TiGo Says
    Show/Hide This

    Topic: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 30 of 45
    1. #1
      Bill's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th October 2007
      Posts : 1,357
      Rep Power : 813
      Likes Received
      145
      Likes Given
      57

      Default Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

      RAIS Jakaya Kikwete amekubali kustaafu kwa lazima kwa Mwansheria Mkuu wa Serikali, Bw. Johnson Mwanyika, ifikapo Novemba 6, mwaka huu.
      Bw. Mwanyika anastaafu kwa lazima katika kipindi ambacho Mkutano wa 17 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania utakuwa ukiendelea, ukitarajia kuhitimisha sakata la mkataba tata wa Richmond, ambao ulisainiwa wakati akiwa Mshauri Mkuu wa Serikali wa mambo yote ya kisheria.

      Habari za kustaafu kwa lazima Bw. Mwanyika ambaye amekanusha mara kadhaa kuhusika kwake na Richmond, zimethibitishwa Dar es Salaam jana na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma.

      Majibu ya maandishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma kwa gazeti hili, iliyosainiwa na Mkuu wa Kitengo cha Habari, Elimu na Mawasiliano (OR-MUU) Bi. Zamarad Kawawa, ilieleza; "Bw. Mwanyika amekubaliwa kustaafu atakapofikisha umri wa kustaafu kwa lazima wa miaka 60 ifikapo tarehe 6 Novemba, 2009."

      Hatua ya Bw. Mwanyika kukubaliwa kutaafu kwa lazima inaibua maswali mengi, hasa kwa kuzingatia kuwa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kifungu cha 59, haina kipengele kinachoeleza kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali atastaafu baada ya kufikisha umri wa miaka 60.

      Kifungu kidogo cha (5) kinaeleza kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali atashika madaraka yake mpaka (a) uteuzi wake utakapofutwa na Rais au (b) mara tu kabla ya Rais mteule kushika madaraka ya Rais.

      Kwa maana hiyo ya katiba Bw. Mwanyika angeweka kuacha kushika wadhifa huo ama kwa kuachishwa na Rais au kusubiri mwakani baada ya Uchaguzi Mkuu, kabla ya Rais mteule kushika wadhifa wa rais.

      Kutokana na wadhifa wake huo, baada ya mkataba kati ya TANESCO na Richmond Development Company LLC kusainiwa, na baadaye bunge kuuda Kamati Teule ya kuchunguza utata uliogubika mkataba huo chini ya Dkt. Harrison Mwakyembe (Kyela), ilibainika kuwa utiaji saini mkataba huo ulisheheni makosa mengi.

      Wakati akiwasilisha taarifa ya kamati iliyochungusa utiaji saini mkataba huo bungeni, Dkt. Mwakyembe alisema;

      "Mkataba umesheheni makosa mengi ya kisheria yanayoashiria udhaifu mkubwa wa kitaalamu katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali au ukosefu wa umakini katika kuiwakilisha serikali."

      Dkt. Mwakyemba alisema Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Wakili wa Serikali, Bw. Donald Chidowu ambaye ushiriki wake katika GNT haukuwa na tija yoyote, hivyo, "Wawajibishwe na mamlaka ya juu ya nchi kwa kuchangia kuiingiza nchi katika mkataba wa aibu," alisema Dkt. Mwakyembe wakati akiwasilisha mapendekezo ya Kamati yake kwa bunge kuhusu hatua alizopaswa kuchukuliwa Mwanyika.

      Baada ya Kamati hiyo kutoa mapendekezo hayo, Serikali kupitia Waziri Mkuu, Bw. Mizengo Pinda, ilitoa ufafanuzi kuhusu utekelezaji wa mapendekezo ya kamati, akisema kikatiba, Mamlaka ya Nidhamu ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

      "Kwa hiyo, Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambaye alikuwa miongoni mwa watendaji wakuu watatu waliokuwa wanaishauri Serikali, suala lake la kuhusishwa kwake katika mchakato mzima wa mkataba huo linashughulikiwa na Ofisi ya Rais, IKULU," alisema Bw. Pinda.

