Hello JFers
Below is an extract from the speech of minister for infrastructure development specifically on issues related to ICT... the whole budget speech is found at ministry website... http://www.infrastructure.go.tz/HOTU...6_07_Final.pdf
thanks that the website is now looks at least good.
Things to note, there is enough emphasize on IXPs, hope that this time it will happen!!! However I have one concern... especially....
I quoteaccording to my knowledge the last service provider to join TIX was TTCL and it was June 22, 2005, that means it is about TWO (2) years now since the last peer joined TIX ..."....Watoa huduma za takwimu na tovuti waliendelea kujiunga kwenye mitambo ya mawasiliano ya Kitaifa (Internet Exchange Point) iliyopo Dar es Salaam. Faida ya kutumia kituo hiki ni kupunguza gharama kwani watumiaji hawatumii njia ya masafa ya kimataifa wakati wa kufanya mawasiliano hayo ndani ya nchi. Kufanya hivyo kunapunguza uwezekano wa kuvuja kwa siri za kibiashara na kiutawala."-
source http://www.tix.or.tz/peers.html ..
list of prospective TIX peers could have been all of these organizations listed here if after all regulation are in place and they are enforced
http://www.tcra.go.tz/licensing/CLFlicensed_operators.php#AS
I need to be educated on "watoa huduma wanaoendelea kujiunga na IXP" ??? how many since June 2005 and what are those organizations?
The speech.....
---------------------------------START----------------------------------
Huduma za Mawasiliano
12. Mheshimiwa Spika, kuhusu utekelezaji wa Sera ya Mawasiliano, mkakati uliowekwa ni ule wa kuhakikisha kwamba huduma za mawasiliano zinafika vijijini hasa kwenye maeneo yasiyokuwa na mvuto wa kibiashara. Mkakati huo unahusisha kuanzishwa kwa Mfuko wa Mawasiliano (Universal Communications Services Access Fund-UCSAF). Lengo la mfuko huu ni kuhakikisha kuwa huduma za mawasiliano zinafika katika maeneo ambayo hayana maslahi mazuri kibishara (hasa vijijini). Aidha, hivi sasa Serikali iko kwenye mchakato wa kutafuta fedha kwa ajili ya Ujenzi wa Mkonga wa Mawasiliano wa Kitaifa (National Communications Infrastructure Backbone) utakaokidhi matumizi ya teknolojia ya kisasa. Mkonga huo utakuwa na urefu wa km 6,000 na utaunganisha Makao Makuu ya Wilaya zote nchini kwa kuanzia.
13. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2006/07 mawasiliano kupitia njia ya tovuti yaliendelea kuimarika ambapo kampuni za watoa huduma (Internet Service Providers) 30 zilitoa huduma hii na watoa huduma za tovuti waliosajiliwa walifikia 400. Hata hivyo, gharama za mawasiliano ya tovuti ziliendelea kuwa juu kutokana na
kukosekana kwa miundombinu na huduma nyingine zinazohitajika katika kuwezesha utoaji wa huduma za mawasiliano. Watoa huduma za takwimu na tovuti waliendelea kujiunga kwenye mitambo ya mawasiliano ya Kitaifa (Internet Exchange Point) iliyopo Dar es Salaam.
Faida ya kutumia kituo hiki ni kupunguza gharama kwani watumiaji hawatumii njia ya masafa ya kimataifa wakati wa kufanya mawasiliano hayo ndani ya nchi. Kufanya hivyo kunapunguza uwezekano wa kuvuja kwa siri za kibiashara na kiutawala.
Ili kueneza mitambo ya tovuti nchini, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) inaendelea na ujenzi wa mtambo wa kupitisha taarifa za tovuti (Internet Exchange Point - IXPs) jijini Arusha ambao unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa Julai 2007. Mtambo huo utakapokamilika utakabidhiwa kwa Chama cha Watoa Huduma za Tovuti ili wauendeshe na kuunganishwa na mtambo uliopo Dar es Salaam.
