'Ripoti' ya Mziray na Mabadiliko ya Chadema kuelekea 2010 - JamiiForums |The Home of Great Thinkers

Go Back   JamiiForums |The Home of Great Thinkers > Public Forums > Jukwaa la Siasa


Jukwaa la Siasa Tanzania & World Politics General Discussion Forum. You need to be registered in order to post your comment(s)


Reply
 
LinkBack Thread Tools Rate Thread Display Modes
Old 22nd December 2007, 07:02 PM   #1
CHADEMA must Reform!
Rev. Kishoka Rev. Kishoka is offline 22nd December 2007, 07:02 PM

Political structure of Chadema resembles CCM! It stinks!

For CHADEMA to be effective on its drive to bring mageuzi, it needs to revamp its leadership structure and organization.

What Chadema has done is to follow the leadership structure and organization blue print of CCM inch by inch. As a result of this, it has failed to separate itself from CCM and thus being ineffective to bring solid changes to political spectrum fo Tanzania!

Mageuzi si kuingia Ikulu pekee, bali ni mabadiliko ya mfumo mzima wa siasa na uendeshaji wake. Chama Cha Demokrasia na Maendeleo, kinabidi kiwe cha kwanza kufanya hivyo,ndipo wengine watafuatilia na Wananchi wanweza kuanza kutofautisha Pumba na Mchele.

Nimewahi kuhoji miaka kadhaa iliopita kuwa siasa za Tanzania ni za mrengo gani baada ya Azimio la Zanzibar na kuja Mageuzi, sikupata jibu la maana zaidi ya watu kudai sisi sasa ni Mabepari na tuna Siasa za vyama vingi!

Mwanzo wa kweli wa mageuzi ya Siasa za Tanzania, utaanzia kwenye mabadiliko ya mfumo na miundo ya vyama vya siasa.

Chadema kiwe cha kwanza kuondokana na mfumowa ki-CCM ambao umelea tabaka la kundi maalum kutawala daima na kufanya maamuzi kwa Taifa zima (wanachama wake)!

Mbowe alipata bahati kuja Marekani wakati wa Uchaguzi wa 2004, je alijifunza yapi? je aliona mkutano mkuu wa chama kupitia kamati kuu na halmashauri kuu za Republican au Democrats zikipanga ni nani awe mgombea uwakilishi wa jimbo u uraisi? Nope!

Structure ya kwetu ni ya Kikomnisti, ile ile ya Wachina, Korea na hata Urusi. Sasa ni vipi mifumo hii ya utendaji italeta maendeleo na demokrasia ya kweli ikiwa Wenyeviti wa Vyama na wale "wateule wakuu" wanapewa nguvu za kufanya maamuzi makubwa kwa kutumia nyadhifa zao?

Kwa mnaoishi Marekani, mwaelewa mfumo wa siasa za vyama. Nguvu za chama na wawakilishi zipo majimboni na si Mkutano Mkuu au Kamati na Halmashauri Kuu!

Ikiwa Chadema itakubali mawazo yangu na kubadilisha mfumo wake ambao umeanza kuleta migooro na ulalamishi wa upendeleo, ukabila, udini na udugu na kuachia nguvu za wawikilishi kukamilishwa na wanachama wake katika ngazi za kata, wilaya hata mkoa, hapo ndipo mageuzi ya kweli katika siasa za Tanzania yatatoka na hiyo itakuwa njia pekee ya kuleta Demokrasia na Maendeleo kwa Taifa.

Mbowe, Slaa, Zitto, Mnyika, Makani, nasubiri vitendo!
__________________
Amani Iwe Nanyi,

Camerlengo

Plu Camerlenghi- Revolutionary Right Reverend Kishoka

"Any existence deprived of freedom is a kind of death." Gen. Michel Aoun

'Who comes to give greeting to the Inkosi-kaas? Who would taste her kiss, whereof the fruit is death? I, the Woodpecker, I, the Slaughterer, I the Swiftfooted! I, Umslopogaas!"

Last edited by Silencer; 24th July 2008 at 04:51 PM..

 
Rev. Kishoka's Avatar
Rev. Kishoka
JF Premium Member
Points: 1,760,733, Level: 100 Points: 1,760,733, Level: 100 Points: 1,760,733, Level: 100
Activity: 6% Activity: 6% Activity: 6%
Join Date: Mon Mar 2006
Location: USA
Posts: 3,481
Thanks: 1,019
Thanked 720 Times in 264 Posts
Views: 11961
Reply With Quote
  #2  
Old 22nd December 2007, 09:05 PM
John Mnyika's Avatar
John Mnyika John Mnyika is offline
John Mnyika has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 454,674, Level: 100 Points: 454,674, Level: 100 Points: 454,674, Level: 100
Activity: 2% Activity: 2% Activity: 2%
 
Join Date: Fri Jun 2006
Location: Tanzania
Posts: 788
Thanks: 4
Thanked 182 Times in 61 Posts
Rep Power: 25
John Mnyika will become famous soon enoughJohn Mnyika will become famous soon enoughJohn Mnyika will become famous soon enoughJohn Mnyika will become famous soon enoughJohn Mnyika will become famous soon enoughJohn Mnyika will become famous soon enoughJohn Mnyika will become famous soon enoughJohn Mnyika will become famous soon enough
Default Re: Chadema Must Reform!

