Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka - JamiiForums |The Home of Great Thinkers

Go Back   JamiiForums |The Home of Great Thinkers > Public Forums > Jukwaa la Siasa


Jukwaa la Siasa Tanzania & World Politics General Discussion Forum. You need to be registered in order to post your comment(s)


Reply
 
LinkBack Thread Tools Rate Thread Display Modes
Old 6th October 2009, 09:36 AM   #1
Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka
Bill Bill is offline 6th October 2009, 09:36 AM

RAIS Jakaya Kikwete amekubali kustaafu kwa lazima kwa Mwansheria Mkuu wa Serikali, Bw. Johnson Mwanyika, ifikapo Novemba 6, mwaka huu.
Bw. Mwanyika anastaafu kwa lazima katika kipindi ambacho Mkutano wa 17 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania utakuwa ukiendelea, ukitarajia kuhitimisha sakata la mkataba tata wa Richmond, ambao ulisainiwa wakati akiwa Mshauri Mkuu wa Serikali wa mambo yote ya kisheria.

Habari za kustaafu kwa lazima Bw. Mwanyika ambaye amekanusha mara kadhaa kuhusika kwake na Richmond, zimethibitishwa Dar es Salaam jana na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma.

Majibu ya maandishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma kwa gazeti hili, iliyosainiwa na Mkuu wa Kitengo cha Habari, Elimu na Mawasiliano (OR-MUU) Bi. Zamarad Kawawa, ilieleza; "Bw. Mwanyika amekubaliwa kustaafu atakapofikisha umri wa kustaafu kwa lazima wa miaka 60 ifikapo tarehe 6 Novemba, 2009."

Hatua ya Bw. Mwanyika kukubaliwa kutaafu kwa lazima inaibua maswali mengi, hasa kwa kuzingatia kuwa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kifungu cha 59, haina kipengele kinachoeleza kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali atastaafu baada ya kufikisha umri wa miaka 60.

Kifungu kidogo cha (5) kinaeleza kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali atashika madaraka yake mpaka (a) uteuzi wake utakapofutwa na Rais au (b) mara tu kabla ya Rais mteule kushika madaraka ya Rais.

Kwa maana hiyo ya katiba Bw. Mwanyika angeweka kuacha kushika wadhifa huo ama kwa kuachishwa na Rais au kusubiri mwakani baada ya Uchaguzi Mkuu, kabla ya Rais mteule kushika wadhifa wa rais.

Kutokana na wadhifa wake huo, baada ya mkataba kati ya TANESCO na Richmond Development Company LLC kusainiwa, na baadaye bunge kuuda Kamati Teule ya kuchunguza utata uliogubika mkataba huo chini ya Dkt. Harrison Mwakyembe (Kyela), ilibainika kuwa utiaji saini mkataba huo ulisheheni makosa mengi.

Wakati akiwasilisha taarifa ya kamati iliyochungusa utiaji saini mkataba huo bungeni, Dkt. Mwakyembe alisema;

"Mkataba umesheheni makosa mengi ya kisheria yanayoashiria udhaifu mkubwa wa kitaalamu katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali au ukosefu wa umakini katika kuiwakilisha serikali."

Dkt. Mwakyemba alisema Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Wakili wa Serikali, Bw. Donald Chidowu ambaye ushiriki wake katika GNT haukuwa na tija yoyote, hivyo, "Wawajibishwe na mamlaka ya juu ya nchi kwa kuchangia kuiingiza nchi katika mkataba wa aibu," alisema Dkt. Mwakyembe wakati akiwasilisha mapendekezo ya Kamati yake kwa bunge kuhusu hatua alizopaswa kuchukuliwa Mwanyika.

Baada ya Kamati hiyo kutoa mapendekezo hayo, Serikali kupitia Waziri Mkuu, Bw. Mizengo Pinda, ilitoa ufafanuzi kuhusu utekelezaji wa mapendekezo ya kamati, akisema kikatiba, Mamlaka ya Nidhamu ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

"Kwa hiyo, Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambaye alikuwa miongoni mwa watendaji wakuu watatu waliokuwa wanaishauri Serikali, suala lake la kuhusishwa kwake katika mchakato mzima wa mkataba huo linashughulikiwa na Ofisi ya Rais, IKULU," alisema Bw. Pinda.

