Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Kigoma Yatengwa! Usafiri balaa ..

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 27
    1. #1
      Ibrah's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd March 2007
      Location : TZ
      Posts : 2,883
      Rep Power : 1202
      Likes Received
      402
      Likes Given
      47

      Default Kigoma Yatengwa! Usafiri balaa ..

      Hali ya usafiri wa Treni ambao ndiyo usafiri pekee wa uhakika kwenda mikoa mingine ni mbaya mno na inazidi kuwa mbaya siku hadi siku. Wasafiri wanasafiri bila taa kitu ambacho ni hatari kwa usalama na afya (maana kwenda haja usiku ni noma)

      Kwa sasa usafiri wa Daraja la 3 ambao ndiyo unamudiwa na watu wengi ni adha tupu tiketi zinauzwa 8 tu na zimeisha! Ukibahatika kupata tiketi basi namba za siti zimegonganishwa kwa watu wengine wawili (na mtajuana wenyewe)na ni juu yenu kupangiana zamu ya kukaa! Ikiwa unataka kusafiri siku unayotaka inakupasa kulipa shilingi 45,000/- ili uweze pata tiketi ya kwenda Dar es Salaam nauli ambayo walipa wasafiri wa Kanda ya Ziwa kutoka Dar kupitia nchi jirani (Kenya na Uganda).
      ''UBAYA UTASHAMIRI NA KUPATA NGUVU ZAIDI IWAPO WATU WEMA WAMEAMUA KUKAA KIMYA '', Edmond Burke
      " What we believe, inevitably affects how we live," Howard Marshall


    2. #2
      Morani75's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st March 2007
      Location : Duniani
      Posts : 662
      Rep Power : 765
      Likes Received
      9
      Likes Given
      0

      Default Re: "Jamhuri ya Kigoma " Yatengwa!

      Ibrah, ni kuwapa pole ndugu zetu wa Kigoma... Unajua quality ya life after mwekezaji inategemea pia huyo mwekezaji nyumbani anaishije!!?? Kumbuka kwenye picha za treni/garimoshi India jamaa wanasafiri wakiwa wamekaa mpaka juu ya garimoshi lenyewe, kufika wanafika lakini ni adha tu ndio kidogo inakuwa tatizo!!

      Mwekezaji mpya TRL (ndio jina jipya hilo after TRC) ametoka India....... So, we are to learn travelling Indian Style

      Personally sitegemei mabadiliko makubwa kwenye hilo shirika letu......

    3. #3
      Ibrah's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd March 2007
      Location : TZ
      Posts : 2,883
      Rep Power : 1202
      Likes Received
      402
      Likes Given
      47

      Default Re: "Jamhuri ya Kigoma " Yatengwa!

      Quote By Morani75 View Post
      Ibrah, ni kuwapa pole ndugu zetu wa Kigoma... Unajua quality ya life after mwekezaji inategemea pia huyo mwekezaji nyumbani anaishije!!?? Kumbuka kwenye picha za treni/garimoshi India jamaa wanasafiri wakiwa wamekaa mpaka juu ya garimoshi lenyewe, kufika wanafika lakini ni adha tu ndio kidogo inakuwa tatizo!!

      Mwekezaji mpya TRL (ndio jina jipya hilo after TRC) ametoka India....... So, we are to learn travelling Indian Style

      Personally sitegemei mabadiliko makubwa kwenye hilo shirika letu......
      Asante sana Morani; hawa Wahindi wa TRL ndiyo wanaoendesha zile treni ambazo watu wanakaa hadi juu ya behewa. Duniani kote hakuna mahali penye usafiri duni wa Treni kama kule India.

      Nakumbuka kuona picha ya namna hiyo kwenye magazeti yetu kama kuna mtu anazo atubandikie hapa.

