Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Sakata la Uteuzi wa Majaji: Bunge lawapiga mkwara wanaolizungumzia

    Report Post
    Page 1 of 3 123 LastLast
    Results 1 to 20 of 47
    1. #1
      Mwana Mpotevu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th September 2011
      Posts : 1,972
      Rep Power : 857
      Likes Received
      908
      Likes Given
      878

      Default Sakata la Uteuzi wa Majaji: Bunge lawapiga mkwara wanaolizungumzia

      Sasa ni wazi Bunge limejipa hadhi ya mahakama, Someni habari ifuatayo


      Veronica Kazimoto, MAELEZO

      Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge imetoa tamko la kuwataka watendaji wa Serikali, Mahakama, vyombo vya habari na taasisi nyingine zote kuacha kuzungumzia suala la Uteuzi wa Majaji wa mahakama kuu kama lilivyowasilishwa Bungeni wakati wa Mjadala wa Bajeti ya Wizara ya Katiba na Sheria kwa Mwaka wa Fedha 2012/13.

      Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Brigedia Jenerali Mstaafu Hassan Ngwilizi (Mb), amesema suala hilo liko mbele ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge ambayo inaendelea na uchunguzi hivyo haitarajiwi taasisi nyingine, nje ya Bunge kulizungumzia suala hili kwa kuwa linajadiliwa.

      “Kamati imeamua kutoa tamko hili kwa madhumuni ya kuhakikisha kuwa uvunjifu wa kanuni na taratibu tulizojiwekea kwa mujibu wa Katiba na Sheria nyingine za nchi kutoendelea kuvunjwa,” amesema Ngwilizi.

      Ngwilizi amenukuu Ibara ya 100 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inayosema kuwa kutakuwa na Uhuru wa mawazo, majadiliano na utaratibu Katika Bunge na uhuru huo hautavunjwa wala kuhojiwa na chombo chochote katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, au katika mahakama au mahali penginepo nje ya Bunge.

      “Uhuru wa utaratibu unaohifadhiwa na ibara hiyo ya Katiba umelipa Bunge mamlaka ya kujiwekea utaratibu wa kushughulikia masuala yake katika Kanuni za Kudumu za Bunge zilizotungwa chini ya Ibara ya 89 (1) ya Katiba”, amesisitiza Ngwilizi.

      Kutolewa kwa tamko hilo na kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, kunatokana na mwongozo ulioombwa na Gosbert Blandes (Mb) wakati wa Hotuba ya Msemaji wa Kambi ya Upinzani kwa Wizara ya Katiba na Sheria,Tundu Lissu Mbunge wa Singida Mashariki.

      Katika maelezo yake, Blandes alinukuu ukurasa wa 9 aya ya 2 katika hotuba hiyo iliyosomeka kuwa watu wanateuliwa kuwa majaji wa mahakama Kuu ambao hawajawahi kupendekezwa na Tume ya Utumishi wa Mahakama.

      Aya hiyo iliendelea kusema kuwa inaelekea watu hao hupewa ujaji kama zawadi ili kuwawezesha kupata mafao ya majaji wastaafu ambayo yameboreshwa na matokeo yake ni kuwa na majaji ambao wamechoka na hawawezi au hawajui namna ya kufanya kazi ya jaji wa mahakama kuu.

      MY TAKE: Ni wazi BUNGE sasa linataka kujifanya ni mahakama kwa kuwafumba watu midomo
      MWANAWAVITTO likes this.
      Don't break the LAW, just Bend It!

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      Mwana Mpotevu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th September 2011
      Posts : 1,972
      Rep Power : 857
      Likes Received
      908
      Likes Given
      878

      Default Re: Sakata la Uteuzi wa Majaji: Bunge lawapiga mkwara wanaolizungumzia

      Hizi kanuni za Bunge nadhani wanazitumia vibaya sasa, imekuwa kama nchi ya kiimla
      Don't break the LAW, just Bend It!

