Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM - Page 4 - JamiiForums |The Home of Great Thinkers

Go Back   JamiiForums |The Home of Great Thinkers > Public Forums > Jukwaa la Siasa


Jukwaa la Siasa Tanzania & World Politics General Discussion Forum. You need to be registered in order to post your comment(s)


Reply
 
LinkBack Thread Tools Rate Thread Display Modes
Old 2nd July 2009, 09:09 PM  
Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM
Keil Keil is offline 2nd July 2009, 09:09 PM

Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Na Ummy Muya

BARAZA Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) limesema kutokana na serikali kutupilia mbali ombi la kunzisha Mahakama ya Kadhi, Waislamu hawataipigia kura CCM katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.

Katika taarifa yake, Bakwata ilifikia hatua ya kusema Waislamu wasimchague Rais Jakaya Kikwete iwapo atasimamishwa na CCM kugombea urais, ikiwa ni pamoja na wabunge na madiwani watakaosimamishwa na chama hicho tawala kutokana na kitendo cha serikali kutupilia mbali hoja ya Mahakama ya Kadhi.

Kauli hiyo imetolewa jana wakati Mufti Issa bin Shaaban Simba alipokuwa akitoa tamko kupinga uamuzi wa serikali kutaka kutumia sheria za dini ya Kiislamu katika mahakama za kawaida badala ya kuanzisha Mahakama ya Kadhi, kitu ambacho alisema anaamini kitawanyima haki Waislamu.

Alisema serikali imedhihirisha kuwa inaendeshwa na Wakristo na si kweli kama serikali haina dini na akamtaka Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe kubatilisha kauli hiyo kwa kuwa inamchafua Rais Jakaya Kikwete mbele ya umma wa Waislamu.

Waziri ametuthibitishia kama Rais Kikwete alikuwa akitulaghai ili tumpigie kura kwa kigezo kuwa suala hilo litashughulikiwa na kupatiwa ufumbuzi na sio kuchanganywa kama ilivyokuwa mwaka 1970 katika Sheria ya Ndoa na kuwanyima haki Waislamu,alisema.

Alisema kwa muda mrefu sana Waislamu wamekuwa kimya wakitumia hekima na busara kudai haki zao, lakini katika hatua hii ambayo serikali imefikia hawapo tayari kuendelea kudhalilishwa na kuwa kitendo hicho ni dhalimu.

Mufti alisema wamekuwa wakiiomba Mahakama ya Kadhi kwa zaidi ya miaka 20 na hivyo hawezi kuendelea kuwa kimya na kupakwa mafuta kwa mgongo wa chupa kwa kuwa mahakama hiyo ni haki yao.

Alisema kauli ya Waziri Chikawe imedhihirisha kuwa serikali ina wenyewe na Waislamu wamewekwa katika tabaka la pili pamoja na Rais Jakaya Kikwete kuwatuliza kwa ahadi kuwa watalipatia ufumbuzi suala hilo.

Natoa wito kwa Masheikh wote nchini na Waislamu wa madhehebu yote kupinga vikali kauli iliyotolewa na Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe na kwamba Waislamu waige mfano wa Waislamu wa Afrika Kusini,alisema Mufti na kuhoji:

Kwa nini iwe Afrika ya Kusini na isiwe Zanzibar, Uganda na Kenya ambazo zipo ndani ya Afrika Mashariki? Kwa niaba ya Waislamu nasema serikali haikututendea haki na imetuchukiza sana,alisema.

Alisema lengo la kuomba mahakama hiyo ni kuhakikisha Waislamu wanashughulikia masuala yao ya ndoa na mirathi na si vinginevyo, hivyo waziri asipotoshe jamii kwa kutumia mifano ambayo haiko sahihi.