      Wakati Rais anafunga miaka 2 ya utawala kuna mwandishi alimwuliza kuhusu usafiri wa Reli , TRL an uwekezaji Muungwana akadai kuwa wakati wa TRC treni ilichukua hadi siku 8 kwenda Kigoma! Nilimshangaaa, maana haijawahi kutokea katika TRC Wasafiri kukaa siku 5 njiani ati kwa kuwa mabehewa ya mizigo yametokea never, Rais aliwadanganya WaTz! Kitu ambacho TRC walikuwa wakifanya ni kubadilisha Wasafiri kuhamia treni nyingine (kubadlishana) na ilikuwa sahihi kabis. Sijui Muungwana alipandaga Treni ya TRC lini!
      ''UBAYA UTASHAMIRI NA KUPATA NGUVU ZAIDI IWAPO WATU WEMA WAMEAMUA KUKAA KIMYA '', Edmond Burke
      " What we believe, inevitably affects how we live," Howard Marshall

    4. KGM is offline
      KGM
      #4
      KGM's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 21st May 2007
      Posts : 225
      Rep Power : 663
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default Re: "Jamhuri ya Kigoma " Yatengwa!

      Ibrah unataka kunitoa machoni.
      Pamoja na serikali kuwa wabaguzi wakubwa sana na kuutenga mkoa wa kigoma makusudi lakini kinachochangia matatizo hayo kikubwa ni ukosefu wa wabunge makini.

      Kigoma haijapata kuwa na MBUNGE Makini anayewatetea hata siku moja. Hukumbuki miezi kama miwili iliyopita tu iliwalazimu FFU kuingia kuwatoa wasalifiri waliokuwa wamekaliana vichwani.
      Kwa kifupi ule sio usafiri.

      Harafu angali wabunge wa kigoma siku ile ya ZITO walivyoshambuliana bungeni. Selukamba&Msambya dhidi ya ZITO.

      Utafikiri ndicho kilicjhowapeleka bungeni.

      Ni aibu sana ndugu zanguni,

      Naomba Jambo forum itusaidie kutuokoa watu wa KIGOMA twafa.

    5. #5
      Kibunango's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th August 2006
      Location : Tampere
      Posts : 6,820
      Rep Power : 44138
      Likes Received
      375
      Likes Given
      1450

      Default Re: "Jamhuri ya Kigoma " Yatengwa!

      Pale Mwanza kuna jamaa zangu kibao toka Kigoma, mara nyingi wamekuwa wakilalamikia suala usafiri. Ni vema suala hili sasa likatupiwa japo jicho la huruma...
      Save Water Drink Beer. "Alcohol doesn't solve any problem,
      But, if you think again, neither does milk."
      Vituko Vya Zenj


    6. #6
      Bill's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th October 2007
      Posts : 1,674
      Rep Power : 932
      Likes Received
      303
      Likes Given
      212

      Default Re: "Jamhuri ya Kigoma " Yatengwa!

      Nafikiri Serikali inasubiri yatokee maafa ili Rais akaweke Mnara wa kumbukumbu katika eneo la Tukio. Kwa nini tunakuwa wazito kujifunza kutoka na uzembe wa yaliyopita. Watu wakifariki ndipo utamwona rais na watendaji wake wanauongelea usafari huu na kuwapa kifuta machozi wafiwa cha shs 50,000/-.

      Mwekezaji gani huyu huduma inamshinda hadi anafika mahali huduma inakuwa duni zaidi ya ile aliyoikuta. Pia inasemekana Serikali imempa mtaji mtaji, it means ameenda kuinvest kwingine na kutuacha na matatizo yetu ya usafir ukizidi kuwa mbovu zaidi.

      Siwezi kuwalaumu wawekezaji, they are here to make business, and not kuwafurahisha wabongo msafiri kwa starehe kama mko kwenye ndege ya chini. Viongozi wetu waliosaini mkataba na hawa jamaa ya kutoa huduma bora na kuboresha miundo mbinu ndio wa kulaumiwa. Hawatufai
      !

    7. #7
      Kakalende's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st December 2006
      Posts : 2,940
      Rep Power : 1238
      Likes Received
      391
      Likes Given
      388

      Default Re: "Jamhuri ya Kigoma " Yatengwa!

