Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Orodha ya ahadi za Kikwete kwa wananchi 2010-2015

    Report Post
    Page 1 of 34 12311 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 668
    1. #1
      Bramo's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 21st October 2009
      Location : Mtimbwani
      Posts : 1,841
      Rep Power : 9093
      Likes Received
      498
      Likes Given
      330

      Default Orodha ya ahadi za Kikwete kwa wananchi 2010-2015

      AHADI - ALIITOA AKIWA WAPI...

      1. Kujenga reli mpya kutoka Dar es Salaam mpaka mikoa ya Kanda ya ziwa - Nzega, Tabora
      2. Mkoa wa Tanga kuwa Jiji la Viwanda - Tanga mjini
      3. Tabora kutumia maji ya Ziwa Victoria - Igunga
      4. Kulipa madeni ya chama cha Ushirika mkoa wa Shinyanga (SHIRECU) - Shinyanga
      5. Kumaliza migogoro ya Ardhi nchini - Dodoma
      6. Wakulima kuacha kutumia jembe la mkono - Dodoma mjini
      7. Kuwapatia trekta wakulima - Kata ya Mrijo, Dodoma
      8. Wananchi kutoondolewa kwenye Ranchi ya Misenyi - Kagera
      9. Kujenga Uwanja wa Ndege Misenyi - Kagera
      10. Kupanua Uwanja wa Ndege Bukoba - Bukoba Mjini
      11. Kujenga uwanja wa ndege mkubwa Kigoma - Kigoma Mjini
      12. Mtukula kupatiwa umeme kutoka Uganda - Kagera
      13. Mikoa ya Kagera, Kigoma, Lindi, Rukwa na Ruvuma kuunganishwa katika gridi ya taifa ya umeme - Kagera
      14. Kuimarisha Takukuru kwa miaka mitatu - Kagera
      15. Hukumu kwa waliopatikana na hati ya kuua albino - Mbeya
      16. Kununua meli kubwa kuliko MV Bukoba - Kagera
      17. Kuanzisha benki ndogondogo kwa ajili ya wajasiriamali
      18. Serikali kuvisaidia vyama vya ushirika - Mwanza
      19. Kuimarisha usalama Ziwa Victoria na Ziwa Tanganyika kwa kupeleka kikosi maalum chenye vifaa kupambana na wahalifu - Mwanza
      20. Wilaya ya Geita kuwa hadhi ya mkoa Januari mwakani - Geita
      21. Kulinda muungano kwa nguvu zote - Pemba
      22. Kuwajengea nyumba waathirika wa mafuriko Kilosa - Morogoro
      23. Kununua meli mpya kubwa Ziwa Nyasa - Mbeya mjini
      24. Kujenga bandari Kasanga – Rukwa
      25. Kumaliza tatizo la walimu miaka mitano ijayo - Songea
      26. Kufufua mgodi wa makaa ya mawe Kiwira - Mbeya
      27. Kuzuia hatari ya kisiwa cha Pangani kuzama - Tanga
      28. Kununua bajaji 400 kwa ajili ya kubeba wajawazito hasa vijijini - Iringa
      29. Kujenga barabara yenye kiwango cha lami kutoka Same mpaka Kisiwani – Kihurio na kuiunganisha na barabara kuu ya Moshi - Dar es salaam - Same mkoani Kilimanjaro
      30. Kumaliza tatizo la maji katika wilaya ya Same - Same Mjini
      31. Kuboresha barabara za Igunga - Tabora
      32. Kusambaza walimu 16,000 katika shule za sekondari zenye upungufu makubwa wa walimu - Kisesa Magu
      33. Kununua vyandarua viwili kwa kila kaya - Mbeya Mjini
      34. Kuzipandisha hadhi hospitali maalumu saba nchini kuwa za rufaa ili kuipunguzia mzigo Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MHN) - Hydom Manyara
      35. Kulinda amani nchini kwa kuzuia chokochoko za kidini, kikabila na kisiasa - Musoma
