhimu wa kitabu hicho.

      Hivyo ningependa kufungua ukumbi kwa kuwakaribisha wenye mawazo na nia ya kubadilisha katiba kutoa mawazo yao.

      Na vilevile kama kutakuwa na watu wanaotaka kuanzisha jumuia ya kufanya mabadiliko ya kikatiba, naomba mjitokeze.
      If we permit feathers to be freely borrowed, who is to tell the peacock from the crow?

    2. Miaka 50

    3. #401
      mgt software's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st November 2010
      Posts : 1,750
      Rep Power : 784
      Likes Received
      140
      Likes Given
      201

      Default Re: Mkapa ataka Katiba mpya

      wakati wa kuanza ni sasa mpaka ujifunge kibwebwe utakuwa umeachwa, tumfunge paka kengere sasa
      "Mtoto wa Maskini Hachagui Malezi, Tanganyika siyo Masikini Masikini ni wewe Unayehonga Haki yako Kwa Mafisadi" Bamugileki

    4. #402
      AMARIDONG's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th June 2010
      Posts : 2,488
      Rep Power : 949
      Likes Received
      53
      Likes Given
      47

      Default Re: Mkapa b.w. Aunga mkono harakati za chadema

      Quote By fareed
      ni upotoshaji kusema kuwa madai ya katiba mpya ni harakati za chadema. Ieleweke kuwa watanzania walianza kudai katiba mpya tangu zamani. Actually, mmoja wa wanasiasa wa kwanza kudai katiba mpya alikuwa ni christoper mtikila wa dp ambaye alisema way back baada ya vyama vingi kuruhusiwa in 1992 kuwa asingeshiriki kwenye uchaguzi wa 1995 bila kuwepo kwa katiba mpya kwa kuwa iliyopo ilitungwa na makada wa ccm mwaka 1977 chini ya utawala wa chama kimoja. Laiti vyama vyote vya upinzani vingesimama pamoja tangu 1995 na kukataa kushiriki kwenye uchagizi mkuu basi tungekuwa na katiba mpya sasa hivi.

      Chadema kimetoa msukumo mpya kudai katiba mpya, lakini kamwe harakati hii haikuasisiwa na chadema. Ni wananchi wenyewe wa tanzania wanaodai katiba mpya, pia ngo zote zinaunga mkono wazo hili.
      acha kudanganya umma madai ya katiba mpya kwa kizazi tulicho nacho ni madai ya msingi na yamesimamiwa wakati wote na chadema ila katiba mpya ni demand ya kihistoria toka enzi za mwalimu and u cant identify crzy mtikila as the mwamzilishi yeye ni kibaraka tuu na hayo madai ameyakuta,hata ndani ya ccm wapo watu 1960"s walishapinga katiba ya jamhuri wa muungano wa tz.

    5. #403
      omarilyas's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th January 2007
      Location : Morogoro
      Posts : 2,494
      Rep Power : 1133
      Likes Received
      67
      Likes Given
      4

      Default Re: Mkapa b.w. Aunga mkono harakati za chadema

      Du kumbe madai ya katiba mpya ni harakati za CHADEMA na sio watanzania na haswa wanaharakati walioanzisha mapambano haya kabla ya mwaka 1992 ilipoanzishwa Chadema...By the way, kila ninapomsikiliza Mbowe na hata Slaa huwa nasikia maombi ya mabadiliko ya katiba na sio Katiba mpya......
      Pasipo na IMANI kuna Uovu, Pasipo na MISINGI kuna Ufedhuli, Pasipo na ITIKADI kuna Ujanjaujanja...Yote haya ni mazalia ya UFISADI

    6. #404
      AMARIDONG's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th June 2010
      Posts : 2,488
      Rep Power : 949
      Likes Received
      53
      Likes Given
      47

      Default Re: Mkapa b.w. Aunga mkono harakati za chadema

      Quote By SIMBA MKUU
      acha kudanganya umma madai ya katiba mpya kwa kizazi tulicho nacho ni madai ya msingi na yamesimamiwa wakati wote na chadema ila katiba mpya ni demand ya kihistoria toka enzi za mwalimu and u cant identify crzy mtikila as the mwamzilishi yeye ni kibaraka tuu na hayo madai ameyakuta,hata ndani ya ccm wapo watu 1960"s walishapinga katiba ya jamhuri wa muungano wa tz.
      katiba ya tanzania ni ya mwaka 1977 huo mwaka 1960 umetoa wapi wewe au unajiandikia tuuu hata mambo huyajui??

