Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: KATIBA MPYA: hivi ndivyo wasemavyo watanzania

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 21
    1. oba
      #1
      oba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st October 2010
      Location : nchi ya kusadikika
      Posts : 273
      Rep Power : 488
      Likes Received
      51
      Likes Given
      88

      Default KATIBA MPYA: hivi ndivyo wasemavyo watanzania

      Wajameni, katika pita pita yangu kwenye mtandao nimekutana na maoni yafuatayo ya mtanzania mmoja juu ya katiba mpya;


      Yafuatayo ni maoni yangu;
      1. Rais apunguziwe madaraka katika uteuzi wa viongozi waandamizi wa serikali au mahakama
      2. Nafasi ya spika wa bunge iwe ni kwa mtanzania yeyote mwenye sifa na huyo mtu atume maombi kwenye kamati maalumu ya bunge, asiwe mbunge wa jimbo au chama chochote ili kuepusha mgongano wa maslahi wakati akitekeleza wajibu wake
      3. Mawaziri wasiwe wabunge ili kurahisisha bunge kuisimamia serikali na kuondoa mgongano wa maslahi bungeni.
      4. Ubunge wa viti maalum uvunjwe kwani kama mawaziri hawatakuwa wabunge, Rais hatakuwa na haja ya kuteua watu kadhaa kuwa wabunge ili wamsaidie kutawala.
      5. Wakuu wa mikoa na wilaya wasiteuliwe na raisi, la ikiwezekana nafasi hizo ziondolewe.
      6. Muungano wa Tanganyika na zanzibar uwe na serikali moja, Pemba liwe jimbo na unguja liwe jimbo katika serikali moja tu. Tanzania bara igawanywe pia katika majimbo. Kila jimbo liwe na seneta na utawala wa ndani na liluhusiwe kuwa na serikali kulingana na uhitaji wake. Serikali kuu iwe na wizara chache tu kama ulinzi, fedha, ndani, nje na afya nyingine ziendeshwe na majimbo husika kulingana na uhitaji wa kila jimbo
      7. Kama serikali moja haiwezekani basi muungano uvunjwe; hakuna sababu ya kuwa na serikali tatu kwani zitaongeza mzigo kwa wananchi wa kuziendesha, serikali mbili zimeshindwa kuleta muungano halisi.
      8. Wataalamu wa sekta mbalimbali wapewe vipaumbele na ikiwezekana wathaminiwe kuliko wanasiasa, hiyo itaongeza uzalendo kwa wataalamu hao ambao tunawahitaji zaidi kuliko wanasiassa.
      9. Madiwani na wabunge wawe wasomi wa japo degree moja, hiyo itawawezesha kudadavua hoja zinazoletwa na wataalamu walio chini yao. Tofauti na sasa ambapo mbunge std VII anapewa jukumu la kuchallenge utalaamu wa injinia au daktari na ikiwezekana kuupinga huku uelewa wake ukiwa ni wa chini kwa ujumla au katika eneo lile.
      10. Nchi hii haina dini na itabaki hivyo...suala la mambo ya dini fulani kama mahakama ya kadhi au mabaraza ya dini fulani yaachiwe waumini wa dini hiyo na serikali isijihusishe na mambo hayo. Itoe uhuru wa kila dini kuendesha mambo yanayoihusu bila kuathiri sheria za nchi wala usalama wa watu wa dini nyingine

      Nitafurahi maoni yangu yakizingatiwa

      My take; Tume husika inafuatilia mijadala hii kwa uhakika?
      "If you don't stand for something you will fall down for anything"- usiposhiriki kuikomboa nchi yako utatawaliwa na mashetani!

