TiGo Internet
    Show/Hide This

    Topic: Mawaziri wenye PhD Feki hawa hapa!

    Report Post
    Page 1 of 5 123 ... LastLast
    Results 1 to 30 of 135
    1. #1
      Mdondoaji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th March 2009
      Posts : 4,448
      Rep Power : 1376
      Likes Received
      666
      Likes Given
      284

      Default Mawaziri wenye PhD Feki hawa hapa!

      Mawaziri sita wanaswa na vyeti feki

      • Vyeti vyao vya elimu vyadaiwa vina utata
      • Yumo Mkuu wa Mkoa na wabunge watatu
      • Orodha yawasilishwa kwa Spika wa Bunge


      Dk. Mary Nagu Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko.


      Dk. Emmanuel Nchimbi, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa-JKT)


      Dk. Makongoro Mahanga, Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana.


      Dr. David Mathayo David, Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika.

      Mawaziri sita na wabunge wanne, wametajwa kuwamo katika orodha ya watuhumiwa 19 wa walighshi vyeti vyao vya elimu.

      Utafiti huru uliofanywa na Mwanaharakati, Kainerugaba Msemakweli kwa msaada wa Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU), katika kipindi cha mwaka mmoja; umebaini kwamba wanasiasa hao wametumia vyeti vya kughushi na kuwasilisha katika ofisi za umma kwamba wana elimu hiyo, kitu ambacho si kweli.

      Utafiti huo ulianza kufanyika Juni 25, mwaka jana hadi Oktoba 9, mwaka huu katika nchi za Marekani, India na Uingereza, ambako vigogo hao wanadaiwa kuwa walisoma na kupata shahada hizo.

      Baada ya kubainika kwamba hawana sifa za elimu wanazodai kwenye wasifu wa elimu zai, ripoti hiyo imekabidhiwa kwa Ofisi ya Spika wa Bunge.

      Kuwasilisha nyaraka za kughushi katika ofisi ya umma ni kinyume cha Katiba na sheria za nchi.

      Akizungumza na waandishi wa habari jana, Msemakweli aliwataja mawaziri hao kuwa ni Dk. Mary Nagu (Viwanda, Biashara na Masoko), na Dk. Diodurus Kamala (Ushirikiano wa Afrika Mashariki) kuwa miongoni mwa vigogo wanaohusika na kashfa hiyo.

      Pia, kuna waziri mwingine mmoja ambaye jina linahifadhiwa kwa sababu hatukuweza kumpata kuzungumzia tuhuma zake jana.

      Mbali na hao, pia Msemakweli aliwataja manaibu waziri, Dk. Makongoro Mahanga (Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana), Dk. David Mathayo David (Kilimo, Chakula na Ushirika) na Dk. Emmanuel Nchimbi (Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa-JKT) kuhusika na kashfa hiyo.

      Wabunge, ambao wametajwa na ripoti hiyo, ni pamoja na William Lukuvi (Ismani-CCM), ambaye pia, ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Victor Mwambalaswa (Lupa-CCM) na Dk. Raphael Chegeni (Busega-CCM).

      Kuna mbunge mwingine ambaye pia alitajwa kwenye kashfa hii na kwa kuwa jana hatumpata kuzungumzia suala hilo, jina lake tumesitiri kwa sasa.

      Vigogo hao wanadaiwa kuwa walighushi taaluma kwa baadhi yao kujiwasilisha kuwa wana shahada za masuala ya kimataifa na diplomasia, biashara na utawala, wengine shahada za uzamili, udaktari wa falsafa, na wengine dhahada za ualimu nakadhalika, wakati si kweli.

      Msemakweli alisema katika taarifa aliyowasilisha kwa ofisi ya Spika aliomba iwawajibishe vigogo hao kwa kashfa hiyo.

      Alisema vigogo hao waliwaghilibu wananchi wa majimbo wanayoyawakilisha na kuwafanya wapate ubunge na kwamba, kwa kutumia shahada hizo za kujipachika, wameweza kuaminiwa na kupewa nafasi za kisiasa na kiutawala.