    7. #405
      DENYO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th September 2010
      Posts : 582
      Rep Power : 566
      Likes Received
      12
      Likes Given
      0

      Default Re: Mkapa b.w. Aunga mkono harakati za chadema

      Hoja ni katiba mpya mimi ninafurahi moto unazidi kuwaka kudai katiba kazi ya wana jf ni kutoa elim ya uraia na kupeleka habari hii tanzania nzima. Ninajua chadema wana kipaumbele cha kudai katiba which is great, lakini tunajua pia chadema peke yao haitoshi tunahitaji watanzania wote, na chadema ipo teyari kusimamia hili kwa nguvu zote. Tusonge mbele bila unafiki pamoja tunaweza.

    8. FemaTV & Radio

    9. #406
      Topical's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd December 2010
      Posts : 5,050
      Rep Power : 1231
      Likes Received
      853
      Likes Given
      707

      Default Katiba Mpya- Vigezo vyake

      Tunahitaji katiba mpya yenye kuzingatia yafuatayo:-

      1. Rais wa JMT uwe wa kupokezana Bara na Zanzibar kila baada ya miaka kumi- kulinda muungano wetu, how? kila chama kitatakiwa kikatiba kumsimamisha mbara/mzenj ikiwa ni wakati wao...hivi watakuwa wanachuana wenyewe kwa wenyewe i.e. wabara vs. wabara, wazenj vs. wazenj

      2. Mawaziri wasiwe wabunge na wabunge wasiwe mawaziri

      3. Kusiwe na wabunge wa viti maalum, wala wakuteuliwa na Rais

      4. Wizara ziwe kwa mujibu wa katiba na shughuli zake ziwe ndani ya Katiba..Rais asiwe na uwezo wa kuongeza wizara hata moja mpaka aliombe bunge...wizara ziwe 13 tu..

      5. Cheo cha ukuu wa mkoa na wilaya ifutwe wabakizwe wakurugenzi

      6. Cheo cha katibu mkuu wizarani ifutwe waziri anatosha (ikiwa kipnegele 2) itakubaliwa..
      7...
      Tujadili!

    10. #407
      AMARIDONG's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th June 2010
      Posts : 2,488
      Rep Power : 949
      Likes Received
      53
      Likes Given
      47

      Default Re: Mkapa b.w. Aunga mkono harakati za chadema

      katiba mpya sio dili sana kwa sasa tuna matatizo mengine yapewe kipaumbele jamani katiba gharama sana

    11. #408
      DENYO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th September 2010
      Posts : 582
      Rep Power : 566
      Likes Received
      12
      Likes Given
      0

      Default Re: Katiba Mpya- Vigezo vyake

      yote sawa ila la rais atoke bara au zenj haina tija kubebana kusikokuwa na maslahi ya taifa, weka private candidate aruhusiwe, na hayo mengine yote na mengine mengi tulishajadala hapa JF

    12. #409
      AMARIDONG's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th June 2010
      Posts : 2,488
      Rep Power : 949
      Likes Received
      53
      Likes Given
      47