      36. Kulinda haki za walemavu - Makete
      37. Kujenga baabara ya Njombe - Makete kwa kiwango cha lami,urefu wa kilomita 109 - Iringa mjini
      38. Kujenga barabara Musoma – Mto wa Mbu Arusha - Arusha
      39. Kuanzisha jimbo la Ulyankulu- Shinyanga Mjini
      40. Kujenga barabara ya lami Manyoni-Kigoma – Kaliua,Tabora
      41. Kukarabati barabara ya Arusha Moshi - Arusha Mjini
      42. Kuboresha barabara ya Handeni, Kondoa, mpaka Singida - Dodoma
      43. Kuwafidia wanakijiji ng’ombe waliopotea wakati wa ukame mwaka 2009 - Longido
      44. Vijiji vyote vilivyoko kilomita 15 kutoka kwenye bomba kuu la mradi mkuu wa maji wa Ziwa Victoria - Shinyanga-Kahama kuunganishiwa maji - Shinyanga
      45. Tatizo la umeme kufikia kikomo Novemba mwaka huu mkoani Arusha – Arusha mjini
      46. Kukopesha wavuvi zana za kilimo - Busekera, Wilaya ya Musoma
      47. Kuwapatia maji wakazi wa Wilaya ya Longido - Longido
      48. Kujenga barabara ya lami kupitia pembezoni mwa Hifadhi ya Taifa ya Seregenti – Ngorongoro
      49. Utekelezaji wa mpango wa maendeleo ya kilimo kuwasaidia wafugaji kuweza kupata na kutunza mifugo yao vizuri - Mbulu mkoani Manyara
      50. Kusambaza maji nchi nzima - Babati vijijini
      51. Kusambaza umeme, utoaji wa huduma za afya, na uboreshaji wa kilimo cha umwagiliaji na utoaji ruzuku kwa wakulima. mwaka 2010-2015 - Babati vijijini
      52. Kuongeza mara tatu idadi ya wananchi wanaonufaika na ruzuku ya pembejeo za kilimo kwa mfumo wa vocha - Iringa
      53. Kuhakikisha Isimani inapata maji ya uhakika - Iringa
      54. Kuiwekea lami barabara inayokwenda katika Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, ambayo ndiyo hifadhi kubwa kuliko zote Tanzania - Iringa
      55. Kulinda usalama wa wananchi kwa ujumla ili kudumisha amani na sifa ya nchi -Ifunda
      56. Kutokomeza malaria 2015 - Bunda, mkoa wa Mara
      57. Kuwapa wanawake nafasi zaidi - Kilolo, Iringa
      58. Ahadi kuisadia Zanzibar kuendeleza miradi mbalimbali ya kijamii - Kibandamaiti Mjini Zanzibar
      59. Kuipandisha hadhi hospitali ya Mnazi Mmoja Zanzibar kuwa ya rufaa - Kibandamaiti mjini Zanzibar
      60. Kuisaidia Zanzibar kila panapohitajika msaada - Kibandamaiti
      61. Serikali kujenga upya bandari ya Mbambabay - Ruvuma
      62. Ununuzi wa Meli mpya yenye uwezo wa kubeba tani 400 - Mbambabay Ruvuma
      63. kufufua chama kikuu cha ushirika cha wakulima wa Mbinga (MBICU) – Ruvuma
      64. Ahadi Rais wa Marekani Barack Obama kuimwagia misaada Tanzania – Ruvuma
      65. Ahadi hakutakuwa na umwagaji wa damu baada ya uchaguzi-Dar es Salaam
      66. Mtwara kuwa mji wa Viwanda – Mtwara
      67. Ahadi ujenzi wa kwanda cha dawa ya kuua viluilui vya mbu - Kibaha
      68. Hospitali ya Tumbi kuwa ya mkoa - Kibaha
      69. Halmashauri ya manispaa ya Kibaha kutenga eneo maalumu la viwanda - Kibaha



      ---2005 Alikuja na Maisha bora kwa kila Mtanzania,hili halina ubishi lilikuwa ni changa la macho kwa Watanzania,Kama haitoshi akasema anawajua kwa majina wala rushwa,lakini hatuoni hata mmoja aliyemchukulia hatua===hii ni kutaka sifa na popularity.

