Wadau mmesikia haya ya Zanzibar... CUF imepigwa chenga ama ? - Page 3 - JamiiForums |The Home of Great Thinkers

Go Back   JamiiForums |The Home of Great Thinkers > Public Forums > Jukwaa la Siasa


Jukwaa la Siasa Tanzania & World Politics General Discussion Forum. You need to be registered in order to post your comment(s)


Reply
 
LinkBack Thread Tools Rate Thread Display Modes
Old 24th November 2009, 08:41 PM  
Wadau mmesikia haya ya Zanzibar... CUF imepigwa chenga ama ?
Lunyungu Lunyungu is offline 24th November 2009, 08:41 PM

Date::11/24/2009Shamhuna,Khatib watia doa shangwe ya Karume, Maalim SeifNa Salma Said, Zanzibar
Â
WAKATI Zanzibar ikiendelea kushangilia maafikiano ya kihistoria baina ya Rais Amani Abeid Karume na katibu mkuu wa CUF, Seif Sharif Hamad, juu ya uwezekano wa kuwepo kwa Serikali ya Mseto, mawaziri wawili wamejitokeza hadharani kutia doa shangwe hizo.

Wameeleza bayana kuwa Serikali ya Mseto si muhimu visiwani hapa.

Naibu Waziri Kiongozi wa Zanzibar, Ali Juma Shamhuna na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Muungano), Mohammed Seif Khatib, wametofautiana na msimamo wa Karume ambaye alisema kuwa uamuzi wa kuwa na Serikali ya Mseto ni wa Wazanzibari wenyewe.

Tamko hilo la Karume alilitoa siku chache baada ya kukutana kwa faragha na Maalim Seif, ambaye baadaye aliitisha mkutano wa hadhara na kueleza kuwa CUF imeamua kumtambua rais huyo kwa kuwa kufanya hivyo kutarahisisha mazungumzo ya kutafuta muafaka.

Lakini Shamhuna, ambaye pia ni Waziri wa Habari wa Serikali ya Mapinduzi (SMZ), alisema Zanzibar haihitaji Serikali ya Mseto wala Serikali ya Umoja wa Kitaifa, bali kinachotakiwa ni kujenga utamaduni wa kukubali matokeo ya uchaguzi ya kushinda na kushindwa.

Alisema hayo katika kipindi cha “Harakati za Kisiasa” kinachorushwa hewani kila siku ya Jumanne na kituo cha redio cha Zenji FM, ambacho kinamilikiwa na Waziri Seif.

Tamko hilo la Shamhuna lilirudiwa kwa siku tatu mfululizo; Jumapili, Jumatatu na jana asubuhi, kuonyesha kuwa hakuna haja ya ajenda hiyo ambayo imekuwa kikwazo kikubwa kwenye mazungumzo ya muafaka baina ya vyama hivyo viwili vikuu visiwani Zanzibar.
Â
“Zanzibar haihitaji Serikali ya Mseto wala Serikali ya Umoja wa Kitaifa wala serikali ya nini hapana, la msingi ni tujenge utamaduni wa kukubali kushindwa na kushinda... tukijenga utamaduni huo tutafanya kazi kwa pamoja na rais atakayeingia madarakani atachagua watu wenye uwezo wa kufanya kazi,” alisema Shamhuna.
Â
Shamhuna alisema watu wengi wanafikiri kwamba suluhisho la mgogoro wa kisiasa visiwani Zanzibar ni kuunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa na serikali hiyo ndio itakayoweza kuondoa matatizo yaliyopo, lakini hilo sio sahihi kwa kuwa hata ikiundwa serikali ya umoja matatizo bado yataendelea kuwepo.

“Masuala yaliyopo yanatokana na baadhi yetu kuweka mbele umimi na si utaifa kwa hivyo kuundwa au kutokuundwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa hakutusaidia,” alisema.

“Kadiri umimi utakavyokuwepo miongoni mwetu wana siasa, tatizo bado litaendelea. Solution (suluhisho) ni kuondoa umimi. Hakuhitajiki hotuba wala hakuhitajiki mikutano, kunataka management,” alisema Shamhuna kwa kujiamini.

Shamhuna alikwenda mbali zaidi na kusema watu wanasahau kwamba Zanzibar ni nchi ya kimapinduzi na wanadhani kwamba ni nchi ya watu kupiga kura na kutangazwa tu huku wengine wakifikiri kuwa Zanzibar ni nchi yenye watu walegevu legevu.
Â
Lakini hakufafanua anamaanisha nini, ingawa suala la mapinduzi limekuwa likizua mgogoro baina ya wafuasi wa vyama hivyo viwili, baadhi wakipinga mapinduzi hayo na wengine wakiunga mkono.