      Default Re: Mkapa b.w. Aunga mkono harakati za chadema

      Quote By son of peasant
      rais mstaafu wa awamu ya tatu, benjamin mkapa, amevunja ukimya baada ya kusema ili kuzuia mifarakano ya kisiasa kwa nchi wanachama wa jumuia ya afrika mashariki, zinahitaji kuwa na katiba mpya, ikiwemo tanzania."nakubaliana na harakati za chadema na vyama vingine vya upinzani kudai katiba mpya ni wakati sasa ccm ifikiri juu ya kuwapa wa tanzania katiba mpya kwani kelele zimekuwa nyingi sana"
      mkapa alisema hayo katika mkutano mkuu wa chama cha wanasheria wa jumuiya uliofanyika mjini bujumbura nchini burundi, mwezi uliopita.
      Kwa mujibu wa taarifa ya rais mkapa, iliyosomwa kwa niaba yake na balozi liberata mulamula, njia pekee ya kuondokana na migogoro ya kisiasa kila nchi inapaswa kuwa na katiba mpya ambayo itaainisha mambo yote ya msingi.
      Alisema kama nchi wanachama zikiwa na katiba mpya mambo mengi yanaweza kufanikiwa, lakini yameshindikana kutokana na nchi hizo kuendelea kutumia katiba zilizorithi kutoka kwa wakoloni.
      Alisema kumekuwa na malalamiko mengi kutokana na chaguzi nyingi toka kwa wanachama jinsi zinavyoendeshwa, huku shutuma na lawama nyingi zikielekezwa kwenye katiba zilizopo.
      Alisema katiba zilizopo zimekuwa zikipendelea zaidi upande mmoja ambao unampa uhuru rais kuamua kila kitu.
      Alisema uundwaji wa katiba, lazima uendane na hali halisi, mahitaji ya kijiografia, kijamii na kisiasa.
      “tunakabiliwa na mtihani mkubwa wa kuunganisha umoja wetu wa kitaifa… kuna baadhi wamegusia juu ya matatizo yetu ya kisiasa na baadhi yetu tunafikiri kuwa siku ya kuadhimisha uhuru ni kilele cha kujenga umoja wetu wa kitaifa… uhuru wetu wa katiba tulizonazo ni ushahidi wa dhuluma hii.
      “…hatuna katiba zingine zaidi ya zile ambazo tumezirithi kutoka kwa wakoloni, katiba ambazo hazina umakini, tunahitaji mpya,” alisema.
      Kwa mujibu wa taarifa hiyo, ambayo tanzania daima imefanikiwa kupata nakala yake, rais mkapa alisema chaguzi nyingi zitakuwa huru na haki endapo kutakuwa na katiba bora.
      Akinukuu maneno ya mwandishi wa vitabu duniani (hakumtaja), ambaye pia ni mwanafalsafa aliyesema, ‘chaguzi za haki ni muhimu kwa katiba bora.’
      alisema katika uundaji wa katiba mpya, ni lazima kuwepo makubaliano maalum, kwa pande zote za kisiasa, kijamii na kijiografia, huku kanuni pamoja na mambo muhimu yakizingatiwa.
      Alisema malumbano na migororo ndani ya nchi, yanasababishwa na muundo wa katiba zinazoonekana kutokidhi haki na usawa.
      “katiba ndiyo moyo wa nchi, moyo wa mwanadamu unaofanya mwili mzima ufanye kazi… hivyo kwa kuangalia mbele tunahitaji kuundwa kwa katiba na mihimili yote ya nchi, tunahitaji katiba huru itakayotulinda katika hatari,” alisema mkapa.
      Akitoa mfano, rais mkapa alisema kumekuwa na sakata la uanzishaji wa mahakama ya kadhi katika nchi za tanzania na kenya, huku akisistiza kama lingekuwa ndani ya katiba isingesababisha malumbano makubwa.
      Kauli ya rais mkapa, imekuja wakati watu wa kada mbalimbali wakiwemo, wanasiasa, wasomi na wanaharakati wakiishinikiza serikali kufanya marekebisho ya katiba iliyopo, kwa madai kuwa haikidhi matakwa.
      Mwanzoni mwa wiki hii, waziri wa sheria na mambo ya katiba, celina kombani, alisema hakuna haja ya kuwa na katiba mpya, kitendo kilichoonekana kupingwa na watu wengi.
      Waziri kombani alisema katiba iliyopo itaendelea kutumika kwani, serikali haina fedha za kufanya maandalizi ya kubadilisha katiba hiyo.
      Jaji mkuu mstaafu mark bomani naye juzi alivunja ukimya na kusema kinachoisumbua serikali iliyoko madarakani ni woga ambao hauna msingi wowote.
      Alisema katiba iliyopo kwa kiasi kikubwa imepitwa na wakati, kwani wakati huu inakinzana katika baadhi ya vifungu, huku ikishindwa kutoa picha halisi ya demokrasia na utawala bora.
      Naye profesa wa chuo kikuu cha dar es salaam na mwanaharakati maarufu, issa shivji, amekuwa mstari wa mbele kupiga kelele mara kwa mara kutaka serikali ibadilishe katiba iliyopo kwa manufaa ya taifa.
      Mwaka 1998 kamati ya white paper iliyoundwa chini ya jaji robert kisanga ilipendekeza umuhimu wa kuwa na katiba mpya, lakini ilipowasilisha ripoti yake ilikemewa kwa kile kilichodaiwa ilivuka mipaka kwa sababu ilikuwa kamati na si tume. Na hiyo ilikuwa awamu ya rais mkapa.
      hongera kwa kutuletea hii hapa wengine hatuna muda na magazeti ila tuna muda sana na jf big up