Mahakama hii haitawakata wezi mikono kwa kuwa nchi hii ina katiba na sheria na sisi tutazirudisha kesi zote za jinai mikononi mwa serikali. Sifahamu hiyo kamati ambayo waziri alisema alikuwa amekaa na kutoa tamko hilo ilikuwa na watu gani,alihoji.
Aliongeza kuwa kutokana na mapungufu hayo waziri arudi tena na kukutana na masheikh ili apate muongozo wa nini Waislamu wanahitaji na sio kuzungumza bila kuwa na usahihi wa kile anachosema.

Wakizungumza na waandishi wa habari baada ya tamko la Bakwata, masheikh walikuwa na mitazamo tofauti. Sheikh wa mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Salum Mussa alisema wapo baadhi ya Waislamu ambao watakubali kutokana na ufinyu wao wa elimu ya dini.
Mussa alisema haoni sababu ya serikali kufanya njia ya mkato katika suala hilo kwani Waislamu wanahitaji Mahakama ya Kadhi kama ilivyo kwa wafanyabiashara ambao wana mahakama yao.

Hukumu inayotolewa katika Mahakama ya Kadhi ni ibada kwa mujibu wa mafundisho ya Mtume Muhammad (S.A.W) hivyo ni lazima kwa atakayetoa hukumu hiyo awe Muislamu na si vinginevyo,alisema.

Namshanga waziri anapotaka sheria hizi zitumiwe katika mahakama za kawaida. Aliona wapi John akawa imamu,alihoji sheikh huyo wa mkoa wa Dar es Salaam.

Naye katibu wa Bakwata wilayani Ilala, Sheikh Issa Ausi alisema historia iko wazi. Waasisi na wanaharakati ambao waliitoa Tanganyika mikononi mwa wakoloni walikuwa Waislamu, na akahoji sababu za serikali kuwa mstari wa mbele kuwafunga midomo leo.
Bakwata imezinduka sasa Waislamu wote tumeungana katika kupigania haki zetu na kutetea maslahi yetu na serikali itambue kuwa Bakwata iko hai hao Wakristo walikuwa wapi wakati sisi tukipigania uhuru,alihoji.

Wakati huohuo, Sheikh Salum Rwambo alisema anawashangaa wabunge Waislamu ambao baadhi ni mahajat na malhaj wanakaa kimya na kushindwa kutetea hoja za msingi na kudai kuwa huo sasa ndio mwisho wao wa kuwaita masheikh na kutaka waombewe dua ili wasipate wepesi katika kampeni zao.

Sheikh Rwambo pia alimsifia mbunge wa Nzega Lucas Selelii kwamba ni miongoni mwa wabunge katika Bunge hilo wanaozungumza ukweli na kwa kujiamini tofauti na wengine ambao wanaenda kukaa bila kufanya kazi zilizowapeleka.


Source: Mwananchi


CCM watajuta kuweka swala la Mahakama ya Kadhi kwenye Ilani yao uchaguzi ya 2005.

Keil
JF Senior Expert Member
Points: 630,431, Level: 100 Points: 630,431, Level: 100 Points: 630,431, Level: 100
Activity: 3% Activity: 3% Activity: 3%
Join Date: Mon Jul 2007
Posts: 1,387
Thanks: 93
Thanked 308 Times in 135 Posts
Views: 5455
Reply With Quote
  #31  
Old 3rd July 2009, 03:12 AM
Mkandara Mkandara is offline
Mkandara Aviator
JF Premium Member
Points: 580,378, Level: 100 Points: 580,378, Level: 100 Points: 580,378, Level: 100
Activity: 2% Activity: 2% Activity: 2%
 
Join Date: Thu Mar 2006
Location: T dot
Posts: 7,288
Thanks: 460
Thanked 737 Times in 324 Posts
Rep Power: 80
Mkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the rough
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Quote:
View Post
asante sana mkuu na hayo ndio maajabu ya viongozi wa dini zetu.sasa inamaana ccm wakirekkebisha hilo tu wapewe kura? swala dogo sana hilo kwa ccm kwa kuataka kura.kama wanaweza kutoa rushwa kupata kura watashindwa kuwapa pendekezo lao hili wapate kura?
There are two things in our job. Criticism i accept with respect. Disrespect i dont accept and dont respect" - Arsene Wenger.
__________________
Exploration of reality
Reply With Quote
  #32  
Old 3rd July 2009, 03:41 AM
Bongolander Bongolander is offline
Bongolander has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 266,138, Level: 100 Points: 266,138, Level: 100 Points: 266,138, Level: 100
Activity: 14% Activity: 14% Activity: 14%
 