      Hata hivyo, katika Mkutano wa 16 wa Bunge uliomalizika mjini Dodoma, Serikali kupitia Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Bw. Adam Malima, ilitangaza utekelezaji wa awamu ya pili mapendekezo ya Kamati ya Dkt. Mwakyembe, ambapo alisema Bw. Mwanyika hakuwa na kosa analoonekana kutenda kutokana na wadhifa wake huo.

      Bw. Malima alisema iwapo mtumishi yeyote wa umma atatajwa na watuhumiwa walioko mahakamani kuwa alihusika katika makosa ya jinai, Serikali haitasita kumfikisha mahakamani

      Hata hivyo utekelezaji wa mapendekezo hayo pamoja na yaliyohusu maofisa wengine ulikataliwa na Bunge na kuiagiza Serikali kuwasilisha upya utekelezaji mwingine wa maazimio yake katika mkutano wa Bunge unaotarajiwa kuanzia Oktoba 27, mwaka huu siku tisa kabla ya Bw. Mwanyika kustaafu.

      Source: Majira 06 October 2009
      Mwandishi: Reuben Kagaruki



    2. #2
      Josh Michael's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th June 2009
      Location : Kibandani
      Posts : 2,401
      Rep Power : 934
      Likes Received
      22
      Likes Given
      80

      Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

      Muda wake umefika labda naye anatayarishiwa mashitaka ya kupelekwa mahakamani.. maana sasa hana ofisi.. itakuwa vizuri labda wakafuata ushauri wa kamati ya Mwakyembe wa kuwajibisha wote kwenye scandal ya Richmond. Naomba kujua wakuu amestafu yeye mwenyewe au ndio umiri wake umefika au amembiwa kufanya hivyo??
      Those who are too smart to engage in politics are punished by being governed by those who are dumber. ~Plato:D

    3. #3
      Mafuchila's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th April 2006
      Posts : 905
      Rep Power : 798
      Likes Received
      4
      Likes Given
      5

      Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

      Mambo haya ndio yanasababisha serikali kuonekana inalichezea Bunge. Kama amekubaliwa kustaafu, manake hajachukuliwa hatua zozote za kinidhanimu kama ilivyoshauriwa na Bunge. Kwa kweli kama Mwanyika amekubaliwa kustaafu bila ya kulazimishwa kisheria (Kuwajibishwa) basi kwa mara nyingine serikali yetu imetuthibitishia kuwa in wenyewe, na wenyewe ni wale waliomtuma Mwanyika kukubaliana na RICHMOND kama ilivyo na wao watamlinda, na kweli wamemlinda mpaka amestaafu.
      Tatizo naona mkataba kati ya Mwanyika na walimtuma ni kumlinda akiwa kazini, nafikiri akitoka hapo itabidi atafute pa kujificha kwani uchaguzi unakaribia na JK anatafuta kura za imani, asije akawa mhanga wa sifa za serikali.
      Now is the time to cut off the infected parts of society from active public life, before they endanger the entire body politic.

    4. #4
      Omumura's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th August 2009
      Posts : 458
      Rep Power : 535
      Likes Received
      7
      Likes Given
      0

      Exclamation Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

      Wakuu ile dana dana iliyokuwepo ya kumshtaki sasa imejionesha wazi ilikuwa inafanywa makusudi ili jamaa astaafu n apate mafao yake, walah haki ya mafisadi, hafungwi mtu hapo!!

    5. #5
      Shishye's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th February 2009
      Location : On earth
      Posts : 270
      Rep Power : 523
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

      Huu ni mwendelezo wa Tanzania zaidi ya uijuavyo! Hakuna hata mmoja aliyewajibishwa tangu varangati la Richmond lianze licha ya kuwepo kwa ushahidi wa wazi. Itakuwa si haki kumwajibisha Mwanyika peke yake ilhali vigogo wenzake wameachiwa kuendelea na pensheni zao. Serikali yetu inajali "watu wake" na imeapa kuwalinda kwa kila hali.

