Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Muungano wa Tanganyika na Zanzibar; Una Faida gani na kwa manufaa ya nani?

    Report Post
    Page 40 of 41 FirstFirst ... 3038394041 LastLast
    Results 781 to 800 of 806
    1. #1
      Rev. Kishoka's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th March 2006
      Location : USA
      Posts : 4,352
      Rep Power : 2562
      Likes Received
      243
      Likes Given
      185

      Default Muungano wa Tanganyika na Zanzibar; Una Faida gani na kwa manufaa ya nani?

      Tumebakiza siku 12 kabla ya maadhimisho ya miaka 46 ya Muungano wa mataifa ya Tanganyika na Zanzibar yaliyozaa Tanzania hapo Jumatatu Aprili 26.

      Imekuwa ni jadi na utamaduni kufurahia sikukuu hii na kuwaenzi waasisi wa Muungano wetu Mwalimu Nyerere na Mzee Abeid Karume kwa matamasha, gwaride na shangwe kebekebe.

      Lakini imekuwa ni dhambi, tena yenye sumu kali kwa mtu yeyote kuhoji au kutaka kuuchambua Muungano huu.

      Lengo lango si kuuliza historia au kudadisi uhalali wa Muungano wa Tanzania bali ni faida zake na manufaa yake kutokana na mfumo wa Muungano kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania, mamlaka zilizoko kama vile Mahakama, Bunge, Baraza la Wawakilishi na ni vitu gani ambavyo ni kwa ajili ya Muungano na vipi si kwa ajili ya Muungano.

      Je kwa nini tuliweka vipengele fulani viwe masuala ya muungano na vingine visiwe?

      Je Muungano huu una maana gani ikiwa vipengele ilivyoko vinakingana na azma kuu ya kuunda Taifa lenye nguvu na umoja?

      Je Wananchi wa Tanzania, wananufaika vipi na Muungano huu na wanaathirika vipi kutokana na Muungano huu na mfumo wake?

      Je kuna haja ya kuupitia Muungano na ama kupengua vipengele fulani au kuunganisha kila kitu na kuwa na sura moja bila kutofautisha ya hili la Watanganyika au Watanzania Bara na lile ni la Wazanzibari?
      Amani Iwe Nanyi,

      Camerlengo

      Plu Camerlenghi- Revolutionary Right Reverend Kishoka

      "Any existence deprived of freedom is a kind of death." Gen. Michel Aoun

      'Who comes to give greeting to the Inkosi-kaas? Who would taste her kiss, whereof the fruit is death? I, the Woodpecker, I, the Slaughterer, I the Swiftfooted! I, Umslopogaas!"


    2. #781
      Pharaoh's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th March 2011
      Posts : 750
      Rep Power : 568
      Likes Received
      121
      Likes Given
      204

      Default

      Quote By ungonella wa ukweli View Post
      Faida nyingi wanapata wazanzibar. Yaani waruhusiwa kumiliki ardhi bara na unguja.wanaruhusiwa kugombea uongozi bara au zanzibar. Wana bunge lao, rais wao, bendera yao, wimbo wao. Nk. Lakini bado wanalalamika tu. Hawatosheki tu labda mji mku uwe zanzibar!
      Wazanzibari ni wezi na ni wanyang'anyi bila hata huruma, hebu tafuteni stori za Watanganyika wanavyonyanyaswa kwao, na isingekuwa uoga wa umma wa tanganyika kujibu (sio serikali) bunge lao lilikuwa lipitishe muswada wa kurudisha wabara wote kama wakimbizi, walisahau hao wabara wachache wameenda juzi tu na ni kwa sekta moja ya Utalii tu, na wale walioenda kupindua mwa 64, nusu yao wazanzibari pamoja na viongozi wapo bara na Mungu atunusuru kwani ni maadui wakubwa hawa, hasa hawa walioko serikalini.

