Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Buzwagi: Lowassa Alikuwa London Siku Ya Mkataba

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 33
    1. #1
      Gembe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th September 2007
      Location : kamnyonge
      Posts : 2,586
      Rep Power : 1515
      Likes Received
      64
      Likes Given
      54

      Post Buzwagi: Lowassa Alikuwa London Siku Ya Mkataba

      habari za kuaminika kutoka London zinasema ya kwamba ,mheshimiwa Lowassa alikuwapo London 17 februari mwaka huu,siku ambayo mkataba wa Buzwagi ulitiwa saini,
      Lowassa aliingia London tarehe 16 february akitokea Paris,Ufaransa ambako alikuwapo kikazi kwa muda wa siku nne,pia mheshima Lowassa alifikia katika Hoteli ya Churchil hill jijini Londoa ambako waziri karamagi alikuwa amefikia.
      na katika Hoteli hiyo ndipo mkataba wa buzwagi uliposainiwa,
      akiwa London,Lowassa alipokutana na watendaji wa serikali waliokuwa na Rais kikwete na kwa Upole wakamuuliza 'Mheshimiwa huko hapa?'Basi naye akawaambia alikuwa amekwenda kufanya Shopping..na kabla ya hapo alimpigia Balozi wa London na kumuelezea kwamba anakuja Lodnon ila asimpangie chumba..

      Je kwa maelezo haya,kwa kuwa Lowassa alikataa asifanyie booking ya chumba ,je wana wa watanzania hamuoni tayari kuna mazingira tata kuhusus mkataba huu?

      huyu Lowassa ana nia gani na SISI?

      Source:Mwanahalisi

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      Kichuguu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th October 2006
      Location : Popote Porini
      Posts : 6,828
      Rep Power : 3269
      Likes Received
      1299
      Likes Given
      913

      Default

      Quote By mkomboziufisadi
      habari za kuaminika kutoka London zinasema ya kwamba ,mheshimiwa Lowassa alikuwapo London 17 februari mwaka huu,siku ambayo mkataba wa Buzwagi ulitiwa saini,
      Lowassa aliingia London tarehe 16 february akitokea Paris,Ufaransa ambako alikuwapo kikazi kwa muda wa siku nne,pia mheshima Lowassa alifikia katika Hoteli ya Churchil hill jijini Londoa ambako waziri karamagi alikuwa amefikia.
      na katika Hoteli hiyo ndipo mkataba wa buzwagi uliposainiwa,
      akiwa London,Lowassa alipokutana na watendaji wa serikali waliokuwa na Rais kikwete na kwa Upole wakamuuliza 'Mheshimiwa huko hapa?'Basi naye akawaambia alikuwa amekwenda kufanya Shopping..na kabla ya hapo alimpigia Balozi wa London na kumuelezea kwamba anakuja Lodnon ila asimpangie chumba..

      Je kwa maelezo haya,kwa kuwa Lowassa alikataa asifanyie booking ya chumba ,je wana wa watanzania hamuoni tayari kuna mazingira tata kuhusus mkataba huu?

      huyu Lowassa ana nia gani na SISI?

      Source:Mwanahalisi
      ..............ukishangaa ya musa.............
      Kichuguuu: Nyumba inayohifadhi mchwa na nguchiro kwa pamoja bila mkwaruzo

    4. #3
      Ibambasi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th July 2007
      Location : Iponyamakalai - Isungang'holo
      Posts : 724
      Rep Power : 753
      Likes Received
      118
      Likes Given
      762

      Default

      Mmhh,
      Sasa ndo ndo mambo yanaanza kufunguka taratibu.Wakiambiwa hii ni serikali ya kishkaji na kisanii wanakuja juu,sasa ni kwa ethics zipi za kiuogozi Waziri Mkuu anmwambia Balozi asimpangie chumba cha kulala?Je ratiba ya Waziri Mkuu ilimruhusu kwenda kufanya shopping huko?Ina maana kuna tofauti kubwa sana (iwe ya bei,aina au ubora wa bidhaa) kati ya maduka ya London na Paris kiasi cha kumfanya huyo Lowassa ashindwe kufanya shopping Paris?kama hakuwa na muda Paris huo wa London ulitoka wapi?