Rev. Kishoka

Kuhusu mageuzi ndani ya CHADEMA tulishaitika mwito huo tayari; mara baada ya uchaguzi mkuu 2005 tulifanya tathmini ya kina na hatimaye tukaandaa Mpango Mkakati(Strategic Plan) ya miaka mitano. Kama sehemu ya Mpango huo tukaamua kubadili Katiba ya chama na kuchukua muundo tofauti kidogo(unaweza kuitazama kupitia www.chadema .net) na kuilinganisha na ya CCM. Ndio maana baada ya hapo tuliamua kuzindua chama upya( bonyeza hapa utapata maelezo yangu kuhusu uzinduzi huo na ni kwa vipi unakifanya CHADEMA kuwa chama tofauti na CCM):

http://www.chadema.net/blogu/mnyika/...a-chadema.html


Kwa hiyo uliyoyaona yametokea 2007 ni matokeo ya mipango na malengo sio bahati nasibu.

Mwaka 2008 ni mwaka wa uchaguzi ambapo tutaunda oganizesheni ya chama kuanzia ngazi ya msingi mpaka taifa, na hata kimataifa; na tutafanya hivi mijini na vijijini. Ni changamoto kwa wanaCHADEMA sasa kuifahamu ratiba husika na kushiriki michakato hii ya uchaguzi na kujenga chama katika maeneo yao.

Kwa kweli tumeamua kabisa kupeleka nguvu zaidi majimbo na hata kupanua uwakilishi wa majimbo kwenye baraza kuu; lakini nguvu za kichama sasa ni katika vitovu vya kimapambano.

Ni hatua nzuri; naamini mabadiliko yanayofuata ya katiba yatatoa mamlaka zaidi kwa ngazi za chini katika kujitawala; ila katiba hii mpya ya mwaka 2006 naamini itawezesha kuwa na muundo na mfumo bora zaidi. Haionekani sasa kwa kuwa mpaka sasa bado tunatumia katiba ya mwaka 2004. Katiba mpya itaanza kutumika mwaka 2008 mara baada ya uchaguzi. Kwa meneno mengine, uchaguzi utakaonza mwezi Februari utaendeshwa kwa katiba mpya ya CHADEMA ambayo imeshazingatia sehemu ya ushauri ambao umeutoa.

Lakini kazi hii si ya kina Mbowe, Makani, Zitto na Mnyika pekee. Ni yako pia wewe na yule. Pamoja tutashinda.

JJ
__________________
Kizazi Kipya, Maisha Mapya
New Generation, New Life

Mabadiliko ya Kweli, Uhuru wa Kweli
Real Change, Real Freedom

John Mnyika
Reply With Quote
  #3  
Old 22nd December 2007, 11:23 PM
Rev. Kishoka's Avatar
Rev. Kishoka Rev. Kishoka is offline
Rev. Kishoka has no status.
JF Premium Member
Points: 1,760,733, Level: 100 Points: 1,760,733, Level: 100 Points: 1,760,733, Level: 100
Activity: 6% Activity: 6% Activity: 6%
 
Join Date: Mon Mar 2006
Location: USA
Posts: 3,481
Thanks: 1,019
Thanked 720 Times in 264 Posts
Rep Power: 132
Rev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to all
Default Re: Chadema Must Reform!

Mnyika,

Kwa mtaji huu wa uamsho mpya unaniambia kuwa mtaondokana na Kamati na Halmashauri Kuu kufanya maamuzi yote ya kiutendaji katika kata, wilaya na Mikoa?

Jee wnaotaka kugombea uchaguzi katika Kata, Wilaya na Mikoa hawatakuwa na hofu ya majina yao kuchujwa kwenye kikao cha siri cha "Wateule"?

Ni nguvu gani wenyeviti wa Chama wa Mikoa walizonazo katika maamuzi ya Kitaifa na uongozi wa Chama Kitaifa?

Je Watendaji wa Chama katika Wilaya na Mikoa watakuwa huru kuchaguliwa na wanachama wao au watakuwa ni Wateule wa Mwenyekiti na kamati yake?

Je Katiba yenu inasemaje kuhusu kutenganisha kofia? Does the Chairman have to be Presidential Candidate? je Kutafuta Ugombea uraisi, maamuzi ni ya wanachama kupitia nguvu zao za kata, wilaya na mikoa au kila kitubado kitakuwa rolled up to Kamati na halmashauri Kuu ambazo zitawasilisha majina ya mchujo kwa Mkutano Mkuu?

