Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Oh No!! Something Here Hidden

    Report Post
    Results 1 to 2 of 2
    1. #1
      MkamaP's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th January 2007
      Posts : 4,675
      Rep Power : 1569
      Likes Received
      310
      Likes Given
      93

      Default Oh No!! Something Here Hidden

      Habari za kawaida
      Posted Date::2/2/2008
      Shule zenye majina ya viongozi hoi mtihani kidato cha nne
      Na Joyce Mmasi

      SHULE za sekondari zenye majina ya viongozi, zimeonekana kufanya vibaya ukilinganisha na heshima za majina ya viongozi hao.


      Matokeo ya Shule ya Sekondari ya Nyerere Memorial yenye wanafunzi 131 waliofanya mtihani; ni wanane tu waliofaulu, wakati 123 wakifanya vibaya.


      Katika shule hiyo mwanafunzi mmoja alipata daraja la kwanza, la pili watano na tatu wawili, 83 daraja la nne na 40 waliambulia patupu.


      Katika Shule ya Sekondari Amani Abeid Karume, wanafunzi waliofeli ni 68 wakati waliofaulu ni tisa tu. Shule hii mwaka 2004 ilikuwa miongoni mwa shule 10 zilizofanya vibaya kitaifa.


      Shule ya Ali Hassan Mwinyi waliofeli ni wanafunzi 97 waliofaulu ni 11 tu wakati katika shule ya Dk Omary Ali Juma waliofeli ni watoto 14 na waliofaulu ni 13.


      Katika Shule ya Sekondari Nelson Mandela imefaulisha wanafunzi wanane na 61 kufanya vibaya, huku shule ya Zakia Meghji iliyokuwa na watahiniwa 84, ni 13 tu waliofaulu huku 71 wakianguka vibaya.


      Shule ya Moringe Sokoine ilijumuisha watahiniwa 104, waliofeli ni 61 huku 43 wakifaulu. Shule ya sekondari ya Kawawa waliofanya vizuri ni 10 na waliofeli ni 89.


      Sekondari nyingine ni yenye jina la JK Nyerere ambapo kati ya wanafunzi 204 waliofanya mtihani 75 walifeli na 129 kufanya vizuri. Shule ya Dk Ali Mohamed Shein iliyokuwa na wanafunzi 21 waliofanya mtihani wa kidato cha nne mwaka jana, ni wanafunzi wawili tu waliofaulu.


      Shule nyingine ni Mererani Benjamin Mkapa ambayo imefaulisha mwanafunzi mmoja tu na kuacha wengine 26 wakifeli wakati Shule ya Frederick Sumaye imefaulisha wanafunzi 45 na 52 kufeli mitihani hiyo.


      Vile vile katika shule yenye jina la J.J Mungai wanafunzi 143 wamefeli na waliofaulu ni 27.


      Orodha hiyo ya shule zenye majina ya viongozi inafungwa na Benjamin Mkapa High School ya Dar es Salaam ambayo imefelisha wanafunzi 173 na 193 kushinda kati ya daraja la kwanza hadi la tatu.


      Baadhi ya viongozi walio hai na wengine marehemu, wamekuwa na tabia ya kuzibatiza au kuruhusu baadhi ya shule kupewa majina yao, lakini viongozi hao hawafuatilii maendeleo ya shule hizo.


      Ni wazi kuwa, kufanya vibaya kwa shule hizo kwa miaka na miaka, si tu kunashusha heshima za viongozi hao, bali pia kunatoa fursa ya wao kujitazama na kuanza kuziangalia shule hizo mara kwa mara. Matokeo ya mitihani Uk 26.

    2. RukaaJuu Final

    3. #2
      MzalendoHalisi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th June 2007
      Posts : 3,942
      Rep Power : 1397
      Likes Received
      72
      Likes Given
      120

      Default Re: Oh No!! Something Here Hidden

      Hii kuita shule majina na Viongozi ni kwa manufaa ya nani? Na je hao wakubwa wanjua kuna shule zinatumia majina yao?
      Uadilifu Kiwe Kigezo Muhimu Zaidi Kuwa Kiongozi Tanzania Kwa Sasa!

    4. Miaka 50

    Similar Topics

    1. Hidden Camera!
      By Ndebile in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 1
      Last Post: 11th December 2011, 20:17
    2. Jfk assassination hidden story
      By Somi in forum International Forum
      Replies: 0
      Last Post: 8th August 2011, 17:51
    3. The Hidden America
      By X-PASTER in forum International Forum
      Replies: 0
      Last Post: 4th July 2011, 02:19
    4. Hidden Passion
      By Martinez in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 5
      Last Post: 31st August 2010, 22:33

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...