14. Mheshimiwa Spika, TCRA imeendelea kusimamia na kudhibiti shughuli za Mawasiliano, Teknolojia ya Mawasiliano na Habari na Utangazaji. Katika kipindi cha mwaka 2006/2007, Mamlaka ilianzisha taasisi iitwayo Tanzania National Information Center (tzNIC) ambayo jukumu lake kubwa ni kugawa na kusajili anuani pepe (e - mail) kwa watumiaji wa huduma za tovuti nchini na majina ya mitandao (domain names registration) kwa watoa huduma za tovuti. Lengo ni kurahisisha utambuzi wa chanzo cha habari inayotumwa kutoka kwa mtumiaji mmoja wa mtandao kwenda kwa mtumiaji mwingine na kupunguza gharama za ada zinazolipwa na watoa huduma kwa
wasajili wa majina ya mitandao nje ya nchi.
15. Mheshimiwa Spika, mfumo mpya wa leseni za mawasiliano (converged licensing framework) uliendelea kutekelezwa kwa kutoa leseni mpya kwa watoa huduma na kusimamia utekelezaji wa viwango vya huduma. Mfumo huu unazingatia umuhimu wa kuharakisha usambazaji wa huduma za mawasiliano nchini. Mfumo huu ulianzisha leseni ya mawasiliano na utangazaji katika ngazi ya kijamii (community) ili kufikisha huduma hizo vijijini. Hatua hii itawawezesha wananchi walio wengi kupata huduma za mawasiliano na taarifa mbalimbali kutoka katika vituo 47 vya redio na vituo 29 vya televisheni vilivyopo nchini. Aidha, Mamlaka imeandaa mpango utakaowezesha kuondoa tatizo la masafa katika miji ya Dar es Salaam, Mwanza na Arusha inayotokana na kuanzishwa kwa vituo vingi vya utangazaji. Mpango huo unazingatia sera iliyowekwa kimataifa ya kubadili teknolojia ya utangazaji kutoka analogue
kwenda digital.
16. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2007/08, Wizara kwa kupitia TCRA itaendelea kusimamia, kudhibiti, kutoa elimu, kuhamasisha na kusaidia utoaji wa huduma bora za mawasiliano nchini ikiwa ni pamoja na kusaidia ujenzi wa mitambo ya tovuti katika Manispaa za Dodoma, Mbeya na Mwanza. Aidha, mradi wa kuunganisha mitambo ya IXPs ya nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki umekwishaanza ambapo mkandarasi ameshateuliwa kutekeleza mradi huo. Mitambo hiyo itarahisisha mawasiliano katika nchi wanachama wa Afrika Mashariki Ili kudhibiti wizi wa simu za mikononi, TCRA itaendelea kushirikiana na watoa huduma za mawasiliano ya simu kuandaa utaratibu utakaohakikisha kuwa watoa huduma wote wanashirikiana kujenga mtambo wa kudhibiti simu za mkononi zilizoibiwa kwa kuzifunga zisitumike kwenye mtandao wowote katika Afrika Mashariki. Vile vile kwa kushirikiana na Tume ya Taifa ya Nguvu za Atomu (Tanzania Atomic Energy Commission), TCRA itapima viwango vya mionzi inayozalishwa na miundombinu ya mawasiliano ili kuhakikisha kuwa haizidi viwango vinavyotolewa na Tume ya
Kudhibiti Mionzi Ulimwenguni.
17. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2006/07, Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) imekamilisha Mradi wa uboreshaji wa huduma ya takwimu na Intaneti kwa wateja kwa kutumia teknolojia ya Asymetric Digital Subscriber Lines (ADSL) katika Makao Makuu ya Mikoa yote Tanzania. Kazi nyingine iliyokamilika ni ya kuweka mitambo mipya ya Digital Microwave Radio katika njia kuu ya Dodoma hadi Mbeya kupitia Iringa na Nyororo, Mwanza - Bukoba –
Kigoma na Mwanza – Musoma. Aidha, mitambo kama hiyo (Digital Microwave Radio) inawekwa kati ya Dar es salaam - Morogoro – Dodoma, Dar es salaam – Tanga – Arusha, Dodoma – Arusha kupitia Kondoa, Mbeya – Sumbawanga na Mtwara – Newala – Masasi – Nachingwea. Kazi hii ipo katika hatua za mwisho na itakamilika
rasmi ifikapo mwishoni mwa Julai, 2007. Aidha, TTCL ipo katika hatua za kubadilisha njia kuu za mawasiliano kati ya Dar es salaam – Zanzibar – Pemba – Tanga itakayohusisha pia njia za kwenda Makunduchi, Bububu, Chake Chake, Mkoani na Wete. Miradi hii inategemewa kukamilika ifikapo mwishoni mwa mwaka huu wa 2007.