Je hata kama mtabakia na Kamati Kuu na Halmashauri Kuu, mchujo wa wagombea uwakilishi kupitia Chadema utaachwa kwa ngazi husika au kwa wagombea waliopita michujo yote kujinadi mbele ya Mkutano Mkuu na si "Wateule" kuchuja na kuweka watu wanaowataka?

Tuendelee kuelimishana!
__________________
Amani Iwe Nanyi,

Camerlengo

Plu Camerlenghi- Revolutionary Right Reverend Kishoka

"Any existence deprived of freedom is a kind of death." Gen. Michel Aoun

'Who comes to give greeting to the Inkosi-kaas? Who would taste her kiss, whereof the fruit is death? I, the Woodpecker, I, the Slaughterer, I the Swiftfooted! I, Umslopogaas!"
Reply With Quote
  #4  
Old 23rd December 2007, 03:07 AM
Kithuku Kithuku is offline
Kithuku has successfully completed his PhD
JF Senior Expert Member
Points: 251,877, Level: 100 Points: 251,877, Level: 100 Points: 251,877, Level: 100
Activity: 1% Activity: 1% Activity: 1%
 
Join Date: Sun Nov 2006
Posts: 1,165
Thanks: 2
Thanked 19 Times in 8 Posts
Rep Power: 26
Kithuku will become famous soon enoughKithuku will become famous soon enoughKithuku will become famous soon enoughKithuku will become famous soon enoughKithuku will become famous soon enoughKithuku will become famous soon enoughKithuku will become famous soon enoughKithuku will become famous soon enough
Default Re: Chadema Must Reform!

Simfahamu huyu Mnyika isipokuwa tu kwa kumsoma hapa, lakini kwa ambayo nimeshasoma toka kwake tayari naona ni mtu makini sana katika anayoyafanya. He sounds intelligent, organised and very well composed. Kila siku zinavyoenda na ninavyosoma post zake humu ndani, namwona anavyozidi kukua siku baada ya siku, yani ukisoma alichoandika mwezi huu utaona kina ukomavu kuliko mwezi uliopita, ni hazina ya ajabu huyu jamaa. Sijui umri wake huyu jamaa, lakini natamani kuona CHADEMA ikikua kwa rate ya huyu jamaa, na kama hili likitokea kuna matumaini mazuri mbeleni ya kupata mifumo mbadala ya kuongoza nchi. Sijajua pia kama yuko hivyo kwa sababu ya uzuri wa chama (maana yake na wanachama wengine wengi wako hivyo pia), au ni personal attributes na qualities zake (ambazo pia CHADEMA inaweza kuzitumia vizuri kujenga chama chao).

Kwa ujumla namtakia heri ndugu Mnyika, na kumtaka aendelee kutumia kipaji alichojaliwa pamoja na wenzie huko kwenye CHADEMA, watupatie matumaini kuwa mabadiliko ya serikali yanawezekana na mbadala upo (maana wako wengi wanaochagua CCM kwa kukosa viable alternatives).
__________________
"Those who cannot remember the past are condemned to repeat it." George Santayana(1863-1952), U.S Philosopher and Poet. Life of Reason, 'Reason in Common Sense', Scribners, 1905, page 284
Reply With Quote
  #5  
Old 23rd December 2007, 06:53 AM
John Mnyika's Avatar
John Mnyika John Mnyika is offline
John Mnyika has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 454,674, Level: 100 Points: 454,674, Level: 100 Points: 454,674, Level: 100
Activity: 2% Activity: 2% Activity: 2%
 
Join Date: Fri Jun 2006
Location: Tanzania
Posts: 788
Thanks: 4
Thanked 182 Times in 61 Posts
Rep Power: 25
John Mnyika will become famous soon enoughJohn Mnyika will become famous soon enoughJohn Mnyika will become famous soon enoughJohn Mnyika will become famous soon enoughJohn Mnyika will become famous soon enoughJohn Mnyika will become famous soon enoughJohn Mnyika will become famous soon enoughJohn Mnyika will become famous soon enough
Default Re: Chadema Must Reform!

Quote:
View Post
Mnyika,

Kwa mtaji huu wa uamsho mpya unaniambia kuwa mtaondokana na Kamati na Halmashauri Kuu kufanya maamuzi yote ya kiutendaji katika kata, wilaya na Mikoa?

Jee wnaotaka kugombea uchaguzi katika Kata, Wilaya na Mikoa hawatakuwa na hofu ya majina yao kuchujwa kwenye kikao cha siri cha "Wateule"?

Ni nguvu gani wenyeviti wa Chama wa Mikoa walizonazo katika maamuzi ya Kitaifa na uongozi wa Chama Kitaifa?

Je Watendaji wa Chama katika Wilaya na Mikoa watakuwa huru kuchaguliwa na wanachama wao au watakuwa ni Wateule wa Mwenyekiti na kamati yake?

