Dakika chache zilizopita Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Freeman Mbowe amewapokea waliokuwa viongozi wa CCJ, Richard Kiyabo aliyekuwa Mwenyekiti, Dickson Ng’hily aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu CCJ Bara na Fred Mpendazoe aliyekuwa Msemaji Mkuu wa CCJ Taifa.
Viongozi hawa wamejinga rasmi na CHADEMA na kukabidhiwa kadi na Mbowe mbele ya Waandishi wa Habari.
Pamoja na kujiunga na CHADEMA Viongozi hawa pia wametoa tamko rasmi la kwanini wamejiunga na chama hiki,Find Attachment hapo chini. Vile Vile Viongozi hawa wametangaza nia ya kugombea Ubunge kupitia CHADEMA kama ifuatavyo;
Dickson Ng’hily -Kugombea Jimbo la Temeke
Richard Kyabo-Kugombea Jimbo la Bukene
Fred Mpendazoe-Kugombea Jimbo la Segerea
Matukio ya picha nadhani Waandishi wa Habari watarusha mambo yakiwa tayari
Binafsi nimefurahishwa sana na uamuzi wa Viongozi hawa na furaha yangu itakamilika wakishinda Ubunge kwenye Majimbo yao.
Wale wanaJF ambao ni wanachama wa CCJ wanashauriwa kujinga mapema na CCJ.
Wenu katika Demokrasia na Maendeleo
Gender Sensitive

Reply With Quote
Follow Us Here