    2. Miaka 50

    3. #2
      JATELO1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st October 2011
      Posts : 1,015
      Rep Power : 901
      Likes Received
      81
      Likes Given
      39

      Default Re: KATIBA MPYA: hivi ndivyo wasemavyo watanzania

      Quote By oba
      Wajameni, katika pita pita yangu kwenye mtandao nimekutana na maoni yafuatayo ya mtanzania mmoja juu ya katiba mpya;


      Yafuatayo ni maoni yangu;
      1. Rais apunguziwe madaraka katika uteuzi wa viongozi waandamizi wa serikali au mahakama
      2. Nafasi ya spika wa bunge iwe ni kwa mtanzania yeyote mwenye sifa na huyo mtu atume maombi kwenye kamati maalumu ya bunge, asiwe mbunge wa jimbo au chama chochote ili kuepusha mgongano wa maslahi wakati akitekeleza wajibu wake
      3. Mawaziri wasiwe wabunge ili kurahisisha bunge kuisimamia serikali na kuondoa mgongano wa maslahi bungeni.
      4. Ubunge wa viti maalum uvunjwe kwani kama mawaziri hawatakuwa wabunge, Rais hatakuwa na haja ya kuteua watu kadhaa kuwa wabunge ili wamsaidie kutawala.
      5. Wakuu wa mikoa na wilaya wasiteuliwe na raisi, la ikiwezekana nafasi hizo ziondolewe.
      6. Muungano wa Tanganyika na zanzibar uwe na serikali moja, Pemba liwe jimbo na unguja liwe jimbo katika serikali moja tu. Tanzania bara igawanywe pia katika majimbo. Kila jimbo liwe na seneta na utawala wa ndani na liluhusiwe kuwa na serikali kulingana na uhitaji wake. Serikali kuu iwe na wizara chache tu kama ulinzi, fedha, ndani, nje na afya nyingine ziendeshwe na majimbo husika kulingana na uhitaji wa kila jimbo
      7. Kama serikali moja haiwezekani basi muungano uvunjwe; hakuna sababu ya kuwa na serikali tatu kwani zitaongeza mzigo kwa wananchi wa kuziendesha, serikali mbili zimeshindwa kuleta muungano halisi.
      8. Wataalamu wa sekta mbalimbali wapewe vipaumbele na ikiwezekana wathaminiwe kuliko wanasiasa, hiyo itaongeza uzalendo kwa wataalamu hao ambao tunawahitaji zaidi kuliko wanasiassa.
      9. Madiwani na wabunge wawe wasomi wa japo degree moja, hiyo itawawezesha kudadavua hoja zinazoletwa na wataalamu walio chini yao. Tofauti na sasa ambapo mbunge std VII anapewa jukumu la kuchallenge utalaamu wa injinia au daktari na ikiwezekana kuupinga huku uelewa wake ukiwa ni wa chini kwa ujumla au katika eneo lile.
      10. Nchi hii haina dini na itabaki hivyo...suala la mambo ya dini fulani kama mahakama ya kadhi au mabaraza ya dini fulani yaachiwe waumini wa dini hiyo na serikali isijihusishe na mambo hayo. Itoe uhuru wa kila dini kuendesha mambo yanayoihusu bila kuathiri sheria za nchi wala usalama wa watu wa dini nyingine

      Nitafurahi maoni yangu yakizingatiwa

      My take; Tume husika inafuatilia mijadala hii kwa uhakika?
      Nimependa michango yako.
      inity likes this.

    4. #3
      Topical's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd December 2010
      Posts : 5,050
      Rep Power : 1231
      Likes Received
      853
      Likes Given
      707

      Default Re: KATIBA MPYA: hivi ndivyo wasemavyo watanzania

      MoU ivunjwe, kanisa liendesha miradi yake peke yake iwe shule, hospitali bila kuchota pesa za umma

      Serikali iendeshe miradi yake bila kutegemea..

      NB. Serikali ziwe tatu; au muungano uvunjwe kabisa
      "Mbowe for Presidency 2015""

    5. #4
      Kikwebo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th August 2006
      Posts : 323
      Rep Power : 716
      Likes Received
      42
      Likes Given
      20

      Default

      Quote By Topical
      MoU ivunjwe, kanisa liendesha miradi yake peke yake iwe shule, hospitali bila kuchota pesa za umma

      Serikali iendeshe miradi yake bila kutegemea..

      NB. Serikali ziwe tatu; au muungano uvunjwe kabisa
      Hapa kazi ipo, naona jino kwa jino.

