Wakati Bunge la Jamuhuri muungano likiendelea kupiga mbiu kuhusu bajeti, wafanyakazi wa serikali wameendamana kupinga kima cha chini cha shiling 84,000
Kwa mtu mwenye maono madogo ambaye afahamu Tanzania anaweza sema 84,000 ina tosha, lakini kwa mtu mwenye upeo wa kufikiri hujiuliza kwanza, ni kiasi gani thamani ya pango nchini Tanzania, jee mlipuko wa bei (inflation) ukoje, jee kiasi hiki ni kwa watu gani, wanafunzi au wana familia? na maswali mengine mengi.
Kinacho sikitisha ni kuona wabunge wanazidishiwa mishahara kwa kazi isiyo ya maana wanayo fanya. Nini bunge la Tanzania linafanya? kuuza Madini kwa bei nafuu, kumruhusu Mkapa kununua ndege au Lowasa kusaini mkataba na Kampuni hewa ya Richmond? Hakuna mtu anayeweza kulitetea bunge hilo lililo na tabia ya mwenda wazimu, kuropoka pasipo sababu.
Kuwalipa watu wenye familia shilling 84000 ni kuwatukana matusi, 84,000 ni theluthi ya matumizi Lowasa na mawaziri wake.
Swala linalo sikitisha ni kwamba mueshimiwa Kikwete, amabaye mara zote hupiga mbiu kwamba anatetea walala hoi safari hii ameamua kuwalalia walala hoi. Kinacho nishangaza ni kwamba hawa mna walipa 84000 wakati nyinyi mkijiongezea millioni za fedha ndio walio wachagua kuwaweka madarakani.
Nini hadhari za kiwangoi kidogo hiki, moja corruption will hike in high percentage every single day, sidhani kama kuna kiongozi atakeye thubutu kufungua mdomo wake na kusema chochote kuhusu rushwa wakati mfanyakazi analipwa 84000.
Madhara ya pili, less utilizing of labor skills, huwezi kumplipa mtu shilling 84000 kisha ukategemea awe productive 100%, huo utakuwa ni wendawazimu na kama sio uchizi, the effect of this is reduction of human production which cause effects on public.
Muda umefika wa bunge mbiu kuwa bunge vitendo, nakuacha mabishano kama watoto wa kike wa miaka 10 wanapobishana kwamba nani ni mchumba wa nani.

Reply With Quote

Follow Us Here