      Alidai ana ushahidi wa kutosha juu ya madai anayoyatoa dhidi ya vigogo hao kwani ameyafanya utafiti wa uhakika na kwamba, kigogo yeyote atakayehisi kuwa ameonewa aende kwenye vyombo vya sheria na yuko tayari kwenda kuthibitisha madai yake.

      Alidai Lukuvi alighushi sifa za taaluma kuwa ni msomi mwenye shahada ya masuala ya kimataifa na diplomasia wakati elimu yake ni darasa la saba na ualimu wa shule ya msingi.

      “Hajawahi kuingia darasa lolote la digrii (Shahada) wala kufanya mtihani wowote wa digrii wala kusoma digrii yoyote, wakati wowote, katika maisha yake yote na mahali popote duniani,” alidai Msemakweli.

      Alisema wakati anaiwakilisha Tanzania nchini Namibia katika mkutano wa wabunge wa Jumuiya ya Madola, Lukuvi aliwasilisha taarifa za kuhusu taaluma yake kwa kudanganya kuwa yeye ni msomi mwenye shahada ya uzamili katika masuala ya biashara na uongozi.

      “Taarifa za kweli ni kwamba baada ya kumaliza elimu ya msingi na kuishia darasa la saba mwaka 1975 Mheshimiwa Lukuvi alienda kusomea ualimu wa shule za msingi katika Chuo Kikuu cha Ualimu, mkoani Tabora,” alisema Msemakweli.

      Alisema Dk. Mahanga “…ameghushi sifa za kuwa ana shahada ya uzamivu (daktari wa falsafa) wakati hajawahi kusoma shahada hiyo wakati wowote na mahali popote duniani”.

      Msemakweli alidai Mwambalaswa ameghushi sifa za taaluma kwamba ana shahada ya uzamivu ya biashara na utawala (MBA) wakati hajawahi kusoma shahada hiyo.

      Alidai Dk. Nagu ameghushi sifa za taaluma na kujiwasilisha kwamba ana shahada ya udaktari wa falsafa wakati hajawahi kusomea udaktari wowote na mahali popote.

      “Yeye amesoma na kuishia shahada ya pili kwa kutumia shahada hiyo ya kujipachika ameweza kuaminiwa na kupewa nafasi za kisiasa na kiutawala wakati… Katika maisha yake hajawahi kusomea udaktari wa aina yoyote,” alidai Msemakweli na kuongeza:

      “Amefanya …kumdanganya Mheshimiwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Taarifa katika Ofisi ya Mheshimiwa Spika na ambayo Mheshimiwa Spika anazo zinaonesha kuwa Mheshimiwa Mary Nagu ni msomi mwenye digrii ya daktari wa falsafa wakati hajawahi kusoma udaktari wowote katika maisha yake yote.”

      Msemakweli alidai “Dk. Nchimbi ameghushi sifa za taaluma na kujifanya kuwa ana digrii ya Uzamivu (Ph.D). Hivyo kujipachika sifa za udaktari,” alisema.

      Alidai Chegeni ameghushi sifa za taaluma na kujiwasilisha kwamba ana digrii ya uzamivu (Ph.D) na hivyo kujifanya dokta wakati hajawahi kusoma digrii yoyote ya udaktari au uzamivu, wakati wowote na mahali popote duniani na vyeti alivyonavyo kuhusu elimu hiyo ni vya kughushi.

      Msemakweli alidai: “Dk. Mathayo ameghushi sifa za taaluma kwamba ana stashahada ya juu katika masuala ya mahusiano ya kimataifa wakati hajawahi kusoma stashahada au diploma hiyo wakati wowote na mahali popote pale duniani.”

      Kwa upande wa Dk. Kamala, Msemakweli alidai: “Ameghushi sifa za taaluma kwamba ana digrii ya uzamivu (Ph.D) wakati hajawahi kusoma digrii hiyo, wakati wowote na mahali popote duniani.”

      Nipashe iliwasiliana na vigogo hao, jana kupata maelezo yao na kwanza alikuwa ni Lukuvi ambaye alikanusha vikali kuwahi kusomea au kudai kwamba, ana shahada ya biashara na kusema kuwa: “Mtu anayedai hivyo ametia chumvi.”

      Alisema aliyonayo ni diploma ya sayansi ya siasa kutoka Urusi na shahada ya taaluma ya Kimataifa kutoka Marekani.