    6. #5
      MARCKO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th June 2011
      Posts : 1,413
      Rep Power : 684
      Likes Received
      153
      Likes Given
      0

      Default Re: KATIBA MPYA: hivi ndivyo wasemavyo watanzania

      Aisee imetulia sana lakini kuusu muungano, wazanzibari wanataka uwaite wananchi na siyo wana majimbo, na serikali tatu kweli haitakua na aja, hivyo muungano haukamatiki tena hata mkia! Yani umeteleza ukaondoka!

    7. RukaaJuu Final

    8. #6
      genekai's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th February 2010
      Location : Loitering!
      Posts : 7,538
      Rep Power : 2087
      Likes Received
      1081
      Likes Given
      1575

      Default Re: KATIBA MPYA: hivi ndivyo wasemavyo watanzania

      Jibu kwa "your take", watu hao wako makini na bila shaka watasema na kutenda watz watakavyo!!!
      The future of this country is being jeopardized by the intellectual slavery of our top leaders

    9. #7
      MARCKO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th June 2011
      Posts : 1,413
      Rep Power : 684
      Likes Received
      153
      Likes Given
      0

      Default Re: KATIBA MPYA: hivi ndivyo wasemavyo watanzania

      Viongozi wa serikali Walivyo wajinga, watakua wanawalazimisha watanganyika na wa zanzibar muungano kwa bunduki, badala ya kuwafahamisha (alternatives) zote zilizopo ili wachague kimoja. Yaani, ccm +police =policcmabwepande/ baharini.

    10. bdo
      #8
      bdo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th November 2006
      Posts : 892
      Rep Power : 886
      Likes Received
      140
      Likes Given
      73

      Default Re: KATIBA MPYA: hivi ndivyo wasemavyo watanzania

      haya ni maoni yako au ni maoni ya watu wengine na yako?

      Quote By oba
      Wajameni, katika pita pita yangu kwenye mtandao nimekutana na maoni yafuatayo ya mtanzania mmoja juu ya katiba mpya;


      Yafuatayo ni maoni yangu;
      1. Rais apunguziwe madaraka katika uteuzi wa viongozi waandamizi wa serikali au mahakama
      2. Nafasi ya spika wa bunge iwe ni kwa mtanzania yeyote mwenye sifa na huyo mtu atume maombi kwenye kamati maalumu ya bunge, asiwe mbunge wa jimbo au chama chochote ili kuepusha mgongano wa maslahi wakati akitekeleza wajibu wake
      3. Mawaziri wasiwe wabunge ili kurahisisha bunge kuisimamia serikali na kuondoa mgongano wa maslahi bungeni.
      4. Ubunge wa viti maalum uvunjwe kwani kama mawaziri hawatakuwa wabunge, Rais hatakuwa na haja ya kuteua watu kadhaa kuwa wabunge ili wamsaidie kutawala.
      5. Wakuu wa mikoa na wilaya wasiteuliwe na raisi, la ikiwezekana nafasi hizo ziondolewe.
      6. Muungano wa Tanganyika na zanzibar uwe na serikali moja, Pemba liwe jimbo na unguja liwe jimbo katika serikali moja tu. Tanzania bara igawanywe pia katika majimbo. Kila jimbo liwe na seneta na utawala wa ndani na liluhusiwe kuwa na serikali kulingana na uhitaji wake. Serikali kuu iwe na wizara chache tu kama ulinzi, fedha, ndani, nje na afya nyingine ziendeshwe na majimbo husika kulingana na uhitaji wa kila jimbo
      7. Kama serikali moja haiwezekani basi muungano uvunjwe; hakuna sababu ya kuwa na serikali tatu kwani zitaongeza mzigo kwa wananchi wa kuziendesha, serikali mbili zimeshindwa kuleta muungano halisi.
      8. Wataalamu wa sekta mbalimbali wapewe vipaumbele na ikiwezekana wathaminiwe kuliko wanasiasa, hiyo itaongeza uzalendo kwa wataalamu hao ambao tunawahitaji zaidi kuliko wanasiassa.
      9. Madiwani na wabunge wawe wasomi wa japo degree moja, hiyo itawawezesha kudadavua hoja zinazoletwa na wataalamu walio chini yao. Tofauti na sasa ambapo mbunge std VII anapewa jukumu la kuchallenge utalaamu wa injinia au daktari na ikiwezekana kuupinga huku uelewa wake ukiwa ni wa chini kwa ujumla au katika eneo lile.
      10. Nchi hii haina dini na itabaki hivyo...suala la mambo ya dini fulani kama mahakama ya kadhi au mabaraza ya dini fulani yaachiwe waumini wa dini hiyo na serikali isijihusishe na mambo hayo. Itoe uhuru wa kila dini kuendesha mambo yanayoihusu bila kuathiri sheria za nchi wala usalama wa watu wa dini nyingine

      Nitafurahi maoni yangu yakizingatiwa

      My take; Tume husika inafuatilia mijadala hii kwa uhakika?

