Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Ikulu Vs gazeti la Mwananchi!

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 35
    1. #1
      AK-47's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th November 2009
      Location : Abbottabad
      Posts : 1,366
      Rep Power : 761
      Likes Received
      149
      Likes Given
      80

      Default Ikulu Vs gazeti la Mwananchi!

      DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
      UNITED REPUBLIC OF TANZANIA


      Telephone: 255-22-2114512, 2116898
      E-mail: [email protected]
      Fax: 255-22-2113425







      PRESIDENT’S OFFICE,
      THE STATE HOUSE,
      P.O. BOX 9120,
      DAR ES SALAAM.
      Tanzania.







      TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


      Gazeti la kila siku la Mwananchi la jana, Jumanne, Juni Mosi, 2010, lilichapisha habari kwenye ukurasa wake wa kwanza chini ya kichwa cha habari, “Waziri Amuumbua Msemaji wa Rais”.

      Katika habari hiyo, gazeti hilo lilidai kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu wa Bunge), Mheshimiwa Philip Marmo alikuwa amepingana na maelezo yaliyotolewa Mei 21, mwaka huu, 2010, na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Salva Rweyemamu, kuhusiana na ziara za mawaziri nje ya nchi na katika mikoa mbali mbali nchini.

      Katika taarifa yake ya Mei 21, mwaka huu, kwa vyombo vya habari, Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais ilikuwa imekanusha habari zilizokuwa zimeandikwa na gazeti hilo hilo la Mwananchi chini ya kichwa cha habari, “Serikali Yahaha Uchaguzi Mkuu: Ikulu yazuia mawaziri kwenda nje, yawatuma mikoani kukutana na viongozi wa Dini na TUCTA’.

      Ikulu imeshangazwa na kusikitishwa sana na kiwango cha juu cha jitihada na juhudi kubwa zinazofanywa na gazeti hili kufitinisha watu na kupotosha umma kwa jambo ambalo halipo, na inapenda kurudia na kusisitiza kama ifuatavyo:
      1. Siyo Ikulu wala Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amewakataza mawaziri kusafiri nje ya nchi kama linavyodai gazeti hili. Hakuna waziri aliyezuiwa kusafiri nje.
      2. Siyo Ikulu wala Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amewaagiza mawaziri kusambaa katika mikoa mbali mbali kukutana na viongozi wa Dini na TUCTA kama linavyodai gazeti hili.

      Kama mawaziri wanakwenda mikoani kuelezea mafanikio makubwa yaliyopatikana chini ya Awamu ya Nne ya uongozi wa Tanzania ni jambo jema. Na hiyo ni sehemu ya wajibu wao na kazi zao kama mawaziri wa Serikali. Na wala siyo wafanye hivyo kwa kutumwa ama kuagizwa na yoyote. Ni wajibu wao wa kikazi na uwajibikaji. Kama tulivyoelezea katika taarifa ya Mei 21, hakuna haja wala hoja ya msingi kwa Serikali kuwatuma Mawaziri ama hata watu wengine wowote kwenda mikoani kuzungumza na viongozi wa kiroho ama wale wa TUCTA. Kama wananchi watakavyokuwa wanakumbuka, mazungumzo kati ya viongozi wa dini na Serikali yamemalizika majuzi. Yalifanyika rasmi na hadharani pale Hoteli ya White Sands, mjini Dar es Salaam. Tena mazungumzo hayo yalikwenda vizuri na yalimalizika vizuri. Viongozi wa dini walifurahi sana.

      Mazungumzo yenyewe yalifungwa na Mheshimiwa Rais Kikwete, na viongozi wa roho walifurahi kiasi cha kwamba wamependekeza kuwa utaratibu wa kuwa na mazungumzo ya namna hiyo liwe ni jambo la kudumu na yafanyike kila mwaka.

      Na Mheshimiwa Rais Kikwete amekubali pendekezo hilo ambako sasa itafanyika mikutano miwili kati ya viongozi wa kiroho na wale wa Serikali kila mwaka. Mkutano mmoja utakuwa kati ya Serikali na kila dhehebu, na ule wa pili utakuwa kama ule uliomalizika White Sands yaani kati ya Serikali na viongozi wote wa kiroho.