    3. #782
      Pharaoh's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th March 2011
      Posts : 750
      Rep Power : 568
      Likes Received
      121
      Likes Given
      204

      Default

      Quote By Bujibuji View Post
      Wapemba wanamjua Nyerere na mchango wake kwa Zanzibar? Hebu waone MUHADHARA WA KUWAAMSHA KUELEKEYA UHURU WETU - YouTube
      Jamhuri ya Kiislamu ya Zanzibar, ndio ndoto yao, na sio yao mradi huu wa afadhili na msukumo toka Iran, Uamsho wa Waislamu ni umoja wa vikundi 35 vya kidini Zanzibar vyenye nia moja ya kujiondoa na msaada wa nje wanao, pia Serikali ya karume ilisaidia.

    4. #783
      kilucha's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 5th April 2012
      Posts : 3
      Rep Power : 0
      Likes Received
      0
      Likes Given
      2

      Thumbs up Muungano?????!!!!

      Mwenzenu ninapata kigugumizi juu ya MUUNGANO. Hivi Huu muungano ambao aka yake JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, Je, ni mali ya nani? Ni watanzania?, Wazanzibar? Watanganyika? ama rais JK? Hii katiba ambayo watanzania wanaenda kuijadili, haihusishi Jamhuri ya MUUNGANO wa Tanzania? Kama inahusu, kwa nini mambo ya MUUNGANO yasipate kujadiliwa? Hivi anyekataa MUUNGANO kujadiliwa yeye ana agenda gani ambayo watanzania haturuhusiwi kuifahamu? Maswali ni mengi lakini majibu sipati, naishia kusema Kama MUUNGANO ni mali ya UMMA basi umma uachwe ujadili mali yake, na kama MUUNGANO ni mali ya MTU binafsi Nawaomba Watanzania tusiuguse katu.

    5. #784
      Fatal5's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 1st July 2011
      Posts : 166
      Rep Power : 436
      Likes Received
      28
      Likes Given
      134

      Default Re: Kwa mara nyingine Zanzibar yauchokonoa muungano!!!

      Quote By kisu View Post
      Mi naona wajitenge, halafu tuwavamie na kugeuza kua wilaya ya pemba na zanzibar kama vile waisraeli walivyo vamia palestina.
      hata burundi na rwanda tunaweza kuivamia kirahisi kabisa tukawa na taifa kubwa ukiangalia nchi hizo ni ndogo ziko katika boda letu la Tanganyika...sijui hili jeshi letu linasubiri nini

    6. #785
      Mohammed Shossi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th January 2011
      Location : Dar es Salaam
      Posts : 3,822
      Rep Power : 1200
      Likes Received
      856
      Likes Given
      255

      Default Muungano usio na ridhaa hauna maana-*Tawfiq

      Mwanasheria Maarufu Zanzibar, Salum Tawfiq akitoa mada katika Kongamano la Kitaifa kuhusu Muungano wa Tanganyika na Zanzibar katika viwanja vya Lumumba Mjini Zanzibar

      Mimi naamini kabisa kwamba Muungano ni ridhaa baina ya Nchi mbili zilizoungana. Muungano wa Serikali mbili au viongozi wawili bila ya baraka za watu wa nchi hizo hauna maana yoyote. Hivyo iwapo upande mmoja katika Muungano utasita kuridhia kubaki katika Muungano, huo unakuwa si Muungano tena. Sasa leo ya nini kuunda Tume na kupoteza mabilioni ya fedha kujaribu kuutenganeza upya Muungano ambao tayari viashiria vyote vinaonesha Muungano ushapitwa na wakati. Si ungetosha tu kuwauliza Watanzania suala la msingi kwanza kabla ya kuingia katika gharama zisizo za lazima. Suala lenyewe: jee unautaka au huutaki? Kungekuwa na haja gani ya kutaka Muungano uwe madhubuti kama walio wengi hawautaki?

