Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Vigogo wastaafu `wakacha'

    Report Post
    Page 2 of 2 FirstFirst 12
    Results 21 to 30 of 30
    1. #1
      Phillemon Mikael's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th November 2006
      Location : mwanza,/uk/santa clara
      Posts : 4,730
      Rep Power : 1596
      Likes Received
      915
      Likes Given
      29

      Default Miaka 48 uhuru: Absentees; Pinda, Salma, Mkapa and Former PMs

      Hapa uwanjani sherehe zinaendelea lakini sherehe hazijafana sana na pia watu wananongona kukosekana kwa waziri mkuu pinda,rais mstaafu mkapa,mawaziri wakuu wastaafu na mke wa rais mama salma kikwete.....

    2. Miaka 50

    3. BAK
      #21
      BAK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2007
      Location : Mfaranyaki
      Posts : 26,644
      Rep Power : 44973
      Likes Received
      8387
      Likes Given
      8365

      Default Re: miaka 48 uhuru: absentees-pinda,salma,mkapa,and former PM's

      Quote By Tina
      Nimesikia wananchi walijiandaa na vuvuzela na kuwazomea Fisadi! Fisadi! Fisadi!.... Wapambe wao kwenye system wamewashtua ndio maana wamekacha sherehe
      Tina, wanastahili kabisa kuzomewa kwa ufisadi walioifanyia nchi yetu. Hata mimi ningekuwepo kiwanjani kama wangezuka ningekuwa ni miongoni mwa hao wazomeaji. Imefika wakati mafisadi lazima waaibishwe kwa uroho wao wa utajiri kupitia dhamana kubwa waliyokabidhiwa na Watanzania ya uongozi.
      Let your graceful words fly out into the World, carried on winds of courage, imagination and joy. Let them inspire others to step into action

    4. #22
      Mzito Kabwela's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 28th November 2009
      Location : MPUMBULI
      Posts : 7,243
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1087
      Likes Given
      7

      Default Re: Miaka 48 uhuru: Absentees; Pinda, Salma, Mkapa and Former PMs

      ....................na mke wa rais mama salma kikwete.....[/QUOTE]

      Labda alikuwa hajamaliza kuosha vyombo

    5. BAK
      #23
      BAK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2007
      Location : Mfaranyaki
      Posts : 26,644
      Rep Power : 44973
      Likes Received
      8387
      Likes Given
      8365

      Default Re: Miaka 48 uhuru: Absentees; Pinda, Salma, Mkapa and Former PMs

      Quote By mzittokabwela
      ....................na mke wa rais mama salma kikwete.....
      Labda alikuwa hajamaliza kuosha vyombo[/QUOTE]

      Ha ha ha ha hili jina lako limeniacha hoi...LOL! umeongeza m mwanzoni na la mwishoni siyo LOL! Karibu jamvini ;)
      Let your graceful words fly out into the World, carried on winds of courage, imagination and joy. Let them inspire others to step into action

    6. #24
      Mzito Kabwela's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 28th November 2009
      Location : MPUMBULI
      Posts : 7,243
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1087
      Likes Given
      7

      Default Re: Miaka 48 uhuru: Absentees; Pinda, Salma, Mkapa and Former PMs

      Quote By Bubu Ataka Kusema
      Labda alikuwa hajamaliza kuosha vyombo
      Ha ha ha ha hili jina lako limeniacha hoi...LOL! umeongeza m mwanzoni na la mwishoni siyo LOL! Karibu jamvini ;)[/QUOTE]

      Asante Bubu

    7. #25
      Kubwajinga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd January 2008
      Location : Ilala, Tanzania 10001
      Posts : 1,638
      Rep Power : 707
      Likes Received
      72
      Likes Given
      128

      Default Re: Miaka 48 uhuru: Absentees; Pinda, Salma, Mkapa and Former PMs

      Quote By Phillemon Mikael
      Hapa uwanjani sherehe zinaendelea lakini sherehe hazijafana sana na pia watu wananongona kukosekana kwa waziri mkuu pinda,rais mstaafu mkapa,mawaziri wakuu wastaafu na mke wa rais mama salma kikwete.....
      Mama Kikwete sio ajabu kabaki USA au katangulia Denmark anakoenda mumewe mara tu akitoka uwanja wa Taifa.

      Hii familia na wapambe wao wameamua kuitafuna nchi kwa shoping na utalii na inaelekea hawathamini tena siku ya Uhuru wetu.