Kazi inayoendelea hivi sasa ni kuondoa mitambo ya simu za kukoroga (Magneto) kwa kutumia huduma ya simu za mikononi zinazotumia teknolojia ya ‘Code Division Multiple Access -(CDMA)’ katika maeneo ya Mwakaleli, Lwanga, Itigi, Misungwi, Ngudu, Malya, Urambo, Sikonge, Mtera, Mvumi, Ruangwa, Nachingwea, Ndanda, Liwale na
Kaliua. Kazi hii inategemewa kukamilika mwishoni mwa Julai, 2007.
18. Mheshimiwa Spika, TTCL imeendelea na kazi ya kubadilisha mitambo ya zamani na kuweka mipya katika miji ya Arusha, Mkoani (Pemba), Moshi, Tanga, Singida, Bukoba na Kigoma. Mitambo ya simu za kukoroga imeondolewa na kufungwa ya kisasa katika maeneo ya Utete, Kibiti, Ikwiriri, Mafia na Kilwa Masoko. Aidha, Kampuni inaendelea na ujenzi wa njia kuu za mawasiliano kwa kutumia mkonga wa kigae (Optical fibre cable) ili kuimarisha njia za mawasiliano na kutekeleza azma ya Serikali kuwa na mawasiliano bora, imara na ya kisasa kwa nia ya kuunganisha nchi za Afrika Mashariki. Kampuni imeendelea na hatua ya awali ya ujenzi wa mkonga wa kigae kati ya Arusha – Musoma – Mwanza kupitia mbuga za wanyama za Ngorongoro na Serengeti, Mwanza – Shinyanga –Isaka – Rusumo (Rwanda) – Kabanga (Burundi) na Nyakanazi – Bukoba. Wakandarasi wa kazi hiyo wameshapatikana na inategemewa kukamilika ifikapo mwishoni mwa 2007. Aidha, mkonga wa kigae utajengwa kati ya Morogoro – Iringa – Mbeya na Somanga – Lindi – Mtwara. Ujenzi wa njia kuu kati ya Mbeya – Kasumulo Songwe Malawi utakaounganisha mawasiliano kwenda hadi umekamilika.
19. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2007/08, TTCL imepanga kutekeleza mipango ya kuboresha na kupanua njia kuu za mawasiliano (Digital Microwave Backbone) katika njia za Morogoro – Ifakara – Mahenge, Songea – Tunduru – Masasi – Mtwara, Njombe – Makete – Ludewa na Moshi – Marangu – Rombo Mkuu. Aidha, kampuni itaanza kutoa huduma za simu za mikononi katika Wilaya zote nchini na kupeleka mkonga wa kigae kwa wateja wakubwa ili kuboresha huduma za simu. Kwa kuanzia kampuni imetoa zabuni ya kuweka mtandao unaotumia teknolojia ya Optic Fibre kwenda Ikulu ya Zanzibar na hoteli zote za kitalii zilizoko maeneo ya Kiwengwa, Zanzibar. Pia mitambo tisa ya kuunganisha simu kwenda katika maeneo ya Mtwara – Tandahimba – Newala – Masasi, Dodoma – Kondoa na Sumbawanga – Namanyere – Mpanda itabadilishwa ifikapo mwishoni mwa mwaka 2007
20. Mheshimiwa Spika, Kampuni ya Simu 2000 Limited katika mwaka 2006/07, iliendelea na majukumu yake ikiwa ni pamoja na kusimamia na kuuza mali ilizokabidhiwa na kufuatilia malipo ya pensheni za waliokuwa wafanyakazi wa Shirika la Posta na Simu la Afrika Mashariki. Majukumu mengine ni kufuatilia kesi zilizorithiwa na zinazojitokeza katika uendeshaji wa Kampuni. Aidha, Kampuni iliweza kuuza nyumba tatu na viwanja viwili. Kampuni inaendelea na kazi zake hadi hapo itakapokoma na kukabidhi majukumu yake kwa Consolidated Holding Corporation (CHC) Desemba, 2007.
