Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Kamanda Kamuhanda: Siwezi kujiuzulu

    Report Post
    Page 5 of 6 FirstFirst ... 3456 LastLast
    Results 81 to 100 of 104
    1. #1
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,153
      Rep Power : 3544
      Likes Received
      3036
      Likes Given
      460

      Default Kamanda Kamuhanda: Siwezi kujiuzulu

      JUMAMOSI, SEPTEMBA 22, 2012 08:48 NA ELIZABETH MJATTA

      KAMANDA wa Polisi, Mkoa wa Iringa, Michael Kamuhanda, ameibuka na kusema hawezi kujiuzulu kutokana na kifo cha aliyekuwa Mwandishi wa Habari wa Kituo cha Channel ten, Daud Mwangosi, aliyeuawa hivi karibuni mkoani Iringa.

      Kamanda Kamuhanda alitoa msimamo huo jana alipokuwa akihojiwa na Kituo cha Radio cha Radio One wakati wa kipindi cha Kumepambazuka.

      “Ninachofahamu mimi ni kwamba, kesi ya msingi iko mahakamani na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ameshaunda kamati ambayo inachunguza mwenendo mzima wa tukio hili na baadaye itatoa taarifa.

      “Kwa hiyo, siwezi kujiuzulu kwa sababu tukio hilo la kifo lilitokea wakati wa kutimiza wajibu wa kutii sheria bila shuruti,” alisema Kamanda Kamuhanda.

      Alipoulizwa kuhusiana na kuwajibika kutokana na mauaji hayo alisema, hawezi kuwajibika kwa sababu hana makosa.

      “Niwajibike kwa kosa lipi?, kuna kosa mtu anaweza akawajibika, lakini kama huna kosa huwezi kuwajibika, haiwezekani watu waliofanya makosa wenyewe kwa kuandamana bila uhalali wasiwajibike halafu mimi niwajibike, haiwezekani.

      “Sisi tunapokuwa kazini, tunalinda raia na mali zao na ndiyo tulilofanya na mara zote tunasisitiza utii wa sheria bila kushurutishwa.

      “Kwa hiyo, hicho ndicho kilichokuwa kinafanyika, kilichofanyika ndiyo utii wa sheria bila shuruti, wangetii sheria bila shuruti yote yasingetokea,” alisema.

      Septemba 2 mwaka huu, Mwangosi aliuawa kwa kupigwa na kitu kinachodhaniwa kuwa ni bomu alipokuwa kazini katika Kijiji cha Nyololo, Wilaya ya Mufindi, mkoani Iringa.

      Baada ya kulipuliwa na kitu hicho, mwili wake ulisambaratika vipande vipande ingawa pia askari mmoja aliyekuwa jirani naye, pia alijeruhiwa mguu.

      Baada ya tukio hilo, waandishi wa habari, wanaharakati na watu mbalimbali, walilaani tukio hilo na kutoa matamko yao wakitaka Kamanda Kamuhanda ajiuzulu, kutokana na mauaji hayo.

      Septemba 12 mwaka huu, askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia mwenye namba G2573, Pasificus Simon, alipandikizwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mfawidhi Wilaya ya Iringa, kwa kosa mauaji ya marehemu Mwangosi.

      Mtuhumiwa huyo alipofikishwa mahakamani hapo, hakutakiwa kujibu lolote kutokana na kosa linalomkabili haliwezi kusikilizwa katika mahakama hiyo. Hadi sasa mshitakiwa yuko mahabusu.

      Pasco likes this.

    2. Study Abroad

    3. #81
      BHULULU's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th June 2012
      Posts : 2,994
      Rep Power : 8375
      Likes Received
      827
      Likes Given
      691

      Default Re: Kamanda Kamuhanda: Siwezi kujiuzulu

      Huyu mzee naona anakaribia kufa narudia tena kufa.Kulikuwa na watu wana kiburi kama akina Dito, wako wapi?

    4. #82
      Kolero's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2010
      Location : Magubike
      Posts : 419
      Rep Power : 1155
      Likes Received
      84
      Likes Given
      291

      Default Re: Kamanda Kamuhanda: Siwezi kujiuzulu

      Quote By nngu007
      JUMAMOSI, SEPTEMBA 22, 2012 08:48 NA ELIZABETH MJATTA

      KAMANDA wa Polisi, Mkoa wa Iringa, Michael Kamuhanda, ameibuka na kusema hawezi kujiuzulu kutokana na kifo cha aliyekuwa Mwandishi wa Habari wa Kituo cha Channel ten, Daud Mwangosi, aliyeuawa hivi karibuni mkoani Iringa.

