Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: JK anoa panga CCM; WABUNGE WALIOWEKA SAINI KUMNG’OA PINDA KUKATWA NEC

    Report Post
    Results 1 to 15 of 15
    1. #1
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,153
      Rep Power : 3544
      Likes Received
      3037
      Likes Given
      460

      Default JK anoa panga CCM; WABUNGE WALIOWEKA SAINI KUMNG’OA PINDA KUKATWA NEC



      • WABUNGE WALIOWEKA SAINI KUMNG’OA PINDA KUKATWA NEC

      na Mwandishi wetu

      PANGA la vikao vya juu vya mchujo ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), limenolewa.


      Vikao hivyo vya mwisho vya mchujo ambavyo vitaendeshwa na Mwenyekiti wake taifa, Rais Jakaya Kikwete, vinatarajia kuanza rasmi Septemba 21 na 26.

      Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili, umebaini kuwa wakati vikao hivyo vikianza, CCM imepanga mkakati mzito kukata majina ya baadhi ya wagombea uongozi ambao pia ni wabunge ndani ya Bunge la Muungano.


      Kundi lingine la walengwa wa mkakati ule ni la viongozi wa CCM hasa wenyeviti wa mikoa na wilaya waliokuwa wakiendeleza makundi na malumbano na kusababisha kuporomoka kwa hadhi ya chama hicho.


      Habari zaidi kutoka ndani ya CCM, zinasema kuwa NEC imepanga kufanya maamuzi magumu ya kuwakata baadhi ya wagombea waliokuwa wakiandamwa na tuhuma za ufisadi hata kama watakuwa wamepita bila kupingwa au kupitishwa na vikao vya chini.


      Tayari Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge, mmoja kati ya makada wanaoandamwa kwa tuhuma za ufisadi, amepita bila kupingwa wakati majeruhi mwingine wa ufisadi, Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa, amepitishwa na vikao vya chini, sasa wanasubiri idhini ya NEC.


      Duru za siasa kutoka ndani ya CCM, zinasema kuwa wabunge wanaolengwa kwenye panga hilo ni wale waliokuwa kimbelembele kuikosoa serikali bungeni na kufikia hatua ya kusaini majina yao kwenye fomu zilizokuwa zikipitishwa na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, ili kupata saini 70 za kumng’oa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.


      Tayari athari za saini za kutaka kumng’oa Waziri Pinda zimeshaonekana kwa Mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono ambaye hivi karibuni alienguliwa katika kikao cha mchujo wilayani na yeye kutahadharisha kama jina lake halitapitishwa NEC, ndani ya CCM patachimbika.


      Mkono ambaye ni wakili maarufu nchini, aliwania nafasi ya Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazee taifa. Wengine waliowania nafasi hiyo ni Mbunge wa Bukoba Vijijini, Joson Rweikiza, Matha Mlata na Salum Chicago.


      Waliopendekezwa na vikao vya chini kuwania kiti hicho ni Abdallah Bulembo, Matha Mlata na Halima Mamuya.


      Kwa upande wa Umoja wa Wanawake, waliopendekezwa ni pamoja na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sofia Simba, Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango na Mayrose Kavura Majinge.


      Mbunge mwingine aliyekwishaenguliwa na vikao vya chini ni Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji na Uwezeshaji, Dk. Mary Nagu, ambaye alikuwa akichuana vikali na Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye.


      “Tunaambiwa wabunge wengi walioomba NEC watakatwa hasa wale waliotaka kumng’oa Pinda na sababu ya pili ni kwamba wabunge wana nafasi kumi za NEC ndani ya Bunge, hivyo hawana sababu ya kuwania NEC nje ya Bunge,” alisema mtoa habari wetu.


      Mkono, Nagu na wengine waliopendekezwa kuachwa na vikao vya chini, sasa wanategemea kudra za NEC.


      Mkoani Shinyanga, taarifa zinasema kuwa mgawanyiko umetokea baada ya kuwapo taarifa kwamba kuna mpango wa kulikata jina la mwenyekiti wa sasa wa CCM mkoa huo, Khamis Mgeja.


      Habari zinasema kuwa mkakati huo unapangwa na vigogo wa CCM kutoka ofisi ndogo ya makao makuu, Lumumba, jijini Dar es Salaam na kumhusisha mtoto wa kigogo.


      Hatua hiyo imedaiwa kuwa ni moja ya mikakati ya viongozi hao kupanga safu ya uongozi mwaka 2015 ambapo Mgeja anatajwa kuwa mmoja wa watu anaopingana nao hivyo kuwa kikwazo katika kufanikisha mipango yao.


      Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana kutoka kwa baadhi ya wana CCM mjini hapa, inadaiwa kwamba vigogo hao hivi sasa wanajitahidi kuwashawishi wajumbe wa vikao vya juu ili kuhakikisha jina la Mgeja linakatwa na linabakizwa la mtu ambaye ni chaguo lao.


