TMF|JamiiForums Blog
  • Member Login:
http://www.jamiiforums.com/zain.jpg

+ Reply to Topic
Page 1 of 3 1 2 3 LastLast
Results 1 to 20 of 45
  1. #1
    JF Senior Expert Member Bill will become famous soon enough Bill will become famous soon enough Bill will become famous soon enough Bill will become famous soon enough Bill will become famous soon enough Bill will become famous soon enough Bill will become famous soon enough Bill will become famous soon enough
    Join Date
    Fri Oct 2007
    Posts
    772
    Thanks : 61
    Thanked 84 Times in 50 Posts
    Rep Power
    24

    Default Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

    RAIS Jakaya Kikwete amekubali kustaafu kwa lazima kwa Mwansheria Mkuu wa Serikali, Bw. Johnson Mwanyika, ifikapo Novemba 6, mwaka huu.
    Bw. Mwanyika anastaafu kwa lazima katika kipindi ambacho Mkutano wa 17 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania utakuwa ukiendelea, ukitarajia kuhitimisha sakata la mkataba tata wa Richmond, ambao ulisainiwa wakati akiwa Mshauri Mkuu wa Serikali wa mambo yote ya kisheria.

    Habari za kustaafu kwa lazima Bw. Mwanyika ambaye amekanusha mara kadhaa kuhusika kwake na Richmond, zimethibitishwa Dar es Salaam jana na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma.

    Majibu ya maandishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma kwa gazeti hili, iliyosainiwa na Mkuu wa Kitengo cha Habari, Elimu na Mawasiliano (OR-MUU) Bi. Zamarad Kawawa, ilieleza; "Bw. Mwanyika amekubaliwa kustaafu atakapofikisha umri wa kustaafu kwa lazima wa miaka 60 ifikapo tarehe 6 Novemba, 2009."

    Hatua ya Bw. Mwanyika kukubaliwa kutaafu kwa lazima inaibua maswali mengi, hasa kwa kuzingatia kuwa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kifungu cha 59, haina kipengele kinachoeleza kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali atastaafu baada ya kufikisha umri wa miaka 60.

    Kifungu kidogo cha (5) kinaeleza kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali atashika madaraka yake mpaka (a) uteuzi wake utakapofutwa na Rais au (b) mara tu kabla ya Rais mteule kushika madaraka ya Rais.

    Kwa maana hiyo ya katiba Bw. Mwanyika angeweka kuacha kushika wadhifa huo ama kwa kuachishwa na Rais au kusubiri mwakani baada ya Uchaguzi Mkuu, kabla ya Rais mteule kushika wadhifa wa rais.

    Kutokana na wadhifa wake huo, baada ya mkataba kati ya TANESCO na Richmond Development Company LLC kusainiwa, na baadaye bunge kuuda Kamati Teule ya kuchunguza utata uliogubika mkataba huo chini ya Dkt. Harrison Mwakyembe (Kyela), ilibainika kuwa utiaji saini mkataba huo ulisheheni makosa mengi.

    Wakati akiwasilisha taarifa ya kamati iliyochungusa utiaji saini mkataba huo bungeni, Dkt. Mwakyembe alisema;

    "Mkataba umesheheni makosa mengi ya kisheria yanayoashiria udhaifu mkubwa wa kitaalamu katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali au ukosefu wa umakini katika kuiwakilisha serikali."

    Dkt. Mwakyemba alisema Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Wakili wa Serikali, Bw. Donald Chidowu ambaye ushiriki wake katika GNT haukuwa na tija yoyote, hivyo, "Wawajibishwe na mamlaka ya juu ya nchi kwa kuchangia kuiingiza nchi katika mkataba wa aibu," alisema Dkt. Mwakyembe wakati akiwasilisha mapendekezo ya Kamati yake kwa bunge kuhusu hatua alizopaswa kuchukuliwa Mwanyika.

