Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM - JamiiForums |The Home of Great Thinkers

Go Back   JamiiForums |The Home of Great Thinkers > Public Forums > Jukwaa la Siasa


Jukwaa la Siasa Tanzania & World Politics General Discussion Forum. You need to be registered in order to post your comment(s)


Reply
 
LinkBack Thread Tools Rate Thread Display Modes
Old 2nd July 2009, 09:09 PM   #1
Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM
Keil Keil is offline 2nd July 2009, 09:09 PM

Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Na Ummy Muya

BARAZA Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) limesema kutokana na serikali kutupilia mbali ombi la kunzisha Mahakama ya Kadhi, Waislamu hawataipigia kura CCM katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.

Katika taarifa yake, Bakwata ilifikia hatua ya kusema Waislamu wasimchague Rais Jakaya Kikwete iwapo atasimamishwa na CCM kugombea urais, ikiwa ni pamoja na wabunge na madiwani watakaosimamishwa na chama hicho tawala kutokana na kitendo cha serikali kutupilia mbali hoja ya Mahakama ya Kadhi.

Kauli hiyo imetolewa jana wakati Mufti Issa bin Shaaban Simba alipokuwa akitoa tamko kupinga uamuzi wa serikali kutaka kutumia sheria za dini ya Kiislamu katika mahakama za kawaida badala ya kuanzisha Mahakama ya Kadhi, kitu ambacho alisema anaamini kitawanyima haki Waislamu.

Alisema serikali imedhihirisha kuwa inaendeshwa na Wakristo na si kweli kama serikali haina dini na akamtaka Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe kubatilisha kauli hiyo kwa kuwa inamchafua Rais Jakaya Kikwete mbele ya umma wa Waislamu.

Waziri ametuthibitishia kama Rais Kikwete alikuwa akitulaghai ili tumpigie kura kwa kigezo kuwa suala hilo litashughulikiwa na kupatiwa ufumbuzi na sio kuchanganywa kama ilivyokuwa mwaka 1970 katika Sheria ya Ndoa na kuwanyima haki Waislamu,alisema.

Alisema kwa muda mrefu sana Waislamu wamekuwa kimya wakitumia hekima na busara kudai haki zao, lakini katika hatua hii ambayo serikali imefikia hawapo tayari kuendelea kudhalilishwa na kuwa kitendo hicho ni dhalimu.

Mufti alisema wamekuwa wakiiomba Mahakama ya Kadhi kwa zaidi ya miaka 20 na hivyo hawezi kuendelea kuwa kimya na kupakwa mafuta kwa mgongo wa chupa kwa kuwa mahakama hiyo ni haki yao.

Alisema kauli ya Waziri Chikawe imedhihirisha kuwa serikali ina wenyewe na Waislamu wamewekwa katika tabaka la pili pamoja na Rais Jakaya Kikwete kuwatuliza kwa ahadi kuwa watalipatia ufumbuzi suala hilo.

Natoa wito kwa Masheikh wote nchini na Waislamu wa madhehebu yote kupinga vikali kauli iliyotolewa na Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe na kwamba Waislamu waige mfano wa Waislamu wa Afrika Kusini,alisema Mufti na kuhoji:

Kwa nini iwe Afrika ya Kusini na isiwe Zanzibar, Uganda na Kenya ambazo zipo ndani ya Afrika Mashariki? Kwa niaba ya Waislamu nasema serikali haikututendea haki na imetuchukiza sana,alisema.

Alisema lengo la kuomba mahakama hiyo ni kuhakikisha Waislamu wanashughulikia masuala yao ya ndoa na mirathi na si vinginevyo, hivyo waziri asipotoshe jamii kwa kutumia mifano ambayo haiko sahihi.

