Mauzo ya simu za mikononi kwa baadhi ya sehemu duniani yanatazamiwa kufikia bil 1 mpaka mwaka 2009 na simu za mikono zinazotumia mtandao ni nyingi zaidi ya mara 4 ukilinganisha na computer zilizounganishwa katika mtandao .
Kampuni ya Dotmobi (www.dotmobi.net) inasema theluthi mbili ya watu wote duniani wameunganishwa na simu za viganja duniani leo hii na zaidi ya nusu ya watu wote ulimwenguni wanatazamiwa kuanza kutumia simu zilizounganishwa na internet hapo mwaka 2008 .
Uchunguzi uliofanywa na IPSOS unasema kwamba 29% ya watumiaji wote wa simu za mikononi uingereza walitafuta habari na taarifa kwa kutumia simu hizo kwa mwaka 2005 , sijui idadi ya Tanzania au afrika kwa ujumla makampuni ya simu yanaweza kutueleza zaidi .
Taarifa hizi zinavutia na kutia moyo na itaanzisha njia zuri zaidi za watu kuweza kutangaza bidhaa na biashara zao zingine kwa njia ya simu za viganja ingawa hatujawahi kusikia habari sana kuhusu matangazo ya simu hizi mara kwa mara na ni kampuni chache sana zinajitokeza katika kutangaza bidhaa zao kwa njia ya simu
Mfano Tanzania tulikuwa na sherehe za sabasaba makampuni ya simu yangewekeana mkataba maalumu wa kutangaza bidhaa za watu wengine ambao wako ndani ya mabanda ya sabasaba , au mfano niko katika gari naenda mjini nikifika mbuyuni natakiwa kupata tangazo katika simu mbele yako ni office za dstv mambo kama haya
Mpaka sasa makampuni mengi ya matangazo na watangazaji wenyewe hawatilii mkazo sana kutangaza kwa njia ya simu za mikono katika ripoti moja iliyotolewa na Forrester Research inayoitwa "Interactive Marketing Channels to Watch in 2007." Inasema ni asilimia 13 tu ya watangazaji hutumia ujumbe mfupi sms na asilimia 11 tu hutuma matangazo yao katika tovuti zinazotumia WAP .
Kwa Tanzania nimeona kuna mfano livingroom , kismati sms na kampuni zingine zilizojitokeza kutangaza bidhaa zao kwa njia hii ya simu za mikono , hata televisheni ya ITV ina mchezo wake wa kipima joto sina uhakika kama hutumia zile namba kutangaza bidhaa za watu wengine au biashara zao ila kwa Celtel mfano siku fulani niliwahi kupata tangazo lao kwa simu yangu walitangaza bidhaa Fulani za cocacola .
Inavyoonekana watangazaji wengi na makampuni mengi ya simu za mikono hawana uhakika kuhusu biashara hii , pia watu wengi wanaotumia simu za mikono hawajapata elimu ya kutosha na sababu za kutangaza katika search engine za simu za mikono kama CELTEL inawateja mil 2 kwa taarifa nilizonazo sioni sababu ya kwanini washindwe .
MIPAKA NA UJUAJI WA MOBILE SEARCH
Ingawa kuna itadi kubwa ya watumiaji wa simu za mikono ambao hutembelea mitandao kadhaa ya tovuti kuna mipaka na mambo kadhaa ambayo kwa kiasi Fulani yanaweza kuzuia ukuaji wa mobile search pia .
· GHARAMA NA UENDESHAJI – usafirishaji wa taarifa toka sehemu moja kwenda kwingine inaweza kuwa ni shuguli pevu ukifananisha na mtandao wa computer , mfano niko mbuyuni napata tangazo la DSTV kesho nikienda Mbezi Beach natakiwa nipate tangazo nikokaribu na WHITESANDS hapa wataalamu wanasemaje ? ITAENDELEA
· UKUBWA WA KIOO - ( screen size )Simu nyingi zina vioo vidogo kwahiyo inampa mtumiaji wakati mgumu anapotembelea tovuti zingine kwa njia ya simu yake
· URAISI WA KUTUMIA – ( Ease of use ) kwa sababu ya udogo wa kioo ( screen ) mtumiaji anapata wakati mgumu kutafuta na kuclick vitu katika kurasa.
· CONTENT NDOGO – Watoa huduma wengi wa simu hawawapi wateja wao content zima au zote za tovuti ay huduma wanazotafuta katika mtandao
USHINDANI NA KUPANUKA KWA WIFI
Sababu ingine ambayo inaweza kuzuia ukuaji wa mobile search ni kuongezeka au kukua kwa huduma za kasi za WIFI katika sehemu nyingi , viwanja vya ndege , mahoteli , vyuo , maduka makubwa na kadhalika na wakati mwingi ni bure , hii inawafanya watu watumie laptops , PDA na zana zingine zaidi ya simu za mikono .
CLICK http://pwani.blogspot.com/2007/08/ma...le-search.html KWA HABARI ZAIDI

Reply With Quote

Follow Us Here