    Baada ya Kamati hiyo kutoa mapendekezo hayo, Serikali kupitia Waziri Mkuu, Bw. Mizengo Pinda, ilitoa ufafanuzi kuhusu utekelezaji wa mapendekezo ya kamati, akisema kikatiba, Mamlaka ya Nidhamu ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

    "Kwa hiyo, Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambaye alikuwa miongoni mwa watendaji wakuu watatu waliokuwa wanaishauri Serikali, suala lake la kuhusishwa kwake katika mchakato mzima wa mkataba huo linashughulikiwa na Ofisi ya Rais, IKULU," alisema Bw. Pinda.

    Hata hivyo, katika Mkutano wa 16 wa Bunge uliomalizika mjini Dodoma, Serikali kupitia Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Bw. Adam Malima, ilitangaza utekelezaji wa awamu ya pili mapendekezo ya Kamati ya Dkt. Mwakyembe, ambapo alisema Bw. Mwanyika hakuwa na kosa analoonekana kutenda kutokana na wadhifa wake huo.

    Bw. Malima alisema iwapo mtumishi yeyote wa umma atatajwa na watuhumiwa walioko mahakamani kuwa alihusika katika makosa ya jinai, Serikali haitasita kumfikisha mahakamani

    Hata hivyo utekelezaji wa mapendekezo hayo pamoja na yaliyohusu maofisa wengine ulikataliwa na Bunge na kuiagiza Serikali kuwasilisha upya utekelezaji mwingine wa maazimio yake katika mkutano wa Bunge unaotarajiwa kuanzia Oktoba 27, mwaka huu siku tisa kabla ya Bw. Mwanyika kustaafu.

    Source: Majira 06 October 2009
    Mwandishi: Reuben Kagaruki


  2. #2
    JF Senior Expert Member Josh Michael will become famous soon enough Josh Michael will become famous soon enough Josh Michael will become famous soon enough Josh Michael will become famous soon enough Josh Michael will become famous soon enough Josh Michael will become famous soon enough Josh Michael will become famous soon enough Josh Michael will become famous soon enough
    Join Date
    Fri Jun 2009
    Location
    Kibandani
    Posts
    2,105
    Thanks : 1,289
    Thanked 235 Times in 179 Posts
    Rep Power
    26

    Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

    Muda wake umefika labda naye anatayarishiwa mashitaka ya kupelekwa mahakamani.. maana sasa hana ofisi.. itakuwa vizuri labda wakafuata ushauri wa kamati ya Mwakyembe wa kuwajibisha wote kwenye scandal ya Richmond. Naomba kujua wakuu amestafu yeye mwenyewe au ndio umiri wake umefika au amembiwa kufanya hivyo??
    Those who are too smart to engage in politics are punished by being governed by those who are dumber. ~Plato:D

  3. #3
    JF Senior Expert Member Mafuchila will become famous soon enough Mafuchila will become famous soon enough Mafuchila will become famous soon enough Mafuchila will become famous soon enough Mafuchila will become famous soon enough Mafuchila will become famous soon enough Mafuchila will become famous soon enough Mafuchila will become famous soon enough
    Join Date
    Sat Apr 2006
    Posts
    868
    Thanks : 7
    Thanked 42 Times in 21 Posts
    Rep Power
    26

    Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

    Mambo haya ndio yanasababisha serikali kuonekana inalichezea Bunge. Kama amekubaliwa kustaafu, manake hajachukuliwa hatua zozote za kinidhanimu kama ilivyoshauriwa na Bunge. Kwa kweli kama Mwanyika amekubaliwa kustaafu bila ya kulazimishwa kisheria (Kuwajibishwa) basi kwa mara nyingine serikali yetu imetuthibitishia kuwa in wenyewe, na wenyewe ni wale waliomtuma Mwanyika kukubaliana na RICHMOND kama ilivyo na wao watamlinda, na kweli wamemlinda mpaka amestaafu.
    Tatizo naona mkataba kati ya Mwanyika na walimtuma ni kumlinda akiwa kazini, nafikiri akitoka hapo itabidi atafute pa kujificha kwani uchaguzi unakaribia na JK anatafuta kura za imani, asije akawa mhanga wa sifa za serikali.
    Now is the time to cut off the infected parts of society from active public life, before they endanger the entire body politic.