      UTATUZI WA KUDUMU WA KERO ZA MUUNGANO

      Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ambao juzi tu ulitimiza miaka 48 umejaa kero ambazo kila upande, hasa Zanzibar, unaona zimekua karaha. Muungano huu na kero zimekuwa ni vitu vinavyokwenda pamoja – huwezi kuzungumzia Muungano bila ya kuanza kutaja mapungufu yake. Katika mada hii, nitajaribu kupendekeza namna ambavyo kero hizi tunaweza kuzitatua.

      Mwalimu Nyerere akihojiwa na Gazeti la Observer la Uingereza tarehe 18 Aprili 1968 alisema:
      Kama ni Rais wa Tanzania, ni jukumu langu kulinda kuwepo kwa Jamhuri ya Muungano. Lakini iwapo umma wa Wazanzibari, bila ya kutumiwa na wageni, wakiwa na sababu zao binafsi, wakaona kuwa Muungano hauna maslahi kwao, sitoweza kuwalazimisha kubaki katika Muungano. Muungano utakuwa tayari umesita kuwepo endapo upande mmoja utaondoa ridhaa yake. (Tafsiri ni yangu).

      Nukuu hiyo ndio chimbuko la mada yangu. Katika harakati au wasemavyo siku hizi “mchakato” wa kupitishwa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya Mwaka 2011, Wazanzibari wameonesha wazi kwamba wamechoshwa na Muungano uliopo sasa. Wazanzibari walio wengi pamoja na viongozi wao, wakiwemo Mawaziri na viongozi wa dini, wamesema waziwazi kwamba Muungano huu wa miaka 48 hauna maslahi kwao. Na “Baba wa Taifa” alishaota ndoto hio; leo kero za Muungano zinaonekana zaidi kwa ndugu mdogo (Small Brother) kuliko kwa kaka mkubwa (Big Brother).
      Wapo baadhi ya Watanganyika ambao nao wamekuwa wakidai Tanganyika yao lakini hawa ni katika wachache. Waliowengi, kuwepo au kutokuwepo kwa Zanzibar katika Muungano hakuathiri chochote kwao. Hawa wanaona ukubwa wa ardhi, idadi ya watu na rasilmali nyingi walonazo zinaitoa Zanzibar kama mshiriki mwenza (equal partner) katika Muungano. Hili likichanganyika na “kero ya Wazanzibari” kila siku kufanya kelele linawafanya waone Muungano hauna maana tena kwa Tanzania.

      Wapo Watanganyika wengine wanaona Zanzibar “haina shukrani” kwa kuwa ati Zanzibar inategemea kila kitu – kuanzia chakula, nguvu kazi na hata fedha za kuendeshea nchi kutoka Bara. Hawa ndio wengi wanaosema Muungano unawanufaisha zaidi Wazanzibari na itakuwa ni kujitia kitanzi iwapo Zanzibar itajitowa katika Muungano.

      Tabaan. Kwa wote hawa basi na warudi wenyewe kwa Mwalimu Nyerere. Sasa Zanzibar na Wazanzibari washaridhika kwamba Muungano umewachosha. Kuna haja gani ya kuunda Tume ya Katiba kukusanya maoni ya wananchi?
      Sheria ya kuanzisha Tume ya Katiba imeweka hadidu za rejea au muongozo kwa Tume hiyo ambayo inategemewa kuanza rasmi kazi yake mwanzo wa mwezi wa Mei, 2012. Hadidu rejea hizi zimetajwa katika kifungu cha 8, 9 na 17 vya Sheria hiyo (Nam. 8 ya 2011). Baadhi ya majukumu yake ni:
      Kukusanya maoni ya wananchi Kutoa mapendekezo kwa kila hadidu rejea
      Kutayarisha na kuwasilisha ripoti kwa kuzingatia hadidu rejea
      Agenda kubwa kwa Wazanzibari ambayo ni suala la kuwepo au kutokuwepo kwa Muungano si miongoni mwa hadidu rejea za Tume ya Katiba. Na wakati wa kuapishwa kwa Wajumbe wa Tume Ikulu Dar es Salaam tarehe 13 Aprili 2012, Rais Kikwete alisema wazi kwamba wanaohubiri kuvunjika kwa Muungano hawatasikilizwa! Mtu ataweza kujiuliza: nini sasa faida ya kukusanya maoni kama kiini cha matatizo hutaki kijadiliwe? Katika kulijadili hili naomba tukakisome tena kitabu cha Baraza la Katiba, Zanzibar:

