Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM - Page 2 - JamiiForums |The Home of Great Thinkers

Go Back   JamiiForums |The Home of Great Thinkers > Public Forums > Jukwaa la Siasa


Jukwaa la Siasa Tanzania & World Politics General Discussion Forum. You need to be registered in order to post your comment(s)


Reply
 
LinkBack Thread Tools Rate Thread Display Modes
Old 2nd July 2009, 09:09 PM  
Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM
Keil Keil is offline 2nd July 2009, 09:09 PM

Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Na Ummy Muya

BARAZA Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) limesema kutokana na serikali kutupilia mbali ombi la kunzisha Mahakama ya Kadhi, Waislamu hawataipigia kura CCM katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.

Katika taarifa yake, Bakwata ilifikia hatua ya kusema Waislamu wasimchague Rais Jakaya Kikwete iwapo atasimamishwa na CCM kugombea urais, ikiwa ni pamoja na wabunge na madiwani watakaosimamishwa na chama hicho tawala kutokana na kitendo cha serikali kutupilia mbali hoja ya Mahakama ya Kadhi.

Kauli hiyo imetolewa jana wakati Mufti Issa bin Shaaban Simba alipokuwa akitoa tamko kupinga uamuzi wa serikali kutaka kutumia sheria za dini ya Kiislamu katika mahakama za kawaida badala ya kuanzisha Mahakama ya Kadhi, kitu ambacho alisema anaamini kitawanyima haki Waislamu.

Alisema serikali imedhihirisha kuwa inaendeshwa na Wakristo na si kweli kama serikali haina dini na akamtaka Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe kubatilisha kauli hiyo kwa kuwa inamchafua Rais Jakaya Kikwete mbele ya umma wa Waislamu.

Waziri ametuthibitishia kama Rais Kikwete alikuwa akitulaghai ili tumpigie kura kwa kigezo kuwa suala hilo litashughulikiwa na kupatiwa ufumbuzi na sio kuchanganywa kama ilivyokuwa mwaka 1970 katika Sheria ya Ndoa na kuwanyima haki Waislamu,alisema.

Alisema kwa muda mrefu sana Waislamu wamekuwa kimya wakitumia hekima na busara kudai haki zao, lakini katika hatua hii ambayo serikali imefikia hawapo tayari kuendelea kudhalilishwa na kuwa kitendo hicho ni dhalimu.

Mufti alisema wamekuwa wakiiomba Mahakama ya Kadhi kwa zaidi ya miaka 20 na hivyo hawezi kuendelea kuwa kimya na kupakwa mafuta kwa mgongo wa chupa kwa kuwa mahakama hiyo ni haki yao.

Alisema kauli ya Waziri Chikawe imedhihirisha kuwa serikali ina wenyewe na Waislamu wamewekwa katika tabaka la pili pamoja na Rais Jakaya Kikwete kuwatuliza kwa ahadi kuwa watalipatia ufumbuzi suala hilo.

Natoa wito kwa Masheikh wote nchini na Waislamu wa madhehebu yote kupinga vikali kauli iliyotolewa na Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe na kwamba Waislamu waige mfano wa Waislamu wa Afrika Kusini,alisema Mufti na kuhoji:

Kwa nini iwe Afrika ya Kusini na isiwe Zanzibar, Uganda na Kenya ambazo zipo ndani ya Afrika Mashariki? Kwa niaba ya Waislamu nasema serikali haikututendea haki na imetuchukiza sana,alisema.

Alisema lengo la kuomba mahakama hiyo ni kuhakikisha Waislamu wanashughulikia masuala yao ya ndoa na mirathi na si vinginevyo, hivyo waziri asipotoshe jamii kwa kutumia mifano ambayo haiko sahihi.

Mahakama hii haitawakata wezi mikono kwa kuwa nchi hii ina katiba na sheria na sisi tutazirudisha kesi zote za jinai mikononi mwa serikali. Sifahamu hiyo kamati ambayo waziri alisema alikuwa amekaa na kutoa tamko hilo ilikuwa na watu gani,alihoji.
Aliongeza kuwa kutokana na mapungufu hayo waziri arudi tena na kukutana na masheikh ili apate muongozo wa nini Waislamu wanahitaji na sio kuzungumza bila kuwa na usahihi wa kile anachosema.