      Quote By Ibrah View Post
      Hali ya usafiri wa Treni ambao ndiyo usafiri pekee wa uhakika kwenda mikoa mingine ni mbaya mno na inazidi kuwa mbaya siku hadi siku. Wasafiri wanasafiri bila taa kitu ambacho ni hatari kwa usalama na afya (maana kwenda haja usiku ni noma)

      Kwa sasa usafiri wa Daraja la 3 ambao ndiyo unamudiwa na watu wengi ni adha tupu tiketi zinauzwa 8 tu na zimeisha! Ukibahatika kupata tiketi basi namba za siti zimegonganishwa kwa watu wengine wawili (na mtajuana wenyewe)na ni juu yenu kupangiana zamu ya kukaa! Ikiwa unataka kusafiri siku unayotaka inakupasa kulipa shilingi 45,000/- ili uweze pata tiketi ya kwenda Dar es Salaam nauli ambayo walipa wasafiri wa Kanda ya Ziwa kutoka Dar kupitia nchi jirani (Kenya na Uganda).
      Ibrah ni kweli usafir wa treni una matatitizo makubwa na si kwa Kigoma tu bali kwa wale wote wanaoitegemea reli ya kati hasa kule kusikopitiwa na barabara kuu. Yule mwekezaji wa kihindi tusitegemee miujiza kwani hatuoni lolote la kuvutia kule ambako amekuwa akiendesha reli kwa muda mrefu.

      Hoja yako ya "jamhuri" pamoja na kutengwa kiusafiri haileti matumaini bali inaondoa kabisa matumaini. Isijekuwa kuna hoja za kujitenga? tunafahamu kuwa wenyeji wa mkoa huu wanashabihiana lugha na nchi jirani; na vilevile wakazi wengi wa pale Ujiji walipewa uraia na hayati Mwalimu mara tu baada ya uhuru.

      Baadhi yetu tulifanyia kazi Kigoma kwa miaka kadhaa, tulitegemea zaidi usafiri wa barabara kupitia Kasulu-Kibondo-Nyakanazi, na huko tunajiunga na barabara kuu inayotokea mikoa ya kanda ya ziwa.

    8. #8
      MzalendoHalisi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th June 2007
      Posts : 4,049
      Rep Power : 1422
      Likes Received
      106
      Likes Given
      208

      Default Re: "Jamhuri ya Kigoma " Yatengwa!

      1. Viongozi toka Kigoma pia wamewaangusha wana Kigoma- kusema kweli sijawahi ona msukumo wa kweli toka kwa viongozi wanaotoka Kigoma! Angalia mfano wa 1.4 Bil toka kwa wana kagera!

      2. Sasa utamlaumu nani??? wakti viongozi wamekimbia Kigoma na kujenga Mz na Dar?

      3. Jawabu kudumu ni kujenga daraja Malagarasi- na barabara lami na kuwa na usafiri wa uhakika wa barabara- haya ndo mambo ya kutetea kwa nguvu na Wanakigoma kuondoa shilingi ktk budgeti! Ahadi tu za serikali kila siku over daraja na barabara- sasa 46 years! Hamna kitu!

      Sasa kama Kigoma wanachagua wabunge wanaotetea mambo ya Kitaifa kama Bugwazi na Zitto kwa nini wanashindwa kutetea infrustructure ya Kigoma?
      Uadilifu Kiwe Kigezo Muhimu Zaidi Kuwa Kiongozi Tanzania Kwa Sasa!

    9. #9
      Kitila Mkumbo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th February 2006
      Posts : 3,940
      Rep Power : 6971
      Likes Received
      1102
      Likes Given
      36

      Default Re: "Jamhuri ya Kigoma " Yatengwa!

      Quote By KGM View Post
      Ibrah unataka kunitoa machoni.
      Pamoja na serikali kuwa wabaguzi wakubwa sana na kuutenga mkoa wa kigoma makusudi lakini kinachochangia matatizo hayo kikubwa ni ukosefu wa wabunge makini.

