Hotuba ya Waziri wa Fedha Bungeni (iko kwenye tovuti ya taifa yaani http://www.tanzania.go.tz) inaonyesha kwamba serikali imetenga shilingi trilioni 1.0861 kwa ajili ya sekta ya Elimu, kwa kipindi cha 2007/08.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Ufundi inaonekana kwenye hiyo sehemu ya tovuti ya taifa vile vile, na inaonyesha kwamba kwa mwaka 2007/08, fedha zilizotengwa kwa ajili ya wizara hiyo ni
sh. 265,679,865,700 (shilingi bilioni 265.68).
Hotuba ya Wizara ya Sayansi na Elimu ya Juu haionekani kwenye hiyo tovuti ya taifa. Hata hivyo, ukiondoa fedha zilizotengewa Wizara ya Mama Sitta kweny hizo 1.0861 tr/- za Elimu, utakuta zinabaki
sh. 820,320,134,300 (shilingi bilioni 820.32). Kwa vile ziko Wizara mbili tu za Elimu, ina maanisha Wizara ya Waziri Msola imetengewa 820.32 bn/- ? Hizi ni 308.76% zaidi ya fedha zilizotengwa kwa ajili ya Wizara ya Mama Sitta! Naamnini kuna udanganyifu hapa.
Ifahamike vile vile kwamba ukilinganisha Bajeti ya Mama Sitta ya mwaka jana na hii ya sasa, utaona fedha zilizotengwa kwa ajili ya matumizi ya kawaida zimeongezeka kwa 16% (toka 133,964,077,900/- hadi 155,447,119,000) wakati fedha za matumizi ya maendeleo zimeongezeka kwa 4% tu (toka 105,686,632,100/- hadi 110,232,746,700/-).
Serikali ambayo kila siku inasema inakazania Elimu itaongezaje fedha za matumizi ya maendeleo za Wizara ya Elimu na Ufundi kwa asilimia 4 tu? Tunajidanganya wenyewe. Tunaficha ugonjwa tulionao wa kuinyima Elimu fedha, lakini tukumbuke Waswahili husema "Anayeficha ugonjwa, kifo kitamsema".
Augustine Moshi

Reply With Quote

Follow Us Here