      ---Juzi amekuja na mpya ya kumpatia kila mwanafunzi Computer ambayo iko connected kwa internet, it's high time now kwa watanzania kuhoji uwezo wa RAIS wetu,ni kwamba anafanya Wa Tanzania ni wapumbavu sana kiasi kwamba hawawezi ku reason kuwa hilo sual haliwezekani???

      Hata kwa wanafunzi tu wa vyuo vikuu hilo suala halitekelezeki leo anatuambia ataanza na shule za msingi,umeme ni tatizo..hivi jk anajua kuwa its only 10% ya wa Tanzania wana access na umeme na 0.05% ya watanzania ndo wanaweza kutuima computer na wana access na internet,hata kwa nchi ambazo zimeendelea kuzidi sisi hilo suala halipo,,yeye anataka kuhadaa Wa Tanzania aili aendelee kubaki madarakani!!!!!me nadhani pia JK na uwezo mdogo sana wa ku reason ndo maana hata hafikirii kuwa suala kama hilo watu wenye akili timamu hawawezi kusadiki,inahitaji mtu mwenye akili za mwenda wazimu kuamini ahadi kama hizo.

      ----WITO WANGU
      Nawaomba wana JF wooote..mu influence watu wenu wa karibu wasimchague JK na CCM yake,watatoa ahadi nyingi sana,watasema watajenga fly over,watasema watajenga majumba angani--->tuwapuuuze na ahadi zao hizo...tuwaulize kati ya zile walizoahidi 2005 ni ngapi wametekeleza mpaka tuwape ajira nyingine kwa miaka mitano!!!!!!

      Watakuja na gia ya kuwa wamejenga DOdoma University,tuwapuuze pia kwa sababbu kwanza ulikuwa ni ukumbi wa bunge wa zamani (chimwaga),halafu huo ni wajibu wake...tuipuuzie kete ya kipuuzi kama hii.
      SAY NO TO CCM-----SAY NO TO JK-----WANYIMENI KURA


    2. #2
      Bigirita's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th February 2007
      Location : Under a mango tree
      Posts : 11,353
      Rep Power : 3065
      Likes Received
      3110
      Likes Given
      4232

      Default Re: JK na ahadi zake za kisanii---!

      nimekusoma mwana
      * LOVE COMES NATURALLY; HATE IS TAUGHT.....by nngu007 wa JF

    3. #3
      IsayaMwita's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th March 2008
      Location : Tarime
      Posts : 1,049
      Rep Power : 875
      Likes Received
      82
      Likes Given
      6

      Default Re: JK na ahadi zake za kisanii---!

      Bramo,

      Mbona hutuambii tumchague nani?

      soma hii thread (je Dr. Slaa akitupa jalamba ushindi utakuwepo?)

    4. #4
      Bramo's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 21st October 2009
      Location : Mtimbwani
      Posts : 1,841
      Rep Power : 9093
      Likes Received
      498
      Likes Given
      330

      Default Re: JK na ahadi zake za kisanii---!

      Ngoja tusie CHADEMA watamsimamisha nani...ila nawaaasa na CCM na JK wake.
      Sio siri,chadema ndo mbadala wa CMM

    5. #5
      Mpeni sifa Yesu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd May 2010
      Location : Dar es Salaam
      Posts : 472
      Rep Power : 555
      Likes Received
      18
      Likes Given
      1

      Default Re: JK na ahadi zake za kisanii---!

