Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Tamko la Vijana 'WASOMI' wa vyuo vikuu Mkoa wa Dodoma Dhidi ya wabunge wa CHADEMA

    Report Post
    Page 1 of 28 12311 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 544
    1. #1
      Mzanzibara's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 15th September 2010
      Posts : 14
      Rep Power : 0
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Tamko la Vijana 'WASOMI' wa vyuo vikuu Mkoa wa Dodoma Dhidi ya wabunge wa CHADEMA

      Waraka huu umesomwa muda si mrefu mbele ya vyombo vya habari zaidi ya 15 huko Dodoma.

      TAMKO LA VIJANA WASOMI WA VYUO VIKUU WA MKOA WA DODOMA, KUHUSU KITENDO CHA BAADHI YA WABUNGE WA CHADEMA KUTOKA NJE YA UKUMBI WA BUNGE.

      NDUGU WAANDISHI WA HABARI,
      NDUGU WANANCHI,.


      Awali ya yote nawashukuru sana kuhitikia wito wetu wa gfafla kuja kujumika pamoja nasi leo hii, akhsanteni sana.

      Sisi vijana wasomi wa vyuo vikuu mbalimbali vilivyoko mkoa wa Dodoma kwa pamoja tunapenda kuweka wazi maoni yetu juu ya kitendo kilichofanywa na Wabunge wa CHADEMA jana 18.11.2010 wakati Mhe. Rais alihutubia Bunge.


      Kwanza tumeshtushwa na kitendo hicho na kuweka wazi masikitiko yetu kwa kuwa kilichofanyika ni kinyume na matarajio ya wapiga kura waliowachagua waheshimiwa wabunge hao kuwawakilisha ndani ya chombo hicho kikubwa na chenye heshima kubwa ndani na nje ya nchi.


      Bunge ni sehemu ya kuwakilisha wananchi kwa hoja chini ya kanuni zilizopo bila kujali itikadi ya chama chochote cha siasa na kazi kubwa ya mbunge ni kuishauri na kuisimamia Serikali kwa niaba ya wananchi waliomchagua au kuwachagua.


      Kwa mantiki hiyo basi kama Wabunge hawamtambui Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania maana yake hawana kazi ya kufanya ndani ya Bunge kwani kazi yao kubwa ni kuishauri na kuisimania Serikali sasa kama hawaitambui Serikali hiyo hawana sababu ya kuendelea kuwepo Bungeni.


      Pili Baada ya uchaguzi wa Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda, wabunge hao pia walinukuliwa na vyombo vya habari na ushaidi tunao wakiweka wazi kumkubali kiongozi huyo, na kauli mbiu yake ya ‘Bunge moja’ je, kitendo walichofanya inaashiria utekelezaji wa kauli mbiu ya Bunge moja?


      Tatu msimamo wa kutomtambua Rais ni wa CHADEMA kama chama na waliotoka nje ya Bunge ni wabunge sasa ni vema wabune hao watambue na kutafakari upya kama kweli wanawawakilisha Bungeni wananchi au cha na kutekeleza misimamo yao bila kujali maslahi ya waliowachagua na kumpa kura nyingi Rais Kikwete?.


      Nne Kwa badhi ya wabunge wa CHADEMA kutomtambua Rais wakati akilihutubia bunge ni wazi kuwa hata sheria zitakzopitishwa na Bunge hawatahusika kwa kuwa mwenye mamlaka ya mwisho kukubali sheria iliyotungwa na Bunge itumike ni Rais ambaye wanadai hawamtutambui.


      Ni dhahiri kuwa watashindwa kufanya kazi yao ya uwakilishi na usimamizi wa Serikali Bungeni .


      Je wanawaonesha watanzania dalili gani kama si kutaka kuleta machafuko nchini na mgawanyiko ndani ya Bunge na kwa Jamii kwa ujumla?.


      Wananchi waliowachagua wabunge hao wanapaswa kutafakari upya wawakilishi waliowachagua kama wana uelewa wa kutosha kuhusu bunge, sisi vijana wa vyuo vikuu tunajua na tunatambua kuwa Rais ni Sehemu ya Bunge na Bunge haliwezi kukamilika bila Rais na hii ndio maana kila sheria inayopitishwa na Bunge ni lazima yeye Rais aweke sahihi yake.


      Katika mazungumo yake na waandishi wa habari wiki hii Mweneykiti wa CHADEMA MHE. Freeman Mbowe, alinukuliwa na vyombo vya habari akisema wabunge wake na madiwani wanaweza kuendelea kuwakilisha wananchi licha ya kutomtambua Rais.


      Sisi tunasema hili si sahihi bali ni upotoshaji mkubwa, kamwe mtoto hawezi kudai kuwa hamtabui Baba yake kisha anaendelea kumwita Baba na kutumia kila kitu kinachotolewa na Baba huyo huyo. Huo ni utovu wa nidhamu au kukosa maadili.