      Kamanda Kamuhanda alitoa msimamo huo jana alipokuwa akihojiwa na Kituo cha Radio cha Radio One wakati wa kipindi cha Kumepambazuka.

      “Ninachofahamu mimi ni kwamba, kesi ya msingi iko mahakamani na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ameshaunda kamati ambayo inachunguza mwenendo mzima wa tukio hili na baadaye itatoa taarifa.

      “Kwa hiyo, siwezi kujiuzulu kwa sababu tukio hilo la kifo lilitokea wakati wa kutimiza wajibu wa kutii sheria bila shuruti,” alisema Kamanda Kamuhanda.

      Alipoulizwa kuhusiana na kuwajibika kutokana na mauaji hayo alisema, hawezi kuwajibika kwa sababu hana makosa.

      “Niwajibike kwa kosa lipi?, kuna kosa mtu anaweza akawajibika, lakini kama huna kosa huwezi kuwajibika, haiwezekani watu waliofanya makosa wenyewe kwa kuandamana bila uhalali wasiwajibike halafu mimi niwajibike, haiwezekani.

      “Sisi tunapokuwa kazini, tunalinda raia na mali zao na ndiyo tulilofanya na mara zote tunasisitiza utii wa sheria bila kushurutishwa.

      “Kwa hiyo, hicho ndicho kilichokuwa kinafanyika, kilichofanyika ndiyo utii wa sheria bila shuruti, wangetii sheria bila shuruti yote yasingetokea,” alisema.

      Septemba 2 mwaka huu, Mwangosi aliuawa kwa kupigwa na kitu kinachodhaniwa kuwa ni bomu alipokuwa kazini katika Kijiji cha Nyololo, Wilaya ya Mufindi, mkoani Iringa.

      Baada ya kulipuliwa na kitu hicho, mwili wake ulisambaratika vipande vipande ingawa pia askari mmoja aliyekuwa jirani naye, pia alijeruhiwa mguu.

      Baada ya tukio hilo, waandishi wa habari, wanaharakati na watu mbalimbali, walilaani tukio hilo na kutoa matamko yao wakitaka Kamanda Kamuhanda ajiuzulu, kutokana na mauaji hayo.

      Septemba 12 mwaka huu, askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia mwenye namba G2573, Pasificus Simon, alipandikizwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mfawidhi Wilaya ya Iringa, kwa kosa mauaji ya marehemu Mwangosi.

      Mtuhumiwa huyo alipofikishwa mahakamani hapo, hakutakiwa kujibu lolote kutokana na kosa linalomkabili haliwezi kusikilizwa katika mahakama hiyo. Hadi sasa mshitakiwa yuko mahabusu.

      Hapa linalotakiwa ni kweli siyo kujiuzulu bali kufikishwa mahakamani kujibu shtaka la mauaji. Kutii sheria bila shuruti pale haihusiki, kamanda nadhani inafaa apewe video clips aangalie, tukio la mauaji lilitokea baada ya watu kutii amri yake na kutawanyika. Pia ajue kuwa yale hayakuwa maandamano kama anavyodai labda atumie sheria ya Mkusanyiko, alafu ajue aliyeuawa si kiongozi wa chama, bali Mwandishi wa habari aliyekuwa kazini tena akiwa na amani na si katika fujo kama yeye alivyokuwa pale. Mbaya zaidi, Mwandishi hakuwa na silaha yoyote hatarishi, alikuwa ameshawekwa chini ya mikono ya askari zaidi ya mmoja(asome sheria ya kumu-arrest mtu) na kosa lake Kamanda, alikuwa pale maeneo ya tukio akishuhudia toafuti na ilivyokuwa kwa afande Zomba(hakuwepo katika tukio). Kifupi, mazingira ya mauaji, uwepo wake ndio ulizidisha hata wale askari kutotii amri ya kumuacha aliyokuwa anawaeleza kamanda aliyekuwa nao, badala yake walikuwa wanatii huyu kamanda Kamuhanda. Ni katika hili, yeye ilipaswa awe mshtakiwa namba moja, askari hao wengine pamoja na huyo aliyepelekwa mahakamani washrakiwa namba mbili na kufuata. Kung'ang'ania utii wa sheria bila shuruti haina mshiko hapo, na ikutumiwa hivyo atasababisha watu kudai kujiuzulu kwa viongozi wake wa juu, yeye sasa hivi akiri amesababisha haya yote, haikuwa maandamano ajue hilo,aangalie video clips zimsaidie anapoongea badala ya haya aliyosema.
      "Religion ... is the opium of the people"-Karl Marx.