      “Sijawahi kusoma biashara na wala sina Masters (shahada ya pili) ya biashara. Kama ana ushahidi athibitishe,” alisema Lukuvi.

      Dk. Mahanga alisema hayuko tayari kusema lolote kwa vile mtu aliyetoa madai hayo ahamjui.

      Kwa upande wake, Dk. Nagu alipoulizwa na Nipashe, alisema: “Ngoja kesho niongee na mtu huyo kwani sasa hivi niko Morogoro, nitawasiliana naye kisha tutaongea Jumanne (kesho) .”

      Dk. Nchimbi alisema: “Mimi sijamsikia (huyo mtu). Wewe mwenzangu umepata kumsikia. Mimi mpaka nipate bahati ya kumsikia.”

      Dk. Chegeni alipoulizwa na mwandishi wa Nipashe juu madai ya elimu yake, naye alimuuliza mwandishi kuwa: “Mtu akikuuliza mimi ni mume wa mama yako utajibu nini?” Lakini mwandishi alipomtaka ajibu swali aliloloulizwa, aliongeza: “Kama mtu huyo amesema ana haki ya kusema.”

      Mwambalaswa alisema watu wanaomhusisha na kashfa hiyo kama si katika kundi la mafisadi, basi watakuwa ni watu ambao walioshindwa kufuatilia kuhusu ukweli wa elimu yake.

      Alisema shahada anayodaiwa kughushi aliipata kihalali katika nchi za Uholanzi na Uingereza.

      Naye Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashilillah alipoulizwa kama barua ya Msemakweli imefika katika Ofisi ya Spika, alisema kwamba, bado hajaiona.

      “Nimesikia suala hilo leo asubuhi kutoka kwa waandishi wa habari. Mimi barua sijaiona. Sina uhakika, hivyo siwezi kusema lolote,” alisema Kashilillah na kuongeza kuwa Spika amesafiri.

      Source: Nipashe.

      Mie niliwahi kusemaga nyuma sasa hivi ulimwengu wa mtandao ni mpana huna haja ya kudanganya mtu akigoogle atapata details zako zote sasa nao wazee wanaumbuka. PhD za miezi sita, masters ya miezi miwili wapi na wapi???


    2. #2
      WildCard's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd April 2008
      Posts : 4,793
      Rep Power : 1471
      Likes Received
      836
      Likes Given
      16

      Default Re: Mawaziri sita wanasa na vyeti feki.

      "Dr" Mzindakaya vipi?

    3. #3
      Mtanzania's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 4th May 2006
      Location : UK
      Posts : 5,162
      Rep Power : 1661
      Likes Received
      129
      Likes Given
      37

      Default Re: Mawaziri sita wanasa na vyeti feki.

      Hili suala tumelijadili mara nyingi sana hapa JF. Kuna haja ya kutenganisha kati ya kugushi vyeti na kusoma vyuo visivyotambulika.

      Labda kama mwandishi ndiye kaandika vibaya; kwa aliyechunguza kama atasema hawa jamaa wameforge vyeti, wanaweza kumshinda kirahisi. Walichofanya wao ni kutumia titles ambazo hazilingani na elimu yao kama inavyotambuliwa na taasisi mbalimbali za elimu.

      Yule wa wilaya moja, nafikiri ni mkoa wa Mara, yeye ndiye ka forge cheti maana ni kweli hajawahi kusoma popote. Pia huenda Lukuvi naye kama ni kweli hajawahi kusoma popote.

      Hao akina Kamala wanavyo hivyo vyeti na vimetolewa na institutions ambayo zipo kihalali lakini tu elimu wanayotoa haikidhi requirements zinazotakiwa kwenye elimu zao.

      Sidhani kama spika Sitta anaweza kufanya lolote kwenye hili; wanaoweza kufanya jambo ni wananchi ambao baada ya kujua ukweli huu wanaweza kuwawajibisha wabunge wao. Pia kwa rais aliyewapa kazi, anaweza kuona hawana sifa tena na kuwaondoa kwenye hizo nafasi zao.

