Wadau, hivi karibuni kinara wa utabiri wa nyota nchini Sheikh Yahya Hussein alitoboa siri kuwa kuanguka jukwaani kwa Kikwete wakati wa uzinduzi wa KAmpeni za Urais ni kwa sababu ya kutumiwa Majini na mahasimu wake katika kinyang'anyiro cha kugombea Urais! KAtika kauli hiyo, Sheikh Yahya alibainisha kuwa sasa anatoa ulinzi rasmi wa Kimapepo kwa Kikwete kauli ambayo imechukuliwa kwa mifazamo tofauti.
Bahati mbaya hata Kiwete mwenyewe amekaa kimya juu ya kauli hiyo ya Ulinzi wa Majini anaopewa na Sheikh Yahya na sisi Watanzania tunashindwa kujua kuwa ameukubali ulinzi huo au la. BAhati mbaya hata Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rai kwa sasa ni kama iko likizo au kwenye Kampeni na kusahau wajibu wake wa kutolea ufafanuzi kauli tata zinazolenga kumdhalilisha Kikwete, kuidhalilisha Serikali, kuidhalilisha Ikulu na Watanzania zilizotolewa na Mpiga ramli huyo ajiitaye Sheikh!
Jana kwenye kamapeni za Kikwete na CCM pale Uwanaj wa Sheikh Amri Abeid Arusha, mpiga kura mmoja nilimsikia akisema amekuja kusikiliza tamko la Kikwete kukanusha kupewa Ulinzi wa Kipepo na Sheikh Yahya ili ajue kama ampe kura yake au la. Bahati mbaya sikukaa hadi mwisho maana Mh. Kikwete alianza kuhutubia saa 12 jioni.
Nahofia sana, tena sana iwapo atachaguliwa kuwa Rais huku Ikulu na yeye 'Rais' akilindwa na Majini. Nina hofu kubwa Ikulu kugeuzwa kuwa sehemu ya Waganga wa kienyeji na Wachawi, na Wapuiga Ramli. Huku kuakuwa ni kuidhoofisha Ikulu na nchi kwa ujumla. Tafadhali sana Kikwete au Kurugenzi ya MAwasiliano ya Ikulu itoe tamko ii wengine tufanye maamuzi ya uchaguzi wa Rais hata kwa kigezo hicho.

Reply With Quote

Follow Us Here