Je Katiba yenu inasemaje kuhusu kutenganisha kofia? Does the Chairman have to be Presidential Candidate? je Kutafuta Ugombea uraisi, maamuzi ni ya wanachama kupitia nguvu zao za kata, wilaya na mikoa au kila kitubado kitakuwa rolled up to Kamati na halmashauri Kuu ambazo zitawasilisha majina ya mchujo kwa Mkutano Mkuu?

Je hata kama mtabakia na Kamati Kuu na Halmashauri Kuu, mchujo wa wagombea uwakilishi kupitia Chadema utaachwa kwa ngazi husika au kwa wagombea waliopita michujo yote kujinadi mbele ya Mkutano Mkuu na si "Wateule" kuchuja na kuweka watu wanaowataka?

Tuendelee kuelimishana!

Rev. Kishoka

Nimeambatanisha Katiba ya CHADEMA- isome halafu tuendelee kuelimishana.

Utaona kwa katiba hii mamlaka ya maamuzi yapo kwenye chama ngazi husika kuhusiana na yale mambo ambayo yanahusu ngazi hiyo. Utanona kwamba hapo kwamba chama hakiendeshwi na 'wateule wachache'! Chama ni cha wananchama kupitia vyombo vyao vya maamuzi. Ngazi ya juu inaingilia ngazi ya chini kama tu kuna masuala yamekiukwa.

Hii katiba kuna mambo yapo humo ni ya mpito, naamini siku za baadaye tutafanya mabadiliko mengine makubwa zaidi- baadhi ya miundo ipo kama hatua za awali za kuitambulisha na baadaye itakuja kupewa nguvu zaidi katika mabadiliko yajayo. Katika mabadiliko ya mwaka 2006 tulikuwa makundi matatu ya mawazo(sio kambi): wapo waliokataa mabadiliko, wapo waliotaka mabadiliko kiasi na wapo waliotaka mabadiliko makubwa kupindukia. Katiba unayoiona ni compromise ya makundi yote matatu; ukiona katiba ya 2004 ukalinganisha na hii utaelewa nasema nini. Na kwa kweli ilikuwa kazi ngumu kufanya haya mabadiliko kwa kuwa binadamu wengi kwa asili ni watu wa mazoea na hivyo kuhofia mabadiliko- karibu mchakato huu utuzalishie migogoro lakini kwa kuwa tulihusisha wanachama kwa kupata maoni yao kuanzia chini tulipata uhalali wa hoja za kufanya yaliyofanyika! Hivyo wazo la local parties kuwa autonomous kama ilivyo baadhi ya nchi duniani nalo lilijitokeza, lakini zingine zilionekana ni radical reforms sana ukilinganisha na mazingira ya kisiasa ya Tanzania- hivyo ililbidi kuwa makini kuepuka institutional crush! Unaweza kujiuliza ilikuwaje tukaweza kukubaliana kubadili rangi za bendera na kuzindua chama upya? Against uniforms and bendera ambazo tayari zilikuwa zimesambaa? Kwa hiyo, kwangu mimi huu ulikuwa mwazo mzuri wa reforms- tutaendelea zaidi katika awamu itakayofuata ya mabadiliko ndani ya chama.

Kwa katiba hii watu wako huru kuchaguliwa na wanachaguliwa na wengi. Katiba iko kimya kuhusu kutenganisha kofia kwa hiyo si lazima uwe mwenyekiti kuwa mgombea Urais na si lazima Rais awe Mwenyekiti.

Katiba imedokeza mchakato wa mchujo; lakini haijaingia kiundani sana. Kuna mambo mengine yapo kwenye taratibu- kwa mfano, kabla ya kamati kuu, baraza kuu na mkutano mkuu- tunafanya kwanza primaries kama ilivyo Marekani ili kushindanisha wanaotaka kugombea Urais ambao wanachama wana haki ya kuchagua wampendae- kwa hiyo mapendekezo ya jina kwa National Congress yanategemea Primaries- So far ni CHADEMA pekee ndio inatumia mfumo huu Tanzania!

Kuna nyaraka nyingine muhimu ambazo ni vyema zikasomwa baada ya kusoma katiba: Kanuni, Itifaki na Maadili; Taratibu za Mabaraza ya Wanawake, Wazee na Vijana Nk. Ukisoma mambo yote haya utabaini kwamba CHADEMA ni Chama cha Demokrasia na Maendeleo. Karibu

JJ
Attached Files
File Type: pdf katiba_2006.pdf (76.9 KB, 21 views)
__________________
Kizazi Kipya, Maisha Mapya
New Generation, New Life

Mabadiliko ya Kweli, Uhuru wa Kweli
Real Change, Real Freedom

John Mnyika
Reply With Quote
  #6  
Old 23rd December 2007, 07:13 AM
John Mnyika's Avatar
John Mnyika John Mnyika is offline
John Mnyika has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 454,674, Level: 100 Points: 454,674, Level: 100 Points: 454,674, Level: 100
Activity: 2% Activity: 2% Activity: 2%
 
Join Date: Fri Jun 2006
Location: Tanzania
Posts: 788
Thanks: 4
Thanked 182 Times in 61 Posts
Rep Power: 25
John Mnyika will become famous soon enoughJohn Mnyika will become famous soon enoughJohn Mnyika will become famous soon enoughJohn Mnyika will become famous soon enoughJohn Mnyika will become famous soon enoughJohn Mnyika will become famous soon enoughJohn Mnyika will become famous soon enoughJohn Mnyika will become famous soon enough
Default Re: Chadema Must Reform!

