Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Mkapa arusha kombora; Awashutumu viongozi wa dini, Serikali

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 23
    1. #1
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,246
      Rep Power : 3564
      Likes Received
      3069
      Likes Given
      463

      Default Mkapa arusha kombora; Awashutumu viongozi wa dini, Serikali

      JUMATANO, SEPTEMBA 19, 2012 08:49 NA DEBORA SANJA, DODOMA

      *Awashutumu viongozi wa dini, Serikali
      *Asema viongozi wastaafu hawathaminiwi
      RAIS mstaafu, Benjamin Mkapa, ameibuka na kusema kuwa, hivi sasa baadhi ya viongozi wa Serikali na viongozi wa dini, wamekuwa hawawathamini na kuwajali viongozi wastaafu.

      Amesema hali hiyo imekuwa ikitafsiriwa na kuonekana kuwa, viongozi hao hawana jipya mbele ya jamii.

      Rais Mkapa alitoa kauli hiyo mjini hapa jana alipokuwa akihutubia katika ibada maalumu ya kumbukumbu ya miaka 40 ya uaskofu wa Askofu Mstaafu Mathias Isuja wa Jimbo Katoliki Dodoma.

      Mkapa alisema, kuna dhana iliyojengeka, kuwa viongozi waliostaafu wanakuwa hawana jipya na hawathaminiwi tena kutokana na kustaafu kwao kwa mujibu wa sheria.

      “Hivi sasa imezuka tabia kwa baadhi ya viongozi wa nchi na makanisa kuona kuwa mtu akistaafu basi anakosa hekima.

      “Mtu akistaafu anaonekana kuwa ni mufilisi tu asiye na kitu na nataka mfahamu kuwa, kustaafu siyo kuchoka na wala michango ya wastaafu siyo mibovu bali inatakiwa kuangaliwa,’’ alisema Rais mstaafu Mkapa.

      Aidha, alisema nchi imekuwa ikikumbwa na matatizo kutokana na ubishi na ujuaji wa wananchi hali inayosababisha nchi isipige hatua ipasavyo katika maendeleo.

      “Siku hizi watu hawaambiliki na chimbuko kubwa la matatizo ni ujuaji mwingi, kila mtu anaamini kuwa anajua, na hili jambo ni la hatari.

      “Wengine hawakuwapo wakati nchi hii inapata uhuru na hata wakati uhuru unapiganiwa, wao waliikuta nchi ikiwa huru.

      “Lakini utakuta wanasimulia mambo mengi ambayo hata hawayajui na hayana msingi wowote,” alisema Mkapa.

      Aliwataka pia viongozi kujenga tabia ya kujifunza bila kuchoka na kwamba viongozi lazima wawe mfano kwa kupenda kusoma.

      Akimzungumzia Askofu Isuja, Mkapa alisema Isuja alikuwa ni kiunganishi cha wananchi wa Dodoma pamoja na Tanzania, kwani alipenda kufanya kazi zake kwa uwazi na ukweli wakati wote. Mimi namfananisha Askofu Isuja na mtumishi mwema katika shamba la bwana,” alisema.

      Kwa upande wake, Askofu Isuja aliwashukuru maaskofu wote, mapadre, watawa, waumini wa Kanisa Katoliki wakiwamo wa Jimbo la Dodoma na Serikali kwa kipindi chote walichompa ushirikiano wakati akitumikia Jimbo la Dodoma.

      Askofu Isuja pia alihimiza amani nchini na kuwataka Watanzania kuwa na upendo bila kujali ubaguzi wowote miongoni mwao.

      Mbali na viongozi hao, katika ibada hiyo alikuwapo pia Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycap Kardinali Pengo ambaye ndiye aliyeongoza ibada.

      Walikuwapo pia viongozi mbalimbali wa Kanisa Katoliki nchini, pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali.

      ENGINEERSJYC likes this.

    2. Miaka 50

    3. #2
      Jasusi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th May 2006
      Posts : 10,625
      Rep Power : 2893
      Likes Received
      3844
      Likes Given
      12244

      Default Re: Mkapa arusha kombora; Awashutumu viongozi wa dini, Serikali

      Mkapa anataka wamjali kwa lipi? Siye yeye aliyefuga na kukuza ufisadi na kusaidia kumweka Kikwete mamlakani?
      Sasa kama hujaacha legacy nzuri tukuthamini kwa lipi?
      BAK, jmushi1, Ndinani and 1 others like this.