Akizungumzia urais, Shamhuna alisema Zanzibar haihitaji rais kijana wala mzee, lakini inahitaji rais meneja ambaye ataweza kuwakusanya watu wote pamoja na kukabiliana na changamoto zilizopo sasa katika visiwa vya Unguja na Pemba.
Â
“Karume anamaliza muda wake; nikiulizwa tunataka rais wa aina gani nitajibu tunataka rais meneja (kiongozi) sijui nimefahamika,” alisema waziri huyo machachari.
“Kwa hapa tulipofikia, tunataka tuwe na kiongozi meneja na sio lazima awe kijana kama wengi mnavyodhani. Zanzibar hatutaki rais kijana wala mzee, tunataka meneja ili aweze kuondoa challenges (changamoto) zote...sasa nani ana quality (ubora) ya umeneja,” alihoji.
Â
Alisema rais wa aina hiyo atachagua watu wenye kuweza kufanya kazi hata bila ya kujali ametoka wapi.
Â
“Sio huyu anatoka wapi na huyu anatoka wapi watu ni inclusive government (serikali inayojumuisha) na sio idadi ya watu kutoka chama cha siasa... tufanye hivyo kwa matakwa yetu na sio kulazimishwa, hapo tutajenga umoja na tutafanya kazi.”
Â
Shamhuna alisema mbio za urais kwa ajili ya uchaguzi wa mwaka 2010 tayari zimeshaunda makundi zaidi ya matatu na kwamba tayari wapo watu wameshaanza kupigia debe viongozi wao. Alisema watu hao wameanza kutoa lugha za vitisho kuwa mgombea wa kundi lao asipopitishwa na CCM, hawatakipigia kura chama hicho.
Â
“Tunawasikia wanasema hivyo wengine wanasema sasa ni zamu yetu; wengine wanasema sisi vijana tuchagueni ili tufanye mabadiliko ya nchi; wengine wameamua kunyamaza kimya; tegemeo lao hatulijui. Sasa tuna makundi matatu mpaka manne hivi yanayotafuta urais wa Zanzibar,” alisema Shamhuna. Â
Â
Akizungumzia suala linalopendekezwa na baadhi ya watu kuwa safari hii rais atoke Pemba ili kupunguza joto la kisiasa, Shamhuna aliwaita watu wenye mapendekezo hayo kuwa wamefilisika kisiasa.
Â
“Zanzibar hatuchagui rais kwa zamu na suala la kusema sasa zamu yetu Wapemba; zamu yetu  Waunguja limekwisha. Hiyo ni hoja batili na anayezungumza lugha hiyo sijui nimuite kwa lugha gani,” alisema Shamhuna.
Â
“Rais Amani anaondoka na Rais Kikwete anaendelea kipindi cha pili na hapa mitazamo tofauti kwa kuwa anayeondoka anataka arithiwe na ni nani huyo wa kurithi?

“Muungano unataka apatikane mtu kutoka Zanzibar ambaye ataweza kufanya naye kazi hivyo ndio mitizamo miwili ya msingi hii, mitizamo ya kuwa anatoka Pemba au Unguja ni mitizamo ya umimi na huko ni kufilisika kisiasa kwa jinsi navyoangalia suala hilo haraka haraka.”
 Â
Naye Waziri Seif, ambaye anatajwa kama mmoja wa watu wanaoweza kujitokeza kuwania urais wa Zanzibar, aliwaambia wananchi wa kisiwani Pemba wiki hii kwamba umoja wa Wazanzibari hauhitaji kushirikishwa chama kingine chochote kwa kuwa CCM pekee inaweza kuweka umoja na mshikamano kwa kuwa hiyo ndio sera ya chama hicho.

Aliwaambia wananchi wa kisiwa hicho kwamba MwanaCCM wa Pemba anakuwa ni CCM wa kweli kweli kwa kuwa wanakabiliana na mambo mbalimbali yanayofanywa na wapinzani, lakini wameweza kumudu na kuvumilia bila ya kutoka katika chama hicho.