    4. #3
      Return Of Undertaker's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th June 2012
      Posts : 659
      Rep Power : 541
      Likes Received
      462
      Likes Given
      0

      Default Huu sasa Uhuni wa Bunge: Wamesema ni Marufuku kuzungumzia swala la majaji feki popote pale

      Kamati ya Haki na Maendeleo ya Bunge inetangaza kuwa ni marufuku ama kwa vyombo vya habari, taasisi yoyote ile au mtu mmoja mmoja kuzungumzia au kujadili swala la majaji Makanjanja walio ripotiwa na Mh Mbunge Tundu Lissu kuwa uteuzi wao umevunja sheria na sasa kama taasisi ndio wenye mamlaka ya kushughurikia ukweli wa jambo hilo na si vinginevyo na atakaye kiuka sheria na hatua kali itachukuliwa dhidi yake....

      Hizi marufuku kwanini huwa zinakuja kwa vitu vyenye ukweli na utata hasa kwenye maslai ya watu flani na si taifa?

      Olimboka, Said Kubenea, madaktari, mauwaji ya raia nk jaribu kufikiria kunani hapo?????
      Jasusi likes this.

    5. #4
      PakaJimmy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th April 2009
      Posts : 14,701
      Rep Power : 22524
      Likes Received
      6358
      Likes Given
      2841

      Default Re: Huu sasa Uhuni wa Bunge: Wamesema ni Marufuku kuzungumzia swala la majaji feki popote pale

      Nimeona live Itv tangazo hilo la kidicteta likitangazwa na mtu mwenye sura ya Hassan Ngwilizi.
      Ni nzuri sana maana wanaweka bold kwenye ukweli...!

    6. #5
      Tume ya Katiba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th April 2012
      Location : Chumbuni-Zanzibar
      Posts : 2,679
      Rep Power : 0
      Likes Received
      538
      Likes Given
      273

      Default Re: Huu sasa Uhuni wa Bunge: Wamesema ni Marufuku kuzungumzia swala la majaji feki popote pale

      Acha tabia ya kuleta habari nusu nusu.

    7. Miaka 50

    8. #6
      Filipo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th January 2011
      Location : Kiding'a
      Posts : 6,349
      Rep Power : 18614
      Likes Received
      3508
      Likes Given
      1663

      Default Re: Huu sasa Uhuni wa Bunge: Wamesema ni Marufuku kuzungumzia swala la majaji feki popote pale

      Too late! Tumeshajadili hadi tumeelewa. Tumeshajua ukweli na tumetosheka. Kilichobaki ni kutumia kura zetu vizuri!

    9. #7
      Kaunga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th November 2010
      Location : Wild wild west
      Posts : 8,431
      Rep Power : 13323
      Likes Received
      7662
      Likes Given
      6911

      Default Re: Huu sasa Uhuni wa Bunge: Wamesema ni Marufuku kuzungumzia swala la majaji feki popote pale

      Do we have freedom of experession in TZ?

    10. #8
      Return Of Undertaker's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th June 2012
      Posts : 659
      Rep Power : 541
      Likes Received
      462
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By Tume ya Katiba
      Acha tabia ya kuleta habari nusu nusu.
      Una matatizo ya akili
      majorbuyoya likes this.

    11. #9
      CHUAKACHARA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd June 2011
      Posts : 3,021
      Rep Power : 7642
      Likes Received
      990
      Likes Given
      752

      Default Re: Huu sasa Uhuni wa Bunge: Wamesema ni Marufuku kuzungumzia swala la majaji feki popote pale

      Quote By Return Of Undertaker
      Kamati ya Haki na Maendeleo ya Bunge inetangaza kuwa ni marufuku ama kwa vyombo vya habari, taasisi yoyote ile au mtu mmoja mmoja kuzungumzia au kujadili swala la majaji Makanjanja walio ripotiwa na Mh Mbunge Tundu Lissu kuwa uteuzi wao umevunja sheria na sasa kama taasisi ndio wenye mamlaka ya kushughurikia ukweli wa jambo hilo na si vinginevyo na atakaye kiuka sheria na hatua kali itachukuliwa dhidi yake....

