Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Wanasiasa waenguliwa Tume ya Katiba Mpya

    Report Post
    Results 1 to 18 of 18
    1. #1
      abdulahsaf's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st August 2010
      Posts : 860
      Rep Power : 723
      Likes Received
      123
      Likes Given
      1

      Default Wanasiasa waenguliwa Tume ya Katiba Mpya

      Tuesday, 29 March 2011


      Mwandishi Wetu

      MUSWADA maalumu wa kuunda Tume ya kukusanya maoni na kupendekeza muundo wa Katiba mpya ya Tanzania, unatarajiwa kuwasilishwa katika Bunge la Aprili, mwaka huu.

      Habari zilizolifikia gazeti hili jana zimeeleza kuwa muundo wa tume hiyo hautawashirikisha wabunge, wajumbe wa Baraza la Wawakilishi, Madiwani wala kiongozi yeyote wa kisiasa.

      Tume hiyo inayotarajiwa kuwa na wajumbe 30, itaundwa na Rais Jakaya Kikwete kwa kushirikiana na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohammed Shein na wajumbe wake watakuwa ni wanataaluma, hususan wanasheria na kwamba suala la jinsia litazingatiwa.

      Taarifa hizo zinaeleza pia kuwa Tume itaundwa na idadi sawa ya wajumbe kutoka Tanzania Bara na Visiwani na inatarajiwa kuwa na majukumu mbalimbali ikiwamo kuwahamasisha watu kujua maana na muundo wa Katiba.

      Majukumu mengine ya tume hiyo yaliyotajwa kwenye muswada huo ni kukusanya maoni kutoka kwa wananchi, kuchunguza na kuainisha muundo wa Katiba kulingana na mifumo ya kisiasa, kidemokrasia, uongozi, sheria za kiutawala na Serikali.

      Mara baada ya Bunge kupitisha muswada huo, Rais Jakaya Kikwete anatarajiwa kuusaini na kuiunda haraka iwezekanavyo tume hiyo ili ifikapo Juni mwaka huu ianze kazi yake.

      Kamati hiyo itatoa rasimu ya katiba hiyo mpya ikipendekeza pia muundo wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano utakavyokuwa.

      Mchakato wa kuunda tume hiyo unakuja baada ya Rais Kikwete kuwataka wananchi kuwa watulivu akisema suala hilo litaratibiwa kwa umakini ili kuwa na katiba bora ambayo itawasaidia Watanzania kwa muda mrefu.

      Tamko la Rais Kikwete la kuunda tume hiyo ndilo lililozima wimbi la madai ya Katiba mpya lililoshika kasi miongoni mwa watu wa kada mbalimbali ikiwamo wanasiasa, wasomi na wananchi wa kawaida.

      Katika mijadala hiyo, Katiba iliyopo imeelezewa kuwa imepitwa na wakati na haiendani na mahitaji ya mazingira ya sasa ya nchi.

      Vuguvugu hilo lilianza mara baada ya Uchaguzi Mkuu, Novemba mwaka jana na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kudai kuwa Katiba ya sasa haitoi haki ya kidemokrasia kwenye uchaguzi.


    2. #2
      Muro's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 27th October 2010
      Posts : 168
      Rep Power : 472
      Likes Received
      2
      Likes Given
      0

      Default Re: Wanasiasa waenguliwa Tume ya Katiba Mpya

      Haitoshi kuunda tume,iwe na wanasiasa au la, kinachotakiwa na wananchi ni katiba mpya kabla ya 2013 na siyo 2015,hivyo time frame ni muhimu sana,na smart objectives kuwa nini kifanyike lini na kwisha ni lini siyo maneno maneno tu.