      Sisi vijana wa vyuo vikuu Mkoa wa Dodoma tunawaomba Watanzania wote wenye nia njema na Taifa letu kuwapuuza wabunge wa CHADEMA na kutambua kuwa lengo lao ni kutaka kutuhamisha kutoka kwenye ajenda ya msingi ya Maendeleo na kubaki kwenye malumbano ya kisiasa kama tulivyoshuhudia katika nchi jirani.


      Kamwe tusikubali kudanganywa na watu wachache.


      Mwisho tungependa kuwaomba Wabunge wa CHADEMA wawaombe radhi watanzania kwa kuvuruga tashwira safi ya Bunge letu lisilo na ubaguzi na itikadi za kisiasa vinginevyo wanawadharau watanzania waliowachagua wakidhani kwamba niwaadilifu wa Taifa na si cha chama chao.


      Tutambue kuwa kazi kubwa ya CHADEMA na Wabunge wake kwa sasa ni kuwachanganya watanzania ili badala ya kuendelea na shughuli za ujenzi wa taifa wabaki na malumbano ya hapa na pale kwa manufaa yao binafsi.


      Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Bunge letu na kutuepusha na ubaguzi kama huu uliofanywa na baadhi ya Wabunge wa CHADEMA.


      Aksanteni sana.


      IMESOMWA NA THOBIAS MWESIGA RICHARD

      KWA NIABA YA WANAFUNZI WA VYUO VIKUU MKOA WA DODOMA


    2. #2
      Kisu changariba's Avatar
      Member Array
      Join Date : 19th October 2010
      Posts : 29
      Rep Power : 445
      Likes Received
      1
      Likes Given
      1

      Default Re: Yanayojiri dakika hii:TAMKO LA VIJANA WASOMI WA VYUO VIKUU MKOA WA DODOMA.

      Watoto wanaponzwa na vibeer na chips kuku zitolewazo Dom Hotel. Cant you guys use yoyr heads?? Shule inawasidia nini kama hata tamko mnaandikiwa na vigogo??

    3. #3
      edwinito's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 3rd December 2008
      Posts : 199
      Rep Power : 576
      Likes Received
      6
      Likes Given
      3

      Default Re: Yanayojiri dakika hii:TAMKO LA VIJANA WASOMI WA VYUO VIKUU MKOA WA DODOMA.

      Nonsense!!!!!!

    4. #4
      pascaldaudi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th March 2009
      Posts : 535
      Rep Power : 628
      Likes Received
      91
      Likes Given
      134

      Default Re: Yanayojiri dakika hii:TAMKO LA VIJANA WASOMI WA VYUO VIKUU MKOA WA DODOMA.

      Elimu haijawakomboa, My poor Tanzania kama hawa vijana ndo taifa la kesho wanakuwa na akili finyu kiasi hiki, kweli maisha magumu na umasikini ni urithi wetu!
      "BY FOCUSING ON WHAT DIVIDES US, WE MAY ACT IN ERROR AS WE FAIL TO SEE WHAT UNITES US"

    5. #5
      Anyisile Obheli's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th December 2009
      Location : Rohoni
      Posts : 3,261
      Rep Power : 1129
      Likes Received
      69
      Likes Given
      82

      Default Re: Yanayojiri dakika hii:TAMKO LA VIJANA WASOMI WA VYUO VIKUU MKOA WA DODOMA.

      hawa wasinasibu kuwa ni vijana wasomi bali ni vijana wanaokariri
      hiyo taarifa yao imejaa, mapungufu kibao sasa kama usomi umeishia kwenye mtazamo huo ni
      dhahili kuwa serkali imeingia hasara kubwa sana kuwa na taifa la wasomi wa aina hiyo
      siku za mbeleni
      ........................HAKUNA TIBA YA KIFO............
      HESHIMU WATU NA PIA JIHESHIMU, KISHA, MPENDE MUNGU


    6. #6
      MILKYWAY GALAXY's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 12th December 2008
      Posts : 153
      Rep Power : 574
      Likes Received
      33
      Likes Given
      1

      Default Re: Yanayojiri dakika hii:TAMKO LA VIJANA WASOMI WA VYUO VIKUU MKOA WA DODOMA.

      Sasa nimeelewa kwanini rafiki yangu alinisihi sana nisimpeleke mwanangu chuo kikuu dodoma.

      He was RIGHT!