Mahakama hii haitawakata wezi mikono kwa kuwa nchi hii ina katiba na sheria na sisi tutazirudisha kesi zote za jinai mikononi mwa serikali. Sifahamu hiyo kamati ambayo waziri alisema alikuwa amekaa na kutoa tamko hilo ilikuwa na watu gani,alihoji.
Aliongeza kuwa kutokana na mapungufu hayo waziri arudi tena na kukutana na masheikh ili apate muongozo wa nini Waislamu wanahitaji na sio kuzungumza bila kuwa na usahihi wa kile anachosema.

Wakizungumza na waandishi wa habari baada ya tamko la Bakwata, masheikh walikuwa na mitazamo tofauti. Sheikh wa mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Salum Mussa alisema wapo baadhi ya Waislamu ambao watakubali kutokana na ufinyu wao wa elimu ya dini.
Mussa alisema haoni sababu ya serikali kufanya njia ya mkato katika suala hilo kwani Waislamu wanahitaji Mahakama ya Kadhi kama ilivyo kwa wafanyabiashara ambao wana mahakama yao.

Hukumu inayotolewa katika Mahakama ya Kadhi ni ibada kwa mujibu wa mafundisho ya Mtume Muhammad (S.A.W) hivyo ni lazima kwa atakayetoa hukumu hiyo awe Muislamu na si vinginevyo,alisema.

Namshanga waziri anapotaka sheria hizi zitumiwe katika mahakama za kawaida. Aliona wapi John akawa imamu,alihoji sheikh huyo wa mkoa wa Dar es Salaam.

Naye katibu wa Bakwata wilayani Ilala, Sheikh Issa Ausi alisema historia iko wazi. Waasisi na wanaharakati ambao waliitoa Tanganyika mikononi mwa wakoloni walikuwa Waislamu, na akahoji sababu za serikali kuwa mstari wa mbele kuwafunga midomo leo.
Bakwata imezinduka sasa Waislamu wote tumeungana katika kupigania haki zetu na kutetea maslahi yetu na serikali itambue kuwa Bakwata iko hai hao Wakristo walikuwa wapi wakati sisi tukipigania uhuru,alihoji.

Wakati huohuo, Sheikh Salum Rwambo alisema anawashangaa wabunge Waislamu ambao baadhi ni mahajat na malhaj wanakaa kimya na kushindwa kutetea hoja za msingi na kudai kuwa huo sasa ndio mwisho wao wa kuwaita masheikh na kutaka waombewe dua ili wasipate wepesi katika kampeni zao.

Sheikh Rwambo pia alimsifia mbunge wa Nzega Lucas Selelii kwamba ni miongoni mwa wabunge katika Bunge hilo wanaozungumza ukweli na kwa kujiamini tofauti na wengine ambao wanaenda kukaa bila kufanya kazi zilizowapeleka.


Source: Mwananchi


CCM watajuta kuweka swala la Mahakama ya Kadhi kwenye Ilani yao uchaguzi ya 2005.

Keil
JF Senior Expert Member
Points: 628,831, Level: 100 Points: 628,831, Level: 100 Points: 628,831, Level: 100
Activity: 4% Activity: 4% Activity: 4%
Join Date: Mon Jul 2007
Posts: 1,385
Thanks: 91
Thanked 300 Times in 133 Posts
Views: 5444
Reply With Quote
  #2  
Old 2nd July 2009, 09:15 PM
Kituko Kituko is offline
Kituko has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 89,555, Level: 100 Points: 89,555, Level: 100 Points: 89,555, Level: 100
Activity: 28% Activity: 28% Activity: 28%
 
Join Date: Mon Jan 2009
Posts: 1,046
Thanks: 52
Thanked 162 Times in 121 Posts
Rep Power: 24
Kituko will become famous soon enoughKituko will become famous soon enoughKituko will become famous soon enoughKituko will become famous soon enoughKituko will become famous soon enoughKituko will become famous soon enoughKituko will become famous soon enoughKituko will become famous soon enough
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

kaaaazi kwelikweli
Reply With Quote
  #3  
Old 2nd July 2009, 09:18 PM
Tumain's Avatar
Tumain Tumain is offline
Tumain has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 266,004, Level: 100 Points: 266,004, Level: 100 Points: 266,004, Level: 100
Activity: 48% Activity: 48% Activity: 48%
 