    5. #83
      msnajo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th January 2011
      Posts : 665
      Rep Power : 555
      Likes Received
      75
      Likes Given
      92

      Default Re: Kamanda Kamuhanda: Siwezi kujiuzulu

      Wakuu naomba kuuliza swali la ufahamu, "Mada kama hizi mbona siwaoni Ritz na Zomba"? Au wao wanahusika kwenye mada za CDM tu???

    6. #84
      Thesi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th August 2010
      Posts : 727
      Rep Power : 4675
      Likes Received
      186
      Likes Given
      320

      Default Re: Kamanda Kamuhanda: Siwezi kujiuzulu

      Chondechonde watanzania wenzangu tusiache huu uppuzi uendeleee. Tunaomba vyama vya siasa bila kujali ni chama gani wakishirikiana na wananchi wote tuandee maandamano ya kulazimisha huyu muuaji pamoja na wenzake kujiuzulu. Amenikera kweli huyu shetani.
      Kolero likes this.

    7. Paw
      #85
      Paw's Avatar
      Super Moderator Array
      Join Date : 14th November 2010
      Posts : 1,546
      Rep Power : 2843
      Likes Received
      613
      Likes Given
      2049

      Default Re: Kamanda Kamuhanda: Siwezi kujiuzulu

      Majibu yake yamenistua sana.

      Hakika sheria si mali kitu kwa the keeper.
      jmushi1 likes this.
      (BADILIKA, bofya hapa ===> ####)

    8. Miaka 50

    9. #86
      Kolero's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2010
      Location : Magubike
      Posts : 419
      Rep Power : 1155
      Likes Received
      84
      Likes Given
      291

      Default Re: Kamanda Kamuhanda: Siwezi kujiuzulu

      Quote By SUPERXAVERY
      acheni kelele, kamanda kesha ongea, andamaneni tena tuwatwale mitwe.
      Afterall mna uhakika gani kuwa bomu lililomuua mwangosi limetoka kwenye bunduki ya yule dogo. Inawezekana walikuja nalo ili wawalipue polisi kwa jazba na kumbe wameua mwandishi.
      Ni mawazo yako Mkuu kama vile hao unaotaka waache kelele nao wanavyotoa mawazo yao. Kuhusu hilo bomu tayari jibu lishatolewa na mamlaka husika kumbe hatujadili jambo hilo na hatunasababu ya kutumia neno"inawezekana" bali tunajadili wahusika wa mauaji ili wachukuliwe hatua stahiki.
      "Religion ... is the opium of the people"-Karl Marx.

    10. #87
      tenende's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th January 2012
      Posts : 1,067
      Rep Power : 584
      Likes Received
      206
      Likes Given
      483

      Default Re: Kamanda Kamuhanda: Siwezi kujiuzulu

      Yuko salama mikononi mwa ccm waliomtuma!.

    11. #88
      tenende's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th January 2012
      Posts : 1,067
      Rep Power : 584
      Likes Received
      206
      Likes Given
      483

      Default Re: Kamanda Kamuhanda: Siwezi kujiuzulu

      Quote By SUPERXAVERY
      acheni kelele, kamanda kesha ongea, andamaneni tena tuwatwale mitwe.
      Afterall mna uhakika gani kuwa bomu lililomuua mwangosi limetoka kwenye bunduki ya yule dogo. Inawezekana walikuja nalo ili wawalipue polisi kwa jazba na kumbe wameua mwandishi.
      Unajua hujui kuwa hujui!. Coincidence: Kamuhanda (mhaya), alimtuma Pasificus Simon (mhaya), kumuua Mwangosi (Mnyakyusa) na mtetezi wake OCD - Mwampamba (mnyakyusa) akajeruhiwa. Haya yanasemwa site!.

    12. #89
      timbilimu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd September 2010
      Location : DSM
      Posts : 2,662
      Rep Power : 974
      Likes Received
      577
      Likes Given
      10

      Default Re: Kamanda Kamuhanda: Siwezi kujiuzulu

      Nikisoma habari kama hii najiuliza maswali mengi,jibu ninalopata ni kwamba hatuna jeshi la Polisi hapa,bali watu wasiokua na nidhamu wala mafunzo ambao wanajiita Polisi. Ni heri ya mgambo kuliko hawa watu wanajiita Polisi hapa Tanzania!

