Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Siogopi kulogwa: Dk. Magufuli

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 32
    1. #1
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,226
      Rep Power : 3560
      Likes Received
      3060
      Likes Given
      462

      Default Siogopi kulogwa: Dk. Magufuli

      ALHAMISI, SEPTEMBA 20, 2012 06:32 NA GABRIEL MUSHI

      WAZIRI wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, amesema ingawa majukumu ya wizara yake ni ya hatari na ya mateso, kamwe haogopi kurogwa. Dk. Magufuli alitoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam jana, wakati akizungumza katika sherehe ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Barabara ya Usafiri wa Haraka (BRT).

      Dk. Magufuli aliyasema hayo mbele ya Rais Jakaya Kikwete, alipokuwa akimzungumzia Mkurugenzi Mtendaji wa Mradi wa Mabasi yaendayo Kasi, DART, Cosmas Takule, ambaye alisema ameshindwa kutimiza wajibu.

      Alisema pia kwamba, kutokana na kutowajika kwa mkurugenzi huyo, kama angekuwa yuko chini yake angekuwa ameshamfukuza kazi.

      “Mkurugenzi huyu anachelewesha kulipa fidia ili kumaliza migogoro inayoibuka kwenye miradi ya ujenzi jijini Dar es Salaam.

      “Siwachongei kwako Mheshimiwa Rais, lakini DART wanatukwaza, kuna vituo viwili kati ya saba ambavyo huyu mkurugenzi alitakiwa kuwalipa fidia wakazi wanaoathiriwa na vituo hivyo lakini amechelewesha fidia hadi muda wa mkandari kuwapo eneo la kazi umekwisha na kitendo hiki kimetuingiza hasara sisi kwa kulazimika kumlipa mkandarasi huyo.

      “Lakini kwa kuwa Waziri Hawa Ghasia yupo katika sherehe hizi, nadhani atalichukulia hatua kwa sababu suala la kulipa fidia na kushughulikia migogoro ya watu hao lipo chini yake kwa kupitia DART.

      “Kazi hii ya ujenzi tunajua ni mateso, ni risk sana kwa sababu unapomsema mtu wakati anakuangalia anaweza kukuroga ukashangaa umeanguka chini ghafla.

      “Kwa hiyo, nimeamua kumsema hapa huyu mkurugenzi mbele yako kwa sababu siogopi kulogwa, kwani hata kama akiniloga, kwa Jina la Yesu atashindwa tu,” alisema Dk. Magufuli.

      Katika hatua nyingine, alimtaka Rais Kikwete, asitishike na maneno machafu yanayotolewa na baadhi ya watu, badala yake aendelee na safari zake za nje ya nchi ili kuomba misaada zaidi kwa wafadhili.

      “Tunahitaji marais wenye uwezo wa kuzungumza kizungu ili tuweze kupata misaada. Kwa mfano, hivi sasa Rais amezungumza na Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia na amekubali kutujengea barabara za juu pale Ubungo.

      “Mheshimiwa Rais, endelea kusafiri kwa sababu hauwezi kukaa ndani kila wakati, kwani hata mwanaume ukikaa ndani tu mkeo atakuuliza, leo huendi hata kusalimia majirani?

      “Kusafiri kwako ni sawa na mvuvi ambaye akitaka samaki lazima aende baharini au ziwani au ukimtaka mke lazima uende kwa mkwe.

      “Usiogope kutukanwa kwa sababu ni jambo la kawaida kwa kiongozi, tena hii barabara ikikamilika wataomba kibali cha kuandamana humo humo,” alisema.

      Kuhusu mradi huo, alisema ujenzi wa barabara hiyo itakayoanzia Kimara Mwisho hadi Kivukoni, itagharimu Sh bilioni 241.

      “Fedha hizi kwa kiwango kikubwa zimetolewa kwa mkopo na Benki ya Dunia ambazo ni Dola za Marekani milioni 225.62 na zilizobakia Serikali yetu imezitoa.

      Naye Rais Kikwete, alimtaka Dk. Magufuli kuacha kuendelea kutenga maeneo ya muda kwa ajili ya ujenzi wa miradi mbalimbali kwa sababu ni hasara kwa Serikali.

      “Kwa mfano hapa Jangwani lilikuwa ni eneo zuri la kucheza mpira, sasa watoto wetu sijui wataenda kucheza wapi, mwisho wa siku watakwenda kucheza michezo mingine kama kubeba dawa za kulevya.

