Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Prof. Tibaijuka: Mliopora maeneo jisalimisheni; aanza kwa kasi!

    Report Post
    Page 1 of 8 123 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 158
    1. #1
      Ustaadh's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th October 2009
      Posts : 408
      Rep Power : 572
      Likes Received
      7
      Likes Given
      1

      Default Prof. Tibaijuka: Mliopora maeneo jisalimisheni; aanza kwa kasi!

      WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, amewataka wananchi waliopora viwanja na maeneo ya wazi nchini na kujenga, wajisalimishe kwa mazungumzo, kwa sababu huenda wakaokoa hata matofali kabla hatua zaidi hazijachukuliwa.

      Profesa Tibaijuka alisema hayo Dar es Salaam jana wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mikakati ya wizara hiyo na kueleza kuwa masuala ya ardhi yasipofanyiwa kazi, sekta nyingine zitazorota.


      “Umefika wakati sasa, tunataka kubadilisha mwonekano wa miji ... na kwa wanaosema wanatumia jeuri ya pesa, tutawashughulikia, lakini baada ya kufanya utafiti wa kutosha, kwa sababu hatuwezi kukurupuka, hivyo waliopora viwanja tunawataka wajisalimishe,” alisema Profesa Tibaijuka ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa zamani wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kushughulikia Makazi (UN-Habitat).


      Alisema, migogoro ya ardhi hawataimaliza bila wananchi kuwasaidia na kwa sasa, watarudisha askari wa ardhi ili kuhakikisha wanapunguza migogoro ikiwamo ya wanaojenga holela na katika maeneo ya wazi.


      Tibaijuka alisema, kati ya hekta 900,000 ni asilimia mbili tu ya maeneo ndiyo yaliyopimwa, hivyo wizara yake itahakikisha inapimwa, ili miji iwe katika hali inayotakiwa kwa sababu kwa sasa hairidhishi.


      Aidha, Profesa Tibaijuka alisema si maendeleo yote yanahitaji fedha, hivyo kwa muda huu waliopewa na Rais, kuna mambo ambayo watayafanyia kazi kwa haraka ikiwamo kuandika majina ya mitaa yote.


      “Watu wengi hawatambui mitaa wanayoishi inaitwaje, kwa sababu wala haina majina na unakuta anashindwa kabisa kuelekeza, lakini tukiiandika tutawasaidia, hivyo tutafanya jambo hili kwa haraka maana haihitaji fedha,” alifafanua mbunge huyo wa Muleba Kusini.


      Katika hatua nyingine, alisema kuna upungufu wa nyumba milioni tatu nchini, hivyo wanapaswa kujenga miji kwa kuboresha nyumba zilizopo na kuzijenga ambazo hazina viwango na kuziuza kwa wananchi.


      “Wananchi wanatakiwa kutambua wanahitaji nyumba au ardhi, lakini watambue kama ni viwanja lazima waende nje ya mji, ila kama ni nyumba zipo ila zinahitaji maboresho na tutafanikiwa, kwa kuwa na benki za nyumba na mikopo ya nje, kwa sababu sekta binafsi pekee hazitaweza bila kuwa na fedha ... tuwaachie wahandisi wetu wajenge nyumba sisi tununue,” alisema.


      Alisema, watafanya kazi kwa kushirikiana kwa karibu na Ofisi ya Mazingira ili kuhakikisha miji inakuwa safi na salama; na kuboresha bonde la Mto Msimbazi, Dar es Salaam, ambalo limefanya hali ya hospitali ya Taifa Muhimbili kuwa mbaya.


      Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Patrick Rutabanzibwa, alikiri baadhi ya wafanyakazi wake kushiriki kugawa maeneo ya wazi na kueleza kuwa tayari ameanza kuwachukulia hatua za kisheria, ikiwamo kufanya mabadiliko ya vitengo kwa nia ya kuboresha utendaji kazi.


