Re: Clip ya Video ya Bw. Lwakatare (mtazamo tofauti)
CDM walifanyie hili swala uchunguzi huru. Inawezekana Lwakatare ni sehemu ya mpango au ni video fake ya kuidhoofisha CDM.
CDM itafute ukweli bila kutegemea jeshi la polisi kwani kama Lwakatare ni sehemu ya mpango matokeo ya uchunguzi utakaotolewa utakuwa ni ule wa kuiweka CDM pabaya.
Rwakatare aliacha lini Usalama wa Taifa wa CCM? Na kwanini CCM mpaka sasa hawajasema kitu? Hatuoni tunahangaika na magamba tu hapa?.......Tafakari chukua hatua!!!!!!
CDM walifanyie hili swala uchunguzi huru. Inawezekana Lwakatare ni sehemu ya mpango au ni video fake ya kuidhoofisha CDM.
CDM itafute ukweli bila kutegemea jeshi la polisi kwani kama Lwakatare ni sehemu ya mpango matokeo ya uchunguzi utakaotolewa utakuwa ni ule wa kuiweka CDM pabaya.
Unajua wao walidhani baada ya kuiweka Youtube ingepewa coverage nzito na vyombo vya habari, kumbe wakawa wamesahau kwamba waandishi wana hasira na Ccm na serikali yake kwa waliyomfanyia Mwangosi, nasikia huko lumumba ni lawama na kuchanganyikiwa, mtaji mkubwa wateja hakuna!
hawa jamaa hamnazo kweli wameshindwa kuelewa kuwa hata hiyo 10%, ni watu wanaojitambua tayari
Nashauri viongozi wa siasa wawe makini na wanachama wageni au wanaohamia bila sababu na bila kuwachunguza wanawavisha madaraka makubwa.
Lwakatare alifukuzwa CUF baada ya CUF kulalamika siri za ndani kuvuja.
Nasikitishwa na viongozi wa CHADEMA kumkumbatia na wakati wakijua wazi. Ni kweli ile clip unamuonyesha.
Tuachie jeshi la polisi litende haki yake
Haki wapi? Ktk serikali dhalimu kama hii unaweya kusema itende haki wakati hapo ndipo wanachukulia uwezekano wa kuwakandamiza upinzani ambao wamewashinda ktk kusimama kwa hoja badala yake sasa wamekuwa wakitumia vyombo vya usalama? Ni mtanzania yupi leo atakuambia ana imani na police, mahakma ama usalama wa taifa na hata kuzisimamia sheria zilizowekwa? Nadhani watakokuambia wana imani navyo ni hawa hawa wadhalimu wetu wanaovitumia kwa maslahi yao
Baadhi ya wagonjwa wa UKIMWI wana kasumba ya kutokubali kwamba wanaumwa Ukimwi, na huu ndio huwa mwanzo wa mwisho wao, maana bora wangekubali wakanywa dawa za kurefusha maisha wangeweza kuishi muda kidogo kulinganisha na juhudi zao za kukataa kwamba wameathirika.
Ndivyo ambavyo chama nilichodhani kingekuwa chama mbadala ya CCM iliyochoka kingekuwa, yaani CHADEMA. Bahati mbaya sana Chadema kama mgonjwa wa UKimwi asiyetaka kukubali kwamba ameathirika badala yake anabaki kuamini kuwa KAROGWA ndio mwanzo wa mwisho wa Chadema!
Hata kama viongozi wa Chama hichi walikimbia shule wengi na wengine shule zao za magumashi ,inahitaji degree ngapi kujifunza kukubali ukweli hata kama unauma? Ugonjwa huu wa kukataa kwamba unaumwa wakati unaumwa na kudhani unarogwa utakizika Chama hichi kilichoanza kuonyesha matumaini...na hapa CCM na wapambe wao watakuwa wamefanikiwa sana.
