Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Neno La Leo: Afrika Viongozi Hawana Shukrani!

    Report Post
    Results 1 to 6 of 6
    1. #1
      maggid's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd December 2006
      Posts : 776
      Rep Power : 800
      Likes Received
      654
      Likes Given
      33

      Default Neno La Leo: Afrika Viongozi Hawana Shukrani!

      Viongozi Afrika hawana shukrani

      Na Maggid Mjengwa,

      HISTORIA ni mwalimu mzuri. Nimekumbushia hilo mara kwa mara. Kabla ya kuwa Waziri Mkuu wa Uingereza, Winston Churchill alipata kuwa waziri wa masuala ya majini ( Marine Minister). Ilikuwa ni wakati wa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia. Winston Churchill ambaye pia alikuwa askari mwanamaji, aliacha ofisi yake na kuongoza vikosi vya wanamaji katika vita hivyo. Na hata baada ya vita kwisha, Churchill akafanywa kuwa ‘ Waziri wa Vita’ ( Defence Minister). Baadae, Winston Churchill akaja kuwa Waziri Mkuu wa Uingereza.
      Pamoja na ukweli, kuwa Winston Churchill aliiongoza vema Uingereza na hata kuweza kufanikisha ushindi katika Vita Kuu ya Pili ya Dunia, bado, Waingereza hawakumchagua Winston Churchill katika uchaguzi mkuu wa mwaka 1945. Inaweza kusemwa, kuwa wapiga kura wa Uingereza hawakuwa na shukrani. Kwamba wapiga kura wa Uingereza hawakumpima Churchill kwa historia bali kwa yatakayokuja. Kuna cha kujifunza, maana, Afrika kiongozi ukihangaika ukawajengengea watu wako barabara na madaraja, kuna shukrani watakazokupa. Afrika Rais anaweza kuitwa ' Rais wa Barabara, au Rais wa Maji' kama katika muda wake wa uongozi ameweza kuwasaidia watu wake katika kujenga barabara na kuwaletea maji. Wapiga kura Afrika wana shukrani, tatizo ni baadhi ya viongozi Afrika kukosa shukrani.



      Ndio, nchi zetu kimsingi bado changa, na demokrasia zetu pia.

      Maana, nchi nyingi katika bara letu hili la Afrika mwaka huu na mwakani zitatimiza miaka hamsini tangu kupata uhuru wake kutoka kwa wakoloni. Ni nusu karne. Ni muda mrefu. Yamkini shingo zetu wanadamu ni ndefu, lakini maisha yetu ni mafupi sana. Ndio, muda wetu wa kuishi humu duniani ni mfupi sana. Na historia itabaki kuwa hakimu kwa tunayoyafanya sasa.
      Maana, wengi wetu tunaishi na kuziacha nchi zetu tulizozaliwa hata kabla hatujatimiza miaka 70 humu duniani. Lakini, nchi tulizozaliwa tunaziacha zikiwa na wanadamu wenzetu. Ni watoto wetu, ni wajukuu zetu. Na sisi Waafrika tumekuwa ni watu wabinafsi sana. Ni watu tunaoishi bila kufikiria sana ya kesho na kesho kutwa. Tunajiangalia sisi tu.
      Sehemu kubwa ya matatizo ya nchi zetu hizi yanatokana na ubinafsi huo. Na bahati mbaya kabisa, baadhi ya viongozi tuliowapa dhamana za uongozi ndio wenye kuongoza kwa matendo yenye kutanguliza maslahi yao binafsi. Katiba za nchi zetu ni kielelezo halisi cha ubinafsi huo. Maana, wakoloni walitengeneza katiba ili ziwasaidie katika kututawala. Katiba ya mkoloni ilikuwa na maana moja kubwa; kuonyesha namna ya kuwatawala watu wa nchi iliyo mikononi mwa wakoloni. Na nchi zetu nyingi zimerithi misingi ya katiba hizo za kikoloni. Katiba nyingi za nchi za Kiafrika zinaonyesha namna ambavyo Waafrika wachache walio katika mamlaka ya Kiserikali watakavyowatawala “ Waafrika” wenzao! Na hilo ndilo ‘Neno La Leo’. Fikiri kwa bidii.
      Maggid,
      Kinondoni Biafra.