    4. #3
      denoo49's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th March 2011
      Location : Kijijini
      Posts : 739
      Rep Power : 756
      Likes Received
      138
      Likes Given
      20

      Default Re: Mkapa arusha kombora; Awashutumu viongozi wa dini, Serikali

      Jamaa kadiri siku zinavyokimbia kuelekea 2015 ndo'anavyozidi kuchangayikiwa na kutokwa "POVU".
      Kwa hiyo alitaka walioipatia nchi uhuru ndo'waopekee wazungumzie kuhusu uhuru, sasa nini maana ya kua na historia? Na anataka watakaosimulia hiyo histora wawe wakina nani?
      Mbona linapokuja swalia la MGODI KIWILA NA MCHUCHUMA, hatoi hayo maneno yake....!

    5. BAK
      #4
      BAK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2007
      Location : Mfaranyaki
      Posts : 26,619
      Rep Power : 44968
      Likes Received
      8370
      Likes Given
      8347

      Default Re: Mkapa arusha kombora; Awashutumu viongozi wa dini, Serikali

      Huyu fisadi Mkapa alipokuwa madarakani aliwathamini wastaafu au alikuwa busy kuwaibia Watanzania? Mbona alishindwa kuwalipa wastaafu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

      Quote By Jasusi
      Mkapa anataka wamjali kwa lipi? Siye yeye aliyefuga na kukuza ufisadi na kusaidia kumweka Kikwete mamlakani?
      Sasa kama hujaacha legacy nzuri tukuthamini kwa lipi?
      Jasusi likes this.
      Let your graceful words fly out into the World, carried on winds of courage, imagination and joy. Let them inspire others to step into action

    6. #5
      Foum Jnr's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 27th July 2012
      Location : UK
      Posts : 157
      Rep Power : 375
      Likes Received
      76
      Likes Given
      76

      Default Re: Mkapa arusha kombora; Awashutumu viongozi wa dini, Serikali

      maneno yake yanaonyesha mambo asiokubaliana nayo yeye:-
      a) Kuupinga uhuru wa wananchi wa kushiriki katika maamuzi yanayowahusu. Unaposema kila mtu mjuaji unaashiria masuala ya ujuzi ni ya elite maalum, wengine hawana maana. kauli potufu and undemocratic kama ulivyokuwa utawala wake wa wataalamu wengi waliowazuia wananchi kujua ili kuiifisidi nchi kwa muongozo wa matumbo yao.

      b) Kama kutowajali pensioners, yeye kachangia pa kubwa katika kupuuza malalamiko ya pensioners hata wale wa EAC iliyovunjwa, jee aliwasaidia nini alipokuwa madarakani? Kama ni kwa viongozi waliomtangulia basi na ajiulize yeye mwenyewe perception yake kwa mzee mwinyi wakati ule, ajitathmini zaidi hii culture ieanza wapi kama si kwake?

      c) sioni kama ana-lecture ya kuwapa watanzania kwa sasa, credibility yake sio nzuri kutokana na history ya utawala wake, nilishangaa juzi Mh Sumae akikemea jeshi la polisi kwa kumuua Mwagosi wakakti alipokuwa yeye mtawala na wenzake watu zaidi ya kumi waliuliwa na jeshi la polisi baada ya ku-protest election result, hizi ndio legacy zao ambazo wametuachia watanzania kama mfumo wa kutawaliwa, sasa unalalalamika nini?

      Wakati wa kuhadaa wananchi umepitwa, watulie tu wakalime vijijini na kuwa neutral ili kujenga heshima zao upya.

    7. RukaaJuu Final

    8. #6
      bagwell's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 19th September 2012
      Posts : 113
      Rep Power : 358
      Likes Received
      25
      Likes Given
      0

      Default Re: Mkapa arusha kombora; Awashutumu viongozi wa dini, Serikali

      Hana lolote yeye ndio aliekua kinara wa kutowajali wastaafu na badala yake alihalalisha rushwa kua maji ya kunywa...ati wamjali kwa lipi wamjali?

    9. #7
      Mwanaweja's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th February 2011
      Posts : 3,481
      Rep Power : 1116
      Likes Received
      469
      Likes Given
      958

      Default Re: Mkapa arusha kombora; Awashutumu viongozi wa dini, Serikali

      Mkapa ameishiwa point maana yeye alikuwa rais ndie aliyetupatia huu ulengelenge tulio nao na udhaifu unaotusumbua na kututumbukiza kwenye janga la umaskini kiasi kama hiki. alijua kabisa ndio maana ni bora kutumia uongozi huku ikijua siku moja utakuwa mitaani kama yeye leo hayuko kwenye system leo hii anaona madudu lakini alipokuwa kwenye system hakuona hayo yote.