Wakizungumza na waandishi wa habari baada ya tamko la Bakwata, masheikh walikuwa na mitazamo tofauti. Sheikh wa mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Salum Mussa alisema wapo baadhi ya Waislamu ambao watakubali kutokana na ufinyu wao wa elimu ya dini.
Mussa alisema haoni sababu ya serikali kufanya njia ya mkato katika suala hilo kwani Waislamu wanahitaji Mahakama ya Kadhi kama ilivyo kwa wafanyabiashara ambao wana mahakama yao.

Hukumu inayotolewa katika Mahakama ya Kadhi ni ibada kwa mujibu wa mafundisho ya Mtume Muhammad (S.A.W) hivyo ni lazima kwa atakayetoa hukumu hiyo awe Muislamu na si vinginevyo,alisema.

Namshanga waziri anapotaka sheria hizi zitumiwe katika mahakama za kawaida. Aliona wapi John akawa imamu,alihoji sheikh huyo wa mkoa wa Dar es Salaam.

Naye katibu wa Bakwata wilayani Ilala, Sheikh Issa Ausi alisema historia iko wazi. Waasisi na wanaharakati ambao waliitoa Tanganyika mikononi mwa wakoloni walikuwa Waislamu, na akahoji sababu za serikali kuwa mstari wa mbele kuwafunga midomo leo.
Bakwata imezinduka sasa Waislamu wote tumeungana katika kupigania haki zetu na kutetea maslahi yetu na serikali itambue kuwa Bakwata iko hai hao Wakristo walikuwa wapi wakati sisi tukipigania uhuru,alihoji.

Wakati huohuo, Sheikh Salum Rwambo alisema anawashangaa wabunge Waislamu ambao baadhi ni mahajat na malhaj wanakaa kimya na kushindwa kutetea hoja za msingi na kudai kuwa huo sasa ndio mwisho wao wa kuwaita masheikh na kutaka waombewe dua ili wasipate wepesi katika kampeni zao.

Sheikh Rwambo pia alimsifia mbunge wa Nzega Lucas Selelii kwamba ni miongoni mwa wabunge katika Bunge hilo wanaozungumza ukweli na kwa kujiamini tofauti na wengine ambao wanaenda kukaa bila kufanya kazi zilizowapeleka.


Source: Mwananchi


CCM watajuta kuweka swala la Mahakama ya Kadhi kwenye Ilani yao uchaguzi ya 2005.

Keil
JF Senior Expert Member
Points: 628,831, Level: 100 Points: 628,831, Level: 100 Points: 628,831, Level: 100
Activity: 4% Activity: 4% Activity: 4%
Join Date: Mon Jul 2007
Posts: 1,385
Thanks: 91
Thanked 300 Times in 133 Posts
Views: 5443
Reply With Quote
  #11  
Old 2nd July 2009, 10:01 PM
Mzee Mwanakijiji's Avatar
Mzee Mwanakijiji Mzee Mwanakijiji is offline
Mzee Mwanakijiji anawashangaa wanaoitetea sheria mbovu
JF Premium Member
Points: 12,925,461, Level: 100 Points: 12,925,461, Level: 100 Points: 12,925,461, Level: 100
Activity: 92% Activity: 92% Activity: 92%
 
Join Date: Fri Mar 2006
Location: Kijijini
Posts: 18,423
Thanks: 8,352
Thanked 4,580 Times in 1,280 Posts
Rep Power: 44
Mzee Mwanakijiji is on a distinguished roadMzee Mwanakijiji is on a distinguished road
Send a message via MSN to Mzee Mwanakijiji Send a message via Skype™ to Mzee Mwanakijiji
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Mambo yote mengine ambayo sisi tunayapigia kelele hayawafanyi wao kuichukia CCM; yaani yote yaliyofanyika dhidi ya nchi yetu na utajiri wetu wao hayawagusi wala kuwataka waumini wao kuyafanya ya kisiasa na kuiadhibu CCM; yaani yote hayo hayajafikia kiwango cha kuwakera.. isipokuwa hili moja tu?
__________________
Nchi hii imewahi kung' oa masultani wa kila aina. Tukianza kuvumilia masultani wakuchaguliwa tutapanda mbegu ya masultani wa kuzaliwa. - Nyerere katika "Uongozi wetu na Hatima ya Tanzania"
Reply With Quote
  #12  
Old 2nd July 2009, 10:02 PM
Skills4Ever's Avatar
Skills4Ever Skills4Ever is online now
Skills4Ever Die Trying Guru
JF Senior Expert Member
Points: 117,495, Level: 100 Points: 117,495, Level: 100 Points: 117,495, Level: 100
Activity: 5% Activity: 5% Activity: 5%
 