“Nikwambieni ndugu zangu kuwa katika suala la umoja hakuna haja ya kushirikiana na chama kingine kwani CCM wenyewe tunaweza sana kuwaunganisha Wazanzibari wote. Na huku Pemba, CCM anakuwa wa kweli kweli maana vitimbi na vituko anavyofanyiwa na wafuasi wa CUF ni vingi, lakini bado anaweza kubakia kuwa CCM, hilo si jambo dogo,” alisema Khatib katika kipindi kilichorushwa na Zenj FM wakati wa ziara yake kisiwani Pemba.

Hii ni mara ya pili kwa Waziri Shamhuna kupingana na viongozi wakuu wa nchi katika kipindi cha miaka mitatu. Oktoba 5, 2006 Shamhuna alipingana na Rais Kikwete kuhusu suala la mwafaka wa Zanzibar.

Wakati Rais Jakaya Kikwete akisema utatuzi wa mpasuko wa kisiasa Zanzibar umefikia mahali pazuri, Shamhuna, aliibuka na kusema kamwe serikali ya umoja wa kitaifa au ya mseto haitaundwa visiwani.

Shamhuna alitoa msimamo alipokuwa akiwahutubia viongozi wa ngazi mbalimbali na wazee wa CCM wa Kikombweni Wilaya ya Kaskazini A, Unguja na hotuba hiyo kutangazwa na vyombo vya habari vya SMZ.
 "Hakuna Serikali ya Mseto itakayoundwa nchini kama inavyodaiwa na viongozi wa chama cha upinzani," alisema Shamhuna.
Facebook

Lunyungu
JF Senior Expert Member
Points: 1,697,655, Level: 100 Points: 1,697,655, Level: 100 Points: 1,697,655, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
Join Date: Tue Dec 2006
Location: Malampaka
Posts: 4,706
Thanks: 1
Thanked 205 Times in 111 Posts
Views: 624
Reply With Quote
  #21  
Old 25th November 2009, 09:31 AM
K4jolly K4jolly is offline
K4jolly has no status.
JF Premium Member
Points: 67,229, Level: 100 Points: 67,229, Level: 100 Points: 67,229, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Thu May 2009
Posts: 362
Thanks: 30
Thanked 64 Times in 43 Posts
Rep Power: 21
K4jolly will become famous soon enoughK4jolly will become famous soon enoughK4jolly will become famous soon enoughK4jolly will become famous soon enoughK4jolly will become famous soon enoughK4jolly will become famous soon enoughK4jolly will become famous soon enoughK4jolly will become famous soon enough
Default Re: Wadau mmesikia haya ya Zanzibar ? CUF imepigwa chenga ama ?

Quote:
View Post

Lakini Shamhuna, ambaye pia ni Waziri wa Habari wa Serikali ya Mapinduzi (SMZ), alisema Zanzibar haihitaji Serikali ya Mseto wala Serikali ya Umoja wa Kitaifa, bali kinachotakiwa ni kujenga utamaduni wa kukubali matokeo ya uchaguzi ya kushinda na kushindwa.
Shamhuna kamaliza kazi. Hivi Seif kwanini ameogopa uchaguzi mapema hivyo?? Nadhani alijua tiyari kisha shindwa wacha aombe vyeo vya bure.
Reply With Quote
  #22  
Old 25th November 2009, 12:48 PM
Pakacha Pakacha is offline
Pakacha has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 85,785, Level: 100 Points: 85,785, Level: 100 Points: 85,785, Level: 100
Activity: 3% Activity: 3% Activity: 3%
 
Join Date: Tue Apr 2008
Posts: 637
Thanks: 23
Thanked 26 Times in 23 Posts
Rep Power: 23
Pakacha will become famous soon enoughPakacha will become famous soon enoughPakacha will become famous soon enoughPakacha will become famous soon enoughPakacha will become famous soon enoughPakacha will become famous soon enoughPakacha will become famous soon enoughPakacha will become famous soon enough
Default Re: Wadau mmesikia haya ya Zanzibar ? CUF imepigwa chenga ama ?