    3. #3
      HISIA KALI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th October 2010
      Location : Mjini kwa mjomba
      Posts : 643
      Rep Power : 567
      Likes Received
      80
      Likes Given
      1

      Default Re: Wanasiasa waenguliwa Tume ya Katiba Mpya

      Quote By abdulahsaf View Post
      Written by mkulima // 30/03/2011 // Habari // No comments

      Tuesday, 29 March 2011 21:20//
      Mwandishi Wetu
      MUSWADA maalumu wa kuunda Tume ya kukusanya maoni na kupendekeza muundo wa Katiba mpya ya Tanzania, unatarajiwa kuwasilishwa katika Bunge la Aprili, mwaka huu.Habari zilizolifikia gazeti hili jana zimeeleza kuwa muundo wa tume hiyo hautawashirikisha wabunge, wajumbe wa Baraza la Wawakilishi, Madiwani wala kiongozi yeyote wa kisiasa.
      Tume hiyo inayotarajiwa kuwa na wajumbe 30, itaundwa na Rais Jakaya Kikwete kwa kushirikiana na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohammed Shein na wajumbe wake watakuwa ni wanataaluma, hususan wanasheria na kwamba suala la jinsia litazingatiwa.
      Taarifa hizo zinaeleza pia kuwa Tume itaundwa na idadi sawa ya wajumbe kutoka Tanzania Bara na Visiwani na inatarajiwa kuwa na majukumu mbalimbali ikiwamo kuwahamasisha watu kujua maana na muundo wa Katiba.
      Majukumu mengine ya tume hiyo yaliyotajwa kwenye muswada huo ni kukusanya maoni kutoka kwa wananchi, kuchunguza na kuainisha muundo wa Katiba kulingana na mifumo ya kisiasa, kidemokrasia, uongozi, sheria za kiutawala na Serikali.
      Mara baada ya Bunge kupitisha muswada huo, Rais Jakaya Kikwete anatarajiwa kuusaini na kuiunda haraka iwezekanavyo tume hiyo ili ifikapo Juni mwaka huu ianze kazi yake.Kamati hiyo itatoa rasimu ya katiba hiyo mpya ikipendekeza pia muundo wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano utakavyokuwa.
      Mchakato wa kuunda tume hiyo unakuja baada ya Rais Kikwete kuwataka wananchi kuwa watulivu akisema suala hilo litaratibiwa kwa umakini ili kuwa na katiba bora ambayo itawasaidia Watanzania kwa muda mrefu.
      Tamko la Rais Kikwete la kuunda tume hiyo ndilo lililozima wimbi la madai ya Katiba mpya lililoshika kasi miongoni mwa watu wa kada mbalimbali ikiwamo wanasiasa, wasomi na wananchi wa kawaida.Katika mijadala hiyo, Katiba iliyopo imeelezewa kuwa imepitwa na wakati na haiendani na mahitaji ya mazingira ya sasa ya nchi.
      Vuguvugu hilo lilianza mara baada ya Uchaguzi Mkuu, Novemba mwaka jana na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kudai kuwa Katiba ya sasa haitoi haki ya kidemokrasia kwenye uchaguzi.
      Hii ya idadi sawa ya wajumbe kutoka Bara na Visiwani mimi sikubaliane nayo. Rule of majority lazima ipewe nafasi kwenye hii process. Of course lazima wananchi kwa ujumla wao wapate nafasi ya kupiga kura ya kukubali katiba mpya. Sasa bara kuna watu wengi zaidi ya Visiwani na ikitokea watu wa bara wakapiga kura ya maamuzi tofauti na wale wa Visiwani ni nini kitatokea?

    4. #4
      Taso's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th June 2010
      Posts : 1,182
      Rep Power : 800
      Likes Received
      309
      Likes Given
      124

      Default Re: Wanasiasa waenguliwa Tume ya Katiba Mpya

      Quote By abdulahsaf View Post
      Wanasiasa waenguliwa Tume
      "Wanasiasa waenguliwa Tume..." kwani walikuwemo kwenye Tume?

      Madai ya uongo na kweli yasiyoenda shule.

    5. smz is offline
      smz
      #5
      smz's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th December 2010
      Posts : 251
      Rep Power : 485
      Likes Received
      28
      Likes Given
      1

      Default Re: Wanasiasa waenguliwa Tume ya Katiba Mpya

      Kwa maana hiyo Tume itawajibika kwa raisi, au?


    6. #6
      Sooth's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th April 2009
      Posts : 929
      Rep Power : 702
      Likes Received
      314
      Likes Given
      200

      Default Re: Wanasiasa waenguliwa Tume ya Katiba Mpya

      Mi naona hiyo tume itakuwa na watu wengi kupita kiasi. Labda kwa sababu sijui hadidu za rejea za tume hiyo, lakini pamoja na hayo, watu 30 ni wengi sana, hasa ukifikiria hali ya nchi kiuchumi ambapo wafadhili hawajatoa pesa walizoahidi katika bajeti.
      "There is a very thin line between inflation and extortion."-Sooth.