Join Date: Tue Jul 2007
Location: Tandale
Posts: 2,281
Thanks: 9
Thanked 195 Times in 103 Posts
Rep Power: 27
Bongolander will become famous soon enoughBongolander will become famous soon enoughBongolander will become famous soon enoughBongolander will become famous soon enoughBongolander will become famous soon enoughBongolander will become famous soon enoughBongolander will become famous soon enoughBongolander will become famous soon enough
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Sijui kama ni sahihi kabisa kusema CCM nadio ina makosa, kuna watu ndani ya CCM ndio tatizo, japokuwa wanaiwakilisha CCM, kuna uwezekano wa kuwaondoa hao wabovu mafisadi na walaghai, na chama kikaendelea vizuri kabisa. Lakini at least hata watu wa dini wameanza kufahamu ukweli wa mambo!!
Reply With Quote
  #33  
Old 3rd July 2009, 06:44 AM
kinepi_nepi's Avatar
kinepi_nepi kinepi_nepi is offline
kinepi_nepi fighting for justice
JF Senior Expert Member
Points: 348,712, Level: 100 Points: 348,712, Level: 100 Points: 348,712, Level: 100
Activity: 1% Activity: 1% Activity: 1%
 
Join Date: Thu Aug 2007
Posts: 507
Thanks: 0
Thanked 4 Times in 3 Posts
Rep Power: 24
kinepi_nepi will become famous soon enoughkinepi_nepi will become famous soon enoughkinepi_nepi will become famous soon enoughkinepi_nepi will become famous soon enoughkinepi_nepi will become famous soon enoughkinepi_nepi will become famous soon enoughkinepi_nepi will become famous soon enoughkinepi_nepi will become famous soon enough
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Quote:
View Post
Ngoma ndio inaanza kupigwa anayeweza aingie na acheze...suala hilo zito sana sana waangalie lisije likaleta machafuko na mpasuko...haya amani yetu tu tusije kuipoteza
Tanzania haijawahi kuwa na amani, bali utii wa woga.
__________________
Tanzania itakuwa huru wananchi wakimiliki nchi yao wenyewe sio baadhi ya wateule wachache.Haki na sheria kwa wote bila kujali rangi,cheo,na utajiri wa mtu.
Reply With Quote
  #34  
Old 3rd July 2009, 07:02 AM
BinMgen's Avatar
BinMgen BinMgen is offline
BinMgen has no status.
Senior Member
Points: 75,562, Level: 100 Points: 75,562, Level: 100 Points: 75,562, Level: 100
Activity: 2% Activity: 2% Activity: 2%
 
Join Date: Wed Jun 2008
Posts: 210
Thanks: 7
Thanked 17 Times in 12 Posts
Rep Power: 22
BinMgen will become famous soon enoughBinMgen will become famous soon enoughBinMgen will become famous soon enoughBinMgen will become famous soon enoughBinMgen will become famous soon enoughBinMgen will become famous soon enoughBinMgen will become famous soon enoughBinMgen will become famous soon enough
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Quote:
View Post
Mambo yote mengine ambayo sisi tunayapigia kelele hayawafanyi wao kuichukia CCM; yaani yote yaliyofanyika dhidi ya nchi yetu na utajiri wetu wao hayawagusi wala kuwataka waumini wao kuyafanya ya kisiasa na kuiadhibu CCM; yaani yote hayo hayajafikia kiwango cha kuwakera.. isipokuwa hili moja tu?
.
NDIO!