Hivi inahitaji degree ngapi kujua kuwa Rwakatare ambaye siasa zake za upinzani alianzia CUF na wakati huo CUF ilikuwa na tabia zinazoonekana leo CHADEMA? Wakati CUF ikiwa na Rwakatare ndo ilikuwa chanzo cha vurugu za kisiasa nchini,mara kuingiza visu, mara majambia, mara maandamano, mara watu kuuawa na wengine kupoteza viungo vya miili yao!! Sasa Rwakatare huyuhuyu yuko Chadema leo, Chadema wameiga tabia zilezile zilizowamaliza CUF na wakadhani Chadema wao watakuwa na muujiza wa kuishi.
Dawa hapa nikujua mmeteleza na kuamka sio unateleza unabaki chini unalalamika!!
sijaona cha maana ulichoandika hapa zaidi ya kuwadhalili waathirika wa ukimwi na kuweka ushabiki kama siyo kutekeleza ulichotumwa na magamba
Jamaa waliambiwa madhara ya oil chafu wakapuuza sasa yanawatokea puani, wanaanza oooh CCM ndo wamepanga. Kama kweli CCM wamepanga haya basi wamewazidi kwa mbali sana,vita hii Chadema hawaiwezi kabisa...Rwakatare apigilia msumari wa mwisho kweli jeneza la Chadema.
na ndivyo mfa maji (ccm) anavyoamini na mwisho wake atakufa tu
Jamaa waliambiwa madhara ya oil chafu wakapuuza sasa yanawatokea puani, wanaanza oooh CCM ndo wamepanga. Kama kweli CCM wamepanga haya basi wamewazidi kwa mbali sana,vita hii Chadema hawaiwezi kabisa...Rwakatare apigilia msumari wa mwisho kweli jeneza la Chadema.
na ndivyo mfa maji (ccm) anavyoamini kwa kutapatap na mwisho wake atakufa tu
Re: Clip ya Video ya Bw. Lwakatare (mtazamo tofauti)
By Njoka Ereguu
Nimeangalia clip ya video ya Bw. Lwakatare zaidi ya mara 5, nilichobaini and i stand to be corrected, kwa kiwango kikubwa clip ilie ilivyoandaliwa inaonyesha kweli kwa sauti ni Bw. Lwakatare, kama mtaanagalia katika clip nyingine mfano ile ya Obama iliyowekwa humu utaona tofauti kubwa katika sauti yake halisi na ile ya kubambikizwa maneno. Ilivyo clip ya Lwakatare na teknolojia yetu, natamani sana kuamini alitengeneza mwenyewe, ila swali la msingi ni kwa sababu zipi alitengeneza na je ni kweli yeye ni mtu hatari ni maswali ya kuendelea kujiuliza.
Hisia kubwa inanijia ni kuwa upo uwezekano pia Bw. Lwakatare alinunuliwa kutengeneza hiyo picha na watu ambao pia malengo yao hatujui hadi leo na ni suala ambayo yeye anaweza kuchunguzwa na kuelezea ukweli. Cha msingi uchunguzi wa kweli ufanyike bila kuendelea kubahatisha kama ambavyo siku zote tunafanya ili kubaini genge hili la wauaji ambalo sasa ni wazi limejikita zaidi katika mrengo wa maslahi ya kisiasa.
Tafakari bila ushabiki wa kisiasa na chukua hatua, tusipotafuta majibu ya kweli hata wale ambao wanadhani ni sehemu ya genge hilo in a long run hawako salama.
Lwakatare anajua na Mungu wake, kama kweli alitengeneza au la! Jambo moja ninaloliona hivi sasa ni kuwa nchi ipo kizani, kiwango cha kukosa matumaini cha wananchi wa nchi hii ni kikubwa mno.
Viongozi walotegemewa wanaelekea kuvaa viatu vinavyowapwaya kwa kiasi kichotarajiwa. Pale wanapotegemea kupata neno la faraja kutoka kwa viongozi wao wanakuwa mabubu.
Pale wanapotegemea kusikia neno la kuonesha njia, viongozi wanalalamika.
Tumeamua kujitengenezea nyuklia yetu wenyewe, iko kwenye kinu inatokota.
Mi si Mtabiri wala Nabii, ila hii nyuklia yetu inaelekea kuna siku itafyatuka. Sina imani kama itachagua wa kumdhuru na wa kutomdhuru.