      Ndugu zangu kweli nimeamini huyu jamaa uwezo wake wa kufikiri na kutenda ni afadhali wa yule Ziro wa Mtanzania (kama bado yupo),ndo sababu juzi kule Mbeya ati anasema mkataba wa Buzwagi safi.Na je hii ni kudhihirisha alichosema Zitto kuwa Muungwana hakujua utiaji saini wa Buzwagi na kwa maana hiyo Karamagi na Lowassa walimpiga changa la macho swahiba wao Muungwana?Kama ndo hivyo basi mwaka huu kazi ipo.Na labda ndo sababu za mino'ngono hapa mjini kuwa Muungwana na Lowassa hawaivi tena yani ni paka na panya.Kama hivi ndivyo I pity you my beloved Tanzania...yaani wengine wapo buzy kuiba,kuuza nchi...!!!

    5. #4
      MegaPyne's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 4th May 2006
      Posts : 589
      Rep Power : 100000
      Likes Received
      2
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By mkomboziufisadi
      habari za kuaminika kutoka London zinasema ya kwamba ,mheshimiwa Lowassa alikuwapo London 17 februari mwaka huu,siku ambayo mkataba wa Buzwagi ulitiwa saini,
      Lowassa aliingia London tarehe 16 february akitokea Paris,Ufaransa ambako alikuwapo kikazi kwa muda wa siku nne,pia mheshima Lowassa alifikia katika Hoteli ya Churchil hill jijini Londoa ambako waziri karamagi alikuwa amefikia.
      na katika Hoteli hiyo ndipo mkataba wa buzwagi uliposainiwa,
      akiwa London,Lowassa alipokutana na watendaji wa serikali waliokuwa na Rais kikwete na kwa Upole wakamuuliza 'Mheshimiwa huko hapa?'Basi naye akawaambia alikuwa amekwenda kufanya Shopping..na kabla ya hapo alimpigia Balozi wa London na kumuelezea kwamba anakuja Lodnon ila asimpangie chumba..

      Je kwa maelezo haya,kwa kuwa Lowassa alikataa asifanyie booking ya chumba ,je wana wa watanzania hamuoni tayari kuna mazingira tata kuhusus mkataba huu?

      huyu Lowassa ana nia gani na SISI?

      Source:Mwanahalisi
      Hii habari inaukweli kiasi fulani.

      Lowassa ahudhuria mkutano wa Afrika UfaransaBy Saidi Nguba | Published 02/15/2007 | Habari Mpya |

      Na Mwandishi Maalum, Nice, Ufaransa

      WAZIRI Mkuu Edward Lowassa amekuwa miongoni mwa viongozi na wakuu wa nchi za Afrika wanaohudhuria mkutano wa siku mbili mjini hapa ulioanza leo (Alhamisi Feb. 15, 2007)kujadili hali ya baadaye ya Afrika.

      Lowassa anamwakilisha Rais Jakaya Kikwete katika mkutano huo wa 24, unaoitwa ‘Mkutano wa wakuu wa nchi za Afrika na Ufaransa’ ambao mada yake mwaka huu ni “Afrika na uwiano wa utulivu duniani” (Africa and Global Balance).

      Akizungumza katika ufunguzi wa mkutano huo, Rais Jacques Chirac alisema kuwa yapo matumaini makubwa ya kuleta maendeleo ya kiuchumi katika Afrika, kwa vile Afrika ni tajiri ila watu wake ndiyo masikini.

      Chirac alisema kuwa kwa kuwa Afrika peke yake ina zaidi ya theluthi moja ya madini yote duniani, ikisaidiwa na kama madini hayo hayakuporwa, bara hilo na watu wake watapiga hatua kubwa ya maendeleo.

      “Afrika mpya inakuja…naipenda Afrika kwa moyo wangu wote,” Rais huyo wa Ufaransa alisema na kuitaka Jumuiya ya Kimataifa kuusaidia kwa hali na mali Umoja wa Afrika katika jitihada zake za kuleta maendeleo ya kisiasa na kiuchumi ya Afrika.

      Aliongeza: “Hali inayoonekana kwamba Afrika ni bara masikini siyo ukweli wa mambo…kuna mambo mawili ya kufanya, tuiache Afrika mali zake ziporwe au tuisaidie Afrika ipate maendeleo…tukiisaidia Afrika watu wake watapata maendeleo”.

      Mapema, akizungumza kwa niaba ya nchi za Afrika, Mwenyekiti wa sasa wa Umoja wa Afrika (AU) Rais John Kufour wa Ghana alisema Afrika inabidi kuheshimiwa na kwamba hali ya Afrika sasa inabadilika kuwa nzuri kutokana na kukua kwa demokrasia na uchumi.