    13. #90
      jmushi1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd November 2007
      Posts : 14,375
      Rep Power : 16492
      Likes Received
      4298
      Likes Given
      5491

      Default Re: Kamanda Kamuhanda: Siwezi kujiuzulu

      Quote By Paw
      Majibu yake yamenistua sana.

      Hakika sheria si mali kitu kwa the keeper.
      Mkuu hata humu nadhani yupo,maana kuna watu huwa wanaposti maneno kama hayo kabisa.Yaani ya ku justify kile kifo kwa namna anayoifanya Kamuhanda.Mkuu muwe mnawalima ban ili at least tupate hata justice kidogo hapa kume enzi marehemu.Huku tukisubiri haki ichukuwe mkondo wake na huko uraiani God willing!
      "One of the penalties for refusing to participate in politics is that you end up being governed by your inferiors"-Plato

    14. #91
      Mujwahuzia's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 17th November 2011
      Posts : 137
      Rep Power : 406
      Likes Received
      31
      Likes Given
      3

      Default Re: Kamanda Kamuhanda: Siwezi kujiuzulu

      Waandishi wa habari mnazidi konyesha udhaifu mwingine baada ya Kifo cha Mtanzania mwenzetu D. Mwangosi mimi sisemi mwandishi wa habari tu bali mtanzania mwenzetu kwa maana mlolongo wa mauaji yanayo ligusa jeshi la polisi ni mengi sasa nilifurahi sana kusikia Azimio la wanahabari baada ya kifo cha huyu ndugu yetu lilikuwa kuanzia siku hiyo hadi siku 40 wanahabari hawataaandika habari yoyote inayohusiana na jeshi la Polisi ajabu hata wiki mbili baadhi ya vyombo vya habari vina waaalika watuhumiwa wa mauaji ya ndugu zetu nao wanaishia kutoa matamko kama mliyoyasikia ndugu zangu mnajipendekeza kwao ili iweje????????????? wengine walisema pale Jngwani kwamba hawana Ugonvi na Waziri E.Nchimbi, wala hawana ugonvi na serikali yao nikajiuliza wanahabari ninyi mgonvi wenu katika hili ni nani hasa??endapo baada ya kumuona waziri mwenye Dhamana na chombo anachokiongoza mkamtumia salaamu za kumpenda sasa mgonvi wenu ni nani hasaaaaaaaaaaaaaaaaaa?????????

    15. #92
      Elli's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 17th March 2008
      Location : Kijito-Upele
      Posts : 8,513
      Rep Power : 0
      Likes Received
      2102
      Likes Given
      1839

      Default Re: Kamanda Kamuhanda: Siwezi kujiuzulu

      Kamanda wa uongo huyu, kamanda gani mwoga vile, kama kweli wanajiamini si wangeweka silaha chini zikapigwa kavukavu? sasa wewe unakuja na bunduki?

    16. #93
      Ndallo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st October 2010
      Location : LaRusa
      Posts : 4,100
      Rep Power : 6358
      Likes Received
      1450
      Likes Given
      407

      Default Re: Kamanda Kamuhanda: Siwezi kujiuzulu

      Quote By Miaghay
      Failure
      Thanks!
      '' Mtu ni Utu sio Kitu''

    17. Paw
      #94
      Paw's Avatar
      Super Moderator Array
      Join Date : 14th November 2010
      Posts : 1,546
      Rep Power : 2843
      Likes Received
      613
      Likes Given
      2049

      Default Re: Kamanda Kamuhanda: Siwezi kujiuzulu

      Quote By jmushi1
      .....Mkuu muwe mnawalima ban ili at least tupate hata justice kidogo hapa.....
      Hahaha mkuu.
      Kanuni za JF hazuruhusu kuwa bias kwenye maamuzi na hakuna aliye juu yake.
      (BADILIKA, bofya hapa ===> ####)

    18. #95
      jmushi1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd November 2007
      Posts : 14,375
      Rep Power : 16492
      Likes Received
      4298
      Likes Given
      5491

      Default Re: Kamanda Kamuhanda: Siwezi kujiuzulu

      Quote By Paw
      Hahaha mkuu.
      Kanuni za JF hazuruhusu kuwa bias kwenye maamuzi na hakuna aliye juu yake.
      Ha ha ha!sawa mkuu,ila sidhani kama justice iko bias.Hakuna justification ya kuwaua raia wasokuwa na hatia kwa kusema ukweli mkuu.So unaweza usimlime Kamuhanda ban humu,however ukamwambia azingatie ubinaadam kidogo.Kwa mfano kuna picha humu iko wazi kabisa kuwa polisi ameuwa,lakini utashangazwa upotoshaji wa wazi wa either kujustify tukio lile ama kusema ni chama cha upinzani kimefanya mauwaji.

