Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Tanzania inahitaji Wizara ngapi?

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 28
    1. #1
      Mwanagenzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th September 2006
      Location : Mtandaoni
      Posts : 762
      Rep Power : 806
      Likes Received
      10
      Likes Given
      10

      Default Tanzania inahitaji Wizara ngapi?

      What is the optimal size for the cabinet for Tanzania?

      Kumekuwa na mjadala kuhusu ukubwa wa baraza la mawaziri la serikali ya awamu ya nne. Kwa sasa baraza lina wizara 22. Kuna manaibu waziri 30. Pia kuna mawaziri wa nchi 7 (chini ya ofisi ya rais, makamu wa rais na waziri mkuu). Kwa ujumla, baraza la mawaziri lina watu zaidi ya 60, ukiongeza na makamu wa rais, rais wa Zanzibar, rais mwenyewe na mwanasheria mkuu wa serikali.

      Je, tuna wizara nyingi mno bila sababu?
      Je, kuna haja ya kuwa na manaibu waziri?
      Inawezekana kuwa na wasaidizi wa mawaziri lakini wasio na ngazi au hadhi ya waziri, hivyo kupunguza gharama?

      Rais anatumia vigezo vya changamoto na mahitaji ya taifa kama msingi mkuu wa uundwaji wa baraza au anatumia hoja ya uwakilishi wa watu (jinsi (sex-as opposed to jinsia ambayo ni gender), kanda (geographical coverage and tribal balance), na dini (uislam vs ukristo)? Au pengine ukada, urafiki na kulipa fadhila?

      Je, inawezekana suala la wizara zipi ziwepo katika serikali likawekwa kama suala la kudumu angalau kwa miaka 10 hivi likiendana na dira ya taifa, badala ya rais kuongozwa na visheni binafsi au ilani ya chama chake (wakati mwingine hizi mbili zaweza kutofautiana!) bila ya kujali rais atatoka kwenye chama kipi?
      Nadhani hii itasaidia hata wananchi wote kujua nini kipaumbele cha taifa! Na pia itapunguza uwezekano wa rais kujiundia baraza kwa matakwa yake binafsi badala ya taifa, kadhalika malalamiko kutoka kwa wadau na wananchi kwa ujumla.

      Binafsi, naona kuwa mtu au nchi maskini zinakuwa na matatizo mengi kiasi kwamba kila kitu kina kuwa "priority" na hii inachangia kuwa na serikali kubwa kwa matarajio kuwa kwa kufanya hivyo serikali itaweza kuwafikia na kuwahudumia wananchi wake kwa ufanisi zaidi. Ndiyo maana unakuta karibu kila suala lina wizara yake badala ya kusema wizara moja ishughulikie masuala kadhaa kwa wakati mmoja. Hii ni changamoto. Tusipoangalia tutakuta siku moja tuna wizara ya ukimwi, wizara ya ukame, wizara ya kuzuia rushwa, wizara ya kero za wanafunzi (mimba na usafiri), wizara ya kushughulikia migogoro nk.

      Angalia baadhi ya nchi na wizara zao (idadi):
      Marekani 15 (mwaka 1901 walikuwa na wizara 9 tu pamoja na AG),
      Uingereza 22 (Blair alikuwa na 23),
      Ujerumani 14,
      Kanada 27 (wakati wa Waziri Mkuu Brian Mulroney walikuwa na 40),
      Ufaransa 15 (Chirac alikuwa na 30)
      Israel 27 (mawaziri kutoka vyama vitano vya siasa)
      Japan 17 (mawaziri - wakiwemo mawaziri wa nchi)
      China - mawaziri 28 - wakiwemo mawaziri wa nchi
      India - mawaziri 23 na mawaziri wa nchi 32, kwenye serikali kuu. Hata hivyo kila jimbo lina wizara zake na jimbo kama Utar Pradesh linaongoza kwa wingi wa mawaziri (105) wakati jimbo la Pondicherry lina wachache kabisa (5). Wenye sera ya majimbo mpo!!

