BARAZA Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) limesema kutokana na serikali kutupilia mbali ombi la kunzisha Mahakama ya Kadhi, Waislamu hawataipigia kura CCM katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.
Katika taarifa yake, Bakwata ilifikia hatua ya kusema Waislamu wasimchague Rais Jakaya Kikwete iwapo atasimamishwa na CCM kugombea urais, ikiwa ni pamoja na wabunge na madiwani watakaosimamishwa na chama hicho tawala kutokana na kitendo cha serikali kutupilia mbali hoja ya Mahakama ya Kadhi.
Kauli hiyo imetolewa jana wakati Mufti Issa bin Shaaban Simba alipokuwa akitoa tamko kupinga uamuzi wa serikali kutaka kutumia sheria za dini ya Kiislamu katika mahakama za kawaida badala ya kuanzisha Mahakama ya Kadhi, kitu ambacho alisema anaamini kitawanyima haki Waislamu.
Alisema serikali imedhihirisha kuwa inaendeshwa na Wakristo na si kweli kama serikali haina dini na akamtaka Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe kubatilisha kauli hiyo kwa kuwa inamchafua Rais Jakaya Kikwete mbele ya umma wa Waislamu.
Waziri ametuthibitishia kama Rais Kikwete alikuwa akitulaghai ili tumpigie kura kwa kigezo kuwa suala hilo litashughulikiwa na kupatiwa ufumbuzi na sio kuchanganywa kama ilivyokuwa mwaka 1970 katika Sheria ya Ndoa na kuwanyima haki Waislamu,alisema.
Alisema kwa muda mrefu sana Waislamu wamekuwa kimya wakitumia hekima na busara kudai haki zao, lakini katika hatua hii ambayo serikali imefikia hawapo tayari kuendelea kudhalilishwa na kuwa kitendo hicho ni dhalimu.
Mufti alisema wamekuwa wakiiomba Mahakama ya Kadhi kwa zaidi ya miaka 20 na hivyo hawezi kuendelea kuwa kimya na kupakwa mafuta kwa mgongo wa chupa kwa kuwa mahakama hiyo ni haki yao.
Alisema kauli ya Waziri Chikawe imedhihirisha kuwa serikali ina wenyewe na Waislamu wamewekwa katika tabaka la pili pamoja na Rais Jakaya Kikwete kuwatuliza kwa ahadi kuwa watalipatia ufumbuzi suala hilo.
Natoa wito kwa Masheikh wote nchini na Waislamu wa madhehebu yote kupinga vikali kauli iliyotolewa na Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe na kwamba Waislamu waige mfano wa Waislamu wa Afrika Kusini,alisema Mufti na kuhoji:
Kwa nini iwe Afrika ya Kusini na isiwe Zanzibar, Uganda na Kenya ambazo zipo ndani ya Afrika Mashariki? Kwa niaba ya Waislamu nasema serikali haikututendea haki na imetuchukiza sana,alisema.
Alisema lengo la kuomba mahakama hiyo ni kuhakikisha Waislamu wanashughulikia masuala yao ya ndoa na mirathi na si vinginevyo, hivyo waziri asipotoshe jamii kwa kutumia mifano ambayo haiko sahihi.
Mahakama hii haitawakata wezi mikono kwa kuwa nchi hii ina katiba na sheria na sisi tutazirudisha kesi zote za jinai mikononi mwa serikali. Sifahamu hiyo kamati ambayo waziri alisema alikuwa amekaa na kutoa tamko hilo ilikuwa na watu gani,alihoji.
Aliongeza kuwa kutokana na mapungufu hayo waziri arudi tena na kukutana na masheikh ili apate muongozo wa nini Waislamu wanahitaji na sio kuzungumza bila kuwa na usahihi wa kile anachosema.
Wakizungumza na waandishi wa habari baada ya tamko la Bakwata, masheikh walikuwa na mitazamo tofauti. Sheikh wa mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Salum Mussa alisema wapo baadhi ya Waislamu ambao watakubali kutokana na ufinyu wao wa elimu ya dini.
Mussa alisema haoni sababu ya serikali kufanya njia ya mkato katika suala hilo kwani Waislamu wanahitaji Mahakama ya Kadhi kama ilivyo kwa wafanyabiashara ambao wana mahakama yao.