      Watafanya watakalo maana wanajua hamuwezi kuwafanya lolote. Hata uraisi bado wataendelea nao mwakani.
      "Chunguza Mjomba, Utabaini!"

    6. #6
      Kigogo's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 14th December 2007
      Location : Calabash
      Posts : 5,478
      Rep Power : 1656
      Likes Received
      674
      Likes Given
      183

      Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

      nchi haina rais makini unategemea nini.those kind of games utazisikia sana na hilo bunge lijalo hakuna cha maana kitakachoaamuliwa juu ya RICHMOND,wataanza kubishana tu kwa nini kuna mgao wa umeme and that is it
      ______________________________ _
      Niko tayari kufa huku nimesimama kuliko kuishi huku nimepiga magoti....

    7. #7
      Congo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th March 2008
      Posts : 400
      Rep Power : 599
      Likes Received
      35
      Likes Given
      20

      Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

      Sioni ubaya wowote kustaafu. Kwanza keshatimiza miaka 60 ambao ni umri wa lazima wa mtumishi wa serikali kustaafu. Ingawa inaweza kuonekana ni kulea maovu lakini watumishi wa serikali wafanyapo makosa (ingawa makosa mengine hayatangazwi) na kuwajibika kuadhibiwa, na hasa suala la kufukuzwa kazi, mara nyingi umri wao huangaliwa kabla ya adhabu kutolewa. Hii haiko kisheria lakini ni suala la ubinadamu tu. Hata mahakamani inatokea adhabu kupunguzwa kwa sababu ya umri.
      Wakati mwingine lazima Serikali ionekane imara kuwa haishurutishwi na chombo chochote. Bunge litakapokaa mwezi November itatolewa taarifa kuwa Mwanasheria Mkuu kastaafu kwa lazima. Azimio la bunge litakuwa limetekelezwa.
      Wakianza kufukuzana kwa kila kosa linalotokea habaki mtu serikalini. Kastaafu mwacheni aende. Mengine baadae.
      Halafu kama ni suala la kuwajibishana kuhusu Richmond wa kuondoka ni wengi.

    8. #8
      FirstLady1's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 29th July 2009
      Location : Mama Mwenye Nyumba
      Posts : 12,986
      Rep Power : 3061
      Likes Received
      1905
      Likes Given
      2786

      Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

      aaah siasa za bongo
      Zaburi 35:1 Ee Bwana utete nao wanaoteta nami Upigane nao wanaopigana nami.

    9. #9
      Zwangedaba's Avatar
      Member Array
      Join Date : 1st February 2009
      Posts : 62
      Rep Power : 485
      Likes Received
      0
      Likes Given
      2

      Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

      Labda kuna kitu kinaweza kufuat baada ya huyu jamaa kusitaafu, na ukichukulia kustaafu kweneyewe kumekuwa kwa lazima.
      Praise is well, compliment is well, but affection-that is the last and final and most precious reward that any man can win, whether by character or achievement

    10. #10
      Kaa la Moto's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 24th April 2008
      Location : Bristol
      Posts : 6,168
      Rep Power : 1760
      Likes Received
      217
      Likes Given
      2246

      Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

      Quote By Congo View Post
      Sioni ubaya wowote kustaafu. Kwanza keshatimiza miaka 60 ambao ni umri wa lazima wa mtumishi wa serikali kustaafu. Ingawa inaweza kuonekana ni kulea maovu lakini watumishi wa serikali wafanyapo makosa (ingawa makosa mengine hayatangazwi) na kuwajibika kuadhibiwa, na hasa suala la kufukuzwa kazi, mara nyingi umri wao huangaliwa kabla ya adhabu kutolewa. Hii haiko kisheria lakini ni suala la ubinadamu tu. Hata mahakamani inatokea adhabu kupunguzwa kwa sababu ya umri.
      Wakati mwingine lazima Serikali ionekane imara kuwa haishurutishwi na chombo chochote. Bunge litakapokaa mwezi November itatolewa taarifa kuwa Mwanasheria Mkuu kastaafu kwa lazima. Azimio la bunge litakuwa limetekelezwa.
      Wakianza kufukuzana kwa kila kosa linalotokea habaki mtu serikalini. Kastaafu mwacheni aende. Mengine baadae.
      Halafu kama ni suala la kuwajibishana kuhusu Richmond wa kuondoka ni wengi.
      Wewe Congo,
      Mimi natamani wote wanaohusika na Richmond waondoke kabisa serikalini. Hata kama Kikwete naye ni mhusika aondoke.

      Nina hakika nchi inaweza kuenda mbele vizuri bila wababaishaji hawa wezi wakubwa.

      Hakuna lolote litakaloharibika hata kama serikali yote iliyo madarakani ikiondoka. Ilimradi tubaki na serikali safi yenye hofu ya Mungu kwa kuwajibika kwao.

      Lakini kwa sababu ya ujinga wao na wa baadhi ya watu wanadhani wakiondoka wao basi nchi haitabaki. Ni uongo na udanganyifu wao tu.
      Tumechoka na wezi wa mali za nchi yetu hii tuliyopewa wote na mwenye enzi Mungu wetu.
      Sintamtambua Jakaya Kikwete kama rais wangu maana ni mteule wa NEC.
      ....Pamoja na kansa ya uongozi wa CCM watu wataendelea kukichagua,au watu wanaweza wakachoka na kusema potelea mbali wakachagua chama KINGINE....Julius. Kambarage. NYERERE"

    11. #11
      Shishye's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th February 2009
      Location : On earth
      Posts : 270
      Rep Power : 523
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

      Quote By Congo View Post
      Sioni ubaya wowote kustaafu. Kwanza keshatimiza miaka 60 ambao ni umri wa lazima wa mtumishi wa serikali kustaafu. Ingawa inaweza kuonekana ni kulea maovu lakini watumishi wa serikali wafanyapo makosa (ingawa makosa mengine hayatangazwi) na kuwajibika kuadhibiwa, na hasa suala la kufukuzwa kazi, mara nyingi umri wao huangaliwa kabla ya adhabu kutolewa. Hii haiko kisheria lakini ni suala la ubinadamu tu. Hata mahakamani inatokea adhabu kupunguzwa kwa sababu ya umri.
      Wakati mwingine lazima Serikali ionekane imara kuwa haishurutishwi na chombo chochote. Bunge litakapokaa mwezi November itatolewa taarifa kuwa Mwanasheria Mkuu kastaafu kwa lazima. Azimio la bunge litakuwa limetekelezwa.
      Wakianza kufukuzana kwa kila kosa linalotokea habaki mtu serikalini. Kastaafu mwacheni aende. Mengine baadae.
      Halafu kama ni suala la kuwajibishana kuhusu Richmond wa kuondoka ni wengi.
      Naaaam! Tena watanzania wanajali ubinadamu sana. Lazima unawashangaa sana watu wanojifanya kuwachungua wenzao na kuwaita mafisadi eti? Kufanya makosa kama hayo, wizi na ubadhilifu wa mali ya watanzania ni kosa la kibinadamu tu. Jamani waacheni watanue hadi umri wao wa kustaafu kwa lazima. Dah, ubinadamu!
      "Chunguza Mjomba, Utabaini!"