      “Uvamizi wa maeneo ni mtandao wa watu wa wizarani na manispaa nami nimejitolea kuwashughulikia na tayari kuna waliokuwa wamepora viwanja na nimewataka wavirudishe na wengine walipora na kuwauzia wafanyabiashara wakubwa,” alisema Rutabanzibwa.


      Pia alisema wamesimamisha ujenzi wa eneo la wazi katika hoteli ya Palm Beach na kuahidi kufanya kazi bila kuhofia kashfa, kwani zipo tuhuma amevumishiwa na amezipeleka kwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) na kwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).


      Kwa upande wao, mawaziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Mary Nagu (Uwekezaji na Uwezeshaji) na William Lukuvi (Sera, Uratibu na Bunge), waliripoti rasmi katika Ofisi ya Waziri Mkuu na kuzungumza na wakuu wa idara, vitengo na taasisi chini ya Ofisi hiyo.


      Mawaziri hao waliwataka watendaji kufanya kazi kwa ubunifu, ushirikiano, upendo, uwazi na bidii zaidi, ili kukidhi matarajio ya wananchi.


      Nagu alisisitiza umuhimu wa Ofisi ya Waziri Mkuu kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji bila ngojangoja ambayo ni chanzo cha kuwakatisha tamaa wawekezaji.


      Alisema hakuna uchumi duniani uliofanya vizuri bila uwekezaji, iwe wa kutoka nje au ndani ya nchi husika. Alibainisha kuwa Watanzania ndio wanatakiwa kushika hatamu ya uchumi wao.


      Lukuvi alisisitiza watendaji kuwa wabunifu na kufanya kazi kwa kasi zaidi ili kuongeza ufanisi na hatimaye kufikia malengo ya Ofisi ya Waziri Mkuu na Taifa kwa jumla.


      Waziri wa Uchukuzi, Omar Nundu aliwaambia watendaji wakuu wa wizara hiyo kuwa anawapa uhuru wa kufanya uamuzi wenye tija na ufanisi na atakayeshindwa atajiondoa mwenyewe.


      Alizungumza na wakurugenzi wakuu wa idara za uchukuzi na wa taasisi mbalimbali akijitambulisha kwao rasmi na kuanza kazi.


      Nundu aliwataka kufahamu dhima waliyonayo katika kuendeleza sekta ya uchukuzi ili katika kipindi cha miaka mitano ijayo, fursa zilizomo zitumike vyema pamoja na kuboresha huduma za usafiri.


      Aliwataka kupeana ushauri ili wasonge mbele, kuwa wadilifu na waaminifu huku wakitoa huduma kwa dhati na kwa wakati muafaka.


      “Hakikisheni mnawajibika kulingana na wakati, katika suala la uchukuzi hatupo peke yetu ulimwenguni, zingatieni matakwa ya wateja,” alisema Nundu na kuongeza:


      “Fanyeni kazi kila mmoja kwa madaraka aliyonayo, toeni uamuzi wenye tija bila upendeleo na hata ubinafsi na hiyo iwe ahadi yenu kwetu,” alisema.


      Alisema, anatarajia kuimarisha kampuni ya reli, kwa lengo la kuipa uwezo wa kutoa huduma bora kwa kusafirisha abiria na mizigo ya ndani na nchi jirani, na kuendelezwa kama mhimili wa mpango wa maendeleo wa eneo la ukanda wa kati.

    2. RukaaJuu Final

    3. #2
      Nyambala's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th October 2007
      Location : Tahiti
      Posts : 4,403
      Rep Power : 1518
      Likes Received
      1019
      Likes Given
      938

      Default Re: Prof. Tibaijuka: Mliopora maeneo jisalimisheni

      The tone is just same ol. one, only that the person is different! We have our popcorns ready mama Tiba.