      Naijeria - mawaziri 23 na mawaziri wa nchi 45 (rais mwenyewe anaongoza wizara 2)
      Misri 30
      Aljeria mawaziri 38 (wakiwemo mawaziri kamili 29)
      Ghana wizara 12
      Zambia wizara 23 (lakini Zambia pia kuna mawaziri wa majimbo na mawaziri wa wilaya!)
      Kenya wizara 25, mawaziri wa nchi 8
      Afrika Kusini wizara 28 (manaibu 21)
      Uganda - licha ya makamu na waziri mkuu, waziri mkuu ana manaibu 3, kuna wizara kamili 22, na mawaziri wa nchi 43. Hivyo baraza zima na rais wake wako 72 (bila Mwanasheria Mkuu)
      ____________
      Ili Tuendelee Tunahitaji Dikteta mwenye Uzalendo na Visheni
      _____________
      "UTU BUSARA UJINGA HASARA,
      "TUPINGANE BILA KUPIGANA"


    2. #2
      Ilongo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th February 2007
      Posts : 431
      Rep Power : 716
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Nielimishe kidogo

      Quote By Mwanagenzi View Post
      What is the optimal size for the cabinet for Tanzania?

      Kumekuwa na mjadala kuhusu ukubwa wa baraza la mawaziri la serikali ya awamu ya nne. Kwa sasa baraza lina wizara 22. Kuna manaibu waziri 30. Pia kuna mawaziri wa nchi 7 (chini ya ofisi ya rais, makamu wa rais na waziri mkuu). Kwa ujumla, baraza la mawaziri lina watu zaidi ya 60, ukiongeza na makamu wa rais, rais wa Zanzibar, rais mwenyewe na mwanasheria mkuu wa serikali.

      Je, tuna wizara nyingi mno bila sababu?
      Je, kuna haja ya kuwa na manaibu waziri?
      Inawezekana kuwa na wasaidizi wa mawaziri lakini wasio na ngazi au hadhi ya waziri, hivyo kupunguza gharama?

      Rais anatumia vigezo vya changamoto na mahitaji ya taifa kama msingi mkuu wa uundwaji wa baraza au anatumia hoja ya uwakilishi wa watu (jinsi (sex-as opposed to jinsia ambayo ni gender), kanda (geographical coverage and tribal balance), na dini (uislam vs ukristo)? Au pengine ukada, urafiki na kulipa fadhila?

      Je, inawezekana suala la wizara zipi ziwepo katika serikali likawekwa kama suala la kudumu angalau kwa miaka 10 hivi likiendana na dira ya taifa, badala ya rais kuongozwa na visheni binafsi au ilani ya chama chake (wakati mwingine hizi mbili zaweza kutofautiana!) bila ya kujali rais atatoka kwenye chama kipi?
      Nadhani hii itasaidia hata wananchi wote kujua nini kipaumbele cha taifa! Na pia itapunguza uwezekano wa rais kujiundia baraza kwa matakwa yake binafsi badala ya taifa, kadhalika malalamiko kutoka kwa wadau na wananchi kwa ujumla.

      Binafsi, naona kuwa mtu au nchi maskini zinakuwa na matatizo mengi kiasi kwamba kila kitu kina kuwa "priority" na hii inachangia kuwa na serikali kubwa kwa matarajio kuwa kwa kufanya hivyo serikali itaweza kuwafikia na kuwahudumia wananchi wake kwa ufanisi zaidi. Ndiyo maana unakuta karibu kila suala lina wizara yake badala ya kusema wizara moja ishughulikie masuala kadhaa kwa wakati mmoja. Hii ni changamoto. Tusipoangalia tutakuta siku moja tuna wizara ya ukimwi, wizara ya ukame, wizara ya kuzuia rushwa, wizara ya kero za wanafunzi (mimba na usafiri), wizara ya kushughulikia migogoro nk.