    7. #7
      seniorita's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st November 2010
      Posts : 675
      Rep Power : 581
      Likes Received
      49
      Likes Given
      141

      Default Re: Yanayojiri dakika hii:TAMKO LA VIJANA WASOMI WA VYUO VIKUU MKOA WA DODOMA.

      pure nonsense; they didnt walk out of their resposibility, but out of their responsibility to the people they represent. Hivi hawa vijana wanawakilisha wenzao wote, au ni kundi tu lililonunuliwa na CCM mafia; for heavens' sake; vijana ndio wanaokuwa more affected by this unfair system, no employment, when they are employed they ar egiven meagre salaries, and when they complain, "I do not need your votes" etc. Mama zenu na baba zenu wanahangaika na ukata vijijini, halafu you bring this nonsense!!!! Someni mpate busara, na si kusoma kuendeleza ujinga, otherwise they is no need mtumie country's resources to harbor foilly; that you can get it even without going to school

    8. #8
      TUKUTUKU's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th September 2010
      Location : KIPALAPALA TU
      Posts : 8,679
      Rep Power : 2180
      Likes Received
      1924
      Likes Given
      748

      Default Re: Yanayojiri dakika hii:TAMKO LA VIJANA WASOMI WA VYUO VIKUU MKOA WA DODOMA.

      Mamluki waliotumwa na baba zao wafisadi!kila tunapopiga hatua katika kutafuta haki na kuweka ustawi mzuri wa jamii wa siku zijazo,lazima watokee watu wa kuturudisha nyuma!Hakuna haja ya kurudi nyuma ,lazima tusonge mbele tuu,ujinga kwetu ni mwiko!!

    9. #9
      Mzanzibara's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 15th September 2010
      Posts : 14
      Rep Power : 0
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Yanayojiri dakika hii:TAMKO LA VIJANA WASOMI WA VYUO VIKUU MKOA WA DODOMA.

      Yaliyosemwa yana mantiki au hayana???

    10. #10
      Dina's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th September 2008
      Location : Ulimwenguni
      Posts : 1,193
      Rep Power : 786
      Likes Received
      320
      Likes Given
      186

      Default Re: Yanayojiri dakika hii:TAMKO LA VIJANA WASOMI WA VYUO VIKUU MKOA WA DODOMA.

      Hawa nao, tukisitisha hiyo ada sijui watafanyaje!
      Waliopo hatuwataki, na wanaotaka tuwape hatuwaamini...........Mrisho Mpoto.

    11. #11
      Anyisile Obheli's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th December 2009
      Location : Rohoni
      Posts : 3,261
      Rep Power : 1129
      Likes Received
      69
      Likes Given
      82

      Default Re: Yanayojiri dakika hii:TAMKO LA VIJANA WASOMI WA VYUO VIKUU MKOA WA DODOMA.

      Quote By edwinito View Post
      Nonsense!!!!!!
      wababishaji tu hao na wezi wachanga wamali za umma, mbona kulingana na
      mwenendo mbaya wa kuhesabu na kutangaza matokeo ya kura
      hawakutoa masikitiko yao, wasomi gani hao wasiokuwa na upeo wa mambo
      mafidhuli wakubwa hawa, hawako fair kabisa
      ........................HAKUNA TIBA YA KIFO............
      HESHIMU WATU NA PIA JIHESHIMU, KISHA, MPENDE MUNGU

    12. #12
      Saharavoice's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 30th August 2007
      Posts : 2,203
      Rep Power : 1043
      Likes Received
      411
      Likes Given
      495

      Default Re: Yanayojiri dakika hii:TAMKO LA VIJANA WASOMI WA VYUO VIKUU MKOA WA DODOMA.

      Hao ni wasomi CCM na wanawakilisha CCM, ngoja tusubiri tamko la wasomi Chadema
      A conclusion is the place where you got tired of thinking



    13. #13
      dotto's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th September 2010
      Posts : 1,469
      Rep Power : 735
      Likes Received
      168
      Likes Given
      29

      Default Re: Yanayojiri dakika hii:TAMKO LA VIJANA WASOMI WA VYUO VIKUU MKOA WA DODOMA.

      Is not the right person. Vyuo vyote TAnzania serikali zao ni CHADEMA. hUYU KIRAKA TU.

    14. #14
      Double X's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 4th November 2010
      Posts : 184
      Rep Power : 473
      Likes Received
      2
      Likes Given
      0

      Default Re: Yanayojiri dakika hii:TAMKO LA VIJANA WASOMI WA VYUO VIKUU MKOA WA DODOMA.

      PAMBAFFFF, mi nilifikiri kuna la maana kumbe ni ----- mtupu!!!wote hamnazo hapo udom!

    15. #15
      Oracles's Avatar
      Member Array
      Join Date : 4th July 2010
      Posts : 12
      Rep Power : 457
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Yanayojiri dakika hii:TAMKO LA VIJANA WASOMI WA VYUO VIKUU MKOA WA DODOMA.

      Wanafunzi?au wametumwa?njaa nyingine bana...hawana ada afu wanamsaidia ------...mmeishiwa ninyi..usomi wenu wa mashaka.