Join Date: Sun Jun 2009
Posts: 3,149
Thanks: 1,154
Thanked 1,065 Times in 683 Posts
Rep Power: 27
Tumain will become famous soon enoughTumain will become famous soon enoughTumain will become famous soon enoughTumain will become famous soon enoughTumain will become famous soon enoughTumain will become famous soon enoughTumain will become famous soon enoughTumain will become famous soon enough
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

watagawanyika tuu hivi, jamaa wanatafuta bei zao. serikali iwaweke lupango waache kelele.
Reply With Quote
  #4  
Old 2nd July 2009, 09:24 PM
Malafyale Malafyale is offline
Malafyale has no status.
Senior Member
Points: 253,130, Level: 100 Points: 253,130, Level: 100 Points: 253,130, Level: 100
Activity: 4% Activity: 4% Activity: 4%
 
Join Date: Mon Aug 2008
Posts: 231
Thanks: 22
Thanked 116 Times in 54 Posts
Rep Power: 22
Malafyale will become famous soon enoughMalafyale will become famous soon enoughMalafyale will become famous soon enoughMalafyale will become famous soon enoughMalafyale will become famous soon enoughMalafyale will become famous soon enoughMalafyale will become famous soon enoughMalafyale will become famous soon enough
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Nao wakristo waungane kuanzisha "mahakama zao kiroho ndani ya katiba"?Nchi hii itakuwaje?anyway siwalaumu ndugu zangu Waislam maana CCM na serikali yake iliwahaidi jambo hili na hata ikawekwa kwenye ilani yao ya uchaguzi,maskini haweakujua kama wanatapeliwa ili watoe kura kama ambavyo ahadi nyingi hewa zilizotolewa!
Bytheway lkn Waislam hawajachambua wazi wanakosa kitu gani kwenye sheria mama zilizopo tz hivi sasa hadi wanapigania mahakama ya kadhi?watapata ni ni ikianzishwa mahakama ya kadhi ambacho sasa hawapati?
Reply With Quote
  #5  
Old 2nd July 2009, 09:28 PM
MkamaP MkamaP is offline
MkamaP has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 292,806, Level: 100 Points: 292,806, Level: 100 Points: 292,806, Level: 100
Activity: 30% Activity: 30% Activity: 30%
 
Join Date: Sat Jan 2007
Posts: 2,585
Thanks: 48
Thanked 214 Times in 163 Posts
Rep Power: 29
MkamaP will become famous soon enoughMkamaP will become famous soon enoughMkamaP will become famous soon enoughMkamaP will become famous soon enoughMkamaP will become famous soon enoughMkamaP will become famous soon enoughMkamaP will become famous soon enoughMkamaP will become famous soon enough
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Quote:
View Post
Nao wakristo waungane kuanzisha "mahakama zao kiroho ndani ya katiba"?Nchi hii itakuwaje?anyway siwalaumu ndugu zangu Waislam maana CCM na serikali yake iliwahaidi jambo hili na hata ikawekwa kwenye ilani yao ya uchaguzi,maskini haweakujua kama wanatapeliwa ili watoe kura kama ambavyo ahadi nyingi hewa zilizotolewa!
Bytheway lkn Waislam hawajachambua wazi wanakosa kitu gani kwenye sheria mama zilizopo tz hivi sasa hadi wanapigania mahakama ya kadhi?watapata ni ni ikianzishwa mahakama ya kadhi ambacho sasa hawapati?
Ni sehemu ya ibaada
Reply With Quote
  #6  
Old 2nd July 2009, 09:29 PM
JokaKuu JokaKuu is offline
JokaKuu has no status.
JF Premium Member
Points: 967,820, Level: 100 Points: 967,820, Level: 100 Points: 967,820, Level: 100
Activity: 14% Activity: 14% Activity: 14%
 