      Angalia baadhi ya nchi na wizara zao (idadi):
      Marekani 15 (mwaka 1901 walikuwa na wizara 9 tu pamoja na AG),
      Uingereza 22 (Blair alikuwa na 23),
      Ujerumani 14,
      Kanada 27 (wakati wa Waziri Mkuu Brian Mulroney walikuwa na 40),
      Ufaransa 15 (Chirac alikuwa na 30)
      Israel 27 (mawaziri kutoka vyama vitano vya siasa)
      Japan 17 (mawaziri - wakiwemo mawaziri wa nchi)
      China - mawaziri 28 - wakiwemo mawaziri wa nchi
      India - mawaziri 23 na mawaziri wa nchi 32, kwenye serikali kuu. Hata hivyo kila jimbo lina wizara zake na jimbo kama Utar Pradesh linaongoza kwa wingi wa mawaziri (105) wakati jimbo la Pondicherry lina wachache kabisa (5). Wenye sera ya majimbo mpo!!

      Naijeria - mawaziri 23 na mawaziri wa nchi 45 (rais mwenyewe anaongoza wizara 2)
      Misri 30
      Aljeria mawaziri 38 (wakiwemo mawaziri kamili 29)
      Ghana wizara 12
      Zambia wizara 23 (lakini Zambia pia kuna mawaziri wa majimbo na mawaziri wa wilaya!)
      Kenya wizara 25, mawaziri wa nchi 8
      Afrika Kusini wizara 28 (manaibu 21)
      Uganda - licha ya makamu na waziri mkuu, waziri mkuu ana manaibu 3, kuna wizara kamili 22, na mawaziri wa nchi 43. Hivyo baraza zima na rais wake wako 72 (bila Mwanasheria Mkuu)

      Mwanagenzi,

      Nini maana ya mawaziri wa nchi? Tofauti kati yao na mawaziri nini? Na je, Nigeria ina jumla ya mawaziri wangapi kwa usahihi kabisa (kama ulivyofanya kwa Uganda)?
      Abstinence is the only key to no regrets!

    3. #3
      Mwanagenzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th September 2006
      Location : Mtandaoni
      Posts : 762
      Rep Power : 806
      Likes Received
      10
      Likes Given
      10

      Default

      Ilongo,
      Unauliza tafsiri yake kwa Kiingereza? Kama ni hivyo Waziri wa Nchi ni Minister of State!
      ____________
      Ili Tuendelee Tunahitaji Dikteta mwenye Uzalendo na Visheni
      _____________
      "UTU BUSARA UJINGA HASARA,
      "TUPINGANE BILA KUPIGANA"

    4. Shy is offline
      Shy
      #4
      Shy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd November 2006
      Posts : 4,922
      Rep Power : 0
      Likes Received
      76
      Likes Given
      0

      Default

      Kwanza mawaziri wote wawe wa kuajiriwa kutokana na ujuzi wao , wabunge wawe wanafanya kazi huko huko katika sehemu zao walizochaguliwa na wananchi wao , haiwezekani mtu kama sumaye alikuwa mbunge wa hanang hapo hapo waziri mkuu angalia umbali wa hanang na dar - sasa unategemea shuguli za maendeleo hanag zinaendeleaje ? labda kwa mtandao siku hizi

      Kunatakiwa wizara chache ambazo chini zinatakiwa zinyambulishwe kwa vikundi vidogo kidogo kutokana na matakwa au sera za wizara hiyo halafu waziri ndio aajiri makatibu wakuu wake na wasaidizi wake wengine kutokana na sifa walizonazo