    16. #16
      Mzanzibara's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 15th September 2010
      Posts : 14
      Rep Power : 0
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Yanayojiri dakika hii:TAMKO LA VIJANA WASOMI WA VYUO VIKUU MKOA WA DODOMA.

      Quote By seniorita View Post
      pure nonsense; they didnt walk out of their resposibility, but out of their responsibility to the people they represent. Hivi hawa vijana wanawakilisha wenzao wote, au ni kundi tu lililonunuliwa na CCM mafia; for heavens' sake; vijana ndio wanaokuwa more affected by this unfair system, no employment, when they are employed they ar egiven meagre salaries, and when they complain, "I do not need your votes" etc. Mama zenu na baba zenu wanahangaika na ukata vijijini, halafu you bring this nonsense!!!! Someni mpate busara, na si kusoma kuendeleza ujinga, otherwise they is no need mtumie country's resources to harbor foilly; that you can get it even without going to school
      Lmao!!Watu wameanza kushtukia Chadema wahuni,wameamka!!

    17. #17
      Mzanzibara's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 15th September 2010
      Posts : 14
      Rep Power : 0
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Yanayojiri dakika hii:TAMKO LA VIJANA WASOMI WA VYUO VIKUU MKOA WA DODOMA.

      Quote By Saharavoice View Post
      Hao ni wasomi CCM na wanawakilisha CCM, ngoja tusubiri tamko la wasomi Chadema
      Yetu macho,mi ntapost tu!

    18. #18
      Milindi's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 3rd March 2009
      Posts : 219
      Rep Power : 568
      Likes Received
      45
      Likes Given
      253

      Default Re: Yanayojiri dakika hii:TAMKO LA VIJANA WASOMI WA VYUO VIKUU MKOA WA DODOMA.

      Nyie mnaojifanya wasomi wakati ni wavivu wa kufikiri acheni hizo,ni wapuuzi na ccm itawafanya kama kondomu.Baada ya kuwatumia na mikopo mtaendelee kupata kwa shida.Mlitaka wananchi waandamane ndipo mjue kuwa uchakachuaji ulifanyika.Ninawapongeza wabunge wa Chadema kwa kufanya hivyo na tunasubiri mchanganuo jinsi hawa walivyoiba mpaka dunia nzima ielewe huyu jamaa si rais halali ila katiba mbovu ndio inamuweka madarakani.Hongera sana Chadema na tunasubiri taarifa rasmi kuhusu jinsi mafisadi hawa walivyoiba kura.

    19. #19
      matawi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th March 2010
      Posts : 1,505
      Rep Power : 770
      Likes Received
      138
      Likes Given
      70

      Default Re: Yanayojiri dakika hii:TAMKO LA VIJANA WASOMI WA VYUO VIKUU MKOA WA DODOMA.

      Kama kweli ni maoni ya wanafunzi Dodoma basi liko tatizo kubwa la wasomi/vijana wetu. Chadema iko vitani kuwapigania watanzania wote kwa dhuluma zinazofanywa na serikali iliyopo madarakani na hiyo move ni ujumbe kwa watanzania na dunia nzima kuhusu udidimizwaji wa demokrasia nchini. Kingine cha kuelewa hapa chadema hawakusema hawatahudhuria mikutano ya bunge wataendelea kama kawaida wao wana tatizo la kikiwete kufoji kura za kumuingiza ikulu huku akifahamu kuwa Rais akiapishwa hakuna chombo au mahakama yoyote inayoweza kutengua . Vijana fuatilieni mambo kiundani. Labda tusubiri TAHLISO kama wana maoni tofauti

    20. #20
      Mimibaba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st July 2009
      Posts : 3,351
      Rep Power : 1572
      Likes Received
      813
      Likes Given
      622

      Default Re: Yanayojiri dakika hii:TAMKO LA VIJANA WASOMI WA VYUO VIKUU MKOA WA DODOMA

      Kama kweli ni wanavyuo you are in the wrong place. Think with your head not with your stomach. Mnajidhalilisha kujishirikisha kwenye issue msiyo na uzoefu nayo. Nawatahadharisha you will be dumped by the same person using you now. Tanzania na Africa haihitaji vilaza

    Page 1 of 28 12311 ... LastLast

    Similar Topics

    1. Wasomi wa vyuo vikuu nguzo imara ya CHADEMA Igunga
      By Gwota in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 23
      Last Post: 7th September 2011, 11:52
    2. Kongamano la CHADEMA Vyuo Vikuu Dodoma
      By Regia Mtema in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 167
      Last Post: 11th April 2011, 08:52
    3. Replies: 45
      Last Post: 14th February 2011, 10:21
    4. Tamko la CHADEMA mkoa wa Dodoma
      By Felixonfellix in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 11
      Last Post: 26th January 2011, 18:57
    5. Replies: 52
      Last Post: 22nd January 2011, 13:24

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...