Quote:
View Post
Nd. Masatu,
Tafadhali zihurumie mbavu zetu!!!
Hayo aliyoyasema Shamhuna ndio msimamo wa SMZ na yale ya Karume ilikuwa babaisha ***** tu! Kwa kweli inatia uchungu, Maalim Seif baada ya miaka zaidi ya 10 ndio sasa anajua maslahi ya Wa-zanzibari? Sasa zogo lote lile lilikuwa la nini? Kwa mimi Seif ndio awe wa mwanzo kupandishwa mahakamani kwa kuwarejesha nyuma Wa-zanzibari kwa ugomvi ambao kumbe sio wa kweli.
Mh!!! Ngida1. Nafikiri una point hapo ya kueleza. Hebu fafanua . Unajua sisi wengine si watu wa Zenj, lakini tuna shauku ya kuyajua yale ya ndani ya huko.
Reply With Quote
  #23  
Old 25th November 2009, 12:53 PM
Pakacha Pakacha is offline
Pakacha has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 85,785, Level: 100 Points: 85,785, Level: 100 Points: 85,785, Level: 100
Activity: 3% Activity: 3% Activity: 3%
 
Join Date: Tue Apr 2008
Posts: 637
Thanks: 23
Thanked 26 Times in 23 Posts
Rep Power: 23
Pakacha will become famous soon enoughPakacha will become famous soon enoughPakacha will become famous soon enoughPakacha will become famous soon enoughPakacha will become famous soon enoughPakacha will become famous soon enoughPakacha will become famous soon enoughPakacha will become famous soon enough
Default Re: Wadau mmesikia haya ya Zanzibar ? CUF imepigwa chenga ama ?

Quote:
View Post
Uzuri wa Shamhuna huwa ni mkweli na haumi maneno! Karume anapodai kuwa suala la serikali ya mseto anawaachia Wazanzibari wenyewe ni kuuma maneno bila kuelezea ukweli wa mambo! Seif na Libumba mmeliwa mchana kweupeee!
-Shamhuna anaongea nadharia tu kama vile Mhadhiri anayetaka kuwababaisha wanafunzi wake tena wale Undergraduates walio katika mwaka wao wa kwanza.
Reply With Quote
  #24  
Old 26th November 2009, 06:30 AM
Ustaadh's Avatar
Ustaadh Ustaadh is offline
Ustaadh says "RISE ABOVE POLITICS"
Senior Member
Points: 76,205, Level: 100 Points: 76,205, Level: 100 Points: 76,205, Level: 100
Activity: 1% Activity: 1% Activity: 1%
 
Join Date: Sun Oct 2009
Posts: 121
Thanks: 3
Thanked 49 Times in 35 Posts
Rep Power: 21
Ustaadh will become famous soon enoughUstaadh will become famous soon enoughUstaadh will become famous soon enoughUstaadh will become famous soon enoughUstaadh will become famous soon enoughUstaadh will become famous soon enoughUstaadh will become famous soon enoughUstaadh will become famous soon enough
Default Re: Wadau mmesikia haya ya Zanzibar ? CUF imepigwa chenga ama ?

Maalim na Profesa wametugeuka lakini mwisho wao hauko mbali. Yote ambayo tumekuwa tunayapigania hakuna hata moja lililotekelezwa na SMZ hivo kitendo chao cha kujikomba kwa SMZ ni usaliti wa hali ya juu. Mlioko bara mwachekelea kwani hilo ndo mlilotaka lakini CUF twasema hatutokata tamaa mpaka kieleweke hiyo ndoa ya mkeka haitadumu!
__________________
"Inawezekana tatizo la paka kwa panya lingekwisha kama paka angefungiwa kengele shingoni: taabu ni kumpata panya wa kuifanya kazi hiyo. Na panya watakuwa wajinga sana wakidhani kuwa paka watajifunga au watafungana kengele shingoni" - Mwl. J. K. Nyerere
Reply With Quote
The Following User Says Thank You to Ustaadh For This Useful Post:
Lampart (26th November 2009)
  #25  
Old 26th November 2009, 09:26 AM
Mchili Mchili is offline
Mchili Mti Safi
JF Senior Expert Member
Points: 82,245, Level: 100 Points: 82,245, Level: 100 Points: 82,245, Level: 100
Activity: 13% Activity: 13% Activity: 13%
 
Join Date: Wed Aug 2009
Posts: 374
Thanks: 118
Thanked 67 Times in 58 Posts
Rep Power: 21
Mchili will become famous soon enoughMchili will become famous soon enoughMchili will become famous soon enoughMchili will become famous soon enoughMchili will become famous soon enoughMchili will become famous soon enoughMchili will become famous soon enoughMchili will become famous soon enough
Default Re: Wadau mmesikia haya ya Zanzibar ? CUF imepigwa chenga ama ?