      Yapo madai kwamba mkakati wa vigogo hao unaungwa mkono na baadhi ya wabunge wa CCM mkoani Shinyanga ambao hawamuungi mkono Mgeja.


      Baadhi ya wachambuzi wa masuala ya kisiasa wamewaeleza waandishi wa habari mjini Shinyanga kwamba tayari kuna vikao vingi vya usiku vinavyofanywa na mawakala wa vigogo hao kwa lengo la kuhakikisha Mgeja hachaguliwi hata kama NEC itakuwa imerejesha jina lake.


      Katika hali isiyokuwa ya kawaida mmoja wa wagombea ambaye alipata fununu za jina lake kupendekezwa kuwa miongoni mwa wagombea nafasi ya uenyekiti wa mkoa, aliamua kufanya sherehe kubwa katika moja ya baa eneo la Lubaga ambako alisikika akitamba kwamba yeye ni chaguo la Rais Jakaya Kikwete.


    2. Study Abroad

    3. #2
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,153
      Rep Power : 3544
      Likes Received
      3037
      Likes Given
      460

      Default Re: JK anoa panga CCM; WABUNGE WALIOWEKA SAINI KUMNG’OA PINDA KUKATWA NEC

      Hakuna Demokrasia ndani ya CCM; Sasa Mkono ni FISADI kwanini na wengine Wamepita? CHENGE n.w

      Msicheze na ZITTO KABWE ndio aliyeanzisha... wa CCM ni scape goat... Kikwete kafurahi kapata wa kutupa nje ya NEC



    4. #3
      Kimbunga's Avatar
      JF Platinum Member Array
      Join Date : 4th October 2007
      Location : Kisiwani Juma
      Posts : 7,472
      Rep Power : 6167
      Likes Received
      3038
      Likes Given
      1015

      Default Re: JK anoa panga CCM; WABUNGE WALIOWEKA SAINI KUMNG’OA PINDA KUKATWA NEC

      Hivi Filikunjombe naye anagombea NEC? Huu ni mtihani mwingine kwa CCM yaani mtu apite bila kupingwa halafu jina lake lisirudishwe? Naona CCM wanataka kusababisha vita y majimaji!
      Wambugani likes this.

    5. #4
      bagwell's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 19th September 2012
      Posts : 113
      Rep Power : 357
      Likes Received
      25
      Likes Given
      0

      Default Re: JK anoa panga CCM; WABUNGE WALIOWEKA SAINI KUMNG’OA PINDA KUKATWA NEC

      Huyo mtoto wa kigogo hakuna mwengine isipokua Prince Ridhwan mna yeye na Nape Nauye wameigeuza CCM kama mali yao ila kila lenye mwanzo halikosi kua na mwisho...CCM Oyeeeeeeeeeeeeee

    6. #5
      Mzalendo JR's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th June 2012
      Posts : 900
      Rep Power : 530
      Likes Received
      274
      Likes Given
      212

      Default Re: JK anoa panga CCM; WABUNGE WALIOWEKA SAINI KUMNG’OA PINDA KUKATWA NEC

      Kwa maelezo haya nashawishika kutambua kua katika usukaji wa jopo la mawaziri lililowaondoa kina Ngeleja and Co halikuwafurahisha.

      Na pia nashawishika waliteuliwa kiushkaji/undugu au ujamaa wa karibu na si utendaji. Ili kumuokoa W/Mkuu ilimbidi kuunda upya jopo la Mawaziri ili kukata maneno ya Watanzania.

      Kisasi ndio historia ya huyu jamaa kama mnakumbuka mwanamziki maarufu anaeozea jera kuna tetesi kisa kilianzia wakati hajawa Mkuu, alipopata rungu tu kasuka kilichompotezea jera.

      Auae kwa panga nae atapitia hapohapo!
      "Happiness is what you think, what you say, and what you do are in harmony"

    7. Miaka 50

    8. #6
      NICE LAMECK's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 2nd April 2012
      Posts : 206
      Rep Power : 400
      Likes Received
      26
      Likes Given
      37

      Default Re: JK anoa panga CCM; WABUNGE WALIOWEKA SAINI KUMNG’OA PINDA KUKATWA NEC

      Haya yetu macho.

