Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: CCM Yakiri dhahiri kuelemewa kwa kasi.

    Report Post
    Results 1 to 15 of 15
    1. #1
      ChescoMatunda's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th January 2009
      Location : dar tz
      Posts : 255
      Rep Power : 579
      Likes Received
      31
      Likes Given
      44

      Default CCM Yakiri dhahiri kuelemewa kwa kasi.

      CHAMA cha Mapinduzi (CCM), sasa kimekiri kuelemewa na wimbi la kukimbiwa na wanachama wake hususan vijana wanaojiunga na vyama vya upinzani baada ya kuona matarajio yao hayapatikani ndani ya chama hicho.

      Kamanda wa Umoja wa Vijana wa CCM mkoa wa Mbeya Dk. Steven Mwakajumilo pamoja na kukiri hali hiyo, alionya kuwa ikiwa chama hicho kinataka kuendelea kuungwa mkono, lazima kichukue hatua za makusudi za kukabiliana na hali ngumu ya maisha ya Watanzania.

      Dk. Mwwakajumilo alisema hayo juzi wakati akiendesha harambee ya mfuko wa vijana wa chama hicho, katika kata ya Ihyela, jijini Mbeya.

      Alisema kuwa vijana wengi nchini kwa muda mrefu wamekuwa wakikabiliwa na matatizo ya kiuchumi, hivyo kuwakatisha tamaa.

      “Vijana wengi wamekimbilia upinzani pengine kwa kuona matarajio yao hayapatikani ndani chama, tunazo sera nzuri sana ndani ya CCM za kumkwamua kijana kiuchumi, lakini inawezekana wimbo tunaoimba ni tofauti na ule tunaoucheza,” alisema Dk. Mwakajumilo.

      Dk. Mwakajumilo ambaye pia ni mchumi na mtumishi wa Benki Kuu ya Tanzania alitoa wito kwa kila tawi la CCM mahali lilipo kujizatiti kwa kuanzisha vikundi vya vijana vya ujasiriamali ili kuwajengea uwezo wa kiuchumi sambamba na kulipatia uwezo tawi husika kufanya shughuli za maendeleo ya chama.

      “Kila tawi la CCM mahali lilipo lijizatiti kuanzisha vikundi vya ujasiriamali, ndipo litakuwa na uwezo hata wa kujenga nyumba na ofisi za chama,” alisema Dk. Mwakajumilo.

      Dk. Mwakajumilo aliahidi kufanya operesheni ya kuanzisha vikundi hivyo vya ujasiriamali katika kila tawi la CCM ndani ya kata ya Ihyela jijini Mbeya ili kuonyesha mfano wa uanzishwaji wa vikundi hivyo. Chanzo GAZETI (Tanzania daima).
      kila neno baya unenalo au ufanyalo sasa utatakiwa kutoa hesabu yake siku ya hukumu!!

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      mmwaisoba's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 20th May 2012
      Posts : 426
      Rep Power : 0
      Likes Received
      22
      Likes Given
      0

      Default Re: CCM Yakiri dhahiri kuelemewa kwa kasi.

      Tanzania Daima ni Gazeti la Freeman Mbowe. Huyu bwana amekiri sawa na Shibuda aliposema CHADEMA kunaminyoo tu hakuna watu wa kuchaguliwa Urais. SASA HII JAMII FORUM SI YA KUWEKA PROPAGANDA MUFILISI. Kama vijana wamekimbilia CHADEMA na Slaa utamwitaje maana naye ni ajuza aliyetoka CCM kukimbilia CHADEMA. Hapana shaka CHADEMA INATAPATAPA BAADA YA KUHADAA WAFADHILI WAKE KUWA INGECHUKUA NCHI 2010 IKAANGUKIA PUA SASA INAWEWESEKA MZIMU WA ZITTO KABWE NA SHIBUDA.

    4. #3
      mmwaisoba's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 20th May 2012
      Posts : 426
      Rep Power : 0
      Likes Received
      22
      Likes Given
      0

      Default Re: CCM Yakiri dhahiri kuelemewa kwa kasi.