Mufti hakuna kurudi nyuma!
__________________
Maisha Matamu Lakini Mafupi
Reply With Quote
  #35  
Old 3rd July 2009, 07:15 AM
BinMgen's Avatar
BinMgen BinMgen is offline
BinMgen has no status.
Senior Member
Points: 75,562, Level: 100 Points: 75,562, Level: 100 Points: 75,562, Level: 100
Activity: 2% Activity: 2% Activity: 2%
 
Join Date: Wed Jun 2008
Posts: 210
Thanks: 7
Thanked 17 Times in 12 Posts
Rep Power: 22
BinMgen will become famous soon enoughBinMgen will become famous soon enoughBinMgen will become famous soon enoughBinMgen will become famous soon enoughBinMgen will become famous soon enoughBinMgen will become famous soon enoughBinMgen will become famous soon enoughBinMgen will become famous soon enough
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Quote:
View Post
Tangu lini maamuzi ya kesi mahakamani yakawa ni ibada?? Hii kali wakuu!!
.
Tatizo lako unazani ibada ni kuimba na kuchezangoma tu!.
.
ibada ni kutekeleza maamrisho na kuacha makatazo
__________________
Maisha Matamu Lakini Mafupi
Reply With Quote
  #36  
Old 3rd July 2009, 07:29 AM
BinMgen's Avatar
BinMgen BinMgen is offline
BinMgen has no status.
Senior Member
Points: 75,562, Level: 100 Points: 75,562, Level: 100 Points: 75,562, Level: 100
Activity: 2% Activity: 2% Activity: 2%
 
Join Date: Wed Jun 2008
Posts: 210
Thanks: 7
Thanked 17 Times in 12 Posts
Rep Power: 22
BinMgen will become famous soon enoughBinMgen will become famous soon enoughBinMgen will become famous soon enoughBinMgen will become famous soon enoughBinMgen will become famous soon enoughBinMgen will become famous soon enoughBinMgen will become famous soon enoughBinMgen will become famous soon enough
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Quote:
View Post
Ngoma ndio inaanza kupigwa anayeweza aingie na acheze...suala hilo zito sana sana waangalie lisije likaleta machafuko na mpasuko...haya amani yetu tu tusije kuipoteza
.
Kama noma naiwe noma potelea mbali na ivunjike amani.
.
MUFTI UKO SAWA
.
Katika hili umewaunganisha waislam. Hii ndio bakwata
Inayo hitajiwa na waislam.
__________________
Maisha Matamu Lakini Mafupi

Last edited by BinMgen; 3rd July 2009 at 08:15 AM..
Reply With Quote
  #37  
Old 3rd July 2009, 07:42 AM
kinepi_nepi's Avatar
kinepi_nepi kinepi_nepi is offline
kinepi_nepi fighting for justice
JF Senior Expert Member
Points: 348,712, Level: 100 Points: 348,712, Level: 100 Points: 348,712, Level: 100
Activity: 1% Activity: 1% Activity: 1%
 
Join Date: Thu Aug 2007
Posts: 507
Thanks: 0
Thanked 4 Times in 3 Posts
Rep Power: 24
kinepi_nepi will become famous soon enoughkinepi_nepi will become famous soon enoughkinepi_nepi will become famous soon enoughkinepi_nepi will become famous soon enoughkinepi_nepi will become famous soon enoughkinepi_nepi will become famous soon enoughkinepi_nepi will become famous soon enoughkinepi_nepi will become famous soon enough
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Waisilamu wanahaki ya kupiga kelele kwani ni kweli kwenye ilani ya CCM walisema Mahakama ya kadhi itakuwepo, ila CCM imewapiga mchanga wa macho.