    10. #8
      WildCard's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd April 2008
      Posts : 6,453
      Rep Power : 1979
      Likes Received
      1797
      Likes Given
      59

      Default Re: Mkapa arusha kombora; Awashutumu viongozi wa dini, Serikali

      Katika watu wa kunyonga na kutupa baharini ni Mkapa na aliyekuwa AG wake, Chenge. Mikataba yote MIBOVU, sheria ya sasa ya TAKUKURU na ujinga wa kujiuzia nyumba za serikali kaufanya Mkapa. Leo hii anasimama kwenye mimbari ya makanisa anataka aombwe ushauri upi? Kapata akili mpya wapi?
      Jasusi and Richard like this.

    11. #9
      Manyi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th December 2011
      Posts : 1,731
      Rep Power : 723
      Likes Received
      292
      Likes Given
      263

      Default Re: Mkapa arusha kombora; Awashutumu viongozi wa dini, Serikali

      Hatuna haja ya kuwakumbuka viongozi mafisadi na wezi, waliotuletea hasara katika nchi yetu. Ajiulize mbona Nyerere anakumbukwa na alikuwa anaheshimiwa? hana jipya! Kauza nchi huyu na kuuza madini na mikataba ya ajabu ambayo sana ilaleta shida!

    12. #10
      andrewk's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th April 2010
      Posts : 2,228
      Rep Power : 908
      Likes Received
      283
      Likes Given
      60

      Default Re: Mkapa arusha kombora; Awashutumu viongozi wa dini, Serikali

      Tatizo ni marais wetu kuwa wenyeviti wa vyama vyao, wanapokuwa madarakani wanasimamia vyote, serikali ikigaribu hakuna wa kumraumu, sasa leo atakuja na jipya lipi watu wakamsikiliza? hana mvuto kama Late Mwl Nyerere, kichwa kilikuwa kizuri na alikuwa na ushawishi kubwa sana, alitete hoja zake viziri na zikakubarika

    13. #11
      Ronal Reagan's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th November 2010
      Posts : 2,636
      Rep Power : 961
      Likes Received
      615
      Likes Given
      256

      Default Re: Mkapa arusha kombora; Awashutumu viongozi wa dini, Serikali

      They should EARN the respect they want.

      Otherwise let their kids and family just give the normal and traditional and social respects. But if he want the respect of the public, Mkapa and all leaders are herein categorically advised to work for it.

      Unless Bw. Mkapa analalamikia watu wake wa karibu kutomjali na kumheshimu. Kama ndivyo basi tutamshauri JK aunde tume kuchunguza na pia Bunge liunde Kamati ili kupitia mapendekezo ya hiyo Tume kabla ya uwasilishaji wa siri kwa Mkapa.
      Last edited by Ronal Reagan; 20th September 2012 at 10:50. Reason: editing

    14. Deo
      #12
      Deo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th November 2008
      Posts : 521
      Rep Power : 641
      Likes Received
      89
      Likes Given
      7

      Default Re: Mkapa arusha kombora; Awashutumu viongozi wa dini, Serikali

      Akumbuke aliyowafanyia wale wazee wetu wastaafu wa jumuia ya Afrika mashariki.

      Michango gani yeye anayo? Wizi, ufisadi au kusema uongo kuwa fulani si mwanafamilia?

      Kaa na aibu yako mzee, usiamshe hasira za watu

    15. #13
      Njaare's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th September 2010
      Posts : 570
      Rep Power : 661
      Likes Received
      92
      Likes Given
      168

      Default Re: Mkapa arusha kombora; Awashutumu viongozi wa dini, Serikali

      Quote By nngu007
      JUMATANO, SEPTEMBA 19, 2012 08:49 NA DEBORA SANJA, DODOMA

      *Awashutumu viongozi wa dini, Serikali
      *Asema viongozi wastaafu hawathaminiwi
      RAIS mstaafu, Benjamin Mkapa, ameibuka na kusema kuwa, hivi sasa baadhi ya viongozi wa Serikali na viongozi wa dini, wamekuwa hawawathamini na kuwajali viongozi wastaafu.