Quote:
View Post
Simfahamu huyu Mnyika isipokuwa tu kwa kumsoma hapa, lakini kwa ambayo nimeshasoma toka kwake tayari naona ni mtu makini sana katika anayoyafanya. He sounds intelligent, organised and very well composed. Kila siku zinavyoenda na ninavyosoma post zake humu ndani, namwona anavyozidi kukua siku baada ya siku, yani ukisoma alichoandika mwezi huu utaona kina ukomavu kuliko mwezi uliopita, ni hazina ya ajabu huyu jamaa. Sijui umri wake huyu jamaa, lakini natamani kuona CHADEMA ikikua kwa rate ya huyu jamaa, na kama hili likitokea kuna matumaini mazuri mbeleni ya kupata mifumo mbadala ya kuongoza nchi. Sijajua pia kama yuko hivyo kwa sababu ya uzuri wa chama (maana yake na wanachama wengine wengi wako hivyo pia), au ni personal attributes na qualities zake (ambazo pia CHADEMA inaweza kuzitumia vizuri kujenga chama chao).

Kwa ujumla namtakia heri ndugu Mnyika, na kumtaka aendelee kutumia kipaji alichojaliwa pamoja na wenzie huko kwenye CHADEMA, watupatie matumaini kuwa mabadiliko ya serikali yanawezekana na mbadala upo (maana wako wengi wanaochagua CCM kwa kukosa viable alternatives).

Kithuku

Heshima yako, naamini kabisa utakuwa umenizidi umri- nimefarijika na maneno yako.

Maisha ni kukua katika kila pumzi tunayoendelea kuvuta. Maisha ni kujifunza toka kwa kila mtu- kujifunza mazuri na mabaya, na kufanya maamuzi sahihi. Maisha pia ni kufundisha kwa maneno na vitendo. The golden rule!

Wengine kwa sasa tumeamua kujitoa kafara kwa muda kujenga chama mbadala, uongozi mbadala, sera mbadala, siasa mbadala na Tanzania mbadala. Tunapoteza mengi kwa kufanya hivi kwa sasa, lakini tunajaribu kutazama mbali zaidi. Tunafanya hivyo kwa kuwa tunaamini hivyo vya binafsi tunavyovipoteza kwa sasa, tuna uwezo wa kuvipata wakati ujao- pamoja na kuwa wakati ni ukuta. Lakini hivi tunavyovifanya sasa, ndivyo umma una hitaji kwa sasa. Taifa letu liko katika mtanziko, linahitaji mfumo mbadala. Kama kila mtu atakimbia kutekeleza wajibu huu, hakika historia itakuja kutuhukumu. Lakini kama tukitimiza jukumu hili vizuri, hakika historia itakuja kutuheshimu.

Niliona chama mbadala kupitia CHADEMA, na sasa naliona Tumaini Jipya. Lakini ni wazi chama hiki mbadala inabidi kiboreshwe kuwa mbadala uliobora, na kazi hii haiwezi kufanywa tu kwa kunyoosha vidole kwa mbali. Hatupaswi tu kuomba mambo yatokee ama kushabikia yakitokea, tunapaswa kufanya yatokee. CHADEMA inahitaji kuungwa mkono na wewe na wengine, bahari ni muunganiko wa matone ya maji. Kama matone hayo ya maji yasingekuwa pamoja asingekuwa bahari!

Kwangu mimi yote ninayofanya sasa ni wito, nafanya yote kwa nia ya kutumikia na kutumia vizuri talanta kwa ajili ya mridhiko wa nafsi na maslahi ya wengi. Nayaweza yote haya katika yeye anitiaye nguvu. Bado kitambo kidogo nitatoweka, lakini ni baada ya kutimiza wajibu kwanza. Na kweli hata kutoweka kwangu kutakuwa kimwili tu, roho yangu itaendelea kusimama kidete kuona chama mbadala kinachukua dola Tanzania ili viongozi bora waunganishe nguvu ya umma kutumia rasilimali ambazo Mungu ametujalie kwa manufaa ya kizazi chetu na vijavyo. Nashukuru, tuendelee kuombeana kila la kheri