Hata hivyo, katika Mkutano wa 16 wa Bunge uliomalizika mjini Dodoma, Serikali kupitia Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Bw. Adam Malima, ilitangaza utekelezaji wa awamu ya pili mapendekezo ya Kamati ya Dkt. Mwakyembe, ambapo alisema Bw. Mwanyika hakuwa na kosa analoonekana kutenda kutokana na wadhifa wake huo.

Bw. Malima alisema iwapo mtumishi yeyote wa umma atatajwa na watuhumiwa walioko mahakamani kuwa alihusika katika makosa ya jinai, Serikali haitasita kumfikisha mahakamani

Hata hivyo utekelezaji wa mapendekezo hayo pamoja na yaliyohusu maofisa wengine ulikataliwa na Bunge na kuiagiza Serikali kuwasilisha upya utekelezaji mwingine wa maazimio yake katika mkutano wa Bunge unaotarajiwa kuanzia Oktoba 27, mwaka huu siku tisa kabla ya Bw. Mwanyika kustaafu.

Source: Majira 06 October 2009
Mwandishi: Reuben Kagaruki


Bill
JF Senior Expert Member
Points: 190,494, Level: 100 Points: 190,494, Level: 100 Points: 190,494, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
Join Date: Fri Oct 2007
Posts: 604
Thanks: 30
Thanked 22 Times in 11 Posts
Views: 1610
Reply With Quote
  #2  
Old 6th October 2009, 09:46 AM
Josh Michael's Avatar
Josh Michael Josh Michael is offline
Josh Michael has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 380,205, Level: 100 Points: 380,205, Level: 100 Points: 380,205, Level: 100
Activity: 8% Activity: 8% Activity: 8%
 
Join Date: Fri Jun 2009
Location: Kibandani
Posts: 1,634
Thanks: 389
Thanked 55 Times in 42 Posts
Rep Power: 24
Josh Michael will become famous soon enoughJosh Michael will become famous soon enoughJosh Michael will become famous soon enoughJosh Michael will become famous soon enoughJosh Michael will become famous soon enoughJosh Michael will become famous soon enoughJosh Michael will become famous soon enoughJosh Michael will become famous soon enough
Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

Muda wake umefika labda naye anatayarishiwa mashitaka ya kupelekwa mahakamani.. maana sasa hana ofisi.. itakuwa vizuri labda wakafuata ushauri wa kamati ya Mwakyembe wa kuwajibisha wote kwenye scandal ya Richmond. Naomba kujua wakuu amestafu yeye mwenyewe au ndio umiri wake umefika au amembiwa kufanya hivyo??
__________________
Those who are too smart to engage in politics are punished by being governed by those who are dumber. ~Plato
Reply With Quote
  #3  
Old 6th October 2009, 11:07 AM
Mafuchila Mafuchila is offline
Mafuchila a creator, not a reactor.
JF Senior Expert Member
Points: 302,577, Level: 100 Points: 302,577, Level: 100 Points: 302,577, Level: 100
Activity: 1% Activity: 1% Activity: 1%
 
Join Date: Sat Apr 2006
Posts: 827
Thanks: 0
Thanked 3 Times in 3 Posts
Rep Power: 25
Mafuchila will become famous soon enoughMafuchila will become famous soon enoughMafuchila will become famous soon enoughMafuchila will become famous soon enoughMafuchila will become famous soon enoughMafuchila will become famous soon enoughMafuchila will become famous soon enoughMafuchila will become famous soon enough
Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

