Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Viongozi wa CCJ Wajiunga Rasmi na CHADEMA

    Report Post
    Page 1 of 7 123 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 128
    1. #1
      Regia Mtema's Avatar
      R I P Array
      Join Date : 21st November 2009
      Posts : 2,988
      Rep Power : 1112
      Likes Received
      763
      Likes Given
      397

      Default Viongozi wa CCJ Wajiunga Rasmi na CHADEMA

      Dakika chache zilizopita Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Freeman Mbowe amewapokea waliokuwa viongozi wa CCJ, Richard Kiyabo aliyekuwa Mwenyekiti, Dickson Ng’hily aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu CCJ Bara na Fred Mpendazoe aliyekuwa Msemaji Mkuu wa CCJ Taifa.

      Viongozi hawa wamejinga rasmi na CHADEMA na kukabidhiwa kadi na Mbowe mbele ya Waandishi wa Habari.

      Pamoja na kujiunga na CHADEMA Viongozi hawa pia wametoa tamko rasmi la kwanini wamejiunga na chama hiki,Find Attachment hapo chini. Vile Vile Viongozi hawa wametangaza nia ya kugombea Ubunge kupitia CHADEMA kama ifuatavyo;


      Dickson Ng’hily -Kugombea Jimbo la Temeke
      Richard Kyabo-Kugombea Jimbo la Bukene
      Fred Mpendazoe-Kugombea Jimbo la Segerea

      Matukio ya picha nadhani Waandishi wa Habari watarusha mambo yakiwa tayari

      Binafsi nimefurahishwa sana na uamuzi wa Viongozi hawa na furaha yangu itakamilika wakishinda Ubunge kwenye Majimbo yao.

      Wale wanaJF ambao ni wanachama wa CCJ wanashauriwa kujinga mapema na CCJ.

      Wenu katika Demokrasia na Maendeleo
      Gender Sensitive
      Attached Files
      Kilombero For Change(K4C)-Mfuko wa Maendeleo Kilombero

    2. Miaka 50

    3. #2
      Nemesis's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th February 2008
      Posts : 2,656
      Rep Power : 1517
      Likes Received
      32
      Likes Given
      91

      Default Re: Viongozi wa CCJ Wajiunga Rasmi na CHADEMA Leo

      Find Attachment hapo chini.
      Asante kwa taarifa nzuri, lakini sijaona hii attachment.


    4. #3
      Ntemi Kazwile's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th May 2010
      Location : Bongo salidalam
      Posts : 1,873
      Rep Power : 833
      Likes Received
      135
      Likes Given
      453

      Default Re: Viongozi wa CCJ Wajiunga Rasmi na CHADEMA Leo

      Hakuna attachment mkuu tunaomba uirushe.

      Tunawakaribisha... Mzee wa Chadema mimi nilijiunga Chadema kwa sms lakini mpaka na nikaahidiwa kuwa ningetafutwa na viongozi wa eneo ninalokaa lakini mpaka leo. takribani mwaka umepita sijawaona au kusikia lolote kutoka Chadema.. kulikoni???
      “If people are not laughing at your dreams at least once a week, you are aiming too low.” Robin Sharma.

    5. #4
      Ndachuwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th March 2006
      Location : ARUSHA
      Posts : 2,666
      Rep Power : 1214
      Likes Received
      545
      Likes Given
      419

      Default Re: Viongozi wa CCJ Wajiunga Rasmi na CHADEMA Leo

      Waliokuwa wanachama au wafuasi wao wameachwa wapi?

    6. #5
      Nemesis's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th February 2008
      Posts : 2,656
      Rep Power : 1517
      Likes Received
      32
      Likes Given
      91

      Default Re: Viongozi wa CCJ Wajiunga Rasmi na CHADEMA Leo

      Quote By Vincent Augustino
      Waliokuwa wanachama au wafuasi wao wameachwa wapi?
      Nao watajiunga vyama vingine vya siasa including CCM kwa wale watakao kata tamaa na upinzani.



