Ujumbe Wa Maalim Seif Shariff Hamad Kwa Wazanzibar - JamiiForums |The Home of Great Thinkers

Go Back   JamiiForums |The Home of Great Thinkers > Public Forums > Jukwaa la Siasa


Jukwaa la Siasa Tanzania & World Politics General Discussion Forum. You need to be registered in order to post your comment(s)


Reply
 
LinkBack Thread Tools Rate Thread Display Modes
Old 3rd July 2009, 04:13 PM   #1
Ujumbe Wa Maalim Seif Shariff Hamad Kwa Wazanzibar
Junius Junius is online now 3rd July 2009, 04:13 PM

”Kila Mzanzibari mwenye haki, ahakikishe anajiandikisha kwenye Daftari!”

• Akagua shughuli za Chama, kuhamasisha Daftari
• Aonya rafu za CCM, ZEC na Afisi ya Vitambulisho
• Amwambia Kikwete hatapata kumweka kibaraka wake kuchimba mafuta ya Wazanzibari
• Afanya mikutano mitano ya hadhara
• Jumapili aunguruma Gombani


Katibu Mkuu wa The Civic United Front (CUF – Chama cha Wananchi), Maalim Seif Sharif Hamad, yuko kisiwani Pemba katika ziara ya wiki moja.

Ziara hiyo ilianza tarehe 31 Juni na itamalizika tarehe 4 Julai kwa mkutano mkubwa wa hadhara kwenye viwanja vya Gombani, Chake Chake.

Hadi sasa, Maalim Seif ameshatembelea na kufanya mikutano ya hadhara katika majimbo ya Micheweni, Tumbe na tarehe 3 Julai atakuwapo kwenye jimbo la Mgogoni.

Mbali na kukagua uhai wa Chama na kuonana na wananchi, Maalim Seif anatumia fursa ya ziara hizi kupeleka ujumbe maalum kwa wakaazi wa Pemba, ambao ni kuwataka wajitokeze kwa wingi kwenye zoezi la kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura linalotarajiwa kuanza katika wilaya ya Micheweni, mkoa wa Kaskazini, Pemba, kuanzia tarehe 6 Julai mwaka huu. Kwamba kila mmoja ahakikishe kuwa anaandikishwa kuwa mpiga kura. Ujumbe huu unakwenda sambamba na azma ya CUF kuhakikisha kuwa Pemba inabakia kuwa ngome yake isiyopenyeka wala kutetereka.

Ujumbe huu wa Maalim Seif unakuja katika wakati ambapo tayari CUF imekusanya ushahidi wa kutosha unaothibitisha kuwa kuna ‘utatu’ usio mtakatifu (trinity of the demons) baina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) na Idara ya Vitambulisho Zanzibar, unaopanga njama za kuhakikisha kuwa wakaazi wengi wa Pemba hawaandikishwi kuwa wapiga kura. Katika mtandao huu, njama iliyopangwa ni hii: SMZ iwatumie masheha wake kuhakikisha kuwa hawatoi barua za uthitisho kuwapa watu wanaodai vitambulisho vya Uzanzibari, Idara ya Vitambulisho isimpe kitambulisho hicho mtu ambaye hana barua ya sheha na ZEC isimuandikishe kuwa mpiga kura mtu ambaye hana kitambulisho. Hadi sasa watu 18,000 kisiwani Pemba pekee wamesharipoti kunyimwa vitambulisho hivyo vya ukaazi huku hata zoezi la uandikishaji wapiga kura likiwa halijaanza. Lakini, licha ya kuwepo kwa taarifa hizo, ujumbe wa Maalim Seif kwa wananchi wa Pemba unabakia kuwa ule ule: lazima wahakikishe kuwa kila mwenye haki ya kuwa mpiga kura anaingia kwenye Daftari hilo.

Kwa ZEC, SMZ na Idara ya Vitambulisho, ujumbe wa Maalim Seif ni kwamba kinachofanywa na taasisi hizo kinaipeleka nchi katika machafuko na matatizo makubwa, ambayo ni wao ndio watakaobeba lawama kwa matokeo yoyote yatakayotokea. CUF kila siku itasimama upande wa haki na sio tu kuhakikisha kuwa haki hiyo ipo, lakini kuona kuwa haki hiyo inatendeka.

Kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Kikwete, ujumbe wa Maalim Seif uko wazi. Kwamba Rais Kikwete ndiye Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama na kwamba yeye ndiye mwenye dhamana ya usalama wa raia na mali zao. Kwa hivyo, asijiwache kuchukuliwa na andasa za kihafidhina zilizopo Zanzibar na kuja kusababisha kuvunjiwa heshima yake. Atumie nafasi zake alizonazo kuhakikisha haki inatendeka Zanzibar na sio kutumia nafasi hizo kutafuta wakala wa kumuweka madarakani kwa lengo la kupata wepesi wa kuyachimba mafuta ya Wazanzibari. Hilo halitavumiliwa hata kidogo na Wazanzibari na halitakuwa na manufaa kwake binafsi na kwa nchi nzima kwa jumla. Maalim Seif anamtaka Rais Kikwete asifuate nyayo za mtangulizi wake, Benjamin Mkapa, ambaye anajuilikana kwenye kama kiongozi aliyesimamia mauaji ya Januari 2001 na kuzalisha wakimbizi kwa mara ya mwanzo katika historia ya Tanzania huru.

Kwa jumuiya za kimataifa, hasa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), ambalo linafadhili zoezi hilo la kuandikisha wapiga kura kwenye Daftari la Kudumu, ujumbe wa Maalim Seif ni kwamba taasisi hiyo ya kimataifa ijitoe mara moja katika ufadhili huo hadi hapo itakapohakikishiwa kwa vitendo kwamba SMZ na ZEC hazitumii nafasi zao kuwanyima haki zao Wazanzibari. Kuendelea kufadhili zoezi hili, anasema Maalim Seif, ni sawa na taasisi hiyo ya kimataifa kushiriki katika mpango wa kuiviza demokrasia Zanzibar, ilhali ilivyotakiwa ni kwamba UNDP isaidie kuimarisha demokrasia na haki za binaadamu.


SOURCE: KURUGENZI YA UENEZI NA MAHUSIANO YA UMMA,
THE CIVIC UNITED FRONT,S.L.P 3537,SIMU 0777 414112

 
Junius's Avatar
Junius
JF Senior Expert Member
Points: 445,522, Level: 100 Points: 445,522, Level: 100 Points: 445,522, Level: 100
Activity: 7% Activity: 7% Activity: 7%
Join Date: Wed Mar 2009
Posts: 2,082
Thanks: 142
Thanked 184 Times in 130 Posts
Views: 860
Reply With Quote
  #2  
Old 3rd July 2009, 04:16 PM
Junius's Avatar
Junius Junius is online now
Junius Sir Phillip Francis
JF Senior Expert Member
Points: 445,522, Level: 100 Points: 445,522, Level: 100 Points: 445,522, Level: 100
Activity: 7% Activity: 7% Activity: 7%
 
Join Date: Wed Mar 2009
Posts: 2,082
Thanks: 142
Thanked 184 Times in 130 Posts
Rep Power: 26
Junius will become famous soon enoughJunius will become famous soon enoughJunius will become famous soon enoughJunius will become famous soon enoughJunius will become famous soon enoughJunius will become famous soon enoughJunius will become famous soon enoughJunius will become famous soon enough
Default Re: Ujumbe Wa Maalim Seif Shariff Hamad Kwa Wazanzibar.

Jamani mjumbe hauwawi ehh
Reply With Quote
  #3  
Old 3rd July 2009, 04:21 PM
Masatu Masatu is offline
Masatu Is Magumashi
JF Senior Expert Member
Points: 733,039, Level: 100 Points: 733,039, Level: 100 Points: 733,039, Level: 100
Activity: 4% Activity: 4% Activity: 4%
 
Join Date: Mon Jan 2007
Location: Mbagala, Jeshini
Posts: 3,741
Thanks: 0
Thanked 88 Times in 66 Posts
Rep Power: 0
Masatu is infamous around these parts
Default Re: Ujumbe Wa Maalim Seif Shariff Hamad Kwa Wazanzibar.

Tatizo sio kujiandikisha wala kupiga kura, wenyewe wanasema ile nchi ya mapinduzi haitolewi kwa kipande cha karatasi!
__________________
Mkulima kala Mbegu......
Reply With Quote
  #4  
Old 3rd July 2009, 04:26 PM
Josh Michael's Avatar
Josh Michael Josh Michael is offline
Josh Michael has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 530,781, Level: 100 Points: 530,781, Level: 100 Points: 530,781, Level: 100
Activity: 27% Activity: 27% Activity: 27%
 
Join Date: Fri Jun 2009
Location: Kibandani
Posts: 2,010
Thanks: 1,193
Thanked 197 Times in 152 Posts
Rep Power: 25
Josh Michael will become famous soon enoughJosh Michael will become famous soon enoughJosh Michael will become famous soon enoughJosh Michael will become famous soon enoughJosh Michael will become famous soon enoughJosh Michael will become famous soon enoughJosh Michael will become famous soon enoughJosh Michael will become famous soon enough
Default Re: Ujumbe Wa Maalim Seif Shariff Hamad Kwa Wazanzibar.