    9. #7
      Lyimo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th March 2006
      Posts : 1,799
      Rep Power : 1525
      Likes Received
      796
      Likes Given
      450

      Default Re: JK anoa panga CCM; WABUNGE WALIOWEKA SAINI KUMNG’OA PINDA KUKATWA NEC

      Kama hili likibainika kufanywa kwa madhumuni ya kuwaengua waliopinga malfunctioning ya serikali, basi nashawishika kusema hapo ndiyo CCM itazidi kujichimbia kaburi. Wengi wetu tumebakiwa na chembechembe za kuiamini CCM na serikali yake sababu tu ya hawa wachache sana wasiokubaliana na maovu/hujuma ndani ya chama na serikali. Pia wakilitekeleza hill, basi tutadhihirisha ya kuwa CCM na serikali yake haitusimamii hyena wannchi, bali ipod kwa ajili ya mutants ufisadi na kulinda ufisadi kwa nguvu zote.
      "Wisdom is not a product of schooling, but of the lifelong attempt to acquire it"

    10. #8
      Mamndenyi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 11,892
      Rep Power : 31775
      Likes Received
      5873
      Likes Given
      19165

      Default Re: JK anoa panga CCM; WABUNGE WALIOWEKA SAINI KUMNG’OA PINDA KUKATWA NEC

      ni funika kombe mwanaharamu apite tu hii.
      hata riziwana na maza wake wawepo kwenye kundi la mafisadi pia.
      SIYO WOTE WANAOTANGATANGA WAMEPOTEA

    11. #9
      Daudi Mchambuzi's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 25th November 2010
      Posts : 6,175
      Rep Power : 0
      Likes Received
      2994
      Likes Given
      13624

      Default JK anoa panga CCM; WABUNGE WALIOWEKA SAINI KUMNG’OA PINDA KUKATWA NEC

      Wacha wafu wazike wafu wao.

      Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums

    12. #10
      samora10's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st July 2010
      Location : Kwa-Gude
      Posts : 3,252
      Rep Power : 1102
      Likes Received
      729
      Likes Given
      1163

      Default Re: JK anoa panga CCM; WABUNGE WALIOWEKA SAINI KUMNG’OA PINDA KUKATWA NEC

      CCM wanamalizia miaka yao mitatu iliyobaki.. Wacheni wafanye walitakalo
      ''Mipango na Mikakati imekamilika na sasa tuko kwenye mchakato wa mazungumzo na wafadhili"- M Pinda

    13. #11
      Takalani Sesame's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th June 2008
      Location : Mobile
      Posts : 545
      Rep Power : 665
      Likes Received
      137
      Likes Given
      98

      Default Re: JK anoa panga CCM; WABUNGE WALIOWEKA SAINI KUMNG’OA PINDA KUKATWA NEC

      Mshua mwenyekiti, waifu mgombea ujumbe NEC bila kupingwa so far, mtoto uvccm. Tutafika tu.
      Those who make peaceful revolution impossible will make violent revolution inevitable.
      John F. Kennedy

    14. #12
      Narubongo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd November 2010
      Posts : 1,886
      Rep Power : 810
      Likes Received
      842
      Likes Given
      680

      Default Re: JK anoa panga CCM; WABUNGE WALIOWEKA SAINI KUMNG’OA PINDA KUKATWA NEC

      - bado swala la uwiano ndani ya chama
      - nguvu ya mtandao
      - mambo yetu yale
      "Chadema kinatumia alama ya vidole viwili kama manati, manati kamwe haiwezi kuua tembo" Livingstone Lusinde (2012)

    15. #13
      BASHADA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th July 2011
      Posts : 434
      Rep Power : 483
      Likes Received
      107
      Likes Given
      80

      Default Re: JK anoa panga CCM; WABUNGE WALIOWEKA SAINI KUMNG’OA PINDA KUKATWA NEC

      Mpaka nimecheka aisee. Wenye tuhuma za mafisadi out, Wenye kiherehere kutetea maslahi ya wananchi out. Wanabaki wale wakimya wanaotetea maslahi ya Kiwete na familia yake. Very good move towards the grave. 2015 tutakuja kuweka shada la maua kwenye kaburi la CCM
      eedoh05 likes this.
      WAO WANA PESA SISI TUNA MUNGU. WAO WANA NGUVU YA DOLA SISI TUNA NGUVU YA UMMA.

    16. #14
      Emma.'s Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th June 2012
      Posts : 831
      Rep Power : 513
      Likes Received
      102
      Likes Given
      0

      Default Re: JK anoa panga CCM; WABUNGE WALIOWEKA SAINI KUMNG’OA PINDA KUKATWA NEC

      Kaburi la ccm lipo karibu kumalizika 2015 ndo tamati yao hawa wahuni

    17. #15
      Njowepo's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 26th February 2008
      Location : Santiago
      Posts : 7,591
      Rep Power : 22053
      Likes Received
      992
      Likes Given
      769

      Default Re: JK anoa panga CCM; WABUNGE WALIOWEKA SAINI KUMNG’OA PINDA KUKATWA NEC

      Ccm watakuwa wanapoteza mda bse kwa siasa za sasa watakaotemwa wana pa kwenda

    18. FemaTV & Radio

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...