Hukumu inayotolewa katika Mahakama ya Kadhi ni ibada kwa mujibu wa mafundisho ya Mtume Muhammad (S.A.W) hivyo ni lazima kwa atakayetoa hukumu hiyo awe Muislamu na si vinginevyo,alisema.
Namshanga waziri anapotaka sheria hizi zitumiwe katika mahakama za kawaida. Aliona wapi John akawa imamu,alihoji sheikh huyo wa mkoa wa Dar es Salaam.
Naye katibu wa Bakwata wilayani Ilala, Sheikh Issa Ausi alisema historia iko wazi. Waasisi na wanaharakati ambao waliitoa Tanganyika mikononi mwa wakoloni walikuwa Waislamu, na akahoji sababu za serikali kuwa mstari wa mbele kuwafunga midomo leo.
Bakwata imezinduka sasa Waislamu wote tumeungana katika kupigania haki zetu na kutetea maslahi yetu na serikali itambue kuwa Bakwata iko hai hao Wakristo walikuwa wapi wakati sisi tukipigania uhuru,alihoji.
Wakati huohuo, Sheikh Salum Rwambo alisema anawashangaa wabunge Waislamu ambao baadhi ni mahajat na malhaj wanakaa kimya na kushindwa kutetea hoja za msingi na kudai kuwa huo sasa ndio mwisho wao wa kuwaita masheikh na kutaka waombewe dua ili wasipate wepesi katika kampeni zao.
Sheikh Rwambo pia alimsifia mbunge wa Nzega Lucas Selelii kwamba ni miongoni mwa wabunge katika Bunge hilo wanaozungumza ukweli na kwa kujiamini tofauti na wengine ambao wanaenda kukaa bila kufanya kazi zilizowapeleka.
Source: Mwananchi
CCM watajuta kuweka swala la Mahakama ya Kadhi kwenye Ilani yao uchaguzi ya 2005.
asante sana mkuu na hayo ndio maajabu ya viongozi wa dini zetu.sasa inamaana ccm wakirekkebisha hilo tu wapewe kura? swala dogo sana hilo kwa ccm kwa kuataka kura.kama wanaweza kutoa rushwa kupata kura watashindwa kuwapa pendekezo lao hili wapate kura?
There are two things in our job. Criticism i accept with respect. Disrespect i dont accept and dont respect" - Arsene Wenger.
Sijui kama ni sahihi kabisa kusema CCM nadio ina makosa, kuna watu ndani ya CCM ndio tatizo, japokuwa wanaiwakilisha CCM, kuna uwezekano wa kuwaondoa hao wabovu mafisadi na walaghai, na chama kikaendelea vizuri kabisa. Lakini at least hata watu wa dini wameanza kufahamu ukweli wa mambo!!
Ngoma ndio inaanza kupigwa anayeweza aingie na acheze...suala hilo zito sana sana waangalie lisije likaleta machafuko na mpasuko...haya amani yetu tu tusije kuipoteza
Tanzania haijawahi kuwa na amani, bali utii wa woga.
__________________
Tanzania itakuwa huru wananchi wakimiliki nchi yao wenyewe sio baadhi ya wateule wachache.Haki na sheria kwa wote bila kujali rangi,cheo,na utajiri wa mtu.
Mambo yote mengine ambayo sisi tunayapigia kelele hayawafanyi wao kuichukia CCM; yaani yote yaliyofanyika dhidi ya nchi yetu na utajiri wetu wao hayawagusi wala kuwataka waumini wao kuyafanya ya kisiasa na kuiadhibu CCM; yaani yote hayo hayajafikia kiwango cha kuwakera.. isipokuwa hili moja tu?
Ngoma ndio inaanza kupigwa anayeweza aingie na acheze...suala hilo zito sana sana waangalie lisije likaleta machafuko na mpasuko...haya amani yetu tu tusije kuipoteza
.
Kama noma naiwe noma potelea mbali na ivunjike amani.
.
MUFTI UKO SAWA
.
Katika hili umewaunganisha waislam. Hii ndio bakwata
Inayo hitajiwa na waislam.
__________________
Maisha Matamu Lakini Mafupi
Last edited by BinMgen; 3rd July 2009 at 08:15 AM..
Waisilamu wanahaki ya kupiga kelele kwani ni kweli kwenye ilani ya CCM walisema Mahakama ya kadhi itakuwepo, ila CCM imewapiga mchanga wa macho.