Mambo haya ndio yanasababisha serikali kuonekana inalichezea Bunge. Kama amekubaliwa kustaafu, manake hajachukuliwa hatua zozote za kinidhanimu kama ilivyoshauriwa na Bunge. Kwa kweli kama Mwanyika amekubaliwa kustaafu bila ya kulazimishwa kisheria (Kuwajibishwa) basi kwa mara nyingine serikali yetu imetuthibitishia kuwa in wenyewe, na wenyewe ni wale waliomtuma Mwanyika kukubaliana na RICHMOND kama ilivyo na wao watamlinda, na kweli wamemlinda mpaka amestaafu.
Tatizo naona mkataba kati ya Mwanyika na walimtuma ni kumlinda akiwa kazini, nafikiri akitoka hapo itabidi atafute pa kujificha kwani uchaguzi unakaribia na JK anatafuta kura za imani, asije akawa mhanga wa sifa za serikali.
__________________
Now is the time to cut off the infected parts of society from active public life, before they endanger the entire body politic.
Reply With Quote
  #4  
Old 6th October 2009, 11:25 AM
Omumura Omumura is online now
Omumura has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 78,655, Level: 100 Points: 78,655, Level: 100 Points: 78,655, Level: 100
Activity: 11% Activity: 11% Activity: 11%
 
Join Date: Thu Aug 2009
Posts: 325
Thanks: 16
Thanked 54 Times in 29 Posts
Rep Power: 21
Omumura will become famous soon enoughOmumura will become famous soon enoughOmumura will become famous soon enoughOmumura will become famous soon enoughOmumura will become famous soon enoughOmumura will become famous soon enoughOmumura will become famous soon enoughOmumura will become famous soon enough
Exclamation Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

Wakuu ile dana dana iliyokuwepo ya kumshtaki sasa imejionesha wazi ilikuwa inafanywa makusudi ili jamaa astaafu n apate mafao yake, walah haki ya mafisadi, hafungwi mtu hapo!!
Reply With Quote
  #5  
Old 6th October 2009, 11:26 AM
Shishye's Avatar
Shishye Shishye is offline
Shishye has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 71,840, Level: 100 Points: 71,840, Level: 100 Points: 71,840, Level: 100
Activity: 3% Activity: 3% Activity: 3%
 
Join Date: Thu Feb 2009
Location: On earth
Posts: 253
Thanks: 0
Thanked 41 Times in 21 Posts
Rep Power: 21
Shishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enough
Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

Huu ni mwendelezo wa Tanzania zaidi ya uijuavyo! Hakuna hata mmoja aliyewajibishwa tangu varangati la Richmond lianze licha ya kuwepo kwa ushahidi wa wazi. Itakuwa si haki kumwajibisha Mwanyika peke yake ilhali vigogo wenzake wameachiwa kuendelea na pensheni zao. Serikali yetu inajali "watu wake" na imeapa kuwalinda kwa kila hali.

Watafanya watakalo maana wanajua hamuwezi kuwafanya lolote. Hata uraisi bado wataendelea nao mwakani.
__________________
"Chunguza Mjomba, Utabaini!"
Reply With Quote
  #6  
Old 6th October 2009, 12:12 PM
Kigogo's Avatar
Kigogo Kigogo is offline
Kigogo amekatazwa kuvaa suti
JF Premium Member
Points: 110,288, Level: 100 Points: 110,288, Level: 100 Points: 110,288, Level: 100
Activity: 23% Activity: 23% Activity: 23%
 
Join Date: Fri Dec 2007
Location: Kipatimu
Posts: 1,428
Thanks: 17
Thanked 257 Times in 182 Posts
Rep Power: 25
Kigogo will become famous soon enoughKigogo will become famous soon enoughKigogo will become famous soon enoughKigogo will become famous soon enoughKigogo will become famous soon enoughKigogo will become famous soon enoughKigogo will become famous soon enoughKigogo will become famous soon enough
Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

nchi haina rais makini unategemea nini.those kind of games utazisikia sana na hilo bunge lijalo hakuna cha maana kitakachoaamuliwa juu ya RICHMOND,wataanza kubishana tu kwa nini kuna mgao wa umeme and that is it
__________________
_______________________________
Kagatui kamusii atiagwako ageni=The Oilskin of the house is not for rubbing on the skin of strangers
Reply With Quote
  #7  
Old 6th October 2009, 12:18 PM
Congo Congo is offline
Congo has no status.
Senior Member
Points: 91,533, Level: 100 Points: 91,533, Level: 100 Points: 91,533, Level: 100
Activity: 2% Activity: 2% Activity: 2%
 