    7. #7
      Gurti's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 19th November 2010
      Posts : 208
      Rep Power : 476
      Likes Received
      47
      Likes Given
      20

      Default Re: Wanasiasa waenguliwa Tume ya Katiba Mpya

      Kwani hoja ya katiba mpya ilianzishwa na wanasheria? Wanasiasa lazima wawepo. Hatutaki changa la macho.

    8. mob is online now
      mob
      #8
      mob's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th December 2009
      Posts : 649
      Rep Power : 614
      Likes Received
      114
      Likes Given
      42

      Default Re: Wanasiasa waenguliwa Tume ya Katiba Mpya

      kama idadi sawa zanzibar in wakazi wangapi na bara in wakazi wangapi?

    9. #9
      MTAZAMO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th February 2011
      Posts : 4,448
      Rep Power : 2250
      Likes Received
      1902
      Likes Given
      2828

      Default

      Quote By smz View Post
      Kwa maana hiyo Tume itawajibika kwa raisi, au?
      Hili la wanasiasa kutokuwepo limekaa kisiasa zaidi hata zitolewe sababu zipi.nguzo za maendeleo kwa mujibu wa azimio la arusha(kama sikosei) ni watu,ardhi na siasa safi.kuna mambo ya kisiasa lazima kundi lao lihusike direct maana wapo wanasiasa wanasheria n.k.fatilia uteuzi wa hao wataalam kama hujakuta wote wanakadi za ccm!

    10. #10
      Mr. Zero's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th June 2007
      Posts : 4,102
      Rep Power : 1445
      Likes Received
      485
      Likes Given
      72

      Default Re: Wanasiasa waenguliwa Tume ya Katiba Mpya

      Quote By Gurti View Post
      Kwani hoja ya katiba mpya ilianzishwa na wanasheria? Wanasiasa lazima wawepo. Hatutaki changa la macho.

      Cha maana iwe inakidhi mahitaji yetu kwa sasa!! Kama wataleta sarakasi, hatukubali!!
      "The Only Necessary for the Triumph of Evil is for Good Men to do Nothing" Edmund Burke (1729 - 97)

    11. #11
      De Javu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th May 2010
      Location : Onboard Pirate-ship off Somalia
      Posts : 267
      Rep Power : 522
      Likes Received
      22
      Likes Given
      6

      Default Re: Wanasiasa waenguliwa Tume ya Katiba Mpya

      Quote By mob View Post
      kama idadi sawa zanzibar in wakazi wangapi na bara in wakazi wangapi?
      Kinachojadiliwa hapa ni Katiba ya MUUNGANO, Muungano ni wa sehemu mbili baina ya Tanganyika na Zanzibar ili kutenda haki ni lazima iwe hivyo. Katiba iliyopo ndio inayopigiwa kelele kua haitendei haki upande mmoja,pia hao wajumbe wataangalia pande wanazotoka kuona mahitaji/maslahi/mapungufu ya kila upande. Kumaliza matatizo ni lazima pande mbili zilizoungana zikae upya kujadili aina ya muungano/katiba utakaonufaisha pande zote.
      If you think EDUCATION is expensive....Try IGNORANCE and see how much it costs.

    12. #12
      Mzalendo Mkuu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd November 2010
      Posts : 569
      Rep Power : 556
      Likes Received
      104
      Likes Given
      288

      Default Re: Wanasiasa waenguliwa Tume ya Katiba Mpya

      Quote By smz View Post
      Kwa maana hiyo Tume itawajibika kwa raisi, au?
      Bila shaka yoyote. Hii ndiyo hali halisi maana mwenye kisu ndiye anayekula nyama. Shida ya tume yetu ni kule kuundwa na rais kwa vyovyote vile tumeitawajibika kwake. Hapo ndipo siasa inapokuwa na nguvu hata kama ndani ya tume hakuna wanasiasa. Tuombe heri

    13. #13
      Haika's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd March 2008
      Posts : 1,716
      Rep Power : 924
      Likes Received
      249
      Likes Given
      367

      Default Re: Wanasiasa waenguliwa Tume ya Katiba Mpya

      Wanasiasa ni watu wapi hao?
      mfano mtu kama Lamwai anaweza kuwamo?