    7. #6
      Watu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th May 2008
      Location : Dar es Salaam
      Posts : 1,046
      Rep Power : 772
      Likes Received
      232
      Likes Given
      134

      Default Re: Viongozi wa CCJ Wajiunga Rasmi na CHADEMA Leo

      Quote By Vincent Augustino
      Waliokuwa wanachama au wafuasi wao wameachwa wapi?

      by default wanachama=chadema si ndio waipiga debe/kura wao

    8. #7
      Kamaka's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th June 2010
      Location : Gallaxy
      Posts : 528
      Rep Power : 560
      Likes Received
      24
      Likes Given
      78

      Default Re: Viongozi wa CCJ Wajiunga Rasmi na CHADEMA Leo

      Ingependeza kwa wale wanchanma nao kujiunga ili kuleta upinzani wa kweli
      Aluta continua

    9. #8
      Lyangalo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th September 2009
      Location : Kintinku-Dodoma
      Posts : 613
      Rep Power : 631
      Likes Received
      61
      Likes Given
      14

      Default Re: Viongozi wa CCJ Wajiunga Rasmi na CHADEMA Leo

      habari njema kwa Chadema ila hakuna attachment, labda unatudanganya?
      A MAN'S BEST OR WORST CHOICE IN LIFE IS HIS WIFE

    10. #9
      muheza2007's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 19th March 2010
      Posts : 126
      Rep Power : 492
      Likes Received
      11
      Likes Given
      4

      Default Re: Viongozi wa CCJ Wajiunga Rasmi na CHADEMA Leo

      Kwahiyo mzee Mwanakijiji naye kajiunga na CHADEMA?

    11. #10
      TIMING's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th April 2008
      Location : Roaming...
      Posts : 20,103
      Rep Power : 12256
      Likes Received
      6016
      Likes Given
      6866

      Default Re: Viongozi wa CCJ Wajiunga Rasmi na CHADEMA Leo

      Quote By Gender Sensitive
      Dakika chache zilizopita Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Freeman Mbowe amewapokea waliokuwa viongozi wa CCJ,Richard Kyabo aliyekuwa Mwenyekiti,Dickson Ng’hily aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu CCJ Bara na Fred Mpendazoe aliyekuwa Msemaji Mkuu wa CCJ Taifa .Viongozi hawa wamejinga rasmi na CHADEMA na kukabidhiwa kadi na Mbowe mbele ya Waandishi wa Habari. Pamoja na kujiunga na CHADEMA Viongozi hawa pia wametoa tamko rasmi la kwanini wamejiunga na chama hiki,Find Attachment hapo chini. Vile Vile Viongozi hawa wametangaza nia ya kugombea Ubunge kupitia CHADEMA kama ifuatavyo;
      Dickson Ng’hily -Kugombea Jimbo la Temeke
      Richard Kyabo-Kugombea Jimbo la Bukene
      Fred Mpendazoe-Kugombea Jimbo la Segerea

      Matukio ya picha nadhani Waandishi wa Habari watarusha mambo yakiwa tayari

      Binafsi nimefurahishwa sana na uamuzi wa Viongozi hawa na furaha yangu itakamilika wakishinda Ubunge kwenye Majimbo yao.

      Wale wanaJF ambao ni wanachama wa CCJ wanashauriwa kujinga mapema na CCJ.

      Wenu katika Demokrasia na Maendeleo
      Gender Sensitive
      Wow.... GS, My friend;

      I am proud of CCJ leaders na pia i am very proud of CHADEMA for accepting this change. Hii ndiyo ndoto yangu kwenye upinzani, fighting the common enemy.

      Najua MMM naye atakua hepi na kusema ukweli huu ni uamuzi wa busara sana... UNGANENI NA KUWA NA SAUTI ZAIDI BUNGENI, ITS ONLY THEN NDIPO DEMOKRASIA YA KWELI ITAPATIKANA

      BTW, HEBU CORRECT HIZO SPELLING, HAO NI OFFICE MATES KWA SASA

      AT LIST THIS WILL ALSO SWING THE MEDIA ATTENTION TO UPINZANI
      .....Ana sifa zote, nzuri na mbaya!!!