Kwani Karume akiamua Shamhuna ataweza kupinga? Na ndio maana kikao chao kikawa cha siri ili watu kama kina shamhuna wasivuruge mambo na kama kuna mambo ya serikali ya umoja atashangaa hivyo hivyo. Ujue serikali ya mseto ikija baadhi ya mawaziri wa sasa watapoteza kazi kwa hiyo hawataki kusikia hicho.

Binafsi naona kuheshimiana na kutendeana haki bila kujali idiology ya mzanzibar ndicho muhimu zaidi kuliko hiyo serikali ya mseto.
Reply With Quote
  #26  
Old 26th November 2009, 09:33 AM
Mchili Mchili is offline
Mchili Mti Safi
JF Senior Expert Member
Points: 82,245, Level: 100 Points: 82,245, Level: 100 Points: 82,245, Level: 100
Activity: 13% Activity: 13% Activity: 13%
 
Join Date: Wed Aug 2009
Posts: 374
Thanks: 118
Thanked 67 Times in 58 Posts
Rep Power: 21
Mchili will become famous soon enoughMchili will become famous soon enoughMchili will become famous soon enoughMchili will become famous soon enoughMchili will become famous soon enoughMchili will become famous soon enoughMchili will become famous soon enoughMchili will become famous soon enough
Default Re: Wadau mmesikia haya ya Zanzibar ? CUF imepigwa chenga ama ?

Quote:
View Post
Shamhuna kamaliza kazi. Hivi Seif kwanini ameogopa uchaguzi mapema hivyo?? Nadhani alijua tiyari kisha shindwa wacha aombe vyeo vya bure.
Seif alichofanya ni kutafuta fair play kwenye uchaguzi ujao na sio serikali ya mseto kama wengi mnavyofikiri. Unajua Pemba na Unguja wakielewana hata huo muungano wa bara hauhitajiki. Na hilo Karume na Seif wameliona na wamechoka na malumbano yasiyojenga nchi. Kwa hiyo usishangae Karume akakubali kuiachia CUF washinde uraisi mwakani japo ccm hawatapendezwa na hilo.
Reply With Quote
  #27  
Old 26th November 2009, 11:39 AM
MrFroasty's Avatar
MrFroasty MrFroasty is offline
MrFroasty Fighting for Zanzibar's freedom till the end
JF Senior Expert Member
Points: 107,692, Level: 100 Points: 107,692, Level: 100 Points: 107,692, Level: 100
Activity: 3% Activity: 3% Activity: 3%
 
Join Date: Tue Jun 2009
Posts: 418
Thanks: 21
Thanked 159 Times in 120 Posts
Rep Power: 21
MrFroasty will become famous soon enoughMrFroasty will become famous soon enoughMrFroasty will become famous soon enoughMrFroasty will become famous soon enoughMrFroasty will become famous soon enoughMrFroasty will become famous soon enoughMrFroasty will become famous soon enoughMrFroasty will become famous soon enough
Default Re: Wadau mmesikia haya ya Zanzibar... CUF imepigwa chenga ama ?

Naona watu wote munapiga kelele tuu, wengine kuonesha kuwa wao wanaogopa wazanzibari wasiungane kwa kulinda muungano...n.k

Jambo la msingi ambalo hapa limekosekana ni NIDHAMU, Shamhuna na Khatibu na Sophia ni watovu wa nidhamu.Hawa hawastahiki kutoa maoni ambayo yanapingana na kiongozi wa nchi (regardless of Pindas perspective ofcoz).

Serekali na vyama vina utaratibu wao wa kutoa msimamo, sio tuu huyu kasema vile ...nahisi kama Karume angelimchukulia hatua za nidhamu huyu Shamhuna kwa kutoa kauli zinazokwenda kinyume na uongozi wake.Otherwise wanatunganya wananchi!
__________________
MZALENDO.NET-Zanzibar na Zama za ukweli na uwazi...
Reply With Quote
  #28  
Old 26th November 2009, 01:01 PM
Lampart Lampart is offline
Lampart has no status.
Senior Member
Points: 89,387, Level: 100 Points: 89,387, Level: 100 Points: 89,387, Level: 100
Activity: 16% Activity: 16% Activity: 16%
 
Join Date: Fri Sep 2009
Posts: 138
Thanks: 394
Thanked 58 Times in 42 Posts
Rep Power: 21
Lampart will become famous soon enoughLampart will become famous soon enoughLampart will become famous soon enoughLampart will become famous soon enoughLampart will become famous soon enoughLampart will become famous soon enoughLampart will become famous soon enoughLampart will become famous soon enough
Default Re: Wadau mmesikia haya ya Zanzibar ? CUF imepigwa chenga ama ?