    14. #14
      Rangi 2's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 5th February 2011
      Location : Bwiru-Mwanza
      Posts : 102
      Rep Power : 444
      Likes Received
      18
      Likes Given
      74

      Default Re: Wanasiasa waenguliwa Tume ya Katiba Mpya

      Eeh Bwanae! Bunge ndio liainishe sifa za watanzania wanaopaswa kushiriki katika Tume ya katiba mpya.

    15. #15
      Hofstede's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th July 2007
      Posts : 3,604
      Rep Power : 21345
      Likes Received
      981
      Likes Given
      988

      Default Re: Wanasiasa waenguliwa Tume ya Katiba Mpya

      Quote By nickname View Post
      Tuesday, 29 March 2011 21:20
      Mwandishi Wetu
      MUSWADA maalumu wa kuunda Tume ya kukusanya maoni na kupendekeza muundo wa Katiba mpya ya Tanzania, unatarajiwa kuwasilishwa katika Bunge la Aprili, mwaka huu.Habari zilizolifikia gazeti hili jana zimeeleza kuwa muundo wa tume hiyo hautawashirikisha wabunge, wajumbe wa Baraza la Wawakilishi, Madiwani wala kiongozi yeyote wa kisiasa.

      Tume hiyo inayotarajiwa kuwa na wajumbe 30, itaundwa na Rais Jakaya Kikwete kwa kushirikiana na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohammed Shein na wajumbe wake watakuwa ni wanataaluma, hususan wanasheria na kwamba suala la jinsia litazingatiwa.

      Taarifa hizo zinaeleza pia kuwa Tume itaundwa na idadi sawa ya wajumbe kutoka Tanzania Bara na Visiwani na inatarajiwa kuwa na majukumu mbalimbali ikiwamo kuwahamasisha watu kujua maana na muundo wa Katiba.

      Majukumu mengine ya tume hiyo yaliyotajwa kwenye muswada huo ni kukusanya maoni kutoka kwa wananchi, kuchunguza na kuainisha muundo wa Katiba kulingana na mifumo ya kisiasa, kidemokrasia, uongozi, sheria za kiutawala na Serikali.

      Mara baada ya Bunge kupitisha muswada huo, Rais Jakaya Kikwete anatarajiwa kuusaini na kuiunda haraka iwezekanavyo tume hiyo ili ifikapo Juni mwaka huu ianze kazi yake.Kamati hiyo itatoa rasimu ya katiba hiyo mpya ikipendekeza pia muundo wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano utakavyokuwa.

      Mchakato wa kuunda tume hiyo unakuja baada ya Rais Kikwete kuwataka wananchi kuwa watulivu akisema suala hilo litaratibiwa kwa umakini ili kuwa na katiba bora ambayo itawasaidia Watanzania kwa muda mrefu.

      Tamko la Rais Kikwete la kuunda tume hiyo ndilo lililozima wimbi la madai ya Katiba mpya lililoshika kasi miongoni mwa watu wa kada mbalimbali ikiwamo wanasiasa, wasomi na wananchi wa kawaida.Katika mijadala hiyo, Katiba iliyopo imeelezewa kuwa imepitwa na wakati na haiendani na mahitaji ya mazingira ya sasa ya nchi.

      Vuguvugu hilo lilianza mara baada ya Uchaguzi Mkuu, Novemba mwaka jana na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kudai kuwa Katiba ya sasa haitoi haki ya kidemokrasia kwenye uchaguzi.