      Amenifurahisha Mwambalaswa anayekimbilia kwamba ni mafisadi ndio wanamtuhumu. Kwanini ashindwe kujibu swali la wazi kama hilo?

    4. #4
      Nyauba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th July 2008
      Posts : 978
      Rep Power : 697
      Likes Received
      14
      Likes Given
      7

      Default Re: Mawaziri sita wanasa na vyeti feki.

      Hawa kwa nyadhifa walizo nazo kwenye jamii hawahitajii kusukumwaa kuwajibikaa kwa hilii..

      kama elimu yao inatiliwaa shakaa wanawajibikaa kujitokeza na kujiteteaaaa....

    5. #5
      RealTz77's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th May 2009
      Location : far from politics
      Posts : 707
      Rep Power : 599
      Likes Received
      9
      Likes Given
      13

      Default Re: Mawaziri sita wanaswa na vyeti feki

      sasa vijana na form four walifoji vyeti wakaingia BOT mkawapeleka mahakamani,why not these big potatoes? uwajibikaji ni muhimu incase wameforge,yani kila mtu Dr, Dr thats why, hatuoni hata UPhd katika kazi za maPhd's wengi nchini?
      am not 40, am 18 yrs old with 22yrs experience!

    6. #6
      Mtu B's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd December 2008
      Posts : 871
      Rep Power : 655
      Likes Received
      19
      Likes Given
      3

      Default Re: Mawaziri sita wanasa

      Hao mafisadi wa elimu mbona wanafahamika siku nyingi na wameshasemwa sana lakini hakuna hatua iliyochukuliwa. Kuna mwingine Moses Warioba alifoji PhD, akapewa hadi uprofesa na ukuu wa chuo Mzumbe kwa cheti cha kughushi, na amekula bata kwa kwenda mbele hadi amestaafu, kudadadeki! Nchi hii bwana! Kama kuna maprofesa wa kughushi katika vyuo vikuu, unategemea nini katika sehemu nyingine?

      Nafikiri hii nchi inahitaji jitu kama Benito Mussolini au Adolf Hitler.

    7. #7
      Mtu B's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd December 2008
      Posts : 871
      Rep Power : 655
      Likes Received
      19
      Likes Given
      3

      Default Re: Mawaziri sita wanasa na vyeti feki.

      Quote By WildCard View Post
      "Dr" Mzindakaya vipi?
      Huyo anaeleweka ni dr wa university ya kijadi ya Lyamba Lya Mfipa

    8. #8
      Calnde's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th October 2008
      Location : Still looking where to settle
      Posts : 1,366
      Rep Power : 762
      Likes Received
      247
      Likes Given
      148

      Default Re: Mawaziri sita wanaswa na vyeti feki

      Hapo kwa Lukuvi hata mie nna shaka. But anyway ngoja tuhuma hizo zithibitishwe kwanza may be that is the reason why our country always is having unsound decisions
      In the end will remember,not the words of our enemies but the silence of our friends.

    9. #9
      Kyachakiche's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th February 2009
      Posts : 747
      Rep Power : 624
      Likes Received
      14
      Likes Given
      38

      Default Re: Mawaziri sita wanasa

      Kuelekea uchaguzi mkuu mwakani tutaona na kusikia mengi. Utetezi wa walio wengi utakuwa 'MAFISADI WANANIANDAMA, ama WABAYA WANGU WANANYEMELEA JIMBO LANGU" Hawatajibu hoja/swali

    10. #10
      WildCard's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd April 2008
      Posts : 4,793
      Rep Power : 1471
      Likes Received
      836
      Likes Given
      16

      Default Re: Mawaziri sita wanaswa na vyeti feki

      Naona wote mmewapa UWAZIRI! Wenye vyeo wakiliona hili patakuwa hapatoshi humu. Hapo WAZIRI ni "Dr" Nagu tu wengine ni manaibu.

    11. #11
      Mdondoaji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th March 2009
      Posts : 4,448
      Rep Power : 1376
      Likes Received
      666
      Likes Given
      284

      Default Re: Mawaziri sita wanasa na vyeti feki.

      Quote By Mtanzania View Post
      Hili suala tumelijadili mara nyingi sana hapa JF. Kuna haja ya kutenganisha kati ya kugushi vyeti na kusoma vyuo visivyotambulika.