      “Lakini uliniambia hili eneo la Jangwani ni kituo cha muda kwa ajili ya mradi huu, sitaki kusikia tena hili suala la eneo la muda kwa sababu mnaitia hasara Serikali, haina maana kutumia gharama kujenga mahali halafu baadaye pavunjwe eti kwa sababu palikuwa kwa muda.

      “Pia kwako Mkuu wa Mkoa, natoa muda wa wiki mbili mkamilishe suala la Kituo cha Ubungo, kile kituo kinatakiwa kuhamishwa kwa sababu kinahudumia mabasi 300 kwa siku, wakati mradi huu ukikamilika kutakuwa na mabasi mengine zaidi ya 180.

      “Mabasi yote hayo hayawezi kukaa katika kituo hicho, hivyo wewe mkuu wa mkoa nakupa muda wa wiki moja ukae na DART na TANROADS mniletee majibu ya sehemu ya kudumu ya Kituo cha Ubungo,” alisema Rais Kikwete.

      Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Mhandisi Patrick Mfugale, alisema mradi wa ujenzi huo unatarajia kukamilika Machi 8 mwaka 2015 na kukabidhiwa rasmi Septemba 8 mwaka huo huo.

      “Mradi huu utakuwa na vituo vikubwa vitano na vidogo 29, barabara hizo zinajengwa na mkandarasi mkuu kutoka Ujerumani kwa kupitia Kampuni ya Strabag kwa kushirikiana na Mkandarasi Mshauri kutoka Australia.

      “Jambo kubwa linalotukwaza kutekelea mradi huu ni kitendo cha baadhi ya wakazi kufungulia maji machafu ya chooni kwenye barabara, pia baadhi ya mamlaka kama vile TANESCO na DAWASCO kutotoa miundombinu yao haraka kwenye maeneo ya ujenzi na changamoto nyingine ndogondogo,” alisema Mfugale.

      Makanyaga and mpunumpunyenye like this.

    2. Miaka 50

    3. #2
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,226
      Rep Power : 3560
      Likes Received
      3060
      Likes Given
      462

      Default Re: Siogopi kulogwa: Dk. Magufuli

      Kwanini Imani hizo toka kwa WAZIRI na Wakati Serikali inasema hakuna vitu kama hivyo?

    4. #3
      andybird314's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd January 2012
      Location : Tanzania
      Posts : 2,674
      Rep Power : 966
      Likes Received
      552
      Likes Given
      283

      Default Re: Siogopi kulogwa: Dk. Magufuli

      huyu atakuwa mchawi

    5. #4
      Precise pangolin's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 4th January 2012
      Posts : 5,687
      Rep Power : 1913
      Likes Received
      1583
      Likes Given
      676

      Default Re: Siogopi kulogwa: Dk. Magufuli

      Huyu waziri mwenye Imani za kichawi anatakiwa kufukuzwa Mara moja hafai hata kuwa mjumbe wa nyumba kumi
      EH_Mzalendo likes this.

    6. #5
      Njowepo's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 26th February 2008
      Location : Santiago
      Posts : 7,606
      Rep Power : 22057
      Likes Received
      997
      Likes Given
      784

      Default Re: Siogopi kulogwa: Dk. Magufuli

      Kuna usemi kuwa mchawi ukimsema kweupe hakulogi ngoo
      Naona Magufuri ameamua kuuapply huu msemo!
      Chukua tahadhari mwaya maana unawindwa sana na wabaya wako

    7. FemaTV & Radio

    8. #6
      asigwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st September 2011
      Location : TANDHANIYA
      Posts : 4,389
      Rep Power : 1265
      Likes Received
      1208
      Likes Given
      1253

      Default Re: Siogopi kulogwa: Dk. Magufuli

      duh...msgufuli nsyr katoa mpya ila binafsi namkubali sana huyu jamaa.........
      !!..BAR ikiwa na wahudumu wa KIUME TUPU sikai dakika nyingi..!!

    9. #7
      NusuMutu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th September 2011
      Location : Mpulungu
      Posts : 421
      Rep Power : 471
      Likes Received
      74
      Likes Given
      20

      Default Re: Siogopi kulogwa: Dk. Magufuli

      Yes,kwa jina la Yesu!
      EH_Mzalendo likes this.