  4. #4
    JF Senior Expert Member Omumura will become famous soon enough Omumura will become famous soon enough Omumura will become famous soon enough Omumura will become famous soon enough Omumura will become famous soon enough Omumura will become famous soon enough Omumura will become famous soon enough Omumura will become famous soon enough
    Join Date
    Thu Aug 2009
    Posts
    383
    Thanks : 19
    Thanked 67 Times in 38 Posts
    Rep Power
    22

    Exclamation Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

    Wakuu ile dana dana iliyokuwepo ya kumshtaki sasa imejionesha wazi ilikuwa inafanywa makusudi ili jamaa astaafu n apate mafao yake, walah haki ya mafisadi, hafungwi mtu hapo!!

  5. #5
    JF Senior Expert Member Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough
    Join Date
    Thu Feb 2009
    Location
    On earth
    Posts
    266
    Thanks : 0
    Thanked 47 Times in 26 Posts
    Rep Power
    22

    Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

    Huu ni mwendelezo wa Tanzania zaidi ya uijuavyo! Hakuna hata mmoja aliyewajibishwa tangu varangati la Richmond lianze licha ya kuwepo kwa ushahidi wa wazi. Itakuwa si haki kumwajibisha Mwanyika peke yake ilhali vigogo wenzake wameachiwa kuendelea na pensheni zao. Serikali yetu inajali "watu wake" na imeapa kuwalinda kwa kila hali.

    Watafanya watakalo maana wanajua hamuwezi kuwafanya lolote. Hata uraisi bado wataendelea nao mwakani.
    "Chunguza Mjomba, Utabaini!"

  6. #6
    JF Premium Member Kigogo will become famous soon enough Kigogo will become famous soon enough Kigogo will become famous soon enough Kigogo will become famous soon enough Kigogo will become famous soon enough Kigogo will become famous soon enough Kigogo will become famous soon enough Kigogo will become famous soon enough
    Join Date
    Fri Dec 2007
    Location
    Kipatimu
    Posts
    2,081
    Thanks : 19
    Thanked 433 Times in 325 Posts
    Rep Power
    27

    Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

    nchi haina rais makini unategemea nini.those kind of games utazisikia sana na hilo bunge lijalo hakuna cha maana kitakachoaamuliwa juu ya RICHMOND,wataanza kubishana tu kwa nini kuna mgao wa umeme and that is it
    _______________________________
    Kagatui kamusii atiagwako ageni=The Oilskin of the house is not for rubbing on the skin of strangers

  7. #7
    Senior Member Congo will become famous soon enough Congo will become famous soon enough Congo will become famous soon enough Congo will become famous soon enough Congo will become famous soon enough Congo will become famous soon enough Congo will become famous soon enough Congo will become famous soon enough
    Join Date
    Thu Mar 2008
    Posts
    219
    Thanks : 25
    Thanked 30 Times in 19 Posts
    Rep Power
    23

    Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

    Sioni ubaya wowote kustaafu. Kwanza keshatimiza miaka 60 ambao ni umri wa lazima wa mtumishi wa serikali kustaafu. Ingawa inaweza kuonekana ni kulea maovu lakini watumishi wa serikali wafanyapo makosa (ingawa makosa mengine hayatangazwi) na kuwajibika kuadhibiwa, na hasa suala la kufukuzwa kazi, mara nyingi umri wao huangaliwa kabla ya adhabu kutolewa. Hii haiko kisheria lakini ni suala la ubinadamu tu. Hata mahakamani inatokea adhabu kupunguzwa kwa sababu ya umri.
    Wakati mwingine lazima Serikali ionekane imara kuwa haishurutishwi na chombo chochote. Bunge litakapokaa mwezi November itatolewa taarifa kuwa Mwanasheria Mkuu kastaafu kwa lazima. Azimio la bunge litakuwa limetekelezwa.
    Wakianza kufukuzana kwa kila kosa linalotokea habaki mtu serikalini. Kastaafu mwacheni aende. Mengine baadae.
    Halafu kama ni suala la kuwajibishana kuhusu Richmond wa kuondoka ni wengi.