      Viongozi wengine aliozungumza ni pamoja na Rais wa sasa wa Umoja wa Ulaya, Kiongozi wa Ujerumani, Chansela Angela Merekel ambaye alisema hakuna jinsi nyingine ila kuisaidia Afrika kwa ajili ya mandeleo yake na dunia nzima kwa jumla.

      Waziri Mkuu Lowassa aliwasili Nice jana (Jumatano Feb. 14, 2007) akiongoza ujumbe wa Tanzania kwenye mkutano huo kumwakilisha Rais Kikwete.

      Miongoni mwa waliomo kwenye ujumbe wa Tanzania ni pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje, Bernard Membe; Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Muhammed Seif Khatib na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo Zanzibar, Mahmood Thabit Kombo.

      Kesho (Ijumaa Feb. 16, 2007) mkutano huo utafungwa rasmi mchana na kutakuwa na mkutano wa waandishi wa habari kuelezea matokeo yake.

    6. Dua
      #5
      Dua's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th November 2006
      Posts : 3,534
      Rep Power : 1364
      Likes Received
      9
      Likes Given
      0

      Default

      Huo mkataba ni mzuri kwa sababu JK, EL wanafaidika nao binafsi na ndiyo sababu Karamagi wala hashituki, anaendelea kula kuku na biskuti.

      Hadi pale Wananchi wa Tanzania na ambao ndio walipa kodi watakaposema basi ndio hawa mafisadi wataacha (Hawawezi kuacha kwa hiari). Uhujumu wa uchumi sheria yake lazima iwe kunyongwa hadi kufa na kufilisiwa.
      Dua la kuku halimpati mwewe

    7. Miaka 50

    8. #6
      Mwakilishi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st January 2007
      Posts : 521
      Rep Power : 733
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default

      1. Hii habari ya kuwa Waziri Mkuu Mheshimiwa Lowassa alikuwepo London, tena kwenye hotel ya Churchill uliposiniwa mkataba wa Buzwagi, siku mkataba uliposainiwa mbona haikuwahi kusemwa huko nyuma?

      2. Kama alikwenda London kufanya shopping kama inavyodaiwa, ukizingatia alikuwa Ufaransa hapo jirani tu je ni kosa?

      3. Vilevile alipokwenda London bila shaka alikuwa na taarifa za Waziri Karamagi kuwepo huko akaamua kwenda kumsalimia hapo hotelini, je ni kosa?

      4. Ikiwa alimpigia simu Balozi na kumtaarifu kuwa anakuja London ila asimfanyie booking ya hoteli hamuoni kwamba hakuwa anajaribu kuficha chochote vinginevyo angejiendea kimyakimya.

      5. Sidhani kama alienda kwa kujiiba au kujificha, yeye ni waziri mkuu na anajua kuna Watanzania huko London tena wengi tu na wanamjua na watamwona na watamuuliza.

      6. Hii hoja ya kumlundika na Mheshimiwa Karamagi ingekuwa na nguvu kama Waziri Mkuu angejiiba kimyakimya toka Dar kwenda huko hotelini London. Lakini tayari alikuwa huko Ufaransa kikazi.

      Kwa kutumua msemo wa mwanaJF mmoja hapa "mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni"

    9. #7
      DAR si LAMU's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st March 2007
      Posts : 2,979
      Rep Power : 5718
      Likes Received
      151
      Likes Given
      0

      Default !

      Quote By Mwakilishi
      1. Hii habari ya kuwa Waziri Mkuu Mheshimiwa Lowassa alikuwepo London, tena kwenye hotel ya Churchill uliposiniwa mkataba wa Buzwagi, siku mkataba uliposainiwa mbona haikuwahi kusemwa huko nyuma?

      2. Kama alikwenda London kufanya shopping kama inavyodaiwa, ukizingatia alikuwa Ufaransa hapo jirani tu je ni kosa?

      3. Vilevile alipokwenda London bila shaka alikuwa na taarifa za Waziri Karamagi kuwepo huko akaamua kwenda kumsalimia hapo hotelini, je ni kosa?

      4. Ikiwa alimpigia simu Balozi na kumtaarifu kuwa anakuja London ila asimfanyie booking ya hoteli hamuoni kwamba hakuwa anajaribu kuficha chochote vinginevyo angejiendea kimyakimya.

