Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Mfalme Mgonjwa...

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 24
    1. #1
      maggid's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd December 2006
      Posts : 795
      Rep Power : 808
      Likes Received
      660
      Likes Given
      40

      Default Mfalme Mgonjwa...

      Ndugu zangu,

      KUNA tunaokumbuka kisa cha mfalme simba na wanyama wenzake. Mfalme simba alipatwa na ugonjwa. Akabaki kibandani asiweze kutembea. Na njaa nayo ikamshika. Wanyama wengi walimtembelea mfalme kumjulia hali. Walikwenda akina pundamilia, twiga, swala na wengineo. Kila aliyeingia kibandani kwa mfalme hakutoka nje.

      Mfalme simba katika kiu yake ya nyama akamtamani sana kobe. Ni kobe katika wanyama wote ambaye hakuonekana katika nyumba ya mfalme simba kumjulia hali. Simba akatuma ujumbe akilalamika; “Enenda ukamwambie kobe, nashangaa katika kuugua kwangu sijamwona kuja kunijulia hali”!

      Ujumbe ukamfikia kobe. Siku moja kobe naye akaenda kumjulia hali mfalme simba. Hakufika mpaka iliko nyumba ya mfalme simba. Alisimama mbali na kutamka: “Ewe mfalme wangu simba, nimekuja kukujulia hali, waendeleaje na afya yako?”.

      Mfalme simba akajibu: “Mbona salamu hizo unazitoa ukiwa mbali hivyo?”. Kobe akamjibu mfalme wake: “ Kuna jambo linanishangaza mfalme wangu, naona nyayo zote za wanyama zimeelekea kwako, lakini hakuna nyayo zinazorudi”!

      Katika jamii yetu sasa kuna akina mfalme simba wagonjwa na wenye njaa ya nyama. Wamewatafuna twiga, swala, pundamilia na wengineo. Sasa wanawatamani akina kobe pia!
      Ndio, katika nchi yetu sasa kuna harakati za kimakundi. Tunaziona ndani ya chama tawala, tunaziona nje ya chama hicho. Kuna wenye kuongoza harakati hizo.

      Na Watanzania tulio wengi tumekuwa ni watu wa kupenda sana kutafuna maneno. Kuna mawili makubwa ambayo ni mapungufu yetu; mosi, hatuna misimamo, pili, tukiwa nayo hatuisimamii.

      Tunapenda sana kuzungumza tusichomaanisha na mara nyingi hatumaanishi tunachozungumza. Na Mtanzania haumizi kichwa kujiuliza; “ kwanini nizungumze”. Maana suala si unachozungumza, bali ni kwanini unazungumza.

      Na kwanini wananchi wanaonekana kukata tamaa na kukosa imani kwa kinachozungumzwa na viongozi wao. Ndio, kikubwa kinachokosekana hapa ni namna nzuri ya kuwasiliana na wananchi ili kuwafahamisha na labda kuwaelimisha juu ya kilichotokea.

      Watanzania wengi hawana taarifa muhimu kuweza kutafsiri matukio na kinachozungumzwa na viongozi wao. Ni ukweli kuwa Watanzania walio wengi wanaishi vijijini. Ni takribani asilimia 21 tu ya Watanzania wenye fursa ya kupata taarifa muhimu juu ya kinachoendelea katika nchi yao; ni kupitia magazeti, runinga na redio. Waliobaki asilimia sabini na tisa ya Watanzania ndio hao wa Manzese Dar es Salaam, Mwanjelwa Mbeya, Kihesa na Kilolo Iringa na kwingineko.

      Ni hawa wasio na taarifa za kutosha kutafsiri mambo na hata kufanya maamuzi yanayotokana na kuwa na taarifa (informed decisions). Ni asilimia 79 hii ya Wanzania wa Mwanjelwa , Kilolo na kwingineko wenye kuiweka Serikali madarakani kwa wingi wa kura zao.
      Media, kwa maana ya ya wanahabari ndio walipaswa wajitoe kwenye vita vya kimakundi na kuwasaidia Watanzania hawa kupata taarifa zitakazowawezesha kufanya maamuzi sahihi.

      Lakini miongoni mwa wanahabari hawa, kuna walioingia katika foleni ya kwenda kuwajulia hali wafalme wagonjwa. Wamejiingiza kwenye vita ya kimakundi. Wamelisahau jukumu lao, wamelisahau kundi kuu. Ni kundi lile la asilimia 79 ya Watanzania.

