Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Katiba Mpya Uchaguzi Ujao na Hali ya Muungano

    Report Post
    Results 1 to 8 of 8
    1. #1
      Profesa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th October 2010
      Location : Anywhere in Africa
      Posts : 511
      Rep Power : 751
      Likes Received
      219
      Likes Given
      322

      Default Katiba Mpya Uchaguzi Ujao na Hali ya Muungano

      1. Raisi aliyepita ni wa Bara, na wa sasa ni Bara, atakaekuja atatoka Bara au Visiwani?
      2. Raisi wa sasa ni Muislamu, na ajaye atakuwa Muislamu kwa kuwa awamu ya tatu itakuwa ngumu kuacha kuwapa nafasi Wazanzibari ambao wengi ni waislamu? kulinda muungano?
      3. Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ni ya mseto, ya bara ni ya chama kimoja, iwapo mseto utapatikana bara kwa chama tofauti na mseto wa Zanzibar hii itamaanisha nini?

      Napendekeza yafuatayo ili kunusuru mgogoro mgumu utakao tokana na hojaji hizo hapo juu:

      1. Serikali ya Muungano iwe ya serikali tatu,
      a. Revolutionary state of Zanzibar, and
      b. the State of Tanganyika,
      c. United Republic of Tanzania

      Ambazo zote ziko semi autonomous isipokuwa tu kwa maswala ya ulinzi na usalama pamoja na uhamiaji (isipokuwa polisi), Afya, Revenues, Bank and monetary (kama kuna kitengo kingine muhimu mtaniongezea). Kutakuwa na bunge mojala Jmahuri ya Muungano wa Tanzania, na mabaraza mawilii, Baraza la wawakilishi la Tanganyika na baraza la wawakilishi wa Zanzibar.

      2. Kuwe na Mgombea binafsi ili watu kama Mheshimiwa Augustine Ramadhani ambaye ni Mkristo, akiridhia anaweza kugombea Uraisi na kunusuru mgogoro wa sasa.

      3. Madaraka ya raisi yatenganishwe na madaraka ya chama, na Rais asisimamie shughuli za chama iwapo atachaguliwa, ili awajibike kwa utendaji wake. Pia itasaidia raisi kuhangaika kutumia muda mwingi kusimamia interest za chama badala ya interest za Kitaifa. Na hii itasaidia sana kupunguza mgogoro pale ambapo serikali inabidi kuwa ya mseto, ukizaingatia nguvu ya upinzani inaongezeka.

      4. Wajumbe wa tume ya uchaguzi wa serikali ya Muungano wawe wa kuomba nafasi hiyo na kupitishwa na Bunge, na Bunge linaweza kupendekeza majina yao iwapo hawatajitokeza na kupitishwa na Bunge.

      5. Nafasi ya Uwaziri na Ukatibu Mkuu zote ziwe za kuomba na ziwe proffessional post na sio political. Ila bado Waziri apewe nafasi ya kuingia Bungeni.

      6. Nafasi za Wakuu wa Mkoa na Wilaya wabaki ili kulinda interest za Raisi, na Raisi apewe mamlaka ya kuwateua, hawa ndio watakaokuwa administrative officers na wanatoa balanmced supervissions na kusimamia presindents orders and wishes in respective jurisdictions.

      Tutaendelea....
      Communist likes this.

    2. Miaka 50

    3. #2
      Communist's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st June 2012
      Location : Ubungo
      Posts : 2,726
      Rep Power : 2266
      Likes Received
      601
      Likes Given
      783

      Default Re: Katiba Mpya Uchaguzi Ujao na Hali ya Muungano

      Basi piga kura hapa kuhusu aina ya muungano, tupate picha kuhusu uchaguzi ujao: http://www.jamiiforums.com/jukwaa-la...ba-ifuate.html
      Profesa likes this.
      Simple life is healthier than egoism.

