Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Kanisa Katoliki 'lapigilia msumari' adhabu dhidi ya waumini

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 29
    1. #1
      Molemo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Posts : 8,418
      Rep Power : 10873
      Likes Received
      3798
      Likes Given
      426

      Post Kanisa Katoliki 'lapigilia msumari' adhabu dhidi ya waumini




      KANISA Katoliki katika Jimbo la Sumbawanga, mkoani Rukwa, limevunja ukimya na kunena kuhusu mambo yaliyosababisha waumini wake, kutengwa na wengine kuwekewa pingamizi kwa kukufuru utatu mtakatifu wakati wa uchaguzi mkuu, uliomalizika Oktoba 31 mwaka huu.

      Hatua hiyo imekuja siku kadhaa baada ya baadhi ya vyombo vya habari, kuandika na kuchapisha habari kuhusu sakata hilo huku kanisa likiwa halizungumzi lolote.

      Kitendo hicho, kiliwafanya baadhiya wananchi waliowahi kusoma habari hizo kutaka kujua ukweli kuhusu madai kuwa kanisa, limewatenga baadhi ya waumini wake kwa kukufuru utatu mtakatifu wakati wa uchaguzi mkuu.

      Jana, Wakili wa Kiaskofu katika Jimbo la Sumbawanga, Padri Modest Katonto, alikiri kuhusu adhabu hiyo kwa baadhi ya waumini wa kanisa hilo na kwamba hakuna anayeweza kuitengua.

      "Kanisa lingependa ifahamike kuwa hakuna mamlaka yoyote ya kidunia, inayoweza kuwaoondolea waumini hao adhabu hiyo, isipokuwa kwa jitihada za mtu mwenyewe binafsi kujipatanisha na kanisa kwa wale waliotengwa," alisema Padri Katonto.
      Kanisa hilo pia limesema halina itikadi za kisiasa na kwamba adhabu zimetolewa kwa waumini hao, hazijali wadhifa wa mtu yeyote katika jamii.

      Alisema kilichozingatiwa ni makosa ya kwenda kinyume cha imani na kushabikia mafundisho potofu.

      Wakili huyo wa kiaskofu, alisema waumini waliokumbwa na adhabu hizo wako katika makundi mawili na kwamba la kwanza, ni la waliotengwa kwa kosa la kujilinganisha na utatu mtakatifu na kushabikia mafundisho potofu, huku wakijua wazi kuwa kitendo hicho ni cha uovu.

      Kwa mujibu wa Padri Katonto, kundi hilo lina jumla ya waumini 27.
      Alisema kwa mujibu wa sheria ya kanisa namba 1364, kosa lililofanywa na watu hao, linawatenga na umoja wa kanisa hata bila kutangaziwa au kujulishwa na kiongozi wa kanisa.

      Alisema chini ya adhabu waliyopewa, waumini hao wamepoteza haki ya kushiriki katika idaba zote za hadhara za kanisa katoliki, kutoshiriki katika maadhimisho ya sakramenti, kutopokea akramenti na kutoshirki katika shughuli za uongozi wa kanisa .
      Alisema "ikiwa aliyetengwa atahudhuria au atakuwepo katika mazingira ya inapofanyika ibada, lazima aondoke au au kama hatatoka, ibada itasitishwa. Na ikiwa atakufa bila kutubu, hatapewa maziko ya kanisa," alisema Padri Katonto.
      Padri Kantonto alisema kundi la pili ni la waumini waliowekewa pingamizi ambao hata hivyo, hakutaja idadi yao.

      Alisema chini ya pingamizi walilowekewa, waumini hao wananyimwa haki ya kupata huduma za kanisa kwa muda, wakati makosa yao yakichunguzwa na kwamba kama itabainika kuwa hawakufanya, watarudishiwa huduma zote.

      Alisema hata hivyo, pingamizi hilo haliwaondowi watu wa kundi katika umoja na kanisa, kama ilivyo kwa waliotengwa.

      Alisema katika kipindi cha uchaguzi mkuu, kanisa lilijitahidi kuwakumbusha waumini wake kuhusu nafasi zao na wajibu wao, lakini kinyume chake kanisa limeshuhudia, na kusikia baadhi ya waumini wakionyesha utovu wa nidhamu kwa kukufuru utatu mtakatifu.

      "Walikufuru utatu mtakatifu, baadhi ya wagombea wakajifafanisha na Mungu mwenye nafsi tatu, kukufuru msalaba mtakatifu wa kanisa kwa kuuzika, kukejeli, kutukana na kudharau viongozi wa kanisa na wakristo wenzao," alisisitiza Padri Katonto.