      Quote By Kituko
      sherehe kama hizo haziwezi kuwa na nguvu tena kwani uzalendo wa hii nchi umeshaisha, Watanzania wameshakata tamaa na viongozi wao na hakuna matumaini ya future kabisa, kadri kunavyokucha gape la utajili na umaskini ndio linazidi kukua na tunakoelekea maskini hatakuwa hana chake kabisa
      Sio uongo. Kwa nini mtu akaungue na jua uwanja wa Taifa wakati hali yake kiuchumi ni mbaya kupita kiasi ingawa anawaona waungwana wachache wakijirusha tu na mali za umma kila kukicha?

      Upinzani wanapoteza nafasi ya kuchukua nchi na kuleta mabadiliko maana wananchi wanashindwa kuwaamini kutokana na jinsi mambo yao nao yalivyo ya kibinafsi.

      Watanzania wanasononeka tu maana hawana pa kukimbilia. Inasikitisha sana.

    8. RukaaJuu Final

    9. #26
      KILITIME's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 17th November 2009
      Posts : 239
      Rep Power : 531
      Likes Received
      11
      Likes Given
      11

      Talking Re: Miaka 48 uhuru: Absentees; Pinda, Salma, Mkapa and Former PMs

      Quote By mzittokabwela
      Labda alikuwa hajamaliza kuosha vyombo
      Sio kwamba kimekatikia? Ha ha haaa, just kidding!

    10. #27
      Phillemon Mikael's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th November 2006
      Location : mwanza,/uk/santa clara
      Posts : 4,730
      Rep Power : 1596
      Likes Received
      915
      Likes Given
      29

      Default Re: Miaka 48 uhuru: Absentees; Pinda, Salma, Mkapa and Former PMs

      Quote By mzittokabwela
      Ha ha ha ha hili jina lako limeniacha hoi...LOL! umeongeza m mwanzoni na la mwishoni siyo LOL! Karibu jamvini ;)
      Asante Bubu[/QUOTE]


      Kweli safari hii tunashuhudia ze comedy!

    11. BAK
      #28
      BAK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2007
      Location : Mfaranyaki
      Posts : 26,644
      Rep Power : 44973
      Likes Received
      8387
      Likes Given
      8365

      Default Re: Miaka 48 uhuru: Absentees; Pinda, Salma, Mkapa and Former PMs

      Quote By Kubwajinga
      Mama Kikwete sio ajabu kabaki USA au katangulia Denmark anakoenda mumewe mara tu akitoka uwanja wa Taifa.

      Hii familia na wapambe wao wameamua kuitafuna nchi kwa shoping na utalii na inaelekea hawathamini tena siku ya Uhuru wetu.







      Sio uongo. Kwa nini mtu akaungue na jua uwanja wa Taifa wakati hali yake kiuchumi ni mbaya kupita kiasi ingawa anawaona waungwana wachache wakijirusha tu na mali za umma kila kukicha?

      Upinzani wanapoteza nafasi ya kuchukua nchi na kuleta mabadiliko maana wananchi wanashindwa kuwaamini kutokana na jinsi mambo yao nao yalivyo ya kibinafsi.

      Watanzania wanasononeka tu maana hawana pa kukimbilia. Inasikitisha sana.
      Mkuu KJ, miaka ile tulikuwa tunaambiwa kwamba sisi ni mmoja ya nchi maskini sana duniani na hatuna mjomba wala shangazi wakutunusuru na hali yetu hiyo ya umaskini. Sasa tumegundua kumbe tuna utajiri wa hali ya juu ambao kama tungekuwa na viongozi bora, makini na walioweka mbele maslahi ya nchi yetu basi tungeweza kabisa kuinua viwango vya maisha ya Watanzania walio wengi kwa kiwango cha juu kabisa na kuifanya nchi yetu ipige hatua kubwa katika maendeleo.

      Bahati mbaya tuna viongozi ambao ni magoigoi ambao hawastahili kuwa hata wajumbe wa nyumba kumi kumi. Wanajibaraguza na kubwabwaja kila kukicha katika jitihada zao za kutuzuga kwamba wanaiongoza nchi kumbe hakuna lolote bali ni WIZI na UFISADI MTUPU!

      Tukiwaambia kwamba wang'atuke maana haturidhishwi kabisa na uongozi wao wanajidai kutoelewa tunaongea nini na kutuona sisi hamnazo! na hata kuthubutu kutuita Wehu!