JJ
__________________
Kizazi Kipya, Maisha Mapya
New Generation, New Life

Mabadiliko ya Kweli, Uhuru wa Kweli
Real Change, Real Freedom

John Mnyika
Reply With Quote
  #7  
Old 23rd December 2007, 08:35 AM
Kasheshe's Avatar
Kasheshe Kasheshe is offline
Kasheshe a responsible citizen!
JF Premium Member
Points: 301,365, Level: 100 Points: 301,365, Level: 100 Points: 301,365, Level: 100
Activity: 13% Activity: 13% Activity: 13%
 
Join Date: Fri Jun 2007
Location: Bububu
Posts: 2,579
Thanks: 221
Thanked 204 Times in 114 Posts
Rep Power: 28
Kasheshe will become famous soon enoughKasheshe will become famous soon enoughKasheshe will become famous soon enoughKasheshe will become famous soon enoughKasheshe will become famous soon enoughKasheshe will become famous soon enoughKasheshe will become famous soon enoughKasheshe will become famous soon enough
Default Re: Chadema Must Reform!

Mnyika kweli anajitahidi, lakini namshauri akae na wazee karibu sana hata wa CCM/TANU/ASP/HIZZIB/ZPPP/CUF/PPT/MAKINI kupata uzoefu namna ya kulainisha mambo,,, kwa kuwa CHADEMA kikiwa chama kikubwa ukumbuke misuguano haitaepukika,,, sasa wanatakiwa walioandaliwa kuweza kulainisha na kwenda mbele!!!

Kuna Moja tu ninalo liona, siasa sio Rocket Science,,, kijana yeyote mzuri, mwenye exposure kama ya Mnyika kwenye mambo ya Kitaifa na Kimataifa anaweza kushaini kwenye siasa za sasa ambazo zimekuwa chini ya Wazee kama Kingunge, na wengineo mradi tu akubali kwamba primary occupation yake iwe siasa!!! hapa utaonekana Kipanga...

Sina ufahamu zaidi wa Historia ya Mnyika other than,,, kujichanganya kwenye mambo ya Vijana wa kitaifa na Kiafrika na ile issue ya Ubungo!!!

Mtu ambaye mimi binafsi namkubali bila matatizo yoyote ni Kitila Mkumbo,,, unapokuwa President kwenye institution yenye demokrasia ya hali ya juu hapa nchini kama ile ya DARUSO,,, pale ni sehemu nzuri sana ya kujua huyu ni Kiongozi au La... Najua hashaini kwa kuwa Kitila inaonyesha anakazi nyingine Primary na Siasa ni by the way, au kazi ya Pili,,, lakini Lau siasa ingekuwa his primary JOB... mambo yangekuwa mengine!!!

Infact mtanisamehe lakini nina haki ya kutoa maoni yangu!!! Kitila Mkumbo ni Zaidi ya hata Zitto, as I said ni kwa kuwa mguu ndani, mguu nje!!! na wakati mwingine ni vyombo vimekujenga?


Kuna siku moja mchangiaji mmoja alisema Pro. Issa Shivji apewe kesi,,, anasahau kwamba kufundisha na ku-practise ni vitu viwili tofauti,,, Maprofessa ni watu wanaamini kwenye taaluma na nadharia,,, lakini kwenye vitendo/practises mara nyingi ni Vilaza wa hali ya juu sana. Ndio maana kwenye makampuni yanayotafuta faida, hata kwenye idara zao za R&D unakuta ni mara chache sana kuna maprofessa huko!!!!

Kwa hiyo Mnyika na Zitto waanapractise ndio maana wanaonekana kazi zao, kuna vijana wengi vipanga kwa maana hata shuleni hawajaunga unga na pia vichwani wako fiti sana but hawana platform ya kutokea,,, kwenye taifa makini huwa wanatafutwa na kupelekwa sehemu stahiki!!!
Reply With Quote
  #8  
Old 23rd December 2007, 09:22 AM
John Mnyika's Avatar
John Mnyika John Mnyika is offline
John Mnyika has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 454,674, Level: 100 Points: 454,674, Level: 100 Points: 454,674, Level: 100
Activity: 2% Activity: 2% Activity: 2%
 
Join Date: Fri Jun 2006
Location: Tanzania
Posts: 788
Thanks: 4
Thanked 182 Times in 61 Posts
Rep Power: 25
John Mnyika will become famous soon enoughJohn Mnyika will become famous soon enoughJohn Mnyika will become famous soon enoughJohn Mnyika will become famous soon enoughJohn Mnyika will become famous soon enoughJohn Mnyika will become famous soon enoughJohn Mnyika will become famous soon enoughJohn Mnyika will become famous soon enough
Default Re: Chadema Must Reform!

Quote:
View Post
Mnyika kweli anajitahidi, lakini namshauri akae na wazee karibu sana hata wa CCM/TANU/ASP/HIZZIB/ZPPP/CUF/PPT/MAKINI kupata uzoefu namna ya kulainisha mambo,,, kwa kuwa CHADEMA kikiwa chama kikubwa ukumbuke misuguano haitaepukika,,, sasa wanatakiwa walioandaliwa kuweza kulainisha na kwenda mbele!!!