Join Date: Thu Mar 2008
Posts: 194
Thanks: 13
Thanked 17 Times in 11 Posts
Rep Power: 22
Congo will become famous soon enoughCongo will become famous soon enoughCongo will become famous soon enoughCongo will become famous soon enoughCongo will become famous soon enoughCongo will become famous soon enoughCongo will become famous soon enoughCongo will become famous soon enough
Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

Sioni ubaya wowote kustaafu. Kwanza keshatimiza miaka 60 ambao ni umri wa lazima wa mtumishi wa serikali kustaafu. Ingawa inaweza kuonekana ni kulea maovu lakini watumishi wa serikali wafanyapo makosa (ingawa makosa mengine hayatangazwi) na kuwajibika kuadhibiwa, na hasa suala la kufukuzwa kazi, mara nyingi umri wao huangaliwa kabla ya adhabu kutolewa. Hii haiko kisheria lakini ni suala la ubinadamu tu. Hata mahakamani inatokea adhabu kupunguzwa kwa sababu ya umri.
Wakati mwingine lazima Serikali ionekane imara kuwa haishurutishwi na chombo chochote. Bunge litakapokaa mwezi November itatolewa taarifa kuwa Mwanasheria Mkuu kastaafu kwa lazima. Azimio la bunge litakuwa limetekelezwa.
Wakianza kufukuzana kwa kila kosa linalotokea habaki mtu serikalini. Kastaafu mwacheni aende. Mengine baadae.
Halafu kama ni suala la kuwajibishana kuhusu Richmond wa kuondoka ni wengi.
Reply With Quote
  #8  
Old 6th October 2009, 12:18 PM
FirstLady1's Avatar
FirstLady1 FirstLady1 is online now
FirstLady1 has no status.
JF Premium Member
Points: 303,030, Level: 100 Points: 303,030, Level: 100 Points: 303,030, Level: 100
Activity: 100% Activity: 100% Activity: 100%
 
Join Date: Wed Jul 2009
Posts: 3,443
Thanks: 561
Thanked 746 Times in 534 Posts
Rep Power: 27
FirstLady1 will become famous soon enoughFirstLady1 will become famous soon enoughFirstLady1 will become famous soon enoughFirstLady1 will become famous soon enoughFirstLady1 will become famous soon enoughFirstLady1 will become famous soon enoughFirstLady1 will become famous soon enoughFirstLady1 will become famous soon enough
Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

aaah siasa za bongo
__________________
2010 niko kikazi zaidi
Reply With Quote
  #9  
Old 6th October 2009, 12:23 PM
Zwangedaba's Avatar
Zwangedaba Zwangedaba is offline
Zwangedaba is making progress!
Member
Points: 67,832, Level: 100 Points: 67,832, Level: 100 Points: 67,832, Level: 100
Activity: 1% Activity: 1% Activity: 1%
 
Join Date: Sun Feb 2009
Posts: 26
Thanks: 0
Thanked 0 Times in 0 Posts
Rep Power: 0
Zwangedaba will become famous soon enoughZwangedaba will become famous soon enoughZwangedaba will become famous soon enoughZwangedaba will become famous soon enoughZwangedaba will become famous soon enoughZwangedaba will become famous soon enoughZwangedaba will become famous soon enoughZwangedaba will become famous soon enough
Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

Labda kuna kitu kinaweza kufuat baada ya huyu jamaa kusitaafu, na ukichukulia kustaafu kweneyewe kumekuwa kwa lazima.
__________________
Praise is well, compliment is well, but affection--that is the last and final and most precious reward that any man can win, whether by character or achievement
Reply With Quote
  #10  
Old 6th October 2009, 12:31 PM
Mchukia Fisadi's Avatar
Mchukia Fisadi Mchukia Fisadi is offline
Mchukia Fisadi is The NEXT MP 2010
JF Premium Member
Points: 309,217, Level: 100 Points: 309,217, Level: 100 Points: 309,217, Level: 100
Activity: 13% Activity: 13% Activity: 13%
 