Quote:
View Post
.......Kwa hiyo usishangae Karume akakubali kuiachia CUF washinde uraisi mwakani japo ccm hawatapendezwa na hilo.
Hilo halitotokea na kama likitokea basi wengine tutaingia tena JOZANI!!!!
Reply With Quote
  #29  
Old 26th November 2009, 01:19 PM
Kibunango's Avatar
Kibunango Kibunango is offline
Kibunango Mapinduzi Daima...! CCM Damu.
JF Senior Expert Member
Points: 10,820,469, Level: 100 Points: 10,820,469, Level: 100 Points: 10,820,469, Level: 100
Activity: 39% Activity: 39% Activity: 39%
 
Join Date: Tue Aug 2006
Location: Tampere
Posts: 4,870
Thanks: 351
Thanked 207 Times in 169 Posts
Rep Power: 4033
Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!
Send a message via MSN to Kibunango Send a message via Yahoo to Kibunango
Default Re: Wadau mmesikia haya ya Zanzibar ? CUF imepigwa chenga ama ?

Quote:
View Post
Hilo halitotokea na kama likitokea basi wengine tutaingia tena JOZANI!!!!
Huogopi nyani wekundu?
__________________
Save Water Drink Beer. "Alcohol doesn't solve any problems,
But, if you think again, neither does milk."
Vituko Vya Zenj
Reply With Quote
The Following User Says Thank You to Kibunango For This Useful Post:
Lampart (27th November 2009)
  #30  
Old 26th November 2009, 01:48 PM
T_Tonga T_Tonga is offline
T_Tonga has no status.
Senior Member
Points: 79,769, Level: 100 Points: 79,769, Level: 100 Points: 79,769, Level: 100
Activity: 1% Activity: 1% Activity: 1%
 
Join Date: Tue Jul 2007
Posts: 83
Thanks: 0
Thanked 3 Times in 3 Posts
Rep Power: 23
T_Tonga will become famous soon enoughT_Tonga will become famous soon enoughT_Tonga will become famous soon enoughT_Tonga will become famous soon enoughT_Tonga will become famous soon enoughT_Tonga will become famous soon enoughT_Tonga will become famous soon enoughT_Tonga will become famous soon enough
Default Re: Wadau mmesikia haya ya Zanzibar... CUF imepigwa chenga ama ?

kwani shamhuna ni nani hata mumpe sifa zote hizo ungekuwa unamjua shamhuna wala usingesema kitu huyu jamaa ni msaka tonge tu na mpenda ulwa wewe huoni hata katika kamati kuu hayumo amekataliwa kwao kwenye jimbo lake amashindwa kaikosa nafasi na sasa ataikosa tena nafasi hiyo ya uakilishi shamhuna hana tofauti na huyo asha ngedere na alipokuwa hana uaziri alikuwa analia tu lakini mambo ni kangaja huwenda yakaja mtakuja ona haya
Reply With Quote
Reply

Bookmarks

Tags
ama, chenga, cuf, haya, imepigwa, mmesikia, wadau, zanzibar


Currently Active Users Viewing This Thread: 1 (0 members and 1 guests)
 
Thread Tools
Display Modes Rate This Thread
Rate This Thread:

Posting Rules
You may not post new threads
You may not post replies
You may not post attachments
You may not edit your posts

BB code is On
Smilies are On
[IMG] code is On
HTML code is Off
Trackbacks are Off
Pingbacks are Off
Refbacks are On


Similar Threads
Thread Thread Starter Forum Replies Last Post
Muungano na kero zake: Tuuvunje? Sam Jukwaa la Siasa 3855 16th February 2010 01:10 PM
Tukumbuke Zamani: Historia Ya Taifa Letu Katika Picha Field Marshall ES Jamii Photos 1261 6th January 2010 03:40 PM
Hotuba ya Seif Shariff! JokaKuu Jukwaa la Siasa 131 11th December 2009 04:12 PM
Muafaka CCM na CUF, pande mbili za shilingi! MwanaCCM Jukwaa la Siasa 148 13th July 2009 10:13 AM
Islam and the catholic crusade movement in zanzibar Shy Habari na Hoja mchanganyiko 6 19th September 2008 06:28 PM

Tuma Ukurasa huu kwa rafiki yako!


All times are GMT +3. The time now is 04:44 PM.

Powered by JamiiForums.com
Copyrights reserved to JamiiForums.com