      Hivyo, kwa sasa Serikali haina sababu ya kuwatuma mawaziri wake kwenda kuzungumza na viongozi wa dini wakati mkutano kati ya pande hizo mbili umemalizika majuzi tu, tena vizuri, kwa kushirikisha viongozi wa kiroho kutoka mikoa yote.

      Aidha, mazungumzo kati ya Serikali na TUCTA pia yamemalizika. Mazungumzo hayo yalimalizika Mei 8, mwaka huu, 2010, mjini Dar es Salaam. Haya nayo yalimalizika vizuri na pande hizo mbili zilikubaliana. Lililobakia sasa ni Serikali kuyafanyia kazi makubaliano yaliyofikiwa katika mazungumzo hayo kupitia taratibu na michakato mbalimbali ya Kiserikali ukiwamo mchakato wa Bajeti.

      Sasa, kama mazungumzo kati ya Serikali na TUCTA yamefanyika vizuri na pande hizo mbili zimekubaliana, Serikali ama Ikulu, ina sababu gani ya kutuma mawaziri kwenda kuzungumza na viongozi wa TUCTA mikoani? Wanazungumza nini tena?

      Hivyo, Ikulu inapenda kuwaambia wananchi kuwa kama ilivyokuwa kwenye habari ile ya Mei 21, habari ya jana ya gazeti hilo pia siyo ya kweli na ni ya kufitinisha watu na inastahili kudharauliwa na kupuuzwa.


      Imetolewa na:


      Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
      Ikulu,
      DAR ES SALAAM.


      02 Juni, 2010
      An Eye for an Eye Makes the whole World Blind


    2. #2
      Obuntu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th February 2008
      Posts : 516
      Rep Power : 688
      Likes Received
      23
      Likes Given
      6

      Default Re: Ikulu Vs gazeti la Mwananchi!

      Salva Rweyemamu @ Work

    3. #3
      Kiranja Mkuu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th February 2010
      Posts : 2,084
      Rep Power : 890
      Likes Received
      284
      Likes Given
      34

      Default Re: Ikulu Vs gazeti la Mwananchi!

      Salva, mbona ni wewe tu unayepelekeshwa kasi?
      Habib halahala na wasemaji na waandishi wengine wa marais waliokutangulia wamekufundisha nini kwa matendo yao?

    4. #4
      Eng. SALUFU CA's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 12th May 2010
      Location : KIBAMBA KWA MANGI
      Posts : 146
      Rep Power : 492
      Likes Received
      12
      Likes Given
      28

      Default Re: Ikulu Vs gazeti la Mwananchi!

      Hapa kazi ipo wajamene!!!!!!!!

    5. #5
      Albedo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th February 2008
      Posts : 5,033
      Rep Power : 1588
      Likes Received
      1114
      Likes Given
      561

      Default Re: Ikulu Vs gazeti la Mwananchi!

      Quote By AK-47 View Post
      Kama mawaziri wanakwenda mikoani kuelezea mafanikio makubwa yaliyopatikana chini ya Awamu ya Nne ya uongozi wa Tanzania ni jambo jema. Na hiyo ni sehemu ya wajibu wao na kazi zao kama mawaziri wa Serikali. Na wala siyo wafanye hivyo kwa kutumwa ama kuagizwa na yoyote. Ni wajibu wao wa kikazi na uwajibikaji.
      Nilikuwa Sifahamu kumbe moja ya Job Description za Mawaziri ni Kufafanua Mafanikio ya Serikali kwa Wananchi.
      "SISI SOTE NI NDUGU TATIZO NI CCM" Chris Lukosi kada wa CCM



    6. #6
      Albedo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th February 2008
      Posts : 5,033
      Rep Power : 1588
      Likes Received
      1114
      Likes Given
      561

      Default Re: Ikulu Vs gazeti la Mwananchi!

      BTW: Wanaposema wanaenda kufafanua wanenda kufanya nini hasa?
      "SISI SOTE NI NDUGU TATIZO NI CCM" Chris Lukosi kada wa CCM


    7. #7
      Ochu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th May 2008
      Posts : 969
      Rep Power : 760
      Likes Received
      21
      Likes Given
      12

      Default Re: Ikulu Vs gazeti la Mwananchi!

      what is the difference between cabinet of ministers and the president? uelewa wa huyu salva ni mdogo sana...anajichanganya

    8. #8
      Zogwale's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 10th July 2008
      Posts : 6,133
      Rep Power : 6511
      Likes Received
      1253
      Likes Given
      538

      Default Re: Ikulu Vs gazeti la Mwananchi!