    2. Miaka 50

    3. #2
      Kichuguu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th October 2006
      Location : Popote Porini
      Posts : 6,836
      Rep Power : 3272
      Likes Received
      1315
      Likes Given
      916

      Default Re: Neno La Leo: Afrika Viongozi Hawana Shukrani!

      Maggid,

      Article yako ina udhaifu mkubwa sana unapoanza kwa kichwa kuwa viongozi wa Afrika hawana shukurani halafu sehemu kubwa article inajumuisha kuwa waafrika wote ni wabinafsi na hivyo kuhalalisha ubinafsi wa viongozi wa Afrika. Usije kujinyonga kwa kuonyeshwa udhaifu huo. Tambua kuwa ubinfasi ni tabia ya binadamu wote, ila viongozi thabiti huweka sheria za kubana ubinafsi huo. Nyerere aliweka miiko ya uongozi kupitia Azimio lake la Arusha kuwabana viongozi wasiwe wabinafsi lakini Azimio hilo likabomolewa ili kuhalalisha ubinafsi wa viongozi; kwani Nyerere alikuwa mzungu? Marekani wana sheria thabiti sana za kuwabana viongozi wasijinufaishe kwa nafasi zao za uongozi lakini bado kuna wanaoshikwa kwa kukiuka sheria hizo na hivyo kufungwa miaka mingi jela.
      Kichuguuu: Nyumba inayohifadhi mchwa na nguchiro kwa pamoja bila mkwaruzo

    4. #3
      Kituko's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th January 2009
      Posts : 3,716
      Rep Power : 1288
      Likes Received
      497
      Likes Given
      175

      Default Re: Neno La Leo: Afrika Viongozi Hawana Shukrani!

      Quote By maggid
      Viongozi Afrika hawana shukrani

      Na Maggid Mjengwa,

      HISTORIA ni mwalimu mzuri. Nimekumbushia hilo mara kwa mara. Kabla ya kuwa Waziri Mkuu wa Uingereza, Winston Churchill alipata kuwa waziri wa masuala ya majini ( Marine Minister). Ilikuwa ni wakati wa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia. Winston Churchill ambaye pia alikuwa askari mwanamaji, aliacha ofisi yake na kuongoza vikosi vya wanamaji katika vita hivyo. Na hata baada ya vita kwisha, Churchill akafanywa kuwa ‘ Waziri wa Vita’ ( Defence Minister). Baadae, Winston Churchill akaja kuwa Waziri Mkuu wa Uingereza.
      Pamoja na ukweli, kuwa Winston Churchill aliiongoza vema Uingereza na hata kuweza kufanikisha ushindi katika Vita Kuu ya Pili ya Dunia, bado, Waingereza hawakumchagua Winston Churchill katika uchaguzi mkuu wa mwaka 1945. Inaweza kusemwa, kuwa wapiga kura wa Uingereza hawakuwa na shukrani. Kwamba wapiga kura wa Uingereza hawakumpima Churchill kwa historia bali kwa yatakayokuja. Kuna cha kujifunza, maana, Afrika kiongozi ukihangaika ukawajengengea watu wako barabara na madaraja, kuna shukrani watakazokupa. Afrika Rais anaweza kuitwa ' Rais wa Barabara, au Rais wa Maji' kama katika muda wake wa uongozi ameweza kuwasaidia watu wake katika kujenga barabara na kuwaletea maji. Wapiga kura Afrika wana shukrani, tatizo ni baadhi ya viongozi Afrika kukosa shukrani.



      Ndio, nchi zetu kimsingi bado changa, na demokrasia zetu pia.

