Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM - Page 5 - JamiiForums |The Home of Great Thinkers

Go Back   JamiiForums |The Home of Great Thinkers > Public Forums > Jukwaa la Siasa


Jukwaa la Siasa Tanzania & World Politics General Discussion Forum. You need to be registered in order to post your comment(s)


Reply
 
LinkBack Thread Tools Rate Thread Display Modes
Old 2nd July 2009, 09:09 PM  
Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM
Keil Keil is offline 2nd July 2009, 09:09 PM

Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Na Ummy Muya

BARAZA Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) limesema kutokana na serikali kutupilia mbali ombi la kunzisha Mahakama ya Kadhi, Waislamu hawataipigia kura CCM katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.

Katika taarifa yake, Bakwata ilifikia hatua ya kusema Waislamu wasimchague Rais Jakaya Kikwete iwapo atasimamishwa na CCM kugombea urais, ikiwa ni pamoja na wabunge na madiwani watakaosimamishwa na chama hicho tawala kutokana na kitendo cha serikali kutupilia mbali hoja ya Mahakama ya Kadhi.

Kauli hiyo imetolewa jana wakati Mufti Issa bin Shaaban Simba alipokuwa akitoa tamko kupinga uamuzi wa serikali kutaka kutumia sheria za dini ya Kiislamu katika mahakama za kawaida badala ya kuanzisha Mahakama ya Kadhi, kitu ambacho alisema anaamini kitawanyima haki Waislamu.

Alisema serikali imedhihirisha kuwa inaendeshwa na Wakristo na si kweli kama serikali haina dini na akamtaka Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe kubatilisha kauli hiyo kwa kuwa inamchafua Rais Jakaya Kikwete mbele ya umma wa Waislamu.

Waziri ametuthibitishia kama Rais Kikwete alikuwa akitulaghai ili tumpigie kura kwa kigezo kuwa suala hilo litashughulikiwa na kupatiwa ufumbuzi na sio kuchanganywa kama ilivyokuwa mwaka 1970 katika Sheria ya Ndoa na kuwanyima haki Waislamu,alisema.

Alisema kwa muda mrefu sana Waislamu wamekuwa kimya wakitumia hekima na busara kudai haki zao, lakini katika hatua hii ambayo serikali imefikia hawapo tayari kuendelea kudhalilishwa na kuwa kitendo hicho ni dhalimu.

Mufti alisema wamekuwa wakiiomba Mahakama ya Kadhi kwa zaidi ya miaka 20 na hivyo hawezi kuendelea kuwa kimya na kupakwa mafuta kwa mgongo wa chupa kwa kuwa mahakama hiyo ni haki yao.

Alisema kauli ya Waziri Chikawe imedhihirisha kuwa serikali ina wenyewe na Waislamu wamewekwa katika tabaka la pili pamoja na Rais Jakaya Kikwete kuwatuliza kwa ahadi kuwa watalipatia ufumbuzi suala hilo.

Natoa wito kwa Masheikh wote nchini na Waislamu wa madhehebu yote kupinga vikali kauli iliyotolewa na Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe na kwamba Waislamu waige mfano wa Waislamu wa Afrika Kusini,alisema Mufti na kuhoji:

Kwa nini iwe Afrika ya Kusini na isiwe Zanzibar, Uganda na Kenya ambazo zipo ndani ya Afrika Mashariki? Kwa niaba ya Waislamu nasema serikali haikututendea haki na imetuchukiza sana,alisema.

Alisema lengo la kuomba mahakama hiyo ni kuhakikisha Waislamu wanashughulikia masuala yao ya ndoa na mirathi na si vinginevyo, hivyo waziri asipotoshe jamii kwa kutumia mifano ambayo haiko sahihi.

Mahakama hii haitawakata wezi mikono kwa kuwa nchi hii ina katiba na sheria na sisi tutazirudisha kesi zote za jinai mikononi mwa serikali. Sifahamu hiyo kamati ambayo waziri alisema alikuwa amekaa na kutoa tamko hilo ilikuwa na watu gani,alihoji.
Aliongeza kuwa kutokana na mapungufu hayo waziri arudi tena na kukutana na masheikh ili apate muongozo wa nini Waislamu wanahitaji na sio kuzungumza bila kuwa na usahihi wa kile anachosema.

