Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka - Page 2 - JamiiForums |The Home of Great Thinkers

Go Back   JamiiForums |The Home of Great Thinkers > Public Forums > Jukwaa la Siasa


Jukwaa la Siasa Tanzania & World Politics General Discussion Forum. You need to be registered in order to post your comment(s)


Reply
 
LinkBack Thread Tools Rate Thread Display Modes
Old 6th October 2009, 09:36 AM  
Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka
Bill Bill is offline 6th October 2009, 09:36 AM

RAIS Jakaya Kikwete amekubali kustaafu kwa lazima kwa Mwansheria Mkuu wa Serikali, Bw. Johnson Mwanyika, ifikapo Novemba 6, mwaka huu.
Bw. Mwanyika anastaafu kwa lazima katika kipindi ambacho Mkutano wa 17 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania utakuwa ukiendelea, ukitarajia kuhitimisha sakata la mkataba tata wa Richmond, ambao ulisainiwa wakati akiwa Mshauri Mkuu wa Serikali wa mambo yote ya kisheria.

Habari za kustaafu kwa lazima Bw. Mwanyika ambaye amekanusha mara kadhaa kuhusika kwake na Richmond, zimethibitishwa Dar es Salaam jana na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma.

Majibu ya maandishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma kwa gazeti hili, iliyosainiwa na Mkuu wa Kitengo cha Habari, Elimu na Mawasiliano (OR-MUU) Bi. Zamarad Kawawa, ilieleza; "Bw. Mwanyika amekubaliwa kustaafu atakapofikisha umri wa kustaafu kwa lazima wa miaka 60 ifikapo tarehe 6 Novemba, 2009."

Hatua ya Bw. Mwanyika kukubaliwa kutaafu kwa lazima inaibua maswali mengi, hasa kwa kuzingatia kuwa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kifungu cha 59, haina kipengele kinachoeleza kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali atastaafu baada ya kufikisha umri wa miaka 60.

Kifungu kidogo cha (5) kinaeleza kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali atashika madaraka yake mpaka (a) uteuzi wake utakapofutwa na Rais au (b) mara tu kabla ya Rais mteule kushika madaraka ya Rais.

Kwa maana hiyo ya katiba Bw. Mwanyika angeweka kuacha kushika wadhifa huo ama kwa kuachishwa na Rais au kusubiri mwakani baada ya Uchaguzi Mkuu, kabla ya Rais mteule kushika wadhifa wa rais.

Kutokana na wadhifa wake huo, baada ya mkataba kati ya TANESCO na Richmond Development Company LLC kusainiwa, na baadaye bunge kuuda Kamati Teule ya kuchunguza utata uliogubika mkataba huo chini ya Dkt. Harrison Mwakyembe (Kyela), ilibainika kuwa utiaji saini mkataba huo ulisheheni makosa mengi.

Wakati akiwasilisha taarifa ya kamati iliyochungusa utiaji saini mkataba huo bungeni, Dkt. Mwakyembe alisema;

"Mkataba umesheheni makosa mengi ya kisheria yanayoashiria udhaifu mkubwa wa kitaalamu katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali au ukosefu wa umakini katika kuiwakilisha serikali."

Dkt. Mwakyemba alisema Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Wakili wa Serikali, Bw. Donald Chidowu ambaye ushiriki wake katika GNT haukuwa na tija yoyote, hivyo, "Wawajibishwe na mamlaka ya juu ya nchi kwa kuchangia kuiingiza nchi katika mkataba wa aibu," alisema Dkt. Mwakyembe wakati akiwasilisha mapendekezo ya Kamati yake kwa bunge kuhusu hatua alizopaswa kuchukuliwa Mwanyika.

Baada ya Kamati hiyo kutoa mapendekezo hayo, Serikali kupitia Waziri Mkuu, Bw. Mizengo Pinda, ilitoa ufafanuzi kuhusu utekelezaji wa mapendekezo ya kamati, akisema kikatiba, Mamlaka ya Nidhamu ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

"Kwa hiyo, Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambaye alikuwa miongoni mwa watendaji wakuu watatu waliokuwa wanaishauri Serikali, suala lake la kuhusishwa kwake katika mchakato mzima wa mkataba huo linashughulikiwa na Ofisi ya Rais, IKULU," alisema Bw. Pinda.