Ila kuna kunahaja shekh mkuu akaangalia ni ahadi ngapi watanzania tupewa changa la macho, maisha bora, utawala wa sheria, je ni waisilamu wangapi wako mahabusu miaka nenda rudi bila kesi zao kusikilizwa.
Je ni waisilamu wangapi wanakufa kwa kukosa huduma za afya.
je ni waisilamu wangapi wapo shule na hakuna elimu bora.
Je ni waisilamu wangapi wanakufa kwa madawa ya kulevya yanayouzwa na vigogo.
Je ni waisilamu wangapi wameathirika na wizi wa EPA, Richmond< Meremeta deepGreen nk.
Haya yote na mengine mengi ndio nilitegemea shekh mkuu angeyafanya kama sababu za kutoichagua CCM.
Wakishindwa kuwa wa kweli kwa wanayoyaahidi hawawezi kutimiza wanayowapaka nayo mafuta, CCM imegundua ina deal na mandondocha hivyo hawajali kesho Kikwete atakuja msikitini atawashika mkono kesho yake wote mnabadili kauli na kuonekana mtu mzima......
Kama kweli basi kidedea mpaka kieleweke tena kwa yote mpaka Rostam aende keko kama Juma na Omari.
__________________
Tanzania itakuwa huru wananchi wakimiliki nchi yao wenyewe sio baadhi ya wateule wachache.Haki na sheria kwa wote bila kujali rangi,cheo,na utajiri wa mtu.
Mkandara anasema tumjibu Mufti kwa hoja. Zilizotolewa umeona ni vioja? Haya angalia hizi:
Mufti anadai Sheria ya Ndoa ya 1970 imewanyima Waislamu haki. Hakuweza kueleza kwani hakielezeki. Si kweli. Na kama ingekuwa kweli basi angesema kipengele husika ni kipi ili kiangaliwe.
Mufti kasema Waislamu wanataka mahakama ya kushughulikia mirathi na ndoa. Nani kawanyima kuanzisha? Si lazima iwe sehemu ya serikali.
Mufti kasema Waislamu wanapashwa kuwa na mahakama yao kama wafanyabiashara walivyo na mahakama yao. Yaani anataka kusema Waislamu ni kikundi tu kama kilivyo kikundi cha wafanyabiashara? Anawakosea haki Waislamu.
Tatizo si kuwa na mahakama tatizo ni kudhalilishwa na kuonewa waislamu. Mzee Mwanakijiji kuhusu alleged grand corruption cases ni still allegation hakuna substance wala proof katika hilo bali ni accusations tu.
Mdondoaji ni kipi hicho unachodondoa jamani mbona ulichoandika kimekaa kaa vibaya hivyo? YAANI UNASEMA ISSUES ZA EPA, RICHMOND, MEREMETA, TANGOLD, DEEP GREEN NA ZINGINE HAZINA PROOF? Did you mean what you wrote au keyboard ilikosa ushirikiano? Kama you meant what you wrote then you have to think twice kwani you could be in a wrong forum I suppose.
Hoja ya msingi ni kwamba Waislamu wamekosa demokrasia ndani ya taasisi zao kwa kile tunaita kimombo co-option of few islamic leaders by Government.Taasisi za kikristu kama vile Tanzania Episcopol Council na nyinginezo huwa haziingiliwi na serikali, lakini inapokuja swala zima la uchaguzi ndani ya taasisi za kiislam, serikali ina ingilia(influence) na ndio maana Wapo wanao mkubal sheikh Mkuu na wasiomkubali ndani ya sheikh mkuu. Kwa hiyo hoja ya msingi nikuangalia demokrasia ndani ya taasis za kiislam. Kwa mfano ndani ya kanisa la lutherani (KKT) kumekuwa kunafukuta sehemu mbali mbali kama vile upareni, meru n.k, sababu kubwa utafiti ulibainisha kuwa ni mgawanyo wa rasilimali. Fukuto kubwa ndani ya uisilamu husababishwa na ukosefu wa demokrasia ndani ya taasisi hizo because for some reasons the government does not want the muslims to collectivelly pick the leadership they want. Kwa hiyo hili swala ni lazima litizamwe upya ili lipatiwe ufumbuzi. Wakati civil war inaanza watu huwa hawatangazi ila ilalipuka tu. utasikia tu , fujo mwembe chai, fujo za kkt upareni, vijana wakiislamu wakizuia wazee kuingia misikitini, wakulima wakichinjana na wafugaji, chuo kikuu hakukaliki n.k.