      Hizi marufuku kwanini huwa zinakuja kwa vitu vyenye ukweli na utata hasa kwenye maslai ya watu flani na si taifa?

      Olimboka, Said Kubenea, madaktari, mauwaji ya raia nk jaribu kufikiria kunani hapo?????
      Hopeless, Bunge halina mamlaka ya kumkataza mtu kusema. ni mahakama tu yenye uwezo huo. Hii mijitu imelewa ebunge!

    12. #10
      Baba V's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th December 2010
      Location : Buguruni Mnyamani
      Posts : 10,871
      Rep Power : 30216
      Likes Received
      4696
      Likes Given
      3477

      Default Re: Huu sasa Uhuni wa Bunge: Wamesema ni Marufuku kuzungumzia swala la majaji feki popote pale

      Ndo tunajadili hapa

    13. #11
      Havizya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd April 2012
      Posts : 776
      Rep Power : 515
      Likes Received
      156
      Likes Given
      60

      Default Re: Huu sasa Uhuni wa Bunge: Wamesema ni Marufuku kuzungumzia swala la majaji feki popote pale

      Hofu yao, aibu ya kwao. Wao kila afanyalo President ni kupiga makofi tu! Makosa ya uteuzi wa majaji yamewekwa wazi, na kumbu kumbu ziko serekalini huko huko! Ya nini kubwabwaja? Waache watz wahoji yanayotendeka nchini kwao.

    14. #12
      Emeka Anyaoku's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd April 2012
      Posts : 430
      Rep Power : 443
      Likes Received
      134
      Likes Given
      0

      Default Re: Huu sasa Uhuni wa Bunge: Wamesema ni Marufuku kuzungumzia swala la majaji feki popote pale

      Wafungie mitandao.kila kitu wanaweka vizuizi.Hizi sio zile enzi za zidumu fikra za mwenyekiti.

    15. #13
      mwakidondo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th May 2012
      Posts : 472
      Rep Power : 448
      Likes Received
      52
      Likes Given
      51

      Default Re: Huu sasa Uhuni wa Bunge: Wamesema ni Marufuku kuzungumzia swala la majaji feki popote pale

      Hilo zuio binafsi sina tatizo nalo, maana tukiachwa tuendelee kulijadili bila kikomo kama ambavyo tayari tumefanya hatutafikia hitimisho lolote. Bila chombo/taasisi yenye mamlaka ishughulikie jambo hili ili mwisho mwema na wenye manufaa kwa watanzania uweze kufikiwa. Tumeshaongea na kuandika mengi sana kuhusu jambo hili lakini nani katujibu au japo kutusikiliza hivyo ni vema sasa lishughulikiwe kikamilifu na vyombo husika nasi tusubiri majibu mwafaka.

    16. #14
      Nyalotsi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th July 2011
      Posts : 2,653
      Rep Power : 926
      Likes Received
      587
      Likes Given
      83

      Default Re: Sakata la Uteuzi wa Majaji: Bunge lawapiga mkwara wanaolizungumzia

      Sisi tutaendelea kuzungumza. Hizo kanuni za bunge zinawahusu wao ndo maana hazipo hadharani ili nasi tuzisome. Hili suala lilishazungumzi siku nyingi kabla hata lisu hajawa mbunge. Lisu alipata tu uwanja wa kulizungumzia vizuri na wao kwa ulimbukeni wakaanza kuomba ushahidi kumbe wanamvua nguo bwana wao wanayemtumikia. Bahati mbaya jamaa mwenyewe yuko uchi toka siku nyingi lakini bado anadunda na kengele zake hadharani

    17. #15
      Nyalotsi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th July 2011
      Posts : 2,653
      Rep Power : 926
      Likes Received
      587
      Likes Given
      83

      Default Re: Sakata la Uteuzi wa Majaji: Bunge lawapiga mkwara wanaolizungumzia

      Sisi tutaendelea kuzungumza. Hizo kanuni za bunge zinawahusu wao ndo maana hazipo hadharani ili nasi tuzisome. Hili suala lilishazungumzi siku nyingi kabla hata lisu hajawa mbunge.