      Katiba Tuitakayo – Sheria ya Kuandika Katiba Mpya ya Tanzania na Suala la Muungano kwa Zanzibar, hususan Sura ya Nne (Uk.22 – 29).
      Maana yake ni kwamba kwa mujibu wa Sheria ya Tume, hata kama Wazanzibari asilimia 100 wakisema wamechoshwa na Muungano hawatasikilizwa! Hapa ndio udhaifu mkubwa wa Sheria ya Tume unapoonekana. Nini hasa faida ya kuunda Tume na kutumia zaidi ya bilioni 40 na kumalizia kwa kuongeza tu katika orodha ya kero za Muungano?
      Napenda hapa niunganishe hili la kuundwa kwa Tume ya Katiba na kupitishwa kwa Marekebisho ya 10 ya Katiba ya Zanzibar (Sheria Nam. 9/2010). Marekebisho haya yameingiza vifungu vingi ambavyo kwa maumbile yake vinaonekana vikisisitiza Utaifa (Nationhood) wa Zanzibar. Kifungu cha 1 kinasema:
      Zanzibar ni Nchi ambayo eneo la mipaka yake ni eneo lote la visiwa vya Unguja na Pemba pamoja na visiwa vidogo vilivyoizunguka na bahari yake ambayo kabla ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ikiitwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar.
      Kifungu cha 2A nacho kimetowa mamlaka kwa Rais wa Zanzibar kuigawa Zanzibar katika mikoa, wilaya na maeneo mengineyo. Pia viko vifungu vyengine vinavyoonesha dhahir kujibu kejeli ya kaka zetu wakubwa kwamba Zanzibar ni mkoa tu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Tunafahamu jinsi mara kadhaa wanasiasa wa Tanzania Bara na hata Mahkama ya juu kabisa ya Tanzania (Mahkama ya Rufaa) walivyosisitiza kwamba Zanzibar si Nchi. Kwa maana hiyo hata ukifanya njama ya kutaka kumuondoa Rais wa Zanzibar madarakani kwa mtutu wa bunduki, hiyo haitokuwa uhaini (treason).

      Ni sawa sawa na kujaribu kuiondosha Halmashauri ya Mji wa Chake Chake, si jambo la kushtua!
      Mimi naamini kabisa kitendo cha Baraza la Wawakilishi kupitisha Marekebisho hayo kimekuja katika wakati muwafaka kabisa. Unapokuwa na mwenzako ambae hafahamu lugha unayozungumza inabidi utafute lugha pekee atakayoifahamu. Kubadilisha Katiba imekuwa lugha muwafaka kuwafanya wenzetu waone nini tunataka. Marekebisho ya Katiba yameibua lawama tele kutoka kwa wanasiasa na hata miongoni mwa wanasheria mahiri wa Tanzania Bara. Wengine wamesema Muungano wa Tanzania haupo tena pale Zanzibar ilipojitangaza kuwa ni Nchi! Mie naziona hizi zote ni kelele za mlango tu.
      Kwa upande mwengine naamini Marekebisho ya Katiba ya Zanzibar ya 2010 pamoja na kuwepo kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa (GNU) ndiko kulikopelekea kaka zetu wakubwa kuleta kiini macho cha Tume ya Katiba. Kama kweli lengo la Tume ni kushughulikia kero za Muungano na kuufanya Muungano wetu kuwa madhubuti basi hilo lilipaswa kufanywa zamani sana, pale kelele za Wazanzibari na hata za makundi kama G 55 ya Tanzania Bara yalipoibuka kudai Serikali ya Tanganyika na ya Zanzibar.