      My Take: Nionavyo mimi ni kweli wanasiasa wanatakiwa wakae pembeni wasiingilie mchakato wa katiba mpya.Wanasiasa wanatakiwa washiriki mchakato wa katiba mpya kwa kutoa maoni na pia uwahamasisha wananchi watoe maoni kwa Tume ya Katiba.Hii itasaidia mchakato wa Katiba mpya uende haraka na Katiba mpya ipatikane kabla ya 2015.
      Mkuu hivi na wewe kama great thinker kweli umeingia kwenye huu mkenge na mchezo wa kunguni kutoka juu ya shuka kujificha chini ya shuka?. Huu ni mchezo wa kitoto ambao CCM wanataka kuucheza ili kulinda masilahi yao. Huwezi kusema wanasiasa wasiwemo wakati wateuzi wa tume hiyo ni wanasiasa tena wote wa kutoka CCM. Hakuna jipya hapa kama mteuzi ni Mwanasiasa tume hiyo itakuwa answerable kwa mwanasiasa na hakuna mtu atakayekuwa tayari kuteua watu ambao hana imani kuwa watamlindia masilahi yake. Kinachotakiwa kufanyika hapa zaidi ya hili changa la macho ni.

      Ilitakiwa Muswada upelekwe bungeni wa kutaka tume hiyo iundwe na
      1. Mwakilishi wa kila chama chenye mbunge mmoja au zaidi bungeni
      2. Kila taasisi ya dini yaani waislam na wakristo watoe wawakilishi wawili wawili
      3. TANGO, au umoja wa NGO utoe mwakilishi mmoja
      4. Taasisi za elimu ya juu za serikali zitoe wawakilishi wawili
      5. Taasisi za elimu ya juu za binafsi zitoe mwakilishi mmoja
      6. Serikali ya Jamhuri itoe wawakilishi wawili na ya Zanzibar wawili

      Kazi za hii tume ambayo katika muswada huo na budget yake iwekwe kabisa itakuwa ni

      1. Kumchagua mwenyekiti, makamu mwenyekiti na katibu wa tume miongoni mwao ambao kazi zao hazitakuwa beyond organising public hearings na kukusanya maoni ambapo baada ya kila mkutano kila mjumbe anapewa kopi yake na kazi ya katibu ni kuwa na maoni yote kwa muda wowote na wakati wowote electronically, I mean kwenye video na muhtasari kwenye hard copy.

      2. Tume hii iwe huru kuajiri wanasheria na wataalam waliobobea katika fani mbalimbali katika kuhakikisha kuwa kazi yao inaenda vizuri wakiwemo wa kisheria, IT, fedha etc.

      3. Kuyaunganisha mawazo ya wananchi wote na kuyafanyia tathmini ili kuondoa yanayopingana na kisha kuchapisha rasimu yake kama katiba na kuirudisha tena kwa wananchi kuijadili kwa totality na kuongeza ama kufanyia marekebisho baadhi. Na baada ya hapo inapigiwa kura na wajumbe wa tume hiyo kwa kigezo kuwa kilichomo ndani ya rasimu ni maoni solely ya wananchi na hakuna kipengele chochote kilichopachikwa either na wanatume au nje. Ili Rasimu ipite ni lazima wajumbe wote waikubali si kwa kuwa yaliyomo yamewafurahisha la bali kwa kuonesha kuwa kumbukumbu zao za maoni ya wananchi na kilichomo havitofautiani.

      4. Baada ya hapo rasimu hiyo inaanza kunadiwa kwa wananchi kwa ajili ya kuipitishwa kwa referendum na tume ya kusimamia referendum hiyo inachaguliwa na kuundwa na Tume hiyo kwa wajumbe wote kuwakubali watendaji wa tume kwa sauti moja.

      Wakati wa referendum sasa hapo watu wanaweza kuchukua upande na kazi ya tume inakuwa imefikia kikomo pale tu rasimu hiyo inapokuwa imepitishwa na asilimia si chini ya 60% wananchi ya wapiga kura wote walioandikishwa na tume ya uchaguzi ya referendum ambayo itapata maagizo yote kutoka kwenye tume ya katiba, Mchakato huu utatakiwa uwe umekamilika mwishoni mwa 2012 ili kutoa nafasi kwa vyama na serikali kujiandaa na uchaguzi wa 2015 kwa kutumia katiba mpya.

      HUU MCHAKATO UKIFANYIKA NDIYO UTAKUWA UMEWAENGUA WANASIASA KATIKA KUINFLUENCE OUTCOME YA TUME HII NA SI KWA KUCHAGULIWA NA SHEIN AU KIKWETE.