Join Date: Mon Jul 2006
Posts: 3,389
Thanks: 298
Thanked 432 Times in 244 Posts
Rep Power: 111
JokaKuu is a glorious beacon of lightJokaKuu is a glorious beacon of lightJokaKuu is a glorious beacon of lightJokaKuu is a glorious beacon of lightJokaKuu is a glorious beacon of lightJokaKuu is a glorious beacon of lightJokaKuu is a glorious beacon of lightJokaKuu is a glorious beacon of lightJokaKuu is a glorious beacon of lightJokaKuu is a glorious beacon of lightJokaKuu is a glorious beacon of light
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

..Kikwete alishachomoa kuhusu ahadi ya Mahakama ya Kadhi.

..alidai waliotumbukiza suala hilo kwenye ilani ni Philip Mangula[mkristo] na Ngombale Mwiru[hana dini].
Reply With Quote
  #7  
Old 2nd July 2009, 09:30 PM
Tumain's Avatar
Tumain Tumain is offline
Tumain has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 266,004, Level: 100 Points: 266,004, Level: 100 Points: 266,004, Level: 100
Activity: 48% Activity: 48% Activity: 48%
 
Join Date: Sun Jun 2009
Posts: 3,149
Thanks: 1,154
Thanked 1,065 Times in 683 Posts
Rep Power: 27
Tumain will become famous soon enoughTumain will become famous soon enoughTumain will become famous soon enoughTumain will become famous soon enoughTumain will become famous soon enoughTumain will become famous soon enoughTumain will become famous soon enoughTumain will become famous soon enough
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Quote:
View Post
Nao wakristo waungane kuanzisha "mahakama zao kiroho ndani ya katiba"?Nchi hii itakuwaje?anyway siwalaumu ndugu zangu Waislam maana CCM na serikali yake iliwahaidi jambo hili na hata ikawekwa kwenye ilani yao ya uchaguzi,maskini haweakujua kama wanatapeliwa ili watoe kura kama ambavyo ahadi nyingi hewa zilizotolewa!
Bytheway lkn Waislam hawajachambua wazi wanakosa kitu gani kwenye sheria mama zilizopo tz hivi sasa hadi wanapigania mahakama ya kadhi?watapata ni ni ikianzishwa mahakama ya kadhi ambacho sasa hawapati?
wewe mkristo inakuhusu nini?
Unajuaje walichokosa kwenye mahakama mama?
wapeni haki zao what is the issue here?
Reply With Quote
  #8  
Old 2nd July 2009, 09:31 PM
Lunyungu Lunyungu is offline
Lunyungu Kisu Kikali Mno
JF Senior Expert Member
Points: 1,697,655, Level: 100 Points: 1,697,655, Level: 100 Points: 1,697,655, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Tue Dec 2006
Location: Malampaka
Posts: 4,706
Thanks: 1
Thanked 204 Times in 111 Posts
Rep Power: 33
Lunyungu will become famous soon enoughLunyungu will become famous soon enoughLunyungu will become famous soon enoughLunyungu will become famous soon enoughLunyungu will become famous soon enoughLunyungu will become famous soon enoughLunyungu will become famous soon enoughLunyungu will become famous soon enough
Default Baada ya Mufti kusema ni kweli Waislam hawatapiga kura ?

Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM


Mufti Issa bin Shaaban Simba, amekasilishwa na uamuzi wa serikali kuhusu Mahakama ya Kadhi.

Na Ummy Muya

BARAZA Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) limesema kutokana na serikali kutupilia mbali ombi la kunzisha Mahakama ya Kadhi, Waislamu hawataipigia kura CCM katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.

Katika taarifa yake, Bakwata ilifikia hatua ya kusema Waislamu wasimchague Rais Jakaya Kikwete iwapo atasimamishwa na CCM kugombea urais, ikiwa ni pamoja na wabunge na madiwani watakaosimamishwa na chama hicho tawala kutokana na kitendo cha serikali kutupilia mbali hoja ya Mahakama ya Kadhi.