    12. #11
      Ndachuwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th March 2006
      Location : ARUSHA
      Posts : 2,666
      Rep Power : 1214
      Likes Received
      545
      Likes Given
      419

      Default Re: Viongozi wa CCJ Wajiunga Rasmi na CHADEMA Leo

      Quote By Nemesis
      Nao watajiunga vyama vingine vya siasa including CCM kwa wale watakao kata tamaa na upinzani.
      Huu nao ni ufisadi, kwanini kiongozi mzima ukajiunge na kundi ambalo wewe una imani tofauti na wao? Hapa linakuja jibu kuwa wote wanaojiita upinzani ni vikundi vya kuganga njaa tuu, ramani ikiwa mbaya wanakimbilia kwingine. Mimi naamini katika mikono na miguu yangu

    13. #12
      S. S. Phares's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2006
      Posts : 3,042
      Rep Power : 1247
      Likes Received
      16
      Likes Given
      110

      Default Re: Viongozi wa CCJ Wajiunga Rasmi na CHADEMA Leo

      Hahaaa hahahaaaaaa ninachoweza kusema kwa sasa ni "Kidumu Chama Cha Mapinduzi".

    14. #13
      kipipili's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th July 2009
      Posts : 1,279
      Rep Power : 755
      Likes Received
      59
      Likes Given
      12

      Default Re: Viongozi wa CCJ Wajiunga Rasmi na CHADEMA Leo

      Quote By Ntemi Kazwile
      Hakuna attachment mkuu tunaomba uirushe.

      Tunawakaribisha... Mzee wa Chadema mimi nilijiunga Chadema kwa sms lakini mpaka na nikaahidiwa kuwa ningetafutwa na viongozi wa eneo ninalokaa lakini mpaka leo. takribani mwaka umepita sijawaona au kusikia lolote kutoka Chadema.. kulikoni???
      Mkuu Ntemi mfumo wa kusajili online bado haujatengemaa, kwani kuna masuala ambayo yanakuhitaji uwepo wako physically kama kulipia kadi na kusubmit picha, hivyo ushauri wangu ni kwako kufika katika ofisi ya chadema iliyo karibu nawe na ujisajiri. Kama uko Dar unaweza fika makao makuu pale kinondoni mtaa wa ufipa. Asante

    15. #14
      Dark City's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th October 2008
      Location : Roaming
      Posts : 11,583
      Rep Power : 23558
      Likes Received
      6999
      Likes Given
      11355

      Default Re: Viongozi wa CCJ Wajiunga Rasmi na CHADEMA Leo

      Ngoja basi Bunge livunjwe ili tuone na wale vigogo wao kama watajiunga nao!
      "WE ALWAYS DON'T CHANGE UNTIL THE COST OF STAYING THE SAME EXCEEDS THE COST OF CHANGE....LOOKING BEYOND THE 31 OKTOBA 2010 LANDMARK"

      Retired Maj Gen DC (1947)...[email protected]

    16. #15
      Nemesis's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th February 2008
      Posts : 2,656
      Rep Power : 1517
      Likes Received
      32
      Likes Given
      91

      Default Re: Viongozi wa CCJ Wajiunga Rasmi na CHADEMA Leo

      Quote By Vincent Augustino
      Waliokuwa wanachama au wafuasi wao wameachwa wapi?
      swali hili nililijibu hivi
      Nao watajiunga vyama vingine vya siasa including CCM kwa wale watakao kata tamaa na upinzani.
      sasa tena unaongelea viongozi!
      Huu nao ni ufisadi, kwanini kiongozi mzima ukajiunge na kundi ambalo wewe una imani tofauti na wao? Hapa linakuja jibu kuwa wote wanaojiita upinzani ni vikundi vya kuganga njaa tuu, ramani ikiwa mbaya wanakimbilia kwingine. Mimi naamini katika mikono na miguu yangu
      Labda sijakuelewa. Lakini ni dhahiri kuwa kuhama chama cha siasa n kujiunga na chama kingine ni ruksa na haki ya kila mtu. Na hiyo ndiyo demokrasia vinginevyo watu wasingehama vyama tawala kujiunga na upinzani.