      Maana, nchi nyingi katika bara letu hili la Afrika mwaka huu na mwakani zitatimiza miaka hamsini tangu kupata uhuru wake kutoka kwa wakoloni. Ni nusu karne. Ni muda mrefu. Yamkini shingo zetu wanadamu ni ndefu, lakini maisha yetu ni mafupi sana. Ndio, muda wetu wa kuishi humu duniani ni mfupi sana. Na historia itabaki kuwa hakimu kwa tunayoyafanya sasa.
      Maana, wengi wetu tunaishi na kuziacha nchi zetu tulizozaliwa hata kabla hatujatimiza miaka 70 humu duniani. Lakini, nchi tulizozaliwa tunaziacha zikiwa na wanadamu wenzetu. Ni watoto wetu, ni wajukuu zetu. Na sisi Waafrika tumekuwa ni watu wabinafsi sana. Ni watu tunaoishi bila kufikiria sana ya kesho na kesho kutwa. Tunajiangalia sisi tu.
      Sehemu kubwa ya matatizo ya nchi zetu hizi yanatokana na ubinafsi huo. Na bahati mbaya kabisa, baadhi ya viongozi tuliowapa dhamana za uongozi ndio wenye kuongoza kwa matendo yenye kutanguliza maslahi yao binafsi. Katiba za nchi zetu ni kielelezo halisi cha ubinafsi huo. Maana, wakoloni walitengeneza katiba ili ziwasaidie katika kututawala. Katiba ya mkoloni ilikuwa na maana moja kubwa; kuonyesha namna ya kuwatawala watu wa nchi iliyo mikononi mwa wakoloni. Na nchi zetu nyingi zimerithi misingi ya katiba hizo za kikoloni. Katiba nyingi za nchi za Kiafrika zinaonyesha namna ambavyo Waafrika wachache walio katika mamlaka ya Kiserikali watakavyowatawala “ Waafrika” wenzao! Na hilo ndilo ‘Neno La Leo’. Fikiri kwa bidii.
      Maggid,
      Kinondoni Biafra.
      HEADING yako inazungumzia viongozi lakini ndani ya habari yako unazungumzia waafrika kwa ujumla, na mimi nitawaongelea Binadamu kwa ujumla wao
      ubinafsi ni Hulka ya Binadamu haijalishi rangi wala kabila
      wazungu wa Zimbabwe walikuwa wabinafsi kwa kuchukua Ardhi kubwa yenye rutuba na kuwapa Waafrica ardhi ya mawe, Makaburu Africa kusini Waliwabagua waafrica kwa ubinafsi wao na kujifanya kuwa wao ni bora kuliko wengine, Zanzibar hapo Waarabu walikuwa wanawabagua Waafrika kwa ubinafsi wao wa kijiona wao ni bora kuliko Waafrica
      ubinafsi ni hulka ya binadamu na hata maandiko matakatifu yanazungumzia hilo la "kumpenda jirani yako kama unavyojipenda wewe mwenyewe", hapa ina maana ya kutoa ubinafsi na umimi, SIAMINI KWAMBA NA WEWE (MAGGID) UMEKUWA BRAIN WASHED KIASI CHA KUJIDHARAU MWAFRIKA KWA KIASI HICHO

    5. #4
      maggid's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd December 2006
      Posts : 776
      Rep Power : 800
      Likes Received
      654
      Likes Given
      33

      Default Re: Neno La Leo: Afrika Viongozi Hawana Shukrani!

      Quote By Kituko
      HEADING yako inazungumzia viongozi lakini ndani ya habari yako unazungumzia waafrika kwa ujumla, na mimi nitawaongelea Binadamu kwa ujumla wao
      ubinafsi ni Hulka ya Binadamu haijalishi rangi wala kabila
      wazungu wa Zimbabwe walikuwa wabinafsi kwa kuchukua Ardhi kubwa yenye rutuba na kuwapa Waafrica ardhi ya mawe, Makaburu Africa kusini Waliwabagua waafrica kwa ubinafsi wao na kujifanya kuwa wao ni bora kuliko wengine, Zanzibar hapo Waarabu walikuwa wanawabagua Waafrika kwa ubinafsi wao wa kijiona wao ni bora kuliko Waafrica
      ubinafsi ni hulka ya binadamu na hata maandiko matakatifu yanazungumzia hilo la "kumpenda jirani yako kama unavyojipenda wewe mwenyewe", hapa ina maana ya kutoa ubinafsi na umimi, SIAMINI KWAMBA NA WEWE (MAGGID) UMEKUWA BRAIN WASHED KIASI CHA KUJIDHARAU MWAFRIKA KWA KIASI HICHO
      Ndugu zangu,
      Kichuguu na Kituko ( Na majina yenu nayo ni ya vituko!)