      Naamini uwaziri ukiwa wa kuajiriwa basi hata mgombea wa upinzani anaweza kuomba nafasi ya uwazi kama anasifa hizo lakini anatakiwa aachane na chama chake yaani siasa na afanye kazi kwa masilahi ya taifa kwa ujumla

      huo ndio mchango wangu kwa usiku wa leo

    5. #5
      Field Marshall ES's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 27th April 2006
      Posts : 13,740
      Rep Power : 0
      Likes Received
      329
      Likes Given
      208

      Default

      Mzee Mwanangezi,

      Nafikiri cha muhimu katika kuhukumu namba ya baraza la mawaziri wa Muungwana, ni kazi walioifanya so far, kama ni nzuri au mbaya, au hairidhishi,

      Than yes, tunaweza kuongelea the fairness ya idadi ya wizara na mawaziri!


    6. #6
      Ilongo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th February 2007
      Posts : 431
      Rep Power : 716
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By Mwanagenzi View Post
      Ilongo,
      Unauliza tafsiri yake kwa Kiingereza? Kama ni hivyo Waziri wa Nchi ni Minister of State!
      Ni kwa vile naona unatofautisha kwa kusema mawaziri ... (idadi) na mawaziri wa nchi ... (idadi). Kwa hiyo nilitaka nijue tofauti ni nini hasa, wanakuwa categorized vipi kiutendaji?

      Lakini tukiachana na hilo, je nikisema kwamba Nigeria inazo wizara 25 na mawaziri 68 nitakuwa sahihi ama hapana?
      Abstinence is the only key to no regrets!

    7. #7
      Kasheshe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th June 2007
      Location : Bububu
      Posts : 3,630
      Rep Power : 1351
      Likes Received
      196
      Likes Given
      344

      Default

      Hoja yangu kubwa katika hili for long run, sio idadi kwa kuwa idadi ni matokeo tu ya mfumo mbaya wa Katiba, Uteuzi n.k wa Mawaziri,

      Maswali yangu yangekuwa Wanateuliwa je? Wanasifa gani? Wana nguvu gani ya maamuzi? Je watoke kwenye wabunge au watoke nje ya Bunge? je wapitishiwe bungeni kupitishwa kama ilivyo kwa waziri mkuu? Je wana nguvu gani... Je wapunguziwe madaraka?,,, tukijibu maswahili haya yote kwa uzalendo na sio hisia za kichama kushika hatamu,,, we will endup on 13-25 ministries... hence jibu lako litakuwa rahisi zaidi...

      Shangazi yangu aliwahi kuniasa siku moja kwamba,,, "ukijikwaa kidole na kuanguka, usiangalie kule ulikoangukia bali pale ulipojikwaa"

      Swahili hili linaangalia tulipoangukia sio tulikojikwaa kidole chetu...

      Mahojiano mema.

    8. #8
      Mwanagenzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th September 2006
      Location : Mtandaoni
      Posts : 762
      Rep Power : 806
      Likes Received
      10
      Likes Given
      10

      Default

      Komandoo ES,
      Kwa hiyo tusubiri miaka mitano ndiyo tuone kama tunahitaji wizara za namna gani??

      Je, kama wizara 15, kwa mfano, zingeweza kutuongoza kwa ufanisi huo huo, si tungekuwa tumepunguza gharama?

      Akija rais mwingine baada ya hapo naye apangue wizara? Ikumbukwe kuwa hili nalo lina gharama zake (ajira kwa watumishi, ofisi na samani nk).

      Mfano, bajeti ya 2005/2006 (kabla ya uchaguzi)ilipangwa kiasi cha kuweza kuhimili ukubwa wa serikali ya awamu ya nne iliyoundwa Januari 2006?