      Amesema hali hiyo imekuwa ikitafsiriwa na kuonekana kuwa, viongozi hao hawana jipya mbele ya jamii.

      Rais Mkapa alitoa kauli hiyo mjini hapa jana alipokuwa akihutubia katika ibada maalumu ya kumbukumbu ya miaka 40 ya uaskofu wa Askofu Mstaafu Mathias Isuja wa Jimbo Katoliki Dodoma.

      Mkapa alisema, kuna dhana iliyojengeka, kuwa viongozi waliostaafu wanakuwa hawana jipya na hawathaminiwi tena kutokana na kustaafu kwao kwa mujibu wa sheria.

      “Hivi sasa imezuka tabia kwa baadhi ya viongozi wa nchi na makanisa kuona kuwa mtu akistaafu basi anakosa hekima.

      “Mtu akistaafu anaonekana kuwa ni mufilisi tu asiye na kitu na nataka mfahamu kuwa, kustaafu siyo kuchoka na wala michango ya wastaafu siyo mibovu bali inatakiwa kuangaliwa,’’ alisema Rais mstaafu Mkapa.

      Aidha, alisema nchi imekuwa ikikumbwa na matatizo kutokana na ubishi na ujuaji wa wananchi hali inayosababisha nchi isipige hatua ipasavyo katika maendeleo.

      “Siku hizi watu hawaambiliki na chimbuko kubwa la matatizo ni ujuaji mwingi, kila mtu anaamini kuwa anajua, na hili jambo ni la hatari.

      “Wengine hawakuwapo wakati nchi hii inapata uhuru na hata wakati uhuru unapiganiwa, wao waliikuta nchi ikiwa huru.

      “Lakini utakuta wanasimulia mambo mengi ambayo hata hawayajui na hayana msingi wowote,” alisema Mkapa.

      Aliwataka pia viongozi kujenga tabia ya kujifunza bila kuchoka na kwamba viongozi lazima wawe mfano kwa kupenda kusoma.

      Akimzungumzia Askofu Isuja, Mkapa alisema Isuja alikuwa ni kiunganishi cha wananchi wa Dodoma pamoja na Tanzania, kwani alipenda kufanya kazi zake kwa uwazi na ukweli wakati wote. Mimi namfananisha Askofu Isuja na mtumishi mwema katika shamba la bwana,” alisema.

      Kwa upande wake, Askofu Isuja aliwashukuru maaskofu wote, mapadre, watawa, waumini wa Kanisa Katoliki wakiwamo wa Jimbo la Dodoma na Serikali kwa kipindi chote walichompa ushirikiano wakati akitumikia Jimbo la Dodoma.

      Askofu Isuja pia alihimiza amani nchini na kuwataka Watanzania kuwa na upendo bila kujali ubaguzi wowote miongoni mwao.

      Mbali na viongozi hao, katika ibada hiyo alikuwapo pia Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycap Kardinali Pengo ambaye ndiye aliyeongoza ibada.

      Walikuwapo pia viongozi mbalimbali wa Kanisa Katoliki nchini, pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali.


      Ha ha haaaaaa! Huyu Mzee kasahau ule msemo wa "Fainali uzeeni".

      Akumbuke pia pia kuwa mwalimu Nyerere alitufundisha kuwa Heshma ya mtu itokane na huduma yake kwa jamii. Kama huduma yako haikuwa muafaka watu watakuheshimu ukiwa madarakani kwa sababu umeshika mpini. Ukiachia madaraka utaonekana kama takataka.

      Ushauri wa bure kwa walioshikilia madaraka nikuwa wakumbuke kuwa fainali ni uzeeni. Kama ulikuwa huna busara ukiwa kazini hatutategemea uwe na hekima ukistaafu.

    16. #14
      Kibagata's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st April 2012
      Posts : 522
      Rep Power : 464
      Likes Received
      71
      Likes Given
      16

      Default Re: Mkapa arusha kombora; Awashutumu viongozi wa dini, Serikali

      Mwizi tu huyo.