      Hakuna lisilowezekana kwa Mungu, anaponya, anaokoa. kwa ushauri na maombi, tuwasiliane ([email protected]). karibu kwa Yesu.


    6. #6
      n'golofu's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 15th May 2010
      Posts : 7
      Rep Power : 463
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: JK na ahadi zake za kisanii---!

      nimekupata vizuri

    7. #7
      King'asti's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th November 2009
      Location : The Jungle
      Posts : 17,853
      Rep Power : 29102
      Likes Received
      12273
      Likes Given
      4933

      Default Re: JK na ahadi zake za kisanii---!

      Asubuhi nimemsikia Waziri wa Nishati na Madini clouds anajifagilia kuwa umeme utafika katika kila makao makuu ya wilaya Tz nzima (sijui alikuwa anatania..?) Hivi ilani ya uchaguzi si inatakiwa kumalizika kabla ya miaka 5 kwisha? Ama ndo yale ya kupimwa viatu mwaka huu, afu miaka mingine 5 ya kuviagiza, afu mingine mitano ya kuvigawanya... the story has no end!
      I can be changed by what happens to me. But I refuse to be reduced by it-Maya Angelou


    8. #8
      Ngambo Ngali's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th April 2009
      Posts : 2,593
      Rep Power : 1036
      Likes Received
      537
      Likes Given
      411

      Default Re: JK na ahadi zake za kisanii---!

      Japan's prime minister, Yukio Hatoyama, today said he would resign just eight months after he took office, after failing to honour election promises to bring sweeping change to domestic policy and fundamentally alter the country's relations with the US.
      The world's second biggest economy faces yet another period of uncertainty after Hatoyama, whose Democratic party won by a landslide last year, became Japan's fourth prime minister in as many years to step down after a year or less in power.
      In a further blow to the Democrats five weeks before upper house elections, Ichiro Ozawa, the architect of last year's election victory, will also step down amid a political funding scandal.
      "Since last year's elections, I tried to change politics so that the people of Japan would be the main characters," Hatoyama said in a nationally televised address to party members.
      Although he has had some success in shifting power from bureaucrats to politicians, Hatoyama conceded that he had failed to win public support for his administration's handling of the economy and, crucially, his recent decision on the fate of a US military base on the southern island of Okinawa.
      "That was mainly because of my failings," he said, his eyes filling with tears. "The public has refused to hear me."
      His fate was in effect sealed by his decision last week to renege on a campaign promise to move a US marine airbase off Okinawa – a move he hoped would demonstrate his determination to end Japan's subservience to Washington's foreign policy.
      In the end, US intransigence and the lack of a viable alternative site forced him to accept a 2006 agreement to move the base from its city centre location to an offshore site on the island's northern coast.
      His change of heart enraged politicians and residents on Okinawa, who accused him of betrayal, and sent his public support ratings below 17%, compared with over 70% when he took office last September.
      Hatoyama, 63, said the importance of maintaining a strong US alliance in the face of a rising China and instability on the Korean peninsula had forced him to cave in to Washington's demands.




      Wallahi, nadhani viongozi wetu watatambua madhara ya ahadi hewa za kampeni, mwenzao kacheki caona umaarufu umeshuku akaogopa kuandikwa vibaya kwenye historia, akaamua kuandikwa vizuri akaachia ngazi. Viongozi wetu wanangoja mpaka wananchi wawafukuze kazi ili wawe negative part of history.
      Injustice anywhere is a threat to justice everywhere.

    9. #9
      Malunde-Malundi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th January 2008
      Posts : 1,254
      Rep Power : 834
      Likes Received
      111
      Likes Given
      40

      Default Re: JK na ahadi zake za kisanii---!