      Ndiyo maana napendekeza kuwa na dira fulani ya kitaifa kuhusu ukubwa wa serikali kwa kuzingatia vipaumbele na changamoto zilizopo.
      ____________
      Ili Tuendelee Tunahitaji Dikteta mwenye Uzalendo na Visheni
      _____________
      "UTU BUSARA UJINGA HASARA,
      "TUPINGANE BILA KUPIGANA"

    9. #9
      MzalendoHalisi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th June 2007
      Posts : 4,049
      Rep Power : 1422
      Likes Received
      106
      Likes Given
      208

      Default Set National Priorities 1st

      Wandugu,
      As a nation we need to identify our national priorities first for 1st 10 years! Then for next 10 year period! Our cabinet then will depend on what pressing priorities have been identified based on some criteria!

      Initially I will go for a small government on the following areas
      1. National Defence and Security
      2. Services Sector- Heath,
      3. Services Sector Education (including higher learning)
      4. Finance and Planning
      5. Infrastructure and Communication
      6. Minerals, energy, natural resources & tourism
      7. Agricultural sector development
      8. Trade, Industries, Coo-operatives
      9. Vocational Training, skills development, technology & Science
      10. Local Government and Regional Administration
      11. Foreign Affairs
      12.
      13.
      15.

      I would start with 15 Ministries. Each with a Deputy Minister total 30 i.e. half of preset Cabinet.

    10. #10
      Mwanagenzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th September 2006
      Location : Mtandaoni
      Posts : 762
      Rep Power : 806
      Likes Received
      10
      Likes Given
      10

      Default

      Quote By ilongo View Post
      Ni kwa vile naona unatofautisha kwa kusema mawaziri ... (idadi) na mawaziri wa nchi ... (idadi). Kwa hiyo nilitaka nijue tofauti ni nini hasa, wanakuwa categorized vipi kiutendaji?


      Lakini tukiachana na hilo, je nikisema kwamba Nigeria inazo wizara 25 na mawaziri 68 nitakuwa sahihi ama hapana?



      Mawaziri wa nchi (ministers of state) wanakuwa sawa na manaibu waziri kiutendaji. Mpaka juzi juzi tu hapa Kenya walikuwa wakitumia jina la Waziri Msaidizi (Assistant Minister) lakini mawaziri hao wamepinga jina hilo wakidai linawadhalilisha na hivyo wamebadilishiwa na sasa wanatumia hilo la Waziri wa Nchi. Kumbuka hata kwa Tanzania kila waziri ana msaidizi wake (personal assistant) ambaye si waziri bali katibu myeka na hivyo hao wenzetu walilichukulia kwa mwanga huo.



      Hakika unaweza kuwa sahihi. Kwa mfano, hata sisi tuna wizara 22 lakini mawaziri, kwa maana ya kujumuisha mawaziri kamili, mawaziri wa nchi na manaibu waziri, unapata zaidi ya 50.
      ____________
      Ili Tuendelee Tunahitaji Dikteta mwenye Uzalendo na Visheni
      _____________
      "UTU BUSARA UJINGA HASARA,
      "TUPINGANE BILA KUPIGANA"

    11. #11
      omarilyas's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th January 2007
      Location : Morogoro
      Posts : 2,495
      Rep Power : 1137
      Likes Received
      69
      Likes Given
      5

      Default

      Tunahitaji mawaziri kadiri ya mahitaji ya kisiasa, kijamii na kiuchumi.....number not issue ya kutuumiza kichwa bali mfumo unaotumika kupata hao mawaziri ndio muhimu zaidi...kama kula watakula tu hata kama una mawaziri watano tu...

      Vilevile mafao yao kuwekwa sawa kulingana na hali halisi ya ya mtanzania

      Tanzanianjema
      Pasipo na IMANI kuna Uovu, Pasipo na MISINGI kuna Ufedhuli, Pasipo na ITIKADI kuna Ujanjaujanja...Yote haya ni mazalia ya UFISADI

    12. #12
      MzalendoHalisi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th June 2007
      Posts : 4,049
      Rep Power : 1422
      Likes Received
      106
      Likes Given
      208