Re: RWAKATARE apigilia msumari wa mwisho jeneza la CHADEMA
By KibopaII
Baadhi ya wagonjwa wa UKIMWI wana kasumba ya kutokubali kwamba wanaumwa Ukimwi, na huu ndio huwa mwanzo wa mwisho wao, maana bora wangekubali wakanywa dawa za kurefusha maisha wangeweza kuishi muda kidogo kulinganisha na juhudi zao za kukataa kwamba wameathirika.
Ndivyo ambavyo chama nilichodhani kingekuwa chama mbadala ya CCM iliyochoka kingekuwa, yaani CHADEMA. Bahati mbaya sana Chadema kama mgonjwa wa UKimwi asiyetaka kukubali kwamba ameathirika badala yake anabaki kuamini kuwa KAROGWA ndio mwanzo wa mwisho wa Chadema!
Hata kama viongozi wa Chama hichi walikimbia shule wengi na wengine shule zao za magumashi ,inahitaji degree ngapi kujifunza kukubali ukweli hata kama unauma? Ugonjwa huu wa kukataa kwamba unaumwa wakati unaumwa na kudhani unarogwa utakizika Chama hichi kilichoanza kuonyesha matumaini...na hapa CCM na wapambe wao watakuwa wamefanikiwa sana.
Hivi inahitaji degree ngapi kujua kuwa Rwakatare ambaye siasa zake za upinzani alianzia CUF na wakati huo CUF ilikuwa na tabia zinazoonekana leo CHADEMA? Wakati CUF ikiwa na Rwakatare ndo ilikuwa chanzo cha vurugu za kisiasa nchini,mara kuingiza visu, mara majambia, mara maandamano, mara watu kuuawa na wengine kupoteza viungo vya miili yao!! Sasa Rwakatare huyuhuyu yuko Chadema leo, Chadema wameiga tabia zilezile zilizowamaliza CUF na wakadhani Chadema wao watakuwa na muujiza wa kuishi.
Dawa hapa nikujua mmeteleza na kuamka sio unateleza unabaki chini unalalamika!!
Aaahhhh!! Watu wengine bana yan hata sielewi unasaidikaje, ila kwa kuwa Umeamua kuaminisha akili yako hicho ulichopost hapo juu fair enough!!
Re: Clip ya Video ya Bw. Lwakatare (mtazamo tofauti)
Kuna mtazamo mwingine wa hili sakata la video ya Lwakatare, mtazamo ambao nasdhindwa kuunganisha dots.. Naomba msaada
1. Kuna thread moja iliwekwa jana ikionyesha akina Michuzi wakipongezana kutokana na Usalama wa Taifa (TISS) ‘kuleta kitu hiki’ na kwamba ni ‘kete kubwa kwetu’ – bila shaka kete kubwa dhidi ya Chadema. Katika thread hiyo kulizuka tatizo la kutafsiri (yaani kulikuwapo ambiguity) kuhusu maneno (intepretation) ya pongezi hizo kwa TISS ni kwa ajili ya nini hasa – yaani kwa jitihada halali za TISS kuchunguza na hatimaye kupatikana hiyo video; au pongezi zililenga kwa wao TISS ‘kuipika’ hiyo videoa kwa ajili ya kubambikizia CDM? 2. Sasa hata tuchukue hiyo tafsiri ya kwanza – kwamba TISS ndiyo walifanikisha kuchunguza na kupatikana hiyo video ambayo bila shaka itakuwa ni ‘ushahidi’ mkubwa wa kesi dhidi ya Lwakatare na pengine CDM pia, jee hii ndiyo njia sahihi kwa TISS, au tuseme ndiyo utaratibu wao wa kuuweka kwanza ushahidi huu muhimu mtandaoni kabla ya sualakupelekwa mahakamani? Nasema hivi iwapo video hiyo ni kutokana na jitihada zao za halali wenyewe TISS yaani wao ndiyo exclusive owner wa hiyo video kama jinsi akina Michuzi walitaka sis tuamini. Inakuwaje waitumbukize kwanza mtandaoni? Ndivy utaratibu siku hizi? 3. Kwa nini TISS wasingekaa nayo kimya kimya tu halafu kuishtukizia mahakamani baada ya kumkamata Lwakatare? Ushahidi mkuu wa kesi unawekwa bayana kwa jamii kwa njia ya mtandaoni kabla ya kesi kuanza? 