Watanzania tunajigamba kuwa tumefanikiwa kuutokomeza usultani kwa msingi kwamba tumewarejeshea wananchi/wadau mchakato mzima wa kujipatia viongozi wao ima ikiwa ni kwa kuwachagua au kuwateua. Hata hivyo, tunahitaji ukweli wa dai hili kutokana na tabia nzima iliyomo na iliyozoeleka ndani ya CCM katika upatikanaji wa viongozi ambayo ni yenye kukinzana na na dhana yote ya hapo juu.
Dalili kwamba ndani ya CCM kuna usultani mweusi ni kutokana na tabia ya viongozi walioko madarakani ama waliowahi kuweko madarakani kuamua kwa makusudi kuwaachia jamaa zao (watoto wao) nafasi hizo kwa misingi ya kurithishana, jambo ambalo ni sifa kuu ya usultani.
Mifano hai ya kuthibitisha hoja hiyo ni kama ifuatayo:
Marehemu Abeid Amani Karume aliekuwa rais wa mwanzo wa Zanzibar amerithiwa na mwanawe Amani Abeid Karume ambae ni raisi wa sasa wa Zanzibar. Marehemu Yussuf Himid aliekuwa waziri na member wa baraza la mapinduzi amerithiwa na mwanawe Mansoor Yussuf Himid ambae ni Waziri wa nishati, ardhi na ujenzi. Mwengine ni marehemu Thabitin Kombo ambae nae pia alikuwa waziri katika serikali ya awamu ya kwanza na pia member wa baraza la mapinduzi amerithiwa na mwanawe Mahmood Thabiti kombo ambae ni naibu waziri wa habari na michezo, na kubwa lililopo sasa ni hata mzee Mwinyi nae anaonekana kwenda mbio katika kumuandaa kijana wake Dr Hussein Mwinyi ili nae aje arithi nafasi aliyokuwa nayo baba yake ya kuwa raisi wa zanzibar. Je! CCM tunataka kuwaambia watanzania kuwa hakuna watu wengine Tanzania wenye sifa ama kama walizonazo warithi hao au hata zilizo bora zaidi ya hizo na kuweza kushika nyadhifa kama hizo kwa misingi ya uwezo na uzalendo?

Reply With Quote
Follow Us Here