      Alisema vitendo hivyo vimesikitisha mno mama kanisa kwa sababu vimeambatana na usaliti wa imani na maadili ya kikristo.


      "Lakini pia vitendo hivyo ni makwazo kwa wana kanisa na wakristo wa madhehebu mengine na watu wote wenye mapenzi mema," alisema.
      Alisema wanaotenda makosa kama hayo kwa mujibu wa sheria, kanisa, lina haki ya msingi ya kuwaadhibu na kwamba adhabu hizo si ngeni ndani ya kanisa.
      Kasisi huyo alifafanua kuwa shutuma dhidi ya kanisa kuwa limewatenga na kuweka pingamizi waumini wake kwa sababu za itikadi za kisiasa ikiwa ni pamoja na kuipigia kura CCM ni uwongo na uzushi wenye lengo la uchochezi.

      "Kanisa Katoliki linahoji hivi uchochezi huo unafanywa kwa maslahi na manufaa ya nani," alisema.
      Alisisitiza kuwa kamwe kanisa halitokaa kimya bila kukemea uovu kwa hofu ya vitisho na uzushi unaolenga katika kutetea maslahi ya kundi la watu wachache wasio na dhamira safi.

    2. Miaka 50

    3. #2
      Gurtu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th May 2010
      Posts : 880
      Rep Power : 638
      Likes Received
      150
      Likes Given
      6

      Default Re: Kanisa Katoliki 'lapigilia msumari' adhabu dhidi ya waumini

      Watu waache kuingilia mambo ya imani nyingine. Habari hii ilivyokuwa ikiripotiwa kwa mara ya kwanza zilikuwa na upotoshaji mwingi na hasa kuchochea vurugu zilisizo na maana. Muumini anayejua imani yake na kuadhibiwa kadiri ya imani hiyo anapolalamika kwenye vyombo vya habari ni ulimbukeni wa hali ya juu.

      Kadiri ya ufafanuzi wa Padre huyo wa Kanisa, wahusika wamenyimwa sakramenti za kanisa kwa sababu kwa matendo na maneno yao wameasi kanisa. Wataendeleaje kung'ang'ani imani ambayo wanaikejeli?

    4. LAT
      #3
      LAT's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th November 2010
      Posts : 4,526
      Rep Power : 1498
      Likes Received
      1156
      Likes Given
      1659

      Default Re: Kanisa Katoliki 'lapigilia msumari' adhabu dhidi ya waumini

      umeamua kuleta thread inayochanganya dini na siasa .... kama kanisa linavyotaka kutofautisha dini na siasa .... na kusisitiza umuhimu wa maadili na ubora wa viongozi... please be very careful here ..... take note .... maadili ya viongozi.... maisha ndani ya imani... na siasa kama daraja la kupata uongozi.... vitu vitatu tofauti:

      discard this thread, it is potentially baffling

    5. #4
      TIMING's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th April 2008
      Location : Roaming...
      Posts : 20,083
      Rep Power : 12251
      Likes Received
      6014
      Likes Given
      6847

      Default Re: Kanisa Katoliki 'lapigilia msumari' adhabu dhidi ya waumini

      hapo ndio tunaposema imani imechakachuliwa
      .....Ana sifa zote, nzuri na mbaya!!!

    6. #5
      Ndahani's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 3rd June 2008
      Location : Somewhere
      Posts : 9,646
      Rep Power : 4016
      Likes Received
      2940
      Likes Given
      5063

      Default Re: Kanisa Katoliki 'lapigilia msumari' adhabu dhidi ya waumini

      Huu ndio ule udini alioukemea mkuu? Maana naona kuna watu wanali underestimate kanisa
      We are all inventors, each sailing out on a voyage of discovery, guided each by a private chart, of which there is no duplicate. The world is all gates, all opportunities.
      Ralph Waldo Emerson

    7. FemaTV & Radio

    8. #6
      Mwanamageuko's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st October 2010
      Location : Baitul Lahm
      Posts : 1,175
      Rep Power : 673
      Likes Received
      81
      Likes Given
      211

      Default Re: Kanisa Katoliki 'lapigilia msumari' adhabu dhidi ya waumini

      hapa ya Ngoswe namuachia mwenyewe kwa kweli!
      "...If crime fighters fight crime and fire fighters fight fire, what do freedom fighters fight?"