Sisi yetu macho lakini sijaona tofauti kati ya Jk na Mkapa na hii itadhibitisha mwakani wakati wa uchaguzi maana wakati ule Mkapa nguvu za CUF zilimshindwa ndio maana akamua kutumia Nguvu Kubwa sana
Reply With Quote
  #5  
Old 3rd July 2009, 05:44 PM
Ngongo Ngongo is offline
Ngongo has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 468,374, Level: 100 Points: 468,374, Level: 100 Points: 468,374, Level: 100
Activity: 3% Activity: 3% Activity: 3%
 
Join Date: Sat Sep 2008
Posts: 722
Thanks: 157
Thanked 317 Times in 135 Posts
Rep Power: 23
Ngongo will become famous soon enoughNgongo will become famous soon enoughNgongo will become famous soon enoughNgongo will become famous soon enoughNgongo will become famous soon enoughNgongo will become famous soon enoughNgongo will become famous soon enoughNgongo will become famous soon enough
Default Re: Ujumbe Wa Maalim Seif Shariff Hamad Kwa Wazanzibar.

Maalim Seif Shariff Hamad awaachie wengine kila uchaguzi ni yeye tu haoni wenza Mbowe,Cheyo na Mzee wa Kiraracha wamekimbilia kwenye majimbo yao uchaguzi.Maalimu Seif badala ya kuimarisha CUF bara kaamua kubaki na Pemba yake !!!.Ndiyo maana Lwakatare kawakimbia baada ya kubaini hyiki chama macho na masikio yako Zanzibar tu.


Maalim Seif Shariff Hamad hajui mafuta ni mambo ya muungano na yataendelea kuwa ya muungano atake asitake.Lau kama anataka kubadili katiba sharti hoja ilepelekwe bungeni si Gombani au Chake chake.
Reply With Quote
  #6  
Old 3rd July 2009, 05:59 PM
Pakacha Pakacha is offline
Pakacha has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 87,041, Level: 100 Points: 87,041, Level: 100 Points: 87,041, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Tue Apr 2008
Posts: 638
Thanks: 23
Thanked 27 Times in 24 Posts
Rep Power: 23
Pakacha will become famous soon enoughPakacha will become famous soon enoughPakacha will become famous soon enoughPakacha will become famous soon enoughPakacha will become famous soon enoughPakacha will become famous soon enoughPakacha will become famous soon enoughPakacha will become famous soon enough
Default Re: Ujumbe Wa Maalim Seif Shariff Hamad Kwa Wazanzibar.

Quote:
View Post
Jamani mjumbe hauwawi ehh
Tabaan. Hauwawi !!!Junius. Tunashukuru kwa hayo uliyotuwekea jamvini. Mimi nikichangia mada nasema kwa maoni yangu. Seif Muflis- hana mpya. Nielewe Junius siikandii CUF hata siku moja. Nina imani kamili na CUF.
Reply With Quote
  #7  
Old 3rd July 2009, 06:09 PM
Junius's Avatar
Junius Junius is online now
Junius Sir Phillip Francis
JF Senior Expert Member
Points: 445,522, Level: 100 Points: 445,522, Level: 100 Points: 445,522, Level: 100
Activity: 7% Activity: 7% Activity: 7%
 
Join Date: Wed Mar 2009
Posts: 2,082
Thanks: 142
Thanked 184 Times in 130 Posts
Rep Power: 26
Junius will become famous soon enoughJunius will become famous soon enoughJunius will become famous soon enoughJunius will become famous soon enoughJunius will become famous soon enoughJunius will become famous soon enoughJunius will become famous soon enoughJunius will become famous soon enough
Default Re: Ujumbe Wa Maalim Seif Shariff Hamad Kwa Wazanzibar.