      Kigoma haijapata kuwa na MBUNGE Makini anayewatetea hata siku moja. Hukumbuki miezi kama miwili iliyopita tu iliwalazimu FFU kuingia kuwatoa wasalifiri waliokuwa wamekaliana vichwani.
      Kwa kifupi ule sio usafiri.

      Harafu angali wabunge wa kigoma siku ile ya ZITO walivyoshambuliana bungeni. Selukamba&Msambya dhidi ya ZITO.

      Utafikiri ndicho kilicjhowapeleka bungeni.

      Ni aibu sana ndugu zanguni,

      Naomba Jambo forum itusaidie kutuokoa watu wa KIGOMA twafa.

      Sasa hii bwana inabidi iwe next agenda ya Zitto, tena aibebee mbeleko haraka sana. Hali hii inatisha, yaani nikisoma maandishi yenu ni kama nawaona hao wapiga kura wa CCM wakiwa pale stesheni Dar kuelekea Kigoma-ni balaa kubwa.
      A Struggle Without Casualties is No Struggle-Steve Biko

    10. #10
      Mtu wa Pwani's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th December 2006
      Posts : 4,265
      Rep Power : 1498
      Likes Received
      171
      Likes Given
      168

      Default Re: "Jamhuri ya Kigoma " Yatengwa!

      huu ni uhuni na kwenda kinyume na katiba ya jamhuri ya muungano kuutangaza mkoa wa kigoma kuwa jamhuri.

      kabla ya yote alieleta mada hii na kuipa jina hilo amekusudia fitna na shari na sio kuwasilisha matatizo ya wanakigoma au kutafuta suluhisho la kweli.

      mtu huyu ashindwe na alegee
      Our job is not to make up anybody's mind, but to open minds and to make the agony of the decision-making so intense you can escape only by thinking. ~Author Unknown

    11. #11
      Masatu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th January 2007
      Location : Mbagala, Jeshini
      Posts : 3,739
      Rep Power : 1178
      Likes Received
      18
      Likes Given
      0

      Default Re: Kigoma Yatengwa! Usafiri balaa ..

      Kama mkiona namna gani vipi mnaweza kujiunga na Jamhuri ya Burundi isiwe taabu ishakuwa nongwa sasa mbona watu wa Mtwara miaka nenda miaka rudi wanasota na barabara mbaya tena Mtwara hata ukitupisha jiwe kutoka Dar kwa mkono linafika au jogoo akiwika Dar Mtwara anasikika...

      Anyway msikwazike na maneno haya si ndio majibu tunayowapa Wazanzibari wakilalamika?
      Mkulima kala Mbegu......

    12. #12
      Mwafrika's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th November 2006
      Posts : 4,546
      Rep Power : 1561
      Likes Received
      3
      Likes Given
      0

      Default Re: "Jamhuri ya Kigoma " Yatengwa!

      Quote By KGM View Post
      Ibrah unataka kunitoa machoni.
      Pamoja na serikali kuwa wabaguzi wakubwa sana na kuutenga mkoa wa kigoma makusudi lakini kinachochangia matatizo hayo kikubwa ni ukosefu wa wabunge makini.

      Kigoma haijapata kuwa na MBUNGE Makini anayewatetea hata siku moja. Hukumbuki miezi kama miwili iliyopita tu iliwalazimu FFU kuingia kuwatoa wasalifiri waliokuwa wamekaliana vichwani.
      Kwa kifupi ule sio usafiri.

      Harafu angali wabunge wa kigoma siku ile ya ZITO walivyoshambuliana bungeni. Selukamba&Msambya dhidi ya ZITO.

      Utafikiri ndicho kilicjhowapeleka bungeni.