    4. #3
      Profesa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th October 2010
      Location : Anywhere in Africa
      Posts : 511
      Rep Power : 751
      Likes Received
      219
      Likes Given
      322

      Default Re: Katiba Mpya Uchaguzi Ujao na Hali ya Muungano

      Nimepiga kura tayari Communist. Inapendeza hakikisha unatuandalia kareport ka matokeo na pia kuona uwezekano wa kukasambaza karipoti hako. Shukrani.
      Fredrick Sanga likes this.

    5. #4
      Fredrick Sanga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th January 2011
      Location : Kijitonyama
      Posts : 2,982
      Rep Power : 2590
      Likes Received
      637
      Likes Given
      776

      Default Re: Katiba Mpya Uchaguzi Ujao na Hali ya Muungano

      6. Wajumbe wa tume ya uchaguzi wa serikali ya Muungano wawe wa kuomba nafasi hiyo na kupitishwa na Bunge, na Bunge linaweza kupendekeza majina yao iwapo hawatajitokeza na kupitishwa na Bunge. This is good

      5. Nafasi ya Uwaziri na Ukatibu Mkuu zote ziwe za kuomba na ziwe proffessional post na sio political. Ila bado Waziri apewe nafasi ya kuingia Bungeni. That is good, ila wakubalike na bunge na bunge liwe na veto ya kuwatoa, Hawa jamaa wana viburi sana.

      6. Nafasi za Wakuu wa Mkoa na Wilaya wabaki ili kulinda interest za Raisi, na Raisi apewe mamlaka ya kuwateua, hawa ndio watakaokuwa administrative officers na wanatoa balanmced supervissions na kusimamia presindents orders and wishes in respective jurisdictions
      . Hapana, Hapana. Wachaguliwe na wananchi wakati wa uchaguzi mkuu, na wawe wenyiviti wa hamashauri na mikoa. Pia bunge na wananchi wawe na veto ya kuwaondoa.

      "If a leader is not coming from the people he is leading, he has already lost the legitimacy of being a leader (e.g. kwa kanga na kofia na fulana na rushuwa). The same applies to when a leader has seized to stand for the right of the people he is leading, he has lost the righteousness of becoming a leader" (Haki na watu; by JK Senior)
      Profesa likes this.
      We shall overcome, righteousness shall always prevail.

    6. #5
      Profesa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th October 2010
      Location : Anywhere in Africa
      Posts : 511
      Rep Power : 751
      Likes Received
      219
      Likes Given
      322

      Default Re: Katiba Mpya Uchaguzi Ujao na Hali ya Muungano

      Quote By Fredrick Sanga
      6. Wajumbe wa tume ya uchaguzi wa serikali ya Muungano wawe wa kuomba nafasi hiyo na kupitishwa na Bunge, na Bunge linaweza kupendekeza majina yao iwapo hawatajitokeza na kupitishwa na Bunge. This is good

      5. Nafasi ya Uwaziri na Ukatibu Mkuu zote ziwe za kuomba na ziwe proffessional post na sio political. Ila bado Waziri apewe nafasi ya kuingia Bungeni. That is good, ila wakubalike na bunge na bunge liwe na veto ya kuwatoa, Hawa jamaa wana viburi sana.

      6. Nafasi za Wakuu wa Mkoa na Wilaya wabaki ili kulinda interest za Raisi, na Raisi apewe mamlaka ya kuwateua, hawa ndio watakaokuwa administrative officers na wanatoa balanmced supervissions na kusimamia presindents orders and wishes in respective jurisdictions
      . Hapana, Hapana. Wachaguliwe na wananchi wakati wa uchaguzi mkuu, na wawe wenyiviti wa hamashauri na mikoa. Pia bunge na wananchi wawe na veto ya kuwaondoa.

      "If a leader is not coming from the people he is leading, he has already lost the legitimacy of being a leader (e.g. kwa kanga na kofia na fulana na rushuwa). The same applies to when a leader has seized to stand for the right of the people he is leading, he has lost the righteousness of becoming a leader" (Haki na watu; by JK Senior)
      Sikatai kabisa Bwana Fredrick Sanga, changamoto ya Democrasia inayoanza kukomaa ni pale ambapo, kama atatokea mtu mzuri wa kueneza propaganda nzuri kuliko wewe Raisi, basi hakuna maagizo wala vission utakayo ipresent na ikatekelezwa kwa urahisi, kwa kuwa hakuna mahali ambapo una meno.