Hata hivyo, katika Mkutano wa 16 wa Bunge uliomalizika mjini Dodoma, Serikali kupitia Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Bw. Adam Malima, ilitangaza utekelezaji wa awamu ya pili mapendekezo ya Kamati ya Dkt. Mwakyembe, ambapo alisema Bw. Mwanyika hakuwa na kosa analoonekana kutenda kutokana na wadhifa wake huo.

Bw. Malima alisema iwapo mtumishi yeyote wa umma atatajwa na watuhumiwa walioko mahakamani kuwa alihusika katika makosa ya jinai, Serikali haitasita kumfikisha mahakamani

Hata hivyo utekelezaji wa mapendekezo hayo pamoja na yaliyohusu maofisa wengine ulikataliwa na Bunge na kuiagiza Serikali kuwasilisha upya utekelezaji mwingine wa maazimio yake katika mkutano wa Bunge unaotarajiwa kuanzia Oktoba 27, mwaka huu siku tisa kabla ya Bw. Mwanyika kustaafu.

Source: Majira 06 October 2009
Mwandishi: Reuben Kagaruki


Bill
JF Senior Expert Member
Points: 195,399, Level: 100 Points: 195,399, Level: 100 Points: 195,399, Level: 100
Activity: 3% Activity: 3% Activity: 3%
Join Date: Fri Oct 2007
Posts: 623
Thanks: 32
Thanked 29 Times in 18 Posts
Views: 1686
Reply With Quote
  #11  
Old 6th October 2009, 12:47 PM
Shishye's Avatar
Shishye Shishye is offline
Shishye has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 72,974, Level: 100 Points: 72,974, Level: 100 Points: 72,974, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Thu Feb 2009
Location: On earth
Posts: 258
Thanks: 0
Thanked 42 Times in 22 Posts
Rep Power: 22
Shishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enough
Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

Quote:
View Post
Sioni ubaya wowote kustaafu. Kwanza keshatimiza miaka 60 ambao ni umri wa lazima wa mtumishi wa serikali kustaafu. Ingawa inaweza kuonekana ni kulea maovu lakini watumishi wa serikali wafanyapo makosa (ingawa makosa mengine hayatangazwi) na kuwajibika kuadhibiwa, na hasa suala la kufukuzwa kazi, mara nyingi umri wao huangaliwa kabla ya adhabu kutolewa. Hii haiko kisheria lakini ni suala la ubinadamu tu. Hata mahakamani inatokea adhabu kupunguzwa kwa sababu ya umri.
Wakati mwingine lazima Serikali ionekane imara kuwa haishurutishwi na chombo chochote. Bunge litakapokaa mwezi November itatolewa taarifa kuwa Mwanasheria Mkuu kastaafu kwa lazima. Azimio la bunge litakuwa limetekelezwa.
Wakianza kufukuzana kwa kila kosa linalotokea habaki mtu serikalini. Kastaafu mwacheni aende. Mengine baadae.
Halafu kama ni suala la kuwajibishana kuhusu Richmond wa kuondoka ni wengi.
Naaaam! Tena watanzania wanajali ubinadamu sana. Lazima unawashangaa sana watu wanojifanya kuwachungua wenzao na kuwaita mafisadi eti? Kufanya makosa kama hayo, wizi na ubadhilifu wa mali ya watanzania ni kosa la kibinadamu tu. Jamani waacheni watanue hadi umri wao wa kustaafu kwa lazima. Dah, ubinadamu!
__________________
"Chunguza Mjomba, Utabaini!"
Reply With Quote
  #12  
Old 6th October 2009, 01:13 PM
Robweme Robweme is offline
Robweme has no status.
Senior Member
Points: 61,063, Level: 100 Points: 61,063, Level: 100 Points: 61,063, Level: 100
Activity: 13% Activity: 13% Activity: 13%
 