      Watanzania tumeshachoka kudhalilishwa ndani ya nchi yetu na Viongozi mafisadi, Wahindi wanaosaini mikataba yao wenyewe bila hata muwakilishi wa Serikali na kuita ni mikataba ambayo imejaa WIZI MTUPU! Wazungu wanaoingia nchini wakiwa maskini na kuondoka wakiwa mabilionea baada ya kuiba rasilimali zetu. Mafisadi walio na kiburi cha hali ya juu ambao wanajua fika kwamba Serikali iliyo madarakani inawaogopa na kamwe haiwezi kuwafanya chochote eti kwa kuwa "nchi itawaka moto".

      Kuna kila sababu ya Watanzania kutohudhuria sherehe hizo hata uchaguzi wa mwaka ujao haitakuwa vibaya kama tukiususia. Tunaenda kuchagua chama gani na Rais gani? Kama ni kumchagua Kikwete, achaguliwe tena kwa lipi hasa kubwa alilolifanya kwa maslahi ya Watanzania tangu aingie madarakani? Kama kuchagua chama cha mafisadi si bora wapigiwe kura na mafisadi wanaowakingia kifua. Mfanyakazi na Mkulima uipigie kura CCM kwa kipi ulichofanyiwa na CCM tangu waliposhinda ushindi wa kishindo 2005!? CHADEMA walitupa matumaini kwamba angalau wanaweza kuongeza idadi ya viti vyao bungeni, sasa na wao sijui wamepatwa na yepi yarabi! Ikiwa imebakia miezi karibu 10 kabla ya uchaguzi mkuu wameanza kukashifiana hadharani na kufukuzana ndani ya chama.

      Ahhhhh! inasikitisha kweli kuona nchi yetu ikiendelea kuwa kichwa cha mwendawazimu mwaka hadi mwaka, chaguzi hadi chaguzi.


      Let your graceful words fly out into the World, carried on winds of courage, imagination and joy. Let them inspire others to step into action

    12. #29
      Indume Yene's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th March 2008
      Location : Chumbani
      Posts : 2,151
      Rep Power : 4954
      Likes Received
      334
      Likes Given
      312

      Default Re: Miaka 48 uhuru: Absentees; Pinda, Salma, Mkapa and Former PMs

      Inawezekana Lowassa alimsindikiza mkwe pamoja na binti yake kwenye Honeymoon....aaaahh aahahaha..

    13. #30
      Halisi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th January 2007
      Posts : 3,037
      Rep Power : 2178
      Likes Received
      455
      Likes Given
      243

      Default Vigogo wastaafu `wakacha'

      Wazee wastaafu ambao miaka yote hushiriki sherehe za maadhimisho ya sherehe za Uhuru, mwaka huu hawakuhudhuria, Je, hizi ni chuki na wivu tu kwa JK? ama kuna mengine zaidi? ama ni dharura tu zimeingiliana? TUJADILI



      Vigogo wastaafu `wakacha`




      Na Muhibu Said



      10th December 2009



      Yumo Mkapa, Lowassa, Sumaye na Warioba
      Wengine ni Dk Salim, Dk Salmin na Malecela