    10. #8
      genekai's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th February 2010
      Location : Loitering!
      Posts : 7,519
      Rep Power : 2083
      Likes Received
      1070
      Likes Given
      1571

      Default Re: Siogopi kulogwa: Dk. Magufuli

      Bila shaka atakuwa anaamini katika ushirikina!!!!
      The future of this country is being jeopardized by the intellectual slavery of our top leaders

    11. #9
      Zamaulid's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th May 2009
      Location : PANDAGI CHIZA
      Posts : 3,696
      Rep Power : 1308
      Likes Received
      956
      Likes Given
      409

      Default Re: Siogopi kulogwa: Dk. Magufuli

      Quote By andybird314
      huyu atakuwa mchawi
      inakuwaje anajishuku namna hii!!

    12. #10
      Join Date : 25th May 2009
      Location : PANDAGI CHIZA
      Posts : 3,696
      Rep Power : 1308
      Likes Received
      956
      Likes Given
      409

      Default Re: Siogopi kulogwa: Dk. Magufuli

      Quote By Genecius Kaiza
      Bila shaka atakuwa anaamini katika ushirikina!!!!
      na huenda anatembea na tunguli kiunoni!
      genekai likes this.

    13. #11
      Mabreka's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th August 2012
      Posts : 627
      Rep Power : 464
      Likes Received
      181
      Likes Given
      415

      Default Re: Siogopi kulogwa: Dk. Magufuli

      viongoz wengine hata hawajitambui,
      mi nahis alikuwa anatania manke ni aibu

    14. #12
      Lokissa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th November 2010
      Location : Goba
      Posts : 4,092
      Rep Power : 5807
      Likes Received
      1024
      Likes Given
      2876

      Default Re: Siogopi kulogwa: Dk. Magufuli

      mchawi siku zote hushuku kila mtu ni mchawi
      kwa karne hii bad anaamini kulogwa badala ya kutenda kazi
      anajikosha tu huyu mbele ya JK kama juzi alivosema JK
      huwa anasafiri ili kuomba ufadhili na uwekezaji
      ufadhili wa nini wakati tumeachia madini yetu, mfauta na gesi yanachukuliwa tukiwachekea?
      Magufulu amefilisika sera
      hafai hata kuwa balozi wa nyumba kumi
      You may know me but you have no Idea who I am !

    15. #13
      Nicholas's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th March 2006
      Posts : 5,062
      Rep Power : 3630
      Likes Received
      1290
      Likes Given
      2146

      Default Re: Siogopi kulogwa: Dk. Magufuli

      Mbona hakuitolea Kibondo, sumbawanga, pangani, singida au hata karagwe?
      SIMPLY THE RADICAL: I can`t wait to see the criminalization of CCM,UWT,Bunch of Policemen/women,and all wanafiki na wachumia tumbo.

    16. #14
      Cynic's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th January 2009
      Location : Around
      Posts : 2,153
      Rep Power : 967
      Likes Received
      317
      Likes Given
      186

      Default Re: Siogopi kulogwa: Dk. Magufuli

      “Tunahitaji marais wenye uwezo wa kuzungumza kizungu ili tuweze kupata misaada. Kwa mfano, hivi sasa Rais amezungumza na Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia na amekubali kutujengea barabara za juu pale Ubungo.

      Mheshimiwa Rais, endelea kusafiri kwa sababu hauwezi kukaa ndani kila wakati, kwani hata mwanaume ukikaa ndani tu mkeo atakuuliza, leo huendi hata kusalimia majirani?

      “Kusafiri kwako ni sawa na mvuvi ambaye akitaka samaki lazima aende baharini au ziwani au ukimtaka mke lazima uende kwa mkwe.
      Hizi ni kauli za mtu mwenye Ph.D.!! Aibu! Na inaonyesha hizo phd za UDSM ni za hovyo hovyo tu

    17. #15
      Kifarutz's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th August 2012
      Posts : 1,148
      Rep Power : 571
      Likes Received
      169
      Likes Given
      4

      Default Re: Siogopi kulogwa: Dk. Magufuli

      Hata Ikulu kuna kamati ya wachawi na wana posho kutoka kwa JK, mmeishayasahau ya kule bungeni? List ya viongozi wanaamini uchawi ni ndefu!