    11. #9
      Ibnu Mussa's Avatar
      Member Array
      Join Date : 27th June 2012
      Posts : 19
      Rep Power : 511
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: KATIBA MPYA: hivi ndivyo wasemavyo watanzania

      Maoni yangu uwepo muungano wa mkataba. Kama nyinyi mnataka wa serikali tatu basi haya yafuatayo yahamishwe kutoka bara yapelekwezanzibar:

      raisi wa taganyika achaguliwe zanzibar, makao makuu ya ccm yawepo zanzibar, bunge zanzibar,benki kuu zanzibar,wizara zote zanzibar, raisi na waziri mkuu atoke zanzibar. Hapo ndipo wataganyika mtakapoujua muungano.

    12. #10
      lukindo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th March 2010
      Posts : 1,575
      Rep Power : 781
      Likes Received
      415
      Likes Given
      481

      Default Re: KATIBA MPYA: hivi ndivyo wasemavyo watanzania

      nilimsikia 'mwanakijiji' mmoja Kisarawe (sina uhakika na jina) anaitwa Kondo, nilipenda sana wazo lake na ndipo niliona kuwa wale wanaosema 'Watanzania ni wajinga' wanakosea.

      Alipendekeza kuwa: Wimbo wa taifa ufutwe tubakiwe na bendera pekee kama kitambulisho cha taifa.
      Mzee Warioba alipomuuliza ni kwa nini anapendekeza hivyo akasema kuwa ule wimbo una kipengele cha kibaguzi kinachosema "...wabariki viongozi wake".

      Sasa yeye anasema tunafanya makosa kuwaombea hawa 'viongozi' wakati wametusaliti na wanakula rushwa na ndipo Mzee Warioba akawa anamuuliza kuwa ni kwa nini hicho kipengele kisibadilishwe na kuwa "...wabariki watu wake"? katika kuondoa huo utata.

      Sasa mimi usahihi wa wazo hilo naona ni mkubwa mno na nasubiria kuona kama litakuwemo kwenye hiyo katiba ndipo nitajua haki imetendeka
      mito likes this.

    13. #11
      mizambwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th October 2008
      Posts : 1,439
      Rep Power : 975
      Likes Received
      368
      Likes Given
      1811

      Default Re: KATIBA MPYA: hivi ndivyo wasemavyo watanzania

      Quote By lukindo
      Sasa yeye anasema tunafanya makosa kuwaombea hawa 'viongozi' wakati wametusaliti na wanakula rushwa na ndipo Mzee Warioba akawa anamuuliza kuwa ni kwa nini hicho kipengele kisibadilishwe na kuwa "...wabariki watu wake"? katika kuondoa huo utata.
      Namuunga mkono kabisa KWA 100% huu wimbo hauna maana yoyote katika uhalisia wa mambo.


      MIZAMBWA
      NABII MTARAJWIA!!!
      SASA NIMEAMINI KUWA TANZANIA BILA CCM INAWEZEKANA!!!!, TUANDAE KABURI LA KUIZIKA MWAKA 2015

    14. #12
      KUCHI's Avatar
      Member Array
      Join Date : 27th December 2010
      Posts : 33
      Rep Power : 432
      Likes Received
      4
      Likes Given
      2