      Kichwa Cha habari hakifanani na yaliyoandikwa kwa huyu jamaa wa CHAGA DEVELOPMENT MANIFESTOS ALIYEWEKA HII MADA, TOA MADA SIYO

    5. #4
      Mystery's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 8th March 2012
      Posts : 601
      Rep Power : 483
      Likes Received
      208
      Likes Given
      149

      Default Re: CCM Yakiri dhahiri kuelemewa kwa kasi.

      Quote By almasiomary
      Tanzania Daima ni Gazeti la Freeman Mbowe. Huyu bwana amekiri sawa na Shibuda aliposema CHADEMA kunaminyoo tu hakuna watu wa kuchaguliwa Urais. SASA HII JAMII FORUM SI YA KUWEKA PROPAGANDA MUFILISI. Kama vijana wamekimbilia CHADEMA na Slaa utamwitaje maana naye ni ajuza aliyetoka CCM kukimbilia CHADEMA. Hapana shaka CHADEMA INATAPATAPA BAADA YA KUHADAA WAFADHILI WAKE KUWA INGECHUKUA NCHI 2010 IKAANGUKIA PUA SASA INAWEWESEKA MZIMU WA ZITTO KABWE NA SHIBUDA.
      Kunywa pombe kabla ya kula, ndiyo matokeo yake haya!!

    6. #5
      Lyimo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th March 2006
      Posts : 1,799
      Rep Power : 1525
      Likes Received
      796
      Likes Given
      450

      Default Re: CCM Yakiri dhahiri kuelemewa kwa kasi.

      Tatizo lililopo ndani ya CCM yetu, hakuna hata mmoja wa kushaurika. Hapo Nikisubiri sawa na kumpigia mbuzi gitaa kwa ufundi wote.
      "Wisdom is not a product of schooling, but of the lifelong attempt to acquire it"

    7. Miaka 50

    8. #6
      BADILI TABIA's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 13th June 2011
      Location : DUNIANI
      Posts : 14,555
      Rep Power : 5614
      Likes Received
      6211
      Likes Given
      2281

      Default Re: CCM Yakiri dhahiri kuelemewa kwa kasi.

      wanadhani vikundi vya ujasiriamali ndo itarudisha vijana?
      Ccm inabidi ijisafishe taka zote, ije ikiwa safi nyeuoe ili wananchi waiamini, lakini kuanzisha vikundi vya ujasiriamali ilhali imejaa taka haisaidii

    9. #7
      JERO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th March 2012
      Posts : 362
      Rep Power : 435
      Likes Received
      26
      Likes Given
      0

      Default Re: CCM Yakiri dhahiri kuelemewa kwa kasi.

      Ccm bye bye mbwembwe zote chini n ful kunuka!Wanajifanya wajuaaaji kumbe ni hamneni,kaz wanayo!.Tumewapa kaza wameshdwa kufanya na kuleta maendeleo,je tutawaaminije!?,wanakimbilia udini,ukabila na ukanda kuwachafua wenzao,ccm ni dustbin tena isiyofaaa!

    10. #8
      kupelwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th August 2011
      Location : DAR-ES-SALAAM
      Posts : 456
      Rep Power : 482
      Likes Received
      120
      Likes Given
      31

      Default Re: CCM Yakiri dhahiri kuelemewa kwa kasi.