      Badala yake hali ya kisiasa ikawachwa kuwa tete. Waliokosoa Muungano wakaitwa wasaliti wasioitakia mema Tanzania. Kuunda Tume ya Katiba sasa hivi ni sawa na kujaribu kuyazuia maji ya bahari yasifike ufukweni wakati wa bamvua!
      Suala la kuwepo au kutukuwepo kwa Muungano ndio suala la msingi hata kabla ya kuunda Tume. Hapa Zanzibar tunayo Sheria ya Kura ya Maoni, 2010. Bara hawana, lakini hilo haliathiri chochote. Kama alivyonukuliwa Nyerere mwanzoni mwa mada hii;

      Muungano hauwezi kuwepo endapo upande mmoja utaukutaa. Cha msingi ni kulipeleka suala hili kwa wananchi wenyewe walitolee uamuzi. Kwani viongozi wanahofu ya kitu gani? Isije ikatufika hadithi ya Abunuwasi ya kuwekwa uchi halafu tukaamini hatuonekani!
      Mimi naamini kabisa kwamba Muungano ni ridhaa baina ya Nchi mbili zilizoungana. Muungano wa Serikali mbili au viongozi wawili bila ya baraka za watu wa nchi hizo hauna maana yoyote. Hivyo iwapo upande mmoja katika Muungano utasita kuridhia kubaki katika Muungano, huo unakuwa si Muungano tena. Sasa leo ya nini kuunda Tume na kupoteza mabilioni ya fedha kujaribu kuutenganeza upya Muungano ambao tayari viashiria vyote vinaonesha Muungano ushapitwa na wakati. Si ungetosha tu kuwauliza Watanzania suala la msingi kwanza kabla ya kuingia katika gharama zisizo za lazima. Suala lenyewe: jee unautaka au huutaki? Kungekuwa na haja gani ya kutaka Muungano uwe madhubuti kama walio wengi hawautaki?
      Kwa mawazo yangu endapo Wazanzibari watasema hawautaki Muungano, dawa iliyobaki ni moja tu nayo ni kumaliza taratibu mambo ya Muungano. Udugu wa watu wetu na mahusiano ya kidiplomasia yatandelea. Marehemu Karume aliunasibisha Muungano na koti: likikubana utalivua tu. Nadhani koti la Muungano limekuwa linawabana sana Wazanzibari na lililobaki ni kulivua tu. Tukingoja sana itabidi tulichane kwani litashindwa kuvuka!
      Ahsanteni Sana
      Imetayarishwa na:
      Salum Toufiq, Wakili

      (Mada iliyotolewa katika Kongomano lililofanyika Lumumba tarehe 01 Mei 2012)

      *
      GHIBUU likes this.
      Siwezi kuikana kweli kwa kuchelea upweke wa kitambo, nikajitenga na furaha ya kweli itakayotokea pale uwongo utakapojitenga - Zitto Z. Kabwe


    7. #786
      Vunjavunja's Avatar
      Member Array
      Join Date : 18th May 2012
      Posts : 80
      Rep Power : 373
      Likes Received
      11
      Likes Given
      0

      Default Je huu ni muungano?

      Serikali ya zanzibar kuzui mchele usiingezwe Tanzania bara si wanamaana kwamba muungano hawahutambui, ili mimi sijalielewa.

    8. #787
      Power G's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 20th April 2011
      Location : Msoga Kijijini
      Posts : 2,431
      Rep Power : 1000
      Likes Received
      801
      Likes Given
      275

      Default Re: Je huu ni muungano?