      Default Re: KATIBA MPYA: hivi ndivyo wasemavyo watanzania

      Kimsingi naunga mkono maoni ya obi, hata hivyo nashauri ili tujenge jamii makini ni vyema katiba yetu ikaweka misingi ya majukumu ya serikali itakayokua madarakani( bila kujali chama kitakachotawala) na siyo kuachia kila serikali ikiingia madarakani inakuja na mambo yake ambayo baada ya muda mfupi inapoondoka madarakani serikali mpya nayo inakuja na yake so nchi inakosa flow nzuri ya maendeleo, kwa mfano serikali iliyopita iliweka mkazo katika kujenga barabara na mashule laiti ingelikua ni tamko la katiba kwa maana serikali iliyofuata isingeanza na mambo yake leo hii angalau 50% ya tanzania ingefikika kwa barabara za lami, Kwa upande wa muungano, kwa maoni yangu lazima tuwe na sababu za sasa za kuungana, hofu yangu ni kua tunatumia sababu za zamani kuweka muungano wa sasa ndo maana kelele haziishi. mi nafikiri kwa kua tuko kwenye shirikisho la afrika mashariki ni bora tuvunje haka kamuungano ketu halafu Zanzbar na Tanganyika kila moja iwe member wa shirikisho sambamba na nchi nyingine, tukifanya hivi kila upande utapata nafasi ya kujipima kuona umuhimu wa mwenzie ili yule ambae anaona anabanwa, sikubaliani na hoja ya kua eti muungano huu unasaidia usalama wa mipaka hasa kwa kua technolojia imeenda mbele sana hatustahili kulinda mipaka
      kwa magobore, vunja muungano tujipange upya. naishauri tume ya katiba itae ushauri wake kulingana na maoni ya wananchi pia serikali ikubaliane na maoni hayo, itakumbukwa kuwa tume ya hali ya siasa ilieleza kuwa 80% hawakuunga mkono ujio wa vyama vingi but serikali ilichukua maoni yale ikawaeka kapuni ikatumia minority rule . wengi hatutapenda serikali kuamua kwa mabavu tunaomba ifuate maoni ya wananchi.
      inity likes this.

    15. #13
      liganga4's Avatar
      Member Array
      Join Date : 29th August 2010
      Posts : 25
      Rep Power : 448
      Likes Received
      2
      Likes Given
      0

      Default Re: KATIBA MPYA: hivi ndivyo wasemavyo watanzania

      Quote By oba
      Wajameni, katika pita pita yangu kwenye mtandao nimekutana na maoni yafuatayo ya mtanzania mmoja juu ya katiba mpya;


      Yafuatayo ni maoni yangu;
      1. Rais apunguziwe madaraka katika uteuzi wa viongozi waandamizi wa serikali au mahakama
      2. Nafasi ya spika wa bunge iwe ni kwa mtanzania yeyote mwenye sifa na huyo mtu atume maombi kwenye kamati maalumu ya bunge, asiwe mbunge wa jimbo au chama chochote ili kuepusha mgongano wa maslahi wakati akitekeleza wajibu wake
      3. Mawaziri wasiwe wabunge ili kurahisisha bunge kuisimamia serikali na kuondoa mgongano wa maslahi bungeni.
      4. Ubunge wa viti maalum uvunjwe kwani kama mawaziri hawatakuwa wabunge, Rais hatakuwa na haja ya kuteua watu kadhaa kuwa wabunge ili wamsaidie kutawala.
      5. Wakuu wa mikoa na wilaya wasiteuliwe na raisi, la ikiwezekana nafasi hizo ziondolewe.
      6. Muungano wa Tanganyika na zanzibar uwe na serikali moja, Pemba liwe jimbo na unguja liwe jimbo katika serikali moja tu. Tanzania bara igawanywe pia katika majimbo. Kila jimbo liwe na seneta na utawala wa ndani na liluhusiwe kuwa na serikali kulingana na uhitaji wake. Serikali kuu iwe na wizara chache tu kama ulinzi, fedha, ndani, nje na afya nyingine ziendeshwe na majimbo husika kulingana na uhitaji wa kila jimbo
      7. Kama serikali moja haiwezekani basi muungano uvunjwe; hakuna sababu ya kuwa na serikali tatu kwani zitaongeza mzigo kwa wananchi wa kuziendesha, serikali mbili zimeshindwa kuleta muungano halisi.
      8. Wataalamu wa sekta mbalimbali wapewe vipaumbele na ikiwezekana wathaminiwe kuliko wanasiasa, hiyo itaongeza uzalendo kwa wataalamu hao ambao tunawahitaji zaidi kuliko wanasiassa.
      9. Madiwani na wabunge wawe wasomi wa japo degree moja, hiyo itawawezesha kudadavua hoja zinazoletwa na wataalamu walio chini yao. Tofauti na sasa ambapo mbunge std VII anapewa jukumu la kuchallenge utalaamu wa injinia au daktari na ikiwezekana kuupinga huku uelewa wake ukiwa ni wa chini kwa ujumla au katika eneo lile.
      10. Nchi hii haina dini na itabaki hivyo...suala la mambo ya dini fulani kama mahakama ya kadhi au mabaraza ya dini fulani yaachiwe waumini wa dini hiyo na serikali isijihusishe na mambo hayo. Itoe uhuru wa kila dini kuendesha mambo yanayoihusu bila kuathiri sheria za nchi wala usalama wa watu wa dini nyingine