      Quote By almasiomary
      Tanzania Daima ni Gazeti la Freeman Mbowe. Huyu bwana amekiri sawa na Shibuda aliposema CHADEMA kunaminyoo tu hakuna watu wa kuchaguliwa Urais. SASA HII JAMII FORUM SI YA KUWEKA PROPAGANDA MUFILISI. Kama vijana wamekimbilia CHADEMA na Slaa utamwitaje maana naye ni ajuza aliyetoka CCM kukimbilia CHADEMA. Hapana shaka CHADEMA INATAPATAPA BAADA YA KUHADAA WAFADHILI WAKE KUWA INGECHUKUA NCHI 2010 IKAANGUKIA PUA SASA INAWEWESEKA MZIMU WA ZITTO KABWE NA SHIBUDA.
      mdau punguza hasira zenye wivu na husuda.Pasipo shaka nguvu ya chadema ni moto wa tipper na si upepo unaopita.Kukuonyesha kuwa nguvu yake ni kubwa, pamoja na ahadi nyingi arumeru mashariki , ccm iliangukia pua.angalia m4c inavyochangiwa mafdha na wanyonge, ndo hapo utathibitisha namna gani inakubalika.Hili halipingiki, tuchambue ukweli,ccm kipi cha maana imewatendea wakulima hasa wa mikoa ya kanda ya ziwa kwnye zao la pamba kuhusu bei ya zao hilo?ni blabla tu na kuwakatisha tamaa.Mpka wakulima wa korosho , walifikia kuandamana, wakati serikali ipo.je haya huoni yanawakera jamii?pia ufisadi mkubwa unapoibuliwa, na cdm kupigia kelele, ccm inapuuza na kusema propoganda, haya ndo yanayoipa nguvu cdm.Mdau acha wivu na porojo za kwenye mitandao

    11. #9
      HIMO's Avatar
      Member Array
      Join Date : 31st August 2012
      Posts : 25
      Rep Power : 343
      Likes Received
      8
      Likes Given
      4

      Default Re: CCM Yakiri dhahiri kuelemewa kwa kasi.

      ccm kwishney hata gadaffi alikuwa anaambiwa nchi inaondoka anabisha

    12. #10
      WAHEED SUDAY's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th June 2011
      Posts : 2,843
      Rep Power : 2970
      Likes Received
      479
      Likes Given
      315

      Default

      Quote By Lyimo
      Tatizo lililopo ndani ya CCM yetu, hakuna hata mmoja wa kushaurika. Hapo Nikisubiri sawa na kumpigia mbuzi gitaa kwa ufundi wote.
      well said mkuu

    13. #11
      Mwanaweja's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th February 2011
      Posts : 3,451
      Rep Power : 1109
      Likes Received
      457
      Likes Given
      928

      Default Re: CCM Yakiri dhahiri kuelemewa kwa kasi.

      ccm hawaamini ila kumesha kucha kama wanaakili watakuwa kama KANU ilivyopoteza umaarufu mpaka kuwa chama cha kubebwa

    14. #12
      Keil's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd July 2007
      Posts : 2,381
      Rep Power : 1089
      Likes Received
      756
      Likes Given
      292

      Default Re: CCM Yakiri dhahiri kuelemewa kwa kasi.

      Mwakajumilo siyo Dr.

      Labda kama amechakachua zile za ki-CCM CCM ... kama za akina Nchimbi, Kamala na wengineo.

    15. #13
      Kiboko ya washamba's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 15th September 2012
      Posts : 8
      Rep Power : 337
      Likes Received
      2
      Likes Given
      0

      Default Re: CCM Yakiri dhahiri kuelemewa kwa kasi.

      Mnaongea sana CDM.Debe tupu alikosi kelele

    16. #14
      MD25's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th January 2012
      Location : Mugumu, Serengeti
      Posts : 1,894
      Rep Power : 895
      Likes Received
      537
      Likes Given
      64

      Default Re: CCM Yakiri dhahiri kuelemewa kwa kasi.

      Cdm wajiandae kuchukua nchi 2015...

    17. #15
      congobe's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 31st May 2012
      Posts : 123
      Rep Power : 375
      Likes Received
      12
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By almasiomary
      Kichwa Cha habari hakifanani na yaliyoandikwa kwa huyu jamaa wa CHAGA DEVELOPMENT MANIFESTOS ALIYEWEKA HII MADA, TOA MADA SIYO
      wewe una mapenzi na ccm ,yote yanayotendeka mabaya unaona ni mema tu ,acha unafki huwezi mshawishi mtu kwa ujinga kama huu ,tembea mbele huko

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...