Kuna Moja tu ninalo liona, siasa sio Rocket Science,,, kijana yeyote mzuri, mwenye exposure kama ya Mnyika kwenye mambo ya Kitaifa na Kimataifa anaweza kushaini kwenye siasa za sasa ambazo zimekuwa chini ya Wazee kama Kingunge, na wengineo mradi tu akubali kwamba primary occupation yake iwe siasa!!! hapa utaonekana Kipanga...

Sina ufahamu zaidi wa Historia ya Mnyika other than,,, kujichanganya kwenye mambo ya Vijana wa kitaifa na Kiafrika na ile issue ya Ubungo!!!

Mtu ambaye mimi binafsi namkubali bila matatizo yoyote ni Kitila Mkumbo,,, unapokuwa President kwenye institution yenye demokrasia ya hali ya juu hapa nchini kama ile ya DARUSO,,, pale ni sehemu nzuri sana ya kujua huyu ni Kiongozi au La... Najua hashaini kwa kuwa Kitila inaonyesha anakazi nyingine Primary na Siasa ni by the way, au kazi ya Pili,,, lakini Lau siasa ingekuwa his primary JOB... mambo yangekuwa mengine!!!

Infact mtanisamehe lakini nina haki ya kutoa maoni yangu!!! Kitila Mkumbo ni Zaidi ya hata Zitto, as I said ni kwa kuwa mguu ndani, mguu nje!!! na wakati mwingine ni vyombo vimekujenga?


Kuna siku moja mchangiaji mmoja alisema Pro. Issa Shivji apewe kesi,,, anasahau kwamba kufundisha na ku-practise ni vitu viwili tofauti,,, Maprofessa ni watu wanaamini kwenye taaluma na nadharia,,, lakini kwenye vitendo/practises mara nyingi ni Vilaza wa hali ya juu sana. Ndio maana kwenye makampuni yanayotafuta faida, hata kwenye idara zao za R&D unakuta ni mara chache sana kuna maprofessa huko!!!!

Kwa hiyo Mnyika na Zitto waanapractise ndio maana wanaonekana kazi zao, kuna vijana wengi vipanga kwa maana hata shuleni hawajaunga unga na pia vichwani wako fiti sana but hawana platform ya kutokea,,, kwenye taifa makini huwa wanatafutwa na kupelekwa sehemu stahiki!!!
Kaka Kilitime

Naomba turejee kwenye mjadala mama "CHADEMA Must Reform". Naona sasa tunaelekea kujadili nani ana 'pua ndefu' kati ya Kitila, Mnyika na Zitto....(mzaha)

Tuendelee kujadili.

Nasubiri Rev. Kishoka na wengine waje na hoja za ziada kuhusu maboresho ya CHADEMA.

JJ
__________________
Kizazi Kipya, Maisha Mapya
New Generation, New Life

Mabadiliko ya Kweli, Uhuru wa Kweli
Real Change, Real Freedom

John Mnyika
Reply With Quote
  #9  
Old 23rd December 2007, 07:56 PM
Kasheshe's Avatar
Kasheshe Kasheshe is offline
Kasheshe a responsible citizen!
JF Premium Member
Points: 301,365, Level: 100 Points: 301,365, Level: 100 Points: 301,365, Level: 100
Activity: 13% Activity: 13% Activity: 13%
 
Join Date: Fri Jun 2007
Location: Bububu
Posts: 2,579
Thanks: 221
Thanked 204 Times in 114 Posts
Rep Power: 28
Kasheshe will become famous soon enoughKasheshe will become famous soon enoughKasheshe will become famous soon enoughKasheshe will become famous soon enoughKasheshe will become famous soon enoughKasheshe will become famous soon enoughKasheshe will become famous soon enoughKasheshe will become famous soon enough
Default Re: Chadema Must Reform!

Quote:
View Post
Kaka Kilitime

Naomba turejee kwenye mjadala mama "CHADEMA Must Reform". Naona sasa tunaelekea kujadili nani ana 'pua ndefu' kati ya Kitila, Mnyika na Zitto....(mzaha)

Tuendelee kujadili.

Nasubiri Rev. Kishoka na wengine waje na hoja za ziada kuhusu maboresho ya CHADEMA.