Kauli hiyo imetolewa jana wakati Mufti Issa bin Shaaban Simba alipokuwa akitoa tamko kupinga uamuzi wa serikali kutaka kutumia sheria za dini ya Kiislamu katika mahakama za kawaida badala ya kuanzisha Mahakama ya Kadhi, kitu ambacho alisema anaamini kitawanyima haki Waislamu.

Alisema serikali imedhihirisha kuwa inaendeshwa na Wakristo na si kweli kama serikali haina dini na akamtaka Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe kubatilisha kauli hiyo kwa kuwa inamchafua Rais Jakaya Kikwete mbele ya umma wa Waislamu.

Waziri ametuthibitishia kama Rais Kikwete alikuwa akitulaghai ili tumpigie kura kwa kigezo kuwa suala hilo litashughulikiwa na kupatiwa ufumbuzi na sio kuchanganywa kama ilivyokuwa mwaka 1970 katika Sheria ya Ndoa na kuwanyima haki Waislamu,alisema.

Alisema kwa muda mrefu sana Waislamu wamekuwa kimya wakitumia hekima na busara kudai haki zao, lakini katika hatua hii ambayo serikali imefikia hawapo tayari kuendelea kudhalilishwa na kuwa kitendo hicho ni dhalimu.

Mufti alisema wamekuwa wakiiomba Mahakama ya Kadhi kwa zaidi ya miaka 20 na hivyo hawezi kuendelea kuwa kimya na kupakwa mafuta kwa mgongo wa chupa kwa kuwa mahakama hiyo ni haki yao.

Alisema kauli ya Waziri Chikawe imedhihirisha kuwa serikali ina wenyewe na Waislamu wamewekwa katika tabaka la pili pamoja na Rais Jakaya Kikwete kuwatuliza kwa ahadi kuwa watalipatia ufumbuzi suala hilo.

Natoa wito kwa Masheikh wote nchini na Waislamu wa madhehebu yote kupinga vikali kauli iliyotolewa na Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe na kwamba Waislamu waige mfano wa Waislamu wa Afrika Kusini,alisema Mufti na kuhoji:

Kwa nini iwe Afrika ya Kusini na isiwe Zanzibar, Uganda na Kenya ambazo zipo ndani ya Afrika Mashariki? Kwa niaba ya Waislamu nasema serikali haikututendea haki na imetuchukiza sana,alisema.

Alisema lengo la kuomba mahakama hiyo ni kuhakikisha Waislamu wanashughulikia masuala yao ya ndoa na mirathi na si vinginevyo, hivyo waziri asipotoshe jamii kwa kutumia mifano ambayo haiko sahihi.

Mahakama hii haitawakata wezi mikono kwa kuwa nchi hii ina katiba na sheria na sisi tutazirudisha kesi zote za jinai mikononi mwa serikali. Sifahamu hiyo kamati ambayo waziri alisema alikuwa amekaa na kutoa tamko hilo ilikuwa na watu gani,alihoji.

Aliongeza kuwa kutokana na mapungufu hayo waziri arudi tena na kukutana na masheikh ili apate muongozo wa nini Waislamu wanahitaji na sio kuzungumza bila kuwa na usahihi wa kile anachosema.

Wakizungumza na waandishi wa habari baada ya tamko la Bakwata, masheikh walikuwa na mitazamo tofauti. Sheikh wa mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Salum Mussa alisema wapo baadhi ya Waislamu ambao watakubali kutokana na ufinyu wao wa elimu ya dini.

Mussa alisema haoni sababu ya serikali kufanya njia ya mkato katika suala hilo kwani Waislamu wanahitaji Mahakama ya Kadhi kama ilivyo kwa wafanyabiashara ambao wana mahakama yao.

Hukumu inayotolewa katika Mahakama ya Kadhi ni ibada kwa mujibu wa mafundisho ya Mtume Muhammad (S.A.W) hivyo ni lazima kwa atakayetoa hukumu hiyo awe Muislamu na si vinginevyo,alisema.