Join Date: Wed May 2009
Posts: 179
Thanks: 0
Thanked 13 Times in 8 Posts
Rep Power: 21
Robweme will become famous soon enoughRobweme will become famous soon enoughRobweme will become famous soon enoughRobweme will become famous soon enoughRobweme will become famous soon enoughRobweme will become famous soon enoughRobweme will become famous soon enoughRobweme will become famous soon enough
Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

Quote:
View Post
Mambo haya ndio yanasababisha serikali kuonekana inalichezea Bunge. Kama amekubaliwa kustaafu, manake hajachukuliwa hatua zozote za kinidhanimu kama ilivyoshauriwa na Bunge. Kwa kweli kama Mwanyika amekubaliwa kustaafu bila ya kulazimishwa kisheria (Kuwajibishwa) basi kwa mara nyingine serikali yetu imetuthibitishia kuwa in wenyewe, na wenyewe ni wale waliomtuma Mwanyika kukubaliana na RICHMOND kama ilivyo na wao watamlinda, na kweli wamemlinda mpaka amestaafu.
Tatizo naona mkataba kati ya Mwanyika na walimtuma ni kumlinda akiwa kazini, nafikiri akitoka hapo itabidi atafute pa kujificha kwani uchaguzi unakaribia na JK anatafuta kura za imani, asije akawa mhanga wa sifa za serikali.
Nadhani tuvute subira kidogo kwani hata akisitaafu sio kwamba hawezi kuchukuliwa hatua za kisheria.
Anaweza kusitaafu na akachukuliwa hatua za kisheria vilevile.
Asante.
Reply With Quote
  #13  
Old 6th October 2009, 01:53 PM
Chakaza's Avatar
Chakaza Chakaza is online now
Chakaza mchukia mafisadi
JF Premium Member
Points: 108,191, Level: 100 Points: 108,191, Level: 100 Points: 108,191, Level: 100
Activity: 14% Activity: 14% Activity: 14%
 
Join Date: Sat Mar 2007
Posts: 889
Thanks: 47
Thanked 118 Times in 84 Posts
Rep Power: 25
Chakaza will become famous soon enoughChakaza will become famous soon enoughChakaza will become famous soon enoughChakaza will become famous soon enoughChakaza will become famous soon enoughChakaza will become famous soon enoughChakaza will become famous soon enoughChakaza will become famous soon enough
Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

Tusubiri tuone kama wabunge katika kikao chao cha Novemba kama hili watalipokeaje. Maana hapa wamepigwa changa la macho.
.
__________________
Hatutajua chochote iwapo hatutahoji na kudadisi
Reply With Quote
  #14  
Old 6th October 2009, 02:40 PM
Tumain's Avatar
Tumain Tumain is offline
Tumain has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 266,004, Level: 100 Points: 266,004, Level: 100 Points: 266,004, Level: 100
Activity: 48% Activity: 48% Activity: 48%
 
Join Date: Sun Jun 2009
Posts: 3,149
Thanks: 1,154
Thanked 1,065 Times in 683 Posts
Rep Power: 27
Tumain will become famous soon enoughTumain will become famous soon enoughTumain will become famous soon enoughTumain will become famous soon enoughTumain will become famous soon enoughTumain will become famous soon enoughTumain will become famous soon enoughTumain will become famous soon enough
Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

Nenda baba nenda iwe kwa kujiuzulu, kwa lazima au kwa umri who care! tunakusubiri mahakamani kama wenzako kina Mgonja na Yona na Mramba etc.
Reply With Quote
  #15  
Old 6th October 2009, 02:43 PM
Shishye's Avatar
Shishye Shishye is offline
Shishye has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 72,974, Level: 100 Points: 72,974, Level: 100 Points: 72,974, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Thu Feb 2009
Location: On earth
Posts: 258
Thanks: 0
Thanked 42 Times in 22 Posts
Rep Power: 22
Shishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enough
Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

Quote:
View Post
Nadhani tuvute subira kidogo kwani hata akisitaafu sio kwamba hawezi kuchukuliwa hatua za kisheria.
Anaweza kusitaafu na akachukuliwa hatua za kisheria vilevile.
Asante.
Sio Tanzania!
Sio chini ya serikali ya Kikwete!
Sio baada ya kuona kilichotokea kwa watangulizi wa hili saga!