      Ngoma nzitoooo. Sasa nini kitafuata kwa gazeti la Mwananchi! Hivi ni nani share holders pale Mwananchi Communication Ltd. Maana RA alishaondoa zile za kwake!!!Je aliziondoa ki amani au ni kwa mikiki??!! Salva ni kibaraka wa nani Vile!!! usikute ni anguko la Mwananchi linaandaliwa maana na uchanguzi u karibu, ni lazima yabaki magazeti yale ambayo yanapigia filimbi au vibaraka wa.... malizia. Connect the dot.
      "Kama unaingia Ikulu kwa njia ya rushwa, je ni biashara gani iko huko ya kuwezesha kulipa fadhila ya rushwa hiyo???"

    9. #9
      nguvumali's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd September 2009
      Location : nimerudi Mwanza
      Posts : 3,737
      Rep Power : 1245
      Likes Received
      543
      Likes Given
      151

      Default Re: Ikulu Vs gazeti la Mwananchi!

      Quote By Ochu View Post
      what is the difference between cabinet of ministers and the president? uelewa wa huyu salva ni mdogo sana...anajichanganya
      inawezekana mpaka leo hajui kwanini yupo pale Ikulu, yeye na premi Kibanga ni waropokaji tu, ni sawa na vijana wa kijiweni.
      The most potent weapon of the oppressor is the mind of the oppressed

    10. #10
      Katavi's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 31st August 2009
      Location : Lyamba Lya Mfipa
      Posts : 19,931
      Rep Power : 16839
      Likes Received
      2650
      Likes Given
      2034

      Default Re: Ikulu Vs gazeti la Mwananchi!

      Hao mawaziri wanakuja mikoani kueleza mafanikio gani? Au ndio kampeni zimeanza!

    11. #11
      nguvumali's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd September 2009
      Location : nimerudi Mwanza
      Posts : 3,737
      Rep Power : 1245
      Likes Received
      543
      Likes Given
      151

      Default Re: Ikulu Vs gazeti la Mwananchi!

      Quote By Maane View Post
      Ngoma nzitoooo. Sasa nini kitafuata kwa gazeti la Mwananchi! Hivi ni nani share holders pale Mwananchi Communication Ltd. Maana RA alishaondoa zile za kwake!!!Je aliziondoa ki amani au ni kwa mikiki??!! Salva ni kibaraka wa nani Vile!!! usikute ni anguko la Mwananchi linaandaliwa maana na uchanguzi u karibu, ni lazima yabaki magazeti yale ambayo yanapigia filimbi au vibaraka wa.... malizia. Connect the dot.
      Lilipokua linaanza liliitikisa Serikali, hadi kufikia kutumika kwa sheria ya kazi plus zile za uhamiaji kuwatimua Wahariri na management ya wale Wakenya, hahaha.

      Ukweli hauzimwi kwa vitisho, Salva anasema uwongo, jamaa wametumwa kuandaa uwanja wa kampeni za Kikwete kwa kisingizio cha mafanikio, yeye anahubiri uongo kuwa si kweli hakuna kitu kama hicho, sijui sasa anapinga nini.
      The most potent weapon of the oppressor is the mind of the oppressed

    12. #12
      Nyauba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th July 2008
      Posts : 984
      Rep Power : 754
      Likes Received
      22
      Likes Given
      7

      Default Re: Ikulu Vs gazeti la Mwananchi!

      Kurugenzi ya mawasiliano ikulu imeendeleaa kuonyeshaa uwezo mdogo katika kuratibu mawasiliano kati ya ikulu na umma wa watanzania! hivi ningependaa kuuliza, je sifa muhimu ya kuwa mtaalamu wa mawasiliano kwa umma ni kufahamu/kusomea uandishi wa HABARI???

      uzoefu unaonyesha kwamba hapa nchini tasnia ya habari sio career of choice!!! hii ni kutokana na mfumo wetu wa kielimu ambao wachahce hapo nyuma (waliochaguliwa kwa kufauluu) hupenda zaidi kujiunga na tasnia nyingine kama sheria, uchumi,uhandisi, udaktari, na biashara kwa maana ya chagua la kwanza zaidi. Tasnia nyingine huafuatie kwa maana ya kupata nafasi ya kujiunga elimu ya juu. Uandishi wa habari na mawasiliano kwa umma ni tasnia muhimu iliyopaswaa kuwa na wajiungajii wengi wenye uwezoo wa kutathiminii na kuchambuaa mambo kwa upanaa kwa kuelewaa vema tasniaa nyingine zote.