      Mkuu, kwani hujui kwamba kwenye muungano cha Tanganyika ni cha wote na cha zanzibar ni chao peke yao?
      TANZANIA ITAJENGWA NA WENYE MOYO NA KULIWA NA WENYE MENO KAMA AKINA EL, JK, EC na RA

    9. #788
      Vunjavunja's Avatar
      Member Array
      Join Date : 18th May 2012
      Posts : 80
      Rep Power : 373
      Likes Received
      11
      Likes Given
      0

      Default Re: Je huu ni muungano?

      Sasa kwanini sisi wabara tusizuie bidhaa zote zinazotoka bara kuenda zanzibar?

    10. #789
      Power G's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 20th April 2011
      Location : Msoga Kijijini
      Posts : 2,431
      Rep Power : 1000
      Likes Received
      801
      Likes Given
      275

      Default Re: Je huu ni muungano?

      Quote By Vunjavunja View Post
      Sasa kwanini sisi wabara tusizuie bidhaa zote zinazotoka bara kuenda zanzibar?
      Mkuu, sisi hatuwezi kuzuia kwa sababu Chetu ni Chao, lakini Chao siyo Chetu asilani.
      TANZANIA ITAJENGWA NA WENYE MOYO NA KULIWA NA WENYE MENO KAMA AKINA EL, JK, EC na RA

    11. #790
      mkomatembo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th December 2011
      Location : Bweleo
      Posts : 1,026
      Rep Power : 643
      Likes Received
      234
      Likes Given
      1274

      Default Re: Je huu ni muungano?

      Bara michele imejaa tele, wanachokataa wao ni kusababisha KUPANDA KWA BEI ZA MCHELE, Zanzibar wapo makini na wanayoyafanya, kisa cha sukari kupanda bei ni sababu ya kutoa sukari hapa tanzania na kupelea Kenya ambapo kigunia kimoja kilikuwa kinafika mpaka LAKI, hivo kufanya sukari yote kupelekwa huko na hapa bei ikipaa kupita kiasi, wanachotaka kudhibiti wao ni bei, ikiwa wataruhusu vitu vije kuuzwa huku basi bila shaka wafanya biashara wote watavusha vitu huku na matokeao yake bei zitapaa.

      Ninapenda jinsi Shein anavofanya kazi, yupo serious na kazi zake, kila siku utaona ana vikao na watu kuhusu maendeleo ya nchi yake! jamaa hataki mchezo, na ninaamini kama ataendelea hivo basi Zanzibar itapata mafanikio bila shaka.
      Last edited by mkomatembo; 18th May 2012 at 11:06.
      takashi and mtu kitu like this.

    12. #791
      mtu kitu's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 23rd April 2011
      Posts : 123
      Rep Power : 441
      Likes Received
      27
      Likes Given
      4

      Default Re: Je huu ni muungano?

      @@@ mkomatembo

      Pia hii ni kudhibiti pia wafanya biashara ,kwani kule zenji sukari na mchele wamepunguza ushuru ,sasa hawa wa bara wanaweza kupitisha mchele na sukari kule na kukwepa ushuru kirahisi.......
      tutizame jambo kwa undani.

    13. #792
      Vunjavunja's Avatar
      Member Array
      Join Date : 18th May 2012
      Posts : 80
      Rep Power : 373
      Likes Received
      11
      Likes Given
      0

      Default Re: Je huu ni muungano?

      Kwahiyo unamana hizi ni nchi mbili tofauti kama kila upande una mahamuzi yake si bora muungano uvunjwe ili zanzibari wakawe na maendeleo mazuri kuliko kakaa na muungano ambao hau tusaidii.