      Ziwekeni AHADI ZAKE ZOTE TUZIPE ALAMA ILI HATIMAYE TUPATE MAJIBU YA UHAKIKA YA MATOKEO YAKE ALIYOPATA;

      NAANZA NA MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA-AMEPATA D(19)-FAIL;SABABU KILA MMOJA ANA YA KWAKE

    10. #10
      Augustine Moshi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd April 2006
      Posts : 1,832
      Rep Power : 1853
      Likes Received
      184
      Likes Given
      85

      Default Re: JK na ahadi zake za kisanii---!

      Rais Mkapa aliwahi kusema kitu kikubwa kinachohatarisha usalama wa nchi za Kiafrika ni kuweko kwa vikundi vinavyohodhi madaraka. Kikundi kilichoko madarakani Tanzania sasa ni kile kile ambacho kimetutawala tangu tupate Uhuru miaka 50 iliyopita. Na bado kinang’ang'ania madaraka.

      JK aliwahadaa wana UDSM kwamba ataboresha uenjinia. Kutokana na kushuka kwa uwezo wa kufikiri hapo Kilimani (walimshangilia sana), wasomi wetu hawakutambua kwamba hizo ahadi hazikuwa funded.

      JK aliahidi kukamilisha haraka barabara ya Mtwara hadi Mwanza. Hiyo barabara ingemalizika mwaka 2007 kama JK hangekuwa Rais.

      JK aliahidi kumaliza kabisa shida ya maji Dar es Salaam. Aliahidi kumaliza shida ya umeme Tanzania. Aliahidi kumaliza upungufu wa waalimu. Maneno matupu.

      Thanks to 50 years of misrule by TANU and CCM, Tanzania is now the economic backwater of East Africa. If we elect the same people, we will get the same result.

      It is 100% against our national interest to return CCM to power.
      Last edited by Augustine Moshi; 5th June 2010 at 02:21.
      Adili and muchetz like this.

    11. #11
      taffu69's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th February 2007
      Posts : 1,325
      Rep Power : 895
      Likes Received
      262
      Likes Given
      196

      Default Re: JK na ahadi zake za kisanii---!

      Quote By Mpeni sifa Yesu View Post
      Hiyo slide show inatia uchungu sana, hiyo ni sehemu tu ya mateso wanayopata akina mama wa Tanzania na wananchi wengine kwa ujumla. Inauma sana Serikali inapoyafumbia macho matatizo ya msingi yanayowakabili wananchi wake kwa kisingizio cha ukosefu wa fedha lakini fedha kwa ajili ya safari za nje za rais pamoja na wapambe wake, kununua magari ya kifahari, kutuma mawaziri mikoani kwa safari ambazo hazina tija yote hayo hayakosi fedha za kugharamia. Ni aibu rais wa nchi kutamka hadharani kuwa kila mwanafunzi wa primary school atapatiwa computer ilhal mwanafunzi huyo hana jengo la kujisetiri wakati wa mvua ama jua achilia mbali dawati la kukalia.

    12. #12
      mpuguso's Avatar
      Member Array
      Join Date : 1st October 2009
      Posts : 47
      Rep Power : 503
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default Re: JK na ahadi zake za kisanii---!

      Za kuambiwa changanya na zako!!!!!!!!! ahahahahaahah, Mbaiwayu hiyoooo.

      Najaribu kufuatilia nicknames za viongozi wetu wastaafu

      mwalimu aliitwa Mchonga meno
      Mzee mwinyi aliitwa Ruksa
      Mkapa aliitwa ukapa
      Mzee Jakaya na guess ataitwa Mbaiwayu!

      ahaha its fun!

    13. #13
      Ngambo Ngali's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th April 2009
      Posts : 2,593
      Rep Power : 1036
      Likes Received
      537
      Likes Given
      411

      Default Re: JK na ahadi zake za kisanii---!

      Quote By Malunde-Malundi View Post
      Ziwekeni AHADI ZAKE ZOTE TUZIPE ALAMA ILI HATIMAYE TUPATE MAJIBU YA UHAKIKA YA MATOKEO YAKE ALIYOPATA;

      NAANZA NA MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA-AMEPATA D(19)-FAIL;SABABU KILA MMOJA ANA YA KWAKE
      Ajira millioni moja ziko wapi?
      Injustice anywhere is a threat to justice everywhere.