      Tunaziona nyayo za baadhi ya wanahabari zikienda kwa wafalme wagonjwa, hatuzioni nyayo zao za kurudia!
      Wanahabari walipaswa kuwa daraja la kupitisha taarifa kutoka chini kwa wananchi kwenda juu kwa viongozi, na kinyume chake.

      Lakini, miongoni mwa wanahabari hao, wameamua kwa makusudi kulivunja daraja hilo. Ni kweli kuwa kila mwanadamu kwa namna moja au nyingine ananunulika, lakini kwa wengine, bei zao ni utu na heshima, basi. Wanasukumwa kufanya yale yenye maslahi mapana kwa taifa.

      Na hilo ni Neno La Leo. ( Limechapwa pia kwenye Mwananchi, leo Jumapili)
      Maggid,
      Iringa
      MIGNON, Butola, Narubongo and 3 others like this.


    2. #2
      mukizahp2's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 28th July 2012
      Location : tandare
      Posts : 224
      Rep Power : 391
      Likes Received
      54
      Likes Given
      505

      Default re: Mfalme Mgonjwa...

      Mtazamo wangu ...wewe mwenyewe mjengwa umekwenda kumuona mfalme mgojwa na haukurudi,yaani hiyo habari yako ni nzuri sana, na unajiongelea wewe mwenyewe na wanahabari wenzako wachache mlioamua kuasi makubaliano ya wanahabari wenzenu,wanahabari wa iringa waliamua hakuna kuandika habari za polisi ..

      Ila wewe ukaona lazima uandike,najua uliongoza harambee ya mchango kwa marehemu mwangosi lakini ulitakiwa kufuata maamuzi ya wanahabari wenzako...wewe na michuzi ni wasaliti
      Mimibaba, OSOKONI and Chum Chang like this.

    3. #3
      hippocratessocrates's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st July 2012
      Posts : 1,507
      Rep Power : 2129
      Likes Received
      581
      Likes Given
      166

      Default re: Mfalme Mgonjwa...

      Divide and rule worked...

    4. #4
      we gule's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 30th June 2012
      Posts : 124
      Rep Power : 375
      Likes Received
      10
      Likes Given
      65

      Default re: Mfalme Mgonjwa...

      Ila naamini kwa kadiri siku zinvyokwenda Watanzania wanaanza kubadilika kidogokidogo ,kwani hiyo asilimia kidogo amabayo inapata hizo taarifa watakuwa nichachu ya kwa hao wengine .

      Ni ukweli haupingiki katika ufukara na umasikini uliopo sio rahisi jamii kuielimisha ,kuihabarisha mabadiliko yanayotokea na kuwafikia kwa wakati muafaka kwani kila siku kukicha watu wapo kwenye mihangaiko ya kutafuta ka ugali kao na wanaowazunguka.

      Leo hii fanya utafiti kidogo tu pale Kariakoo uliza maswali rahisi tu; hivi jana ITV Kulikuwa na taarifa gani muhimu au Gazeti za jana kulikuwa na habari gani kuu au Muulize Mkuu wa mkoa wa Katavi ninani na tumaini huwezi kupata jibu lolote sasa katatika mazingira kama hayo hao wapo mjini, vipi mwanakijiji aliyepo Nyagwijima Kibondo, aliyepo Mambali Nzega, aliyepo Namanyele Rukwa awe na taaarifa ?

      Bado kuna kazi kubwa inahahitajika kwanza kuondoa Umasikini halafu Ujinga na mengine yatafuata.

    5. #5
      andybird314's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd January 2012
      Location : Tanzania
      Posts : 2,802
      Rep Power : 996
      Likes Received
      578
      Likes Given
      297

      Default re: Mfalme Mgonjwa...

      wanatafunwa kwa tamaa zao wenyewe au bila kujua


    6. #6
      dudus's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th February 2011
      Posts : 2,339
      Rep Power : 1018
      Likes Received
      1323
      Likes Given
      531

      Default Re: Mfalme Mgonjwa...

      Bora mfalme simba yeye alikuwa anawala jumla tena ni lishe aliyoandikiwa na mola wake!

      Lifalme letu la leo (mfumo) linakamata, linabaka na kujeruhi vibaya, linaua, na hatimaye linaacha maiti porini ikiliwa na kunguru, fisi, na ndege mwitu.

