| Find/Invite Friends | Register | Calendar | Search | Today's Posts | Mark Forums Read |
| FAQ | Members List | Bongo Flava | Zilipendwa | Taarab | Injili |
|
|
#1 | |||||||||||
|
||||||||||||
|
Views: 5083
|
||||||||||||
|
#2
|
|||||||||||
|
|||||||||||
|
..zenj ni ya waarabu!
..kwa kuwa wao ndo waliokuwa wakimiliki eneo hilo la afrika kipindi hicho. ..zenj ni nchi kubwa ijitawalie yenyewe mambo yake na si kuwa kama mkoa! ..ina maana kwamba zenj imedhulumiwa aridhi yake iliyo bara mashariki mwa afrika! ..ina maana zenj ni ile ya zamani,na haiwezi badilika moyoni mwa watu! ..ina maana zenj haipo tena,lilobaki ni jina!
__________________
Dar na Lamu yote ni miji ya pwani,lakini haifanani! |
|
#3
|
|||||||||||
|
|||||||||||
|
JokaKuu,
Pokea 5 kwa hii thread! JF inatupa mwanga kweli! Niniuliza swali moja dogo- "kizungumkuti" maana yake ni nini? Neno linatumika tu Zenj au pia Pwani/bara? |
|
#4
|
||||||||||||
|
||||||||||||
Mengine yote safi lakini kisha likoroga,siwezi hata kummaliza! Wakati wenzetu nchi kama Marekani wanajaribu kwa kila hali kufuta kasumba za kutawaliwa ktk elimu zao na kufundisha mwanzo mpya wenye mwanga, leo kiongozi anaturudisha karne 10 nyuma tukumbukie Dola ambayo ilitukuza zaidi biashara ya Utumwa wa mwafrika!.Huyu jamaa hawezi kabisa kuzungumza nje ya asili yake mwenyewe na hii ni hatari sana. Ni sawa na Ian Smith ahutubie kwa kuanza kusikifia historia ya Utawala wa kaburu!
__________________
Exploration of reality Last edited by Mkandara; 28th July 2007 at 12:58 AM.. |
||||||||||||
|
#5
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
Mkandara kumbuka kuna tofauti kubwa sana kati ya mtazamo wa watu weusi wa Marekani ambao kwao ukichanganya damu na mtu mweupe japo kiduchu basi wewe ni mtu mweusi hata kama una rangi nyeupe vipi. Mtazamo huo ukasababisha watu weusi wawe na mtazamo hasi wa watu weupe na kujivunia weusi wao. Hata hivyo ukienda Zanzibar na sehemu nyingine ambapo watu wamechangia damu na waarabu watu hujitukuza kwa kuwa na damu ya kiarabu na kutojivunia weusi wao. Utaona kuwa hata kama mtu ni mweusi vipi kwa vile ana nasaba ya kiarabu basi hujiita yeye mwarabu hata kama kwa waarabu wenyewe yawezekana asiwe mwarabu.
Ni hapa ndipo inapokuja dhana ya uarabu siyo rangi au ancestry bali ni tamaduni, mila, n.k Hivyo baadhi yao huhalalisha uarabu wao kwa kudai kuwa uarabu ni nasaba bora. Katika hili utaona mgongano wa mawazo kati ya weusi ambao hawajachangia damu kule Zanzibar na weusi ambao wamechangia damu.