Wakizungumza na waandishi wa habari baada ya tamko la Bakwata, masheikh walikuwa na mitazamo tofauti. Sheikh wa mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Salum Mussa alisema wapo baadhi ya Waislamu ambao watakubali kutokana na ufinyu wao wa elimu ya dini.
Mussa alisema haoni sababu ya serikali kufanya njia ya mkato katika suala hilo kwani Waislamu wanahitaji Mahakama ya Kadhi kama ilivyo kwa wafanyabiashara ambao wana mahakama yao.

Hukumu inayotolewa katika Mahakama ya Kadhi ni ibada kwa mujibu wa mafundisho ya Mtume Muhammad (S.A.W) hivyo ni lazima kwa atakayetoa hukumu hiyo awe Muislamu na si vinginevyo,alisema.

Namshanga waziri anapotaka sheria hizi zitumiwe katika mahakama za kawaida. Aliona wapi John akawa imamu,alihoji sheikh huyo wa mkoa wa Dar es Salaam.

Naye katibu wa Bakwata wilayani Ilala, Sheikh Issa Ausi alisema historia iko wazi. Waasisi na wanaharakati ambao waliitoa Tanganyika mikononi mwa wakoloni walikuwa Waislamu, na akahoji sababu za serikali kuwa mstari wa mbele kuwafunga midomo leo.
Bakwata imezinduka sasa Waislamu wote tumeungana katika kupigania haki zetu na kutetea maslahi yetu na serikali itambue kuwa Bakwata iko hai hao Wakristo walikuwa wapi wakati sisi tukipigania uhuru,alihoji.

Wakati huohuo, Sheikh Salum Rwambo alisema anawashangaa wabunge Waislamu ambao baadhi ni mahajat na malhaj wanakaa kimya na kushindwa kutetea hoja za msingi na kudai kuwa huo sasa ndio mwisho wao wa kuwaita masheikh na kutaka waombewe dua ili wasipate wepesi katika kampeni zao.

Sheikh Rwambo pia alimsifia mbunge wa Nzega Lucas Selelii kwamba ni miongoni mwa wabunge katika Bunge hilo wanaozungumza ukweli na kwa kujiamini tofauti na wengine ambao wanaenda kukaa bila kufanya kazi zilizowapeleka.


Source: Mwananchi


CCM watajuta kuweka swala la Mahakama ya Kadhi kwenye Ilani yao uchaguzi ya 2005.

Keil
JF Senior Expert Member
Points: 628,831, Level: 100 Points: 628,831, Level: 100 Points: 628,831, Level: 100
Activity: 4% Activity: 4% Activity: 4%
Join Date: Mon Jul 2007
Posts: 1,385
Thanks: 91
Thanked 300 Times in 133 Posts
Views: 5449
Reply With Quote
  #41  
Old 3rd July 2009, 08:22 AM
Kingwele Kingwele is offline
Kingwele has no status.
Senior Member
Points: 96,277, Level: 100 Points: 96,277, Level: 100 Points: 96,277, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Fri Aug 2006
Posts: 98
Thanks: 0
Thanked 4 Times in 2 Posts
Rep Power: 24
Kingwele will become famous soon enoughKingwele will become famous soon enoughKingwele will become famous soon enoughKingwele will become famous soon enoughKingwele will become famous soon enoughKingwele will become famous soon enoughKingwele will become famous soon enoughKingwele will become famous soon enough
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Quote:
View Post
Bakwata hawana ubavu huo wanabwaka tu, wao wenyewe credibility yao ni questionable wasafishe nyumba yao kwanza.

Hawana jipya zaidi ya kutafuta njia ya kutokea na kuficha madudu yao. Ni ukweli usio na shaka uislam haupo kitaasisi kama ukristo na madhehebu yake catholics, Lutheran, Anglican nk. Bakwata ni kikundi cha wajanja wachache wasio na mandate yeyote kwa waislam ndio maana no body is taking them serious.

Masatu.. nakuunga mkono 100% kuhusu credibility ya BAKWATA kwenye safu za waislamu.

Ila ni ukweli usiopingika kuwa at least kwa hili they have said some thing.... yaani kwa maneno mengine ile kauli ya enough is enough wameithibitisha. Nadhani tuwapongeze.

Unajuwa sikutegemea kusikia kauli hii kutoka BAKWATA. Maana hawakuwa na kuumauma maneno..they went very straight to the pint na kuita nyeupe ni white.