      5. Sidhani kama alienda kwa kujiiba au kujificha, yeye ni waziri mkuu na anajua kuna Watanzania huko London tena wengi tu na wanamjua na watamwona na watamuuliza.

      6. Hii hoja ya kumlundika na Mheshimiwa Karamagi ingekuwa na nguvu kama Waziri Mkuu angejiiba kimyakimya toka Dar kwenda huko hotelini London. Lakini tayari alikuwa huko Ufaransa kikazi.

      Kwa kutumua msemo wa mwanaJF mmoja hapa "mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni"
      ..uchambuzi mzuri wa pumba ipi,mchele upi!
      Dar na Lamu yote miji ya pwani, lakini haifanani!

    10. #8
      Kufakunoga's Avatar
      Member Array
      Join Date : 24th September 2007
      Posts : 35
      Rep Power : 602
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default

      Unajua mwakilishi wanasheria wana kitu kinaitwa `circumstancial evidence` ushaidi wa mazingira.kitendo cha lowassa kwenda London,wakati mkataba ukisainiwa huko,na leo anajitokeza hadhalani kuutetea kwamba hauna kasoro kwa mtu mwenye uelewa lazima atilie shaka.

    11. #9
      Mwakilishi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st January 2007
      Posts : 521
      Rep Power : 733
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default

      Nakusikia Kufakunoga, ila mimi nadhani kinachoendelea hapa ni waziri mkuu amejaribu bila mafanikio kumsitiri waziri Karamagi mbele ya wananchi.

      Nisingetegemea amkane au amshutumu waziri wake wa madini mbele ya kadamnasi, especially ukichukulia kuwa Mheshimiwa Rais mwenyewe ambaye ndie bosi wao kauchuna. Wote wanafahamu huo mkataba bomu lakini ndio hivyo hakuna wa kumfunga paka kengele.

    12. #10
      Mpaka Kieleweke's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th February 2007
      Posts : 2,665
      Rep Power : 1166
      Likes Received
      675
      Likes Given
      7

      Default

      Mwakilishi inaonekana kuwa wewe ni mgeni wa kujua protocal za nchi .
      Waziri mkuu ni kiongozi na hawezi kwenda kimya kimya tena London na kumwambia balozi wake asimfanyie booking ya chumba , hii sio sahihi hata kidogo.

      Na pia kwenye hili kuna kila sababu ya watanzania kuilalamikia uingereza kwa kumpokea kiongozi wetu na bila kufuatia protocal za kumpokea kiongozi mkubwa wa nchi na ndio maana hata wakiwa wanasafir wakiwa wanajaza mafuta kwenye viwanja vya ndege huwa protocal inazingatiwa je?kwenda kulala hotelini na tena hata balozi hajamwandalia mazingira ya ulinzi n.k hii ni sawa?

      Huyu alikwenda na walinzi wanagapi?
      Ni kwa nini walinzi tuliowapa jukumu la kumlinda waziri wetu mkuu wamruhusu kwenda na mlinzi mmoja?
      Hapa kuna deal tena inawezekana hawa jamaa walipokea cha kwao in cash ndio maana jamaa kaamua kufuata hadi london kwenyewe.

    13. #11
      Gembe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th September 2007
      Location : kamnyonge
      Posts : 2,586
      Rep Power : 1515
      Likes Received
      64
      Likes Given
      54

      Default

      nchi imejaa usaniii mtupu,mambo yote sasa hivi yanafanywa kisanii sana,kuna jambo linakuja.kuna msanii mmoja anakaribia kupewa madaraka pale magogoni,na alihusika kusuka dili la Richmond.stay tuned

    14. #12
      Mwakilishi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st January 2007
      Posts : 521
      Rep Power : 733
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default

      Mpaka Kieleweke,

      Naomba nivumilie kidogo mkuu, inawezekana kabisa sielewi vizuri hizi taratibu za kiitifaki lakini:

      1. Kama alikuwa anakwenda shopping yake binafsi (kama tulivyoelezwa) baada ya kazi Ufaransa, sioni sababu ya yeye kupokewa kiserikali na Uingereza, angekuwa amekwenda kikazi bila shaka hilo lingefanyika.

      2. Si ajabu alikwenda na mlinzi mmoja katika jitihada za kubana matumizi, yaani asionekane anatumbua pesa ya walipa kodi kwa kuandamana na msafara mzima kwa ajili ya shopping yake binafsi, angeandamana na msafara wake wote kwa ajili ya shopping binafsi bila shaka tungelalamika ubadhirifu wake.