    9. #7
      Somi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th February 2009
      Posts : 270
      Rep Power : 578
      Likes Received
      14
      Likes Given
      2

      Default Re: Kanisa Katoliki 'lapigilia msumari' adhabu dhidi ya waumini

      Nafikiri hawa jamaa waliotengwa waliona ccm ndio kila kitu wakasahau imani yao muhimu ya dini waliyobatizwa nayo sijui tuite ni ulimbukeni au kiburi au makusudi? Ok waende kwenye dini ya mafisadi ya freemasons. Walijua kwakuwa wao ni ccm hawataguswa

    10. #8
      Njaare's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th September 2010
      Posts : 568
      Rep Power : 660
      Likes Received
      92
      Likes Given
      165

      Default Re: Kanisa Katoliki 'lapigilia msumari' adhabu dhidi ya waumini

      Quote By LAT
      umeamua kuleta thread inayochanganya dini na siasa .... kama kanisa linavyotaka kutofautisha dini na siasa .... na kusisitiza umuhimu wa maadili na ubora wa viongozi... please be very careful here ..... take note .... maadili ya viongozi.... maisha ndani ya imani... na siasa kama daraja la kupata uongozi.... vitu vitatu tofauti:

      discard this thread, it is potentially baffling
      Hii thread hapa ni mahali pake kwa sababu inaelezea suala ambalo waandishi wa magazeti ya Serikali walisema limefanya kisisa.

    11. #9
      Gad ONEYA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th October 2010
      Posts : 2,544
      Rep Power : 947
      Likes Received
      122
      Likes Given
      559

      Default Re: Kanisa Katoliki 'lapigilia msumari' adhabu dhidi ya waumini

      bora sisi tunaoabudu kwenye mapango, t-shirt za njano na kijani hazifiki ila mbuzi na kondoo tu, aulabda kuku!

    12. #10
      Paschal Matubi's Avatar
      Member Array
      Join Date : 15th September 2008
      Posts : 82
      Rep Power : 647
      Likes Received
      9
      Likes Given
      18

      Default Kanisa Katoliki 'lapigilia msumari' adhabu dhidi ya waumini

      Can. 1364(1):

      An apostate from the faith, a heretic or a schismatic incurs a latae sententiae excommunication, without prejudice to the provision of Can. 194 §1, n. 2; a cleric, moreover, may be punished with the penalties mentioned in Can. 1336 §1, nn. 1, 2 and 3.

    13. #11
      Candid Scope's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th November 2010
      Posts : 7,606
      Rep Power : 15261
      Likes Received
      3731
      Likes Given
      2865

      Default Re: Kanisa Katoliki 'lapigilia msumari' adhabu dhidi ya waumini

      Serikali inatilia mkazo kila siku kutoshabikia mambo ya udini, lakini nimeshangaa sana jinsi gazeti la Serikali la Habari leo lilivyokuwa linaandika kila kukicha habari hiyo na magazeti mengine kwa busara kutochafulia wino kwenye magazeti yao kuhusu jambo hilo. Yangefanya hivyo magazeti ya kawaida mengine kinyume cha matakwa ya serikali yangetishiwa kufungiwa, lakini serikali wala haikutamka cho chote juu ya uchochezi huo wa gazeti la serikali kuhusu habari hiyo. Jamani tunaenda wapi sasa?

    14. #12
      Lole Gwakisa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th November 2008
      Posts : 2,959
      Rep Power : 1132
      Likes Received
      462
      Likes Given
      330

      Default Re: Kanisa Katoliki 'lapigilia msumari' adhabu dhidi ya waumini

      Kwa wale wanaotaka mahakama ya kadhi mnatakiwa kicopy na kupaste utaratibu huu wa wakatoliki bila kuomba ruzuku ya serikali
      Yours faithfully!

    15. #13
      samirnasri's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th November 2010
      Posts : 1,210
      Rep Power : 675
      Likes Received
      169
      Likes Given
      50

      Default Re: Kanisa Katoliki 'lapigilia msumari' adhabu dhidi ya waumini

      Tunashukuru kwa ufafanuzi huu maana serikali kupitia gazeti lake ilijaribu kupotosha ukweli ili ionekane jamaa wametengwa kwa u ccm wao kitu ambacho si cha kweli.