  8. #8
    JF Premium Member FirstLady1 will become famous soon enough FirstLady1 will become famous soon enough FirstLady1 will become famous soon enough FirstLady1 will become famous soon enough FirstLady1 will become famous soon enough FirstLady1 will become famous soon enough FirstLady1 will become famous soon enough FirstLady1 will become famous soon enough
    Join Date
    Wed Jul 2009
    Posts
    8,039
    Thanks : 1,977
    Thanked 2,973 Times in 1,912 Posts
    Rep Power
    38

    Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

    aaah siasa za bongo
    Malaki 2:15, 16
    Kwa hiyo jihadharini roho zenu; mtu awaye yote asimtende mke wa ujana wake mambo ya hiana. Maana mimi nakuchukia kuachana, asema BWANA.

  9. #9
    Member Zwangedaba will become famous soon enough Zwangedaba will become famous soon enough Zwangedaba will become famous soon enough Zwangedaba will become famous soon enough Zwangedaba will become famous soon enough Zwangedaba will become famous soon enough Zwangedaba will become famous soon enough Zwangedaba will become famous soon enough
    Join Date
    Sun Feb 2009
    Posts
    26
    Thanks : 0
    Thanked 0 Times in 0 Posts
    Rep Power
    0

    Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

    Labda kuna kitu kinaweza kufuat baada ya huyu jamaa kusitaafu, na ukichukulia kustaafu kweneyewe kumekuwa kwa lazima.
    Praise is well, compliment is well, but affection--that is the last and final and most precious reward that any man can win, whether by character or achievement

  10. #10
    JF Premium Member Mchukia Fisadi will become famous soon enough Mchukia Fisadi will become famous soon enough Mchukia Fisadi will become famous soon enough Mchukia Fisadi will become famous soon enough Mchukia Fisadi will become famous soon enough Mchukia Fisadi will become famous soon enough Mchukia Fisadi will become famous soon enough Mchukia Fisadi will become famous soon enough
    Join Date
    Thu Apr 2008
    Location
    Southern china
    Posts
    3,390
    Thanks : 2,354
    Thanked 664 Times in 376 Posts
    Rep Power
    29

    Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

    Quote Originally Posted by Congo View Post
    Sioni ubaya wowote kustaafu. Kwanza keshatimiza miaka 60 ambao ni umri wa lazima wa mtumishi wa serikali kustaafu. Ingawa inaweza kuonekana ni kulea maovu lakini watumishi wa serikali wafanyapo makosa (ingawa makosa mengine hayatangazwi) na kuwajibika kuadhibiwa, na hasa suala la kufukuzwa kazi, mara nyingi umri wao huangaliwa kabla ya adhabu kutolewa. Hii haiko kisheria lakini ni suala la ubinadamu tu. Hata mahakamani inatokea adhabu kupunguzwa kwa sababu ya umri.
    Wakati mwingine lazima Serikali ionekane imara kuwa haishurutishwi na chombo chochote. Bunge litakapokaa mwezi November itatolewa taarifa kuwa Mwanasheria Mkuu kastaafu kwa lazima. Azimio la bunge litakuwa limetekelezwa.
    Wakianza kufukuzana kwa kila kosa linalotokea habaki mtu serikalini. Kastaafu mwacheni aende. Mengine baadae.
    Halafu kama ni suala la kuwajibishana kuhusu Richmond wa kuondoka ni wengi.
    Wewe Congo,
    Mimi natamani wote wanaohusika na Richmond waondoke kabisa serikalini. Hata kama Kikwete naye ni mhusika aondoke.

    Nina hakika nchi inaweza kuenda mbele vizuri bila wababaishaji hawa wezi wakubwa.

    Hakuna lolote litakaloharibika hata kama serikali yote iliyo madarakani ikiondoka. Ilimradi tubaki na serikali safi yenye hofu ya Mungu kwa kuwajibika kwao.