      Neno huzaa neno, yakawa maneno, na ndio maana ya ' Neno la Leo'. Msihangaike na heading, ni kichwa tu, yasemeni yaliyo mioyoni mwenu!

    6. #5
      Kituko's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th January 2009
      Posts : 3,716
      Rep Power : 1288
      Likes Received
      497
      Likes Given
      175

      Default Re: Neno La Leo: Afrika Viongozi Hawana Shukrani!

      Quote By maggid
      Ndugu zangu,
      Kichuguu na Kituko ( Na majina yenu nayo ni ya vituko!)

      Neno huzaa neno, yakawa maneno, na ndio maana ya ' Neno la Leo'. Msihangaike na heading, ni kichwa tu, yasemeni yaliyo mioyoni mwenu!
      HEADING uliYoandika, haiendani na ulichoandika, UBINAFSI NI HULKA YA BINADAMU WOTE period

    7. RukaaJuu Final

    8. #6
      Kaa la Moto's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th April 2008
      Location : Bristol
      Posts : 6,857
      Rep Power : 1951
      Likes Received
      435
      Likes Given
      4283

      Default Re: Neno La Leo: Afrika Viongozi Hawana Shukrani!

      Maggid,
      Ni kweli sio rahisi mtu kuelewa nini hasa ni mada katika tahariri yako. Para ya kwanza unazungumzia shukrani za wapiga kura hata hivyo humo umechanganya mambo nadriki kuita ovyo ovyo. Na nikupinge tu kuwa sijawahi kusikia rais anayeitwa rais wa barabara, au madaraja. Nitajie mmoja kama mfano. Hizo ni ideas zako tu na una sababu. Lakini pia si kweli kwamba mtu akifanya mema watu hawana shukrani. Huo ni uongo na narudia ni uongo.

      Sasa ngoja tugeukie upande wa pili. Ubinafsi ni kitendo kinachotokana na ukosefu wa upendo tu.

      Mtu asiye na upendo kwa wengine siku zote lazima ataishia kuwa mbinafsi. Lakini si kwamba waafrika wote hatuna upendo kwa wengine. Hapana. Tuna viongozi wetu waliozungukwa na watu wasio na upendo na hivyo kuwaambukiza hali hiyo ambayo si njema.

      Mwenye upendo hujali wenzie. Uumia pamoja nao. Upata uchungu pamoja nao. Ulia nao. Uwapa kipaumbele wengine. Hana visasi kwa mahasimu wake. Huyo ndiye mwenye upendo. Na kwa kuwa ni kitu cha tunu wasicho nacho baadhi ya viongozi wetu wa kiafrika ndio sbabu tumefikia hapa tulipo.

      Waafrika wengi tumejawa na upendo na ndio sababu tunaonewa vya kutosha na watawala na tumewavumilia tu.
      wakati Cuf wanataka kuchukua nchi mwaka 2000 CCM walikuja na single ya kusema Cuf ni waislamu na kwa sasa wanadai sisi Chadema ni chama cha wakristo sasa CCM nacho ni cha watu gani? Watu wakajibu mashetaaaaaniiiiii.!---Wana Kigoma.

      ....Pamoja na kansa ya uongozi wa CCM watu wataendelea kukichagua,au watu wanaweza wakachoka na kusema potelea mbali wakachagua chama KINGINE....Julius. Kambarage. NYERERE"

    Similar Topics

    1. Neno La Leo: Afrika Kuku Hachimbiwi Kaburi!
      By maggid in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 1
      Last Post: 3rd March 2011, 21:24
    2. Replies: 2
      Last Post: 29th January 2011, 07:47
    3. Viongozi wanajeshi huwa hawana mafanikio kisiasa
      By Mzalendo Mkuu in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 4
      Last Post: 3rd January 2011, 14:08
    4. Neno La Leo: Viongozi Afrika Hawana Shukrani!
      By maggid in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 0
      Last Post: 12th August 2010, 13:42
    5. NENO LA SHUKRANI WA WANA Jfs WOTE - (MSIBA WA MAMA YANGU MZAZI)
      By tete'a'tete in forum Matangazo madogo
      Replies: 12
      Last Post: 11th April 2010, 12:09

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...