Ila kuna kunahaja shekh mkuu akaangalia ni ahadi ngapi watanzania tupewa changa la macho, maisha bora, utawala wa sheria, je ni waisilamu wangapi wako mahabusu miaka nenda rudi bila kesi zao kusikilizwa.
Je ni waisilamu wangapi wanakufa kwa kukosa huduma za afya.
je ni waisilamu wangapi wapo shule na hakuna elimu bora.
Je ni waisilamu wangapi wanakufa kwa madawa ya kulevya yanayouzwa na vigogo.

Je ni waisilamu wangapi wameathirika na wizi wa EPA, Richmond< Meremeta deepGreen nk.
Haya yote na mengine mengi ndio nilitegemea shekh mkuu angeyafanya kama sababu za kutoichagua CCM.

Wakishindwa kuwa wa kweli kwa wanayoyaahidi hawawezi kutimiza wanayowapaka nayo mafuta, CCM imegundua ina deal na mandondocha hivyo hawajali kesho Kikwete atakuja msikitini atawashika mkono kesho yake wote mnabadili kauli na kuonekana mtu mzima......
Kama kweli basi kidedea mpaka kieleweke tena kwa yote mpaka Rostam aende keko kama Juma na Omari.
__________________
Tanzania itakuwa huru wananchi wakimiliki nchi yao wenyewe sio baadhi ya wateule wachache.Haki na sheria kwa wote bila kujali rangi,cheo,na utajiri wa mtu.
Reply With Quote
  #38  
Old 3rd July 2009, 07:44 AM
Augustine Moshi Augustine Moshi is offline
Augustine Moshi has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 548,651, Level: 100 Points: 548,651, Level: 100 Points: 548,651, Level: 100
Activity: 2% Activity: 2% Activity: 2%
 
Join Date: Sat Apr 2006
Posts: 1,144
Thanks: 27
Thanked 74 Times in 35 Posts
Rep Power: 107
Augustine Moshi is a glorious beacon of lightAugustine Moshi is a glorious beacon of lightAugustine Moshi is a glorious beacon of lightAugustine Moshi is a glorious beacon of lightAugustine Moshi is a glorious beacon of lightAugustine Moshi is a glorious beacon of lightAugustine Moshi is a glorious beacon of lightAugustine Moshi is a glorious beacon of lightAugustine Moshi is a glorious beacon of lightAugustine Moshi is a glorious beacon of lightAugustine Moshi is a glorious beacon of light
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Mkandara anasema tumjibu Mufti kwa hoja. Zilizotolewa umeona ni vioja? Haya angalia hizi:
  • Mufti anadai Sheria ya Ndoa ya 1970 imewanyima Waislamu haki. Hakuweza kueleza kwani hakielezeki. Si kweli. Na kama ingekuwa kweli basi angesema kipengele husika ni kipi ili kiangaliwe.
  • Mufti kasema Waislamu wanataka mahakama ya kushughulikia mirathi na ndoa. Nani kawanyima kuanzisha? Si lazima iwe sehemu ya serikali.
  • Mufti kasema Waislamu wanapashwa kuwa na mahakama yao kama wafanyabiashara walivyo na mahakama yao. Yaani anataka kusema Waislamu ni kikundi tu kama kilivyo kikundi cha wafanyabiashara? Anawakosea haki Waislamu.
Reply With Quote
  #39  
Old 3rd July 2009, 07:56 AM
Bobby Bobby is offline
Bobby has no status.
Senior Member
Points: 103,458, Level: 100 Points: 103,458, Level: 100 Points: 103,458, Level: 100
Activity: 3% Activity: 3% Activity: 3%
 