Hakuna mwenye nia wala haja ya kuwachukulia hatua yoyote yenye tija wote wale waliohusika na njama za kuiibia nchi hii kupitia Ricmond, achilia mbali wizi mwingine wowote. Serikali iko macho "kiulinzi" bwana!
__________________
"Chunguza Mjomba, Utabaini!"
Reply With Quote
  #16  
Old 6th October 2009, 02:51 PM
Mzee Mwanakijiji's Avatar
Mzee Mwanakijiji Mzee Mwanakijiji is online now
Mzee Mwanakijiji anawashangaa wanaoitetea sheria mbovu
JF Premium Member
Points: 12,862,855, Level: 100 Points: 12,862,855, Level: 100 Points: 12,862,855, Level: 100
Activity: 100% Activity: 100% Activity: 100%
 
Join Date: Fri Mar 2006
Location: Kijijini
Posts: 18,372
Thanks: 8,186
Thanked 4,445 Times in 1,251 Posts
Rep Power: 44
Mzee Mwanakijiji is on a distinguished roadMzee Mwanakijiji is on a distinguished road
Send a message via MSN to Mzee Mwanakijiji Send a message via Skype™ to Mzee Mwanakijiji
Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

Ni upuuzi mtupu. KWA nini hawakutii maelekezo ya bunge walipotakiwa kufanya hivyo? Hivi si ndivyo walivyofanya kwa Mgonja pia?
__________________
Nchi hii imewahi kung' oa masultani wa kila aina. Tukianza kuvumilia masultani wakuchaguliwa tutapanda mbegu ya masultani wa kuzaliwa. - Nyerere katika "Uongozi wetu na Hatima ya Tanzania"
Reply With Quote
  #17  
Old 6th October 2009, 02:52 PM
Shishye's Avatar
Shishye Shishye is offline
Shishye has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 72,974, Level: 100 Points: 72,974, Level: 100 Points: 72,974, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Thu Feb 2009
Location: On earth
Posts: 258
Thanks: 0
Thanked 42 Times in 22 Posts
Rep Power: 22
Shishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enough
Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

Quote:
View Post
Nenda baba nenda iwe kwa kujiuzulu, kwa lazima au kwa umri who care! tunakusubiri mahakamani kama wenzako kina Mgonja na Yona na Mramba etc.
Angekuwa ni kweli ana kosa lolote, angeshughulikiwa akiwa bado ofisini. Huu ni uzushi tu, Mwanyika ni mtu safi. Anastaafu baada ya kuifanyia "serikali" yake kazi ya kukumbukwa na anaondoka na pensheni yake. Hata wazusshi wakijifanya kumzonga mahakamani, mambo hayatakuwa tofauti na yaliyowatokea mafisadi wa EPA. Kelele kwa sana but business as ususal!
__________________
"Chunguza Mjomba, Utabaini!"
Reply With Quote
  #18  
Old 6th October 2009, 02:57 PM
Shishye's Avatar
Shishye Shishye is offline
Shishye has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 72,974, Level: 100 Points: 72,974, Level: 100 Points: 72,974, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Thu Feb 2009
Location: On earth
Posts: 258
Thanks: 0
Thanked 42 Times in 22 Posts
Rep Power: 22
Shishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enough
Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

Quote:
View Post
Ni upuuzi mtupu. KWA nini hawakutii maelekezo ya bunge walipotakiwa kufanya hivyo? Hivi si ndivyo walivyofanya kwa Mgonja pia?
Hii inaonyeesha wazi jinsi gani Bunge letu lipo tu. Hivi kuna haja gani ya kuwa nalo?
__________________
"Chunguza Mjomba, Utabaini!"
Reply With Quote
  #19  
Old 6th October 2009, 03:03 PM
Tumain's Avatar
Tumain Tumain is offline
Tumain has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 266,004, Level: 100 Points: 266,004, Level: 100 Points: 266,004, Level: 100
Activity: 48% Activity: 48% Activity: 48%
 