      Ni aibu sana ndugu zanguni,

      Naomba Jambo forum itusaidie kutuokoa watu wa KIGOMA twafa.
      Hivi sheria ya Tanzania inasema kuwa lazima Mbunge wa sehemu fulani apige kelele Bungeni ndio barabara ijengwe? Umuhimu wa mkoa wa Kigoma (mkoa wa mpakani) haujulikani kwa serikali mpaka mbunge wa Kigoma aseme? miaka yote hii toka uhuru hakuna mtu serikalini anajua hili?

      Hii ni aibu kwa serikali kuu?

    13. #13
      Mwafrika's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th November 2006
      Posts : 4,546
      Rep Power : 1561
      Likes Received
      3
      Likes Given
      0

      Default Re: "Jamhuri ya Kigoma " Yatengwa!

      Quote By Mzalendohalisi View Post
      1. Viongozi toka Kigoma pia wamewaangusha wana Kigoma- kusema kweli sijawahi ona msukumo wa kweli toka kwa viongozi wanaotoka Kigoma! Angalia mfano wa 1.4 Bil toka kwa wana kagera!

      2. Sasa utamlaumu nani??? wakti viongozi wamekimbia Kigoma na kujenga Mz na Dar?

      3. Jawabu kudumu ni kujenga daraja Malagarasi- na barabara lami na kuwa na usafiri wa uhakika wa barabara- haya ndo mambo ya kutetea kwa nguvu na Wanakigoma kuondoa shilingi ktk budgeti! Ahadi tu za serikali kila siku over daraja na barabara- sasa 46 years! Hamna kitu!

      Sasa kama Kigoma wanachagua wabunge wanaotetea mambo ya Kitaifa kama Bugwazi na Zitto kwa nini wanashindwa kutetea infrustructure ya Kigoma?
      Mkuu Mzalendo,

      Ni jukumu la serikali kujenga miundombinu kutokana na pesa ya kodi inayotozwa kwa wananchi. Sidhani kama ni vyema wananchi kuchangishana kujenga barabara wakati huo huo wakilipa kodi!

      Kinaumiza kusikia kuwa wizi wa benki kuu ni zaidi ya billioni mia moja (kwa figure za Kikwete) na zaidi ya tilioni moja (kwa report ya Slaa) na wachache wanafaidika huku miundombinu ya nchi ikidumaa!

      Aibu kabisa kwa serikali kuu (to be specific serikali ya ccm) na viongozi wake!

    14. #14
      DAR si LAMU's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st March 2007
      Posts : 2,979
      Rep Power : 5722
      Likes Received
      151
      Likes Given
      0

      Default Re: "Jamhuri ya Kigoma " Yatengwa!

      Quote By kibunango View Post
      Pale Mwanza kuna jamaa zangu kibao toka Kigoma, mara nyingi wamekuwa wakilalamikia suala usafiri. Ni vema suala hili sasa likatupiwa japo jicho la huruma...
      ..dawa ni barabara ya lami tu!wabunge wa kigoma wako wapi?
      Dar na Lamu yote miji ya pwani, lakini haifanani!

    15. #15
      Kasana's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd April 2007
      Posts : 553
      Rep Power : 735
      Likes Received
      3
      Likes Given
      6

      Default Re: "Jamhuri ya Kigoma " Yatengwa!

      [QUOTE]
      Quote By Ibrah View Post
      Asante sana Morani; hawa Wahindi wa TRL ndiyo wanaoendesha zile treni ambazo watu wanakaa hadi juu ya behewa. Duniani kote hakuna mahali penye usafiri duni wa Treni kama kule India.

      Nakumbuka kuona picha ya namna hiyo kwenye magazeti yetu kama kuna mtu anazo atubandikie hapa.
      Mkuu,
      Tanzania ina matatizo mengi, na karibia kila sehemu inamatatizo yake,kuna mikoa kama Rukwa ambao wako kimya.

      Usafiri wa treni wa india huwezi kulinganisha na nchi zetu za kajambanani, india iko advanced katika usafiri wa terni, na wana grades za treni pia., na wananjia nyingi, siyo kama sisi, treni moja kwa wakati mmoja! Si sahihi kwa ulivyosema kuhusu India.