      Default

      Mwanamageuzi,
      Tutahitaji kuwa na katiba mpya- maanake mabadiliko mengine hayatawezekana hadi new katiba! My view we begin small then we increase as we go on. We need also to be flexible- and pragmatic- hivi ikitokea tukagundua mafuta mengi sana- contributing 50% of exports- we may need A Minister for Oil/Petroleum kama ilivyo Nigeria, Iran, Venezuela nk

    13. #13
      omarilyas's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th January 2007
      Location : Morogoro
      Posts : 2,495
      Rep Power : 1137
      Likes Received
      69
      Likes Given
      5

      Default

      Quote By Mzalendohalisi View Post
      Mwanamageuzi,
      Tutahitaji kuwa na katiba mpya- maanake mabadiliko mengine hayatawezekana hadi new katiba! My view we begin small then we increase as we go on. We need also to be flexible- and pragmatic- hivi ikitokea tukagundua mafuta mengi sana- contributing 50% of exports- we may need A Minister for Oil/Petroleum kama ilivyo Nigeria, Iran, Venezuela nk
      Hadi hivi sasa it is viable kutenganisha Oil and Energy with Minerals.....Wakati mwengine tuwe tayari kuthubutu kula vidonge vichungu ili kuwezesha/kuboresha uponyeshaji

      Tanzanianjema
      Pasipo na IMANI kuna Uovu, Pasipo na MISINGI kuna Ufedhuli, Pasipo na ITIKADI kuna Ujanjaujanja...Yote haya ni mazalia ya UFISADI

    14. #14
      Kasheshe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th June 2007
      Location : Bububu
      Posts : 3,630
      Rep Power : 1351
      Likes Received
      196
      Likes Given
      344

      Default Let think BIG! no simple answer for difficult questions

      Quote By Mzalendohalisi View Post
      Mwanamageuzi,
      Tutahitaji kuwa na katiba mpya- maanake mabadiliko mengine hayatawezekana hadi new katiba! My view we begin small then we increase as we go on. We need also to be flexible- and pragmatic- hivi ikitokea tukagundua mafuta mengi sana- contributing 50% of exports- we may need A Minister for Oil/Petroleum kama ilivyo Nigeria, Iran, Venezuela nk
      Mzalendohalisi,

      Kula kumi! bado tunafikiria kijima!

    15. #15
      omarilyas's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th January 2007
      Location : Morogoro
      Posts : 2,495
      Rep Power : 1137
      Likes Received
      69
      Likes Given
      5

      Default

      Quote By kilitime View Post
      Mzalendohalisi,

      bado tunafikiria kijima!
      Wakati twafakamia kula kibepari.....nakupata kaka...

      Tanzanianjema
      Pasipo na IMANI kuna Uovu, Pasipo na MISINGI kuna Ufedhuli, Pasipo na ITIKADI kuna Ujanjaujanja...Yote haya ni mazalia ya UFISADI

    16. #16
      Ilongo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th February 2007
      Posts : 431
      Rep Power : 716
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By Mwanagenzi View Post
      Mawaziri wa nchi (ministers of state) wanakuwa sawa na manaibu waziri kiutendaji. Mpaka juzi juzi tu hapa Kenya walikuwa wakitumia jina la Waziri Msaidizi (Assistant Minister) lakini mawaziri hao wamepinga jina hilo wakidai linawadhalilisha na hivyo wamebadilishiwa na sasa wanatumia hilo la Waziri wa Nchi. Kumbuka hata kwa Tanzania kila waziri ana msaidizi wake (personal assistant) ambaye si waziri bali katibu myeka na hivyo hao wenzetu walilichukulia kwa mwanga huo.



      Hakika unaweza kuwa sahihi. Kwa mfano, hata sisi tuna wizara 22 lakini mawaziri, kwa maana ya kujumuisha mawaziri kamili, mawaziri wa nchi na manaibu waziri, unapata zaidi ya 50.
      Asate sana Mwanagenzi kwa ufafanuzi. In fact hilo la idadi nalo lilikuwa linanipa utata kwa maana kuna mahala nilisoma watu wanasifia Nigeria kwamba ina mawaziri wachache kuliko Tanzania.