Takbiir.
Reply With Quote
  #42  
Old 3rd July 2009, 08:32 AM
De Novo's Avatar
De Novo De Novo is offline
De Novo !
JF Premium Member
Points: 270,159, Level: 100 Points: 270,159, Level: 100 Points: 270,159, Level: 100
Activity: 54% Activity: 54% Activity: 54%
 
Join Date: Sat Apr 2008
Location: Dar - Tz
Posts: 4,175
Thanks: 1,343
Thanked 1,363 Times in 829 Posts
Rep Power: 30
De Novo will become famous soon enoughDe Novo will become famous soon enoughDe Novo will become famous soon enoughDe Novo will become famous soon enoughDe Novo will become famous soon enoughDe Novo will become famous soon enoughDe Novo will become famous soon enoughDe Novo will become famous soon enough
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Wajameni.... Sintojiingiza kwenye uchambuzi wa kidini, siwezi na sina upeo

Swali ni moja tu, JE WASIPOWAPA CCM WATAWAPA NANI WENGINE? CUF? CHADEMA? TADEA?

...i think its just a move to score some points kwa waumini wake now that anajongelea upinzani wa kiti chake
__________________
I am on the move...
Reply With Quote
  #43  
Old 3rd July 2009, 08:49 AM
Mwiba's Avatar
Mwiba Mwiba is offline
Mwiba has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 902,192, Level: 100 Points: 902,192, Level: 100 Points: 902,192, Level: 100
Activity: 1% Activity: 1% Activity: 1%
 
Join Date: Tue Oct 2007
Posts: 2,984
Thanks: 0
Thanked 13 Times in 8 Posts
Rep Power: 69
Mwiba is a jewel in the roughMwiba is a jewel in the roughMwiba is a jewel in the roughMwiba is a jewel in the roughMwiba is a jewel in the roughMwiba is a jewel in the roughMwiba is a jewel in the roughMwiba is a jewel in the roughMwiba is a jewel in the roughMwiba is a jewel in the roughMwiba is a jewel in the rough
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Kwa ufupi CCM inaendelea kushikwa pabaya maana kila wanapojaribu kuziba kunatoboka na kuvuja kwengine.
Inaelekea wanapoteza wapiga kura kwenye mambo yahusuyo Muungano,Ufisadi na sasa waiislamu wenye siasa kali bado wakiristu wenye siasa kali naona wao bado wanajikurubisha kwa kila hali ,wakiristu amkeni wacheni kuikumbatia CCM ,vyama mbadala vimejaa tele ahadi za CCM zitawatoa vibega.
__________________
Light travels faster than sound. This is why some people appear bright until you hear them speak.
Reply With Quote
  #44  
Old 3rd July 2009, 08:58 AM
Lole Gwakisa's Avatar
Lole Gwakisa Lole Gwakisa is offline
Lole Gwakisa has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 224,685, Level: 100 Points: 224,685, Level: 100 Points: 224,685, Level: 100
Activity: 4% Activity: 4% Activity: 4%
 
Join Date: Wed Nov 2008
Posts: 1,179
Thanks: 289
Thanked 275 Times in 138 Posts
Rep Power: 24
Lole Gwakisa will become famous soon enoughLole Gwakisa will become famous soon enoughLole Gwakisa will become famous soon enoughLole Gwakisa will become famous soon enoughLole Gwakisa will become famous soon enoughLole Gwakisa will become famous soon enoughLole Gwakisa will become famous soon enoughLole Gwakisa will become famous soon enough
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Quote:
View Post
Mbona Dawa Ndogo Sana kwa hili jambo!

Wape mahakama yao, 60% ya waislamu Tanzania watabadilisha dini.
He he he! kwa nini mkuu wanaogopa kukatwa viganja?
Reply With Quote
  #45  
Old 3rd July 2009, 08:58 AM
7ceven 7ceven is offline
7ceven Mkulima
Member
Points: 69,912, Level: 100 Points: 69,912, Level: 100 Points: 69,912, Level: 100
Activity: 2% Activity: 2% Activity: 2%
 