      Anyways mkuu,ni kweli kama justice ikichukuwa mkondo wake,basi hawataweza kutetea unyama kama ule humu ndani.

      Kazi njema mkuu.
      Last edited by jmushi1; 24th September 2012 at 15:56.
      Paw likes this.
      "One of the penalties for refusing to participate in politics is that you end up being governed by your inferiors"-Plato

    19. #96
      Monyiaichi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th July 2012
      Posts : 540
      Rep Power : 454
      Likes Received
      113
      Likes Given
      69

      Default Re: Kamanda Kamuhanda: Siwezi kujiuzulu

      kwanza kabisa aliyekuwa anamuhoji hakuwa na nia ya kujua mengi kutoka kwa muhojiwa;
      alikuwa anatimiza wajibu wake wa kazi kwa waandamanaji walioshindwa kutii sheria bila shuruti, hivi mwangisi alikuwa akiandamana? huwa hakuna exemption kati ya waandishi wa habari na raia wengine? kama ipo kwa nini mwangisi ameuawa wakati yeye sio mwandamanaji? ( walao ingekuwa na raia angesingizia hicho anachokisema). halafu hakumfahamu marehemu kabla ya mauaji kutekelezwa? mbona picha zilimuonyesha amejiegesha pembeni akifuatilia tukio zima? kwa hiyo sasa mmeamua kusema tu hata uongo wa wazi bila kujali ukweli ulioko wazi?
      Mungu akitujalia uzima tutajua ukweli tu, yatajidhihirisha tu kwa namna yoyote ile

    20. #97
      kasumbaleza's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 19th June 2011
      Posts : 376
      Rep Power : 0
      Likes Received
      48
      Likes Given
      58

      Default Re: Kamanda Kamuhanda: Siwezi kujiuzulu

      kesi ipo mahakamani kujiuzulu kunatoka wapi

    21. #98
      Safari_ni_Safari's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th October 2007
      Location : Kibaruani
      Posts : 11,880
      Rep Power : 24131
      Likes Received
      4611
      Likes Given
      2624

      Default Re: Kamanda Kamuhanda: Siwezi kujiuzulu

      Kamuhanda kikwetu ni neno baya sana

      Soki Ozali Mwasi Yaka, Soki Ozali Mobali Koya Te


    22. #99
      Azipa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th March 2012
      Posts : 933
      Rep Power : 547
      Likes Received
      226
      Likes Given
      1

      Default

      Quote By msnajo
      Wakuu naomba kuuliza swali la ufahamu, "Mada kama hizi mbona siwaoni Ritz na Zomba"? Au wao wanahusika kwenye mada za CDM tu???
      Kwenye mada zinazocompromise position ya JK Ritz na Zomba ni observers tu. Baadae JK atawadebrief ili kutathmini upepo

      Mfano mwingine ni ile mada ya gas na oil hutamwona Ritz au Zomba kule. Maslahi ya JK yameguswa

    23. #100
      Safari_ni_Safari's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th October 2007
      Location : Kibaruani
      Posts : 11,880
      Rep Power : 24131
      Likes Received
      4611
      Likes Given
      2624

      Default Re: Kamanda Kamuhanda: Siwezi kujiuzulu

      Quote By Azipa
      Kwenye mada zinazocompromise position ya JK Ritz na Zomba ni observers tu. Baadae JK atawadebrief ili kutathmini upepo

      Mfano mwingine ni ile mada ya gas na oil hutamwona Ritz au Zomba kule. Maslahi ya JK yameguswa
      Kwa sasa wako kwenye SHIMIWI kule Morogoro wakisimamia hii timu ya IKULU


      Soki Ozali Mwasi Yaka, Soki Ozali Mobali Koya Te


    24. FemaTV & Radio
    Page 5 of 6 FirstFirst ... 3456 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...