    12. #12
      Robweme's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 20th May 2009
      Posts : 178
      Rep Power : 492
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

      Quote By Mafuchila View Post
      Mambo haya ndio yanasababisha serikali kuonekana inalichezea Bunge. Kama amekubaliwa kustaafu, manake hajachukuliwa hatua zozote za kinidhanimu kama ilivyoshauriwa na Bunge. Kwa kweli kama Mwanyika amekubaliwa kustaafu bila ya kulazimishwa kisheria (Kuwajibishwa) basi kwa mara nyingine serikali yetu imetuthibitishia kuwa in wenyewe, na wenyewe ni wale waliomtuma Mwanyika kukubaliana na RICHMOND kama ilivyo na wao watamlinda, na kweli wamemlinda mpaka amestaafu.
      Tatizo naona mkataba kati ya Mwanyika na walimtuma ni kumlinda akiwa kazini, nafikiri akitoka hapo itabidi atafute pa kujificha kwani uchaguzi unakaribia na JK anatafuta kura za imani, asije akawa mhanga wa sifa za serikali.
      Nadhani tuvute subira kidogo kwani hata akisitaafu sio kwamba hawezi kuchukuliwa hatua za kisheria.
      Anaweza kusitaafu na akachukuliwa hatua za kisheria vilevile.
      Asante.

    13. #13
      Chakaza's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 10th March 2007
      Location : everywhere
      Posts : 2,336
      Rep Power : 1181
      Likes Received
      317
      Likes Given
      247

      Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

      Tusubiri tuone kama wabunge katika kikao chao cha Novemba kama hili watalipokeaje. Maana hapa wamepigwa changa la macho.
      .
      Hatutajua chochote iwapo hatutahoji na kudadisi

    14. #14
      Tumain's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th June 2009
      Posts : 3,213
      Rep Power : 1094
      Likes Received
      6
      Likes Given
      0

      Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

      Nenda baba nenda iwe kwa kujiuzulu, kwa lazima au kwa umri who care! tunakusubiri mahakamani kama wenzako kina Mgonja na Yona na Mramba etc.

    15. #15
      Shishye's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th February 2009
      Location : On earth
      Posts : 270
      Rep Power : 523
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

      Quote By Robweme View Post
      Nadhani tuvute subira kidogo kwani hata akisitaafu sio kwamba hawezi kuchukuliwa hatua za kisheria.
      Anaweza kusitaafu na akachukuliwa hatua za kisheria vilevile.
      Asante.
      Sio Tanzania!
      Sio chini ya serikali ya Kikwete!
      Sio baada ya kuona kilichotokea kwa watangulizi wa hili saga!

      Hakuna mwenye nia wala haja ya kuwachukulia hatua yoyote yenye tija wote wale waliohusika na njama za kuiibia nchi hii kupitia Ricmond, achilia mbali wizi mwingine wowote. Serikali iko macho "kiulinzi" bwana!
      "Chunguza Mjomba, Utabaini!"

    16. #16
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 26,634
      Rep Power : 22539
      Likes Received
      8482
      Likes Given
      4308

      Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

      Ni upuuzi mtupu. KWA nini hawakutii maelekezo ya bunge walipotakiwa kufanya hivyo? Hivi si ndivyo walivyofanya kwa Mgonja pia?
      mwanakijiji@jamiiforums.com
      Binafsi NAKERWA, NAKASIRISHWA, NA KUCHUKIZWA sana na haya mambo kwamba eti "ameshauriwa vibaya na wasaidizi wake!" Huwa mara zote najiuliza ikiwa anashauriwa vibaya ni kwanini basi kila wakati awe anachukua huo ushauri mbaya!! - NasDaz

    17. #17
      Shishye's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th February 2009
      Location : On earth
      Posts : 270
      Rep Power : 523
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

      Quote By Tumain View Post
      Nenda baba nenda iwe kwa kujiuzulu, kwa lazima au kwa umri who care! tunakusubiri mahakamani kama wenzako kina Mgonja na Yona na Mramba etc.
      Angekuwa ni kweli ana kosa lolote, angeshughulikiwa akiwa bado ofisini. Huu ni uzushi tu, Mwanyika ni mtu safi. Anastaafu baada ya kuifanyia "serikali" yake kazi ya kukumbukwa na anaondoka na pensheni yake. Hata wazusshi wakijifanya kumzonga mahakamani, mambo hayatakuwa tofauti na yaliyowatokea mafisadi wa EPA. Kelele kwa sana but business as ususal!
      "Chunguza Mjomba, Utabaini!"