    Lakini kwa sababu ya ujinga wao na wa baadhi ya watu wanadhani wakiondoka wao basi nchi haitabaki. Ni uongo na udanganyifu wao tu.
    Tumechoka na wezi wa mali za nchi yetu hii tuliyopewa wote na mwenye enzi Mungu wetu.
    AISEEEEE-WATANZANIA 2010 HADANGANYIKI MTU. MADILIKO NI MUHIMU.
    CHAGUA DR W. SLAA(SIRAHA) KWA MABADILIKO YA MAENDELEO YA TANZANIA

  11. #11
    JF Senior Expert Member Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough
    Join Date
    Thu Feb 2009
    Location
    On earth
    Posts
    266
    Thanks : 0
    Thanked 47 Times in 26 Posts
    Rep Power
    22

    Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

    Quote Originally Posted by Congo View Post
    Sioni ubaya wowote kustaafu. Kwanza keshatimiza miaka 60 ambao ni umri wa lazima wa mtumishi wa serikali kustaafu. Ingawa inaweza kuonekana ni kulea maovu lakini watumishi wa serikali wafanyapo makosa (ingawa makosa mengine hayatangazwi) na kuwajibika kuadhibiwa, na hasa suala la kufukuzwa kazi, mara nyingi umri wao huangaliwa kabla ya adhabu kutolewa. Hii haiko kisheria lakini ni suala la ubinadamu tu. Hata mahakamani inatokea adhabu kupunguzwa kwa sababu ya umri.
    Wakati mwingine lazima Serikali ionekane imara kuwa haishurutishwi na chombo chochote. Bunge litakapokaa mwezi November itatolewa taarifa kuwa Mwanasheria Mkuu kastaafu kwa lazima. Azimio la bunge litakuwa limetekelezwa.
    Wakianza kufukuzana kwa kila kosa linalotokea habaki mtu serikalini. Kastaafu mwacheni aende. Mengine baadae.
    Halafu kama ni suala la kuwajibishana kuhusu Richmond wa kuondoka ni wengi.
    Naaaam! Tena watanzania wanajali ubinadamu sana. Lazima unawashangaa sana watu wanojifanya kuwachungua wenzao na kuwaita mafisadi eti? Kufanya makosa kama hayo, wizi na ubadhilifu wa mali ya watanzania ni kosa la kibinadamu tu. Jamani waacheni watanue hadi umri wao wa kustaafu kwa lazima. Dah, ubinadamu!
    "Chunguza Mjomba, Utabaini!"

  12. #12
    Senior Member Robweme will become famous soon enough Robweme will become famous soon enough Robweme will become famous soon enough Robweme will become famous soon enough Robweme will become famous soon enough Robweme will become famous soon enough Robweme will become famous soon enough Robweme will become famous soon enough
    Join Date
    Wed May 2009
    Posts
    179
    Thanks : 0
    Thanked 13 Times in 8 Posts
    Rep Power
    22

    Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

    Quote Originally Posted by Mafuchila View Post
    Mambo haya ndio yanasababisha serikali kuonekana inalichezea Bunge. Kama amekubaliwa kustaafu, manake hajachukuliwa hatua zozote za kinidhanimu kama ilivyoshauriwa na Bunge. Kwa kweli kama Mwanyika amekubaliwa kustaafu bila ya kulazimishwa kisheria (Kuwajibishwa) basi kwa mara nyingine serikali yetu imetuthibitishia kuwa in wenyewe, na wenyewe ni wale waliomtuma Mwanyika kukubaliana na RICHMOND kama ilivyo na wao watamlinda, na kweli wamemlinda mpaka amestaafu.
    Tatizo naona mkataba kati ya Mwanyika na walimtuma ni kumlinda akiwa kazini, nafikiri akitoka hapo itabidi atafute pa kujificha kwani uchaguzi unakaribia na JK anatafuta kura za imani, asije akawa mhanga wa sifa za serikali.
    Nadhani tuvute subira kidogo kwani hata akisitaafu sio kwamba hawezi kuchukuliwa hatua za kisheria.
    Anaweza kusitaafu na akachukuliwa hatua za kisheria vilevile.
    Asante.