__________________
Nchi hii imewahi kung' oa masultani wa kila aina. Tukianza kuvumilia masultani wakuchaguliwa tutapanda mbegu ya masultani wa kuzaliwa. - Nyerere katika "Uongozi wetu na Hatima ya Tanzania" |
|
#6
|
|||||||||||
|
|||||||||||
|
Mzee Mwanakijiji,
Nimekupata na ndivyo navyoelewa matatizo ya Zanzibar yalipotokea!.. hawa jamaa mpaka leo hii kuna watu hujatambulisha kama Wapemba! na hujisifia kwa Upemba wao. Hao wengine akina point five nao hujiita Ma - colored, kiasi kwamba kuna ujinga fulani ktk baadhi ya watu hawa ambao hujaribu sana kuutangaza bara, sasa wanapokuja huku na kukuta sisi hatuelewi kitu wanashindwa kuelewa kabisa kwa nini hatuwezi kuelewa na kuzitukuza tofauti hizo. Ndio maana hata ktk Mapinduzi utawasikia wakizungumzia Uarabu ama Uislaam kama vile Mapinduzi ni tukio lililokuja kuondoa Uislaam ama rangi za watu. Na kibaya zaidi ni pale wanapozidi kuleta historia za nyuma ambazo ni kumbukumbu mbaya sana kwa mtu mweusi. It's not fun at all! Hawa watu wameshindwa hata kuona kuwa kuundwa kwa CCM Kulikuwa na malengo ya kuondoa kabisa ile historia ya vyama kuwa wawakilishi wa ASILI zao!..wameipoteza historia ya vyama vyao kuwakilisha asili za watu na kuifanya kama ni vyama vyenye demokrasia. That was then leo hii haiwezekani kabisa demokrasia kusimamia rangi za watu. Na kwamba huo ulikuwa mwanzo mpya pamoja na kwamba ni mgumu sana lakini wameshindwa kabisa kutazama mazuri ya mseto huo kwa faida ya kizazi hiki cha Wazanzibar wenye asili tofauti. Lakini bado tu watajaribu kuvuta hawa Masultan ktk hutuba zao jambo ambalo linazidi kuwapa nguvu CCM kuwa hawa jamaa wanamkumbuka sana Sultan. Ndio maana huyu jamaa sina kabisa imani naye hata siku moja! Even Amerika nyenyewe kama taifa, mshikaji wewe unaishi huko! umeona hata sehemu moja wakizungumzia sana mazuri ya Utawala wa Muingereza kabla ya Mapinduzi yao?.. Hapana!... historia kubwa ya nchi hiyo inaanza kwa Abraham Lincon. Sidhani kama kuna asilimia 1 ya wamarekani wanamkumbuka Mtawala wao wa mwisho kama vile sisi tunavyo jaribu kumbuka utawala wa Sultan.
__________________
Exploration of reality |
|
#7
|
|||||||||||
|
|||||||||||
|
Mkandara,
Mbona neno kasumba unalitumia vibaya sana? Ukifuatilia sana basi kila kitu ni kasumba tu, kuanzia wakataoliki kwenye makanisa yao, elimu madarasani, music tunayocheza na kusikiliza nk. Elewa maana ya culture (the way we do things here)utakuta kwa mtu aliyekulia katika jamii fulani hawezi kukwepa baadhi ya mambo ambayo yanatendeka hapo mahali. Utakuwa unamwonea huyu mtu ukimhusisha na kasumba kila saa. Inabidi ukae na Wazanzibar na uwasome na kuwajua ndio utajua mawazo ya Hamad ndio mawazo ya Wazanzibari walio wengi. je hilo ni kasumba? Mimi sina jibu. Kushindwa kutambua historia na culture ya sehemu fulani ndio mwanzo wa migogoro mbalimbali duniani. Ndio maana akina Bush na Blair wanafikiri wanaweza kupeleka democracy Iraq, kumbe sehemu kama zile , bila a very powerful figure mambo hayaendi. |
| The Following User Says Thank You to Mtanzania For This Useful Post: | ||
Mzenji73 (12th December 2009) | ||
|
#8
|
|||||||||||
|
|||||||||||
|
ikiwa kweli hiyo ndio hali basi ipo dhulma kubwa sana inamaana chako kiwe chako changu kiwe chetu duh inafaa muungano kweli uangaliwe tena kwa nini mtu mzima anafanya urafiki na mtoto mdogo hapo pana nini kama si kutaka kumuharibu maana bara ni kubwa sana kuliko visiwa vya zanzibar lakini kosa sio tanganyika bali kosa liko kwa upande wa visiwani wao wakipewa ubalozi tu wa muda hujisahau mpaka watimuliwe ndio huanza tena kulalamika lakini wakiwa kwenye serekali hukaa kimya juzi nilion kwene gazeti waziri wa mambo ya nje kasema kuanzia sasa akienda safari za nje atachukua wajumbe wa baraza la wawakilishi japo mmoja alisema hayo kwenye mwaka koga makunduchi duh jamani kweli huo ni muungano au mtengano mimi nimesema muungano huu hauna muda iko siku watu watagawana mbao mungu ajaalie hiwe hivyo