      3. Kitendo cha kumtaarifu Balozi na kumwambia asimtafutie chumba hotelini sioni kama kina tatizo, kwani angeshindwa nini kumwambia balozi am-bookie chumba hapo Churchill hotel? Mimi nadhani hakuwa na mpango wa kulala huko labda alirudi Paris siku hiyohiyo(sina uhakika lakini)

      Mimi hapa najaribu kuangalia pande zote za hili suala.

    15. #13
      Ibambasi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th July 2007
      Location : Iponyamakalai - Isungang'holo
      Posts : 724
      Rep Power : 753
      Likes Received
      118
      Likes Given
      762

      Default

      We Mwakilishi unatoka dunia ipi?
      Hivi ni sawa kwa Waziri Mkuu kwenda London bila kuwa na utaratibu wowote ule wa kiprotokali?swala la kwamba eti angetokea hapa Dar ndo ingekuwa issue halina msingi kabisa,ndhani wewe unataka kuimply kwamba Karamagi na Lowassa kukutana hapo Churchill ilikuwa ni coincidence,as a matter of fact and with due respect,coincidences do not work that way,kuhusu kuwa hii habari haikuwa hapo nyuma,kumbuka kuwa hili ni swala la ushahidi,na ushahidi si lazima upatikane muda huo huo tukio linapotokea ndo sababu leo hii katika inquest ya Diana kuna ushahidi mpya wa CCTV kutoka kwenye ile lift ya hotel kule Ufaransa na ni mwaka 1997,hivyo basi swala la msingi hapa ni kuwa tume huru iundwe na kuchunguza mienendo ya viongozi wote wanaohusishwa na Buzwagi,kwa nini wakutane Churchill wao wawili (coincidence!!!),pili kwa nini amzuie Balozi Maajar asimpangie chumba?what was so special mpaka akatae chumba?Lowassa ana maswali ya kujibu...just let's wait and see as...THE DRAMA KEEPS UNFOLDING...

    16. #14
      Mwafrika's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th November 2006
      Posts : 4,546
      Rep Power : 1556
      Likes Received
      3
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By mkomboziufisadi
      habari za kuaminika kutoka London zinasema ya kwamba ,mheshimiwa Lowassa alikuwapo London 17 februari mwaka huu,siku ambayo mkataba wa Buzwagi ulitiwa saini,
      Lowassa aliingia London tarehe 16 february akitokea Paris,Ufaransa ambako alikuwapo kikazi kwa muda wa siku nne,pia mheshima Lowassa alifikia katika Hoteli ya Churchil hill jijini Londoa ambako waziri karamagi alikuwa amefikia.
      na katika Hoteli hiyo ndipo mkataba wa buzwagi uliposainiwa,
      akiwa London,Lowassa alipokutana na watendaji wa serikali waliokuwa na Rais kikwete na kwa Upole wakamuuliza 'Mheshimiwa huko hapa?'Basi naye akawaambia alikuwa amekwenda kufanya Shopping..na kabla ya hapo alimpigia Balozi wa London na kumuelezea kwamba anakuja Lodnon ila asimpangie chumba..

      Je kwa maelezo haya,kwa kuwa Lowassa alikataa asifanyie booking ya chumba ,je wana wa watanzania hamuoni tayari kuna mazingira tata kuhusus mkataba huu?

      huyu Lowassa ana nia gani na SISI?

      Source:Mwanahalisi
      Oh jamani, hivi mangapi ambayo bado yako sirini. Sishangai sasa kusikia kuwa kabla hoja ya Buzwagi haijaletwa bungeni Lowasa aliwaita wabunge wa ccm na kuwapa somo. Hivi kuna mangapi hapa yanafichwa?

    17. #15
      Mwafrika's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th November 2006
      Posts : 4,546
      Rep Power : 1556
      Likes Received
      3
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By Mwakilishi
      Mpaka Kieleweke,

      Naomba nivumilie kidogo mkuu, inawezekana kabisa sielewi vizuri hizi taratibu za kiitifaki lakini:

      1. Kama alikuwa anakwenda shopping yake binafsi (kama tulivyoelezwa) baada ya kazi Ufaransa, sioni sababu ya yeye kupokewa kiserikali na Uingereza, angekuwa amekwenda kikazi bila shaka hilo lingefanyika.