    17. #16
      Kyachakiche's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th February 2009
      Posts : 824
      Rep Power : 691
      Likes Received
      38
      Likes Given
      127

      Default Re: Viongozi wa CCJ Wajiunga Rasmi na CHADEMA Leo

      Namsubiri MZEE MWANAKIJIJI atoe tamko kwanza!

    18. #17
      edwinito's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 3rd December 2008
      Posts : 199
      Rep Power : 573
      Likes Received
      6
      Likes Given
      3

      Default Re: Viongozi wa CCJ Wajiunga Rasmi na CHADEMA Leo

      TAMKO LA VIONGOZI WA CHAMA CHA JAMII (CCJ) KUWATAKA
      WANACHAMA WA CCJ WAGOMBEE NAFASI ZA KUCHAGULIWA
      KATIKA UCHAGUZI MKUU UJAO KUPITIA CHADEMA
      UTANGULIZI
      Ndugu Viongozi, Wanahabari, Wanachama na Wananchi kwa ujumla.
      Tunayo furaha kubwa isiyo na kifani, kwa kuungana nanyi katika
      mkutano huu ambao unaandika historia mpya yenye kuleta mabadiliko
      ya kweli katika taifa letu la Tanzania. Historia ambayo itakumbukwa
      kizazi hata kizazi, historia itakayowafanya Watanzania wajivunie na
      kuifaidi nchi yao.
      Ndugu zangu kabla sijaeleza nini kimetuleta hapa, napenda
      kuwarudisha nyuma kidogo. January 18 mwaka huu sisi wananchi
      wazalendo tulikutana jijini Dar es Salaam kutekeleza wajibu wetu
      kikatiba wa kuunganisha mawazo yetu pamoja na kuunda chama cha
      siasa kwa jina la Chama Cha Jamii (CCJ).
      CCJ kilizingatia changamoto zote zinazoikabili nchi yetu tangu na
      baada ya uhuru na kilibeba matarajio ya wananchi wa leo na kesho,
      kikiwa na lengo kuu la kuleta mageuzi ya kitaifa ya kidemokrasia,
      kiuchumi, kijamii, na kisiasa kwa faida yetu sisi sote na vizazi vijavyo.
      USAJILI WA MUDA
      Mwezi huo huo CCJ ilipeleka maombi ya usajili wa muda katika ofisi ya
      Msajili wa Vyama vya Siasa nchini. Na baada ya urasimu wa hapa na
      pale, hatimaye Machi 3, 2010 CCJ ilipata cheti cha usajili wa muda. Hii
      ilikuwa ni hatua ya mwanzo kabisa ili kiweze kuanza shughuli za
      kutafuta wanachana na hatimaye kikitimiza masharti yaliyopo kwa
      mujibu wa Sheria ya Vyama vya Siasa ya 1992, kiweze kupewa usajili
      wa kudumu.
      Hata hivyo, toka mwanzo ofisi ya msajili wa vyama vya siasa nchini,
      imekuwa ikionyesha nia yake waziwazi ya kutotaka kukipa CCJ usajili
      wa kudumu hata kama kitatimiza masharti. Ndani ya siku si chini ya
      sabini (70), CCJ kilikamilisha masharti yote na kupeleka maombi ya
      usajili wa kudumu. Msajili kupitia vyombo vya habari kwa mara nyingine
      aliweka wazi nia yake ya kutotoa cheti cha usajili wa kudumu kwa CCJ.
      Ndugu wananchi, kutokana na shinikizo toka kwa watanzania wenye
      uchungu na nchi hii na wenye kutaka kuona mabadiliko, pia shinikizo
      toka kwa ofisi za kibalozi zilizopo nchini, chama cha wanasheria tawi la
      Arusha bila kusahau wanachama wa CCJ, hatimaye tarehe 3/5/2010
      msajili kwa shingo upande aliamua kufanya uhakiki wa wanachama wa
      CCJ kwa mikoa minne akianzia Dar es Salaam, Pwani, Morogoro na
      baadaye Mjini Magharibi.
      Ndugu zangu nyote ni mashahidi wa hujuma tulizofanyiwa kiasi cha
      kupelekea kusitishwa kwa zoezi zima la uhakiki. Na kwa kuwa nia ya
      msajili ilikuwa ni kuichafua CCJ, alitangaza kuwa CCJ-Dar ina
      wanachama 13 tu, na licha ya kuwa tulimwandikia barua ya kusitisha
      zoezi la uhakiki bado aliendelea na Pwani kisha kutoa tamko kuwa
      CCJ-Pwani haina hata ofisi licha ya wanachama. Baadaye akasema
      Zanzibar tuna mwanachama mmoja, yote haya aliyafanya kwa
      makusudi ili CCJ ionekane si kitu.
      Msajili ameonyesha dharau na kejeli za wazi kwa watanzania,
      tungependa kuwafahamisha Watanzania kwamba, wananchi wengi
      sehemu mbalimbali za nchi yetu watu wa kila rika, dini mbalimbali