Join Date: Thu Apr 2008
Location: Southern china
Posts: 2,487
Thanks: 795
Thanked 272 Times in 134 Posts
Rep Power: 26
Mchukia Fisadi will become famous soon enoughMchukia Fisadi will become famous soon enoughMchukia Fisadi will become famous soon enoughMchukia Fisadi will become famous soon enoughMchukia Fisadi will become famous soon enoughMchukia Fisadi will become famous soon enoughMchukia Fisadi will become famous soon enoughMchukia Fisadi will become famous soon enough
Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

Quote:
Quote:
View Post
Sioni ubaya wowote kustaafu. Kwanza keshatimiza miaka 60 ambao ni umri wa lazima wa mtumishi wa serikali kustaafu. Ingawa inaweza kuonekana ni kulea maovu lakini watumishi wa serikali wafanyapo makosa (ingawa makosa mengine hayatangazwi) na kuwajibika kuadhibiwa, na hasa suala la kufukuzwa kazi, mara nyingi umri wao huangaliwa kabla ya adhabu kutolewa. Hii haiko kisheria lakini ni suala la ubinadamu tu. Hata mahakamani inatokea adhabu kupunguzwa kwa sababu ya umri.
Wakati mwingine lazima Serikali ionekane imara kuwa haishurutishwi na chombo chochote. Bunge litakapokaa mwezi November itatolewa taarifa kuwa Mwanasheria Mkuu kastaafu kwa lazima. Azimio la bunge litakuwa limetekelezwa.
Wakianza kufukuzana kwa kila kosa linalotokea habaki mtu serikalini. Kastaafu mwacheni aende. Mengine baadae.
Halafu kama ni suala la kuwajibishana kuhusu Richmond wa kuondoka ni wengi.
Wewe Congo,
Mimi natamani wote wanaohusika na Richmond waondoke kabisa serikalini. Hata kama Kikwete naye ni mhusika aondoke.

Nina hakika nchi inaweza kuenda mbele vizuri bila wababaishaji hawa wezi wakubwa.

Hakuna lolote litakaloharibika hata kama serikali yote iliyo madarakani ikiondoka. Ilimradi tubaki na serikali safi yenye hofu ya Mungu kwa kuwajibika kwao.

Lakini kwa sababu ya ujinga wao na wa baadhi ya watu wanadhani wakiondoka wao basi nchi haitabaki. Ni uongo na udanganyifu wao tu.
Tumechoka na wezi wa mali za nchi yetu hii tuliyopewa wote na mwenye enzi Mungu wetu.
__________________
If OUR God offends you, then I suggest you consider another part of the world as your new home, because OUR God is part of our culture.
Reply With Quote
Reply

Bookmarks

Tags
amkubalia, kikwete, kungoka, mwanyika


Currently Active Users Viewing This Thread: 1 (0 members and 1 guests)
 
Thread Tools
Display Modes Rate This Thread
Rate This Thread:

Posting Rules
You may not post new threads
You may not post replies
You may not post attachments
You may not edit your posts

BB code is On
Smilies are On
[IMG] code is On
HTML code is Off
Trackbacks are Off
Pingbacks are Off
Refbacks are On


Similar Threads
Thread Thread Starter Forum Replies Last Post
Nidhamu ya Chama: Kiini cha Kudorora Viongozi wa CCM! Mzee Mwanakijiji Jukwaa la Siasa 94 13th May 2009 01:45 AM
Urithi wa Kikwete na haiba iso sababu Pundit Jukwaa la Siasa 25 27th December 2008 08:42 AM
Miaka miwili Kikwete Ikulu, tumaini lililopotea Bubu Ataka Kusema Jukwaa la Siasa 2 16th December 2007 11:40 PM
Kikwete Relieved As Mkapa Opts Out Nyamgluu Habari na Hoja mchanganyiko 0 14th July 2006 06:43 AM

Tuma Ukurasa huu kwa rafiki yako!


All times are GMT +3. The time now is 02:09 PM.

Powered by JamiiForums.com
Copyrights reserved to JamiiForums.com