      Maumivi, fedheha, udhalilishaji, na kila aina ya aibu.

    7. #7
      Nicholas's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th March 2006
      Posts : 6,409
      Rep Power : 3903
      Likes Received
      1512
      Likes Given
      2661

      Default Re: Mfalme Mgonjwa...

      Pia hii hadith inamfaa na 6, kapiga kelele ya mwakyembe, ya ufisadi, na wengine ila yeye yupo mbio sana, kaja CDM amani haijamjia, afadhali hata kobe kuliko 6.
      SIMPLY THE RADICAL: I can`t wait to see the criminalization of CCM,UWT,Bunch of Policemen/women,and all wanafiki na wachumia tumbo.

    8. #8
      majebere's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd April 2012
      Posts : 2,300
      Rep Power : 0
      Likes Received
      334
      Likes Given
      114

      Default Re: Mfalme Mgonjwa...

      hizi hadithi za simba na sungura ndio zililaza akili ya wantanzania.

    9. #9
      MIGNON's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd November 2009
      Posts : 581
      Rep Power : 664
      Likes Received
      173
      Likes Given
      135

      Default Re: Mfalme Mgonjwa...

      Mambo haya si katika habari bali hata fani zingine pia. Angalia madaktari,kugoma,kuomba msamaha na wengine kupinga msamaha.Hapo mfalme Simba anajichukulia ki ulaini.

    10. #10
      King Kong III's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th October 2010
      Location : Enaboishu-Umenyeni
      Posts : 12,365
      Rep Power : 5155
      Likes Received
      3334
      Likes Given
      2738

      Default Re: Mfalme Mgonjwa...

      Usaliti Usalitini.........

    11. #11
      Narubongo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd November 2010
      Posts : 1,886
      Rep Power : 814
      Likes Received
      850
      Likes Given
      680

      Default Re: Mfalme Mgonjwa...

      naona umeanza kupuliza
      mukizahp2 likes this.
      "Chadema kinatumia alama ya vidole viwili kama manati, manati kamwe haiwezi kuua tembo" Livingstone Lusinde (2012)

    12. #12
      Chum Chang's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd April 2012
      Posts : 1,006
      Rep Power : 565
      Likes Received
      238
      Likes Given
      286

      Default Re: Mfalme Mgonjwa...

      Quote By mukizahp2 View Post
      mtazamo wangu ...wewe mwenyewe mjengwa umekwenda kumuona mfalme mgojwa na haukurudi,yaani hiyo habari yako ni nzuri sana, na unajiongelea wewe mwenyewe na wanahabari wenzako wachache mlioamua kuasi makubaliano ya wanahabari wenzenu,wanahabari wa iringa waliamua hakuna kuandika habari za polisi ..

      Ila wewe ukaona lazima uandike,najua uliongoza harambee ya mchango kwa marehemu mwangosi lakini ulitakiwa kufuata maamuzi ya wanahabari wenzako...wewe na michuzi ni wasaliti
      kuna hoja imewekwa kuh unafiki wa waandishi.maggid kaka unachoandika sicho unachomanisha

      kwanza toa boliti kwenye jicho lako ndipo uwaangalie watanzania jamani maggid si aliwahi kuweka tangazo la kuomba kazi na akaweka historia yake moja ya mambo yanayonishangaza ni lile tangazo ya kuwa yeye ni mswidi.....

      Sasa sijui kama ni mtz au muiringa na la mwisho amemsaliti mwangosi japo anachangisha pesa kwa yule mjane hali anawalamba miguu maafande kwa kuwapamba kwenye blog yake
      mukizahp2 likes this.

    13. #13
      peri's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd March 2011
      Posts : 1,193
      Rep Power : 656
      Likes Received
      372
      Likes Given
      40

      Default Re: Mfalme Mgonjwa...

      maggid umetoa ujumbe mzuri sana ila ni watu wachache sana ambao wanakuelewa/watakuelewa ulichoandika.
      Wengi ni wagonjwa tayari, makundi yanawatafuna mpaka wanashindwa kutumia akili zao kutafsiri mambo wanataka watafsiriwe na watu wanaowaamini na kuwapenda.
      Wanaogopa kutofautiana nao ndiomana hawataki kufikiri kwa akili zao bali wanataka wasaidiwe kufikiri.
      maggid likes this.