  13. #13
    JF Premium Member Chakaza will become famous soon enough Chakaza will become famous soon enough Chakaza will become famous soon enough Chakaza will become famous soon enough Chakaza will become famous soon enough Chakaza will become famous soon enough Chakaza will become famous soon enough Chakaza will become famous soon enough
    Join Date
    Sat Mar 2007
    Posts
    1,119
    Thanks : 106
    Thanked 217 Times in 153 Posts
    Rep Power
    26

    Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

    Tusubiri tuone kama wabunge katika kikao chao cha Novemba kama hili watalipokeaje. Maana hapa wamepigwa changa la macho.
    .
    Hatutajua chochote iwapo hatutahoji na kudadisi

  14. #14
    JF Senior Expert Member Tumain will become famous soon enough Tumain will become famous soon enough Tumain will become famous soon enough Tumain will become famous soon enough Tumain will become famous soon enough Tumain will become famous soon enough Tumain will become famous soon enough Tumain will become famous soon enough
    Join Date
    Sun Jun 2009
    Posts
    3,358
    Thanks : 1,173
    Thanked 1,111 Times in 718 Posts
    Rep Power
    28

    Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

    Nenda baba nenda iwe kwa kujiuzulu, kwa lazima au kwa umri who care! tunakusubiri mahakamani kama wenzako kina Mgonja na Yona na Mramba etc.

  15. #15
    JF Senior Expert Member Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough
    Join Date
    Thu Feb 2009
    Location
    On earth
    Posts
    266
    Thanks : 0
    Thanked 47 Times in 26 Posts
    Rep Power
    22

    Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

    Quote Originally Posted by Robweme View Post
    Nadhani tuvute subira kidogo kwani hata akisitaafu sio kwamba hawezi kuchukuliwa hatua za kisheria.
    Anaweza kusitaafu na akachukuliwa hatua za kisheria vilevile.
    Asante.
    Sio Tanzania!
    Sio chini ya serikali ya Kikwete!
    Sio baada ya kuona kilichotokea kwa watangulizi wa hili saga!

    Hakuna mwenye nia wala haja ya kuwachukulia hatua yoyote yenye tija wote wale waliohusika na njama za kuiibia nchi hii kupitia Ricmond, achilia mbali wizi mwingine wowote. Serikali iko macho "kiulinzi" bwana!
    "Chunguza Mjomba, Utabaini!"

  16. #16
    JF Premium Member Mzee Mwanakijiji is on a distinguished road Mzee Mwanakijiji is on a distinguished road Mzee Mwanakijiji is on a distinguished road
    Join Date
    Fri Mar 2006
    Location
    Kijijini
    Posts
    20,614
    Thanks : 13,457
    Thanked 8,383 Times in 2,415 Posts
    Rep Power
    51

    Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

    Ni upuuzi mtupu. KWA nini hawakutii maelekezo ya bunge walipotakiwa kufanya hivyo? Hivi si ndivyo walivyofanya kwa Mgonja pia?
    Hadithi mpya ya "HASIRA YA BABA-2" Inaendelea..!.. angalia kwenye Jukwaa la Mapenzi na Mahusiano! - Search Facebook "mimi mwanakijiji"

  17. #17
    JF Senior Expert Member Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough
    Join Date
    Thu Feb 2009
    Location
    On earth
    Posts
    266
    Thanks : 0
    Thanked 47 Times in 26 Posts
    Rep Power
    22

    Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

    Quote Originally Posted by Tumain View Post
    Nenda baba nenda iwe kwa kujiuzulu, kwa lazima au kwa umri who care! tunakusubiri mahakamani kama wenzako kina Mgonja na Yona na Mramba etc.
    Angekuwa ni kweli ana kosa lolote, angeshughulikiwa akiwa bado ofisini. Huu ni uzushi tu, Mwanyika ni mtu safi. Anastaafu baada ya kuifanyia "serikali" yake kazi ya kukumbukwa na anaondoka na pensheni yake. Hata wazusshi wakijifanya kumzonga mahakamani, mambo hayatakuwa tofauti na yaliyowatokea mafisadi wa EPA. Kelele kwa sana but business as ususal!
    "Chunguza Mjomba, Utabaini!"