      Role ya Hawa wakuu wa Mikoa na Wilaya ni muhimu sana kupunguza viburi vya wakurugenzi. Je unajua kwa mfumo ulivyo, Mkuu wa Wilaya ndiye anayeweza kutoa maagizo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri na si vinginevyo? na ndani ya Wilaya Moja kunaweza kuwa na halmashauri moja?

      Huwezi kuwa raisi halafu usiwe na some levels of power, otherwise uongozi wako utakuwa na mapengo. Kwa kawaida, Nchi inatakiwa iwe na mfumo ambao hata kama Raisi ni Dhaifu, isiyumbe, bado natafakari njia bora zaidi iwapo kama tuatmpigia mkuu wa wilaya kura, itakuwaje? majukumu yake yatakuwa ni yapi?

      Nahisi atakuwa hana wadhifa, labda tuje na utaratibu wa Majimbo ambao binafsi ninaukubali, wasioukubali ni wale wanaohofia kuwa watu wa maeneo fulani watarudi nyumba kimaendeleo!!??? Ni arrangements tu na kuwepo kwa subsdising grants kwa halmashauri kama za Mikindani na kwengineko ambazo revenue collection iko chini. Majombo ni sawa na kuwekza ushindani katika biashara ya kisiasa. Jimbo gani zuri? Linazalisha mali kwa wingi?

      Lina watu wenye uwezo mkubwa? Muhimu nji kuto limit movement order ya watu ambao ni raia au wana permit nchini. Nitafurahi kwa mfano Wamasai wakipata Jimbo lao wakasimamia vema kwa sheria zao utaratibu wa Malisho kwa mila zao bila kubughudhiwa na waroho wa Ardhi wanaotaka kuwagawia Waarabu wakati wao hawagain wala haieleweki nchi inagain kiasi gani!!Mfano: Kama ni kwagawa eneo wamasai waamue sio Mzanzibar aje awaamulie wamasai.

      Hapo ndipo mipaka inapokuwa. Nikimaanisha aidea ya Ardhi kuwa ya serikali iwe na categories, na process ambazo zinailipa baraza la eneo husika la ardhi mamlaka makubwa kabisa, wakikataa kusiwe na power nyingine ya kuamua matumizi ya ardhi yao, ila kwa sasa kuna mwanya ndio maana wanakuja tuuu bila mpangilio, wanamaniputale mambo na madocument yao complicated masikini wazee wale achilia mbali hicho kiingereza, mkataba hawaujui na hata kama kama wana nahati ya kuuona na wanochanganyikiwa ale wanapoondolewa.

      Unadhani kwanini kuna migogoro, wenye kuitaka ardhi huhakikisha interest zao zinalindwa zaidi za yule mwenye nayo, na mwenye dhamana ambaye ni kiongozi anakiuka miiko na kumpa favour mwekezaji...

      TUNAHITAJI KATIBA MPYA KWAKWELI

    7. RukaaJuu Final

    8. #6
      Communist's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st June 2012
      Location : Ubungo
      Posts : 2,726
      Rep Power : 2266
      Likes Received
      601
      Likes Given
      783

      Default Re: Katiba Mpya Uchaguzi Ujao na Hali ya Muungano

      Nakubaliana na wewe kabisa.
      Lakini angalia sana hoja ya madaraka ya raisi, kila mtu anateuliwa (Sanga is right in a way, you are talking the same thing)

      Tunataka Job Description za wafuatao:
      Mameya
      Wabunge
      Wenyeviti wa halmashauri
      Wenyeviti wa mikoa
      Wakuu wa mikoa
      Wakuuwa wilaya
      RAS
      DAR
      Wakurugenzi NK