    4. #3
      mfereji maringo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th November 2010
      Posts : 843
      Rep Power : 600
      Likes Received
      138
      Likes Given
      47

      Default Re: Prof. Tibaijuka: Mliopora maeneo jisalimisheni

      mnaanzaga kwa mkwara, mwisho prrraaagggghhhhh...

    5. #4
      Gurudumu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th February 2008
      Posts : 2,338
      Rep Power : 1056
      Likes Received
      223
      Likes Given
      104

      Default Re: Prof. Tibaijuka: Mliopora maeneo jisalimisheni

      Huyu mama kumbe naye Hana tofauti na JK? Anadhani bado tunahitaji kutangaziwa kwamba kuna vigogo waliohodhi viwanja na maeneo ya wazi? Kwa nini asitutatangazi amerejesha viwanja na maeneo ya wazi mangapi na bado mangapi. Atuambie amechukua hatua gani kwa maafisa wa wizara yake na halmashauri waliofanya huo ufisadi.

      Kubwa zaidi atutangazie kufuta hati ya "kuuza" eneo la Kigamboni na raia wake. Atutangazie hatua alizochukua dhidi ya ardhi ya loliondo iliyouzwa kwa waarabu na wananchi kufukuzwa, kupigwa, kuuawa, kuchoma nyumba na kuteketeza mali na mifugo yao.

      Tunakaka atutangazie baada ya kutekeleza na alishindwa pia atutangazie. Asiendeleze usanii wa JK

    6. #5
      Kigogo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th December 2007
      Location : Calabash
      Posts : 8,196
      Rep Power : 2095
      Likes Received
      1233
      Likes Given
      313

      Default Re: Prof. Tibaijuka: Mliopora maeneo jisalimisheni

      huyu mama bana...eti wajisalimishe?anacheza tu hakuna la maana hapo analoongea
      ______________________________ _
      Niko tayari kufa huku nimesimama kuliko kuishi huku nimepiga magoti....

    7. Miaka 50

    8. #6
      Safari_ni_Safari's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th October 2007
      Location : Kibaruani
      Posts : 12,014
      Rep Power : 24158
      Likes Received
      4736
      Likes Given
      2652

      Default Re: Prof. Tibaijuka: Mliopora maeneo jisalimisheni

      Waanze kujisalimisha CCM....pale Mango Garden ni open space na wao wamepatwaa...pale opposite na Meridien mwananyamala ni open space wamepatwaa....pale Kishamapendo Ilala ni open sapace na walipatwaa...list ni ndefu sana...Sinza ndio balaa kabisa

      Soki Ozali Mwasi Yaka, Soki Ozali Mobali Koya Te


    9. #7
      Njowepo's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 26th February 2008
      Location : Santiago
      Posts : 7,634
      Rep Power : 22062
      Likes Received
      1009
      Likes Given
      803

      Default Re: Prof. Tibaijuka: Mliopora maeneo jisalimisheni

      Ngoja tuone ili la open space pale palm beach linakuwaje?
      WB Tanzania lead economist Jacques Morisset said the GDP doubled in 10 years, but it has failed to produce any significant decline in poverty levels.

    10. #8
      genekai's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th February 2010
      Location : Loitering!
      Posts : 7,547
      Rep Power : 2089
      Likes Received
      1096
      Likes Given
      1575

      Default Re: Prof. Tibaijuka: Mliopora maeneo jisalimisheni

      Utekelezaji wa kauli zetu ndo muhimu!
      The future of this country is being jeopardized by the intellectual slavery of our top leaders

    11. #9
      Diehard's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd November 2010
      Posts : 339
      Rep Power : 498
      Likes Received
      35
      Likes Given
      81

      Default Re: Prof. Tibaijuka: Mliopora maeneo jisalimisheni

      Usisahau pale masaki nyumba za sitta na wenzake, Rose Garden hivi ni eneo la nani huwa linakuwa na sheshe za msimu kisha kimya

    12. #10
      Tekelinalokujia's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th September 2010
      Location : Planet Earth
      Posts : 344
      Rep Power : 510
      Likes Received
      31
      Likes Given
      166

      Default Re: Prof. Tibaijuka: Mliopora maeneo jisalimisheni

      Drama za kuelekea 2015 zimeanza, JK alipoanza that time aliwapeleka hawa mabwana AR kwenye ile hoteli ya kitalii kuwapa darasa tukajua kazi pevu itaanza kumbe wapi walikua wanakula goodtime tuu.

