Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Semina elekezi ya Chadema

    Report Post
    Results 1 to 11 of 11
    1. #1
      Luteni's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th January 2010
      Posts : 2,269
      Rep Power : 943
      Likes Received
      239
      Likes Given
      73

      Default Semina elekezi ya Chadema

      KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willbrod Slaa, amepanga kufanya ziara nchi nzima kuwafunda madiwani wa chama hicho.

      Mwaka huu, CHADEMA kimeshinda halmashauri 12 za Mwanza Mjini, Musoma Mjini, Karatu, Moshi Mjini, Ukerewe, Kigoma Mjini, Mbulu, Arusha, Moshi Vijijini, Hanang, Mbeya Mjini na Iringa Mjini.

      Dk. Slaa alitangaza azma yake hiyo jana katika mkutano wake wa ndani wa madiwani wa halmashauri ya mji wa Musoma Mjini na baadhi ya wabunge wa mikoa ya Kanda ya Ziwa.

      Madiwani wa CHADEMA na CUF wamemteua diwani wa kata ya Nyamatare, Alex Kisusura, kuwa Meya wa Manispaa ya Musoma, huku Angela Lima diwani wa Kamnyonge, akiteuliwa kuwa Naibu Meya wa Manispaa ya Musoma Mjini.

      Tayari ameshatembelea halmashauri ya Jiji la Mwanza ambako aliwapatia madiwani mbinu mbalimbali za kuongoza halmashauri hiyo, na kufanikisha uteuzi wa Meya wa jiji hilo Bwana Josephat Manyerere.

      Tunawatakia mafanikio mema Chadema katika harakati zenu za ukombozi.
      Luteni is a True Revolutionist.

    2. Miaka 50

    3. #2
      Mtu wa Mungu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th November 2010
      Posts : 424
      Rep Power : 517
      Likes Received
      13
      Likes Given
      1

      Default Re: Semina elekezi ya Chadema

      Hizi ni habari njema na mwanzo mzuri sana wanamaendeleo!!!!!!!!!!!!!!!!! !!!!!!

    4. #3
      Consultant's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th June 2008
      Location : N/A
      Posts : 1,348
      Rep Power : 828
      Likes Received
      106
      Likes Given
      69

      Default Re: Semina elekezi ya Chadema

      Angeunganisha semina elekezi hizi na mikutano ya wananchi kila anakopita ingekuwa bomba sana - two in one, cost effective!

      Taabu tu ni kwamba watawala wanaweza kumnyima vibali vya kufanya mikutano kwa sababu zisizo na mashiko
      It's true that money cannot buy happiness, but I would rather cry in Mercedez than on a Motorcycle

    5. #4
      Misterdennis's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th June 2007
      Posts : 1,038
      Rep Power : 819
      Likes Received
      68
      Likes Given
      226

      Default Re: Semina elekezi ya Chadema

      Wananchi waliompigia kura , tungependa tumsikie anasema nini, hata apite tu kutoa shukurani kwa wananchi.
      Jinsi ilivyo sasa wanannchi hawajui kinachoendela, ni kama amewaacha "solemba". Inahitajika aseme na wapiga kura wake.

    6. #5
      Jile79's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th May 2009
      Posts : 3,770
      Rep Power : 1267
      Likes Received
      213
      Likes Given
      9

      Default Re: Semina elekezi ya Chadema

      Good news kwa dr.slaa na chadema....wasisahau bundi zitto kabwe anawanyemelea
      Mvumilivu hula mbivu... Ila mvundika mbivu hula mbovu


    7. #6
      Kigogo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th December 2007
      Location : Calabash
      Posts : 8,202
      Rep Power : 2096
      Likes Received
      1234
      Likes Given
      313

      Default Re: Semina elekezi ya Chadema

      daaaah yaani Dr.Slaa utadhani mwalimu wangu wa fizikia wakati niko shule...very stratergic na moves zake
      ______________________________ _
      Niko tayari kufa huku nimesimama kuliko kuishi huku nimepiga magoti....

    8. #7
      mfarisayo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd November 2010
      Location : tanganyika
      Posts : 3,164
      Rep Power : 1068
      Likes Received
      466
      Likes Given
      1108

      Default Re: Semina elekezi ya Chadema

      Plan nzuri ila angalizo watu kama kina Zitto kabwe lazima washughulikiwe mapema ili mipango iende kama ilivyopangwa.

    9. #8
      Butola's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th January 2010
      Posts : 1,521
      Rep Power : 783
      Likes Received
      266
      Likes Given
      647

      Default Re: Semina elekezi ya Chadema

      Quote By Luteni
      Mwaka huu, CHADEMA kimeshinda halmashauri 12 za Mwanza Mjini, Musoma Mjini, Karatu, Moshi Mjini, Ukerewe, Kigoma Mjini, Mbulu, Arusha, Moshi Vijijini, Hanang, Mbeya Mjini na Iringa Mjini..
      Masahihisho:

      CCM imeshinda katika Jiji la Mbeya kwa kuwa na jumla ya Madiwani 28 dhidi ya 18 wa Chadema; na pia CCM imeshinda Iringa Mjini ikiwa na jumla ya Madiwani 20 dhidi ya 2 tu wa Chadema.

    10. #9
      Chakaza's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2007
      Location : everywhere
      Posts : 3,563
      Rep Power : 1479
      Likes Received
      893
      Likes Given
      530

      Default Re: Semina elekezi ya Chadema

      Watu wengine sasa ndio watatambua kuwa Slaa ni kichwa.
      Hatutajua chochote iwapo hatutahoji na kudadisi

    11. #10
      Bams's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th October 2010
      Posts : 830
      Rep Power : 602
      Likes Received
      333
      Likes Given
      9

      Default Re: Semina elekezi ya Chadema

      CHADEMA ni lazima waweke uongozi wa mfano kwa uongozi wa 'chumia tumbo' wa CCM. Kwa kuwa nyuma yao kuna wananchi, ni lazima watafanikiwa. Wawaache CCM ambao nyuma yao kuna chama chao, wanachi wakiwa wametupwa mbali.

    12. #11
      RealMan's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th November 2010
      Location : Daslam
      Posts : 1,686
      Rep Power : 2968
      Likes Received
      598
      Likes Given
      324

      Default Re: Semina elekezi ya Chadema

      Habari njema hii. Nimekuasante kamanda
      -- Many leaders are Alive Only because its Illegal to shoot them!--

    Similar Topics

    1. Chadema yatoa semina elekezi kwa viongozi wake
      By figganigga in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 3
      Last Post: 3rd December 2011, 21:23
    2. Jakaya anahitaji semina elekezi
      By Ptz in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 7
      Last Post: 23rd September 2011, 20:46
    3. Decision making- semina elekezi
      By Mtazamaji in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 0
      Last Post: 9th June 2011, 17:27
    4. Ni matokeo ya semina elekezi ?
      By Sir R in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 4
      Last Post: 2nd June 2011, 23:23
    5. Semina elekezi na ziara za chadema
      By Felixonfellix in forum JF Chit-Chat
      Replies: 0
      Last Post: 16th May 2011, 19:42

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...