      Hiyo ya Kenya nimeisikia BBC kwamba jamaa (mawaziri wasaidizi) walikuwa hawashirikishwi na mawaziri wenzao katika utendaji, kwa hiyo wakaonekana hawana kazi.

      Kuhusu Tanzania, nadhani ukubwa wa Baraza la Mawaziri linategemea na mapenzi ya Rais husika. Anayo mamlaka ya kupunguza ama kuongeza Wizara kadri anavyoona inamfaa. Mpaka pale litakapokuwa limeainishwa Kikatiba, then ndiyo tunaweza kuongelea suala la idadi. Vinginevyo, tukiendelea na Katiba hii tuliyo nayo basi suala la idadi ya wizara na mawaziri litabaki kuwa utashi wa Rais. Na ndiyo maana unaweza kuona kwa sasa hivi kuna wizara ambazo hapo kabla zilikuwa na naibu mmoja mmoja, lakini sasa hivi wapo wawili.

      Nakumbuka hata Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa haikuwahi kuwa na naibu Waziri, sasa hivi inao wawili.
      Abstinence is the only key to no regrets!

    17. #17
      Mwanagenzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th September 2006
      Location : Mtandaoni
      Posts : 762
      Rep Power : 806
      Likes Received
      10
      Likes Given
      10

      Default

      Tanzania Njema et al,
      Kama umenisoma, kwangu mimi pia, hoja si idadi. Ndiyo maana nimejaribu kuonyesha nchi nyingine mbalimbali wana mawaziri wangapi. Binafsi hapo mwanzoni sikujua kuwa Uganda, kwa mfano, wana baraza kubwa kuliko letu, japo kiuchumi na kiumaskini (soma shida na kero) hatutofautiani sana. Lakini ukiangalia watu wengi wamekuwa wakilaumu kuwa serikali yetu ni kubwa mno pengine kana kwamba ni kubwa kuliko zote duniani! Lakini utafiti wangu umeonyesha kuwa si kweli.
      ____________
      Ili Tuendelee Tunahitaji Dikteta mwenye Uzalendo na Visheni
      _____________
      "UTU BUSARA UJINGA HASARA,
      "TUPINGANE BILA KUPIGANA"

    18. #18
      MzalendoHalisi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th June 2007
      Posts : 4,049
      Rep Power : 1422
      Likes Received
      106
      Likes Given
      208

      Default

      Tanzanianjema,
      Afadhali kula kijima kuliko kula kilafi!!!! Ulafi una matatizo makubwa ndugu yangu! Walafi waongopwe kama ukoma!

    19. #19
      omarilyas's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th January 2007
      Location : Morogoro
      Posts : 2,495
      Rep Power : 1137
      Likes Received
      69
      Likes Given
      5

      Default

      Quote By Mzalendohalisi View Post
      Walafi waongopwe kama ukoma!
      bahati mbaya siku hizi tunawakimbilia kuwakumbatia. Wao ndio wamekuwa rolemodels wetu. Wasio walafi wanaonekana ama hayawani ama washamba. Kazi kwelikweli.....

      Ndio mambo ya soko huru bongo style.

      Tanzanianjema
      Pasipo na IMANI kuna Uovu, Pasipo na MISINGI kuna Ufedhuli, Pasipo na ITIKADI kuna Ujanjaujanja...Yote haya ni mazalia ya UFISADI

    20. #20
      Saidi Yakubu's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 6th March 2006
      Location : colchester,united Kingdom
      Posts : 109
      Rep Power : 790
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default

      Nawaunga mkono wale wote wanaodhani kwamba hoja ya msingi hapa inatakiwa kuwa ni upi mchango wao katika maendeleo ya nchi na si idadi ya wizara.