    16. #14
      leseiyo's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 25th October 2007
      Posts : 117
      Rep Power : 618
      Likes Received
      2
      Likes Given
      0

      Default Re: Kanisa Katoliki 'lapigilia msumari' adhabu dhidi ya waumini

      Kwa mara ya kwanza habari hii iliripotiwa kwa kupotoshwa na Gazeti la Serikali asorry CCM la Habari Leo na lilidai kwamba, waumini hao walitengwa kwa sababu ya kuiunga mkono CCM.Najiuliza hivi gazeti hili lililenga nini?Ni hali ya hatari kuwa na gazeti la serikali lenye kuchochea uvunjifu wa amani na mgawanyiko miongoni mwa wanajamii.

    17. #15
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14621
      Likes Received
      2841
      Likes Given
      1961

      Default Re: Kanisa Katoliki 'lapigilia msumari' adhabu dhidi ya waumini

      Ama kweli ukistaajabu ya Slaa utayakuta ya Kanisa.

    18. #16
      BURAKEYE's Avatar
      Member Array
      Join Date : 17th December 2010
      Posts : 23
      Rep Power : 431
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default Re: Kanisa Katoliki 'lapigilia msumari' adhabu dhidi ya waumini

      Poor beleiver,opt to other religions there is no such thing as going beyond GOD but beyond CHURCH PRINCIPALS and as said beyond TRINITY, Remember no where in the bible does the world TRINITY exist because THE WHOLE IDEA IS FABRICATION. The DOGMA of which can not be explain by the bishops themselves.

    19. #17
      Gsana's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th August 2010
      Location : Dar es salaam
      Posts : 2,227
      Rep Power : 888
      Likes Received
      215
      Likes Given
      30

      Default

      Quote By Dar Es Salaam
      Ama kweli ukistaajabu ya Slaa utayakuta ya Kanisa.
      umeona ehe? Sasa kaka dsm,si uwaambie wenzio wawe na mahakama kama izi? Haziitaji bajeti ya serikali kama mahakama ya Kadhi inavolazimisha. Pia mwambie mwandishi wenu Petty Siame aache kuandika unafiki. Waende kwa mbunge ndo wawe na dini walioitaka sasa. "ROMA LOUCUTA" means "rome is an end/everything no one else"

    20. #18
      Afrika Furaha's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th December 2010
      Location : Afrika Kijijini
      Posts : 329
      Rep Power : 492
      Likes Received
      5
      Likes Given
      7

      Default

      Quote By BURAKEYE
      Poor beleiver,opt to other religions there is no such thing as going beyond GOD but beyond CHURCH PRINCIPALS and as said beyond TRINITY, Remember no where in the bible does the world TRINITY exist because THE WHOLE IDEA IS FABRICATION. The DOGMA of which can not be explain by the bishops themselves.
      Ptuuuuuuuuuuu! Uharo mtupu!

    21. #19
      BURAKEYE's Avatar
      Member Array
      Join Date : 17th December 2010
      Posts : 23
      Rep Power : 431
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default Re: Kanisa Katoliki 'lapigilia msumari' adhabu dhidi ya waumini

      i repeat no where in the bible does the word TRINITY EXIST, It is bitter truth but u should swallow

    22. #20
      Babuyao's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th June 2009
      Posts : 1,719
      Rep Power : 850
      Likes Received
      177
      Likes Given
      148

      Default Re: Kanisa Katoliki 'lapigilia msumari' adhabu dhidi ya waumini

      Quote By Gsana
      umeona ehe? Sasa kaka dsm,si uwaambie wenzio wawe na mahakama kama izi? Haziitaji bajeti ya serikali kama mahakama ya Kadhi inavolazimisha. Pia mwambie mwandishi wenu Petty Siame aache kuandika unafiki. Waende kwa mbunge ndo wawe na dini walioitaka sasa. "ROMA LOUCUTA" means "rome is an end/everything no one else"
      Msemo huo unasema "Roma locuta causa finita" - yaani 'Roma ikishatamka mambo yamekwisha'! Hakuna zaidi.
      God writes straight with crooked lines.

    Page 1 of 2 12 LastLast

    Similar Topics

    1. Uhuni wa Firel Castro dhidi ya kanisa katoliki!
      By Tango73 in forum KATIBA Mpya
      Replies: 1
      Last Post: 2nd July 2011, 22:17
    2. Replies: 1
      Last Post: 20th December 2010, 17:18
    3. Waraka: Kanisa Katoliki laandaa waumini uchaguzi 2010
      By Halisi in forum Tanzania 2010-2015
      Replies: 1339
      Last Post: 28th July 2010, 19:32
    4. Kanisa Katoliki yaanzisha kampeni kupima ukimwi waumini wake Tanzania
      By MwanaFalsafa1 in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 2
      Last Post: 21st June 2009, 09:33

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...