    16. #16
      Mpendanchi-2's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th April 2009
      Posts : 311
      Rep Power : 582
      Likes Received
      18
      Likes Given
      10

      Default Re: Wanasiasa waenguliwa Tume ya Katiba Mpya

      Quote By Hofstede View Post
      Mkuu hivi na wewe kama great thinker kweli umeingia kwenye huu mkenge na mchezo wa kunguni kutoka juu ya shuka kujificha chini ya shuka?. Huu ni mchezo wa kitoto ambao CCM wanataka kuucheza ili kulinda masilahi yao. Huwezi kusema wanasiasa wasiwemo wakati wateuzi wa tume hiyo ni wanasiasa tena wote wa kutoka CCM. Hakuna jipya hapa kama mteuzi ni Mwanasiasa tume hiyo itakuwa answerable kwa mwanasiasa na hakuna mtu atakayekuwa tayari kuteua watu ambao hana imani kuwa watamlindia masilahi yake. Kinachotakiwa kufanyika hapa zaidi ya hili changa la macho ni.

      Ilitakiwa Muswada upelekwe bungeni wa kutaka tume hiyo iundwe na
      1. Mwakilishi wa kila chama chenye mbunge mmoja au zaidi bungeni
      2. Kila taasisi ya dini yaani waislam na wakristo watoe wawakilishi wawili wawili
      3. TANGO, au umoja wa NGO utoe mwakilishi mmoja
      4. Taasisi za elimu ya juu za serikali zitoe wawakilishi wawili
      5. Taasisi za elimu ya juu za binafsi zitoe mwakilishi mmoja
      6. Serikali ya Jamhuri itoe wawakilishi wawili na ya Zanzibar wawili

      Kazi za hii tume ambayo katika muswada huo na budget yake iwekwe kabisa itakuwa ni

      1. Kumchagua mwenyekiti, makamu mwenyekiti na katibu wa tume miongoni mwao ambao kazi zao hazitakuwa beyond organising public hearings na kukusanya maoni ambapo baada ya kila mkutano kila mjumbe anapewa kopi yake na kazi ya katibu ni kuwa na maoni yote kwa muda wowote na wakati wowote electronically, I mean kwenye video na muhtasari kwenye hard copy.

      2. Tume hii iwe huru kuajiri wanasheria na wataalam waliobobea katika fani mbalimbali katika kuhakikisha kuwa kazi yao inaenda vizuri wakiwemo wa kisheria, IT, fedha etc.

      3. Kuyaunganisha mawazo ya wananchi wote na kuyafanyia tathmini ili kuondoa yanayopingana na kisha kuchapisha rasimu yake kama katiba na kuirudisha tena kwa wananchi kuijadili kwa totality na kuongeza ama kufanyia marekebisho baadhi. Na baada ya hapo inapigiwa kura na wajumbe wa tume hiyo kwa kigezo kuwa kilichomo ndani ya rasimu ni maoni solely ya wananchi na hakuna kipengele chochote kilichopachikwa either na wanatume au nje. Ili Rasimu ipite ni lazima wajumbe wote waikubali si kwa kuwa yaliyomo yamewafurahisha la bali kwa kuonesha kuwa kumbukumbu zao za maoni ya wananchi na kilichomo havitofautiani.

      4. Baada ya hapo rasimu hiyo inaanza kunadiwa kwa wananchi kwa ajili ya kuipitishwa kwa referendum na tume ya kusimamia referendum hiyo inachaguliwa na kuundwa na Tume hiyo kwa wajumbe wote kuwakubali watendaji wa tume kwa sauti moja.

      Wakati wa referendum sasa hapo watu wanaweza kuchukua upande na kazi ya tume inakuwa imefikia kikomo pale tu rasimu hiyo inapokuwa imepitishwa na asilimia si chini ya 60% wananchi ya wapiga kura wote walioandikishwa na tume ya uchaguzi ya referendum ambayo itapata maagizo yote kutoka kwenye tume ya katiba, Mchakato huu utatakiwa uwe umekamilika mwishoni mwa 2012 ili kutoa nafasi kwa vyama na serikali kujiandaa na uchaguzi wa 2015 kwa kutumia katiba mpya.

      HUU MCHAKATO UKIFANYIKA NDIYO UTAKUWA UMEWAENGUA WANASIASA KATIKA KUINFLUENCE OUTCOME YA TUME HII NA SI KWA KUCHAGULIWA NA SHEIN AU KIKWETE.