Huduma ya Simu za Mkononi
21. Mheshimiwa Spika, huduma za simu za mkononi zimeendelea kupanuka katika mikoa yote Tanzania Bara na Tanzania Zanzíbar. Huduma hizi zinatolewa na Kampuni za TTCL, Vodacom, Celtel, Tigo na Zantel. Mwaka 2006 Kampuni hizi zilikuwa na wateja 6,557,970 waliounganishwa kwenye huduma ya simu za mkononi ikilinganishwa
na wateja 3,118,157 kwa mwaka 2005. Ongezeko hili la asilimia 100 kwa mwaka linaonyesha kuwa huduma ya simu za mkononi imekuwa sehemu ya mahitaji muhimu ya kila siku kwa wananchi katika shughuli zao.
Jamii Habari
22. Mheshimiwa Spika, mchakato wa ujenzi na uimarishaji wa Jamii Habari ni zoezi la kudumu na endelevu. Jamii Habari ni nyenzo muhimu katika kuwawezesha wananchi kuwasiliana, kujifunza na kupashana habari. Katika kipindi cha 2006/07, Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, imetekeleza uanzishaji wa somo la teknolojia ya habari na mawasiliano mashuleni. Aidha, Umoja wa Afrika (AU) kwa niaba ya nchi wanachama, Tanzania ikiwa mojawapo, imeingia makubaliano ya awali na Serikali ya India. Makubaliano hayo yanahusu uanzishwaji wa mradi wa ujenzi wa mtandao wa Mawasiliano ya wakuu wa Nchi za Afrika, vyuo vya elimu ya juu, vyuo vya ualimu na hospitali za rufaa nchini (e-government, e-education na e-health). Lengo la mradi huu ni kuboresha utoaji wa elimu huria na huduma za afya (tele-education and tele-medicine services) ili kupunguza gharama za elimu na matibabu. Mradi huu utagharamiwa na Serikali ya India kwa muda wa miaka mitano.
23. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2006/07, Serikali imeendelea kuimarisha vituo vya mawasiliano nchini. Vituo hivyo ni pamoja na Tanzania Global Distance Learning Centre (TGDLC) kilichopo Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) mkoani Dar es Salaam. Kituo hiki kimeendelea kutoa mafunzo kwa viongozi na wataalamu kwa kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEKNOHAMA). Tunategemea kutumia uzoefu huo kupeleka mafunzo hayo katika mikoa na Wilaya zote nchini. Kwa kuanzia Wizara itapeleka mafunzo hayo katika vituo ambavyo vimeshaanzishwa ikiwa ni pamoja na Sengerema Tele Centres kilichopo mkoani Mwanza, Chuo cha Ualimu
Kasulu kinachotumia nishati ya kinyesi cha ng’ombe na Ngara UNHCR Tele Centre kilichoko mkoani Kagera. Vituo vingine ni Wino Tele Centre cha mkoani Ruvuma na Multipurpose Tele Centres zilizoko Kinampanda mkoani Singida, Mpwapwa mkoani Dodoma na kituo cha Mtuwetu kilichopo mkoani Mtwara. Vituo hivyo vimeendelea
kutumiwa na jamii katika kukuza matumizi ya teknolojia ya habari na mawasiliano. Wananchi wameendelea kufaidika katika maeneo ya bishara, elimu, afya, utawala na uendeshaji wa shughuli za kiuchumi na kijamii. Katika mwaka 2006/07 wataalamu wa Wizara walivitembelea vituo vilivyopo katika mikoa ya Singida, Mtwara, Kilimanjaro na Shinyanga kwa lengo la kupata taarifa na kufanya tathmini ya utendaji ya vituo hivyo na kuendelea kushauri na
kuviimarisha. Katika mwaka 2007/08, Wizara ina mpango wa kuanzisha vituo vipya vya Tele Centre na kuhamasisha matumizi ya tekinolojia ya Habari katika sehemu za Ukerewe, Tabora, Same, Hai, Sumbawanga na
Lindi. Aidha, Wizara itaendelea kuviboresha vituo vilivyopo na kuviongezea uwezo.


Reply With Quote


Follow Us Here