      Sherehe za maadhimisho ya miaka 48 ya Uhuru wa Tanganyika, jana zilifana lakini viongozi wengi wastaafu, akiwamo Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa na aliyekuwa Waziri Mkuu katika Serikali ya Awamu ya Nne, Edward Lowassa, kutohudhuria.
      Wengine, ambao hawakuhudhuria ni mawaziri wakuu wastaafu, Dk. Salim Ahmed Salim, Cleopa Msuya, Jaji Joseph Warioba, John Malecela na Frederick Sumaye na Rais Mstaafu wa Zanzibar, Dk. Salmin Amour na Waziri Kiongozi Mstaafu, Dk. Gharib Bilal.
      Hata hivyo, haikuelezwa sababu za viongozi hao kutohudhuria sherehe hizo, zilizoongozwa na Rais Jakaya Kikwete, katika Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam. Katika sherehe hizo, Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad na Mwenyekiti wake, Profesa Ibrahim Lipumba, walikaribishwa kuketi jukwaa kuu lililotumiwa na viongozi mashuhuri (VIP) wa mihimili ya dola, tofauti na viongozi wengine wa vyama vya siasa, ambao walikaa katika sehemu za kawaida.
      Baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani, walioshuhudiwa wakiwa wameketi katika sehemu za kawaida, wakiwamo mabalozi, mawaziri na wabunge, ni pamoja na Mwenyekiti wa United Democtaric Party (UDP), John Cheyo na Rais wa Tadea, John Chipaka.
      Jukwaa walilokaribishwa viongozi hao wa CUF kuketi ikiwa ni mara ya kwanza katika historia ya maadhimisho hayo, ni lile aliloketi Rais Kikwete, Spika wa Bunge, Samuel Sitta na Jaji Mkuu, Augustino Ramadhan.
      Viongozi wengine mashuhuri waliokaa jukwaa hilo, ni Rais wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, Waziri Kiongozi, Shamsi Vuai Nahodha, Makamu wa Rais, Dk. Ali Mohammed Shein na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano, Ali Hassan Mwinyi.
      Sherehe hizo zilipambwa na burudani mbalimbali, likiwamo gwaride la askari wa vikosi vya majeshi ya ulinzi na usalama, lililoongozwa na Brigedia Jenerali, Wilfred Kabunda.
      Pia, zilipambwa na vijana wa halaiki, wasanii wa vikundi vya maonyesho ya sarakasi na ngoma za asili kutoka Uganda, Tanzania Bara na Zanzibar.
      Fursa waliyopata viongozi hao wa CUF jana, imetafsiriwa na wengi kuwa ni sehemu ya utekelezaji kwa vitendo wa serikali wa maridhiano ya kuzika siasa za chuki na uhasama kati ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na CUF Zanzibar.
      Maridhiano hayo yalifikiwa kati ya Rais Karume, ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Maalim Seif, baada ya kufanya mazungumzo ya faragha, Ikulu ya Zanzibar, Novemba 5, mwaka huu.
      Kabla ya Maalim Seif na Profesa Lipumba kukaribishwa katika jukwaa hilo, walifika saa 3:00 asubuhi na kuketi katika sehemu ya kawaida.
      Wakati wakisubiri muda wa kuanza kwa maadhimisho hayo, viongozi wa itifaki waliwaelekeza maofisa wao kwenda kuwaondoa Seif na Lipumba sehemu hiyo na kuwakaribisha jukwaa hilo.
      Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano), Mohamed Seif Khatib, alipotakiwa na Nipashe kuzungumzia hatua hiyo alisema: “Mimi sijui hilo, kwani mimi si kiongozi wa itifaki.” Sherehe hizo zilihudhuriwa na watu mbalimbali, wakiwamo viongozi wa serikali, mashirika ya umma, mawaziri, mabalozi/wawakilishi wao, wabunge, viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama, viongozi wa dini, vyama vya siasa, kiraia, wasomi na wanaharakati wa maendeleo ya jamii na wananchi wa kawaida.
      Zilianza rasmi saa 4:15 asubuhi, mara baada ya Rais Kikwete kuwasili uwanjani hapo akiwa kwenye gari la wazi akiwa ameongozana na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Jenerali Davis Mwamunyange.
      Kabla ya hapo, wakati viongozi mashuhuri wakiwasili, uwanja mzima ulilipuka kwa kupaza sauti za “ruksa!”, “ruksa!”, “ruksa!” huku wakipeperusha bendera za taifa, alipowasili Rais Mstaafu, Mwinyi.
      Rais Kikwete alipowasili gari lake lilimzungusha uwanja mzima, ambapo alitumia fursa hiyo kuwasilimia viongozi na wananchi waliohudhuria sherehe hizo kwa kuwapungia mkono.
      Tukio hilo liliwavutia maelfu ya watu waliohudhuria, ambao walimshangilia kila upande wa uwanja alikopita.