      wakiwepo wasanii, wakulima, wafanyakazi pamoja na wastaafu
      wamekikubali na kukipokea Chama Cha Jamii na wengi wamejiunga.
      Tarakimu zilizopo ofisini, mpaka sasa kuna watanzania takriban 9500
      wamejiunga na CCJ. Aidha wapo watanzania nje ya nchi kama vile
      Marekani, Japani, Uingereza, Korea ya Kusini na Afrika Kusini
      waliojiunga na CCJ.
      Watanzania hawa waliojiunga na CCJ, aidha walifika wao wenyewe
      ofisini au walishawishiwa na wananchi ambao walikuwa tayari
      wamejiunga awali ukiondoa wanachama 102 walio jiunga kwenye
      mkutano wa hadhara wa kuompokea Mh Mpendazoe uliofanyika pale
      Mwembeyanga.
      KUGOMBEA KUPITIA CHADEMA
      Kwa mda mrefu kumekuwa na mazungummzo kati ya CCJ na
      CHADEMA ya kuwa na ushirikiano na hususan katika uchaguzi mkuu
      utakaofanyika oktoba 2010, hii inatokana na ukweli kuwa vyama hivi
      vina itikadi na mwelekeo unaofanana. Ushirikiano huu ungeendelea
      hata baada ya CCJ kupata usajili wa kudumu. Sasa, kwa kuwa muda
      tuliobaki nao ni mchache kwa CCJ kupata usajili wa kudumu na
      kufanya maandalizi ya kutosha kuelekea uchaguzi mkuu, hivyo basi,
      tunatoa wito kwa wanachama wa CCJ wenye sifa na nia ya kugombea
      nafasi za uongozi wa kuchaguliwa katika uchaguzi mkuu ujao,
      kugombea kupitia CHADEMA.
      Ndugu zangu tunafanya hivi si kwa maslahi yetu au ya vyama vyetu,
      isipokuwa tunafanya hivi kwa maslahi ya Taifa. Ndio maana tumeamua
      kuachia nyadhifa zetu na kujiunga CHADEMA kama wanachama wa
      kawaida. Hivyo basi, tunawaomba wanachama wote wa CCJ bila
      kusahau wote wenye mapenzi mema na taifa hili, kuunga mkono
      maamuzi haya na kuwachagua wote watakaosimamishwa na
      CHADEMA.
      Kwa kuwa CCJ tunaamini kuwa Umoja ni Nguvu ya pekee ya wananchi
      katika kujenga Usawa na Uhuru na katika kuondoa Umaskini, Ujinga,
      Maradhi na kupambana na Ufisadi, na kwa kuwa CHADEMA kinaamini
      katika falsafa ya Nguvu na Mamlaka ya Umma ambayo inalenga katika
      kuwaamasisha, kuwaelimisha, kuwashawishi na kuwandaa Watanzania
      wachukue hatua kuimiliki, kuitawala, kuilinda na kuifaidi nchi yao, hivyo
      basi tunatangaza rasmi kuwa Dickson Ngʼhily (Naibu Katibu Mkuu-
      Bara), Richard Kiyabo (Mwenyekiti-Taifa) na Fred Mpendazoe
      (Msemaji-Taifa) watagombea nafasi za uongozi katika uchaguzi mkuu
      ujao kwa tiketi ya CHADEMA mara baada ya kuchukua kadi zao za
      uanachama wa CHADEMA.
      Ndugu zangu nyote ni mashahidi na mnaelewa juu ya utajiri mkubwa
      ambao Mwenyezi Mungu ameuweka ndani ya mipaka ya Tanzania.
      Hata hivyo ni jambo la kusikitisha kuwa wananchi wake ni maskini wa
      kutupwa, hiki ni kitendawili ambacho jibu lake ni la kusikitisha kwani jibu
      ni dhahiri, ni kutokana na uongozi usiojali wanyonge na usio na
      uzalendo wa CCM.
      Ni dhahiri kwamba watanzania wamechoshwa na hali hii na wanahitaji
      mabadiliko ya kweli katika uongozi na uendeshaji wa nchi, hii ni
      kutokana na ukweli kuwa CCM na serikali yake haviwezi kuleta
      mabadiliko hayo na kamwe haitaweza. Ni dhahiri kwamba watanzania
      wamechoka kuishi maisha yasiyo na matumaini, maisha yasiyo na
      mwelekeo wa kesho, hivyo mabadiliko yanahitajika.
      Na hili ndilo tumaini letu na tena hii ndiyo imani tunayoondoka nayo
      kuwa sote kwa pamoja tunahitaji mabadiliko ya dhati na kwa
      ushirikiano huu Tanzania yenye neema bila CCM inawezekana! Huu
      sio wakati wa kupigishwa porojo na kupewa kanga na Tshirts, ni wakati
      wa kusimama pamoja wanaume kwa wanawake, vijana na watoto
      kudai mabadiliko katika sanduku la kupigia kura. Narudia tena
      Tanzania yenye Neema Bila CCM inawezekana.
      Mungu ibariki Tanzania
      Asanteni kwa kunisikiliza.