4. Lakini pengine TISS hawakuwa mmiliki pekee (exclusive owner) ya video hiyo yaani nao waliipata kutoka kwingine (labda from Mchemba?) lakini hata hivyo haikuwa sahihi kitaaluma za mambo ya upelelezi na mashitaka kuiweka kwanza mitandaoni – kwa lengo gani? 5. Na ndiyo sasa nakuja na tatizo langu kubwa kuhusu sakata zima hili: Yeyote yule (TISS au Mchemba) waliiweka video kwanza mtandaoni ili kupima joto ku-test waters) kuhusu uhalisia wake) na wameona kwamba video hiyo imejikuta inatobolewa matundu mengi tu (punched holes) hadi uhalisia wake kuonekana wa mashaka. Kweli TISS hufanya kazi kwa mtindo huu? 6. Mie nadhani ni Mchemba (aliyewahi kutangaza huko nyuma kwamba anayo video ‘inayoonyesha viongozi wa Chadema wakipanga mauaji’ lakini baadaye akajikuta video ina mapugufu mengi kuhusu alichokitangaza na ndiyo maana badala ya kuipeleka polisi (kama jinsi akina Dr Slaa walivyomtaka kuipeleka), au kuwapa TISS wai-deal nayo -- aliona ni vyema aiweke mtandaoni. Na sababu kubwa kufanya hivi ni kwamba iwapo itaonekana ni video ni bomu (yaani ya kughushi), basi isijulikane kama ni yeye ndiyo aliiweka mtandaoni na hivyo kukwepa lawama. Na ndiyo maana kumetokea ugumu wa kumpeleka Lwakatare mahakamani kwa haraka. 7. Video hiyo haimuunganishi moja kwa moja Lwakatare kuhusu kupigwa kwa Kibanda hivyo bila shaka waliokuwa nayo waliishikilia kwanza (was put on hold) hadi “tukio la Kibanda” litokee ndiyo ikawekwa mtandaoni. Hii bila shaka ilitakiwa jamii iwekwe kwanza kisaikolojia kuhusu yatakayofuata.” 8. Na yaliyofuata sasa tumeyaona – watu walipangwa ku-act nafasi zao kama ilivyotakiwa (according to the laid down script). Hawa wengine ni pamoja na Manyerere -- na hata huyo Ludovick na tukio lake lile la kutekwa ili kujitafutia alibi. Nahisi Ludovick atakuwa shahidi tu wa kujaribu kuakandamiza viongozi wengine wa CDM – ingawa hawatajwi katika video. Mimi naona mpango mzima uliosukwa umekwenda kombo mahali fulani. Bado tISS wanakosa uweledi wa kufanya operations zao – kuanzia tukio la kuuwawa kwa Gen Amrani Kombe, Chacha Wangwe, tukio la tindikali la Kubenea, kutekwa kwa Ulimboka na pengine hili la kupigwa kwa Kibanda.
Naomba tujadili hili kwa kina.
We'd all like to vote for the best man, but he's never a candidate.
Re: Clip ya Video ya Bw. Lwakatare (mtazamo tofauti)
Taarifa nilizopata muda huu tukio likiwa linaendelea zinaeleza kwamba Jeshi la Polisi limeingia Ofisi za Chadema Makao Makuu Muda Huu Jumapili ya leo, na Lwakatare... Wanaendelea Na Upekuzi... Wenye Ofisi Hawapo, Wapo Walinzi Tu!!