      Labda kama mwandishi ndiye kaandika vibaya; kwa aliyechunguza kama atasema hawa jamaa wameforge vyeti, wanaweza kumshinda kirahisi. Walichofanya wao ni kutumia titles ambazo hazilingani na elimu yao kama inavyotambuliwa na taasisi mbalimbali za elimu.

      Yule wa wilaya moja, nafikiri ni mkoa wa Mara, yeye ndiye ka forge cheti maana ni kweli hajawahi kusoma popote. Pia huenda Lukuvi naye kama ni kweli hajawahi kusoma popote.

      Hao akina Kamala wanavyo hivyo vyeti na vimetolewa na institutions ambayo zipo kihalali lakini tu elimu wanayotoa haikidhi requirements zinazotakiwa kwenye elimu zao.

      Sidhani kama spika Sitta anaweza kufanya lolote kwenye hili; wanaoweza kufanya jambo ni wananchi ambao baada ya kujua ukweli huu wanaweza kuwawajibisha wabunge wao. Pia kwa rais aliyewapa kazi, anaweza kuona hawana sifa tena na kuwaondoa kwenye hizo nafasi zao.

      Amenifurahisha Mwambalaswa anayekimbilia kwamba ni mafisadi ndio wanamtuhumu. Kwanini ashindwe kujibu swali la wazi kama hilo?
      Unajua ishu inakuja hivi credibility ya nchi inashuka kwasababu ya watu kama hawa imagine mtu anajiita Dr. halafu anaalikwa kwenye Global Forum au mkutano muhimu anaanza kuzungumza kitu hakieleweki unadhani yeye ndio anaaibika bali ni sie tunaoaibika ni afadhali mtu aseme sina hicho cheti watu watasema inawezekana elimu yake ndogo sio kusema vitu havina mwelekeo.

      Pili vitu kama hivi ndio vinasababisha nchi kuingia katika hasara kwani mikataba mtu hafahamu hili wala lile anasign tu akijua baadae ana kitu kidogo sasa unategemea uadilifu utapatikana? Hamna accountability kwasababu mtu hajali na wala hatojali kwasababu yeye reputation kwake sio ishu kuliko maslahi binafsi.


    12. #12
      Mtanzania's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 4th May 2006
      Location : UK
      Posts : 5,162
      Rep Power : 1661
      Likes Received
      129
      Likes Given
      37

      Default Re: Mawaziri sita wanaswa na vyeti feki

      Quote By WildCard View Post
      Naona wote mmewapa UWAZIRI! Wenye vyeo wakiliona hili patakuwa hapatoshi humu. Hapo WAZIRI ni "Dr" Nagu tu wengine ni manaibu.
      Kamala pia ni waziri kamili.

    13. #13
      WildCard's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd April 2008
      Posts : 4,793
      Rep Power : 1471
      Likes Received
      836
      Likes Given
      16

      Default Re: Mawaziri sita wanaswa na vyeti feki

      Quote By Mtanzania View Post
      Kamala pia ni waziri kamili.
      Nina maana ya hao waliotundikwa picha zao hapo juu.

    14. #14
      FirstLady1's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 29th July 2009
      Location : Mama Mwenye Nyumba
      Posts : 12,986
      Rep Power : 3061
      Likes Received
      1905
      Likes Given
      2786

      Default Re: Mawaziri sita wanaswa na vyeti feki

      kama huyu nae ndo hivo akina sie itakuwaje

      Dk. Makongoro Mahanga, Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana.
      Zaburi 35:1 Ee Bwana utete nao wanaoteta nami Upigane nao wanaopigana nami.

    15. #15
      WildCard's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd April 2008
      Posts : 4,793
      Rep Power : 1471
      Likes Received
      836
      Likes Given
      16

      Default Re: Mawaziri sita wanaswa na vyeti feki

      Quote By Firstlady1 View Post
      kama huyu nae ndo hivo akina sie itakuwaje

      Dk. Makongoro Mahanga, Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana.
      Huyu ni msomi mzuri tu kwa viwango vyetu hapa Nchini. Ana CPA na CSP. Sijui huo udaktari feki aliutaka wa nini wakati kuwa MBUNGE au WAZIRI hakuhitaji elimu kuubwa kiivo!