      Baada ya kuhitimisha zoezi hilo, Rais Kikwete alipanda kwenye jukwaa dogo maalum lililotayarishwa kwa ajili yake na kupokea salamu za heshima kutoka vikosi vya majeshi ya ulinzi na usalama. Akiwa amesimama katika jukwaa hilo, alipigiwa mizinga 21 kuashiria heshima kwake kama Amiri Jeshi wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama na mkuu wa nchi.
      Tukio hilo lilifanyika sambamba na kupigwa wimbo wa taifa. Wakati wote huo, watu waliofurika uwanjani hapo, waliungana na Rais kusimama kutoa heshima zao kwa taifa.
      Baada ya hapo, Rais Kikwete alikagua gwaride la vikosi vya majeshi ya ulinzi na usalama kabla ya vikosi hivyo kupita mbele yake kutoa heshima zao za utii kwake. Vikosi hivyo vilijumuisha askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wa nchi kavu, majini na anga. Wengine, ni askari wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) wanaume na wanawake, Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU)-wanaume na wanawake, polisi wa kawaida (wanaume na wanawake) na Magereza (wanaume na wanawake).
      Vikosi vilipita mbele ya jukwaa la VIP kwa awamu mbili tofauti kwa mwendo wa taratibu na kasi na kutoa heshima zao za utii kwa Rais.
      Kivutio pekee kilikuwa kwa vikosi vya askari wanawake, ambao walishangiliwa na kutiwa moyo kwa nyimbo za “wanawake na maendeleo…” kutokana na ukakamavu na ushupavu wa hali ya juu waliouonyesha wakati wa gwaride. Askari wengine walioshangiliwa, ni wa JKT (wanawake na wanaume) na FFU kutokana na mbwembe na ukakamavu walivyovionyesha kila walipokuwa wakipita mbele ya Rais na mbele ya wananchi.
      Hata hivyo, vituko vilitokea kwa baadhi ya askari wa Jeshi la Magereza, baada ya kofia walizokuwa wamevaa kudondoka wakati wakishiriki gwaride kwa ukakamavu wa hali ya juu.
      Baadhi ya askari wa JWTZ walionekana wakisaidia kuokota kofia hizo kwa vile taratibu za jeshi haziruhusu askari aliyedondosha kitu kukiokota anapokuwa ndani ya gwaride. Tukio lingine lililojiri katika sherehe hizo, lililousu wananchi kadhaa, ambao kila baada ya dakika chache, alionekana mtu akibebwa kwenye machela, baada ya kuishiwa nguvu na kuanguka.
      Watu hao walipatiwa huduma ya kwanza katika mahema ya Shirika la Msalaba Mwekundu (Red Cross) yaliyoandaliwa uwanjani hapo.
      Ukiachilia mbali matukio hayo, sherehe hizo zilipambwa na kikundi cha halaiki kilichoundwa na vijana 1,000, wakiwamo 700 kutoka shule kadhaa za Tanzania Bara na 300 Zanzibar.
      Vijana hao wa halaiki, wakiwa wamevalia nadhifu mavazi ya rangi nyeusi, bluu na njano ya bandera ya taifa, waliingia uwanjani kwa mchakamchaka, kisha wakasalimia na kufanya mazoezi.
      Kivutio kikubwa kilikuwa kwa vijana hao, baada ya kuunda umbo la “Miaka 48 ya Uhuru” na kutamka herufi moja moja, herufi zote hizo kwa pamoja na kaulimbiu ya sherehe za mwaka huu isemayo: “Tulinde Uhuru na Amani kwa Maendeleo ya Taifa letu”.
      Vijana hao pia, waliunda halaiki ya umbo la kupiga makasia na kuvua samaki baharini, kuelezea michezo, utamaduni, kilimo kwanza, kukamua maziwa, silaha kwa ajili ya ulinzi, sarakasi, mshazari na kuimba wimbo wa “Tanzania Nakupenda”.
      Baadaye kulikuwa na tafrija Ikulu, kuanzia saa 12:30 jioni mpaka saa 2:30 usiku ikiwa ni sehemu ya maadhimisho hayo.





      CHANZO: NIPASHE
      Tanzania 'njema' inawezekana!

    Page 2 of 2 FirstFirst 12

    Similar Topics

    1. Mwinyi, Malecela na Kinana wakacha Dodoma
      By figganigga in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 19
      Last Post: 22nd November 2011, 13:57
    2. Replies: 12
      Last Post: 22nd September 2011, 16:58
    3. Wasomi wakacha madeni yao Bodi ya Mikopo.......................
      By Rutashubanyuma in forum Business & Economic Forum
      Replies: 0
      Last Post: 9th December 2010, 06:47
    4. Tetesi: Vigogo wastaafu kuingia uwanjani kumwokoa JK
      By Baija Bolobi in forum Tanzania 2010-2015
      Replies: 16
      Last Post: 7th October 2010, 21:33
    5. Wastaafu
      By Ilulu in forum Jamii Photos
      Replies: 6
      Last Post: 16th July 2010, 10:16

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...