Re: RWAKATARE apigilia msumari wa mwisho jeneza la CHADEMA
By Gracious
Tatizo hapa watu wanaongea tu kwa hisia.Ukimpa mtu video nyingine yoyote hana uwezo wa kukwambia hii ni fake au sio fake.How comes wameweza kuona kwamba hii ni fake? Hata layman hawezi kusema ile video ni uongo,Angalia body movements,lips na sauti altogether are supporting the video.Kama wanaweza kutengeneza fake wangetengeneza ya Mbowe au Dr Slaa kabisa ili kuwamaliza chadema full.Lets think wapendwa
Kwa nini Chadema washupaile sana kutetea kwamba the video is not real.Majibu anayo Lwakatare.Yeye ni nani ashindwe kupewa hela na ku act ile muvie(Nina uhakika ali act ile movie kwa sababu inaonekana alikua anajua anarekodiwa na walijiandaa).Lwakatare amact hii muvi akiwa anajua na akiwa na malengo anayoyajua yeye.Lwakatare at this point anaweza akawadanganya CDM kwamba sio yeye ili awaingize king zaidi kwa kumtetea sana alafu baadae aje awaumbue.Ukweli anaujua yeye.
Mpaka sasaivi viongozi wa Chama wameshakosea ku stand bodly kusema the video is fake.How are they so sure? watuthibitishie kwamba ni feki sio tu kuongea.Wasitake kutufanya mazuzu wao wabadili ukweli kuwa uongo na sisi tuwafuate tu.Hiyo itakua sio akili,tujiepushe na ushabiki wa namna hiyo.Tupate evidence.
Katika Hili CHADEMA wanatakiwa kum toa sadaka huyu jamaa.Whether he did it or not,has to be sacked at this time.Ili chama kiweze kuwa na mazingira mazuri ya ku clear this mess baadae.
CHADEMA wasi rely sana kwenye kesi mahakamani.Kesi hiyo inaweza kupigwa danadana kwa hata iaka minne,miezi hata saba mtaambiwa upelelezi bado haujakamilika.Uelewa wa watanzania walio wengi ni mdogo.Ni kwamba mtu akishtakiwa basi ameshatenda hilo kosa.Je chadema wako tayari kuishi na propaganda hiyo chafu kwa muda wote huo.Itachukua dola?
At this time CDM watafute private Investigators hata kutoka nje wachunguze hii ishu ili wajiridhishe.Hii itawasaidia kujua namna ya kujisafisha.
Watafute strong PR Consultants wa kuwasaidia what they should do.
Nimekuelewa Mkuu..
Argue for the sake Of Truth,Not For The Sake Of Win; CCM TUNAPOSEMA HAITOKI Tunamaanisha Ile gesi haitoki kweli.
Re: Clip ya Video ya Bw. Lwakatare (mtazamo tofauti)
Napata shida sana,nairudia kuiangalia ile video ya lwakatare mara kwa mara ili niweze kugundua ufake wake,lakini nashindwa kabisa,,
Imenidisapoint sana hii clip,nikijaribu kumwangalia usoni,hisia zake,jins lips zake zinavocheza anapoyatamka hayo maneno yake yanaendana moja kwa moja,labda nikiri wazi wazi mimi ni mjinga kuhus tenkonolojia iliyotumika pale,
Ila hadi sasa inanisumbua sana,wenzangu wanaosema fake nao siwapingi,ila sijatosheka na hoja zao za kuisema hii clip ni fake,,
Chama kinabid kiwe makini sana katika suala hili..
CCM Wasipate pakutokea..
Argue for the sake Of Truth,Not For The Sake Of Win; CCM TUNAPOSEMA HAITOKI Tunamaanisha Ile gesi haitoki kweli.
Re: Clip ya Video ya Bw. Lwakatare (mtazamo tofauti)
By R.B
Taarifa nilizopata muda huu tukio likiwa linaendelea zinaeleza kwamba Jeshi la Polisi limeingia Ofisi za Chadema Makao Makuu Muda Huu Jumapili ya leo, na Lwakatare... Wanaendelea Na Upekuzi... Wenye Ofisi Hawapo, Wapo Walinzi Tu!!
Umezipata wapi taarifa hizo mkuu??
Argue for the sake Of Truth,Not For The Sake Of Win; CCM TUNAPOSEMA HAITOKI Tunamaanisha Ile gesi haitoki kweli.
Follow Us Here