      Inasikitishaa ikulu kama ofisi ya juu katika taifa letu inakuwaa na kitengo muhimu kama mawasiliano kwa umma chenye watendaji wavivuu kufikiri wanojivikaa ubabe, ukada na itikadii zenyee porojooo rahisii katikaa kuelimishaa umma masualaa muhimu ya Taifa letu.

      Salva Rweyemamu nasikia ni mmoja wa wakongwe wa tasnia ya habari nchini, lakini kwa kipindi chake kuongoza kurugenzi hii ya mawasiliano amejipambanuaa vizuri alivyoo na upeoo mdogoo katika utendajii wake. Je kama huyu ni mmoja wa wakongwe katika tasnia hii, waliobakiaa hali ikojee?

      Napenda kuchukua fursa hii kutoa ushauri kwa wale wote walio kwenye tasnia ya habari kurejeaa tena katika misingi ya taaluma yao na kujielekezaa kuwa na upeoo wa mbelee wenye kujenga umma ikitegemewaa umuhimu wa vyombo vya habari nchini.

      LEO YUKO SALVA IKULU, HUENDA KESHO AKATEULIWA MWINGINE MIONGONI MWAO (KWANI INAAMINIKA TANZANIA UTAALAMU WA MAWASILIANO KWA UMMA SIFA NI KUWA MWANDISHI WA HABARI) Mwalimu hakuwa na taaluma ya uandishi wa habari ila ni mmoja kati ya waandishi mahiri duniani iwe majarida, vitabu hata makala.

    13. #13
      mageuzi1992's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th April 2010
      Posts : 2,057
      Rep Power : 878
      Likes Received
      145
      Likes Given
      115

      Default Re: Ikulu Vs gazeti la Mwananchi!

      Yaani natamani 1995 ingerudi. Wakati ule kiongozi wa serikali mpaka rais akipita tulikuwa tunamuonyesha alama ya vidole viwil yaani ''V'' kiasi kwamba walikuwa wanakosa hata comfidence ya kusimamisha gari. Si mnajua wadau wakatu ule Lyatonga alikuwa na nguvu kiasi kwamba wadau wengi walimpa matumaini?. Sasa hawa mawaziri wakija; maana najua ni kampeni tu. TUWANYOOSHEE alama ya '' V ''

    14. #14
      Invisible's Avatar
      Robot Array
      Join Date : 11th February 2006
      Location : Here...!
      Posts : 9,336
      Rep Power : 100000
      Likes Received
      5036
      Likes Given
      5931

      Red face Re: Ikulu Vs gazeti la Mwananchi!

      Quote By Salva Rweyemamu

      Kama mawaziri wanakwenda mikoani kuelezea mafanikio makubwa yaliyopatikana chini ya Awamu ya Nne ya uongozi wa Tanzania ni jambo jema. Na hiyo ni sehemu ya wajibu wao na kazi zao kama mawaziri wa Serikali. Na wala siyo wafanye hivyo kwa kutumwa ama kuagizwa na yoyote. Ni wajibu wao wa kikazi na uwajibikaji.
      Si mchezo...
      Ficha Upumbavu wako; Usiifiche Hekima yako!
      24/7 Email SUPPORT: [email protected]


    15. #15
      Nemesis's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th February 2008
      Posts : 2,667
      Rep Power : 1523
      Likes Received
      34
      Likes Given
      94

      Default Re: Ikulu Vs gazeti la Mwananchi!

      Habari hii ya Ikulu inazidi kujichanganya kuliko kutoa majibu toshelevu, bado nakubaliana na Mwananchi kwani wametoa vielelezo ikiwa ni pamoja na ratiba ya mawaziri. Ni kweli kuwa Salva alisema mawaziri hawajatumwa mikoani wakati huo huo Marmo akakiri Je, huko si kupingana?

      Taarifa hii inajichanganya kwa kupiga ziara za mawaziri mikoani wakati huo huo inakubali kuwa wameenda kueleza mafanikio ya Serikali, kipi sahihi sasa? this kurugenzi is very low, nashangaa vitu vinavyotoka ikulu vipo low sana. Pale magogoni pamevamiwa!