    13. #11
      QUALITY's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th September 2010
      Posts : 844
      Rep Power : 607
      Likes Received
      109
      Likes Given
      343

      Default Profesor Tibaijuka atamweza Mahanga?

      Profesor Tibaijuka atamweza Mahanga?
      Katika serikali ya Tanzania kumekuwa na mtindo wa kulindana kati ya viongozi, ndiyo maana hata wakati ajenda za mafisadi na ubadhilifu mwingine wa mali za umma ulipofumuka, viongozi waliopaswa kuchukua hatua walifyata mkia.

      Sasa jana (kupitia ITV news ya saa mbili usiku) Professor Tibaijuka ambaye aliteuliwa kuwa waziri wa Ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi alisema “wale wote waliovamia maeneo ya wazi, wajisalimishe”. Mahanga ambaye ni naibu waziri katika serikali ya kikwete ni mmoja wa wananchi wanaoongoza katika kuvamia maeneo mengi ya wazi. Sasa kwa wakazi wa Tabata, wanafahamu pale Bima, kushoto ipo Nyantare Social Hall na Nyantare Bar. Zikiwa zimekamata eneo lililokuwa la wazi na lina ukubwa unaokadiriwa kuwa kama meta kati ya 400 na 600! Hilo lilikuwa eneo la wazi, kwa sasa ni kitega uchumi cha mheshimiwa!

      Pale Segerea, anajenga ghorofa katika eneo la wazi. Sasa Tibaijika ataweza kumkabili kiongozi mwenziwe na kumbomolea vitega uchumi vyake?

      Yetu macho, tunasubili kuona nani atamvika paka kengere!!

    14. #12
      mujusi's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 22nd January 2010
      Posts : 232
      Rep Power : 521
      Likes Received
      47
      Likes Given
      2

      Default Re: Prof. Tibaijuka: Mliopora maeneo jisalimisheni

      Kweli kabisa. Hii shighuli ya maeneo ya wazi na kugawa maeneo ya Fukwe kwa Dar es Salaam ni mfupa uliowashinda Fisi wengi. Katika kipindi toka awamu ya tatu hili jambo limeshindwa na tumezidi kuona open space zinaendelea kuporwa. Kwani hata hilo eneo la Palm Beach limeporwa na kujengwa kip[indi kipi? maeneo yenyewe wanatoa hao hao na ya hao hao. Mama atizame asije akajiuzuru mapema au kuomba ahamishwe Wizara. Vita anayotaka kuingia ni kali ina hitaji support kubwa na ama sivyo watu watamjaji kwa kauli yake.
      Quote By mfereji maringo
      mnaanzaga kwa mkwara, mwisho prrraaagggghhhhh...

    15. #13
      Ndeusoho's Avatar
      Member Array
      Join Date : 26th January 2010
      Posts : 43
      Rep Power : 482
      Likes Received
      4
      Likes Given
      15

      Default Re: Prof. Tibaijuka: Mliopora maeneo jisalimisheni

      Suala la Rose Garden ni kwamba Mheshimiwa Magufuli alikosa uadilifu wakati akiwa Wizara ya Ardhi. Suala hilo lilishafanyiwa kazi kitaalamu na kiutawala na Makamba akiwa mkuu wa mkoa na likafikia mwisho lakini Magufuli kwa sababu zake alilazimisha wataalamu waandike alichotaka. Msisahau kuwa aliwahi kuzuia Boat isisafirishwe kwa kisingizio cha uzito lakini mizigo ya migodini ambayo ni mizito mara mia ikawa inapita.