Join Date: Thu Feb 2008
Posts: 1,417
Thanks: 0
Thanked 78 Times in 51 Posts
Rep Power: 25
Skills4Ever will become famous soon enoughSkills4Ever will become famous soon enoughSkills4Ever will become famous soon enoughSkills4Ever will become famous soon enoughSkills4Ever will become famous soon enoughSkills4Ever will become famous soon enoughSkills4Ever will become famous soon enoughSkills4Ever will become famous soon enough
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Ngoma ndio inaanza kupigwa anayeweza aingie na acheze...suala hilo zito sana sana waangalie lisije likaleta machafuko na mpasuko...haya amani yetu tu tusije kuipoteza
__________________
"No matter how far down the wrong road you've gone,TURN BACK"
Reply With Quote
  #13  
Old 2nd July 2009, 10:07 PM
Mbalamwezi Mbalamwezi is offline
Mbalamwezi has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 142,920, Level: 100 Points: 142,920, Level: 100 Points: 142,920, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Sun Sep 2007
Posts: 505
Thanks: 17
Thanked 5 Times in 2 Posts
Rep Power: 24
Mbalamwezi will become famous soon enoughMbalamwezi will become famous soon enoughMbalamwezi will become famous soon enoughMbalamwezi will become famous soon enoughMbalamwezi will become famous soon enoughMbalamwezi will become famous soon enoughMbalamwezi will become famous soon enoughMbalamwezi will become famous soon enough
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Quote:
Naye katibu wa Bakwata wilayani Ilala, Sheikh Issa Ausi alisema historia iko wazi. Waasisi na wanaharakati ambao waliitoa Tanganyika mikononi mwa wakoloni walikuwa Waislamu, na akahoji sababu za serikali kuwa mstari wa mbele kuwafunga midomo leo.
Duh, hapa kazi ipo....!
Reply With Quote
  #14  
Old 2nd July 2009, 10:08 PM
MwanaFalsafa1's Avatar
MwanaFalsafa1 MwanaFalsafa1 is offline
MwanaFalsafa1 For the love of God and country
JF Premium Member
Points: 532,504, Level: 100 Points: 532,504, Level: 100 Points: 532,504, Level: 100
Activity: 6% Activity: 6% Activity: 6%
 
Join Date: Tue Feb 2008
Posts: 3,621
Thanks: 246
Thanked 466 Times in 308 Posts
Rep Power: 31
MwanaFalsafa1 will become famous soon enoughMwanaFalsafa1 will become famous soon enoughMwanaFalsafa1 will become famous soon enoughMwanaFalsafa1 will become famous soon enoughMwanaFalsafa1 will become famous soon enoughMwanaFalsafa1 will become famous soon enoughMwanaFalsafa1 will become famous soon enoughMwanaFalsafa1 will become famous soon enough
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

I'll believe it when I see it. Siyo wanaongea hapa wakati wakupiga kura wanafanya vingine. History shows kwenye kuiongea tunaongoza lakini kwenye vitendo sifuri.
__________________
"Ask not what your country can do for you, ask what you can do for your country"-JFK.
Reply With Quote
  #15  
Old 2nd July 2009, 10:22 PM
Babuyao Babuyao is online now
Babuyao has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 83,888, Level: 100 Points: 83,888, Level: 100 Points: 83,888, Level: 100
Activity: 5% Activity: 5% Activity: 5%
 
Join Date: Sat Jun 2009
Posts: 507
Thanks: 32
Thanked 44 Times in 29 Posts
Rep Power: 22
Babuyao will become famous soon enoughBabuyao will become famous soon enoughBabuyao will become famous soon enoughBabuyao will become famous soon enoughBabuyao will become famous soon enoughBabuyao will become famous soon enoughBabuyao will become famous soon enoughBabuyao will become famous soon enough
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Quote:
View Post
Ni sehemu ya ibaada
Tangu lini maamuzi ya kesi mahakamani yakawa ni ibada?? Hii kali wakuu!!
Reply With Quote
  #16  
Old 2nd July 2009, 10:23 PM
Mwiba's Avatar
Mwiba Mwiba is offline
Mwiba has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 902,192, Level: 100 Points: 902,192, Level: 100 Points: 902,192, Level: 100
Activity: 1% Activity: 1% Activity: 1%
 