    16. #16
      Ndibalema's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th April 2008
      Location : Mbagala
      Posts : 6,729
      Rep Power : 2030
      Likes Received
      1697
      Likes Given
      1697

      Default Re: Ikulu Vs gazeti la Mwananchi!

      Ikulu inatapa tapa sasa.

      Ninavyoifahamu mimi Ikulu ,laiti kama Mwananchi waliandika habari za kupotosha na za uongo ni lazima wangechukua hatua za gazeti hilo kufungiwa.

      Mnakumbuka gazeti la Mwana Halisi?

      Wasitudanganye, ni swala ambalo lipo wazi Mawazili wanazunguka mikoani kufanya kampeni za kijanja kijanja.

      Hilo hata Rais mwenyewe akilikanusha haisadii kwani wananchi wana akili timamu.
      "Makalio ya sufuria hayaogopi moto"

    17. #17
      Nyumbu-'s Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th May 2009
      Posts : 672
      Rep Power : 647
      Likes Received
      67
      Likes Given
      212

      Default Re: Ikulu Vs gazeti la Mwananchi!

      Kwa hiyo Mawaziri wanaweza kukurupuka tu bila kumuaga Bosi wao? Halafu wote wanaondoka kwa kujituma katika ziara zenye mtazamo mmoja? Kweli upambe ni kazi ngumu, I am lcky siko kama Salva.

      Afadhali nile dona yangu kwa amani kuliko kugeuka kijibwa cha Wakubwa!

    18. #18
      paulss's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th August 2009
      Posts : 3,639
      Rep Power : 4411
      Likes Received
      1106
      Likes Given
      986

      Default Re: Ikulu Vs gazeti la Mwananchi!

      Jamani haya ni mambo ya mfa maji haishi kutapatapa. mbona hawajalichukulia hatua kama limekosa?
      Independent thinker
      Humu jf baadhi yetu wametengeneza haki miliki ya they way they think, you have to think like them and have drawn a line of where one has to belong, you are either "with us" or "against us", if you don't sail the same boat then you are an enemy!. -Pasco wa JF

    19. #19
      Pasco's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd September 2008
      Posts : 9,862
      Rep Power : 7377
      Likes Received
      6196
      Likes Given
      22551

      Default Re: Ikulu Vs gazeti la Mwananchi!

      Quote By Nyauba View Post
      Kurugenzi ya mawasiliano ikulu imeendeleaa kuonyeshaa uwezo mdogo katika kuratibu mawasiliano kati ya ikulu na umma wa watanzania! hivi ningependaa kuuliza, je sifa muhimu ya kuwa mtaalamu wa mawasiliano kwa umma ni kufahamu/kusomea uandishi wa HABARI???

      uzoefu unaonyesha kwamba hapa nchini tasnia ya habari sio career of choice!!! hii ni kutokana na mfumo wetu wa kielimu ambao wachahce hapo nyuma (waliochaguliwa kwa kufauluu) hupenda zaidi kujiunga na tasnia nyingine kama sheria, uchumi,uhandisi, udaktari, na biashara kwa maana ya chagua la kwanza zaidi. Tasnia nyingine huafuatie kwa maana ya kupata nafasi ya kujiunga elimu ya juu. Uandishi wa habari na mawasiliano kwa umma ni tasnia muhimu iliyopaswaa kuwa na wajiungajii wengi wenye uwezoo wa kutathiminii na kuchambuaa mambo kwa upanaa kwa kuelewaa vema tasniaa nyingine zote.

      Inasikitishaa ikulu kama ofisi ya juu katika taifa letu inakuwaa na kitengo muhimu kama mawasiliano kwa umma chenye watendaji wavivuu kufikiri wanojivikaa ubabe, ukada na itikadii zenyee porojooo rahisii katikaa kuelimishaa umma masualaa muhimu ya Taifa letu.

      Salva Rweyemamu nasikia ni mmoja wa wakongwe wa tasnia ya habari nchini, lakini kwa kipindi chake kuongoza kurugenzi hii ya mawasiliano amejipambanuaa vizuri alivyoo na upeoo mdogoo katika utendajii wake. Je kama huyu ni mmoja wa wakongwe katika tasnia hii, waliobakiaa hali ikojee?