      Wakati Rais anafunga miaka 2 ya utawala kuna mwandishi alimwuliza kuhusu usafiri wa Reli , TRL an uwekezaji Muungwana akadai kuwa wakati wa TRC treni ilichukua hadi siku 8 kwenda Kigoma! Nilimshangaaa, maana haijawahi kutokea katika TRC Wasafiri kukaa siku 5 njiani ati kwa kuwa mabehewa ya mizigo yametokea never, Rais aliwadanganya WaTz! !
      Mimi natoka sehemu ambayo miaka nenda miaka rudi, TRC alikuwa partner wangu mkuu katika mambo ya usafiri, tangia enzi zile tunalala chini ya uvungu wa viti! Wakati ule watu walikuwa wanakaliana vichwani na miguuni, ilikuwa inajaza kama vile mabasi ya kwenda mwanza kupitia njia ya kati yanavyojaza! Na ilikuwa inawezekana kukaaa siku kadhaa porini, mvua ikinyesha 'godegode, kidete', treni ya mizigo ikianguka n.k taratibu TRC ikaongeza 'customer care' kwa kuwa inawaleta abiria wake kwa mabasi pindi hali inapokuwa tete.

      TRL imeanza kazi, ni budi wadau tupige kelele pale ambako tunaona wanataka kuturudisha miaka ile tulivyokuwa tunasafiri kama mizigo! ni budi tupige kelele kuona haki za wasafir zinalindwa ikiwemo compensation pindi treni inapochelewa kufika kama ilivyokusudiwa!

      Kitu ambacho TRC walikuwa wakifanya ni kubadilisha Wasafiri kuhamia treni nyingine (kubadlishana) na ilikuwa sahihi kabis. Sijui Muungwana alipandaga Treni ya TRC lini
      Ilikuwa pia inategemea na chanzo cha tatizo! Kama kipindi cha masika, hali ya treni moja kukwama 'Morogoro', nyingine 'Godegode; na nyingine 'Dodoma', ilikuwa jambo la kawaida, hapo huwezi kubadilishana! ni lazima moja ya gode gode iondoke kwanza ifike morogoro, na ya morogoro ifike dodoma ndipo ya dodoma iondoke! piga mahesabu hapo ni siku ngapi njiani! na kufika mapema kwa treni iliyokwama godegode ni majaaliwa ya hali ya mvua ikoje, na ikilzamika kuondoka bila kuangalia miundombinu ikoje, ndio matatizo kama ile ajali ya KIDETE ilivyotokea.
      'Facts' in the past. 'Options' in the present. 'Possibilities' in the future.
      The future can not be 'predicted' but can be 'created'.

    16. BAK is offline
      BAK
      #16
      BAK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2007
      Location : Mfaranyaki
      Posts : 26,841
      Rep Power : 45017
      Likes Received
      8689
      Likes Given
      8738

      Default Re: Kigoma Yatengwa! Usafiri balaa ..

      Mikoa hii (Kigoma, Tanga, Mtwara, Lindi na Rukwa) inadharauliwa kama siyo vile siyo sehemu ya Tanzania, pamoja na kuwa nyuma sana kimaendeleo lakini mgawo wa bajeti ya maendeleo unaotolewa katika mikoa hii ni mdogo sana ukilinganisha na mikoa mingi ambayo hali yao ina ahueni. Labda waombe kujitenga na kuwa sehemu ya nchi jirani ndio vilio vya mikoa hii vitasikilizwa, vinginevyo itabaki kuwa nyuma kimaendeleo milele.
      Let your graceful words fly out into the World, carried on winds of courage, imagination and joy. Let them inspire others to step into action

    17. #17
      MzalendoHalisi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th June 2007
      Posts : 4,049
      Rep Power : 1422
      Likes Received
      106
      Likes Given
      208

      Default Re: Kigoma Yatengwa! Usafiri balaa ..