      Nitafurahi maoni yangu yakizingatiwa

      My take; Tume husika inafuatilia mijadala hii kwa uhakika?
      kila mtanzania anaye stahili kufanya kazi afanye kazi ili kupunguza idadi kubwa ya wavivu kodi ilpwe na wote wanostahili badala ya mzigo wote kuachwa kwa wafanyakazi wachahe huku wafanyabiashara wakiwa ni mawkala tu. pia kodi yetu tuna kila mlipa kodi aone thamani yake. wabunge waishi kwenye maeneo waliyo chaguliwa ili kuleta maana halisi ya uwakilishi na wapiga kura wawe na uwezo wakuwajibisha mbunge badala ya chama kilicho mteuwa.
      nchi yetu ni tajiri raslimali zakila eneo zianze kuwa komboa watu wa eneo hilo kwanza badala ya utaratibu wa sasa ambapo mapato yote yanapelekwa magogon ili wakuu waamue wapi kuna stahili, hii ita punguza ufisadi kwa kiasi kikubwa kwani muda mrefu tumedumaza akili zetu kwa kufikiri dsm ndiyo kilakitu na tumeambukiza vijana wengi kwamba maisha yapo dar pekeyake.
      muungano eidha wa serikali moa vinginevyu naitaka tanganyika yangu nchi yaamaziwa na asali kwani mpaka sasa mikoa ya dsm tanga llindi mtr ndiyoa wanaweza kuzungumza juu ya zenji mimi wa ludewa, mbabay na kyela malawi pia ni ndugu zetu, hivyo basi muungano unatakiwa uzingatie uhuru kamili wa tanganyika kama taifa badala ya ujanjaunja. ruzuku wenye pembejeo na zana za kilimo. soko la maza liwe la uhakika. wataalam wa fani mbalimba wapwe kipaumbele na wao wonyeshe kwa dhati upeo wa wao katika kuletea taifa maendeleo.
      madaraka ya raisi ya punguzwe hasa kwenye uteuzi wa vyeo mbalimbali.
      Last edited by liganga4; 17th August 2012 at 15:21.
      ChescoMatunda likes this.

    16. #14
      mzalendokimathi's Avatar
      Member Array
      Join Date : 11th August 2012
      Posts : 20
      Rep Power : 345
      Likes Received
      2
      Likes Given
      1

      Default Re: KATIBA MPYA: hivi ndivyo wasemavyo watanzania

      Yap, mimi bila kukwaruza maneno naunga mkono kipengele cha 7, na kupendekeza muungano uvunjwe hauna maana yoyote hasa kwa Zanzibar,,,kila mtu achukue kilichokuwa chake,,,miungano ya kijinga, kitapeli na kihuni yameshapitwa na wakati,,,,kila mtu akamate chake.

    17. #15
      mzalendokimathi's Avatar
      Member Array
      Join Date : 11th August 2012
      Posts : 20
      Rep Power : 345
      Likes Received
      2
      Likes Given
      1

      Default Re: KATIBA MPYA: hivi ndivyo wasemavyo watanzania

      Mungu alivyoumba nchi tofauti na hadi makabila tofauti hakuwa mpumbavu wala mwendawazimu alitaka watu wajuane kila mtu anakotoka na akae, ale, alime avune kilicho chake,,,muungano mwisho chumbe.