    19. #18
      Regia Mtema's Avatar
      R I P Array
      Join Date : 21st November 2009
      Posts : 2,988
      Rep Power : 1112
      Likes Received
      763
      Likes Given
      397

      Default Re: Viongozi wa CCJ Wajiunga Rasmi na CHADEMA Leo

      Quote By Ntemi Kazwile
      Hakuna attachment mkuu tunaomba uirushe.

      Tunawakaribisha... Mzee wa Chadema mimi nilijiunga Chadema kwa sms lakini mpaka na nikaahidiwa kuwa ningetafutwa na viongozi wa eneo ninalokaa lakini mpaka leo. takribani mwaka umepita sijawaona au kusikia lolote kutoka Chadema.. kulikoni???
      Pole sana Mkuu.Unapatikana wapi ili tuwasiliane na wewe au tuingie chemba(PM) ili tujadili mustakabali wa chama chetu.Usijali kadi utapata tu. Kuhusu attachement,hiyo hapo imeshawekwa..
      Kilombero For Change(K4C)-Mfuko wa Maendeleo Kilombero

    20. #19
      Regia Mtema's Avatar
      R I P Array
      Join Date : 21st November 2009
      Posts : 2,988
      Rep Power : 1112
      Likes Received
      763
      Likes Given
      397

      Default Re: Viongozi wa CCJ Wajiunga Rasmi na CHADEMA Leo

      Quote By Vincent Augustino
      Waliokuwa wanachama au wafuasi wao wameachwa wapi?
      Tamko lao limewaomba nao kujiunga na CHADEMA na wale waliokuwa na nia ya kugombea Udiwani au Ubunge wameombwa kugombea kupitia CHADEMA.Wengine tulikuwa nao pia kwenye Press hii..
      Kilombero For Change(K4C)-Mfuko wa Maendeleo Kilombero

    21. #20
      Boramaisha's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th April 2009
      Posts : 826
      Rep Power : 682
      Likes Received
      5
      Likes Given
      0

      Default Re: Viongozi wa CCJ Wajiunga Rasmi na CHADEMA Leo

      GS, Habari hii naiona haijakaa sawasawa hakuna uhakika wowote kwamba uliyotubandikia ni ya kweli.