      Hoja za Mwanagenzi zinahitajia maelezo ya ziada ili kuepuka kumislead watu, Uingereza hapa wizara hizo ishirini na mbili lakini mawaziri lukuki:

      1. Wao wanatumia mfumo tofauti kidogo, wana kile wanakiita Secretary of State [kwa waswahili tunaita Waziri] na pia kila wizara ina Minister [pia tunatumia kiswahili]

      Mfano waziri wa Mambo ya Ndani [Secretary of State for Home Affais ambae ni mbunge na anateuliwa na Waziri Mkuu] ana wasaidizi lukuki kuna Home Office Minister for Immigration, kuna mwingine wa Prisons nk,

      Waziri wa Fedha ana nguvu kubwa zaidi na ndio kama Naibu Waziri Mkuu ana nguvu zaidi ya alizonazo Naibu Waziri Mkuu lakini nae ana [hapa anaitwa Chancellor of Exchequer] na ana manaibu lukuki kuna Chief of Treasury, Kisha kuna manaibu wengine kadhaa [John Major alikuwa nao watatu]

      Ukiangalia hivyo utakuwa kuna na zaidi ya mawaziri hao 22. Wabunge wengi pia hapa sio ajabu kuwakuta katika kazi nyingine ''za full time'' ndani ya Downing Street ambazo zinahusika moja kwa moja na Cabinet [ David Milliband ambae sasa ni waziri wa mambo ya nje UK alikuwa ni Head of Policy, Research and Planning wakati wa mwanzo mwanzo wa Blair akiwa mbunge as well]

      Sasa kwa nchi yetu Baraza linaonekana kubwa sana [60 sio mchezo] lakini nadhani ili kusonga mbele na mjadala tungekuwa na mchakato wa majukumu ya mawaziri na manaibu kuona kama kweli wote tunawahitaji au la.

      Ni zoezi linahitaji utafiti kiasi kujua wanahusikaje na vipi wanaingiliana pamoja.

      Hoja ya namna ya kuwateua nayo ni nyeti kiasi, Utaratibu wetu ni kiingereza kuwa waziri lazima awe mbunge lakini Rwanda wenzetu wana mfumo wa kifaransa, waziri ni ''technocrat'' mtaalam wa fani husika, nakumbuka niliwahi kumhoji Waziri wa Rwanda Nyaruhirira ambae ni waziri nchi anaeshughulikia magonjwa sugu na majanga katika Wizara ya Afya na kitaalum ni mtaalam wa magonjwa yanayolipuka [epidemics] yeye anahudhuria bungeni lakini hana haki ya kupiga kura...Uganda ni hivyo hivyo..

      Kwetu inawezekana Waziri wa Afya ni Mtaalam wa michezo, Waziri wa Afya akawa ni mwanasheria nk

      Nadhani sasa tunahitaji mjadala yakinifu kuona kama Rwanda wana mfumo mzuri zaidi au wa kwetu ndio mzuri zaidi....

    Page 1 of 2 12 LastLast

    Similar Topics

    1. 1 HP Water pump inahitaji stabilizer ya watts ngapi?
      By Nyikanavome in forum Tech, Gadgets & Science Forum
      Replies: 3
      Last Post: 14th November 2011, 17:25
    2. Replies: 0
      Last Post: 4th October 2011, 20:57
    3. Tanzania inahitaji katiba mpya sasa
      By Ndumule in forum KATIBA Mpya
      Replies: 0
      Last Post: 4th November 2010, 04:02
    4. Ufisadi: Je - Tanzania inahitaji yaliyotokea Ghana 1979?
      By Zak Malang in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 7
      Last Post: 28th July 2009, 22:26
    5. Tanzania inahitaji sera ya Malezi
      By Gamba la Nyoka in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 1
      Last Post: 26th October 2007, 20:07

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...