    14. #14
      Augustine Moshi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd April 2006
      Posts : 1,832
      Rep Power : 1853
      Likes Received
      184
      Likes Given
      85

      Default Re: JK na ahadi zake za kisanii---!

      Aliahidi, kwenye bajeti ya 2009 / 2010, kwamba angetumia shilingi trilioni 1.1 kwenye Wizara ya Elimu na Ufundi. Si kweli.

      Aliahidi angeshitaki gazeti moja la Uingereza lililoandika kwamba wakati wa kampeni za 2005, Rostam Aziz alikabidhiwa $20 mil. na Iran kwa ajili ya kampeni za Kikwete. Mbona hajafanya hivyo hadi leo?


    15. #15
      Rufiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th June 2006
      Posts : 1,611
      Rep Power : 988
      Likes Received
      324
      Likes Given
      59

      Default Re: JK na ahadi zake za kisanii---!

      Quote By Mpeni sifa Yesu View Post

      Hii inasikitisha sana , nashindwa kuelewa hawa viongozi wetu wanawezaje kupata usingizi huku mamilioni ya wananchi wakinyanyasika. Hizo slide zimeniliza....

    16. #16
      Bigirita's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th February 2007
      Location : Under a mango tree
      Posts : 11,353
      Rep Power : 3065
      Likes Received
      3110
      Likes Given
      4232

      Default Ni sahihi JK kutumia mipango ya serikali kama ahadi za CCM?

      Hili linanitatiza sana, binafsi nafikiri sio sahihi kabisa kwa mgombea urais kutumia mipango ya serilkali kama ahadi za chama chake.

      Kwa mfano, kusema, ....tumeshaanza kufanya uchambuzi yakinifu wa barabara X na tutaanza kkuijenga mwakani.........this is wrong in my opinion.

      Mnasemaje wakuu??
      NYAMKANG'ILI likes this.
      * LOVE COMES NATURALLY; HATE IS TAUGHT.....by nngu007 wa JF

    17. #17
      Kituko's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th January 2009
      Posts : 3,731
      Rep Power : 1295
      Likes Received
      512
      Likes Given
      178

      Default Re: Ni sahihi JK kutumia mipango ya serikali kama ahadi za CCM?

      Quote By Bigirita View Post
      Hili linanitatiza sana, binafsi nafikiri sio sahihi kabisa kwa mgombea urais kutumia mipango ya serilkali kama ahadi za chama chake.

      Kwa mfano, kusema, ....tumeshaanza kufanya uchambuzi yakinifu wa barabara X na tutaanza kkuijenga mwakani.........this is wrong in my opinion.

      Mnasemaje wakuu??
      Tatizo kubwa lipo kwenye katiba yetu, ilikuwa inapasa wakati huu wa kampeni (Mwezi mmoja) 'kipindi cha mpito' nchi iwe chini ya jaji mkuu, ambaye yeye sio mtu wa kugombea kura kama raisi au Spika (Mbunge), sasa hao wote wanaosimamia sheria ni wateule wa Raisi na mpaka sasa Jk anapompa masharti mtu yoyote say TIDO, anampa kama raisi na sio kama Raia Mgombea uraisi,

      wakina Slaa wanachangishana fedha za Kampeni, lakini Jk anatumia fedha za serikali kufanya kampeni zake, wale wanausalama waliokuwa wanamzoazoa pale jangwani siku ya uzindizi wa kampeni walikuwa pale kumlinda raisi na wala sio Mgombea Urais na ni kwa gharama zako wewe mlalahoi,

      kuna mapungufu mengi mno, kiasi watu wanashindwa kutofautisha mambo ya CCM na ya Kiserikali

    18. #18
      Bigirita's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th February 2007
      Location : Under a mango tree
      Posts : 11,353
      Rep Power : 3065
      Likes Received
      3110
      Likes Given
      4232

      Default Re: Ni sahihi JK kutumia mipango ya serikali kama ahadi za CCM?