      Quote By Bubu ataka kusema View Post
      Mikoa hii ( Tanga) inadharauliwa .
      Tanga hawana tatizo la barabara wala hawajatengwa- umefika Tanga mjini barabara zote leo zina lami- je utalinganisha na Kigoma? Kama Tanga wako nyuma ni sababu zaidi za watu wa huko-- angalia hadi leo hii hawana Chuo Kikuu hata kimoja yetu miundombinu iko ok na wanakusanya pesa nyingi TRA!

      Be fair Bubu kwa Tanga!
      Uadilifu Kiwe Kigezo Muhimu Zaidi Kuwa Kiongozi Tanzania Kwa Sasa!

    18. BAK is offline
      BAK
      #18
      BAK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2007
      Location : Mfaranyaki
      Posts : 26,841
      Rep Power : 45017
      Likes Received
      8689
      Likes Given
      8738

      Default Re: Kigoma Yatengwa! Usafiri balaa ..

      Naijua Tanga vizuri sana. Tanga ya miaka 60 na 70 siyo Tanga ya leo imerudi nyuma sana kimaendeleo maana wakuu wameamua kuitelekeza.
      Let your graceful words fly out into the World, carried on winds of courage, imagination and joy. Let them inspire others to step into action

    19. #19
      Malunde-Malundi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th January 2008
      Posts : 1,254
      Rep Power : 834
      Likes Received
      111
      Likes Given
      40

      Default Re: Kigoma Yatengwa! Usafiri balaa ..

      Naamini, Tunaweza kuomba mambo mengi mazuri yafanywe na wanasiasa wakatoa kila ahadi; lakini kama rasilimali zetu hazitumiki vema tutaishia kuongeza madeni ya nje kwa TZ. Kwanza usafi ufanywe ndani ya Kaya yetu, kama vile walau tumeona na bado hatujaridhika tu na ufagiaji alioujaribu(ingawa mdigo), then tubaki na wachache (hata mawaziri) wanaosimamia maslahi ya wananchi(sio matumbo yao kama ilivyodhihirika pale DOM kwa WNM/and CCM MP's) dhidi ya Kabwe; hilo likiisha, rasilimali zikazalisha kadri inavyopaswa kuwa; tukaweka malengo endelevu (yakiwa na Katiba isiyo mawaa) then sasa Dai huo mkoa unaoutaja au eneo unalolitaja; bila hivyo; tutapiga hatua kurudi nyuma tu.

    20. MC is online now
      MC
      #20
      MC's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 5th October 2007
      Location : Roaming !
      Posts : 514
      Rep Power : 700
      Likes Received
      78
      Likes Given
      146

      Default Re: Kigoma Yatengwa! Usafiri balaa ..

      hii hali ni mbaya sana na haikubaliki, bandari ya kigoma inaingiza pesa nyingi sana serikalini kutokana na kuwa mpakani, sasa iweje watu wasitengenezewe miundombinu bora, je ni ubaguzi au, na je kwa nini wananchi wa Kigoma waendeelee kuichagua ccm wakati inawapa mateso haya?
      Love your Country, Fear your Government!

    Page 1 of 2 12 LastLast

    Similar Topics

    1. Msaada: Safari ya Gari Ndogo: Mwanza - Kigoma / Kigoma - Mbeya
      By Baba Sangara in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 6
      Last Post: 22nd December 2011, 08:03
    2. Wanawake wa kigoma balaa!
      By mfocbsjut in forum JF Chit-Chat
      Replies: 99
      Last Post: 23rd November 2011, 07:27
    3. Mabilioni yatengwa kumsafisha Lowassa
      By BAK in forum Tanzania 2010-2015
      Replies: 1
      Last Post: 4th April 2011, 09:33
    4. Usafiri mwingine ni balaa tupu!!!!
      By Katavi in forum Jamii Photos
      Replies: 8
      Last Post: 21st November 2010, 14:08
    5. Kigoma nasikia ni balaa
      By Kashaijabutege in forum Tanzania 2010-2015
      Replies: 16
      Last Post: 1st November 2010, 22:13

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...