    18. #18
      Shishye's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th February 2009
      Location : On earth
      Posts : 270
      Rep Power : 523
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

      Quote By Mzee Mwanakijiji View Post
      Ni upuuzi mtupu. KWA nini hawakutii maelekezo ya bunge walipotakiwa kufanya hivyo? Hivi si ndivyo walivyofanya kwa Mgonja pia?
      Hii inaonyeesha wazi jinsi gani Bunge letu lipo tu. Hivi kuna haja gani ya kuwa nalo?
      "Chunguza Mjomba, Utabaini!"

    19. #19
      Tumain's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th June 2009
      Posts : 3,213
      Rep Power : 1094
      Likes Received
      6
      Likes Given
      0

      Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

      Quote By Shishye View Post
      Angekuwa ni kweli ana kosa lolote, angeshughulikiwa akiwa bado ofisini. Huu ni uzushi tu, Mwanyika ni mtu safi. Anastaafu baada ya kuifanyia "serikali" yake kazi ya kukumbukwa na anaondoka na pensheni yake. Hata wazusshi wakijifanya kumzonga mahakamani, mambo hayatakuwa tofauti na yaliyowatokea mafisadi wa EPA. Kelele kwa sana but business as ususal!
      Mahakama ndio ita-detrmine ana makosa au hana makosa kama mahakama itamkuta ni mtu safi then --- wananchi kama mimi nasema "ishi salama na watoto wako"
      Hivyo hivyo kwa wazee wa EPA kina Mramba, Yona na Mgonja mahakama ikisema ni watu safi too me is a fair play wakaishi salama na watoto wao! maana ulitaka serikali ifanyeje? justice as per our system iko mahakamani kama wewe una-alternative tuambie! tujue!

    20. #20
      Shishye's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th February 2009
      Location : On earth
      Posts : 270
      Rep Power : 523
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

      Quote By Tumain View Post
      Mahakama ndio ita-detrmine ana makosa au hana makosa kama mahakama itamkuta ni mtu safi then --- wananchi kama mimi nasema "ishi salama na watoto wako"
      Hivyo hivyo kwa wazee wa EPA kina Mramba, Yona na Mgonja mahakama ikisema ni watu safi too me is a fair play wakaishi salama na watoto wao! maana ulitaka serikali ifanyeje? justice as per our system iko mahakamani kama wewe una-alternative tuambie! tujue!
      Sikuelewi! Mimi nimesema Mwanyika ni mtu safi maana hajashtakiwa wala hatashtakiwa mpaka aachie ofisi. Nimesema angekuwa na kosa lolote angeshtakiwa kabla hata ya kustaafu. Alternative gani nyingine unataka usikie toka kwangu?
      "Chunguza Mjomba, Utabaini!"

    21. #21
      Fundi Mchundo's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 9th November 2007
      Posts : 4,276
      Rep Power : 2611
      Likes Received
      90
      Likes Given
      65

      Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

      Hivi tena kama kuna kitu kinachoitwa kustaafu kwa lazima kwa nini mtu uombe tena kibali cha kustaafu? Si angekaa kimya hadi hapo ambapo angeombwa kuongeza muda kwa mkataba maalum. Hapo ndipo angeweza kukataa kuongeza muda. Au waandishi wanataka ku-spin kuonyesha kama vile amelazimishwa? Ninachohisi ni kuwa jamaa alimtaarifu Mkuu kuwa muda wake wa kustaafu unakaribia. Si vinginevyo.