    13. #410
      junior2008's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th April 2009
      Posts : 512
      Rep Power : 615
      Likes Received
      38
      Likes Given
      1

      Default Re: Mkapa b.w. Aunga mkono harakati za chadema

      Quote By omarilyas
      Du kumbe madai ya katiba mpya ni harakati za CHADEMA na sio watanzania na haswa wanaharakati walioanzisha mapambano haya kabla ya mwaka 1992 ilipoanzishwa Chadema...By the way, kila ninapomsikiliza Mbowe na hata Slaa huwa nasikia maombi ya mabadiliko ya katiba na sio Katiba mpya......
      Yale maneno mekundu naona son of peasant kachomekea tu. Madai ya katiba mpya ni ya muda mrefu na ni ya watanzania! Wanaharakati, CHADEMA na vyama vingine vya siasa vinawawakilisha tu wananchi. Moja ya madai ya msingi ya CHADEMA ni katiba mpya itakayopelekea sio tume huru ya uchaguzi bali inayokidhi haja ya watanzania wote kwa mazingira ya sasa na demokrasia ya mfumo wa vyama vingi ikiwa ni pamoja na kuondoa sheria zote kandamizi.

    14. #411
      Gad ONEYA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th October 2010
      Posts : 2,544
      Rep Power : 947
      Likes Received
      122
      Likes Given
      559

      Default Re: Katiba Mpya- Vigezo vyake

      Kwanza mchakato uanze!

    15. #412
      Mallaba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th January 2008
      Location : Jerusalem
      Posts : 2,562
      Rep Power : 1090
      Likes Received
      24
      Likes Given
      28

      Default Re: Mkapa ataka Katiba mpya

      Mkapa sio kwamba hawezi kuongea mbele ya Kikwete la hasha, tatizo hapa ni system inayomuzunguka kikwete ni chafu sio kawaida hivyo naona hata akishauri kitu kizuri ataonekana kama yuko against..Mkapa ni jasiri na akiamua anaweza sana,kwani yeye ahajui kuwa uchaguzi ulikuwa wa kisanii?? anajua sana?
      Quote By Robin
      unafiki mtupu !!!!!!!!!hana uthubutu wa kuongea mbele ya kikwete.he is more of international figure and a coward ,traitor in his homeland.
      YOTE YANA MWISHO,IKO SKU TUTAPATA UHURU WETU NA KATIBA MPYA.
      Ee Bwana uyasikilize maneno yangu, ukaangalie kutafakari kwangu.

    16. #413
      Thesi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th August 2010
      Posts : 728
      Rep Power : 4676
      Likes Received
      187
      Likes Given
      321

      Default Re: Mkapa ataka Katiba mpya

      Kinanifuhisha kuwa hata wale walopinga katiba mpya sasa wanaanza kuwa waumini. Heko wapiganaji Dr Slaa, Prof Lipumba, Prof Shivji, Prof Chrid Maina.
      Naamini safari si ndefu watu wataelewa maana ya katiba mpya na faida zake.

    17. #414
      Thesi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th August 2010
      Posts : 728
      Rep Power : 4676
      Likes Received
      187
      Likes Given
      321

      Default Re: Mkapa ataka Katiba mpya

      Kinanifuhisha kuwa hata wale walopinga katiba mpya sasa wanaanza kuwa waumini. Heko wapiganaji Dr Slaa, Prof Lipumba, Prof Shivji, Prof Chrid Maina.
      Naamini safari si ndefu watu wataelewa maana ya katiba mpya na faida zake.