Quote:
View Post
Tabaan. Hauwawi !!!Junius. Tunashukuru kwa hayo uliyotuwekea jamvini. Mimi nikichangia mada nasema kwa maoni yangu. Seif Muflis- hana mpya. Nielewe Junius siikandii CUF hata siku moja. Nina imani kamili na CUF.
Haya mwanakwetu nitafune huku unanipuliza.
Lakini Pakacha,nkukumbushe kitu, namkumbuka Marehemu Prof. Haroub Othman(Mw'mungu amrehemu) wakati fulani akisema katika mambo aliyokuwa hakubaliani nayo na yakimchukiza (akitaka kutoka machozi akisema hivi) ni mbinu na hila za makusudi zinazofanywa na wakubwa za kuwazuilia watu wenye haki,haki zao za msingi kama kujiandikisha na kupiga kura n.k
Kwani kuna tatizo gani ikawa kila mwenye haki ya kuandikishwa akapata haki yake akapiga kura kwa amani na utulivu, ikawa uchaguzi wa kura moja mtu mmoja, halafu chama chochote kikashinda na walishindwa wakaheshimu matokeo?
Reply With Quote
  #8  
Old 3rd July 2009, 06:21 PM
IronBroom's Avatar
IronBroom IronBroom is offline
IronBroom is just that
JF Senior Expert Member
Points: 100,684, Level: 100 Points: 100,684, Level: 100 Points: 100,684, Level: 100
Activity: 3% Activity: 3% Activity: 3%
 
Join Date: Thu Jun 2008
Location: Nyumbani
Posts: 353
Thanks: 65
Thanked 52 Times in 36 Posts
Rep Power: 22
IronBroom will become famous soon enoughIronBroom will become famous soon enoughIronBroom will become famous soon enoughIronBroom will become famous soon enoughIronBroom will become famous soon enoughIronBroom will become famous soon enoughIronBroom will become famous soon enoughIronBroom will become famous soon enough
Default Re: Ujumbe Wa Maalim Seif Shariff Hamad Kwa Wazanzibar.

Quote:
View Post
Tatizo sio kujiandikisha wala kupiga kura, wenyewe wanasema ile nchi ya mapinduzi haitolewi kwa kipande cha karatasi!
Bali?
Reply With Quote
  #9  
Old 3rd July 2009, 06:33 PM
Pakacha Pakacha is offline
Pakacha has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 87,041, Level: 100 Points: 87,041, Level: 100 Points: 87,041, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Tue Apr 2008
Posts: 638
Thanks: 23
Thanked 27 Times in 24 Posts
Rep Power: 23
Pakacha will become famous soon enoughPakacha will become famous soon enoughPakacha will become famous soon enoughPakacha will become famous soon enoughPakacha will become famous soon enoughPakacha will become famous soon enoughPakacha will become famous soon enoughPakacha will become famous soon enough
Default Re: Ujumbe Wa Maalim Seif Shariff Hamad Kwa Wazanzibar.

Quote:
View Post
Tatizo sio kujiandikisha wala kupiga kura, wenyewe wanasema ile nchi ya mapinduzi haitolewi kwa kipande cha karatasi!
Khee!! imekuwa nongwa!!! Waliosema hayo wako wapi? Njooni katika kisanduku cha kura mkishindwa -basi mkae chonjo- Hiyo ndo Demokrasia. Huo ndio ustaarabu.
Reply With Quote
  #10  
Old 3rd July 2009, 06:45 PM
Lamba's Avatar
Lamba Lamba is offline
Lamba has no status.
Senior Member
Points: 108,430, Level: 100 Points: 108,430, Level: 100 Points: 108,430, Level: 100
Activity: 3% Activity: 3% Activity: 3%
 
Join Date: Sun Jan 2007
Posts: 218
Thanks: 7
Thanked 19 Times in 14 Posts
Rep Power: 24
Lamba will become famous soon enoughLamba will become famous soon enoughLamba will become famous soon enoughLamba will become famous soon enoughLamba will become famous soon enoughLamba will become famous soon enoughLamba will become famous soon enoughLamba will become famous soon enough
Default Re: Ujumbe Wa Maalim Seif Shariff Hamad Kwa Wazanzibar.

Aagh huyu Ba Hamad hana mpya hata mimi sina tatizo na cuf, tatizo ni huyu jamaa. Hivi zbar hakuna chama cha tatu chenye nguvu!
__________________
in the abundance of water, the fool is thirsty
Reply With Quote
Reply

Bookmarks

Tags
hamad, maalim, seif, shariff, ujumbe, wazanzibar


Currently Active Users Viewing This Thread: 1 (0 members and 1 guests)
 
Thread Tools
Display Modes Rate This Thread
Rate This Thread:

Posting Rules
You may not post new threads
You may not post replies
You may not post attachments
You may not edit your posts

BB code is On
Smilies are On
[IMG] code is On
HTML code is Off
Trackbacks are Off
Pingbacks are Off
Refbacks are On


Similar Threads
Thread Thread Starter Forum Replies Last Post
Bajeti Mbadala 2007/08 John Mnyika Business & Economic Forum 30 21st June 2007 10:08 PM

Tuma Ukurasa huu kwa rafiki yako!


All times are GMT +3. The time now is 01:30 AM.

Powered by JamiiForums.com
Copyrights reserved to JamiiForums.com