    14. #793
      kookolikoo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th March 2012
      Posts : 1,974
      Rep Power : 761
      Likes Received
      284
      Likes Given
      147

      Default

      Quote By Vunjavunja View Post
      Kwahiyo unamana hizi ni
      nchi mbili tofauti kama kila upande una mahamuzi yake si bora muungano
      uvunjwe ili zanzibari wakawe na maendeleo mazuri kuliko kakaa na
      muungano ambao hau tusaidii.
      mbona hilo la nchi mbili liko wazi? katiba yao mpya inasema bayana zenj ni nchi

    15. #794
      kookolikoo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th March 2012
      Posts : 1,974
      Rep Power : 761
      Likes Received
      284
      Likes Given
      147

      Default

      Quote By Vunjavunja View Post
      Kwahiyo unamana hizi ni
      nchi mbili tofauti kama kila upande una mahamuzi yake si bora muungano
      uvunjwe ili zanzibari wakawe na maendeleo mazuri kuliko kakaa na
      muungano ambao hau tusaidii.
      mbona hilo la nchi mbili liko wazi? katiba yao mpya inasema bayana zenj ni nchi

    16. #795
      Chilisosi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th October 2008
      Posts : 1,808
      Rep Power : 0
      Likes Received
      386
      Likes Given
      498

      Default Hivi huu muungano una faida gani kwetu watanganyika? Lets be serious tunauhitaji kweli?????

      Nimekuwa nasikia makelele kutoka kwa wenzetu kila siku wanasema hatuutaki muungano lakini nikiwaangalia siwaoni kama wana faida yoyote kwetu, hivi kuna mtu anayeweza nipa jibu hawa jamaa wana faida gani kwetu kwa sababu sio tunawaacha wanatukana na kutupigia kelele kila siku. mie naona tuwasikilize halafu tupige kura tanzania nzima tusikie maoni ya wote. sio kila kukicha watu kumi wanatupigia kelele zisizokwisha halafu tunakaa kimya tu

    17. BLB is offline
      BLB
      #796
      BLB's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th November 2011
      Posts : 340
      Rep Power : 452
      Likes Received
      36
      Likes Given
      0

      Default nini faida ya muungano

      hallow wana jf,
      mi kijiswali kidogo2,
      naombeni mnikumbushe faida za muungano we2 na zanzibar....

    18. BLB is offline
      BLB
      #797
      BLB's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th November 2011
      Posts : 340
      Rep Power : 452
      Likes Received
      36
      Likes Given
      0

      Default nini faida ya muungano

      hallow wana jf,
      mi nna kijiswali kidogo2,
      naombeni mnikumbushe faida za muungano we2 na zanzibar....

    19. #798
      kwamwewe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th July 2010
      Posts : 907
      Rep Power : 5419
      Likes Received
      105
      Likes Given
      132

      Default Re: Je huu ni muungano?

      Quote By Vunjavunja View Post
      Sasa kwanini sisi wabara tusizuie bidhaa zote zinazotoka bara kuenda zanzibar?

    20. #799
      baraka moze's Avatar
      Member Array
      Join Date : 21st April 2012
      Posts : 84
      Rep Power : 377
      Likes Received
      3
      Likes Given
      12

      Default Hadi sasa faida za muungano ni zipi? Na hasarabzake ni zipi?

      Pia kuna haja ya kupiga kura ya kuukubari au kuukataa muungano?

    21. #800
      adakiss23's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd January 2011
      Posts : 1,296
      Rep Power : 685
      Likes Received
      285
      Likes Given
      33

      Default Seriously Ipi faida ya Muungano??

      Tusaidiane wadau

      Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
      Brave_Hearts

    Page 40 of 41 FirstFirst ... 3038394041 LastLast

    Similar Topics

    1. kuna siri gani katika muungano wa Tanganyika na Zanzibar?
      By mtoto mzee in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 1
      Last Post: 13th November 2011, 15:53
    2. Replies: 0
      Last Post: 10th November 2011, 12:26
    3. Replies: 7
      Last Post: 6th October 2011, 05:32
    4. Replies: 5
      Last Post: 30th April 2011, 16:49

    User Tag List

    Tags for this Topic

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...