      Napenda kuchukua fursa hii kutoa ushauri kwa wale wote walio kwenye tasnia ya habari kurejeaa tena katika misingi ya taaluma yao na kujielekezaa kuwa na upeoo wa mbelee wenye kujenga umma ikitegemewaa umuhimu wa vyombo vya habari nchini.

      LEO YUKO SALVA IKULU, HUENDA KESHO AKATEULIWA MWINGINE MIONGONI MWAO (KWANI INAAMINIKA TANZANIA UTAALAMU WA MAWASILIANO KWA UMMA SIFA NI KUWA MWANDISHI WA HABARI) Mwalimu hakuwa na taaluma ya uandishi wa habari ila ni mmoja kati ya waandishi mahiri duniani iwe majarida, vitabu hata makala.
      NYAUBA, haya uliyoyasema yamenigusa sana, kwa sababu nilishapitia fani ya habari, na kujisomea mawasiliano ya umma. Ni kweli uandishi wa habari ni sehemu ya mawasiano ya umma, ila mawasiliano ya umma ni more than uandishi wa habari.

      Kumlinganisha Salva na watangulizi wake ni kumuonea bure, Salva ameingia Ikulu wakati media imepanuka zaidi na demands ni kubwa zaidi kuliko waliomtangulia. Nakumbuka vizuri kipindi cha Mwinyi, hakuwahi kuzungumza chochote na waandishi wa habari wowote kipindi chake chote cha miaka 10 madarakani. Balozi Choks, alimaliza kila kitu.

      Kwa maoni yangu, majukumu ya mawasiliano ya Ikulu ni more than what Salva na timu yake can do. Kwa vile Salva alikuwa ni Mhariri, kuandika Press Release ndio the best he can do, nothing more, nothing less; wakati Kazi ya Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu is more than kutoa Press Release. Hawa jamaa wakijibu kitu, majibu yawe yenye substance. Mbona Salva na Premmy were dam good newsroom, wana uwezo na elimu nzuri tuu, lakini hapo Ikulu bado hawa-fit vizuri. Kuna Nini?

      Tukubali tusikubali, umefika wakati, sio Salva hawezi kazi, bali lazima ajenge capable team. Yeye aendelee kuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano, awe na wasaidizi wafuatao:

      1. Press Secretary wa Rais -
      2. Spokesperson wa Rais - Premmy?.
      3. Presidential Producer/Mtangazaji wa Ikulu - Wapate mtu toka TBC
      4. Presdential Photographer - Wapate Mtu toka Daily News/Maelezo
      5. Presidential Videographer - Wapate mtu toka Audio Visual.

      NB- Nimesuggest watu toka sehemu hizo ili wewe rahisi kuwa vetted kwa sababu ukiingia tuu ikulu lazima ama tayari ulikuwa nyoka ana lazima ugeuzwe nyoka ndio Ikulu yenyewe.

    20. #20
      Jabulani's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th March 2009
      Location : Kituo cha Polisi Jamii
      Posts : 3,049
      Rep Power : 5345
      Likes Received
      849
      Likes Given
      262

      Default Re: Ikulu Vs gazeti la Mwananchi!

      Baada ya hapo kichwa cha habari kinachopaswa kufuatia ni "Msemaji wa Rais amuumbua Waziri", maana nilidhani huyu jamaa atafafanua Marmo alimaanisha nini, kama alikuwa anatania tu au vipi.

      Sasa kwa kuwa kauli za Marmo hazijazungumziwa, sijui naye atalichukuliaje hili, kwamba alikurupuka?
      Kamanda wa Polisi Jamii - Kanda Maalumu

    Page 1 of 2 12 LastLast

    Similar Topics

    1. Gazeti la mwananchi la leo....
      By Msanii in forum Tanzania 2010-2015
      Replies: 28
      Last Post: 22nd January 2013, 09:36
    2. Heko gazeti la Mwananchi
      By Sanda Matuta in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 8
      Last Post: 25th November 2011, 11:46
    3. Replies: 137
      Last Post: 16th October 2011, 00:20
    4. Gazeti la Mwananchi na gamba la CCM!
      By Mzee wa Rula in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 5
      Last Post: 8th May 2011, 21:42
    5. Gazeti la Mwananchi na uchaguzi
      By PayGod in forum Tanzania 2010-2015
      Replies: 9
      Last Post: 11th September 2010, 15:41

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...