Join Date: Thu Jan 2008
Posts: 244
Thanks: 44
Thanked 16 Times in 8 Posts
Rep Power: 23
Bobby will become famous soon enoughBobby will become famous soon enoughBobby will become famous soon enoughBobby will become famous soon enoughBobby will become famous soon enoughBobby will become famous soon enoughBobby will become famous soon enoughBobby will become famous soon enough
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Quote:
View Post
Tatizo si kuwa na mahakama tatizo ni kudhalilishwa na kuonewa waislamu. Mzee Mwanakijiji kuhusu alleged grand corruption cases ni still allegation hakuna substance wala proof katika hilo bali ni accusations tu.
Mdondoaji ni kipi hicho unachodondoa jamani mbona ulichoandika kimekaa kaa vibaya hivyo? YAANI UNASEMA ISSUES ZA EPA, RICHMOND, MEREMETA, TANGOLD, DEEP GREEN NA ZINGINE HAZINA PROOF? Did you mean what you wrote au keyboard ilikosa ushirikiano? Kama you meant what you wrote then you have to think twice kwani you could be in a wrong forum I suppose.
Reply With Quote
  #40  
Old 3rd July 2009, 08:06 AM
African African is offline
African has no status.
Member
Points: 63,112, Level: 100 Points: 63,112, Level: 100 Points: 63,112, Level: 100
Activity: 2% Activity: 2% Activity: 2%
 
Join Date: Wed Oct 2008
Posts: 26
Thanks: 0
Thanked 6 Times in 5 Posts
Rep Power: 0
African will become famous soon enoughAfrican will become famous soon enoughAfrican will become famous soon enoughAfrican will become famous soon enoughAfrican will become famous soon enoughAfrican will become famous soon enoughAfrican will become famous soon enoughAfrican will become famous soon enough
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Hoja ya msingi ni kwamba Waislamu wamekosa demokrasia ndani ya taasisi zao kwa kile tunaita kimombo co-option of few islamic leaders by Government.Taasisi za kikristu kama vile Tanzania Episcopol Council na nyinginezo huwa haziingiliwi na serikali, lakini inapokuja swala zima la uchaguzi ndani ya taasisi za kiislam, serikali ina ingilia(influence) na ndio maana Wapo wanao mkubal sheikh Mkuu na wasiomkubali ndani ya sheikh mkuu. Kwa hiyo hoja ya msingi nikuangalia demokrasia ndani ya taasis za kiislam. Kwa mfano ndani ya kanisa la lutherani (KKT) kumekuwa kunafukuta sehemu mbali mbali kama vile upareni, meru n.k, sababu kubwa utafiti ulibainisha kuwa ni mgawanyo wa rasilimali. Fukuto kubwa ndani ya uisilamu husababishwa na ukosefu wa demokrasia ndani ya taasisi hizo because for some reasons the government does not want the muslims to collectivelly pick the leadership they want. Kwa hiyo hili swala ni lazima litizamwe upya ili lipatiwe ufumbuzi. Wakati civil war inaanza watu huwa hawatangazi ila ilalipuka tu. utasikia tu , fujo mwembe chai, fujo za kkt upareni, vijana wakiislamu wakizuia wazee kuingia misikitini, wakulima wakichinjana na wafugaji, chuo kikuu hakukaliki n.k.
Reply With Quote
Reply

Bookmarks

Tags
aagiza, ccm, mufti, simba, waikatae, waislamu


Currently Active Users Viewing This Thread: 1 (0 members and 1 guests)
 
Thread Tools
Display Modes Rate This Thread
Rate This Thread:

Posting Rules
You may not post new threads
You may not post replies
You may not post attachments
You may not edit your posts

BB code is On
Smilies are On
[IMG] code is On
HTML code is Off
Trackbacks are Off
Pingbacks are Off
Refbacks are On


Similar Threads
Thread Thread Starter Forum Replies Last Post
CCM, CUF wapigana Bubu Ataka Kusema Jukwaa la Siasa 9 19th May 2008 08:53 PM
CCM ya biashara ya utumwa Sokomoko Jukwaa la Siasa 8 12th May 2008 05:34 PM
Butiku ana hoja! Bubu Ataka Kusema Jukwaa la Siasa 152 19th October 2007 06:15 PM

Tuma Ukurasa huu kwa rafiki yako!


All times are GMT +3. The time now is 06:13 AM.

Powered by JamiiForums.com
Copyrights reserved to JamiiForums.com