Join Date: Wed Feb 2008
Posts: 38
Thanks: 0
Thanked 0 Times in 0 Posts
Rep Power: 0
7ceven will become famous soon enough7ceven will become famous soon enough7ceven will become famous soon enough7ceven will become famous soon enough7ceven will become famous soon enough7ceven will become famous soon enough7ceven will become famous soon enough7ceven will become famous soon enough
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Na wasiislaam wasiokuwemo Bakwata, kama Answari Sunaah, (Mtaniwia radhi kama nimekosea spelling) nao itabidi waanzishe mahakama ya kadhi yao na ilipiwe na serikali hihi hihi bila kuleta vumbi?
Reply With Quote
  #46  
Old 3rd July 2009, 08:59 AM
Nungunungu's Avatar
Nungunungu Nungunungu is offline
Nungunungu has no status.
Senior Member
Points: 91,422, Level: 100 Points: 91,422, Level: 100 Points: 91,422, Level: 100
Activity: 1% Activity: 1% Activity: 1%
 
Join Date: Tue Feb 2007
Posts: 182
Thanks: 0
Thanked 1 Time in 1 Post
Rep Power: 24
Nungunungu will become famous soon enoughNungunungu will become famous soon enoughNungunungu will become famous soon enoughNungunungu will become famous soon enoughNungunungu will become famous soon enoughNungunungu will become famous soon enoughNungunungu will become famous soon enoughNungunungu will become famous soon enough
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Quote:
View Post
Bakwata hawana ubavu huo wanabwaka tu, wao wenyewe credibility yao ni questionable wasafishe nyumba yao kwanza.

Hawana jipya zaidi ya kutafuta njia ya kutokea na kuficha madudu yao. Ni ukweli usio na shaka uislam haupo kitaasisi kama ukristo na madhehebu yake catholics, Lutheran, Anglican nk. Bakwata ni kikundi cha wajanja wachache wasio na mandate yeyote kwa waislam ndio maana no body is taking them serious.
Masatu,

Nakubaliana na uliyoyaeleza isipokuwa niliyo bold. Tatizo la Waislam Tz ni dogo. Serikali haijawaruhusu wajipange waweke viongozi wenye muono kwenye hiyo Bakwata. Na hilo waislam wanaweza kulifanya kama hawataingiliwa katika mambo yao na Serikali. Hakuna uchaguzi mkuu wa Bakwata utafanyika bila kuingiliwa na serikali. Hata TEC au CCT zikiweka na bogus leaders hakuna cha maana wanachoweza kufanya.

Bahati mbaya ni kuwa serikali inafurahi kuwa na dudu bovu kama Bakwata kisha inalipa nguvu nyingi. Na hapo ndipo watu wanapata fursa ya kuwatukana Waislam.

Waislam wanaweza. Mfano mdogo ambao wewe unaufahamu, tazama tofauti ya shule za Bakwata na zilizoanzishwa na vitaasisi vidogo tu vya Kiislam tena karibuni. Waislam wasipoingiliwa katika masuala yao wanaweza kufanya zaidi ya hapo.
Reply With Quote
  #47  
Old 3rd July 2009, 09:03 AM
Lole Gwakisa's Avatar
Lole Gwakisa Lole Gwakisa is offline
Lole Gwakisa has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 224,685, Level: 100 Points: 224,685, Level: 100 Points: 224,685, Level: 100
Activity: 4% Activity: 4% Activity: 4%
 
Join Date: Wed Nov 2008
Posts: 1,179
Thanks: 289
Thanked 275 Times in 138 Posts
Rep Power: 24
Lole Gwakisa will become famous soon enoughLole Gwakisa will become famous soon enoughLole Gwakisa will become famous soon enoughLole Gwakisa will become famous soon enoughLole Gwakisa will become famous soon enoughLole Gwakisa will become famous soon enoughLole Gwakisa will become famous soon enoughLole Gwakisa will become famous soon enough
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Kukosekana kwa "KICHWA" Sheikh Gorogosi kumeanza kuonekana mapema.
Reply With Quote
  #48  
Old 3rd July 2009, 09:03 AM
Bill Bill is offline
Bill says: Kukumbatia ufisadi pia ni ufisadi
JF Senior Expert Member
Points: 196,431, Level: 100 Points: 196,431, Level: 100 Points: 196,431, Level: 100
Activity: 2% Activity: 2% Activity: 2%
 
Join Date: Fri Oct 2007
Posts: 626
Thanks: 32
Thanked 30 Times in 19 Posts
Rep Power: 24
Bill will become famous soon enoughBill will become famous soon enoughBill will become famous soon enoughBill will become famous soon enoughBill will become famous soon enoughBill will become famous soon enoughBill will become famous soon enoughBill will become famous soon enough
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Quote:
View Post
Mambo yote mengine ambayo sisi tunayapigia kelele hayawafanyi wao kuichukia CCM; yaani yote yaliyofanyika dhidi ya nchi yetu na utajiri wetu wao hayawagusi wala kuwataka waumini wao kuyafanya ya kisiasa na kuiadhibu CCM; yaani yote hayo hayajafikia kiwango cha kuwakera.. isipokuwa hili moja tu?
Nachelea kusema huu ni ubinafsi, kwani hii nchi imeraluliwa na hawa manyang'au wa CCM. Sasa kusema wanakataa CCM kwa sababu tu ya kukatiliwa kwa mahakama ya kadhi ambayo ni sehemu yao ya ibada haingii akili na naweza kusema ni uamuzi wa kukurupuka.

