Mkuu Form 6, nadhani hujamwelewa MM, jana BBC swahili service, waliwa interview watu 3, Waziri Prof Mulugo, Zitto Zuberi Kabwe na mtu 1 toka Kenya, issue ilikuwa ni rasilimali za Africa hasa Madini while Africa hiyo hiyo inakuwa masikini, Waziri Mulugo alijitetea kuwa shida ya Africa including Tanzania ni elimu, hapo ndo inapokuja hoja ya MM, je hivi ni kweli tuliingia mkenge kwenye mikataba hiyo kwasababu ya Elimu? Hata mimi nakataa, issue sio Elimu, kama ni elimu, kuna akina Andrew Chenge, huyu kasoma nadhani Marekani if not England, Dr. Harrison Mwakyembe, digree zake zingine kachukulia Ujerumani, Prof. Shivji n.k, wote hawa ni watu waliobobea katika taaluma hii ya sheria, shida kubwa ya Africa sio elimu ya mikataba, shida ya Africa ni ufisadi na 10%.
Nimeajiliwa na makampuni ya nje mara kadhaa, tena nimekua ninafanya kazi na watu wa mataifa tofauti, Ulaya, Africa kusini, America, Australia, Wafaransa n.k, asilimia kubwa ya hawa wanaokuja huku sometimes hata kusaini hiyo mikataba ni watu ambao wana elimu ya kawaida mno, wengine hata Degree ukweli hawana, kitu cha ajabu nilicho kiona, Viongozi wetu hao mnao waita ni ma dokta na maprofesa utakuta wanawaogopa kweli hadi unashangaa, angalieni siku ili George W. Bush alivyokuja Tanzania, hadharani kabisa Kikwete na yeye Bush walisainiana mkataba fulani mbele ya kamera za Televison, hivi kuna mtu anaweza kujua kilicho kuwepo kwenye ule mkataba? kama pia niona vizuri, mkataba ulitoka Marekani, Kikwete hata hakupewa muda wa kuusoma na may be i seek ushauri kwa watu wake ili wamwambie kitu, muda huo haukuwepo, kilichotokea, Bush akasini then Kikwete naye akatakiwa kusaini, mwisho, hapo unategemea nini? Hivi kama iliandikwa kwa mfano, "Sehemu yote ya Kigamboni kuanzia mwaka huu itakuwa ni sehemu ya Marekani" then Kikwete kwakua hakusoma huo mkataba mwanzoni, then akiwa Ikulu na copy ya mkataba akakiona hico kipengere, unadhani atafanya nini, issue sio elimu, ni umakini na ufisadi tu ndio unateketeza Africa, sometimes nakubaliana na tusi tulilowahi kutukanwa na Peter Botha, rais wa zamani Africa kusini (enzi za ubaguzi) alisema, "Mtu mweusi hana uwezo wa kupanga mipango inayo zidi mwaka 1, akili hiyo hana" anaye pingana na hili aje na jibu hili, kwanini kila sehemu duniana wanapo ishi watu weusi eneo hilo ni masikini?
Follow Us Here