      Nakubaliana na wewe mkuu kwa silimia 100%, hiyo tume ikichaguliwa kwa mfumo uliopendekeza ndiypo itaitwa TUME HURU, vinginevyo kama mswada unavyotaka itakuwa Tume ya Kikwete, na itakwenda kuwakilisha mawazo ya Kikwete hata siku mmoja haitapeleka wazo la mwananchi la kumpunguzia madaraka Kikwete!! hiyo ni ndoto. Ikichaguliwa na Kikwete na Sheni italinda masilihi ya watawala waliopo sasa ambayo ndiyo inalalamikiwa.
      No one will help to build your Future Tanzania !!!! It's you and me , START NOW !!!

    17. #17
      Makucha's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 4th November 2010
      Posts : 189
      Rep Power : 474
      Likes Received
      16
      Likes Given
      0

      Default Re: Wanasiasa waenguliwa Tume ya Katiba Mpya

      Hili linaelekea kuwa jambo zuri kabisa kwa mustabali wa Taifa letu na natumaini wenye nia hjema kwa taifa wataunga mkono mia kwa mia. Wasi wasi wangu ni pale serikali itakapotofautiana, kama inavyoelekea, na wazo hili tufanyeje kwa mbinu za amani hadi kufanikiwa? Tuna tatizo kubwa mikononi mwetu na elimu ya uraia inahitajika sana watu waelewe haki zao na wawe huru kushiriki kuamua watakavyo na si kuburuzwa tu.

    18. #18
      Makucha's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 4th November 2010
      Posts : 189
      Rep Power : 474
      Likes Received
      16
      Likes Given
      0

      Default Re: Wanasiasa waenguliwa Tume ya Katiba Mpya

      Kuhusu uwakilishi sawa wa wajumbe kutoka bara na visiwani ni kichekesho mbali na kutilia mkazo haja ya kuwa na serikali. Ni ukweli kwamba hatuwezi kuwa na katiba moja ikatosha maeneo mbali mbali ya nchi yo yote hapa duniani na ndiyo maana kila nchi ina Katiba yake kukidhi mahitaji kwa mustakabali wa nchi yao. Kama tutarithia serikali tatu ni hapo tu uwakilishi sawa wa wajumbe kutoka bara na visiwani una maana kwa maswala ya muungano tu. Vinginevyo, kama visiwani wenyewe wanavyosema kuwa Zanzibar si sehemu ya Tanzania bali ni nchi yenye mipaka waliotaja; yaani Tanzania bara pia nu nchi yenye mipaka iliyobaki chini ya Muungano jambo ambalo hadi sasa lina baraka za serikali ya Muungano na ya Zanzibar. Yaani hatima ya katiba mpya 50% yake iwekwe chini ya reheni ya watu wachahe hivyo yenye % ndogo sana ya uwiano kieneo na wingi wa watu kati ya bara na visiwani. Hapa akili ipo? Kama nakosea munielemishe. Vinginevyo kama mvutano huu ni mkubwa na ajili ya amani ya nchi zetu bara na visiwani basi uwakilishi wa wajumbe sawa iwe pale tu inapohusu mambo ya muungano - wazungu wanasema in the unlikely event that worst goes to worst. Niko tayari kukosolewa kwa hoja tu.

    Similar Topics

    1. Wanasiasa wasipotoshe Muswada wa Katiba mpya
      By MziziMkavu in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 1
      Last Post: 23rd November 2011, 22:09
    2. Replies: 1
      Last Post: 5th April 2011, 18:08
    3. Wanasiasa waenguliwa Tume ya Katiba Mpya
      By nickname in forum KATIBA Mpya
      Replies: 4
      Last Post: 5th April 2011, 17:06
    4. waliomo kwenye Tume ya Katiba mpya
      By friendsofjeykey in forum KATIBA Mpya
      Replies: 15
      Last Post: 2nd January 2011, 16:41
    5. KATIBA MPYA: Werema asishirikishwe kwenye 'Tume' ya JK
      By Supervisor in forum KATIBA Mpya
      Replies: 7
      Last Post: 1st January 2011, 14:16

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...