      Quote By Kituko View Post
      Tatizo kubwa lipo kwenye katiba yetu, ilikuwa inapasa wakati huu wa kampeni (Mwezi mmoja) 'kipindi cha mpito' nchi iwe chini ya jaji mkuu, ambaye yeye sio mtu wa kugombea kura kama raisi au Spika (Mbunge), sasa hao wote wanaosimamia sheria ni wateule wa Raisi na mpaka sasa Jk anapompa masharti mtu yoyote say TIDO, anampa kama raisi na sio kama Raia Mgombea uraisi,

      wakina Slaa wanachangishana fedha za Kampeni, lakini Jk anatumia fedha za serikali kufanya kampeni zake, wale wanausalama waliokuwa wanamzoazoa pale jangwani siku ya uzindizi wa kampeni walikuwa pale kumlinda raisi na wala sio Mgombea Urais na ni kwa gharama zako wewe mlalahoi,

      kuna mapungufu mengi mno, kiasi watu wanashindwa kutofautisha mambo ya CCM na ya Kiserikali
      mkuu ndo maana nafikiri ni sahihi kabisa kubadilisha this F* katiba. Slaa is right here. siku 100 za mabadiliko makubwa.

      we need this change.
      * LOVE COMES NATURALLY; HATE IS TAUGHT.....by nngu007 wa JF

    19. #19
      Kituko's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th January 2009
      Posts : 3,731
      Rep Power : 1295
      Likes Received
      512
      Likes Given
      178

      Default Re: Ni sahihi JK kutumia mipango ya serikali kama ahadi za CCM?

      Quote By Bigirita View Post
      mkuu ndo maana nafikiri ni sahihi kabisa kubadilisha this F* katiba. Slaa is right here. siku 100 za mabadiliko makubwa.

      we need this change.
      HAYO MABADILIKO ANAYOYASEMA SLAA WALA HAYAHITAJI FEDHA, KILA MTU AKITIMIZA WAJIBU WAKE IPASAVYO, SIKU 100 (1st Quarter) ya mwaka kila kitu kitakuwa kwenye mstari, ni uwajibikaji tu

    20. #20
      Quadrat Jr's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th July 2010
      Location : Barazani kwangu.
      Posts : 1,194
      Rep Power : 762
      Likes Received
      216
      Likes Given
      211

      Default Re: Ni sahihi JK kutumia mipango ya serikali kama ahadi za CCM?

      Quote By Bigirita View Post
      Hili linanitatiza sana, binafsi nafikiri sio sahihi kabisa kwa mgombea urais kutumia mipango ya serilkali kama ahadi za chama chake.

      Kwa mfano, kusema, ....tumeshaanza kufanya uchambuzi yakinifu wa barabara X na tutaanza kkuijenga mwakani.........this is wrong in my opinion.

      Mnasemaje wakuu??
      Si hivyo tu hata ile tabia yake ya kutoa maagizo(kama rais) kwenye jukwaa la kampeni kama alivyofanya mkoani kagera kuigawa ranchi kwa wananchi,ni ukiukwaji wa taratibu!

    Page 1 of 34 12311 ... LastLast

    Similar Topics

    1. Safari za nje za Mhe. Rais Kikwete 2010 - 2015
      By MWANASHERIA in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 462
      Last Post: 29th May 2013, 17:40
    2. Replies: 11
      Last Post: 7th September 2010, 10:17
    3. Orodha ya Majina ya Wabunge Vijana 2010
      By Agwambo in forum Tanzania 2010-2015
      Replies: 42
      Last Post: 11th July 2009, 12:02

    User Tag List

    Tags for this Topic

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...