    14. #14
      maggid's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd December 2006
      Posts : 795
      Rep Power : 808
      Likes Received
      660
      Likes Given
      40

      Default Re: Mfalme Mgonjwa...

      Quote By Chum Chang View Post
      kuna hoja imewekwa kuh unafiki wa waandishi.maggid kaka unachoandika sicho unachomanisha

      kwanza toa boliti kwenye jicho lako ndipo uwaangalie watanzania jamani maggid si aliwahi kuweka tangazo la kuomba kazi na akaweka historia yake moja ya mambo yanayonishangaza ni lile tangazo ya kuwa yeye ni mswidi.....

      Sasa sijui kama ni mtz au muiringa na la mwisho amemsaliti mwangosi japo anachangisha pesa kwa yule mjane hali anawalamba miguu maafande kwa kuwapamba kwenye blog yake
      Chung Chang,

      Unachosema hapa ni uongo mtupu ulioutunga bila aibu. Sijawahi kuweka mahali popote tangazo la mimi kuomba kazi na kuwa mimi ni Mswidi. Mara nyingi uongo kama huu ukiachwa kuna watakaodhani ni ukweli. Na kama ni muungwana unapaswa kuniomba radhi kwa kunitungia uongo bila aibu.

      Maggid

    15. #15
      Chum Chang's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd April 2012
      Posts : 1,006
      Rep Power : 565
      Likes Received
      238
      Likes Given
      286

      Default Re: Mfalme Mgonjwa...

      Uongo wa nini na post uliweka wewe mwenyewe

    16. #16
      idawa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th January 2012
      Posts : 4,966
      Rep Power : 3411
      Likes Received
      1340
      Likes Given
      493

      Default

      Quote By Chum Chang View Post
      kuna hoja imewekwa kuh unafiki wa waandishi.maggid kaka unachoandika sicho unachomanisha

      kwanza toa boliti kwenye jicho lako ndipo uwaangalie watanzania jamani maggid si aliwahi kuweka tangazo la kuomba kazi na akaweka historia yake moja ya mambo yanayonishangaza ni lile tangazo ya kuwa yeye ni mswidi.....

      Sasa sijui kama ni mtz au muiringa na la mwisho amemsaliti mwangosi japo anachangisha pesa kwa yule mjane hali anawalamba miguu maafande kwa kuwapamba kwenye blog yake
      Mkuu hii rangi inaumiza macho,wengine hatuna miwani maalumu.!

    17. #17
      afwe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th October 2010
      Posts : 823
      Rep Power : 602
      Likes Received
      112
      Likes Given
      131

      Default Re: Mfalme Mgonjwa...

      Maggid, well written!

    18. #18
      Mimibaba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st July 2009
      Posts : 3,351
      Rep Power : 1572
      Likes Received
      813
      Likes Given
      622

      Default Re: Mfalme Mgonjwa...

      Ni kweli ameandika vizuri hadi kuainisha cha kufanyika.

      1. Mkakati una mapungufu kwa sababu watekelezaji ni hao hao wanaokwenda kumjulia hali mfalme bia kurejea.

      2. Kwenye zama hizi si kweli 79% hawahabarishwi na vyombo vya habari; kuna watu wanaowafikia wananchi vijijini kuwaelimisha and they make a difference eg M4C.

      3. Sikuipata vizuri role(nafasi) yako ya kujikwamua na mfalme simba, natumaini kuna mkakati

      Ila nashauri tujumuishwe wote kwenye kumpa sumu ale afe.
      Ukweli utakuweka huru daima

    19. #19
      jmushi1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd November 2007
      Posts : 14,426
      Rep Power : 16506
      Likes Received
      4327
      Likes Given
      5510

      Default Re: Mfalme Mgonjwa...

      Wewe kwani ulienda kwa simba ndo ukarudi na michango ya msiba badala ya kupigania haki ya waliyoliwa na simba?
      "One of the penalties for refusing to participate in politics is that you end up being governed by your inferiors"-Plato

    20. #20
      Aggrey86's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th June 2011
      Posts : 713
      Rep Power : 546
      Likes Received
      81
      Likes Given
      90

      Default Re: Mfalme Mgonjwa...

      Hii rangi mkuu wengine tumeshindwa kusoma inaumiza sana!

    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...