Join Date: Sun Jun 2009
Posts: 3,149
Thanks: 1,154
Thanked 1,065 Times in 683 Posts
Rep Power: 27
Tumain will become famous soon enoughTumain will become famous soon enoughTumain will become famous soon enoughTumain will become famous soon enoughTumain will become famous soon enoughTumain will become famous soon enoughTumain will become famous soon enoughTumain will become famous soon enough
Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

Quote:
View Post
Angekuwa ni kweli ana kosa lolote, angeshughulikiwa akiwa bado ofisini. Huu ni uzushi tu, Mwanyika ni mtu safi. Anastaafu baada ya kuifanyia "serikali" yake kazi ya kukumbukwa na anaondoka na pensheni yake. Hata wazusshi wakijifanya kumzonga mahakamani, mambo hayatakuwa tofauti na yaliyowatokea mafisadi wa EPA. Kelele kwa sana but business as ususal!
Mahakama ndio ita-detrmine ana makosa au hana makosa kama mahakama itamkuta ni mtu safi then --- wananchi kama mimi nasema "ishi salama na watoto wako"
Hivyo hivyo kwa wazee wa EPA kina Mramba, Yona na Mgonja mahakama ikisema ni watu safi too me is a fair play wakaishi salama na watoto wao! maana ulitaka serikali ifanyeje? justice as per our system iko mahakamani kama wewe una-alternative tuambie! tujue!
Reply With Quote
  #20  
Old 6th October 2009, 03:20 PM
Shishye's Avatar
Shishye Shishye is offline
Shishye has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 72,974, Level: 100 Points: 72,974, Level: 100 Points: 72,974, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Thu Feb 2009
Location: On earth
Posts: 258
Thanks: 0
Thanked 42 Times in 22 Posts
Rep Power: 22
Shishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enoughShishye will become famous soon enough
Default Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka

Quote:
View Post
Mahakama ndio ita-detrmine ana makosa au hana makosa kama mahakama itamkuta ni mtu safi then --- wananchi kama mimi nasema "ishi salama na watoto wako"
Hivyo hivyo kwa wazee wa EPA kina Mramba, Yona na Mgonja mahakama ikisema ni watu safi too me is a fair play wakaishi salama na watoto wao! maana ulitaka serikali ifanyeje? justice as per our system iko mahakamani kama wewe una-alternative tuambie! tujue!
Sikuelewi! Mimi nimesema Mwanyika ni mtu safi maana hajashtakiwa wala hatashtakiwa mpaka aachie ofisi. Nimesema angekuwa na kosa lolote angeshtakiwa kabla hata ya kustaafu. Alternative gani nyingine unataka usikie toka kwangu?
__________________
"Chunguza Mjomba, Utabaini!"
Reply With Quote
Reply

Bookmarks

Tags
amkubalia, kikwete, kungoka, mwanyika


Currently Active Users Viewing This Thread: 1 (0 members and 1 guests)
 
Thread Tools
Display Modes Rate This Thread
Rate This Thread:

Posting Rules
You may not post new threads
You may not post replies
You may not post attachments
You may not edit your posts

BB code is On
Smilies are On
[IMG] code is On
HTML code is Off
Trackbacks are Off
Pingbacks are Off
Refbacks are On


Similar Threads
Thread Thread Starter Forum Replies Last Post
Nidhamu ya Chama: Kiini cha Kudorora Viongozi wa CCM! Mzee Mwanakijiji Jukwaa la Siasa 94 13th May 2009 01:45 AM
Urithi wa Kikwete na haiba iso sababu Pundit Jukwaa la Siasa 25 27th December 2008 07:42 AM
Miaka miwili Kikwete Ikulu, tumaini lililopotea Bubu Ataka Kusema Jukwaa la Siasa 2 16th December 2007 10:40 PM
Kikwete Relieved As Mkapa Opts Out Nyamgluu Habari na Hoja mchanganyiko 0 14th July 2006 06:43 AM

Tuma Ukurasa huu kwa rafiki yako!


All times are GMT +3. The time now is 02:56 PM.

Powered by JamiiForums.com
Copyrights reserved to JamiiForums.com