    18. #16
      Mbozib's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th April 2012
      Posts : 358
      Rep Power : 430
      Likes Received
      43
      Likes Given
      5

      Default Re: KATIBA MPYA: hivi ndivyo wasemavyo watanzania

      Umesahau jambo moja la muhimu sana nalo ni tume huru ya uchaguzi lazima iundwe na rais asiwe na mamlaka juu ya tume. Na jambo lingine ni kurudisha maadili ya uongozi , pia mahakama zipewe uhuru bila kuingiliwa na wanasiasa ktk kutoa hukumu.

    19. #17
      Ibnu Mussa's Avatar
      Member Array
      Join Date : 27th June 2012
      Posts : 19
      Rep Power : 511
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: KATIBA MPYA: hivi ndivyo wasemavyo watanzania

      Huu muungano wetu kweli ni wa kishenzi. Kama Watanganyika bado wana haja ya kuungana watafute wapuuzi wenzao waungane nao, sisi wazanzibari basi. Tunataka mamlaka kamili sasa.

    20. #18
      Ndoa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd December 2011
      Posts : 629
      Rep Power : 502
      Likes Received
      119
      Likes Given
      46

      Default

      Quote By Ibnu Mussa
      Huu muungano wetu kweli ni wa kishenzi. Kama Watanganyika bado wana haja ya kuungana watafute wapuuzi wenzao waungane nao, sisi wazanzibari basi. Tunataka mamlaka kamili sasa.
      viongozi wa muungano wa bara na zanzibar ndio wapuuzi.

    21. #19
      Sir H's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th March 2012
      Posts : 307
      Rep Power : 425
      Likes Received
      68
      Likes Given
      0

      Default Re: KATIBA MPYA: hivi ndivyo wasemavyo watanzania

      Nachukua fursa hii kumshukuru mtoa mada kwn amejitahd kuzipangilia hoja zke za msingi na zenye tija kabisa!

      Pia niwashukuru wachangiaji wa hoja hii kwn nao wameonyesha umakini,uzalendo na upendo wa hali ya juu sana na hivi ndivyo inavyotupasa kushikamana ili kulinusuru taifa letu na mabaya yasiyofaa hasa kwa watanzania wenyewe

      Katika hoja yake nambarh 10,mtoa mada amezungumzia suala nyeti kabisa "udini"ambalo limekuwa likivunja na kuathiri uhuru wa wengi na kuwanufaisha wachache kwa maslah yao wenyewe nami pia naunga mkono kuwa suala hili likemewe ipasavyo.

      Hali kadhalika mtoa mada ametoa ushauri mzur kabisa kuwa serikali ione umuhimu wa kuacha madaraka yote ya kidini yasimamiwe na dini husika bila ya serikali kuingilia ili kulinda uhuru wa kila mtanzania! Mimi ni mwanafunzi wa kidato cha tano ktk shule fulani hapa nchini tena ya serikali! Nimeanza masomo ktk shule hyo mwezi May na hadi hvi sasa shule hiyo haina mabweni ya kutosha na sisi wanafunzi wa kidato cha tano inatubidi kulala kwnye vyumba vya madarasa huku tukipigwa na baridi ucku kucha! Wakati huohuo,tunaona kwnye vyombo vya habar mara leo kiongozi mkuu wa serikali amehudhuria ufunguzi au mahafali ya st this,st that na madrasa[zilizo chini ya dini] na kutoa mchango wake wa mamilioni kadhaa huku akisema,"kutoa ni moyo si utajiri hvyo naomba mpokee kidogo nlichonacho cha milion 200 tu" Jamani hvi baba wa mji unawezaje kutoa mchango wa harusi tena wa dini wakati kwko wanalala njaa?

      Ifikie pahala sasa watanzania tujitambue hasa ktk mchakato huu wa katiba mpya!

      Wito wngu kwa watanzania wenzangu pamoja na wachangiaji wa mada hii mara tu watakaposoma hizi inscriptions zngu,watoe msaada wa kutambulisha maovu yaliyomo ktk katiba tuliyo nayo kwn kw kufanya hvyo itatia hamasa kwa watanzania kupinga vikali mabaya hayo yaliyomo ktk katiba hii.