      1. Pale umeshasema kuna wakurugenzi, kuna DAD, kuna RAS Nk haw wote wanatoka upande wa muhimili wa serikali
      2. Umesema vission, mtazamo wa dunia ya leo ni kwamba vision inajengwa kuanzia chini kwenda juu, na inamilikiwa na wananchi, Hawa wa serikalini wanatengeneza strategy, na zinapitishwa na wakilishi wa wananchi.
      3. Mkuu wa mkuo basically ni meya wa mkoa, kwanini achaguliwe na rais. Tumwachie hao wakurugenzi, DAD, na MA RAS. Sisi tuje tuwakomoli. wafanye kazi.

      Nitachangia zaidi, nime banwa na shughuli.
      Simple life is healthier than egoism.

    9. #7
      Profesa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th October 2010
      Location : Anywhere in Africa
      Posts : 511
      Rep Power : 751
      Likes Received
      219
      Likes Given
      322

      Default Re: Katiba Mpya Uchaguzi Ujao na Hali ya Muungano

      Wabunge waliochaguliwa majimboni wanaweza kuvuliwa Ubunge iwapo atashtakiwa na kuhukumiwa na mahakama, au kama itathibitika na kamati husika baada ya uchunguzi, amehusika na kuihujumu nchi kiuchumi na kisiasa, na au uchunguzi wowote uwe wa kamati halali au wa chombo cha dola umemtia hatiani kuhusika na kashfa yeyote inayohusiana na ukiukwaji wa maadili yawe ywa kijamii au ya kikazi, au kwa sababu zozote zile, wananchi wamewasilisha malalamiko rasmi ya kutomtaka mbunge wao. Mbunge huyo anaweza kundolewa kwa njia kuu mbili, kwa kura ya maoni ya chama chake (iwapo tuhuma ni za kukiuka misingi na maadili halali ya chama), kwa kura ya maoni ya wananchi, au kwa kura ya maoni ya bunge zima kutegemeana na tuhuma husika. Kura ya maoni inaweza kupigwa kwa kutumia namba ya simu ya wahusika na kwa mfumo ambao utaweza kuitambua simu hiyo (kwa kulingana na register) na namba ya uchaguzi ya muhusika na kumbukumbu zake zilizopo kwenye orodha ya kudumu ya daftari la mpiga kura. Ukokotoaji wa takwimu za kura utakuwa wa wazi na matokeo yatatangazwa wazi.

    10. #8
      Profesa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th October 2010
      Location : Anywhere in Africa
      Posts : 511
      Rep Power : 751
      Likes Received
      219
      Likes Given
      322

      Default Re: Katiba Mpya Uchaguzi Ujao na Hali ya Muungano

      Quote By Communist
      Nakubaliana na wewe kabisa.
      Lakini angalia sana hoja ya madaraka ya raisi, kila mtu anateuliwa (Sanga is right in a way, you are talking the same thing)

      Tunataka Job Description za wafuatao:
      Mameya
      Wabunge
      Wenyeviti wa halmashauri
      Wenyeviti wa mikoa
      Wakuu wa mikoa
      Wakuuwa wilaya
      RAS
      DAR
      Wakurugenzi NK

      1. Pale umeshasema kuna wakurugenzi, kuna DAD, kuna RAS Nk haw wote wanatoka upande wa muhimili wa serikali
      2. Umesema vission, mtazamo wa dunia ya leo ni kwamba vision inajengwa kuanzia chini kwenda juu, na inamilikiwa na wananchi, Hawa wa serikalini wanatengeneza strategy, na zinapitishwa na wakilishi wa wananchi.
      3. Mkuu wa mkuo basically ni meya wa mkoa, kwanini achaguliwe na rais. Tumwachie hao wakurugenzi, DAD, na MA RAS. Sisi tuje tuwakomoli. wafanye kazi.

      Nitachangia zaidi, nime banwa na shughuli.
      Wana Jamvi mwenye nakala ya Job Description za hawa hapo juu waliotajwa na Communist waturushie hapa tafadhali

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...