      Lissu alipata tu uwanja wa kulizungumzia vizuri na wao kwa ulimbukeni wakaanza kuomba ushahidi kumbe wanamvua nguo bwana wao wanayemtumikia. Bahati mbaya jamaa mwenyewe yuko uchi toka siku nyingi lakini bado anadunda na kengele zake hadharani
      .

    18. #16
      JERUSALEMU's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th September 2012
      Posts : 790
      Rep Power : 494
      Likes Received
      231
      Likes Given
      150

      Default Re: Sakata la Uteuzi wa Majaji: Bunge lawapiga mkwara wanaolizungumzia

      SERIKALI yoyote inayo karibia mwisho wake huwa hivi. kila aliyekabidhiwa jukumu kidogo tu anataka atembee juu ya vichwa vya waajiri wake.hilo tutalipinga milele tena ashindwe kabisaa.

    19. #17
      Mzalendo JR's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th June 2012
      Posts : 906
      Rep Power : 532
      Likes Received
      277
      Likes Given
      213

      Default Re: Sakata la Uteuzi wa Majaji: Bunge lawapiga mkwara wanaolizungumzia

      Tutaendelea kujadili utumbo wao kila kukicha hata kama wakija kijiweni kwetu maada ni zilezile, kwani freedom of expression uko wapi?
      "Happiness is what you think, what you say, and what you do are in harmony"

    20. #18
      JERUSALEMU's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th September 2012
      Posts : 790
      Rep Power : 494
      Likes Received
      231
      Likes Given
      150

      Default Re: Huu sasa Uhuni wa Bunge: Wamesema ni Marufuku kuzungumzia swala la majaji feki popote pale

      Huyu Ngwilizi kweli kachoka! ananikumbusha konda aliyekuwa usingizini akakurupuka kumwambia kaka yake anayefungua NET ili alale akamwambia hakuna kuingia wanafunzi wametosha akidhani ile ni daladala.

      Na huyu nae kakurupuka kutukataza waajiri wake tusizungumzie makanjanja wa mahakama kwa sheria ipi? kweli siku ya kufa Nyani miti yote huteleza na hizi ni dalili tosha kuwa 2015 CCM kwtshney.
      Mimibaba likes this.

    21. #19
      ng'wanankamba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th December 2010
      Posts : 262
      Rep Power : 479
      Likes Received
      62
      Likes Given
      68

      Default Re: Sakata la Uteuzi wa Majaji: Bunge lawapiga mkwara wanaolizungumzia

      Tunakoelekea, itafika mahali hakuna tutachokuwa tunakijadili kama taifa, kila utakachogusa utaambiwa hurusiwi kukiongelea kwa amri ya mahakama au bunge, baadaye itakuwa kwa amri ya Ikulu, amri ya polisi, amri ya jeshi n.k. Mungu tunusuru waja wako.

    22. #20
      Bajabiri's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st December 2010
      Posts : 9,741
      Rep Power : 2884
      Likes Received
      1115
      Likes Given
      52

      Default

      Quote By Mwana Mpotevu
      Hizi kanuni za Bunge nadhani wanazitumia vibaya sasa, imekuwa kama nchi ya kiimla
      watawala watu wabaya sana,maana wao wakikaa kwenye mamlaka wanakuja na kanuni kedekede za ukandamizaj,lakin wakitaka nyadhifa wanakuja na kanuni nyiiingi na ibara kibao za kuwasaidia wananchi

    Page 1 of 3 123 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...