      Ktk falsafa yake,mzalendo wa Ghana Kwame Nkrumah aliwah kusema,"thought without practice is blind and practice without thought is empty"hvyo nasi sasa ni muda stahiki kabisa wa kuyafanyia kazi mawazo yetu

      Hata mzee wetu baba wa taifa aliwah kusema ktk chuo cha wellesley 1960 kuwa"we must create the Africa by which the outsiders will look and say,if you real want to see how people live peacefully go to Africa"nasi tuijenge Tanzania mfano kwa wageni

    22. #20
      mtayeshelwa's Avatar
      Member Array
      Join Date : 28th October 2011
      Posts : 79
      Rep Power : 397
      Likes Received
      7
      Likes Given
      9

      Default Re: KATIBA MPYA: hivi ndivyo wasemavyo watanzania

      Quote By oba
      wajameni, katika pita pita yangu kwenye mtandao nimekutana na maoni yafuatayo ya mtanzania mmoja juu ya katiba mpya;


      yafuatayo ni maoni yangu;
      1. Rais apunguziwe madaraka katika uteuzi wa viongozi waandamizi wa serikali au mahakama
      2. Nafasi ya spika wa bunge iwe ni kwa mtanzania yeyote mwenye sifa na huyo mtu atume maombi kwenye kamati maalumu ya bunge, asiwe mbunge wa jimbo au chama chochote ili kuepusha mgongano wa maslahi wakati akitekeleza wajibu wake
      3. Mawaziri wasiwe wabunge ili kurahisisha bunge kuisimamia serikali na kuondoa mgongano wa maslahi bungeni.
      4. Ubunge wa viti maalum uvunjwe kwani kama mawaziri hawatakuwa wabunge, rais hatakuwa na haja ya kuteua watu kadhaa kuwa wabunge ili wamsaidie kutawala.
      5. Wakuu wa mikoa na wilaya wasiteuliwe na raisi, la ikiwezekana nafasi hizo ziondolewe.
      6. Muungano wa tanganyika na zanzibar uwe na serikali moja, pemba liwe jimbo na unguja liwe jimbo katika serikali moja tu. Tanzania bara igawanywe pia katika majimbo. Kila jimbo liwe na seneta na utawala wa ndani na liluhusiwe kuwa na serikali kulingana na uhitaji wake. Serikali kuu iwe na wizara chache tu kama ulinzi, fedha, ndani, nje na afya nyingine ziendeshwe na majimbo husika kulingana na uhitaji wa kila jimbo
      7. Kama serikali moja haiwezekani basi muungano uvunjwe; hakuna sababu ya kuwa na serikali tatu kwani zitaongeza mzigo kwa wananchi wa kuziendesha, serikali mbili zimeshindwa kuleta muungano halisi.
      8. Wataalamu wa sekta mbalimbali wapewe vipaumbele na ikiwezekana wathaminiwe kuliko wanasiasa, hiyo itaongeza uzalendo kwa wataalamu hao ambao tunawahitaji zaidi kuliko wanasiassa.
      9. Madiwani na wabunge wawe wasomi wa japo degree moja, hiyo itawawezesha kudadavua hoja zinazoletwa na wataalamu walio chini yao. Tofauti na sasa ambapo mbunge std vii anapewa jukumu la kuchallenge utalaamu wa injinia au daktari na ikiwezekana kuupinga huku uelewa wake ukiwa ni wa chini kwa ujumla au katika eneo lile.
      10. Nchi hii haina dini na itabaki hivyo...suala la mambo ya dini fulani kama mahakama ya kadhi au mabaraza ya dini fulani yaachiwe waumini wa dini hiyo na serikali isijihusishe na mambo hayo. Itoe uhuru wa kila dini kuendesha mambo yanayoihusu bila kuathiri sheria za nchi wala usalama wa watu wa dini nyingine

      nitafurahi maoni yangu yakizingatiwa

      my take; tume husika inafuatilia mijadala hii kwa uhakika?
      mkuu naomba niunge mkono mapendekezo yako yote ila naomba kutia msisitizo pendekezo la mwisho kwano kuna vikundi vya watu vimejipanga kuingiza mambo ya dini zao kwenye katiba mpya washindwe na walegee tuko macho.

    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...