|
|
#9
|
|||||||||||
|
|||||||||||
|
Wandugu,
1. Seif anaongelea historia ya Wakati wa Usultani na Utumwa ambapo ushawishi wa Zanzibar ulifika mbali hado Kongo! Anashindwa kutambua leo ni 2007, miaka zaidi ya 140 baada ya utumwa na nchi hizi ziko huru na bara lote la Afrika pia! Kwa hiyo yeye angependa Zanzibar itawale eneo la Afrika Mash. Kama wakati wa Usltani? Hayo ni mabo ya zamani- na hapo anakosea! 2. Nyerere na Karume waliona mwanzoni kuwa na serikali tatu- hiyo ya tatu intagharmiwa na nani na kwa utaratibu gani? Manake Zanzibar ina watu 1 milion- halafu Bara 37 milion- total commitment ya kuchangia hii ya Muungano (Serikali ya tatu) ingekuwa taabu kiasi- mwanzoni ilikuwa hivyo. Sijui kama jawabu sasa ni serikali tatu tu! Kwa hiyo zikishakuwepo serikali tatu matatizo ya Zanzibar yataisha? 3. Je matatizo anayeyaongelea Seif- je yahusiana na Muundo wa Muungano tu? Mbona ukiangalia mfano mgawo wa misaada wa 4.5% bado ni mkubwa ukilinganisha na idadi ya watu- actually ingebidi iwe 2.6% ukifanya cross multiplication. Halafu kama ni hii dhana ya misaada- ndo siku zote inaturidisha nyuma Watanzania- eti Muungano unawakatia msaada- je Comoro, Madagaska- leo wako wapi- wana nafuu zaidi ya Tanzania? 4. Haya anayoongelea Seif- hayajengi yanaangalia upande mmoja tu wa udhaifu wa Muungano- hakuna ndoa ambayo haina matatizo- ila hatuwezi kuangalia matatizo tu siku zote- vi vema naye Seif ajenge positive image over Muungano- yeye ukisoma hutuba yake ni malalamiko zaidi- mengine ya kweli, ila anayatumia kisiasa kujijenga! 5. Tatizo jingine pia hakuna uzalishaji- hakuna viwanda- vichache vilivyokuwepo kama cha sukari kilifungwa- je hii inatokana na Muungano? Bei ya karafuu imeshuka- kama ilivyo bei ya kahawa- je Seif atalaumu Muungano? Hayo mafuta yanaongelewa- siku nyingi- je ni Muungano ulikataa yasichimbwe? Inaonekana kila tatizo Zanzibar Seif analaumu Muungano na bara- kwa hiyo watu wamebaki kulaumu tuu- Wapemba wengi wengi wapo Bara, pia Waunguja- wana maduka makubwa ya jumla ya nguo kariakoo- je kuna mtu toka Bara amelaumu! Seif atambue tu watu wa Visiwani ni Watanzania wenzetu- na tunaishi kwa pamoja, hatubaguani- miaka 40 sasa! Swala la kutafuta Mchawi wa matatizo ya Zanzibar na kusema ni Muungano- tu nafikiri Seif anakosea! |
|
#10
|
||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
labda hapa naomba tusaidiwe, mtumwa alikuwa na haki gani chini ya utawala wa waarabu, na wakati utawala wa Sultani unaota mizizi watu weusi (waislamu na wasio waislamu) walikuwa wanafurahia haki gani? Naomba nisaidiwe ni kitu gani mimi kama mtu huru leo hii kinishawishi ili niutamani utawala wa Sultani? Na kwa upande wa ndugu zetu wa Zanzibari, je ni kitu gani ambacho wanakimiss sana toka utawala wa Sultani?
__________________
Nchi hii imewahi kung' oa masultani wa kila aina. Tukianza kuvumilia masultani wakuchaguliwa tutapanda mbegu ya masultani wa kuzaliwa. - Nyerere katika "Uongozi wetu na Hatima ya Tanzania"
«
Previous Thread
|
Next Thread
»
Tuma Ukurasa huu kwa rafiki yako! All times are GMT +3. The time now is 02:02 PM.
Powered by JamiiForums.com
Copyrights reserved to JamiiForums.com | ||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||