      2. Si ajabu alikwenda na mlinzi mmoja katika jitihada za kubana matumizi, yaani asionekane anatumbua pesa ya walipa kodi kwa kuandamana na msafara mzima kwa ajili ya shopping yake binafsi, angeandamana na msafara wake wote kwa ajili ya shopping binafsi bila shaka tungelalamika ubadhirifu wake.

      3. Kitendo cha kumtaarifu Balozi na kumwambia asimtafutie chumba hotelini sioni kama kina tatizo, kwani angeshindwa nini kumwambia balozi am-bookie chumba hapo Churchill hotel? Mimi nadhani hakuwa na mpango wa kulala huko labda alirudi Paris siku hiyohiyo(sina uhakika lakini)

      Mimi hapa najaribu kuangalia pande zote za hili suala.
      Wewe hapa unaangalia huo upande wa Lowasa kwenda kufanya shoping na kwenda na mlinzi mmoja. Mimi naangalia upande wa Lowasa kukutana na Karamagi London kwenye kusaini mkataba wa Buzwagi. Pande zote mbili zimeangaliwa au sio!

    18. #16
      Gembe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th September 2007
      Location : kamnyonge
      Posts : 2,586
      Rep Power : 1515
      Likes Received
      64
      Likes Given
      54

      Default

      where we dare talk openly

    19. #17
      Mpaka Kieleweke's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th February 2007
      Posts : 2,665
      Rep Power : 1166
      Likes Received
      675
      Likes Given
      7

      Default

      Lowassa lazima ajibu hili kuwa ilikuwaje akaenda londoni bila kuwa na ulinzi wala kupita ofisi za ubalozi wetu huko.

      Nguba uje hapa utupe majibu mapema iwezekanavyo kuwa ilikuwaje akaenda mpaka churchil hotel wakati hajautaarifu ubalozi wetu?
      Angeumia ingekuwaje? balozi wetu angelikuwa na wakati mgumu sana kujieleza jinsi alivyomfanya waziri mkuuu wetu kimya kimya.

      Waziri mkuu asema kama balozi zetu haziwezi kumfanyia booking za hotel ili tuweze kujua hilo mapema na balozi nyingine nazo zitaarifiwe mapema ili kutokumfanyia booking.

    20. #18
      Halisi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th January 2007
      Posts : 3,037
      Rep Power : 2177
      Likes Received
      455
      Likes Given
      243

      Default

      KUna habari kwamba LOWASA akiwa Mbeya amejibu na kusema kwamba yeye hahusiki na MKATABA WA BUZWAGI, tusubiri taarifa zaidi. Nadhani wataandika ktk magazeti

    21. #19
      Bill's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th October 2007
      Posts : 1,663
      Rep Power : 926
      Likes Received
      300
      Likes Given
      203

      Default

      EL amekuwa akijaribu kuutetea kwa nguvu zake zote mkataba huu wa Buzwagi na Karamangi, ni kwa sababu anajua yuko nyuma ya pazia.

      EL alijaribu kwa kushirikiana na spika na wa wabunge wa SISIEM kuizima hoja hii, lakini haijawezekana.

      Jitihada za mwisho za EL nikujaribu kudanganya wananchi kwenye majukwaa ya siasa, hili nalo limepata dawa yake sasa.

      Ningetegemea kabisa EL angesema mkataba huu hauna matatizo kwani wakati wa kusainiwa na mimi nilikuwepo tulikuwa chumbani na Kara. Sio kweli kwamba una manufaa kwetu sisi wawili yaani mimi EL na fisadi Kara pamoja na familia zetu.

      Nchi imefakamiwa na walanguzi.
      Last edited by Bill; 24th October 2007 at 18:42. Reason: misspelled

    22. #20
      Mpaka Kieleweke's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th February 2007
      Posts : 2,665
      Rep Power : 1166
      Likes Received
      675
      Likes Given
      7

      Default

      Nchi inakaliwa na mafisadi na hao ni zaidi ya walanguzi.

    23. Study Abroad
    Page 1 of 2 12 LastLast

    Similar Topics

    1. Replies: 1144
      Last Post: 19th March 2010, 07:11
    2. Lowassa amezushiwa Buzwagi 31.10.07
      By mkama in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 5
      Last Post: 12th July 2009, 18:50
    3. Kamati kuuchunguza mkataba wa Buzwagi
      By Halisi in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 5
      Last Post: 21st November 2007, 18:00
    4. Replies: 5
      Last Post: 8th October 2007, 20:52

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...