JJ
Kweli kaka Alaa! kumbe nimetoka nje ya mstari!!! Mdogo wetu, tukipata fursa ya kufunda na kusema ukweli tunamwaga hapo hapo![message sent].
Nimesoma katiba yenu kwa kuanzia nzuri only that itahitaji several frequent reviews, kwa kuwa imeingiza mambo mengine ambayo si lazima yawe kwenye katiba!mengine yanakuwa kwenye ilani za uchaguzi tu! au kwenye program za chama! Katiba nzuri ni ile ambayo inabeba makubwaya ujumla na kuacha details kanuni, ilani na program mbalimbali kwenye...
Mna pakuanzia, sasa tafuteni viongozi wa kukipeleka chama mbele!! Hakikishesheni chama kinakuwa real taasisi, maadili ya wanachama na viongozi. yanaheshiwa.!
Reply With Quote
  #10  
Old 23rd December 2007, 08:11 PM
Rev. Kishoka's Avatar
Rev. Kishoka Rev. Kishoka is offline
Rev. Kishoka has no status.
JF Premium Member
Points: 1,760,733, Level: 100 Points: 1,760,733, Level: 100 Points: 1,760,733, Level: 100
Activity: 6% Activity: 6% Activity: 6%
 
Join Date: Mon Mar 2006
Location: USA
Posts: 3,481
Thanks: 1,019
Thanked 720 Times in 264 Posts
Rep Power: 132
Rev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to all
Default Re: Chadema Must Reform!

Mnyika, Kilitime

Nafikiri ni wakatiumewadia kuwa tunabadilisha mwelekeo wa fikira zetu na nguvu za ushawishi na kuwa ni nguvu za kujenga Taifa na si kuhoji tuu yaliyotokea.

Nimeipitia katiba ya Chadema jana ni nzuri. Nikajiuliza mfumo wake na kama Mnyika navyoelezea hapa inaelekea ni mzuri. Sasa tatizo ni lipi kuwa haina wafuasi wengi hasa vijana na wanataaluma? au ni kwa kuwa wengi wanaogopa mkono wa dola (CCM)?

Kikubwa ambacho kinakera ni kwa Chama cha upinzani chenye nguvu kama Chadema kuonekana kina kosa uadilifu kama CCM. Na hii inatokana na hisi azilizojengeka tangu awali eti n Chama cha Wachaga na kuna ukabila na undugunization.

Ndio maana nikasema, ili Chadema kiwe kamilifu (at least 85%) inabidi kibadili mfumo wake wa kiutendaji na utawala na isionekane kuwa hiki ni chama cha Mtei na mkwewe Freeman.

Nimefurahia jinsi Mnyika ulivyo na uamsho na imani katika chama chako, swali ni jee ni wangapi katika chama Chako wenye mtazamo kama wako?

Jumuiya yenu ya vijana ina nguvu kiasi gani kupambana na Nchimbi na wafuasi wake? Nguvu ninazoulizia ni za mfumo wa utandawazi, mawazo, kujitolea na uhamasishaji si nguvu za fedha ambazo najua Chadema haina kufananisha na Chama Cha Machotaji!

Ni tumaini langu kuwa kama Chadema itaongeza mwendo kasi wake wa reforms and si kusua sua, basi mnaweza kupata japo 15% ya viti vya Bunge.

Reformation ya Chadema ni lazima iende kwa slogan ya Kikwete, Ari, Kasi na Nguvu mpya. Nafikiri mkiendelea kuchelea kufanya kweli ili kwenda na wakati na kupambana na ufidhuli wa CCM, basi itawachukua miaka 46 kufika mahali CCM ilipo leo kimuundo na kiutandawazi.
__________________
Amani Iwe Nanyi,

Camerlengo

Plu Camerlenghi- Revolutionary Right Reverend Kishoka

"Any existence deprived of freedom is a kind of death." Gen. Michel Aoun

'Who comes to give greeting to the Inkosi-kaas? Who would taste her kiss, whereof the fruit is death? I, the Woodpecker, I, the Slaughterer, I the Swiftfooted! I, Umslopogaas!"
Reply With Quote
Reply

Bookmarks

Tags
2010, chadema, kuelekea, mabadiliko, mziray, ripoti


Currently Active Users Viewing This Thread: 1 (0 members and 1 guests)
 
Thread Tools
Display Modes Rate This Thread
Rate This Thread:

Posting Rules
You may not post new threads
You may not post replies
You may not post attachments
You may not edit your posts

BB code is On
Smilies are On
[IMG] code is On
HTML code is Off
Trackbacks are Off
Pingbacks are Off
Refbacks are On


Similar Threads
Thread Thread Starter Forum Replies Last Post
Mbowe vs Chifupa + CHADEMA vs Family Business chinga Jukwaa la Siasa 1070 3rd November 2009 03:03 PM
The Only Thing We Have To Fear ... Freeman A. Mbowe Jamii Intelligence 411 14th May 2009 09:11 AM
Baada ya Kikwete ni Mbowe Mwanaidi Jukwaa la Siasa 62 19th August 2008 11:28 AM
CHADEMA Imebeba utume wa Kizazi Kipya Mwanaidi Jukwaa la Siasa 19 8th June 2007 11:48 AM
Uhusiano kati ya CHADEMA na CONSERVATIVES (UK) <PART 3> wafafanuliwa na JOHN MNYIKA Game Theory Habari na Hoja mchanganyiko 14 6th February 2007 03:00 PM

Tuma Ukurasa huu kwa rafiki yako!


All times are GMT +3. The time now is 12:53 PM.

Powered by JamiiForums.com
Copyrights reserved to JamiiForums.com