      Hata hivyo, kama ni kweli hao waliotajwa wamejiunga na CHADEMA ili wawanie ubunge huo ni uamuzi wao na hauna uhusiano wowote na uamuzi wa wanachama wengine wa CCJ. Mie kama 'aliyekuwa mwanachama mtarajiwa' wa chama cha CCJ ambacho kwa sasa kimenyimwa usajili kwa mizengwe, sidhamirii kujiunga na CHADEMA ama chama chochote ambacho itikadi, sera na malengo yake hayajanigusa ipasavyo. Bado CHADEMA haijagusa moyo wangu ili nipate kuridhika kwamba chama hicho kina malengo thabiti ya kuhakikisha kuwepo kwa maendeleo yatakayolenga 'watu' - Watanzania wote. Mpaka sasa CHADEMA haijatuonyesha itakuwa na mikakati gani na itachukua hatua gani za makusudi kabisa kuhakikisha kwamba walioliibia taifa na kulihujumu wanachukuliwa hatua zinazostahili. Pia sijui CHADEMA kina mipango gani ya kuhakikisha hali za wanyonge wa Tanzania zinakuwa nzuri ndani ya miaka 5 ya uongozi wa CHADEMA, kwa sababu hilo linawezekana kabisa iwapo kuna mipango maalum. Hii blabla ya siasa za mrengo wa kati hazitoshi kututhibitishia chochote. Huenda nanyi kwa siasa zenu za mrengo wa kati mtazidi kukuza matabaka katika jamii.

      CHADEMA Siasa zenu za majimbo zina kasoro kwa wale tunaoamini juu ya kuendeleza ujenzi wa umoja nchini. Juzijuzi nilimsikia kiongozi mwandamizi wa CHADEMA akizungumza na kutetea kwa nguvu zote wagombea wanaowania uongozi - ubunge, udiwani nk. waruhusiwe kupiga kampeni kwa lugha za kikabila badala ya Kiswahili. Hizi ndio sera zenu CHADEMA za maendeleo za kutaka turudi kwenye kuongea kimatumbi na ki-barbeig majukwaani?

      Jingine lililonistua ni kumsikia kiongozi mmoja wa Taasisi moja ya Uchumi nchini (anaweza akawa mwanachama wa CHADEMA) akizungumzia habari ya kutaka kuwepo kwa "middle class" nchini na akawahamasisha Watanzania walio Marekani kuungana na walio nchini kuanzisha hiyo "middle class". Sasa huenda na ninyi CHADEMA siasa zenu za mrengo wa kati zina nia ya kutuletea na kujenga matabaka nchini kama ilivyo kwenye nchi za kibepari - wawepo Watanzania wa juu, wa kati na wa chini! CCJ isipokuwepo, ntaunga mkono chama kinachotetea kwa dhati kabisa usawa na haki sawa kwa kila Mtanzania katika mgawanyo wa keki ya Taifa.

      Kwa maoni yangu, kuwa na wapinzani wengi bungeni ambao hawana itikadi maalum inayowaunganisha nako ni kupoteza wakati na nguvu. Mwisho wa siku nchi itaendeshwa kwa mfumo gani?

    Page 1 of 7 123 ... LastLast

    Similar Topics

    1. Lema awapa Mamiss kadi na wajiunga rasmi CHADEMA
      By never in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 25
      Last Post: 20th August 2011, 09:19
    2. Wanachuo 300 wajiunga CHADEMA
      By Technician in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 60
      Last Post: 22nd March 2011, 20:05
    3. Familia Ya Nyerere Wajiunga Na Chadema?
      By Ndallo in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 22
      Last Post: 3rd March 2011, 17:47
    4. Mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa Iringa na wenzake wajiunga CCM
      By Maxence Melo in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 70
      Last Post: 14th December 2010, 21:41
    5. Mr Sugu na Mkoloni Wajiunga Rasmi na CHADEMA
      By Regia Mtema in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 72
      Last Post: 29th June 2010, 10:08

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...