    16. JS is online now
      JS
      #16
      JS's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 29th September 2009
      Posts : 2,011
      Rep Power : 3306
      Likes Received
      419
      Likes Given
      286

      Default Re: Mawaziri sita wanaswa na vyeti feki

      kaaazi kwelikweli.....watu wanaoshika dhifa za juu ndo kama hivyo na wachini wafanyeje??lakini bado wako innocent till proven guilty by the law of the land of Tanzania.ila ndo wameshachafuliwa tayari
      JF Rocks!!!!!!!!!!!!

    17. #17
      Omumura's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th August 2009
      Posts : 458
      Rep Power : 535
      Likes Received
      7
      Likes Given
      0

      Exclamation Re: Mawaziri sita wanaswa na vyeti feki

      Ni vema veme rungu la TCU likamulika baraza zima la mawaziri jamani!

    18. Zed is offline
      Zed
      #18
      Zed's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th March 2009
      Posts : 348
      Rep Power : 538
      Likes Received
      101
      Likes Given
      80

      Default Re: Mawaziri sita wanaswa na vyeti feki

      Hii sasa kali!
      Tanganyika Law Society, Haki Elimu, Tamwa na wanaharakati wengine watusaidie kuwafungulia mashtaka hawa ili wakajitetee mahakamani na hivyo vyeti vyao!!! Najua ofisi ya Bunge haitafanya lolote!! Watanzania tuwe offensive now! Rais, watazania kwa hili la ufisadi wa kielimu tuwe wakali.
      ...so that our politicians do politics instead of thievery and our beloved thieves do thievery, not politics; ... (Jenerali Ulimwengu)

    19. #19
      WildCard's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd April 2008
      Posts : 4,793
      Rep Power : 1471
      Likes Received
      836
      Likes Given
      16

      Default Re: Mawaziri sita wanaswa na vyeti feki

      Zed,
      Huko Mahakamani nako utakuta JAJI anayepelekewa kesi hizi ana cheti feki cha kidato cha sita! Mambo ni magumu NCHI hii, we acha tu.

      BTW, yale ya Mbunge Chitalilo yaliishia wapi?

    20. #20
      Shishye's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th February 2009
      Location : On earth
      Posts : 270
      Rep Power : 523
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Mawaziri sita wanaswa na vyeti feki

      Namshangaa huyu Msemakweli anavyojaribu kupambana na rais! Hawa wote wameteuliwa na rais, na kabla ya uteuzi kama huo lazima anaangalia CV zao.

      Hakuna mwenye nia ya kuwafanya chochote hawa hata ingekuwa ni kweli wamevunja sheria yoyote ya nchi. Si mpaka serikali ipate ushahidi kamili? Hebu acheni bana.

      Tofauti ya msingi (Tanzania tu) kati ya private sector na public service ni kwamba private sector ina 0% tolerance to fraud, theft, inefficiency, poor performance, ufisadi, na ujinga ujinga wote wakati serikalini wao ni 100%. The more you damage the more you are safe guarded.
      "Chunguza Mjomba, Utabaini!"

    21. #21
      TIMING's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 12th April 2008
      Location : Roaming...
      Posts : 18,658
      Rep Power : 4797
      Likes Received
      5195
      Likes Given
      5895

      Default Re: Mawaziri sita wanaswa na vyeti feki

      Quote By WildCard View Post
      Zed,
      Huko Mahakamani nako utakuta JAJI anayepelekewa kesi hizi ana cheti feki cha kidato cha sita! Mambo ni magumu NCHI hii, we acha tu.

      BTW, yale ya Mbunge Chitalilo yaliishia wapi?
      WC, Hii nchi ngumu sana...

      Tumeshaona wasomi feki
      Bidhaa kibao feki
      mikataba feki
      kesi feki
      dhamana feki
      Raia feki
      ahadi feki
      Mitihani feki

      Sasa subiri utasikia
      Mashtaka feki
      makaripio feki [kutoka kwa mkuu]
      ahadi feki


      sijui tumebakiza nini tena feki

      Kenya ni nchi ya kitu kidogo... Tanzania iwe nchi ya mafeki tu!
      ..... Just a thought!!