  18. #18
    JF Senior Expert Member Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough
    Join Date
    Thu Feb 2009
    Location
    On earth
    Posts
    266
    Thanks : 0
    Thanked 47 Times in 26 Posts
    Rep Power
    22

    Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

    Quote Originally Posted by Mzee Mwanakijiji View Post
    Ni upuuzi mtupu. KWA nini hawakutii maelekezo ya bunge walipotakiwa kufanya hivyo? Hivi si ndivyo walivyofanya kwa Mgonja pia?
    Hii inaonyeesha wazi jinsi gani Bunge letu lipo tu. Hivi kuna haja gani ya kuwa nalo?
    "Chunguza Mjomba, Utabaini!"

  19. #19
    JF Senior Expert Member Tumain will become famous soon enough Tumain will become famous soon enough Tumain will become famous soon enough Tumain will become famous soon enough Tumain will become famous soon enough Tumain will become famous soon enough Tumain will become famous soon enough Tumain will become famous soon enough
    Join Date
    Sun Jun 2009
    Posts
    3,358
    Thanks : 1,173
    Thanked 1,111 Times in 718 Posts
    Rep Power
    28

    Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

    Quote Originally Posted by Shishye View Post
    Angekuwa ni kweli ana kosa lolote, angeshughulikiwa akiwa bado ofisini. Huu ni uzushi tu, Mwanyika ni mtu safi. Anastaafu baada ya kuifanyia "serikali" yake kazi ya kukumbukwa na anaondoka na pensheni yake. Hata wazusshi wakijifanya kumzonga mahakamani, mambo hayatakuwa tofauti na yaliyowatokea mafisadi wa EPA. Kelele kwa sana but business as ususal!
    Mahakama ndio ita-detrmine ana makosa au hana makosa kama mahakama itamkuta ni mtu safi then --- wananchi kama mimi nasema "ishi salama na watoto wako"
    Hivyo hivyo kwa wazee wa EPA kina Mramba, Yona na Mgonja mahakama ikisema ni watu safi too me is a fair play wakaishi salama na watoto wao! maana ulitaka serikali ifanyeje? justice as per our system iko mahakamani kama wewe una-alternative tuambie! tujue!

  20. #20
    JF Senior Expert Member Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough Shishye will become famous soon enough
    Join Date
    Thu Feb 2009
    Location
    On earth
    Posts
    266
    Thanks : 0
    Thanked 47 Times in 26 Posts
    Rep Power
    22

    Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

    Quote Originally Posted by Tumain View Post
    Mahakama ndio ita-detrmine ana makosa au hana makosa kama mahakama itamkuta ni mtu safi then --- wananchi kama mimi nasema "ishi salama na watoto wako"
    Hivyo hivyo kwa wazee wa EPA kina Mramba, Yona na Mgonja mahakama ikisema ni watu safi too me is a fair play wakaishi salama na watoto wao! maana ulitaka serikali ifanyeje? justice as per our system iko mahakamani kama wewe una-alternative tuambie! tujue!
    Sikuelewi! Mimi nimesema Mwanyika ni mtu safi maana hajashtakiwa wala hatashtakiwa mpaka aachie ofisi. Nimesema angekuwa na kosa lolote angeshtakiwa kabla hata ya kustaafu. Alternative gani nyingine unataka usikie toka kwangu?
    "Chunguza Mjomba, Utabaini!"


 

Topic Information

Users Browsing this Topic

There are currently 1 users browsing this thread. (0 members and 1 guests)

     

Tags for this Topic

Bookmarks

Posting Permissions

  • You may not post new threads
  • You may not post replies
  • You may not post attachments
  • You may not edit your posts