    18. #16
      ndomyana's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th January 2012
      Posts : 1,811
      Rep Power : 732
      Likes Received
      179
      Likes Given
      0

      Default Re: Siogopi kulogwa: Dk. Magufuli

      Aibu sana tanzania mtu msomi kiwango cha phd bado linamini kazi za kina majimarefu
      JokaKuu likes this.

    19. #17
      Nicholas's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th March 2006
      Posts : 5,062
      Rep Power : 3630
      Likes Received
      1290
      Likes Given
      2146

      Default Re: Siogopi kulogwa: Dk. Magufuli

      Quote By nngu007


      “Tunahitaji marais wenye uwezo wa kuzungumza kizungu ili tuweze kupata misaada. Kwa mfano, hivi sasa Rais amezungumza na Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia na amekubali kutujengea barabara za juu pale Ubungo.

      “Mheshimiwa Rais, endelea kusafiri kwa sababu hauwezi kukaa ndani kila wakati, kwani hata mwanaume ukikaa ndani tu mkeo atakuuliza, leo huendi hata kusalimia majirani?

      “Kusafiri kwako ni sawa na mvuvi ambaye akitaka samaki lazima aende baharini au ziwani au ukimtaka mke lazima uende kwa mkwe.

      “Usiogope kutukanwa kwa sababu ni jambo la kawaida kwa kiongozi, tena hii barabara ikikamilika wataomba kibali cha kuandamana humo humo,” alisema.

      .....

      kazidi jikomba+kutaka sifa za akina Original comedy..Hajui wachina,Warusi huongea na marekani mambo yahusuyo usalama wa dunia kwa lugha zao?Watu wanaongelea Mabomu ya kuweza angamiza dunia chini ya dk 5, kwa zoezi linaweza rudia hata mara mia ktk hizo dkk 5.Yeti wanaelewana na dunia inakuwa salama.

      Hizi PhD za fasta ni taabu kwelikweli.
      SIMPLY THE RADICAL: I can`t wait to see the criminalization of CCM,UWT,Bunch of Policemen/women,and all wanafiki na wachumia tumbo.

    20. #18
      1800's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th December 2010
      Posts : 1,657
      Rep Power : 891
      Likes Received
      416
      Likes Given
      21

      Default

      Quote By Cynic
      Hizi ni kauli za mtu mwenye Ph.D.!! Aibu! Na inaonyesha hizo phd za UDSM ni za hovyo hovyo tu
      Huyu jamaha uwa ni mtu wa kujikomba kwa M.k.w.e.r.e siku zote,mtu msomi level ya phd unakua na kauli za ajabu namna hiyo?ana tofauti gani na layman anaeburuza mikokoteni?eti rais anaejua kiingereza,MANUFACTURING OF TEACHERS ndio kujua kiingereza sahihi?msomi una amini ushirikina tena katika zama za sayansi na teknolojia?no wonder ikulu inalindwa na kuongozwa kwa imani za kishirikina!anasifia kwenda nje kuomba, aibu gani hii??hakuona ile article jinsi Waingereza walivyomchambua na kumdharau kiongozi wetu mkuu?Magufuri ni bure kabisa,kujikomba na kuropoka kunamfanya azidi kujitia aibu na kua kichekesho tu

    21. #19
      hans79's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th May 2011
      Posts : 1,495
      Rep Power : 767
      Likes Received
      143
      Likes Given
      0

      Default Re: Siogopi kulogwa: Dk. Magufuli

      Mwenzake kamwambia unaitia hasara serikali kwa miradi ya muda mfupi na pia kamwambia ile sehemu ya kuchezea watoto,je hao watoto watacheza wapi?Hv jamani huwa pana kikao cha mawazir na mkiti ni jk,inakuwaje hadi waumbuane barabara?Na kwa nini hakumweleza jk kuwa pana uzembe hadi ayaseme barabarani?Kazi kwa sifa zitaleta matatizo,hii kweli serikali dhaifu.

    22. #20
      Tram Almasi's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 26th February 2009
      Location : Marsabit
      Posts : 753
      Rep Power : 671
      Likes Received
      217
      Likes Given
      92

      Default Re: Siogopi kulogwa: Dk. Magufuli

      Quote By Zamaulid
      inakuwaje anajishuku namna hii!!
      Inaelekea hyo jamaa anaempa za uso ndiyo zake kuroga wanaoingilia anga zake.
      "YouR MoST UNhaPPy CuSToMers ArE YoUr GREateST SOurCE Of LEarNInG"- BiLL GaTEs

    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...