      Amandla......
      Fundi Utumbo

    22. BAK is offline
      BAK
      #22
      BAK's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 11th February 2007
      Location : Mfaranyaki
      Posts : 21,195
      Rep Power : 28219
      Likes Received
      3511
      Likes Given
      4311

      Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

      Quote By Shishye View Post
      Sio Tanzania!
      Sio chini ya serikali ya Kikwete!
      Sio baada ya kuona kilichotokea kwa watangulizi wa hili saga!

      Hakuna mwenye nia wala haja ya kuwachukulia hatua yoyote yenye tija wote wale waliohusika na njama za kuiibia nchi hii kupitia Ricmond, achilia mbali wizi mwingine wowote. Serikali iko macho "kiulinzi" bwana!
      Kikwete asema, "Najivunia rekodi yangu ya kupambana na ufisadi nchini." Mnategemea nini Waungwana! ndiyo maana nimesema huyu jamaa hastahili kabisa kugombea 2010. Akitaka kugombea kwa maoni yangu ni namna nyingine ya ufisadi kutaka kugombea kuiongoza nchi wakati uongozi umeshakushinda na kuna ushahidi wa kutosha kuhusu kushindwa kwake uongozi.
      Let your graceful words fly out into the World, carried on winds of courage, imagination and joy. Let them inspire others to step into action

    23. #23
      Kamakabuzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd December 2007
      Posts : 967
      Rep Power : 727
      Likes Received
      103
      Likes Given
      187

      Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

      Quote By Josh Michael View Post
      Naomba kujua wakuu amestafu yeye mwenyewe au ndio umiri wake umefika au amembiwa kufanya hivyo??

      "Bw. Mwanyika amekubaliwa kustaafu atakapofikisha umri wa kustaafu kwa lazima wa miaka 60 ifikapo tarehe 6 Novemba, 2009."

      Hatua ya Bw. Mwanyika kukubaliwa kutaafu kwa lazima inaibua maswali mengi, hasa kwa kuzingatia kuwa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kifungu cha 59, haina kipengele kinachoeleza kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali atastaafu baada ya kufikisha umri wa miaka 60.

      Kifungu kidogo cha (5) kinaeleza kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali atashika madaraka yake mpaka (a) uteuzi wake utakapofutwa na Rais au (b) mara tu kabla ya Rais mteule kushika madaraka ya Rais.

      Kwa maana hiyo ya katiba Bw. Mwanyika angeweza kuacha kushika wadhifa huo ama kwa kuachishwa na Rais au kusubiri mwakani baada ya Uchaguzi Mkuu, kabla ya Rais mteule kushika wadhifa wa rais."


      Majibu ya swali lako yamo katika maelezo hayo. Ukisoma between the lines utagundua kuwa kuna kitu hapo, lakini bado huyo ni samaki wa kawaida na katika kundi lake bado Hosea! Mapapa bado kabisa hawajaguswa na huenda wasiguswe kabisa kwani JK wakati anajibu maswali tulimsikia wazi akimtetea EL; na baadae EL akaibuka na kusema urafiki wake na JK ulianza zamani, hawawezi kuachana maana hawakukutana barabarani! Je walikutana wapi?

    24. #24
      Mayolela's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st September 2009
      Posts : 385
      Rep Power : 517
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

      Huyu nae anahusika na richmond -tutamshitaki?

    25. #25
      Magezi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th October 2008
      Posts : 2,637
      Rep Power : 1018
      Likes Received
      27
      Likes Given
      33

      Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

      wizi mtupu

    26. #26
      Maane's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 10th July 2008
      Posts : 2,434
      Rep Power : 992
      Likes Received
      71
      Likes Given
      12

      Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

      Kila la heri J. Mwanyika!!! Ukweli ninao ufahamu jamaa hakuwa na raha kabisa na huo wadhifa (from reliable sources). Cheo kile kinakulazimisha kufanya uproffessional decissions!!!! Hakupenda!!! Believe it or not. Ni kwa muda mrefu alitaka ajiuzulu!!! Ingeleta mtikisiko!!!
      "Kama unaingia Ikulu kwa njia ya rushwa, je ni biashara gani iko huko ya kuwezesha kulipa fadhila ya rushwa hiyo???"