Join Date: Tue Oct 2007
Posts: 2,984
Thanks: 0
Thanked 13 Times in 8 Posts
Rep Power: 69
Mwiba is a jewel in the roughMwiba is a jewel in the roughMwiba is a jewel in the roughMwiba is a jewel in the roughMwiba is a jewel in the roughMwiba is a jewel in the roughMwiba is a jewel in the roughMwiba is a jewel in the roughMwiba is a jewel in the roughMwiba is a jewel in the roughMwiba is a jewel in the rough
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Quote:
View Post
Mambo yote mengine ambayo sisi tunayapigia kelele hayawafanyi wao kuichukia CCM; yaani yote yaliyofanyika dhidi ya nchi yetu na utajiri wetu wao hayawagusi wala kuwataka waumini wao kuyafanya ya kisiasa na kuiadhibu CCM; yaani yote hayo hayajafikia kiwango cha kuwakera.. isipokuwa hili moja tu?
Mwanakijiji wacha hiyo,maana wakijihusisha mtakuja na rangi nyengine hapa ,hawa ni wananchi walioipigia kura CCM na waliipigia kwa kuahidiwa kupatiwa dai hilo wanalolidai ni sawa sawa kabisa na mwanaCCM alieahidiwa kujengewa hospitali,daraja,njia ya lami na mambo kabakaba yakiwemo maisha bora sasa ni wakati wa wale wote walioahidiwa na hadi leo hawajapelekewa hata kokoto au matofali kuanza kubadili muelekeo kama hao Waislamu walioipigia kura CCM hivyo kuanza safari ya kuipeleka CCM kaburini. Hao waislamu walioipigia kura CCM wameanza kuonyesha njia sasa huko kwenye wakiristu walioipigia kura CCM na madai yao hayakutekelezwa nao wapige mbiu ya mgambu ile kufanikisha maziko.

Mambo ya utajiri hayawashughulishi wanaCCM hayo ni ya vyama vya upinzani au hulielewi hilo ? Ila inaonyesha viongozi wa CCM wamewadanganya wenzao waliomo kwenye mrengo wa uislamu, hivyo wanajitayarisha kutoa pigo kwa viongozi wao,sasa tatizo upande wetu wapinzani lipo wapi, hivi ukisikia vita vya panzi furaha ya kunguru unakuwa hufahamu maana ?

Hao sidhani wanazungumza na wanachama wa Chadema CUF au vyama vingine vya kambi ya upinzani ,si waislamu wote waliipigia kura CCM,bali wanazungumza na wanachama wa CCM ambao ni Waislamu kubadili muelekeo wa kuhamisha kura zao na kuzipeleka wanakoona madai yao yatatekelezwa ,hivyo Chama chochote kile kinaweza kuchukua dai hilo na kusema kuwa endapo wao watapewa kura hizo watalitekeleza dai hilo,sioni tatizo la kidini hapa.

Ila ngoma ni nzito sana ukiangalia jamaa alivyopiga mahesabu tokea kudai uhuru.Inaonyesha uvumilivu umeanza kugonga ukomo.
__________________
Light travels faster than sound. This is why some people appear bright until you hear them speak.
Reply With Quote
  #17  
Old 2nd July 2009, 10:40 PM
Junius's Avatar
Junius Junius is offline
Junius Sir Phillip Francis
JF Senior Expert Member
Points: 443,794, Level: 100 Points: 443,794, Level: 100 Points: 443,794, Level: 100
Activity: 5% Activity: 5% Activity: 5%
 
Join Date: Wed Mar 2009
Posts: 2,073
Thanks: 141
Thanked 181 Times in 128 Posts
Rep Power: 26
Junius will become famous soon enoughJunius will become famous soon enoughJunius will become famous soon enoughJunius will become famous soon enoughJunius will become famous soon enoughJunius will become famous soon enoughJunius will become famous soon enoughJunius will become famous soon enough
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Quote:
View Post
Ni sehemu ya ibaada
Masikini CCM inakufa polepole kama muasisi wake Nyerere.
Reply With Quote
  #18  
Old 2nd July 2009, 10:46 PM
Pakacha Pakacha is offline
Pakacha has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 85,785, Level: 100 Points: 85,785, Level: 100 Points: 85,785, Level: 100
Activity: 3% Activity: 3% Activity: 3%
 