    16. #14
      Ndeusoho's Avatar
      Member Array
      Join Date : 26th January 2010
      Posts : 43
      Rep Power : 482
      Likes Received
      4
      Likes Given
      15

      Default Re: Prof. Tibaijuka: Mliopora maeneo jisalimisheni

      Atakapokuta viwanja 85% ni ofisi za CCM na nyumba za vigogo hatakuwa na moto huo. Hilo lilimshinda Magufuli licha ya kukabidhiwa orodha ya viwanja vya wazi vilivyovamiwa nchi nzima. Watanzania kinachotutafuna ni unafiki hasa kwenye itikadi za vyama na maamuzi ya Baraza la Mawaziri. Endapo Baraza la Mawaziri lingeweka bayana umuhimu wa kurejeshwa kwa maeneo ya wazi hili lingewezekana. Lakini kwa dhambi ya ubinafsi na ulafi walio nayo maslahi ya umma kamwe hayawezi kuwekwa mbele. Profesa amuulize Magufuli aliyafanyia nini yale majina aliyopewa na orodha ndefu ya viwanja vilivyovamiwa??

    17. #15
      Mtu wa Mungu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th November 2010
      Posts : 424
      Rep Power : 517
      Likes Received
      13
      Likes Given
      1

      Default Re: Prof. Tibaijuka: Mliopora maeneo jisalimisheni

      Wabongo ni watu wa ajabu kweli kweli!!!! Utaona pamoja na vitisho na mikikimikiki yote hii ya prof tiba ni kama ndiyo anawachochea-we kaa tu utakuja ona miezi si mingi!!!!!!!!!!!! Unajua sababu kubwa?-usoni anawaona wenye pesa lakini atakapoanza hatua za kuingia ndani atashtuka kukuta EL, AC, RA, JK, Kingunge, yusufu,ridhwani, miraji, januari, lukuvi, +orodha ndefu sana!!! atafyata na kunyamaza kimya na ndiyo mwisho!!!!!!!!!!! Usichezee bongo-ndiyo mazao ya laana!!!
      Kwani nani ni mgeni kwa pombe????-kwani pombe wa leo na yule wa jana kuna tofauti?????
      Haya-sisi wengine yetu macho na kelele kupitia JF!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

    18. #16
      Pdidy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd November 2007
      Posts : 12,283
      Rep Power : 3443
      Likes Received
      1322
      Likes Given
      855

      Default Re: Prof. Tibaijuka: Mliopora maeneo jisalimisheni

      Prof tiba
      walianza wakina magufuli hao hao wa leo hii na tanroads...tunarudisha nyumba zote za serikali akaishia kugawa kwa mdogo wake aliekuwa ameajiriwa just 3 months serikalini
      mungu akupe mngojezi kwenye matamshi watanzania ni wabaya sana kwenye kumbukumbu hasa unapofanya kosa;;si vibaya kusema lakini matendo ndio yanayowaaibisha watu..mungu akutie nguvu mama

    19. #17
      Ndeusoho's Avatar
      Member Array
      Join Date : 26th January 2010
      Posts : 43
      Rep Power : 482
      Likes Received
      4
      Likes Given
      15

      Default Re: Prof. Tibaijuka: Mliopora maeneo jisalimisheni

      Kazi bado ni pevu. Maeneo ya wazi ni moja. Huko Sinza na Ubungo kuna waliojenga juu ya njia ya bomba la majitaka na majisafi pia. Tena wengine wameuziwa na watumishi wa wizara yako. Na hili la watu kuishi ju ya mabomba ni la hatari kubwa kuliko hata uvamizi wa viwanja vya wazi. Je unajua juu ya watu waliziba barabara ili wajenge nyumba zao kwa hasara ya ubora wa miji yetu. Nadhani inabidi uwe na ratiba kwa sababu hiyo wizara ni kichaa. Kama huamini bado kidogo utagundua kuwa Master Plan ilikuwa imetenga eneo la kujenga reli toka Ubungo hadi Wazo. Hivi unadhani hizi foleni za kijinga zingekuwepo kama reli hiyo ingejengwa. Kazi unayo lakini nenda kwa awamu kwa vile mengine ni magumu kutokana na kikulacho kuwamo nguoni mwako.