    22. #22
      Barubaru's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th April 2009
      Location : Doha, Qatar
      Posts : 4,428
      Rep Power : 1349
      Likes Received
      688
      Likes Given
      231

      Default Re: Mawaziri sita wanaswa na vyeti feki

      Hatari kubwa hasa pale nchi inapokamatwa na matapeli na mafisadi.

      Je watanzania mtapona hapo

    23. #23
      Ndahani's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 3rd June 2008
      Location : Somewhere
      Posts : 5,363
      Rep Power : 1579
      Likes Received
      997
      Likes Given
      1667

      Default Re: Mawaziri sita wanaswa na vyeti feki

      Ipo kazi maana kama hata qualifications ni zakupika, watapika vingapi wakiwa maofisini? Labda Dr Matayo David anajiita Dr kwasababu alisomea vetenary SUA

    24. #24
      TIMING's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 12th April 2008
      Location : Roaming...
      Posts : 18,658
      Rep Power : 4797
      Likes Received
      5195
      Likes Given
      5895

      Default Re: Mawaziri sita wanaswa na vyeti feki

      Quote By Shishye View Post
      Namshangaa huyu Msemakweli anavyojaribu kupambana na rais! Hawa wote wameteuliwa na rais, na kabla ya uteuzi kama huo lazima anaangalia CV zao.

      Hakuna mwenye nia ya kuwafanya chochote hawa hata ingekuwa ni kweli wamevunja sheria yoyote ya nchi. Si mpaka serikali ipate ushahidi kamili? Hebu acheni bana.

      Tofauti ya msingi (Tanzania tu) kati ya private sector na public service ni kwamba private sector ina 0% tolerance to fraud, theft, inefficiency, poor performance, ufisadi, na ujinga ujinga wote wakati serikalini wao ni 100%. The more you damage the more you are safe guarded.
      Shishye, duh...

      Hapo ndipo utakapochoka na vetting system yetu, na kuna wakati jamaa wanachukua hadi 10 months kum-vett mtu ndio wamuajiri, sijui wanatumia mbinu zipi
      ..... Just a thought!!

    25. #25
      mwanamasala's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 20th June 2009
      Posts : 241
      Rep Power : 501
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Mawaziri sita wanaswa na vyeti feki

      Tanzania ,udoctor umekuwa loose sana!Nchi zilizoendelea it is not a big deal.Medical doctors ndio wanajulikana kuwa real doctors.Ukienda vyuo vikuu pia,kwa sababu genuine Phd ziko huko!Condoleesa Rice ana Phd,lakini
      hakujiweka mbele kujiita dr.Hata secretary wa defence wa sasa USA,Robert Gates ,ana Phd ,lakini hujawahia kumsikia anaitwa dr.

      Hata Slaa sio lazima ajiite Dr!Ana JD,sawa na Obama!Umeshamsikia Obama anajiita DR?
      Nafikiri tanzania Phd za akina Salmin Amour na Salim Ahmed Salim zimechangia watu kupata Phd fake online!Dunia nzima kwenye academic circles zinajua Tanzania kuna watu wanu Phd fake!
      Nchi inadidimia kimaadili

    26. Zed is offline
      Zed
      #26
      Zed's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th March 2009
      Posts : 348
      Rep Power : 538
      Likes Received
      101
      Likes Given
      80

      Default Re: Mawaziri sita wanaswa na vyeti feki

      Quote By MTM View Post
      WC, Hii nchi ngumu sana...

      Tumeshaona wasomi feki
      Bidhaa kibao feki
      mikataba feki
      kesi feki
      dhamana feki
      Raia feki
      ahadi feki
      Mitihani feki

      Sasa subiri utasikia
      Mashtaka feki
      makaripio feki [kutoka kwa mkuu]
      ahadi feki


      sijui tumebakiza nini tena feki

      Kenya ni nchi ya kitu kidogo... Tanzania iwe nchi ya mafeki tu!
      Ndio maana hata rais alipoulizwa kwanini Tanzania ni maskini, alikosa jibu! Ina maana hata elimu ya mawaziri wake hajui ni feki?
      ...so that our politicians do politics instead of thievery and our beloved thieves do thievery, not politics; ... (Jenerali Ulimwengu)