Join Date: Tue Apr 2008
Posts: 637
Thanks: 23
Thanked 26 Times in 23 Posts
Rep Power: 23
Pakacha will become famous soon enoughPakacha will become famous soon enoughPakacha will become famous soon enoughPakacha will become famous soon enoughPakacha will become famous soon enoughPakacha will become famous soon enoughPakacha will become famous soon enoughPakacha will become famous soon enough
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Quote:
View Post
Masikini CCM inakufa polepole kama muasisi wake Nyerere.
Haifi -inaimarika. Nyerere alisema CCM haina dini. Sasa tumo humo Ma-pagan. Achana na Mufti. Tukutane kisanduku cha kura.
Reply With Quote
  #19  
Old 2nd July 2009, 11:01 PM
Kidatu Kidatu is offline
Kidatu has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 195,492, Level: 100 Points: 195,492, Level: 100 Points: 195,492, Level: 100
Activity: 4% Activity: 4% Activity: 4%
 
Join Date: Wed Jun 2008
Posts: 613
Thanks: 55
Thanked 17 Times in 13 Posts
Rep Power: 63
Kidatu is a jewel in the roughKidatu is a jewel in the roughKidatu is a jewel in the roughKidatu is a jewel in the roughKidatu is a jewel in the roughKidatu is a jewel in the roughKidatu is a jewel in the roughKidatu is a jewel in the roughKidatu is a jewel in the roughKidatu is a jewel in the roughKidatu is a jewel in the rough
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Sasa itakuwaje wakristo wa madhehebu yote nao wakisema hawatakipigia kura chama cha mapinduzi kama wataruhusu mahakama ya kadhi?.
Reply With Quote
  #20  
Old 2nd July 2009, 11:02 PM
Mwiba's Avatar
Mwiba Mwiba is offline
Mwiba has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 902,192, Level: 100 Points: 902,192, Level: 100 Points: 902,192, Level: 100
Activity: 1% Activity: 1% Activity: 1%
 
Join Date: Tue Oct 2007
Posts: 2,984
Thanks: 0
Thanked 13 Times in 8 Posts
Rep Power: 69
Mwiba is a jewel in the roughMwiba is a jewel in the roughMwiba is a jewel in the roughMwiba is a jewel in the roughMwiba is a jewel in the roughMwiba is a jewel in the roughMwiba is a jewel in the roughMwiba is a jewel in the roughMwiba is a jewel in the roughMwiba is a jewel in the roughMwiba is a jewel in the rough
Default Re: Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Quote:
View Post
Sasa itakuwaje wakristo wa madhehebu yote nao wakisema hawatakipigia kura chama cha mapinduzi kama wataruhusu mahakama ya kadhi?.
CCM itashinda kwa kishindo kikuu.
__________________
Light travels faster than sound. This is why some people appear bright until you hear them speak.
Reply With Quote
Reply

Bookmarks

Tags
aagiza, ccm, mufti, simba, waikatae, waislamu


Currently Active Users Viewing This Thread: 1 (0 members and 1 guests)
 
Thread Tools
Display Modes Rate This Thread
Rate This Thread:

Posting Rules
You may not post new threads
You may not post replies
You may not post attachments
You may not edit your posts

BB code is On
Smilies are On
[IMG] code is On
HTML code is Off
Trackbacks are Off
Pingbacks are Off
Refbacks are On


Similar Threads
Thread Thread Starter Forum Replies Last Post
CCM, CUF wapigana Bubu Ataka Kusema Jukwaa la Siasa 9 19th May 2008 08:53 PM
CCM ya biashara ya utumwa Sokomoko Jukwaa la Siasa 8 12th May 2008 05:34 PM
Butiku ana hoja! Bubu Ataka Kusema Jukwaa la Siasa 152 19th October 2007 06:15 PM

Tuma Ukurasa huu kwa rafiki yako!


All times are GMT +3. The time now is 10:33 PM.

Powered by JamiiForums.com
Copyrights reserved to JamiiForums.com