Namshanga waziri anapotaka sheria hizi zitumiwe katika mahakama za kawaida. Aliona wapi John akawa imamu,alihoji sheikh huyo wa mkoa wa Dar es Salaam.

Naye katibu wa Bakwata wilayani Ilala, Sheikh Issa Ausi alisema historia iko wazi. Waasisi na wanaharakati ambao waliitoa Tanganyika mikononi mwa wakoloni walikuwa Waislamu, na akahoji sababu za serikali kuwa mstari wa mbele kuwafunga midomo leo.

Bakwata imezinduka sasa Waislamu wote tumeungana katika kupigania haki zetu na kutetea maslahi yetu na serikali itambue kuwa Bakwata iko hai hao Wakristo walikuwa wapi wakati sisi tukipigania uhuru,alihoji.

Wakati huohuo, Sheikh Salum Rwambo alisema anawashangaa wabunge Waislamu ambao baadhi ni mahajat na malhaj wanakaa kimya na kushindwa kutetea hoja za msingi na kudai kuwa huo sasa ndio mwisho wao wa kuwaita masheikh na kutaka waombewe dua ili wasipate wepesi katika kampeni zao. Sheikh Rwambo pia alimsifia mbunge wa Nzega Lucas Selelii kwamba ni miongoni mwa wabunge katika Bunge hilo wanaozungumza ukweli na kwa kujiamini tofauti na wengine ambao wanaenda kukaa bila kufanya kazi zilizowapeleka.
Reply With Quote
  #9  
Old 2nd July 2009, 09:55 PM
Masatu Masatu is offline
Masatu Is Magumashi
JF Senior Expert Member
Points: 733,039, Level: 100 Points: 733,039, Level: 100 Points: 733,039, Level: 100
Activity: 4% Activity: 4% Activity: 4%
 
Join Date: Mon Jan 2007
Location: Mbagala, Jeshini
Posts: 3,741
Thanks: 0
Thanked 88 Times in 66 Posts
Rep Power: 0
Masatu is infamous around these parts
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Bakwata hawana ubavu huo wanabwaka tu, wao wenyewe credibility yao ni questionable wasafishe nyumba yao kwanza.

Hawana jipya zaidi ya kutafuta njia ya kutokea na kuficha madudu yao. Ni ukweli usio na shaka uislam haupo kitaasisi kama ukristo na madhehebu yake catholics, Lutheran, Anglican nk. Bakwata ni kikundi cha wajanja wachache wasio na mandate yeyote kwa waislam ndio maana no body is taking them serious.
__________________
Mkulima kala Mbegu......
Reply With Quote
  #10  
Old 2nd July 2009, 09:57 PM
raisi
raisi has no status. Edit
Guest
 
Posts: n/a
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

aaaaaaaahhhhhhhhhhhh big up mufuti
Reply With Quote
Reply

Bookmarks

Tags
aagiza, ccm, mufti, simba, waikatae, waislamu


Currently Active Users Viewing This Thread: 1 (0 members and 1 guests)
 
Thread Tools
Display Modes Rate This Thread
Rate This Thread:

Posting Rules
You may not post new threads
You may not post replies
You may not post attachments
You may not edit your posts

BB code is On
Smilies are On
[IMG] code is On
HTML code is Off
Trackbacks are Off
Pingbacks are Off
Refbacks are On


Similar Threads
Thread Thread Starter Forum Replies Last Post
CCM, CUF wapigana Bubu Ataka Kusema Jukwaa la Siasa 9 19th May 2008 08:53 PM
CCM ya biashara ya utumwa Sokomoko Jukwaa la Siasa 8 12th May 2008 05:34 PM
Butiku ana hoja! Bubu Ataka Kusema Jukwaa la Siasa 152 19th October 2007 06:15 PM

Tuma Ukurasa huu kwa rafiki yako!


All times are GMT +3. The time now is 11:08 PM.

Powered by JamiiForums.com
Copyrights reserved to JamiiForums.com