    27. #27
      Juma Contena's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 21st May 2009
      Posts : 1,129
      Rep Power : 686
      Likes Received
      43
      Likes Given
      7

      Default Re: Mawaziri sita wanaswa na vyeti feki

      Quote By Zed View Post
      Ndio maana hata rais alipoulizwa kwanini Tanzania ni maskini, alikosa jibu! Ina maana hata elimu ya mawaziri wake hajui ni feki?
      alafu sijui ata wafukuza kazi au labda vyeti vyenyewe kawachongea yeye ili awapachike papo walipo.
      the difference between fantasy and realism is that, one is based on wishful thinking and the other purely on facts.

      jambo usilolijua ni kama usiku wa kiza......

    28. #28
      WildCard's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd April 2008
      Posts : 4,793
      Rep Power : 1471
      Likes Received
      836
      Likes Given
      16

      Default Re: Mawaziri sita wanaswa na vyeti feki

      Quote By Zed View Post
      Ndio maana hata rais alipoulizwa kwanini Tanzania ni maskini, alikosa jibu! Ina maana hata elimu ya mawaziri wake hajui ni feki?
      Watanzania tuna sifa kubwa mbili:
      1. Kumiliki au kutumia vitu feki
      2. Kumiliki au kutumia vitu "used".
      Kwenye vitu feki ndio utakuta vyeti, bidhaa za madukani, kubambikiwa watoto,ajira zisizo na malipo stahiki, cd na kanda za muziki za kubumba,....
      Kwa vitu "used" utakuta magari, vifaa vya majumbani na ofisini, mke/mme,....

    29. #29
      Lole Gwakisa's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 5th November 2008
      Posts : 2,590
      Rep Power : 1007
      Likes Received
      325
      Likes Given
      273

      Default Re: Mawaziri sita wanaswa na vyeti feki

      Jamani waruhisiwe sasa waende kusoma na kutetea taaluma zao kama zipo.
      UDSM , na UDOM pale kuna uhaba wa wahadhiri wakati Baraza La Mawaziri kuna chem chem ya wasomi wenye hadhi ya U-"Dr".
      Tuwatumie

    30. #30
      carmel's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th August 2009
      Posts : 2,759
      Rep Power : 1010
      Likes Received
      163
      Likes Given
      121

      Default Re: Mawaziri sita wanaswa na vyeti feki

      Quote By Shishye View Post
      Namshangaa huyu Msemakweli anavyojaribu kupambana na rais! Hawa wote wameteuliwa na rais, na kabla ya uteuzi kama huo lazima anaangalia CV zao.

      Hakuna mwenye nia ya kuwafanya chochote hawa hata ingekuwa ni kweli wamevunja sheria yoyote ya nchi. Si mpaka serikali ipate ushahidi kamili? Hebu acheni bana.

      Tofauti ya msingi (Tanzania tu) kati ya private sector na public service ni kwamba private sector ina 0% tolerance to fraud, theft, inefficiency, poor performance, ufisadi, na ujinga ujinga wote wakati serikalini wao ni 100%. The more you damage the more you are safe guarded.
      A very sad truth
      A gossip betrays a confidence; so avoid a man who talks too much.
      Proverbs 20:19


    Page 1 of 5 123 ... LastLast

    Similar Topics

    1. Matanuzi na kufuru za Mawaziri feki wa Kikwete
      By Mzanaki in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 3
      Last Post: 30th May 2011, 17:28
    2. kwanini viongozi wenye vyeti feki bado wapo madarakani?
      By Papa Diana in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 1
      Last Post: 1st March 2011, 15:37
    3. Mawaziri Wataotemwa Hawa Hapa.
      By Pasco in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 42
      Last Post: 14th November 2010, 18:42
    4. Baada ya Dege feki, rada feki, R'Mond feki, sasa uwanja feki
      By emedichi in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 7
      Last Post: 21st April 2008, 14:14
    5. Wenye kinga ni Rais, Makamu, Waziri Mkuu, mawaziri
      By BAK in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 2
      Last Post: 24th November 2007, 08:44

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...