Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Bungeni: Spika anapaswa kuwa mwanasheria ili kudhibiti kazi zake vyema.

    Report Post
    Results 1 to 2 of 2
    1. #1
      mwitaz's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th February 2012
      Location : Mwanza
      Posts : 250
      Rep Power : 416
      Likes Received
      78
      Likes Given
      2

      Default Bungeni: Spika anapaswa kuwa mwanasheria ili kudhibiti kazi zake vyema.

      Baada kutafakari kwa kina kirefu kuhusu shughuli za Bunge la Jamhuri ya Tanzania nimegundua kuwa kuna udhaifu mkubwa ambao inanilazimu kusema kuna ulazima wa kubadilisha katiba ili kutia sharti ambalo litamruhusu mtu aliyosomea na kubobobea katika Sheria ndiye atakayepaswa kugombea Uspika wa Bunge ili kufanya kazi za Bunge kwa umahiri.

      Tazama mfano mmoja hai unaonekana katika ujumbe wa Mhe. J. Mnyika katika mtandao wa www.facebook.com ufuatao hapa chini:-

      "Kwanini niliomba
      muongozo-Sakata la
      Mgomo wa Madaktari
      Leo, Juni 22, 2012 nilitaka
      kuomba muongozo wa
      Spika kwa mujibu wa Kanuni 49 (2) baada ya
      Waziri wa Afya kutoa kauli
      juu ya utekelezaji wa madai
      ya madaktari.

      Kanuni hiyo
      inataka kauli isiwe ya
      kuzua mjadala lakini aliyoyaeleza waziri juu ya
      uboreshaji wa maslahi ya
      madaktari yanazua mjadala
      kwa kuwa yanatofautiana
      na majibu ya Waziri Mkuu,
      Mizengo Pinda aliyoyatoa bungeni jana, (Juni 21,
      2012) na pia hayana uhalisi.
      Mathalani, wakati serikali
      ikidai imeongeza posho ya
      kuitwa kazini (on call
      allowance) toka Februari, 2012 na kutumia bilioni 7.9
      kwa miezi michache,
      imetenga kwa watumishi
      wa Afya bilioni 18.9 tu kwa
      mwaka mzima wa
      2012/2013 kiwango ambacho hakitoshi.

      Hivyo nilitaka kuomba
      muongozo Spika awezeshe
      kauli hiyo ijadiliwe kama
      ilivyokuwa kwa kauli juu
      ya fedha za rada.
      Nakusudia kumuandikia barua Spika kushauri
      aelekeze kamati ya bunge
      ya huduma za jamii kauli
      hiyo ya waziri.

      Pia bunge halipaswi
      kunyimwa fursa ya
      kutumia mamlaka yake
      kwa mujibu wa ibara ya 63
      ya kuishauri na kuisimamia
      serikali kusuluhisha mgogoro na madaktari ili
      kuepusha mgomo wenye
      athari kwa nchi na
      wananchi kwa kisingizio
      cha kusudio la serikali
      kupeleka mgogoro mahakama kuu kwa kuwa
      mpaka leo taarifa
      iliyotolewa bungeni bado
      hakuna shauri katika
      kitengo cha kazi.

      Hivyo,
      Spika anapaswa kutoa jukumu kwa kamati husika
      ya bunge kuendelea na
      usuluhishi kabla ya serikali
      kukimbilia mahakamani. Wabunge tupewe nakala ya
      taarifa ya majadiliano ya
      pande mbili yaliyochukua
      zaidi ya siku 90 badala ya
      kupewa hotuba ya nusu
      saa ya upande mmoja wa serikali pekee.

      Hata serikali ikizuia mgomo
      wa wazi kwa zuio la
      kimahakama ieleweke
      kuwa mgomo wa chinichini
      kwa watumishi wa afya
      ambao una athari ya muda mrefu kwa maisha ya
      wananchi nchini.

      Mwisho, serikali ipunguze
      matumizi yasiyo ya lazima
      na ipanue wigo wa mapato.

      John John Mnyika.
      Mbunge Jimbo la Ubungo
      (CHADEMA)
      22 Juni, 2012
      Last edited by mwitaz; 23rd June 2012 at 01:13.

    2. Miaka 50

    3. #2
      Satanic_Verses's Avatar
      Member Array
      Join Date : 6th September 2011
      Posts : 37
      Rep Power : 397
      Likes Received
      3
      Likes Given
      22

      Default Re: Bungeni: Spika anapaswa kuwa mwanasheria ili kudhibiti kazi zake vyema.

      Mijadala ya bajeti huchukua asilimia kubwa ya muda wa vikao vya bunge yaani zaidi ya asilimia 70. Vituko vingi kama kufukuzana ukumbini au mbunge kuadhibiwa na bunge hutokea wakati wa bunge la bajeti.

      Ni nadra sana kukuta mitafaruku hii kutokea kwenye vikao vile vya Novemba, February na Aprili ambavyo ni vika 10 kwa session na ndivyo vinavyopitisha miswada mingi kuwa sheria.

      Hivyo, basi harakati nyingi ni wakati wa bajeti kama tunavyoona sasa. Na kama ni hivyo basi Spika anatakiwa awe na uelewa mkubwa wa mambo ya fedha na kama ni sheria basi ni kidogo tu.

      Hivyo, kwa Anne Makinda ambaye ni mtaaluma mzuri wa accounts basi uspika ndiyo saizi yake.

    4. FemaTV & Radio

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...