    27. #27
      Pdidy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd November 2007
      Posts : 11,463
      Rep Power : 3226
      Likes Received
      1045
      Likes Given
      714

      Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

      Huyu nae anajipanga kuelekea mahakamani;hamkumbuki mgonja jamani;nyie subirini watastaafu wengi mwezi wa kumi na moja naona walichofanya ni kusoma na kuwahi nyakati mapema wajipange na mawakili wa kuwasimamia kesi zao

      kazi unayo jk;fadhila zinakuponza;uliambiwa ukawadharau watu;kitumbua kinakutokea puani liveeeeeeeeeeeeeeeeeeee

    28. #28
      Lunyungu's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 7th August 2006
      Location : Malampaka
      Posts : 7,109
      Rep Power : 2327
      Likes Received
      467
      Likes Given
      0

      Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

      Quote By Mchukia Fisadi View Post
      Wewe Congo,
      Mimi natamani wote wanaohusika na Richmond waondoke kabisa serikalini. Hata kama Kikwete naye ni mhusika aondoke.

      Nina hakika nchi inaweza kuenda mbele vizuri bila wababaishaji hawa wezi wakubwa.

      Hakuna lolote litakaloharibika hata kama serikali yote iliyo madarakani ikiondoka. Ilimradi tubaki na serikali safi yenye hofu ya Mungu kwa kuwajibika kwao.

      Lakini kwa sababu ya ujinga wao na wa baadhi ya watu wanadhani wakiondoka wao basi nchi haitabaki. Ni uongo na udanganyifu wao tu.
      Tumechoka na wezi wa mali za nchi yetu hii tuliyopewa wote na mwenye enzi Mungu wetu.

      Maneno haya ni mazito nayameniingia . Hofu ya Mungu na heshima kwa Watanzania walio iweka serikali madarakani .

    29. #29
      Keil's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd July 2007
      Posts : 2,374
      Rep Power : 1036
      Likes Received
      724
      Likes Given
      291

      Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

      Msije mkashangaa mkisikia kwamba Maria Kejo ndiyo Mwanasheria wa Mkuu Serikali ambaye atajaza nafasi itakayoachwa wazi na Bwana Mwanyika.

    30. #30
      WomanOfSubstance's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 30th May 2008
      Posts : 5,464
      Rep Power : 1626
      Likes Received
      655
      Likes Given
      662

      Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

      Quote By Zwangedaba View Post
      Labda kuna kitu kinaweza kufuat baada ya huyu jamaa kusitaafu, na ukichukulia kustaafu kweneyewe kumekuwa kwa lazima.
      Huyu Mkuu ni bahati mbaya tu kajikuta kwenye mkondo mbaya..otherwise he is A MAN OF IMPECABLE CHARACTER - UPRIGHT IN OTHER WORDS.
      Ukikaa kwenye tenga la samaki wabovu nawe utanuka hata kama hujaoza bado.
      Educating the mind without educating the heart is no education at all.... Aristotle



    Page 1 of 2 12 LastLast

    Similar Topics

    1. Replies: 51
      Last Post: 17th October 2011, 19:45
    2. Kikwete: Serikali yangu inapinga Bw. Gbagbo kung'ang'ania madarakani!
      By Gosbertgoodluck in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 44
      Last Post: 29th January 2011, 06:51
    3. All about Edward Hosea, Mwanyika
      By Masanilo in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 226
      Last Post: 22nd December 2010, 16:16
    4. Mwanyika aongea...
      By Invisible in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 26
      Last Post: 14th March 2008, 07:46
    5. Mwanyika Na Hosea.. Itakuaje??
      By Kinyambiss in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 4
      Last Post: 7th February 2008, 00:59

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...