    17. #15
      Wile GAMBA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th September 2011
      Posts : 529
      Rep Power : 494
      Likes Received
      158
      Likes Given
      600

      Default Re: Mkapa arusha kombora; Awashutumu viongozi wa dini, Serikali

      hatumpi nafasi asituletee tene uabe wake wa kimacjinga, ukiona mtu anajialika kwenye sherehe ujue kaishiwa

    18. Ame
      #16
      Ame's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th March 2011
      Location : Global Citizen
      Posts : 1,513
      Rep Power : 1184
      Likes Received
      650
      Likes Given
      2615

      Default Re: Mkapa arusha kombora; Awashutumu viongozi wa dini, Serikali

      Quote By Jasusi
      Mkapa anataka wamjali kwa lipi? Siye yeye aliyefuga na kukuza ufisadi na kusaidia kumweka Kikwete mamlakani?
      Sasa kama hujaacha legacy nzuri tukuthamini kwa lipi?
      Nadhani roho aliyobeba huyu binadamu na mimi ni contrary kama yeye ana holly basi mm nipo opposite ya roho aliyowanayo. Kila mara nikimsikiliza ananikwaza kabisa...yeye ndiye mjuaji kama aliweza kuita raia wenzake wanwivu wa kike what kind of person is he? Kama yeye alishindwa kuheshimu raia nani atamheshimu yeye? Kila action ina reaction yeye anapata reaction ya action zake.
      Jasusi likes this.

    19. #17
      Njoka Ereguu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th April 2012
      Posts : 503
      Rep Power : 459
      Likes Received
      167
      Likes Given
      30

      Default Re: Mkapa arusha kombora; Awashutumu viongozi wa dini, Serikali

      Siku hizi watu hawaambiliki na chimbuko kubwa la matatizo ni ujuaji mwingi, kila mtu anaamini kuwa anajua, na hili jambo ni la hatari.

      “Wengine hawakuwapo wakati nchi hii inapata uhuru na hata wakati uhuru unapiganiwa, wao waliikuta nchi ikiwa huru.

      “Lakini utakuta wanasimulia mambo mengi ambayo hata hawayajui na hayana msingi wowote,” alisema Mkapa.

      Pamoja na wengi kuona kuwa Mzee Makapa ameanza kuchoka kifikra, kauli hii hapa juu ni ya kweli na ndiyo sababu kubwa ya kukwamisha maendeleo ya nchi ambayo pia inatoa fursa kwa wachache kutumia mwanya huo kujinufaisha, tukubali tusikubali bila kubadiliaka maendeleo ni safari ambayo bado ni ndefu sana kwa Tanzania.

    20. #18
      genekai's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th February 2010
      Location : Loitering!
      Posts : 7,540
      Rep Power : 2088
      Likes Received
      1089
      Likes Given
      1575

      Default Re: Mkapa arusha kombora; Awashutumu viongozi wa dini, Serikali

      Ndo maana huwa hapendi kuongea hasa na vyombo vya habari kwa hofu ya kuwa "misquoted", inawezekana hata jambo lenyewe halikuwa kama lilivyoletwa hapa!!!!
      The future of this country is being jeopardized by the intellectual slavery of our top leaders

    21. #19
      Takalani Sesame's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th June 2008
      Location : Mobile
      Posts : 548
      Rep Power : 666
      Likes Received
      139
      Likes Given
      99

      Default Re: Mkapa arusha kombora; Awashutumu viongozi wa dini, Serikali

      Mkapa hana moral authority ya kuwaasa watanzania jambo lolote. Dhambi yake ya kugawa bure mashirika ya umma kwa kisingizio cha ubinafsishaji bado hatujasahau. Mikataba mibovu iliyoingiwa wakati wa utawala wake kwenye sekta ya madini bado ni maumivu makali kwa watanzania. Na pia asifikiri kuwa sisi hatujui kuwa yeye ndie muasisi wa upigaji mkubwa (ufisadi) na kupitia kwake pesa za EPA zilikwapuliwa kusaidia CCM 2005. Mkapa hana budi kwa sasa kukaa kimya na kupumzika na ashukuru JK kaamua 'kumuacha apumzike'.
      Usually when people are sad they don't do anything. They just cry over their condition. But when they get angry they bring about a change. Malcolm X

    22. #20
      bahatil mselle's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 11th November 2011
      Posts : 5
      Rep Power : 381
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default Re: Mkapa arusha kombora; Awashutumu viongozi wa dini, Serikali

      Hana jipya huyo. Laana ya ufisadi aliofanya mauaji ya Wapemba katika utawala wake imeanza kumtafuna na ameanza kuchanganyikiwa. Tutasikia mengi zaidi kadiri atakavyozidi kuchanganyikiwa.
      AKUMBUKE MALIPO NI HAPAHAPA DUNIANI.

    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...