    20. #18
      Pdidy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd November 2007
      Posts : 12,283
      Rep Power : 3443
      Likes Received
      1322
      Likes Given
      855

      Default Re: Prof. Tibaijuka: Mliopora maeneo jisalimisheni

      Quote By ndeusoho
      kazi bado ni pevu. Maeneo ya wazi ni moja. Huko sinza na ubungo kuna waliojenga juu ya njia ya bomba la majitaka na majisafi pia. Tena wengine wameuziwa na watumishi wa wizara yako. Na hili la watu kuishi ju ya mabomba ni la hatari kubwa kuliko hata uvamizi wa viwanja vya wazi. Je unajua juu ya watu waliziba barabara ili wajenge nyumba zao kwa hasara ya ubora wa miji yetu. Nadhani inabidi uwe na ratiba kwa sababu hiyo wizara ni kichaa. Kama huamini bado kidogo utagundua kuwa master plan ilikuwa imetenga eneo la kujenga reli toka ubungo hadi wazo. Hivi unadhani hizi foleni za kijinga zingekuwepo kama reli hiyo ingejengwa. Kazi unayo lakini nenda kwa awamu kwa vile mengine ni magumu kutokana na kikulacho kuwamo nguoni mwako.

      yaani in general akifwata masterplan hadi ikulu inatoka pale ilipo
      pole mama ilo jitahdi ulinywe kavukavu ndio uongozi

    21. #19
      Mtu wa Mungu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th November 2010
      Posts : 424
      Rep Power : 517
      Likes Received
      13
      Likes Given
      1

      Default Re: Prof. Tibaijuka: Mliopora maeneo jisalimisheni

      The list continues-atawakuta ben na anna, siti, salama, ongeza na wewe waliosahauliwa!!!!!!!!!!!!!!!! !!Hizi ni viini macho whereas at the end of the day we are ten years backward in maendeleo-from 12 million maskinis to 15 millions as at 2015!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! !! We unafikiri kwa nini wamekubali aibu yote ya kuiba kura, ni ili wale-sasa nani ataondoa tonge kwenye midomo yao!!!!!!!!!!

    22. #20
      Mchakachuliwaji's Avatar
      Member Array
      Join Date : 23rd November 2010
      Posts : 31
      Rep Power : 437
      Likes Received
      0
      Likes Given
      14

      Default Re: Prof. Tibaijuka: Mliopora maeneo jisalimisheni

      mh,,, yetu macho

    Page 1 of 8 123 ... LastLast

    Similar Topics

    1. Prof Tibaijuka- Kauli yako
      By CHUAKACHARA in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 2
      Last Post: 16th August 2011, 10:27
    2. Prof. Tibaijuka ahamishia kibao kwenye 'beacons'
      By Rutashubanyuma in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 12
      Last Post: 19th January 2011, 02:58
    3. Was BAWATA Prof. Tibaijuka's brain-child?
      By Kashaijabutege in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 1
      Last Post: 3rd January 2011, 16:44
    4. Speed ya Prof. Tibaijuka yaanza kupata vikinza
      By Rutashubanyuma in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 37
      Last Post: 18th December 2010, 14:17
    5. Hongera Prof Tibaijuka kwa 2009 Göteborg Award
      By Ngareni3 in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 20
      Last Post: 19th July 2009, 10:10

    User Tag List

    Tags for this Topic

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...