Naikataa CCM kwa sababu kuu, imeifilisi nchi hii na hakuna matumaini kwa waTZ.
Reply With Quote
  #49  
Old 3rd July 2009, 09:08 AM
Omulangi Omulangi is offline
Omulangi has no status.
Senior Member
Points: 81,219, Level: 100 Points: 81,219, Level: 100 Points: 81,219, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Tue Feb 2008
Posts: 50
Thanks: 0
Thanked 5 Times in 2 Posts
Rep Power: 23
Omulangi will become famous soon enoughOmulangi will become famous soon enoughOmulangi will become famous soon enoughOmulangi will become famous soon enoughOmulangi will become famous soon enoughOmulangi will become famous soon enoughOmulangi will become famous soon enoughOmulangi will become famous soon enough
Smile Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Mi nafikiri tuaiche Tz kama secular nation. Tusiingize halafu ya kidini ili kuwe na fair play kwa dini na imani zote. Wahubiriane misikitini na makanisani na watu wawe converted kwa kutafuta pepo na si maslahi ya kiuchumi, vyeo serkalini n.k
Reply With Quote
  #50  
Old 3rd July 2009, 09:11 AM
Msavila Msavila is offline
Msavila has no status.
Senior Member
Points: 82,180, Level: 100 Points: 82,180, Level: 100 Points: 82,180, Level: 100
Activity: 1% Activity: 1% Activity: 1%
 
Join Date: Wed Jul 2007
Posts: 135
Thanks: 5
Thanked 2 Times in 1 Post
Rep Power: 23
Msavila will become famous soon enoughMsavila will become famous soon enoughMsavila will become famous soon enoughMsavila will become famous soon enoughMsavila will become famous soon enoughMsavila will become famous soon enoughMsavila will become famous soon enoughMsavila will become famous soon enough
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Quote:
View Post
There are two things in our job. Criticism i accept with respect. Disrespect i dont accept and dont respect" - Arsene Wenger.
Let us discuss the issue with clear mind. As far as I am concerned there is nothing wrong with having " mahakama ya Kadhi". The sticking point is to make it a constitutional affair. Its establishment does not need a government hand, it should be internally handled by the Muslim community itself. We all know the legality and acceptability of BAKWATA, an institution established with a government hand, among the Muslim community is not at 100% with alot of discenting voices. Some going as far as calling it a govern;ent tool used to deter development of the concerned community. The isue was a non starter in the parliament. Here again we see how politician can exploit and distabilise a country by giving false or hard to implement promises, just to have your vote.

Muslims, if they will heed to the call, they will be doing all of us a favor to vote CCM out,but will they still have the Kadhi demand?
Reply With Quote
Reply

Bookmarks

Tags
aagiza, ccm, mufti, simba, waikatae, waislamu


Currently Active Users Viewing This Thread: 1 (0 members and 1 guests)
 
Thread Tools
Display Modes Rate This Thread
Rate This Thread:

Posting Rules
You may not post new threads
You may not post replies
You may not post attachments
You may not edit your posts

BB code is On
Smilies are On
[IMG] code is On
HTML code is Off
Trackbacks are Off
Pingbacks are Off
Refbacks are On


Similar Threads
Thread Thread Starter Forum Replies Last Post
CCM, CUF wapigana Bubu Ataka Kusema Jukwaa la Siasa 9 19th May 2008 08:53 PM
CCM ya biashara ya utumwa Sokomoko Jukwaa la Siasa 8 12th May 2008 05:34 PM
Butiku ana hoja! Bubu Ataka Kusema Jukwaa la Siasa 152 19th October 2007 06:15 PM

Tuma Ukurasa huu kwa rafiki yako!


All times are GMT +3. The time now is 03:03 PM.

Powered by JamiiForums.com
Copyrights reserved to JamiiForums.com