    18. #415
      macho_mdiliko's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2008
      Posts : 1,893
      Rep Power : 955
      Likes Received
      403
      Likes Given
      295

      Default Re: Katiba Mpya- Vigezo vyake

      ....Tume huru ya uchaguzi
      ....Madaraka ya ki-mungu mdogo ya urais yapunguzwe.

    19. #416
      Nyangomboli's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th November 2010
      Location : Mwisenge
      Posts : 886
      Rep Power : 608
      Likes Received
      121
      Likes Given
      4

      Default

      Quote By Brooklyn
      Mkuu umesahau Mh. Waziri Mkuu mstaafu Sumaye hakujua kwanini Tanzania ni masikini kwa miaka yote kumi aliyokuwa madarakani MPAKA alipoenda kusoma Marekani ndipo alipogundua kwanini watanzania ni masikini!!

      labda pengine viongozi na wanasiasa wetu wanahitaji refresher course kila baada ya miezi sita!!
      Wallah nakuunga mkono na i am so serious.

    20. #417
      Nyangomboli's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th November 2010
      Location : Mwisenge
      Posts : 886
      Rep Power : 608
      Likes Received
      121
      Likes Given
      4

      Default

      Quote By Mallaba
      Mkapa sio kwamba hawezi kuongea mbele ya Kikwete la hasha, tatizo hapa ni system inayomuzunguka kikwete ni chafu sio kawaida hivyo naona hata akishauri kitu kizuri ataonekana kama yuko against..Mkapa ni jasiri na akiamua anaweza sana,kwani yeye ahajui kuwa uchaguzi ulikuwa wa kisanii?? anajua sana?
      Mkuu naona hapa kujaelewa tatizo au maada ya waheshimiwa. he might be jasiri or whatever we call him. but he was the president of this poor tz for the period of ten yearz. kwa KISANGA iliweka wazi yote haya!?

    21. #418
      Gosbertgoodluck's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd March 2008
      Posts : 2,863
      Rep Power : 1149
      Likes Received
      334
      Likes Given
      4

      Default Re: Mkapa ataka Katiba mpya

      Hiyo kauli imemtoka mdomoni au moyoni? Nahisi kama anachoongea sicho anachofikiri moyoni.

    22. #419
      kagumyamuheto's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th November 2010
      Posts : 287
      Rep Power : 490
      Likes Received
      2
      Likes Given
      0

      Default Re: Mkapa ataka Katiba mpya

      Si amini kama haya yanatoka kwa bro. Nkapa. Anyway kanena. Nashauri tu jk aliweke hili kwenye ilani ya 2015. Ila mchakato wake uanze sasa.
      Kwasasa tufikirie kujenga nchi.

    23. #420
      HISIA KALI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th October 2010
      Location : Mjini kwa mjomba
      Posts : 643
      Rep Power : 563
      Likes Received
      80
      Likes Given
      1

      Default Re: Mkapa ataka Katiba mpya

      Ni kweli nchi nyingi za Afrika, Tanzania ikiwemo zinahitaji katiba mpya. Lakini hili tamko la Mkapa ni la kushangaa kwani alikuja juu za pale tume yake mwenyewe iliposhauri umuhimu wa kuwa na katiba mpya.

    Page 21 of 32 FirstFirst ... 11192021222331 ... LastLast

    Similar Topics

    1. Replies: 2
      Last Post: 16th November 2011, 22:28
    2. sheria ya mabadiliko ya katiba
      By Nyabwire in forum Jukwaa la Sheria (The Law Forum)
      Replies: 1
      Last Post: 31st October 2011, 08:41
    3. Replies: 13
      Last Post: 25th March 2011, 22:48
    4. Mabadiliko ya Katiba hayaepukiki
      By kilimasera in forum KATIBA Mpya
      Replies: 0
      Last Post: 16th December 2010, 08:16
    5. Mabadiliko ya Katiba ni lazima
      By kilimasera in forum KATIBA Mpya
      Replies: 0
      Last Post: 16th December 2010, 08:14

    User Tag List

    Tags for this Topic

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...